RIWAYA: Mifupa 206

RIWAYA: Mifupa 206

Kaka hebu angalia mwanzoni mwa hii post kuna namba ya mtunzi. Pia nenda kwenye riwaya ya tai kwenye mzoga kuna namba ya mtunzi
[emoji113] [emoji113] [emoji39] [emoji39] [emoji7] tuwekee basi the banker
 
Tai kwenye Mzoga na Kisiwa cha Madagascar ni Story Zinazofanana, sema matukio tofauti coz mazingira ya matukio yote ni Rwanda, hii matukio kabla ya mauaji ya kimbari na ile Kisiwa cha Madagascar ni matukio baada ya Mauaji ya kimbari, kwangu naiona kama story 1 yenye season 1 na 2 dats y kwangu Naiona Mifupa 206 ni Bora kwangu Japo ubora utategemea Itaishaje Ila kwangu Hapa JF Riwaya yangu Kali kuliko zote ni PENIELA,
Kisiwa cha madagascar zinaongelea jaribio la mapinduzi nchini burundi na wala sio Rwanda. Hazifanani kabisa kwani kwenye kisiwa cha madagascar jamaa alienda kufatilia barozi wa tanzania nchini burundi aliyetekwa kabla ya tukio la mapinduzi
 
niliyekuwa nikitembea kwenye sayari mpya iliyojitenga na shughuli za binadamu.
Akili yangu ilikuwa hoi taabani kutokana na matukio yote yaliyotokea tangu asubuhi
kulipopambazuka. Bado nilikuwa na jukumu kubwa mbele yangu hata hivyo kwa
wakati huu nilihitaji kwanza kupumzika ili pindi kutakapopambazuka niamke nikiwa
na nguvu mpya za kuendelea na harakati zangu.
Muda mfupi baadaye nikawa nimeingia kwenye barabara iliyokuwa ikikatisha
mbele ya kanisa lile huku nikitembea kwa utulivu kuelekea upande wa kulia. Mara
tu nilipoingia kwenye barabara ile gari moja lilinipita kwa mwendo wa taratibu hata
hivyo sikulitilia maanani. Kwa kumbukumbu sahihi zilizokuwa kichwani mwangu ni
kuwa kituo cha teksi kilikuwa barabara ya mtaa wa tatu kutoka pale nilipokuwa mbele
ya hoteli moja maarufu iliyokuwa ikitazamana na jengo la ofisi za shirika la nyumba
la taifa NHC.
Nilikuwa nimepanga kutembea hadi kwenye kituo kile na kukodi teksi ambayo
ingenipeleka moja kwa moja hadi nyumbani kwangu nikapumzike. Wakati nikitembea
mara kwa mara niligeuka nyuma kutazama kama kungekuwa na gari au mtu yeyote
aliyekuwa akinifuatilia na nilipoona kuwa hali bado ilikuwa shwari nikaendelea na
safari yangu bila wasiwasi.
Nilipofika mbele ya barabara ile eneo kulipokuwa na mzunguko wa barabara
nikashika uelekeo wa upande wa kushoto nikiifuata barabara ya mtaa wa Shaaban
Robert. Mvua kubwa bado ilikuwa ikiendelea kunyesha na njiani nilipishana na
magari machache sana ambayo yalinipita kwa kasi yakiendelea na safari zao. Hivyo
ilinichukuwa muda mfupi tu kugundua kuwa binadamu pekee aliyekuwa akitembea
kwa miguu katika barabara ile nilikuwa ni mimi peke yangu na hali ile ikanipelekea
nijihisi mpweke sana.
Wakati nikitembea nikajikuta nikimkumbuka yule mdunguaji hatari. Alikuwa ni
msichana mrefu mweusi na mrembo sana kiasi kwamba hakuelekea kabisa kufanana
na ile shughuli aliyokuwa akiifanya. Kiu ya kuonana naye ana kwa ana bado ilikuwa
kwenye nafsi yangu hata hivyo niliishia kujipa matumaini tu kwani sikujua ni lini na
wapi ningekutana naye kwa mara nyingine msichana yule mrembo aliyeinusuru roho
yangu kutumbukia shimoni.
Hatimaye nikawa nimeyafikia makutano ya barabara ya mtaa wa Shaaban Robert
na ile barabara ya Samora Avenue na wakati nilipokuwa nikijiandaa kuvuka makutano
yale ili niingie kwenye barabara ya Samora Avenue ghafla mbele yangu nikashtushwa
na mwanga mkali wa taa za gari zilizowashwa ghafla kumulika pale nilipokuwa. Gari
lile lilikuwa limeegeshwa umbali mfupi kabla ya yale makutano ya barabara na hivyo
kunipelekea nisite kuendelea na safari yangu. Hivyo nikapunguza urefu wa hatua
zangu taratibu huku bado nikiutafakari ule mwanga wa taa za lile gari.
Sehemu moja ya nafsi yangu ilinitaka nigeuze na kurudi kule nilipotoka wakati
sehemu nyingine ilinitaka niendelee mbele na safari yangu. Hali ile ikaipelekea akili
yangu ipoteze mhimili wa maamuzi ya haraka na kuifanya miguu yangu iwe mizito.
Hatimaye nikapiga moyo konde na kuendelea mbele.
Sikufika mbali katika safari yangu mara nikaliona lile gari likiacha maegesho na
kuingia barabarani likifuata uelekeo wangu. Tukio lile likapelekea mapigo ya moyo
wangu yapoteze utulivu kabisa huku jasho jepesi likianza kunitoka mwilini. Haraka
nikahisi kuwa mambo hayakuwa shwari tena hivyo nikavuka barabara na kuhamia
upande wa pili na wakati nikifanya vile niliweza kuliona vizuri lile gari. Lilikuwa ni
gari aina ya Landcruiser ya rangi ya samawati. Kitendo cha mimi kuvuka barabara
kikampelekea dereva wa ile gari Landcruiser naye aongeze mwendo kuyakaribia yale
makutano ya barabara. Tukio lile likanipa hakika kuwa mtu yeyote aliyekuwa ndani ya
lile gari basi alikuwa na malengo na mimi na hivyo sikutaka kusubiri ili kupata hakika
ya hisia zangu.
Hivyo mara tu baada ya kuvuka ile barabara niliongeza mwendo wa hatua zangu
huku nikiupeleka mkono wangu mafichoni kuipapasa bastola yangu. Kwa kuwa
nilikuwa karibu zaidi nikayafikia yale makutano ya barabara mapema zaidi kabla ya
ile Landcruiser. Mara tu nilipoyafikia makutano yale nikashika uelekeo wa upande wa
kushoto nikiifuata barabara ya Samora Avenue iliyokuwa ikikatisha kando ya eneo la
makumbusho ya taifa na jumba la tamaduni ama National Museum and House of Culture
kwa upande wa kulia na eneo la Bonitanical Garden kwa upande wa kushoto.
Nikiwa tayari nimeingia kwenye barabara ile nikaongeza mwendo wa urefu
wa hatua zangu na hivyo nikawa ni kama ninayetaka kutembea na kukimbia kwa
wakati mmoja. Hata hivyo jicho langu la pembe halikuacha mara kwa mara kutazama
kilichokuwa kikiendelea nyuma yangu.
Mvua iliendelea kunyesha na wakati huu barabara ya Samora Avenue ilikuwa
imemezwa na ukimya wa aina yake kwani sikuona gari,pikipiki wala mtu yeyote mbele
yangu. Taa kutoka kwenye majengo marefu ya ghorofa yaliyokuwa jirani na barabara
ile zilimulika kikamilifu hata hivyo hazikufanikiwa kutowesha giza lote eneo lile. Ule
mwanga wa taa za gari kutoka nyuma yangu kadiri ulivyokuwa ukiongezeka ukanifanya
nianze kuhisi kuwa lile gari Landcruiser nyuma yangu lilikuwa mbioni kunifikia.
Hivyo kwa kasi ya ajabu nikaanza kutimua mbio na tukio lile likampelekea dereva
wa ile Landcruiser naye azidi kuongeza mwendo hata hivyo mbio zangu hazikuwa za
kubabaisha.
Jasho likaanza kunitoka huku akili yangu ikisumbuka kufikiria nini cha kufanya.
Baada ya muda mfupi nikawa nimelifikia lile eneo la Makumbusho na kujikuta
nikishawishika kuruka uzio wa eneo lile na kuingia ndani kama sehemu salama ya
kuwapotezea malengo wale watu waliokuwa kwenye ile gari Landcruiser iliyokuwa
ikinifukuza nyuma yangu. Hata hivyo kuzidi kutafakari kukanifanya niliweke kando
wazo lile hasa baada ya kukumbuka walinzi waliokuwa wakilinda eneo lile. Hivyo
nikaendelea kutimua mbio safari hii nikiukata upepo kama mwanariadha mzoefu wa
mbio za kimataifa.
Hata hivyo sikufika mbali sana katika safari yangu pale nilipoanza kuhisi vishindo
nyuma yangu. Niligeuka haraka kutazama kule nyuma na mara hii nikawaona mbwa
wakubwa watatu wa polisi aina ya German Shepherd wenye urefu sawa na ule wa beberu
la kisasa mwenye afya ya ziada. Mbwa hao wenye hasira walikuwa wakifukua mbio
kunikaribia na sauti za vishindo vyao barabarani ilinitahadharisha kuwa nilipaswa
kuwa makini sana. Nyuma ya wale mbwa umbali wa mita kadhaa niliwaona wanaume
watano wakikimbia kuwafuata wale mbwa kwa nyuma huku nyuso zao zikiwa
zimekingwa kwa kofia za makoti ya mvua. Wote walikuwa wameshika bunduki zao
mikononi.
Wale mbwa nyuma yangu bila shaka walikuwa na hamu sana na mimi kwani
pamoja na mbio zangu kuwa za kuaminika lakini niligundua haraka kuwa umbali
baina yangu na wao ulikuwa ukipungua kwa kasi ya ajabu katika kila nukta ya sekunde
iliyokuwa ikitoweka na hapo hofu ikaanza kuniingia. Hatimaye nikaupeleka mkono
mafichoni na kuichomoa bastola yangu huku nikiwa nimepanga kuwafyeka wale
mbwa kwa risasi kabla mabosi wao hawajanifikia. Hata hivyo nikajikuta nikisita
kufanya vile kwani sikutaka kuwa wa kwanza kuanzisha shambulizi la risasi pale
nilipokumbuka kuwa sehemu kubwa ya eneo lile ilikuwa ikilindwa kwa umakini wa
hali ya juu kutokana na kwamba eneo lile lilikuwa ofisi nyeti za serikali. Hivyo milio ya
risasi ingeweza kuwavuta walinzi wengi zaidi wa eneo lile na hapo uwezekano wangu
wa kutoka salama ungezidi kuwa mdogo.
Nilivuta pumzi ya kutosha na kuongeza mwendo huku nikikimbia katika mbio
zisizoelezeka kwa urahisi. Hata hivyo wale mbwa nyuma yangu hawakunipa nafasi ya
kuwatoroka kwani nilipogeuka nyuma kuwatazama tena nikagundua kuwa walikuwa
wamejigawa katika mikakati ya kuhakikisha wananidhibiti mapema kabla sijafika
mbali.
Mbwa mmoja alikuwa nyuma yangu upande wa kushoto. Mbwa mwingine
alikuwa nyuma yangu upande wa kulia. Yule mbwa wa mwisho alikuwa hatua chache
nyuma yangu huku wote wakiwa wamekenua meno yao makali na ndimi zao ndefu
zenye uchu zikining’inia nje.
Hatimaye nikawa nimelifikia lile eneo la Botanical Garden lililokuwa upande wa
kushoto wa ile barabara. Eneo lililokuwa na bustani ya maua na vichaka hafifu
vya miti lililozungushiwa uzio wa ukuta mfupi. Wale mbwa ni kama waliokuwa
wameishtukia mapema dhamira yangu kwani nao walikuwa wameongeza kasi zaidi
kiasi cha kuwapelekea mara kwa mara kulikosakosa pindo la koti langu lililokuwa
likipepea kama kishada nyuma yangu.
Niliufikia ule ukuta wa eneo la Botanical Garden kisha nikaudandia hata hivyo wale
mbwa walikuwa werevu sana wa kutambua hila yangu hivyo wakaniwahi. Mbwa
mmoja aliwahi kuliuma pindo la koti langu na mwingine akajirusha na kung’ang’ania
buti langu la mguu wa kushoto kwani ule mguu wangu mwingine tayari nilikuwa
nimeishafanikiwa kuupandisha juu ya ule ukuta.
Nilijitahidi kwa kila hali kujinasua kutoka kwa wale mbwa wakali lakini hilo
halikuwezekana kirahisi kwani wale mbwa walikuwa ving’ang’anizi kama ruba.
Nilipogeuka kutazama kule nyuma wale watu ambao hapo awali nilikuwa nimewaacha
mbali nao pia nikagundua kuwa walikuwa mbioni kunifikia. Mara nikamuona mmoja
wao akiielekeza bunduki yake kwangu na hapo nikajua alikuwa amenuia kunishindilia
risasi. Hivyo sikutaka kusubiri badala yake nikakusanya nguvu na kuupandisha juu ule
mguu wangu wa kushoto.
Halikuwa jambo rahisi kwani yule mbwa hakuuachia mguu wangu na badala yake
akaendelea kuning’inia kwenye buti langu na kwa mbali niliyahisi meno yake makali
yakiikaribia ngozi ya mguu wangu. Yule mbwa bado hakuniachia pamoja na jitihada
zangu zote za kujitahidi kujinasua huku yule mwenzake akiwa bado ameling’ang’ania
pindo la vazi langu.
Hofu ya kudhibitiwa kikamilifu ikaniingia na wakati nikipiga akili nyingine ya
kujinasua kwenye kadhia ile ghafla nikasikia sauti ya mlio mkali wa mfyatuko wa risasi
kisha muda uleule nikasikia unafuu mkubwa katika uzito wa mguu wangu. Haraka
nikageuka tena kutazama kule nyuma walikokuwa wale watu hatari wakinifukuza.
Wale watu sasa walikuwa wameelekezea bunduki zao kwangu na hapo nikajua kuwa
yule bwege wa awali aliyenilenga kwa kutokuwa makini alikuwa amepoteza shabaha
ya kulenga mguu wangu na badala yake akakichakaza vibaya kichwa cha yule mbwa
aliyekuwa ameng’ang’ania mguu wangu.
“You bogus!...yaani nyinyi ndiyo mafala wakubwa sijapata kuona” nikawatukana wale
watu na kabla hawajapata mhimili mzuri wa shabaha zao mimi nikawa nimeshapanda
juu ya ule ukuta. Yule mbwa aliyekuwa ameng’ang’ania pindo la koti langu alikuwa
ameliachia baada ya kushtushwa vibaya na ile sauti mbaya ya risasi.
Kufumba na kufumbua nikawa tayari nimeangukia upande wa ndani wa ule
uzio huku nyuma nikisindikizwa na mvua ya risasi zilizonipunyuapunyua kiasi cha
kutengeneza matundu kwenye ukuta wa uzio ule dhaifu.
Niliangukia chini ndani ya ule ukuta huku nikihema ovyo kisha nikajiviringisha
haraka na kujilaza majanini na hapo nikaanza kutambaa kifudifudi nikijiweka mbali
na eneo lile. Nilipofika mbele sehemu niliyoihisi kuwa salama kidogo nikasimama na
kuanza kutimua mbio nikikatisha katikati ya vichaka vya miti vya eneo lile nikielekea
upande wa pili ambapo ningeupanda ukuta mwingine wa uzio ule na kuangukia nje ya
eneo lile na baada ya hapo ningetokomea zangu mitaani.
Niliendelea kukimbia na baada ya kitambo kifupi nikawa nimeufikia ukuta
mwingine wa upande wa pili wa ule uzio. Hata hivyo wakati nilipokuwa nikijiandaa
kuukwea ukuta ule nilichokiona mbele yangu nje ya ule ukuta kikapeleka baridi nyepesi
ianze kusambaa moyoni mwangu. Kingo za mdomo wangu zikakauka ghafla huku
harufu ya msukumo mkubwa wa damu mwilini ikiyasimanga matundu ya pua yangu.
Magari matatu yanayofanana na lile gari lililokuwa likinifukuza kule nyuma muda
mfupi uliyopita sasa niliyaona yakisimama kwa fujo na mbwembwe za aina yake nje
ya ukuta ule kisha milango yake ikafunguliwa kwa pupa na hapo nikawaona watu
wenye bunduki na makoti ya mvua kama wale wa awali wakishuka haraka na kusogea
kwa tahadhari wakiuzingira ule ukuta wa lile eneo nililojibanza. Nilitulia kwa makini
nikiwatazama kwa kificho watu wale na kwa kweli hapakuwa na sehemu ya kutorokea.
Hivyo niliinama tena chini nikirudi kunyumenyume kwa tahadhari na nilipokifikia
wao akiielekeza bunduki yake kwangu na hapo nikajua alikuwa amenuia kunishindilia
risasi. Hivyo sikutaka kusubiri badala yake nikakusanya nguvu na kuupandisha juu ule
mguu wangu wa kushoto.
Halikuwa jambo rahisi kwani yule mbwa hakuuachia mguu wangu na badala yake
akaendelea kuning’inia kwenye buti langu na kwa mbali niliyahisi meno yake makali
yakiikaribia ngozi ya mguu wangu. Yule mbwa bado hakuniachia pamoja na jitihada
zangu zote za kujitahidi kujinasua huku yule mwenzake akiwa bado ameling’ang’ania
pindo la vazi langu.
Hofu ya kudhibitiwa kikamilifu ikaniingia na wakati nikipiga akili nyingine ya
kujinasua kwenye kadhia ile ghafla nikasikia sauti ya mlio mkali wa mfyatuko wa risasi
kisha muda uleule nikasikia unafuu mkubwa katika uzito wa mguu wangu. Haraka
nikageuka tena kutazama kule nyuma walikokuwa wale watu hatari wakinifukuza.
Wale watu sasa walikuwa wameelekezea bunduki zao kwangu na hapo nikajua kuwa
yule bwege wa awali aliyenilenga kwa kutokuwa makini alikuwa amepoteza shabaha
ya kulenga mguu wangu na badala yake akakichakaza vibaya kichwa cha yule mbwa
aliyekuwa ameng’ang’ania mguu wangu.
“You bogus!...yaani nyinyi ndiyo mafala wakubwa sijapata kuona” nikawatukana wale
watu na kabla hawajapata mhimili mzuri wa shabaha zao mimi nikawa nimeshapanda
juu ya ule ukuta. Yule mbwa aliyekuwa ameng’ang’ania pindo la koti langu alikuwa
ameliachia baada ya kushtushwa vibaya na ile sauti mbaya ya risasi.
Kufumba na kufumbua nikawa tayari nimeangukia upande wa ndani wa ule
uzio huku nyuma nikisindikizwa na mvua ya risasi zilizonipunyuapunyua kiasi cha
kutengeneza matundu kwenye ukuta wa uzio ule dhaifu.
Niliangukia chini ndani ya ule ukuta huku nikihema ovyo kisha nikajiviringisha
haraka na kujilaza majanini na hapo nikaanza kutambaa kifudifudi nikijiweka mbali
na eneo lile. Nilipofika mbele sehemu niliyoihisi kuwa salama kidogo nikasimama na
kuanza kutimua mbio nikikatisha katikati ya vichaka vya miti vya eneo lile nikielekea
upande wa pili ambapo ningeupanda ukuta mwingine wa uzio ule na kuangukia nje ya
eneo lile na baada ya hapo ningetokomea zangu mitaani.
Niliendelea kukimbia na baada ya kitambo kifupi nikawa nimeufikia ukuta
mwingine wa upande wa pili wa ule uzio. Hata hivyo wakati nilipokuwa nikijiandaa
kuukwea ukuta ule nilichokiona mbele yangu nje ya ule ukuta kikapeleka baridi nyepesi
ianze kusambaa moyoni mwangu. Kingo za mdomo wangu zikakauka ghafla huku
harufu ya msukumo mkubwa wa damu mwilini ikiyasimanga matundu ya pua yangu.
Magari matatu yanayofanana na lile gari lililokuwa likinifukuza kule nyuma muda
mfupi uliyopita sasa niliyaona yakisimama kwa fujo na mbwembwe za aina yake nje
ya ukuta ule kisha milango yake ikafunguliwa kwa pupa na hapo nikawaona watu
wenye bunduki na makoti ya mvua kama wale wa awali wakishuka haraka na kusogea
kwa tahadhari wakiuzingira ule ukuta wa lile eneo nililojibanza. Nilitulia kwa makini
nikiwatazama kwa kificho watu wale na kwa kweli hapakuwa na sehemu ya kutorokea.
Hivyo niliinama tena chini nikirudi kunyumenyume kwa tahadhari na nilipokifikia
wao akiielekeza bunduki yake kwangu na hapo nikajua alikuwa amenuia kunishindilia
risasi. Hivyo sikutaka kusubiri badala yake nikakusanya nguvu na kuupandisha juu ule
mguu wangu wa kushoto.
Halikuwa jambo rahisi kwani yule mbwa hakuuachia mguu wangu na badala yake
akaendelea kuning’inia kwenye buti langu na kwa mbali niliyahisi meno yake makali
yakiikaribia ngozi ya mguu wangu. Yule mbwa bado hakuniachia pamoja na jitihada
zangu zote za kujitahidi kujinasua huku yule mwenzake akiwa bado ameling’ang’ania
pindo la vazi langu.
Hofu ya kudhibitiwa kikamilifu ikaniingia na wakati nikipiga akili nyingine ya
kujinasua kwenye kadhia ile ghafla nikasikia sauti ya mlio mkali wa mfyatuko wa risasi
kisha muda uleule nikasikia unafuu mkubwa katika uzito wa mguu wangu. Haraka
nikageuka tena kutazama kule nyuma walikokuwa wale watu hatari wakinifukuza.
Wale watu sasa walikuwa wameelekezea bunduki zao kwangu na hapo nikajua kuwa
yule bwege wa awali aliyenilenga kwa kutokuwa makini alikuwa amepoteza shabaha
ya kulenga mguu wangu na badala yake akakichakaza vibaya kichwa cha yule mbwa
aliyekuwa ameng’ang’ania mguu wangu.
“You bogus!...yaani nyinyi ndiyo mafala wakubwa sijapata kuona” nikawatukana wale
watu na kabla hawajapata mhimili mzuri wa shabaha zao mimi nikawa nimeshapanda
juu ya ule ukuta. Yule mbwa aliyekuwa ameng’ang’ania pindo la koti langu alikuwa
ameliachia baada ya kushtushwa vibaya na ile sauti mbaya ya risasi.
Kufumba na kufumbua nikawa tayari nimeangukia upande wa ndani wa ule
uzio huku nyuma nikisindikizwa na mvua ya risasi zilizonipunyuapunyua kiasi cha
kutengeneza matundu kwenye ukuta wa uzio ule dhaifu.
Niliangukia chini ndani ya ule ukuta huku nikihema ovyo kisha nikajiviringisha
haraka na kujilaza majanini na hapo nikaanza kutambaa kifudifudi nikijiweka mbali
na eneo lile. Nilipofika mbele sehemu niliyoihisi kuwa salama kidogo nikasimama na
kuanza kutimua mbio nikikatisha katikati ya vichaka vya miti vya eneo lile nikielekea
upande wa pili ambapo ningeupanda ukuta mwingine wa uzio ule na kuangukia nje ya
eneo lile na baada ya hapo ningetokomea zangu mitaani.
Niliendelea kukimbia na baada ya kitambo kifupi nikawa nimeufikia ukuta
mwingine wa upande wa pili wa ule uzio. Hata hivyo wakati nilipokuwa nikijiandaa
kuukwea ukuta ule nilichokiona mbele yangu nje ya ule ukuta kikapeleka baridi nyepesi
ianze kusambaa moyoni mwangu. Kingo za mdomo wangu zikakauka ghafla huku
harufu ya msukumo mkubwa wa damu mwilini ikiyasimanga matundu ya pua yangu.
Magari matatu yanayofanana na lile gari lililokuwa likinifukuza kule nyuma muda
mfupi uliyopita sasa niliyaona yakisimama kwa fujo na mbwembwe za aina yake nje
ya ukuta ule kisha milango yake ikafunguliwa kwa pupa na hapo nikawaona watu
wenye bunduki na makoti ya mvua kama wale wa awali wakishuka haraka na kusogea
kwa tahadhari wakiuzingira ule ukuta wa lile eneo nililojibanza. Nilitulia kwa makini
nikiwatazama kwa kificho watu wale na kwa kweli hapakuwa na sehemu ya kutorokea.
Hivyo niliinama tena chini nikirudi kunyumenyume kwa tahadhari na nilipokifikia
kichaka cha miti cha karibu na eneo lile nikageuka nyuma na kuanza kutimua mbio
kuelekea upande mwingine wa ule ukuta wa lile eneo. Niliufikia ule ukuta wa upande
mwingine ndani ya muda mfupi tu na kabla ya sijaukwea nilichungulia tena na
kutazama kule nje. Mara hii nikajisikia kukata tamaa zaidi.
Kulikuwa na magari manne yaliyofanana na yale niliyoyaona muda mfupi nje ya
ukuta kule nilipotoka. Watu kama wale wa awali walikuwa wakishuka kwa pupa kutoka
kwenye yale magari huku baadhi yao wakiwa na mbwa wamewashika kwa minyororo
mikononi mwao. Kwa kweli nilijisikia kukata tamaa huku nikianza kujilaumu kwa
kujiingiza kwenye mtego ule. Nikaanza kuhisi kuwa dakika za muda wangu wa kuwa
huru sasa zilikuwa zikihesabika.
Nikiwa nimejibanza pale kwenye ukuta huku nikiendelea kuchungulia kule nje
akili yangu ilianza kufanya kazi haraka ikisumbuka katika kutafuta namna ya kujinasua
kutoka katika hatari ile ya kukamatwa. Mawazo mengi yalikuwa yakipita kichwani
mwangu na kwa kweli sikuweza haraka kutambua kuwa ni wazo lipi hasa nilipaswa
kulifanyia kazi kwa wakati ule. Nikajishauri kuwa niende kwenye upande ule mwingine
wa ukuta ambao ulikuwa ndiyo pekee sijaufikia. Hata hivyo niliachana na wazo lile
kwani mandhari ya eneo lile nilikuwa nikiyafahamu vizuri.
Nje ya ukuta wa upande ule kulikuwa na eneo kubwa la wazi hivyo watu wale
hatari wangeweza kuutumia vyema uwazi ule kunichapa risasi endapo ningethubutu
kujitokeza. Hivyo kwa tafsiri ya haraka niliyoiona ni kuwa uwepo wangu eneo lile sasa
ulikuwa ukitambulika vizuri na wale watu na sasa walikuwa wamelizingira lile eneo
lote katika kuhakikisha kuwa sipati nafasi ya kuwatoroka.
Kitu kilichonishangaza ni namna nguvu kubwa namna ile ilivyokuwa ikitumika
dhidi yangu kana kwamba mimi nilikuwa tishio kubwa kwenye usalama wa nchi
hii. Kwa kweli hali ile ilinishangaza sana hata hivyo ule haukuwa wakati wa kujiuliza
maswali.
Niliitazama saa yangu ya mkononi na kushangazwa juu ya namna dakika
zilivyokuwa zikiyeyuka. Nilipotazama tena kule nje mara nikauona mwanga wa taa za
ving’ora vilivyokuwa juu ya magari ya wale watu hatari namna ulivyokuwa ukijitahidi
kumulika eneo lile. Hatimaye nikayaacha yale maficho na kurudi tena kule kwenye
kichaka cha miti huku akili yangu ikiendelea kusumbuka namna ya kujinasua kutoka
katika hatari ile ya kukamatwa na wale watu. Kwa kweli niliendelea kujilaumu tena na
tena kwa kujichanganya vibaya kwenye ule mtego rahisi.
Wakati nikiendelea kuwaza mara wazo fulani likanijia akilini pale nilipokumbuka
miundombinu ya majitaka ya jiji la Dar es Salaam. Katika maeneo fulani ya jiji la Dar
es Salaam mifereji ya majitaka kuelekea kwenye bahari ya Hindi ilikuwa imejengewa
chini ya ardhi kwa kukwepa uharibifu ambao ungetokana na shughuli mbalimbali za
watu au kukwepa kutumia sehemu kubwa ya ardhi hiyo ambayo ingeweza kutumika
kwa shughuli zingine zenye manufaa zaidi. Mifereji hiyo iliyojengewa chini ya ardhi
baadhi ilikuwa ikikatisha chini ya barabara za jiji mtaani. Chini ya majengo marefu
ya ghorofa au kandokando ya barabara huku makutano ya mifereji hiyo yakiitwa
chemba. Chemba hizo zilikuwa zimejengewa vizuri kwa zege na kufunikwa kwa
mifuniko imara ya chuma.
Matumaini yangu ya kutoroka yakafufuka upya na sikutaka kuendelea kujishauri
zaidi badala yake nikaanza zoezi la kutafuta chemba hizo kama kungekuwa na yoyote
eneo lile.
Nilichukua tochi yangu ndogo ya kijasusi kutoka kwenye mfuko wa koti langu na
kwa tahadhari nikaiwasha na kuanza kumulika chini katika sehemu tofauti za eneo
lile la hifadhi ya bustani ya miti mbalimbali. Nikaanza kuzunguka upande huu na ule
nikichunguza bila mafanikio. Hali ya mtupo wa damu kwenye mishipa yangu mwilini
ukanitanabaisha kuwa mapigo ya moyo wangu yalikuwa yamepoteza utulivu katika
kiwango cha juu cha hofu.
Ingawa mvua kubwa ilikuwa ikiendelea kunyesha jijini Dar es Salaam lakini ndani
ya koti langu nilihisi joto kali mno. Mikono yangu nayo ikaanza kupoteza utulivu
na nilipoitazama haraka nikagundua kuwa nayo ilikuwa imeanza kutetemeka ovyo.
Wakati nikiendelea na uchunguzi wangu kule nje ya ukuta niliweza kuzisikia kelele
za wale mbwa wakibweka. Sikutaka kujidanganya kuwa nafasi ya kuwatoroka wale
watu kupitia kwenye kuta za ule uzio bado ilikuwepo kwani hadi wakati ule nilikuwa
na hakika kuwa vichochoro na matundu yote ya uzio ule vilikuwa vimezibwa au
kuwekewa mtego wa kuninasa kiulaini.
Baada ya tafutatafuta ya hapa na pale hatimaye nikabahatika kuiona chemba
moja iliyokuwa katikati ya kichaka hafifu cha miti nyuma ya mti wa mpera. Kuiona
chemba ile matumaini yakaongezeka moyoni hivyo nikaisogelea ile chemba na kuanza
kuichunguza kwa haraka. Hata hivyo kabla sijaanza kufanya utundu wangu kupitia
uwazi mdogo uliokuwa baina ya miti iliyokuwa eneo lile niliweza kuona sehemu moja
juu ya ukuta wa uzio wa eneo lile. Wale watu hatari sasa walikuwa wakiwasaidia mbwa
wao kuwapandisha juu ya ule ukuta ili waweze kuingia ndani ya lile eneo na kuanza
kunisaka.
Sikutaka wale mbwa hatari wanifikie tena hivyo niliinama kwenye ile chemba na
mara hii nikaliona kufuli chakavu likiwa limeuzuia kikamilifu ule mfuniko wa chuma
wa ile chemba. Bila kupoteza muda nikaingiza mkono kwenye mfuko wa koti langu
na kuchukua bisbisi fupi na nene,moja ya vifaa vyangu vya kazi kisha nikaipitisha
bisbisi ile katikati ya lile kufuli na ule mfuniko wa chuma wa ile chemba. Nilipomaliza
nikaanza kuikandamiza ile bisbisi kwa chini katika mtindo wa kuharibu lile kufuli.
Lile kufuli lilikuwa la shaba imara sana kama lililofungwa tangu enzi za wakoloni hata
hivyo sikuwa na njia mbadala ya kuepukana nalo.
Nikageuka tena kutazama kwenye ule uwazi na mara hii nikawaona mbwa wawili
wakiruka na kuingia mle ndani ya ule uzio kupitia ngazi waliyowekewa na hapo hofu
ikanishika.
Baada ya kukurukakara za hapa na pale hatimaye nikafanikiwa kuifyatua ile kufuli
na kuitupa kando kisha ile bisbisi nikaichomeka kwenye kingo moja ya ule mfuniko
wa chemba na kuikandamiza chini. Ule mfuniko ukanyanyuka kidogo na hapo
nikapata uwazi wa kuingiza vidole vyangu chini yake na kuunyanyua juu. Nikauondoa
ule mfuniko wa chuma na kuusogeza pembeni. Nilichokiona baada ya kuuondoa
ule mfuniko lilikuwa ni shimo kubwa la chemba ya majitaka lenye kipenyo mraba.
Nikachukua tochi yangu na kuanza kumulika kule chini ya ile chemba. Lilikuwa
shimo refu lenye kina kisichopungua futi nane kwenda chini na mwisho wa shimo
lile kulikuwa na makutano ya mifereji miwili mikubwa iliyopishana na kutengeneza
umbo la msalaba. Kiasi kikubwa cha majitaka kilikuwa kikiendelea kutiririka kwenye
makutano ya mifereji ile.
Haraka nikaitia bastola yangu na ile bisbisi mfukoni na kubakiwa na ile tochi
ndogo yenye mwanga mkali mkononi. Kisha nikaanza kuingia ndani ya ile chemba
nikishuka chini taratibu na kwa uangalifu. Fukuto la mle ndani lilikuwa kali sana kiasi
cha kunifanya nianze kutokwa na jasho jingi mwilini. Mle ndani pembeni ya kuta za
ile chemba kulikuwa na utelezi mkali hata hivyo nilijitahidi kwa kila hali kuikaza misuli
ya miguu yangu katika namna ya kuhakikisha kuwa sitelezi na kuangukia chini ya ile
chemba kwani hiyo ingekuwa hatari zaidi.
Hatimaye nilimaliza kuingia kwenye ile chemba kisha nikausogeza ule mfuniko wa
chuma na kuifunga ile chemba kwa ndani kabla ya wale mbwa hatari hawajanifikia.
Tochi yangu ikiwa mkononi mara tu nilipoufunika ule mfuniko nilianza kushuka kule
chini taratibu nikiweka vituo hapa na pale kukwepa kuteleza vibaya.
Hatimaye nilifika kule chini ya ile chemba. Hewa ya mle ndani ilikuwa nzito
sana na yenye harufu kali ya mchanganyiko wa majitaka na maji ya mvua iliyokuwa
ikiendelea kunyesha sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam. Yale majitaka yalikuwa
yakitiririka kwa kasi mno na kina chake kilikuwa usawa wa mapaja yangu.
Niliachana na ule uelekeo wa yale majitaka yalipokuwa yakielekea kisha nikachukua
mfereji mmoja nikiufuata uelekeo wa yale majitaka yalipokuwa yakitokea. Ule mwanga
wa tochi yangu mkononi uliniwezesha kuona mbele yangu ingawa giza lilikuwa
zito mno na kwenye kuta za mfereji ule uliotengenezwa kwa matofari madogo ya
kuchoma kulikuwa tope zito la utelezi. Ukubwa wa mrefeji ule ulitosha kunifanya
niweze kutembea vizuri pasipo usumbufu wowote. Sikujua ule mfereji ulikuwa
ukielekea wapi hata hivyo nilikuwa na matumaini ya safari yangu.
Ni kama niliyekuwa kwenye ulimwengu mwingine kwani kule chini kulikuwa
kunatisha sana na hewa ilikuwa nzito mno. Ingawa sikutarajia kukutana na hatari
yoyote ya kibinadamu mbele yangu lakini niliikamata vyema bastola yangu mkononi.
Baada ya mwendo mrefu kidogo mara nikawa nimefika kwenye makutano mengine
ya mifereji mitano lakini juu ya makutano yale hapakuwa na chemba kama ya kule
nyuma nilikotokea.
Nguvu ya maji eneo lile ilikuwa imeongezeka kiasi cha kuifanya miguu yangu
ionekane kupwaya kila nilipokuwa nikitupa hatua zangu. Nilipofika kwenye makutano
yale ya mifereji nikasimama na kugeuka nyuma nikichunguza kama kungekuwa na
mtu yeyote aliyekuwa akinifuatilia. Hata hivyo sikuona dalili za uwepo wa kiumbe
chochote kikinifuatilia hivyo nikageuka mbele na kuyatazama yale makutano ya ile
wa magharibi hatimaye nikafika sehemu moja na kuweka kituo. Hewa ya mle ndani
ilikuwa nzito mno na yenye harafu mbaya sana. Mbali na hayo kulikuwa na joto
kali lililonifanya nijute kuvaa lile koti langu refu jeusi la kijasusi hata hivyo sikulivua.
Niliusogeza karibu mkono wangu wa kushoto kisha kikabonyeza kitufe kimoja
kilichokuwa pembeni ya saa yangu ya digital na taa ya saa ile ilipowaka nikatazama
muda. Nilikuwa nimetumia muda wa nusu saa tangu nilipoanza safari yangu kutoka
kwenye ile chemba ya kwanza hivyo nikaushusha mkono wangu na kuendelea na
safari huku nikimwomba Mungu kuwa muda mfupi mbele yangu nikutane na chemba
nyingine.
Ombi langu huwenda lilijibiwa mapema kwani baada ya mwendo mfupi tu wa
safari yangu mara nikawa nimefika kwenye chemba nyingine kubwa yenye makutano
ya mifereji minne. Mifereji miwili kati yake ikiingiza majitaka na mifereji miwili mingine
ikipokea majitaka hayo na kuyatiririsha maeneo mengine. Nilisimama na kuichunguza
vizuri chemba ile na hapo nikagundua kuwa ilikuwa safi kidogo ukilinganisha na
zile chemba nyingine nilizozipita kule nyuma. Kwenye makutano ya mifereji ya ile
chemba hakukuwa na utelezi mkubwa wala takataka nyingi badala yake kulikuwa na
matuta hafifu ya mchanga mwepesi yaliyofanywa na mtiririko wa majitaka mepesi
kutoka maeneo mbalimbali.
Nilisimama chini ya chemba ile na kumulika ule mfuniko wa chuma wa ile chemba.
Nilifurahi kwani ule mfuniko nao ulikuwa msafi na haukuwa na popo kama kwenye ile
chemba ya kule nyuma nilipotoka. Nikiwa pale chini nikayatega vizuri masikio yangu
na kwa kufanya vile kwa mbali nilisikia muungurumo wa kitu fulani kisichoeleweka.
Nikajaribu kuwaza kuwa muungurumo ule ungekuwa ukitokana na kitu gani. Baada
ya kuupisha utulivu kichwani mwangu hisia zikaniambia kuwa huwenda chemba ile
ilikuwa karibu na barabara ya magari na hivyo muungurumo ule huwenda ungeweza
kuwa ni wa injini ya gari lililokuwa likipita karibu na eneo lile. Kwa mara ya kwanza
tangu niingie ndani ya mifereji ile moyo wangu ukawa umerejewa na matumaini ya
ajabu.
Kuelekea kule juu kwenye mfuniko wa chuma wa ile chemba kulikuwa na
ngazi fupi zilizotengenezewa ukutani lakini ngazi zile hazikufika chini kabisa ya ile
chemba kwa sababu za kitaalamu walizokuwa wakizifahamu wajenzi. Hata hivyo
kwangu ilikuwa afadhali sana maana ile chemba ilikuwa tofauti kabisa na zile chemba
nilizozipita kule nyuma. Ile chemba ilikuwa pana kiasi ambacho kupanda kule juu kwa
kukanyaga mguu wangu mmoja upande mmoja wa ile chemba na mguu mwingine
upande wa pili lingekuwa zoezi gumu la kunitoa jasho.
Kwa jitihada binafsi hatimaye nikafanikiwa kuzifikia zile ngazi fupi za chuma kwa
mikono yangu kisha nikajivuta na kuipandisha miguu yangu kwenye zile ngazi halafu
kwa tahadhari ya hali ya juu nikaanza kupanda zile ngazi nikielekea kule juu kwenye
ule mfuniko wa ile chemba. Zoezi lile lilihitaji uangalifu wa hali ya juu kwani zile ngazi
zilikuwa za chuma na zilizodumu kwa muda mrefu kiasi kwamba ile hali ya hewa ya
mle ndani ilikuwa imezipelekea ngazi zile zipate kutu na kuwa dhaifu.
 
Mkuu we achana na huyo jamaa cc tupo macho tunangoja mkuu
 
Back
Top Bottom