Tumosa
JF-Expert Member
- Jul 21, 2016
- 16,527
- 52,623
Pole shemela uvumilivu umekushindathe banker acha ujinga wa kitoto usitufanye sisi watoto wadogo mpumbavu wewe
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pole shemela uvumilivu umekushindathe banker acha ujinga wa kitoto usitufanye sisi watoto wadogo mpumbavu wewe
Mara nyingine uvumilivu ni dhambi shemelaPole shemela uvumilivu umekushinda
Pole sana aiseeMa
Mara nyingine uvumilivu ni dhambi shemela
Nishapoa shemelaPole sana aisee
[emoji106] [emoji106] [emoji106]Nishapoa shemela
Ndio naanza kuisoma lakini imenipagawishaMIFUPA 206 KEVIN e. MPONDA
MSITU WA GOVENDER KIVU YA KASKAZINI
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
UKIMYA WA KUTISHA ulikuwa umetawala eneo lote la msitu wa Govender
katika jimbo hili la Kivu ya Kaskazini nchini D.R Congo. Mvua kubwa
iliyonyesha kwa muda wa masaa matatu ilikuwa imeninyea chapachapa huku
nikiwa nimelalia tumbo langu juu ya tawi nene la mti mrefu na mkubwa aina ya LianaEntada gigas.
Mvua hiyo sasa ilikuwa imeacha athari kubwa za mafuriko ya kutisha na kelele
kali za vyura zilizokuwa zikihanikiza kila mahali pamoja na zile kelele nyingi za ndege
wa mwituni kama Mchochea mvua, Kitwitwi, Yombiyombi, Furukombe, Kanga,
Kware, Nderi, Tetere, Kirukanjia, Kulastara, Hondohondo, Kinega, Kuzumburu,
Gogota, Mnana, Mwewe, Vumatiti, Mwari, Kwarara na wengine wengi mara kwa
mara wakizikung’uta mbawa zao na kuzipa tena uhai sauti zao baada ya kusalimika na
athari za mvua hii kubwa ya aina yake.
Upepo mkali uliyokuwa ukivuma katika msitu huu uliliyumbisha tawi nililolilalia
huku na kule ukilisukasuka ovyo hata hivyo sikuliachia wala kukata tamaa kwani
kanuni za kijeshi zilinifunza uvumilivu hususani nikiwa kama mdunguaji makini
ninayehitaji matokeo mazuri ya kazi yangu.
Muda wa masaa tisa ulikuwa tayari umetokomea tangu nilipoukwea mti huu
mkubwa na mrefu msituni wenye maficho mazuri ya majani mengi makubwa
na matawi imara ya kuubeba uzito wangu bila wasiwasi wowote huku nikiendelea
kusubiri mtu au watu fulani nisiyokuwa na miadi nao wajichanganye kwenye targets
zangu ili niwachakaze vibaya kwa risasi.
Jicho langu la kazi kamwe halikuhama kwenye Eyepiece Lens ama sehemu ya kuona
ya durubini pandikizi yenye nguvu kali iliyokuwa juu ya bunduki yangu maalum ya
kudungulia adui.
Kwa kuwa nilikuwa naipenda sana kazi yangu hii hivyo nilikuwa nimechukua
vifaa vyangu vyote muhimu vya kazi kama bunduki yangu maalum ya kudungulia
adui ama Sniper Rifle aina ya 338 Lapua Magnum yenye uwezo wa kudungua bila bugdha
yoyote windo lililopo ndani ya umbali wa mita 1400 ama sawa na urefu wa viwanja
kumi na nne vya mpira wa miguu na iliyojazwa risasi za kutosha. Redio ya upepo ya
mkononi kwa ajili ya mawasiliano. Kisu chenye dira ama Compass/GPS. Kibuyu cha
maji ya kunywa ama Water Bladder. Filimbi ndogo. Dawa ya kujipaka mwilini kwa
ajili ya kujikinga na wadudu wabaya wenye sumu wa porini ijulikanayo kama Insects
Repellent. Min Thermometer. Mchanganyiko wa chakula chepesi lakini chenye kushibisha
kwa muda mrefu. Vifaa muhimu vya huduma ya kwanza. Vifaa vya kuzuia sauti kali
na wadudu wasiingie masikioni. Kurunzi ndogo mfano wa kalamu yenye mwanga
mkali iitwayo Penlight. Mlipuko mdogo wenye moshi mwingi ambao nikiutupa
hulipuka na kutoa wingu kubwa la moshi ili kumzuia adui asinione wakati nikitoroka
uitwao Chemical Mace. Rangi za kujipaka ili kujikinga nisionekane kwa urahisi na adui
iitwayo Camouflage Paste. Strobe Light ama mlipuko mwingine mdogo ambao nikiulipua
hewani hutoa mwanga mkali wa rangi tofauti pale inapotokea kuwa nimepoteana na
wenzangu ili waweze kufahamu nilipo au pale ninapohisi kuwa mbele yangu kuna
adui ili niweze kuyaona maficho yake na kummaliza. Pia kitabu kidogo na kalamu kwa
ajili ya kuandika mambo muhimu ya kazi yangu pamoja na Laser Ranger Finder ama
kifaa kidogo kinachotumika kutambulisha umbali wa adui.
Kwa muda wa siku tatu sasa nilikuwa sijatongoa lepe la usingizi wa kueleweka.
Mapigano yenye upinzani mkali yaliyodumu kwa muda wa siku tatu kati ya vikosi vya
jeshi la MONUSCO-Organization Stabilization Mission in Democratic Republic of the Congo
chini ya mwamvuli wa Umoja wa Mataifa UNFIB- The United Nations Force Intervention
Brigade na lile la waasi wa M23 yalikuwa yameniacha hoi taabani kwa uchovu. Hata
hivyo tulikuwa tumefanikiwa kuiteka miji mitatu muhimu kutoka mikononi mwa
waasi wa M23. Miji hiyo ikiwa ni mji wa Kitchanga, mji wa Nyiabiondo na mji wa
Kibati.
Kwa kiasi fulani uchovu niliokuwanao ulikuwa umemezwa na furaha ya mafanikio
binafsi niliyoyapata katika kazi yangu. Kwa muda wa wiki mbili tangu vikosi vyetu
vya MONUSCO vilipoanza operesheni zake za kupambana na waasi nilikuwa
nimefanikiwa kuwadungua wapiganaji 18 wa jeshi la waasi la M23 huku wachache
wakifanikiwa kunipa mgongo na kupotelea msituni. Hivyo bado kazi yangu ilikuwa
inaridhisha.
Nikiwa nimelala juu ya tawi la mti huu mrefu mawazo mengi yalikuwa yakipita
kichwani mwangu. Mawazo ambayo mara kwa mara yalikatishwa na sauti za sokwe
waitwao Bonobo na nyani aina ya Black Colobus, Golden Lion Tamarind, Black Titi, Proboscis,
Black-Crested Mangabey, Black-Crested Macaque-Macaca Nigra na Baboon waliokuwa
wakipiga kelele bila sababu ya kueleweka akilini mwangu.
Kuna wakati akili yangu ilipumbazwa kwa muda na kelele za maporomoko ya
maji yaliyokuwa jirani na eneo lile yakitokea sehemu za juu za misitu hii ya Ikweta.
Maporomoko hayo hatari yakisomba magogo,wanyama wa porini na takataka nyingine
za msituni lakini bado jicho langu halikuhama kwenye lenzi ya bunduki yangu.
Kwa muda wa takribani masaa matatu yaliyopita nilikuwa nimepitiwa na nyoka
hatari wenye sumu kali waliopo katika msitu huu kama Rhombic Night Adder, Rhinocero’s
Horned Viper, Albino Burmese Python, Green Mamba na African Bush Viper ambao walipita
mikononi mwangu, shingoni, kichwani, mgongoni na hatimaye kuendelea na safari
zao huku wakiniacha nimeganda kwenye tawi kama sanamu. Hali iliyopelekea mapigo
ya moyo wangu yasimame kwa sekunde kadhaa katika vipindi tofuati.
Kwa kweli msitu ulikuwa unatisha sana ingawa zile sauti za milipuko na kelele za
risasi zilikuwa zimekoma muda mfupi uliyopita baada ya adui kushindwa nguvu na
kukimbia.
Nilikuwa nimefanikiwa kuwadungua wapiganaji wawili wa M23 waliokuwa nyuma
ya gogo umbali wa mita takribani mia sita na ushei wakinitazama. Kazi ilikuwa rahisi
tu kwani risasi moja niliyoiruhusu ilipita katikati ya kioo cha darubini ya mmoja wa
adui wale kisha jichoni na kuufumua vibaya ubongo wake nikimlaza chali. Mwenzake
alinisumbua kidogo akijibanza nyuma ya mti mkubwa uliyokuwa pembeni ya eneo
lile. Sikutaka kuwa na haraka hivyo nilisubiri kwa muda mrefu nikitaka kumwaminisha
adui yule aliyesalia kuwa mambo yalikuwa sawia.
Baada ya kitambo kirefu cha kusubiri yule adui akafanya makosa ambayo
yalimgharimu. Akiamini kuwa mambo yalikuwa sawa sawia akachungulia katikati
ya tundu la mti lililotengenezwa na ndege wa porini aina ya Woodpecker. Jicho langu
makini likiwa kwenye Eyepiece Lens, mkono wangu wa kushoto ulikikamata kilimi cha
bunduki na ule wa kulia ukashika sehemu ya kurekebishia pembe nzuri ya shabaha
kwenye darubini ya juu ya bunduki ama Elevetion Adjastment Knob. Taswira ya adui yule
ilipoenea vizuri kwenye Objective Lens nikabana pumzi ya kutosha kisha nikavuta kilimi
cha Sniper Rifle na hapo kufumba na kufumbua matunda ya kazi yangu yakaonekana.
Risasi moja tu niliyoiruhusu ilipenya kwenye lile tundu la mti yule bwege alipokuwa
akichungulia kisha ikapita jichoni na kulifumua vibaya fuvu lake na hapo nikapapasa
katika mfuko wa gwanda langu la kijeshi na kuchukua pipi ya kijiti kisha nikaimenya
na kuitia mdomoni. Mambo yote yalikuwa kimyakimya kwani bunduki yangu ilikuwa
na kiwambo maalum cha kuzuia sauti ama Sound Suppressor.
Kwa upande huu wa msitu tulikuwa wadunguaji watatu makini kwenye mpango
wa Quick Reaction Force of Task, Group Alpha ya Brigade. Kati ya wadunguaji hao
watatu,wadunguaji wawili tulikuwa ni askari wa kutoka Tanzania Army Special Force.
Yaani mimi Koplo Tsega codename Lady butterfly na Sajenti Chacha Marwa codename
Chameleon. Mdunguaji mwingine akiwa ni wa kutoka jeshi la D.R Congo mwenye cheo
cha Private akifahamika kwa jina la Gina Yhombi-Opango Makiadi codename Lovebird.
Umbali wa kutoka hapa nilipo hadi alipokuwa mdunguaji mwingine ulikuwa si
chini ya mita mia tano na mara kwa mara tuliweza kuwasiliana kupitia redio zetu
za upepo katika kujulishana hali ya usalama ilivyokuwa ikiendelea. Kwa kweli
nilikuwa nimevutiwa sana na Private Gina Yhombi-Opango Makiadi kwa namna
alivyokuwa mpiganaji hodari ingawa alikuwa na umri mdogo zaidi yangu. Binti huyo
wa kikongomani alikuwa amepata shabaha zote wakati wa kufanya mazoezi hali
iliyonishangaza sana kwa uwezo wake mkubwa wa kulenga shabaha.
Nikiwa bado nimelala juu ya tawi hili mawazo mengi yalikuwa yakipita kichwani
mwangu huku nikikumbuka matukio yote yaliyotokea tangu nilipokuwa jijini Dar es
Salaam kabla ya majina yetu yaani mimi na Sajenti Chacha Marwa kupendekezwa
katika mpango wa amani wa hapa Kivu kaskazini nchini D.R Congo.
Sote tulikuwa kwenye tume maalum inayoshughulika na udhibiti na upambanaji
wa biashara haramu ya dawa za kulevya nchini Tanzania. Kwa muda wa miezi
sita tangu tulipojumuishwa kwenye tume hiyo ya kudumu tulikuwa si tu kwamba
tumeiletea mafanikio makubwa tume hiyo lakini pia tulikuwa tumetoa muelekeo
mzuri wa kuwatambua na kuwafikia wachuuzi wakubwa wa biashara hiyo haramu.
Hata hivyo kwa kuwa sisi hatukutaka mambo ya kisiasa katika kukabiliana na wale
washukiwa wa biashara hiyo hivyo mara kwa mara tulikuwa tukikutana na upinzani katika ufanyaji wa kazi yetu kama si kulaumiwa kuwa tulikuwa hatuzingatii misingi ya sheria za nchi na haki za binadamu katika kushughulika na janga hilo lililokuwa mbioni kuimeza kabisa nguvu kazi ya taifa.
Kwa kuzingatia ukubwa wa janga lenyewe tume yetu ilikuwa imeundwa na watu
wa kutoka idara tofauti kutegemeana na umuhimu wa uwepo wa watu hao. Askari wa
kutoka jeshi la wananchi wa Tanzania tulikuwa watatu;yaani mimi Koplo Tsega kutoka
kikosi 92 cha makomandoo Sangasanga mkoani Morogoro. Meja Khalid Makame
kutoka kambi ya kijeshi 521 ya Chukwani kisiwani Zanzibar na Sajenti Chacha Marwa
kutoka kikosi 36 cha kambi ya jeshi Msangani mkoani Pwani. Wengine walikuwa ni
wajumbe wa kutoka shirika la kimataifa la haki za binadamu-Human Rights Watch.
Mwanasheria wa serikali. Wajumbe kutoka idara ya usalama wa taifa. Wanasiasa
kutoka maeneo tofuati ya kiutendaji pamoja na askari polisi waandamizi akiwemo
kamishna mkuu wa jeshi la polisi na wawakilishi wa vijana.
Kitu kilichokuwa kimenishangaza sana ni kuwa wakati kazi yetu ikiwa mbioni
kutoa suluhisho la kudumu katika kukabiliana na biashara hiyo haramu ya dawa za
kulevya nchini Tanzania ndiyo tukapewa barua za kuingizwa kwenye mpango wa
amani ya kudumu hapa nchini D.R. Congo. Tena wanajeshi wote watatu tuliyokuwa
kwenye tume hiyo tukienguliwa bila sababu za kueleweka.
Kwa kuwa kazi yetu katika tume hiyo ilikuwa bado haijafikia ukomo na tulikuwa
tukielekea katika hatua nzuri zaidi ya kuwaweka bayana wafanyabiashara hao.
Tulijaribu kwa kila hali kupingana na hoja ya kujumuishwa kwetu kwenye mpango
wa amani ya kudumu ya hapa D.R Congo lakini hatimaye tuligonga mwamba
kwani viongozi wetu wa juu walitumia mamlaka yao kupingana na hoja zetu. Hivyo
hatukuweza kukaidi zaidi ya kutii amri zao kitendo ambacho kilinitia hasira sana. Hata
hivyo, sikuwa na namna kwani mojawapo ya misingi inayoliletea sifa kubwa jeshi letu
ni utii na nidhamu. Na sasa nilikuwa hapa eneo la Bunagana msituni juu ya mti mrefu
nikitekeleza wajibu wangu kwa taifa.
Niligeuka kuitazama saa yangu ya mkononi na hapo nikagundua kuwa ilikuwa
tayari imekwishatimia saa nane usiku na dakika chache mbele yake. Manyunyu hafifu
ya mvua yalikuwa yameanza kuanguka tena kutoka angani na kwa kweli sikupenda
mvua iendelee kunyesha katika msitu huu ingawa kunyesha kwa mvua kubwa lilikuwa
ni jambo la kawaida sana katika nchi za Ikweta kama nchi hii ya D.R Congo yenye
kilometa za mraba 2,345,410 hali ya hewa ya joto na baridi yenye wastani wa jotoridi
nyuzi 25 digrii sentigredi na wastani wa mvua kiasi cha sentimeta 130 hadi 200 kwa
mwaka ardhini.
Taa nyekundu ndogo iliyowaka haraka kwenye redio yangu ya upepo ikayahamisha
mawazo yangu na hapo nikageuka na kuitupia macho huku nikiitazama kwa mshtuko
kama niliyeshikishwa bomu. Taa ile ilikuwa na maana kuwa kulikuwa na simu
iliyokuwa ikiingia jambo ambalo lilikuwa la kawaida kabisa kutokea lakini sijui ni
kwanini nilishtuka sana.
Haraka nikaizungusha durubini yangu juu ya bunduki ku-scan taswira yoyote iliyokuwa eneo lile na hapo nikaona kuwa hali ilikuwa shwari hivyo nikabonyeza kitufe kwenye redio yangu ya upepo kuruhusu ile simu kuingia. Kwa kufanya hivyo
ile taa nyekundu ikapotea na kuwaka taa ya kijani halafu kukasikika sauti ya mvumo
wa upepo. Koo langu likakauka ghafla pale nilipokumbuka kuwa simu ya namna ile
ilikuwa ikitoka kwa mmoja wa wadunguaji wenzangu katika msitu huu. Ile sauti ya
mvumo wa upepo ilipokoma nikasikia sauti ya upande wa pili wa simu ambayo haraka
niliweza kuitambua kuwa ilikuwa ni sauti ya Sajenti Chacha Marwa codename Chameleon.
“Lady butterfly are you there? ...unanisikia?” sauti ya upande wa pili iliongea hata
hivyo niliitambua haraka kuwa sauti ile ilikuwa ikipwaya kwa hofu na iliyotawaliwa na
kitetemeshi…’Jambo la hatari?’ Nilijiuliza.
“Lady butterfly unanipata?” Ile sauti ikajirudia safari hii kwa nguvu kidogo.
“Ndiyo nakupata Chameleon, any trouble?” Nilimuuliza kwa wasiwasi.
“Yes! I got shot, very severely.”
“What!...umepigwa risasi?” Nilimuuliza kwa taharuki
“Ndiyo! Risasi mbili Lady Butterfly. Risasi moja imenipata begani na nyingine
imenitoboa sehemu ya kushoto kifuani sentimita chache mbali na moyo,” Chameleon
alizungumza kwa sauti hafifu ya kukoroma.
“Oh! My God uko wapi sasa?” Nilimuuliza.
“Nyuma ya jiwe umbali mfupi kutoka pale nilipokuwa,” Chameleon aliendelea
kuongea kwa shida huku sauti yake ikionekana kuzidi kupoteza mhimili.
“Okay! Hold on Sajenti am coming right now.”
“Don’t ever try to come here Lady Butterfly kwani inavyoonekana ni kuwa anajua tulipo
hivyo itakuwa kazi rahisi kwake.”
“Nani?” Nilimuuliza Chameleon kwa mshangao.
“Adui mdunguaji,” Chameleon aliendelea kuniweka bayana lakini sauti yake ilikuwa
ikizidi kuyoyoma.
“Nakuja!” Nilitaka kuzidi kumdadisi Chameleon lakini nilighairi wazo langu kwa
haraka kwani ningekuwa nikipoteza muda wangu na huwenda asingenijibu kutokana
na udhaifu wake.
Nilihisi kuwa bado kulikuwa na nafasi ya kuyaokoa maisha yake endapo ningeweza
kucheza na muda wangu vizuri ingawa maelezo yake yalikuwa na kiasi kikubwa cha
ukweli wa kunionya.
“Chameleon…! Chameleon unanisikia?” Niliita tena lakini mara hii sikujibiwa na
badala yake kwa mbali nilisikia sauti ya mikoromo yake hafifu.
“Chameleon unanisikia?” niliita tena lakini sauti ile upande wa pili ilipoteza uhai
na hapo huzuni ikaniingia moyoni. Machozi yaliyoanza kutafuta makazi machoni
mwangu nikayazuia kwa kufumba macho na kumeza funda kubwa la mate ili
kuitowesha hasira kifuani mwangu.
Bila kupoteza muda zaidi nikaikata ile simu kisha nikabonyeza tena vitufe kadhaa
vya simu yangu halafu nikaishikilia vizuri simu yangu. Baada ya kitambo kifupi cha
kusubiri ili simu yangu ipate signals nzuri za mawasiliano hatimaye ile simu ikaanza kuita tena upande wa pili huku nikitarajia kuisikia sauti ya mdunguaji mwingine Private Gina Yhombi-Opango Makiadi codename Lovebird. Hata hivyo hilo halikutokea kwani ile simu iliendelea kuita mara kadhaa pasipo kupokelewa. Kwa kweli nilijihisi
kuchanganyikiwa. Nikaikata ile simu na kuipigia tena huku nikiwa na kihoro cha aina
yake lakini bado ile simu haikupokelewa na tukio lile likazidi kuwa ishara mbaya zaidi
kwangu.
“Lovebird are you there?...zungumza Lovebird unanisikia?” niliendelea kuita lakini ni
kama niliyekuwa nikijiuliza mimi mwenyewe. Ile simu haikupokelewa wala sauti ya
Lovebird kusikika. Moyo wangu ukapiga kite kwa nguvu kisha koo likanikauka na hapo
baridi nyepesi ikaanza kusafiri taratibu nyuma ya mgongo wangu. Sikuwa na namna ya
kuendelea kusubiri zaidi hivyo nikaizima simu yangu ya upepo na kuichimbia kwenye
mfuko wa gwanda langu huku nikiwa nimeanza kuingiwa na hofu ingawa sikutaka
kupoteza umakini.
Muda mfupi uliyofuata nikaifyatua bi-pod stand ya bunduki yangu Sniper Rifle 338
Lapua Magnum na kuikunja vyema kisha nikaanza kujivuta taratibu nikiteleza kwenye
tawi lile la mti kwa ulaini kama Boomslang nyoka hatari kwa vipenyo. Kwa namna
nilivyojipamba kwa majani mwili mzima jicho lolote la kiumbe hai eneo lile lisingesita
kunifananisha na kichaka.
Kidole cha mkono wangu wa kushoto kikiwa kimekamata vyema kilimi cha Sniper
Rifle nikaifyatua kamba iliyokuwa kiunoni mwangu na kuifunga kwenye tawi imara
la mti kisha kwa msaada wa kamba hiyo nikaanza kushuka kwenye mti ule taratibu
huku mara kwa mara nikiweka vituo kutazama hali ya usalama wa eneo lile. Wakati
nilipokuwa nikikaribia kufika chini ya ule mti mara hisia mbaya zikanijia kuwa sehemu
fulani mbali kidogo kwenye msitu ule macho ya mtu fulani yalikuwa yakinitazama na
hali ile ikazidi kunipa wasiwasi. Hivyo nilipomaliza kushuka chini ya ule mti haraka
nikaivuta ile kamba na kuanza kuikunja na wakati nikifanya hivyo kiasi cha umbali wa
kama mita miamoja na ushei mbele yangu nikakiona kichaka kidogo kikichezacheza
baada ya mwanga mkali wa radi kumulika eneo lile.
Hofu ikazidi kunishika hivyo nilipomaliza kuikunja vizuri ile kamba nikajibanza
nyuma ya ule mti niliyoushuka muda mrefu uliyopita na bila shaka bahati ilikuwa
kwangu kwani ni muda uleule risasi iliniparaza begani na kuvunja tawi la mti uliyokuwa
jirani na eneo lile. Nikajua kuwa maficho yangu tayari yalikuwa yamefichuliwa. Adui
yule alikuwa mdunguaji mahiri sana aliyeweza kucheza vizuri na akili yangu. Ile risasi
moja aliyoifyatua alikaa kimya tena akitaka kuniaminisha kuwa nilikuwa nikiota juu ya
tukio lile au huwenda yale yalikuwa mawazo yangu.
Nilimuelewa vizuri na kwa kutaka kulithibitisha hilo nikautikisa kidogo mti mfupi
usawa wa kimo changu uliyokuwa jirani yangu kwa buti langu gumu mguuni. Mti ule
mfupi ulipotikisika risasi moja akakata vitawi vidogo vya mti ule na kuvipeperusha
hewani na hapo nikajua kuwa adui yule alikuwa mtu makini sana na kazi yake. Kisha
baada ya pale hali ya ukimya ikafuatia tena.
Wakati nikiwa nimejibanza nyuma ya ule mti sikutaka kujiridhisha kuwa pale nilikuwa sehemu salama. Mvua ilikuwa imeanza kunyesha tena sambamba na upepo mkali uliyoanza kuyumbisha matawi ya miti na vichaka vya eneo lile. Ilikuwa ahueni kwangu kwani adui yule mkorofi kwa vyovyote angepoteza umakini kwa kuyumba
kwa vichaka vile. Hivyo kwa kuichangamkia vizuri fursa ile nikajitupa chini na kuanza tutambaa kwa tumbo nikienda mbele kutoka usawa wa ule mti. Muda mfupi baadaye nikawa nimefanikiwa kujichomeka kwenye kichaka cha jirani na eneo lile. Niligeuka tena kutazama kule kwenye kile kichaka na sikuona chochote ingawa hali ile haikuweza kunithibitishia kuwa adui yule alikuwa amenisamehe.
Kichaka kile hakikuwa maficho mazuri ingawa kilinihifadhi kwa muda kidogo
kabla ya kutambaa tena na kuhamia kwenye kichaka kingine kilichoshiba miti zaidi
kilichokuwa eneo lile pembeni. Nikiwa katika kichaka kile niliitumia tena darubini ya
bunduki yangu kulichunguza eneo lile hata hivyo kwa kuwa ule mti niliyojibanza hapo
awali ulikuwa umenizuia kuona kule nyuma ilinibidi nihamie kwenye kichuguu kidogo
kilichokuwa mbele kidogo ya eneo lile.
Nikiwa nyuma ya kichuguu kile niliifyatua bi-pod stand ya Sniper Rifle na kuitega
vyema kisha kupitia darubini yake yenye nguvu nikaanza kufanya scaning makini eneo
lile. Sikuweza kuona kitu chochote eneo lile na hali ile ilinishangaza sana. Kile kichaka
ambacho hapo awali kilikuwa kikitikisika sasa kilikuwa kimetulia pia sikuweza kuona
kiumbe chochote eneo lile hivyo mwishowe nikakata tamaa kabisa huku nikiunyanyua
mkono kuitazama saa yangu ya mkononi na wakati nikifanya hivyo mwanga wa radi
uliyomulika eneo lile ukanisaidia kuona kule mbele.
Mtu fulani alikuwa amechepuka kutoka nyuma ya mti mmoja uliyokuwa eneo
lile na kwenda kujibanza nyuma ya mti mwingine kiasi cha umbali wa mita mia moja
na ushei mbele yangu na hapo nikatabasamu na kujifuta maji ya mvua yaliyokuwa
yakichuruzika uso wangu. Nikajilaza tena vizuri nyuma ya kichuguu kile kisha
nikalisogeza jicho langu kwenye Eyepiece Lens ya darubini ya Sniper Rifle na safari hii
nilichokiona kikanipelekea nizidi kutabasamu.
Yule mtu sasa alikuwa amejibanza nyuma ya ule mti na kwa kuwa ule mti ulikuwa
mwembamba kidogo ilikuwa ni sawa na mtu aliyejifunika shuka fupi kwani mabega
yake yalikuwa yakionekana. Yule mtu alikuwa amejikinga nyuma ya ule mti huku
akiitumia nafasi ile kujaza risasi kwenye bunduki yake na hilo lilikuwa kosa kubwa
kwani nilimjaza vizuri akaenea kwenye Objective Lens ya darubini yangu na hapo
nikavuta pumzi nyingi na kuibana. Risasi moja niliyoiruhusu ikaniletea majibu ya
hakika kwani risasi hiyo ilipenya kwenye bega lake la kulia kisha ikapekenya mfupa
wake na kuendelea mbele na safari. Yule mtu akapiga yowe kali huku bunduki yake
ikimponyoka mkononi na kuangukia chini na hapo akayumbayumba na kupoteza
mhimili. Hilo likawa kosa jingine kwani kwa kufanya vile kichwa chake kikaenea
vizuri kwenye lenzi ya darubini yangu. Tukio lile likanifanya nipige mruzi mwepesi
wa furaha. Risasi nyingine niliyoiruhusu kufunga safari ikakifumua vibaya kichwa cha
yule adui na kuutawanya vibaya ubongo wange huku yule adui akitupwa hewani. Jicho
langu bado halikuhama kwenye Eyepiece Lens ya darubini yangu hivyo yule mtu wakati akitua chini nikamkandamiza kwa risasi nyingine ya kifua iliyomlaza chali kimya. Kazi ikawa imekwisha hivyo nikaitoa pipi yangu ya kijiti kutoka mfukoni kisha nikaimenya na kuitia mdomoni.
Niliendelea kujibanza nyuma ya kile kichuguu huku jicho langu likiendelea kufanya kazi kwenye ile darubini kulichunguza eneo lile hadi pale niliporidhika kuwa hali ya usalama wa eneo lile ilikuwa shwari ndiyo nikachukua mashine yangu ya kazi na kusimama. Niliitazama tena saa yangu ya mkononi na kushtuka kuwa muda ulikuwa
umeenda tangu nilipoongea na Chameleon.
Niliichukuwa tena simu yangu ya upepo na kumpigia Chameleon lakini simu haikupokelewa. Nikampigia tena simu Lovebird lakini bado hali ilikuwa vilevile kwani ile simu yake haikupokelewa. Sikupenda kuendelea kupoteza muda zaidi hivyo muda mfupi uliyofuata nilikuwa nikiupangua msitu ule kwa mbio zisizo za kawaida.
Kwa kuwa nilikuwa nikiyafahamu vizuri maficho ya wenzangu hivyo sikupata shida katika kuwafikia. Nilimkuta Sajenti Chacha Marwa Code-name Chameleon akiwa ameegemea jiwe kubwa kando ya maficho yake na hapo nikajua kuwa baada ya
Chameleon kushambuliwa na adui alikuwa ametoroka kwa shida na kujificha nyuma
ya jiwe lile. Mdomo na macho yake vyote vilikuwa wazi ingawa nilipomsogelea na kumshika alikuwa wa baridi huku kifo tayari kikiwa kimemchukua. Damu nyingi kutoka kwenye majeraha yake ya risasi kifuani na begani ilikuwa imezitotesha vibaya gwanda zake. Kitu cha ajabu na kilichonishangaza ni kuwa Chameleon hakuwa na ile redio yake ya upepo wala ile silaha yake ya kudungulia adui na hali ile ilinitia mashaka
sana. Nilisimama kidogo nikimtazama Chameleon kwa huzuni kama mtu ambaye
nisingeweza kuonana naye tena hapa duniani. Sikuwa na jinsi hivyo nikamsogelea
pale alipoketi na kumfumba mdomo na macho yake huku nikizikumbuka enzi za
urafiki wetu tangu tulipoanza kufahamiana kwenye tume ya udhibiti na upambanaji
wa biashara haramu ya dawa za kulevya jijini Dar es Salaam. Hivyo nikaichukua kamera yangu ndogo na kumpiga picha chache kama sehemu ya kumbukumbu zangu za mwisho kwake.
Muda mfupi baadaye nilikuwa tena porini nikikimbia kuelekea kwenye maficho
ya mdunguaji mwingine Private Gina Yhombi-Opango Makiadi codename Lovebird.
Kwa kweli nilichokiona baada ya kufika kilizidi kupeleka simanzi moyoni mwangu.
Nilimkuta Lovebird akiwa ananing’inia mtini kama nyama ya ng’ombe kwenye mtungo buchani. Ni kama alikuwa kwenye jitihada za kushuka kutoka juu ya mti ule yalipokuwa maficho yake lakini hakuwa amefanikiwa kutimiza adhama yake. Risasi za adui zilimfumania wakati akiwa anakaribia kufika chini ya ule mti na hivyo kumuacha akining’inia kwenye kamba ile huku umauti ukiwa tayari umemfika. Mbaya zaidi ni
kuwa Lovebird hakuwa na kichwa na badala yake kilibakia kichuguu cha shingo yake
tu ambacho kwa wakati huu kilikuwa kikiendelea kuvuja damu taratibu. Risasi kali za
adui zilikuwa zimekifumua kichwa chake na kuutawanya ovyo ubongo wake.Roho iliniuma sana kwa kumpoteza rafiki yule mwenyeji wetu hata hivyo sikuwa na jinsi. Machozi yalinitoka wakati nikichukua picha zake kwa kamera yangu ndogo yadigital. Nilipoendelea kumchunguza vizuri Lovebird nikagundua kuwa kama ilivyokuwa
kwa Chameleon naye pia silaha yake na vitu vyake muhimu vilikuwa vimechukuliwa
bila shaka na adui. Kilichonisikitisha zaidi ni kuwa hata ile kamera yake kubwa ya
ki-uandishi wa habari vitani aina ya Toymaster ilikuwa imekwenda. Mbali na kuwa
mwanajeshi na mdunguaji mahiri Private Gina Yhombi-Opango Makiadi codename
Lovebird pia alikuwa mwandishi wa habari aliyeajiriwa na shirika la habari la The Reuters
kwa mkataba akichukua picha matukio ya vitani. Hivyo ile kamera ya kuchukulia
picha za matukio alikuwa amepewa na shirika hilo.
ITAENDELEA
shtholeNdio naanza kuisoma lakini imenipagawisha
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]the banker acha ujinga wa kitoto usitufanye sisi watoto wadogo mpumbavu wewe
Pumbavuuuuuuuuu!Ndio naanza kuisoma lakini imenipagawisha
Jamaa mjinga sana[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Yaani hapo ndio mnamfukuza kabisaaa[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]Jamaa mjinga sana
Kaweka mgomoYaani hapo ndio mnamfukuza kabisaaa[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Yaani hapo ndio mnamfukuza kabisaaa[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2]
Bora atukanweKaweka mgomo