idawa
JF-Expert Member
- Jan 20, 2012
- 25,284
- 38,364
- Thread starter
-
- #201
SEHEMU YA ISHIRINI NA NNE
"Ninachohitaji ni muda." Kassim Hashir aliendelea. Muda wa kubadili kila kitu. Kumuua Habib Kessy na kampuni yake na kuibuka mtu mpya na kampuni mpya yenye shughuli tofauti kabisa na shughuli za H.K.International."
"Utaweza kufanya hivyo?" Kembo akauliza.
"Kwa nini nisiweze. Iwapo kwanza nilikumuua Kassim Hashir? Ninachohitaji ni muda tu."
"Muda gani?"
"Mimi kugeuka mtu mwigine si tatizo. Nina paspoti nyingine maalum kwa dharura kama hii. Lakini kuuza na kufungua kampuni nyingine kubwa kama H.K.International na akaunta zake kutachukua muda."
"Ndiyo. Muda gani?"
"Kwa vyovyote vile siyo chini ya mwezi mmoja, pengine miwili."
"Jesus!"
"Jambo hili limetokea wakati mbaya sana. Tatizo ni kwamba kwa sasa ninabidhaa nyingi kuliko fedha taslimu. Na bidhaa nyingine ziko njiani. Kuna meli nzima ya makontena toka Ulaya bado haijawasili. Kuna meli nyingine ina magari zaidi ya miambili kutoka Japani iko njiani. Meli nyingine mbili zina malighafi toka Afrika bado hazijatia nanga Ulaya. Vitu vyote hivyo vina thamani ya mamilioni kwa mamilioni kama si mabilioni ya pesa za kigeni. Na sina ujanja hadi vifike vinakokwenda. Kama ni Mungu amepanga jambo hili litokee wakati huu ni yeye pekee anayejua. Nahitaji muda vibaya sana."
"Mambo yakituchachia," Kembo akasema. "Hapatakuwa na muda wowote."
"Hayawezi kutuchachia iwapo tutavitumia vichwa vyetu wenyewe vizuri. Wa kuwashughulikia ni wawili tu. Fensy na huyo Daktari mstaafu."
"Umemsahau mtu wa tatu."
"Mtu wa tatu?" Kassim aliuliza.
"Ndiyo. Huyo kijana X aliyempeleka Dikwe Uwanja wa Gofu."
"Oh!"
"Lakini yeye si tishio. Kamuonea Dikwe kwa sababu Dikwe alikuwa pusha wa kawaida tu, tena mwanafunzi aliyetegemea kisu. Hakuwa katika daraja la Chiko na Fensy."
"Kwa hiyo?"
"Ni moja kati ya mawili kwa kijana huyo. Anunuliwe au alipuliwe chaguo ni lake."
"Kwa hiyo tatizo liko kwa Dokta Makete ?" Kassim aliuliza.
"Hapana. Tatizo lipo kwa Fensy. Ni kweli akishikwa mambo yanaweza kuwa mabaya."
"Kwa nini asifikwe na 'ajali'?"
"Nitafikiria. Kwa sasa atapiga mbizi. Sitaki kupoteza wangu ovyo. Nilipo nina pengo la mmoja."
"Hoza."
"Ndiyo."
Baada ya kupuliza moshi angani, Kassim akasema, "Umesema huyo Dk .Mstaafu si tatizo?"
"Si tatizo. Nilifanya kosa pale mwanzo kumtuma Hoza aende hospitalini na kibweka. Nilipaswa kumpeleka Daktari wa bandia."
"Na sindano ya sumu?"
"Yes."
"Good. I'll fix you up with BMV - Black Mamba Venom. Hutumiwa na Vets [Madaktari wa wanyama] kuwaulia mbwa,farasi n.k. wenye maumivu makali ambao hawana matumaini ya kupona. Ni safi sana. Sekunde thelathini, garantii."
*****************************
Kwa sauti madhubuti kabisa Butu akasema, "Humo chumbani mwa shangazi mna radio. Katika taarifa ya habari ya saa kumi ilitangazwa ajali ya Dk.Makete. Ikatangazwa ile zawadi ya milioni moja kwa yeyote atakayemtaja mtu aliyemgonga Dokta huyo. Kikoti akapandwa na jazba, akidai anamfahamu mtu huyo. Na kuwa ndiye mwajiri wake. Akatuomba tumsaidie kuipata hiyo zawadi."
Bessy na Dennis wakatazamana, macho ya msichana huyo yakiwaka moto kwa ghadhabu. Dennis akarudisha macho kwa Butu na kumwambia, "Endelea."
"Bob akaingiwa na tamaa. Akataka kujua kama huyo mwajiri wake alikuwa tajiri wa kuweza kutoa milioni mbili au tatu za kufumba mdomo. Kikoti akamhakikishia kuwa ni tajiri sana, na kwamba angeweza kutoa hata zaidi. Bob akasema basi ya nini kudai milioni ikiwa wanaweza kupata milioni mbili au tatu.
"Nikajaribu kuwakataza." Butu akaendelea, "Naapa niliwakataza, lakini hawakukubali. Bob akanambia niachane nao na nisimwambie mtu yeyote. Nikaondoka na kuwaacha."
Bessy akatikisa kichwa. "Butu, Butu, Butu! Na ukabaki kimya kweli!"
"Ningefanyeje, afande? Bob alikuwa rafiki yangu mkubwa. Nisingeweza kumsaliti. Lakini baada ya kuwaza usiku kucha nilipania kumlazimisha aje kukuona asubuhi. Angekataa, mimi ningekuja kuripoti. Lakini asubuhi hakuwepo nyumbani kwake. Na nilipofika hapa kituoni nikapata habari kuwa kauwawa. Nikapapatika, nisijue la kufanya."
"Unajua ni lazima nikuweke ndani na kukufungulia shitaka la kuficha siri za uhalifu?" Butu hakujibu. "Kwa vyovyote vile" Bessy akaendelea, "Umeshakwishapoteza kazi yako. Hustahili kuwa askari."
Denny akauliza, "Ni nani huyo mwajiri wa Kikoti?"
"Simjui." Butu akajibu kinyonge. "Kikoti alimwita Bwana Kessy. Jina hilo moja tu."
"Kwa hiyo uliongopa uliposema hakuwa na kazi maalumu?" Bessy akauliza.
"Hapana hata kwa huyo Bwana Kessy nadhani alikuwa kibarua tu. Hakuwa na muda mrefu hapa jijini."
"Alikuwa anafanya kazi gani kwa huyo Kessy?"
"Nadhani alikuwa mtumishi wa nyumbani."
"Sehemu gani hiyo?"
"Nadhani itakuwa Buffalo Hill."
"Nadhani. Nadhani. Nadhani. Ni msaada mkubwa kweli kweli !" Bessy alifoka. Akaongeza, "Na alipokuwa akiishi Kikoti hukujui?"
Butu akatikisa kichwa.
"Ona sasa! Katika kuogopa kumsaliti ndugu yako, umeyaponza maisha yake!"
"Najuta sana, afande, najuta sana."
"Majuto ni mkuu." Bessy alisema kwa ghadhabu.
"Hayasaidii chochote. Angalia ulivyoboronga! Tulikuwa na nafasi ya kuwabamba wote. Huyo aliyemgonga Dk.Makete, hao wauaji, huyo Bob pamoja na Kikoti wake. Na sasa tuko wapi? Pale pale tulipoanzia!"
"Butu," Denny aliita kwa sauti tulivu kabisa. "Unadhani kitu gani kilitokea pale kwa shangazi Suzy baada ya wewe kuondoka?"
"Sijui,Luteni."
"Hukuisikia mipango ya Bob na Kikoti?"
"Hata kidogo. Sikutaka kujihusisha na mipango ya kifumba mdomo."
"Afadhali ungesuburi uisikie mipango yao pengine tungejua anapoishi huyo mlaaniwa!" Bessy alilalama.
Kama vile msichana hakuwa amesemalolote, Denny akaendelea kwa sauti yake tulivu. "Tunafahamu kuwa mtu aliyemgonga ni Kassim Hashir, lakini anatumia jina jingine. Jina Kassim Hashir lilishakufa siku nyingi. Umenielewa Butu?"
"Ndiyo, Luteni."
"Sasa, kama mwajiri wa Kikoti ndiye aliyemgonga babangu na naamini ndiye, ama sivyo Bob na Kikoti wasingeuwawa. Na kama mwajiri wa Kikoti anaitwa Kessy,basi ndiye Kassim Hashir. Sawa Butu?"
"Sawa, Luteni."
"Ni jambo linalofahamika dhahiri kuwa Kassim Hashir, kwa jina jingine Kessy ni mtu mbaya kweli kweli. Ni mnyama. Na anawakora wauaji. Watatu tunawafahamu. Chiko,Fensy na Hoza. Huyo wa tatu sasa ni marehemu. Inspekta Bessy akamuwahi. Je, haikujii akilini mwako kuwa waliowaua Bob na Kikoti ni Chiko na Fensy?"
"Inawezekana kabisa." Alikubali Butu.
Denny akamtazama Bessy na kumwambia, "Tafadhali uliza chumba cha kumbukumbu kama wana faili la Fensy" Bessy akainua simu na kuzungumza na masijala. Kisha akaurudisha chini mkono wa simu,akitikisa kichwa. "Hawana."
"Si kitu." Alisema Denny. "Waambie makachero wako waanze kuwasaka Chiko na Fensy."
Bessy akainua tena mkono wa simu.
Itaendelea
"Ninachohitaji ni muda." Kassim Hashir aliendelea. Muda wa kubadili kila kitu. Kumuua Habib Kessy na kampuni yake na kuibuka mtu mpya na kampuni mpya yenye shughuli tofauti kabisa na shughuli za H.K.International."
"Utaweza kufanya hivyo?" Kembo akauliza.
"Kwa nini nisiweze. Iwapo kwanza nilikumuua Kassim Hashir? Ninachohitaji ni muda tu."
"Muda gani?"
"Mimi kugeuka mtu mwigine si tatizo. Nina paspoti nyingine maalum kwa dharura kama hii. Lakini kuuza na kufungua kampuni nyingine kubwa kama H.K.International na akaunta zake kutachukua muda."
"Ndiyo. Muda gani?"
"Kwa vyovyote vile siyo chini ya mwezi mmoja, pengine miwili."
"Jesus!"
"Jambo hili limetokea wakati mbaya sana. Tatizo ni kwamba kwa sasa ninabidhaa nyingi kuliko fedha taslimu. Na bidhaa nyingine ziko njiani. Kuna meli nzima ya makontena toka Ulaya bado haijawasili. Kuna meli nyingine ina magari zaidi ya miambili kutoka Japani iko njiani. Meli nyingine mbili zina malighafi toka Afrika bado hazijatia nanga Ulaya. Vitu vyote hivyo vina thamani ya mamilioni kwa mamilioni kama si mabilioni ya pesa za kigeni. Na sina ujanja hadi vifike vinakokwenda. Kama ni Mungu amepanga jambo hili litokee wakati huu ni yeye pekee anayejua. Nahitaji muda vibaya sana."
"Mambo yakituchachia," Kembo akasema. "Hapatakuwa na muda wowote."
"Hayawezi kutuchachia iwapo tutavitumia vichwa vyetu wenyewe vizuri. Wa kuwashughulikia ni wawili tu. Fensy na huyo Daktari mstaafu."
"Umemsahau mtu wa tatu."
"Mtu wa tatu?" Kassim aliuliza.
"Ndiyo. Huyo kijana X aliyempeleka Dikwe Uwanja wa Gofu."
"Oh!"
"Lakini yeye si tishio. Kamuonea Dikwe kwa sababu Dikwe alikuwa pusha wa kawaida tu, tena mwanafunzi aliyetegemea kisu. Hakuwa katika daraja la Chiko na Fensy."
"Kwa hiyo?"
"Ni moja kati ya mawili kwa kijana huyo. Anunuliwe au alipuliwe chaguo ni lake."
"Kwa hiyo tatizo liko kwa Dokta Makete ?" Kassim aliuliza.
"Hapana. Tatizo lipo kwa Fensy. Ni kweli akishikwa mambo yanaweza kuwa mabaya."
"Kwa nini asifikwe na 'ajali'?"
"Nitafikiria. Kwa sasa atapiga mbizi. Sitaki kupoteza wangu ovyo. Nilipo nina pengo la mmoja."
"Hoza."
"Ndiyo."
Baada ya kupuliza moshi angani, Kassim akasema, "Umesema huyo Dk .Mstaafu si tatizo?"
"Si tatizo. Nilifanya kosa pale mwanzo kumtuma Hoza aende hospitalini na kibweka. Nilipaswa kumpeleka Daktari wa bandia."
"Na sindano ya sumu?"
"Yes."
"Good. I'll fix you up with BMV - Black Mamba Venom. Hutumiwa na Vets [Madaktari wa wanyama] kuwaulia mbwa,farasi n.k. wenye maumivu makali ambao hawana matumaini ya kupona. Ni safi sana. Sekunde thelathini, garantii."
*****************************
Kwa sauti madhubuti kabisa Butu akasema, "Humo chumbani mwa shangazi mna radio. Katika taarifa ya habari ya saa kumi ilitangazwa ajali ya Dk.Makete. Ikatangazwa ile zawadi ya milioni moja kwa yeyote atakayemtaja mtu aliyemgonga Dokta huyo. Kikoti akapandwa na jazba, akidai anamfahamu mtu huyo. Na kuwa ndiye mwajiri wake. Akatuomba tumsaidie kuipata hiyo zawadi."
Bessy na Dennis wakatazamana, macho ya msichana huyo yakiwaka moto kwa ghadhabu. Dennis akarudisha macho kwa Butu na kumwambia, "Endelea."
"Bob akaingiwa na tamaa. Akataka kujua kama huyo mwajiri wake alikuwa tajiri wa kuweza kutoa milioni mbili au tatu za kufumba mdomo. Kikoti akamhakikishia kuwa ni tajiri sana, na kwamba angeweza kutoa hata zaidi. Bob akasema basi ya nini kudai milioni ikiwa wanaweza kupata milioni mbili au tatu.
"Nikajaribu kuwakataza." Butu akaendelea, "Naapa niliwakataza, lakini hawakukubali. Bob akanambia niachane nao na nisimwambie mtu yeyote. Nikaondoka na kuwaacha."
Bessy akatikisa kichwa. "Butu, Butu, Butu! Na ukabaki kimya kweli!"
"Ningefanyeje, afande? Bob alikuwa rafiki yangu mkubwa. Nisingeweza kumsaliti. Lakini baada ya kuwaza usiku kucha nilipania kumlazimisha aje kukuona asubuhi. Angekataa, mimi ningekuja kuripoti. Lakini asubuhi hakuwepo nyumbani kwake. Na nilipofika hapa kituoni nikapata habari kuwa kauwawa. Nikapapatika, nisijue la kufanya."
"Unajua ni lazima nikuweke ndani na kukufungulia shitaka la kuficha siri za uhalifu?" Butu hakujibu. "Kwa vyovyote vile" Bessy akaendelea, "Umeshakwishapoteza kazi yako. Hustahili kuwa askari."
Denny akauliza, "Ni nani huyo mwajiri wa Kikoti?"
"Simjui." Butu akajibu kinyonge. "Kikoti alimwita Bwana Kessy. Jina hilo moja tu."
"Kwa hiyo uliongopa uliposema hakuwa na kazi maalumu?" Bessy akauliza.
"Hapana hata kwa huyo Bwana Kessy nadhani alikuwa kibarua tu. Hakuwa na muda mrefu hapa jijini."
"Alikuwa anafanya kazi gani kwa huyo Kessy?"
"Nadhani alikuwa mtumishi wa nyumbani."
"Sehemu gani hiyo?"
"Nadhani itakuwa Buffalo Hill."
"Nadhani. Nadhani. Nadhani. Ni msaada mkubwa kweli kweli !" Bessy alifoka. Akaongeza, "Na alipokuwa akiishi Kikoti hukujui?"
Butu akatikisa kichwa.
"Ona sasa! Katika kuogopa kumsaliti ndugu yako, umeyaponza maisha yake!"
"Najuta sana, afande, najuta sana."
"Majuto ni mkuu." Bessy alisema kwa ghadhabu.
"Hayasaidii chochote. Angalia ulivyoboronga! Tulikuwa na nafasi ya kuwabamba wote. Huyo aliyemgonga Dk.Makete, hao wauaji, huyo Bob pamoja na Kikoti wake. Na sasa tuko wapi? Pale pale tulipoanzia!"
"Butu," Denny aliita kwa sauti tulivu kabisa. "Unadhani kitu gani kilitokea pale kwa shangazi Suzy baada ya wewe kuondoka?"
"Sijui,Luteni."
"Hukuisikia mipango ya Bob na Kikoti?"
"Hata kidogo. Sikutaka kujihusisha na mipango ya kifumba mdomo."
"Afadhali ungesuburi uisikie mipango yao pengine tungejua anapoishi huyo mlaaniwa!" Bessy alilalama.
Kama vile msichana hakuwa amesemalolote, Denny akaendelea kwa sauti yake tulivu. "Tunafahamu kuwa mtu aliyemgonga ni Kassim Hashir, lakini anatumia jina jingine. Jina Kassim Hashir lilishakufa siku nyingi. Umenielewa Butu?"
"Ndiyo, Luteni."
"Sasa, kama mwajiri wa Kikoti ndiye aliyemgonga babangu na naamini ndiye, ama sivyo Bob na Kikoti wasingeuwawa. Na kama mwajiri wa Kikoti anaitwa Kessy,basi ndiye Kassim Hashir. Sawa Butu?"
"Sawa, Luteni."
"Ni jambo linalofahamika dhahiri kuwa Kassim Hashir, kwa jina jingine Kessy ni mtu mbaya kweli kweli. Ni mnyama. Na anawakora wauaji. Watatu tunawafahamu. Chiko,Fensy na Hoza. Huyo wa tatu sasa ni marehemu. Inspekta Bessy akamuwahi. Je, haikujii akilini mwako kuwa waliowaua Bob na Kikoti ni Chiko na Fensy?"
"Inawezekana kabisa." Alikubali Butu.
Denny akamtazama Bessy na kumwambia, "Tafadhali uliza chumba cha kumbukumbu kama wana faili la Fensy" Bessy akainua simu na kuzungumza na masijala. Kisha akaurudisha chini mkono wa simu,akitikisa kichwa. "Hawana."
"Si kitu." Alisema Denny. "Waambie makachero wako waanze kuwasaka Chiko na Fensy."
Bessy akainua tena mkono wa simu.
Itaendelea