Riwaya: Msako wa Hayawani

Huku kumekuwa kama nyumba ya ibada mweeeeh! Idawa kama unakitabu niambie nikutafute vp nijipatie copy yangu maana hali ni mbaya wallah
 
Daaah! Mkuu idawa, kama ndio huo umeme au majukumu bac na mungu ashukuliwe
 
SEHEMU YA KUMI NA NANE.


Pamoja na hekaheka zote za usiku, Denny aliamka mapema, akaoga, akavaa na kumuaga mamake. "Nakwenda hospitalini. Hapana haja ya kwenda sote asubuhi hii, wewe utakwenda baadaye."
"Sawa." Alijibu mamake kwa sauti yake ndogo. "Naandaa kifungua kinywa."
"Vizuri kabisa. Nitakaporuridi nitakuwa nimebanwa na ubao." Denny alijibu kumchangamsha mamake ambaye aliguna tu na kwenda jikoni.


Denny akatoka na kuingia garini. Dakika chache baadaye akaliegesha gari nje ya hosptali ya kuu ya taifa. Akaukuta mlango wa chumba cha babake ukiwa wazi, Dk. Beka akimkagua mgonjwa, akamuamkia "Shikamoo mjomba."
"Marahaba Denny," alijibu Dk. Beka, "Karibu"
"Asante." Denny akasimama akimwangalia babake aliyelala ametulia tuli akipumua taratibu.
"Ganzi imeshamtoka." Alielekeza daktari huyo.
"Nimemdunga sindano ya usingizi. Alipozinduka tulizungumza maneno machache." (Kama vile alikuwa anahitaji ushauri wangu)!


"Lakini ukweli ni kwamba anahitaji mapumziko kadri iwezekanavyo. Ukumbuke hilo. Akiamuka usizungumze naye sana."
Denny akakubali kwa kichwa. Akauliza. "Nini hali yake kiujumla?"
"Ni ya kuridhisha kabisa. Hayuko katika hali mbaya. Naamini baada ya wiki mbili au tatu, sanasana wiki nne atarudi nyumbani."
"Akitembea mwenyewe?"
"Denny usitazamie babako kutembea mwenyewe hivi karibuni. Kwa vyovyote sio chini ya mwaka mmoja." Dk.Beka akainuka. Akauliza , "Mamako ana hali gani?"
"Hajambo. Ni mnyonge tu."
"Ni jambo linaloeleweka alisema." Alisema Dk. Beka.
"Tutaonana baadae. Nakwenda kuhudumia wagonjwa wengine."


Mara tu baada ya Dk. Beka kutoka, Bessy akaingia
"Denny!" Denny aliekuwa ameketi akainua uso. "Bessy alfajiri yote hii!"
"Denny kuna mambo yasiyo ya kawaida yametokea jana usiku." Alisema msichana huyo. Kisha akakumbuka ustaarabu. "Lakini kwanza, vipi hali ya mzee?"
"Hajambo. Dk.Beka amemaliza kumkagua sasa hivi. Ni mambo gani yaliyotokea jana?"


"Mengi yametokea jana usiku, kama kawaida ya jiji hili. Lakini mawili si ya kawaida. Askari mmoja, Sajini Bob, amekutwa ameuwawa nje ya gari lake karibu na daraja la Singisa. Ndani ya gari mlikuwa na maiti nyingine. Wote wamepigwa risasi."
"Na tukio jingine?"
"Pusha mmoja aliyetambulika kwa jina la Dikwe amekutwa kaliwa na fisi kwenye Uwanja wa Gofu. Mawindo ya kawaida ya pusha huyo ni nje ya Tupetupe Hoteli."
"Sikioni cha ajabu."
"Denny! Jana usiku ulifika Tupetupe."
"Kwa hiyo?"
"Denny kama ni wewe ulimpeleka Dikwe Uwanja wa Gofu, unacheza mchezo mchafu."
"Kumgonga babangu kwa gari ni mchezo safi? Kutaka kumwua akiwa mahututi kitandani ni mchezo safi?"
"Unakili kuwa ni wewe uliyempeleka Dikwe Uwanja wa Gofu?"
"Sikili chochote. Akh, Bessy, kumetukuchia vibaya. Twende zetu nyumbani tukafungue kinywa. Hukuja na mtu yoyote wa kumlinda wa kumlinda babaangu?"
"Askari mmoja yuko nje. Twende zetu."


**************************************

Mara tu Denny alipoufungua mlango wa mbele, pua zao zikadaka harufu tamu ya staftahi. Akaita. "Mama, nimekuja na Bessy."
"Karibuni huku jikoni." Mama Denny alijibu. "Kila kitu kiko tayari." Wakaingia jikoni. Bessy akasema. "Shikamoo mama."
"Marahaba Bessy, karibu. Utapenda mayai ya kukaanga au macho ya ng'ombe?"
"Macho ya ng'ombe. Lakini si ungeniachia niyatengeneze mwenyewe?"
"Hapana. Labda iko siku jiko hili litakuwa lako. Lakini kwa leo acha nikuandalie. Ketini."


Denny Bessy wakatazamana wakiketi. Bi mkubwa akauliza. "Kaamukaje mzee wenu?"
"Kaamuka vizuri kabisa." Alijibu Denny. "Ganzi imemtoka, lakini mjomba amekataza kuzungumza naye kabisa. Amemdunga sindano ya usingizi. Ukumbuke utakapokwenda usizungumze naye sana. Anahitaji mapumziko. Mjomba amesema anaweza kurudi nyumbani baada wiki mbili au tatu tu."
"Lakini hatakuwa yeye yule tene." Alisema Bi mkubwa kwa sauti nzito.
"Ndiyo, utapita muda ndiyo aweze kutembea mwenyewe. Pengine mwaka mzima."
"Siyo kutembea tu."


Denny akainua uso na kumtazama mama yake. Macho yake yakimsaili. Yakionyeshwa kutatanishwa. Baada ya kimya cha muda, Bi mkubwa akasema. "Nimemwota yule msichana." Alisema hayo kwa sauti nzito zaidi. Iliyojaa majonzi. Sura yake ilikuwa kama hakuwa hapo, yaani mbali sana.
"Msichana gani?" Denny akauliza alipomwona mamake haendelei.
"Aliyeuliwa na Kassim Hashir." Alijibu Bi mkubwa. "Ameniomba...hapana. Ameniamuru nikueleze kisa chote, bila ya kukuficha lolote."
"Kisa cha huo uhasama kati ya baba na huyo Kassim Hashir?"
"Ndiyo."


Denny akasuburi, nusu akiwa na shauku ya kukisikia kisa hicho,nusu akimhofia mama yake. Akimhurumia kusimulia kisa ambacho dhahiri ni kichungu. Akasema. "Mama ,hatuwezi kusubiri mpaka baada ya kula?"
"Unadhani nitatokwa na machozi tena?" Bi mkubwa akatikisa kichwa. "Kipindi cha majonzi kimepita. Nimelia kiasi cha kutosha jana usiku. Usingizini, wakati nikiota ndoto hiyo. Nahisi kuishiwa kabisa na machozi."


Baada ya kimya kifupi Bi mkubwa akaendelea.
"Ilikuwa ni miezi michache tu baada ya mimi na Ray kufunga ndoa. Siku moja msichana huyo akaja hospitalini. Akatukuta mimi nikiwa nesi wa zamu na Ray daktari wa zamu."
"Alikuwa msichana wa kati ya miaka kumi na sita na nane aliyevaa sare za sekondari. Akampa Ray karatasi..."
"Dk.Raymond Makete, wakati huo akiwa kijana kabis, akakipokea kikaratasi hicho. Akakisoma, kiliandikwa, 'Daktari wa zamu, mshughulikie msichana huyo. Kassim Hashir.'


Hakuna hata tafadhali. Wakati huo Kassim Hashir alikuwa kigogo serikalini, mtu wa kuogopwa. Ukimuudhi yeye, umemwudhi fasishti Ibrahim Mbelwa. Ungeweza kuhatarisha maisha yako,au ukatupwa kizuizini na kuteswa kikatili. Dk. Makete akamuuliza msichana huyo, 'Kwani una matatizo gani?'
"Msichana akanong'ona maneno ambayo Makete hakuyaelewa. Akamwuliza, 'Kitu gani?' 'Nna mimba.' alisema msichana huyo kwa sauti ndogo sana.


'Hilo si tatizo, Makete akamwambia. Ni kawaida kwa mwanamke kupata mimba. Au inakusumbua?'
'Hapana'
'Kumbe?'
'Ni ya Kassim.'
'Kwa hiyo.'
'Haitaki. Kanambia niitoe.'
'Hiyo ni bahati mbaya sana. Hapa hatufanyi kazi ya kuua, tunafanya kazi ya kuokoa maisha.'
"Msichana akaumauma mdomo wake wa chini machozi yakimlengalenga.
Dk. Makete akamwuliza, 'Ni ya miezi mingapi?'
'Mnne.'


'Nakushauri usiende ukajaribu kuitoa wewe mwenyewe huko nyumbani.'
'Lakini ningali nasoma'
'Itakubidi uache shule.'
'Babangu...babangu!'
"Dk. Makete akatisa kichwa...'Nashindwa kuelewa kwa nini mnafanya mambo haya na hali mkijua kuwa matokeo yake ni matatizo matupu!'
"Msichana akageuka aondoke."
'Sikiliza!'
"Akageuka tena."
"Pia nakushauri usirudi kwa Kassim Hashir." Dk. Makete alimwambia msichana huyo. "Kassim Hasshir si binadamu. Ni mnyama. Ameshaua watu kadhaa, mmojawapo akiwa babake mzazi."


"Miezi mitatu au mine ikapita." Mama Denny aliendelea kusimulia kisa hicho kwa sauti yake ndogo, ya chini, iliyojaa majonzi. Alizungumza kama anayeota, au mtu anaye zungumza peke yake, kichwa kakiinamisha kama mtu anayesali.
Denny na Bessy wakaendelea kuganda. Hawali,hawaongei,hawakohoi. Hata kupumua hawakupumua kikawaida. Zilikuwa pumzi ndefu, waliziachia pale tu ilipolazimu, haiwezekani tena kuibana. Walikuwa kama watu wanaoangalia sinema ya kusikitisha sana.


Lakini hawakuwa wanasikitishwa na kisa chenyewe. Kwanza. kilikuwa hakijafika mbali. Hadi hapo hapakuwa na chochote cha kuwasikitisha. Miaka nenda, miaka rudi, daima wasichana wasomao walilifanya kosa hilo alilolifanya msichana huyo anayesimuliwa. Kwa sababu moja au nyingine, wanafunzi hufanya mapenzi , hushika mimba, na kuzitoa. Lilikuwa jambo la kawaida kabisa. Na pengine litakuwa hivyo mpaka mwisho wa dunia.
Pili kisa chenyewe kilitoke zamani sana, pengine kabla ya wao kuzaliwa. Na tatu, na hili lilikuwa mhimu zaidi kwao, kisa hicho, kadri walivyokitambua wao, hakikuwahusu sikio wala ndewe.


Kilichowasikitisha wao ni jinsi Bi mkubwa huyo mwenye mvi za kurashia, sura karimu na sauti adhimu ilivyosikitisha. Ni dhahiri alikuwa katika wakati mchungu mno sasa na hapo kale. Kidhati walitamani asiendelee na simulizi ile, lakini midomo yao ilikuwa mizito kama iliyoshonwa.
"Mama.." Denny akajikuta akiupanua mdomo wake, kwa juhudi kubwa "Mama..."
Bi mkubwa akatikisa kichwa, bila ya kukiinua.
"Nakwambia kaniamuru." Akasema kwa sauti ndogo, na ya chini.


"Mama, hakuna mtu yeyote duniani wa kukuamuru kufanya jambo usilotaka kulifanya." Denny akiwa wima, ganzi ya uzezeta ikiwa imemtoka. "Hakuna, si mimi, si baba, si yeyote."
"Denny, aliyeniamuru hayuko duniani."
"Ooh, ndoto! Mama!" Denny akaliza ulimi. Si songo, si bezo. Ni masikitiko tu. "Mama, kwa kweli unanishangaza. Sikutazamia kama ungeweza kuwa mtu wa kuweza kusumbuliwa na ndoto."
"Denny, haikuwa ndoto ya kawaida."
"Kuna ndoto za kawaida na zisizo za kawaida?"


"Ndiyo, Denny. Hata mimi nilikuwa silijui hilo. Hata mimi ningebisha, lakini hii haikuwa ndoto ya kawaida. Sijapata kuota ndoto kama hii. Nyinyi pia hamjapata. Si kila mtu humjia. Hii si ndoto,ni kama ... kama maono."
"Vizuri, utatusimulia siku nyingine. Sasa acha tuendelee na kula."
"Na hali jana mlinibembeleza niwasimulie!" Akakumbusha Bi mkubwa.
"Ooh, sasa si mhimu tena.Dakika yoyote ile sasa tutamshika huyo firauni. Isitoshe, baba ameshazinduka. Atatusimulia yeye kisa hicho."
"Baada ya wiki mbili au tatu?"
"Nakuambia sasa si muhim tena."
"Hapana, Denny huyo msichana kaniamuru na nimemwaidi. Anajua mimi sivunji ahadi. Kwa hiyo keti usikilize."


"Mama, unataka kunilazimisha kusikiliza kisa cha kipumbavu na kisichonihusu?"
"Laiti ungejua!" Uso ukambadilika Denny.
"Naam?"
"Laiti ungejua." Bi mkubwa alirudia kwa sauti yake ndogo.
"Laiti ungejua. Na hilo tatizo lenyewe."
Denny akapumua na kurudi kitini.


Cc chiko Joharia gspace

Itaendelea
 
Last edited by a moderator:
SEHEMU YA KUMI NA TISA.

Kembo alikuwa anatoka bafuni kuoga, kengele ya simu ilipolia sebuleni. Akajifunga taulo vizuri na kuokota mkono wa simu. Akasema, "Yees?"
"Mzee, mimi ni chiko."
"Kitu gani asubuhi yote hii?" Kembo aliuliza kwa ikirahi, akijua ni masula ya pesa tu.
"Mzee, lazima nikuone. Mambo si mazuri." Alijibu chiko.
"Unamaana gani?"
"Hoza amekufa. Na Dikwe ameliwa na fisi baada ya kutekelezwa Uwanja wa Gofu. Bila ya shaka alihojiwa."
"Ndiye nani huyo Dikwe?"


"Rafiki yake Hoza." Alijibu Chiko, akipumua kwa nguvu. "Jana usiku polisi walikwenda Tupetupe Hotel. Wakakipekua chumba cha Hoza na kuwahoji mapusha na maguberi kadhaa. Sisi hatukulala tupetupe, kwa kuhofia wanaweza kurudi."
"Uko wapi sasa hivi?"
"Karibu na soko kuu."
"Umeshafungua kinywa?"
"Bado."
"Nenda Pundamilia Inn, kijichumba namba nane, agiza utakacho. Muhudum akikwambia hicho ni kijichumba maalumu, nitaje mimi."
"Sawa mzee."
"Nitakuwa nawe baada ya dakika kumi au kumi na tano." Alisema Kembo na kuikata simu.


Akabonyeza namba aliyoizoea. Sauti nzito ya Kassim Hashir ikasema, "Yees?"
"Bwana Kessy, ni Kembo hapa."
"Unasemaje?"
"Unatazamia kutoka asubuhi hii?"
"Siyo kabla ya saa nne. Kwani vipi?"
"Kijana wangu mmoja amenipigia simu sasa hivi. Anashuku mambo si mazuri."
"Mabaya kiasi gani?"
"Siwezi kusema mpaka nikutane na kuzungumza naye. Nitamwona baada ya robo saa hivi."
"Unanishauri vipi? Niyeyuka?"


"Hapana , ni mapema mno kwa hatua kama hiyo. Haitatokea haja ya kuchukua hatua kama hiyo. Sioni kwa nini nishindwe kuyadhibiti mambo. Pengine Chiko anataka kutaharuki bure. Pengine anataka kunifanya fal@ anipune kuliko tulivyopatana."
"Sasa unanishauri nini?"
"Tulia. Nitakuja mara tu baada ya kuzungumza na huyu kijana."
"Vizuri"


*************************************


Miezi mitatu au minne ikapita. Kisa cha roba karne kikaendelea. Ndipo Bwana na Bibi Makete walipomona tena yule msichana. Na ndipo walipolijua jina lake Asha Rajabu.
Safari hii hakwenda hapo hospitalini kwa miguu yake, bali kwa ambulance, na kukimbizwa thieta kwa machela, akiwa na majeraha mawili mabaya kwenye tumbo lake lililo fura.


Siku hiyo Dr. Makete na mkewe walipangiwa shughuli za thieta. Wao na msichana huyo walikuwa kama waliopangiwa na Mungu mara hizo mbili.
Mambo yakawa haraka haraka. Wataalamu wa vyombo vya upasuaji, Dk.Makete, mkewe... kila mmoja alikuwa kama cherehani cha umeme.


Ni wakati akimwandaa kwenye meza ya upasuaji ndipo Bi. Makete akamtambua yule msichana. Akaguta, "Ray! Ray! Ni yule msichana wa Kassim Hashir!"
"Ndyo." Akakubali yule msichana kwa sauti dhaifu.
"Ndiye mimi Asha Rajabu."


Kila jozi ya macho ikaenda mezani. Dk. Makete akajongea kando ya meza, huku akiendelea kuvaa glovu za kupasulia. Akasema, "Gosh! Ni yeye!" Kisha akameuliza , "Imekuwaje tena mama?"
"Kassim kanipiga kisu." Alijibu Asha.
"My God! Nilikwambia usirudi kwake!"
"Baba kanifukuza nyumbani. Nilihitaji nauli niende kwa mjomba." Alisita akikusanya pumzi, kisha akaendelea. "Mimi sijali kufa. Lakini mwanangu... angali hai. Tafadhali..."
"Nitahitaji kuwaokoa nyote."


Bi mkumbwa akashusha pumzi na kuendelea. "Operation ikaanza. Ilikuwa ngumu kuliko tulivyotazamia. Ray akapambana nayo kwa karibu masaa mawili mazima."
Akatikisa kichwa. "ilikuwa kazi bure. Wote tuliokuwa humo ndani tulijua kazi bure. Kisu kilikata sehemu mbili nyeti sana. Afadhali ingekuwa sehemu moja. Lakini sehemu mbili , ilikuwa ni operesheni tata ajabu. Lakini Ray hakukubali kushindwa. Wote alitushangaza. Alifanya kazi isivyo kawaida, huku akivujwa jasho usoni. Mungu peke yake ndiye anyefahamu idadi ya vitambaa nilivyovitumia kumfutia jasho."


Bi mkubwa akatikisa tena kichwa. "Ilikuwa kazi bure. Mtu wa kwenye mashine ya mapigo ya moyo aliita mara tatu. 'Dokta... Dokta ... Dokta ...lakini aliendelea tu kushughulika. Kakata hiki, kaunga hiki, katoa hiki, kasafisha hiki... Ikanibidi nimshike bega na kumwambia, 'Ray, it's all over. She is gone! She is dead.'
'God! Ooh Lord! It is horrible!' Ray aliduwaa kama asiyeyaamini macho yake. Msichana yule alikuwa kama ... kama mtu anayemhusu - anaetuhusu kwa karibu sana.


Kwa mara ya kwanza na ya pekee - nikamwona Ray akitokwa machozi, tena hadharani. Sikuweza kujizuia. Hakuna alieweza kujizuia humo chumbani."
Bi mkubwa akatoa leso na kupenga .
Denny akauliza kwa sauti kavu, "Huyo mnyama hakufanywa chochote?"
"Jesus, Denny!" Bessy akaguta. "Badala ya kuuliza habari za yule mtoto!"
"Habari za yule mtoto nazifahamu."
"Are you joking?"
"No, I am bloody not."


Bi mkubwa, kama vile vijana hao hawakusema lolote, akasema, "Kassim Hashir afanywe nini? Nani kati yetu athubutu kushitaki? Na hata kama tungeshitaki, asingefanywa lolote, alikuwa kama nusu - Mungu. Tungejitafutia matatizo ya bure tu."
"Mama," Bessy akauliza kwa sauti ndogo, "Nini matokeo ya mtoto wa Asha, alinusurika au nae alikufa pia?"


"Hapana, yeye alinusurika, mtoto wa kiume mwenye afya nzuri. Kisu kilimkata begani na takoni. Tukamshona na kumfunga. Hadi leo anayo makovu hayo. Atakufa nayo."
Mabega ya Bi mkubwa yakaanza kucheza kabla ya sauti kusikika. "Atakufa nayo." Alirudia. "Atakufa nayo."
Denny akaenda kumshika bega.
"Mama umesema mwenyewe kipindi cha machozi kimepita."


Itaendelea
 
Nimekupenda... Ukirudia kusoma utaelewa zaidi na sidhani kama huko mbele kuna ufafanuzi zaidi ya huo.

Usimpende2 Mkuu, Bali mpe zawad ya kutupostia mara3 Kwa Leo, umekuwa slow sana now dayz
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…