idawa
JF-Expert Member
- Jan 20, 2012
- 25,284
- 38,364
- Thread starter
- #241
SEHEMU YA ISHIRINI NA SABA
Sam Kembo aliingia haraka katika jengo lililotazamana na Tupetupe Hotel. Akazikwea ngazi hadi ghorofa ya pili. Akaenda na kubisha hodi kwenye mlango wa chumba Na. 202. Chiko akaufungua, akisema, "Karibu Kembo."
"Asante."
Kembo akaingia akaona chumba kitupu. Akageuka na kuuliza. "Vipi, mbona uko peke yako? Na unaonekana huna furaha."
"Aah. Yule mtoto amenichefua kwelikweli ." Alijibu Chiko akiurudisha mlango. Kembo akaketi mezani na kuwasha sigara. "Mtoto gani?"
"Aliyempeleka Dikwe Uwanja wa Gofu."
"Kwa hiyo kaja kama ulivyotazamia?"
"Ndiyo. Alikuja na Inspekta Bessy. Kumbe ni mwanae Dk.Makete. Ni kitoto kidogo tu. Hata mambo yake ni ya kitoto. Eti kinajiita komandoo. Hizi sinema zinawaharibu sana. Bila shaka anajiona kama Rambo au Anorld Schwarzenegger."
"Uliweza kuzungumza naye?"
"Ndiyo. Kwa simu yangu ya mfukoni."
"Kwa hiyo amekataa pesa?"
"Kakataa. Kasema anakitaka kichwa cha aliyemgonga babake. Unaona? Ni mambo ya kitoto kabisa. Ni balehe inayomsumbua. Hata aliyemgonga babake hamfahamu. Anamwita - anamwita nani vile? Ooh ndiyo, anamwita Kassim Hashir."
"Eti nani?" Kembo aliuliza, uso ghafla umejikunja.
"Kassim Hashir."
"Gosh, una hakika?"
"Nweza kuwa nimekosea, lakini sidhani. Kwani vipi?"
"Kama ni hivyo Dk.Makete ameshazungumza. Yuko wapi Chox?"
"Amekwenda hospitali kumshughulikia huyo daktari. Kwani vipi?"
"Ni kazi bure. Tunachotaka kumzuia mzee huyo asikiseme ameshakisema."
"Yaani yule School Boy hakuwa akizungumza utumbo? Yaani Bwana Kessy ndiye Kassim Hashir?"
"Achana na hayo." Kembo alisema kwa karaha. Akauliza, "Umezungumza nini na huyo kijana?"
"Hatukuzungumza mengi. Eti anataka tukabiliane. My God, laiti angejua mimi ni nani!" Chiko akatikisa kichwa. "Acha tu, nitaikomesha balehe yake."
"Wapi saa ngapi?"
"Saa kumi na moja jioni. Kiwanda cha zamani cha sukari."
"Chiko unaweza kuwa mtego!"
"Mimi wa kunaswa katika mtego wa kijinga? Bos, unanionaje? Hivi sasa Fensy yuko huko anavinjari. Anapiga simu ya mfukoni kama hii niliyonayo. Akiona kitu chochote zaidi ya huyo School Boy ataniarifu na kuyeyuka. Tutampata huyo 'Rambo' wakati mwingine, mahala pengine."
Kembo akakubali kwa kichwa, akasema, "Kuweni waangalifu."
"Usiwe na wasiwasi bos. Mwingine huyo School Boy kwenye orodha ya marehemu. Ikiwezekana angeshauriwa apitie kwanza kanisani akajiombea kabisa misa ya wafu kabla hajaenda huko kiwanda cha sukari."
**********************************
Mama Denny aliufungua mlango Na. 13 akaingia ndani.Kachero Koplo Koba aliyekuwa ameketi akainuka. akasema, "Karibu, Bi mkubwa. Shikamoo."
"Asante mwanangu," Aliitikia Mama Denny. "Anaendeleaje mgonjwa?"
"Vizuri, ningekushauri usimchoshe sana kwa mazungumzo marefu."
"Nafahamu."
"Nanyosha miguu kwenye korido." Aliendelea Koplo Koba." Nauacha wazi mlango, ukiwa na shida yoyote niite. Kama jina umelisahau, ni Koplo Koba."
"Vizuri mwanangu."
Mama Denny akaenda kando ya kitanda na kukifumbata kiganja cha mumewe kwenye viganja vyake. Mzee Makete akafumbua macho. Akasema kwa sauti dhaifu, "Ooh, ni wewe mama Denny!"
"Ndiyo mpenzi. Unajisikiaje?"
"Uchovu tu."
"Vumilia mpenzi, ndiyo hali ya dunia. Dk.Beka amesema atakuruhusu baada ya siku chache tu."
Baada ya kimya kifupi Mzee Makete akasema, "Mpenzi, Kassim Hashir angali hai. Ndiye aliyenigonga."
"Nafahamu. Polisi tiyari wanamtafuta."
"Huoni kuwa ni wajibu wetu kumweleza Denny ukweli?"
"Nimekwisha mueleza."
"Asante sana. Umenipunguzia mzigo mkubwa sana."
"Nimemweleza kila kitu, tangu mwanzo hadi mwisho. Hata jinsi alivyopata yale makovu."
"Akasemaje?"
"Unamjua jinsi Denny alivyo. Hakubadilika. Kama vile nimemsimulia kisa cha mtu mwingine kabisa."
"Kuna wakati huyu mtoto hunishangaza na kunitia wasiwasi."
"Si peke yako."
"Kama vile ana kasoro." Aliendelea Mzee Makete. "Kama vile si mtu wa kawaida!"
"Yaani taahira?"
"Hapana. Hapana, Denny ni mzima kabisa. Ana akili kama mtu wa wastani. Isipokuwa ana tofauti kidogo na mtu wa kawaida. Hupenda kuishi porini, kufanya mazoezi magumu, kwake hakuna kinachomstua na haogopi kitu hata kama kwa wengine kitaonekana ni kigumu na cha hatari kiasi gani. Inatokana na viini chimbuko bila shaka. Yaani jenetiki."
"Tulifanya makosa kumchukua hali tukijua anaweza kuwa na jenetiki za Kassim Hashir?"
"No. Hapana. Hatukufanya kosa hata kidogo. Tusingemchukua sisi angechukuliwa na mtu mwingine. Au pengie angepelekwa kwenye makazi ya watoto yatima. Pengine asingepeta malezi kama tuliyompa. Hapana, hatukufanya kosa hata kidogo kumchukua."
Bi mkubwa akashusha pumzi. Akasema, "Sijui ningejisikiaje ungesema tulifanya kosa. Unajua tumejizuia kuzaa kwa kuogopa kuja kugawa upendo. Hakuna wa kuthubutu kuninyang'anya Denny wangu. Hakuna."
"Mpenzi,mpenzi,mpenzi - hakuna wa kukunyang'anya Denny wako. Awe taahira, zuzu, awe na bongo au la ni wako. Kihaki, kisheria na Kimungu."
Kachero Koplo Koba alimuona daktari tangu alipozimaliza ngazi na kuingia kwenye korido. Alikuwa mgeni kabisa kwake, lakini tena, hakuwa akiwafahamu madaktari wote wa hospitali hii kubwa. Isitoshe, hakuwa na tofauti yoyote na madaktari wengine. Kama ilikuwepo, basi ni ya huyu kuonekana ni daktari aliyekamilika.
Alivaa kidaktari, pamoja na pima moyo shingoni, Na hata tembea yake ilikuwa ni ya kidaktari.
"Habari za hapa kijana?" Chox alitamka kwa sauti nzito, ya uhakika.
"Salama tu Dokta."
"Good. Very good." Chox alisema akiridhika kwa kichwa. "Dk.Makete yuko peke yake au kuna mtu mwingine ndani?"
"Yuko na mkewe. Amewasili sasa hivi."
"Good. Good. Very good."
Chox akapenya kwenye mlango uliokuwa wazi. Akasema, "Shikamoo Mama Makete."
"Marahaba Dokta. Karibu."
"Asante." Alijibu Chox. Akavichukua vyeti vya matibabu kitandani. Akauliza, "Anajisikiaje mgonjwa wetu?"
"Hajambo. Yuko macho."
"Good. Very good."
Chox akavirudisha vyeti na kumkaribia mgonjwa. Akamuuliza, "How do you feel Doctor?"
"Still very weak." Alijibu Mzee Makete.
"Expected. Most expected. You'll be as good as a new born in no time. You'll see."
Chox akakichukua kipimamoyo na kuanza kumpima mgonjwa. Akasema, "Good. Very good. Very normal. Utahitaji sindano hii moja kwa jioni ya leo." Akaingiza mkono mfukoni na kutoa sindano na kichupa cha dawa. Mzee Makete akasema, "Mpe mke wangu anidunge."
Chox akasita.
"Ooh, usiwe na wasiwasi Dokta." Alisema mama Denny akiinuka. "Mimi ni nesi kamili. Wajua, ni mimi ninayemdunga sindano nyumbani."
"Good. Very good. Very good."
"Chox akampa Mama Denny sindano na kichupa kile cha dawa. Akasema, "Just 2cc"
Mama Denny akaijaza sindano dawa, akakiweka kichupa mezani. Akainua sindano na kupunguza dawa, akitafuta usawa wa 2cc.
"Good. Very good. Exllent. Chox aliafiki akiiangalia sindano.
Itaendelea ...
Sam Kembo aliingia haraka katika jengo lililotazamana na Tupetupe Hotel. Akazikwea ngazi hadi ghorofa ya pili. Akaenda na kubisha hodi kwenye mlango wa chumba Na. 202. Chiko akaufungua, akisema, "Karibu Kembo."
"Asante."
Kembo akaingia akaona chumba kitupu. Akageuka na kuuliza. "Vipi, mbona uko peke yako? Na unaonekana huna furaha."
"Aah. Yule mtoto amenichefua kwelikweli ." Alijibu Chiko akiurudisha mlango. Kembo akaketi mezani na kuwasha sigara. "Mtoto gani?"
"Aliyempeleka Dikwe Uwanja wa Gofu."
"Kwa hiyo kaja kama ulivyotazamia?"
"Ndiyo. Alikuja na Inspekta Bessy. Kumbe ni mwanae Dk.Makete. Ni kitoto kidogo tu. Hata mambo yake ni ya kitoto. Eti kinajiita komandoo. Hizi sinema zinawaharibu sana. Bila shaka anajiona kama Rambo au Anorld Schwarzenegger."
"Uliweza kuzungumza naye?"
"Ndiyo. Kwa simu yangu ya mfukoni."
"Kwa hiyo amekataa pesa?"
"Kakataa. Kasema anakitaka kichwa cha aliyemgonga babake. Unaona? Ni mambo ya kitoto kabisa. Ni balehe inayomsumbua. Hata aliyemgonga babake hamfahamu. Anamwita - anamwita nani vile? Ooh ndiyo, anamwita Kassim Hashir."
"Eti nani?" Kembo aliuliza, uso ghafla umejikunja.
"Kassim Hashir."
"Gosh, una hakika?"
"Nweza kuwa nimekosea, lakini sidhani. Kwani vipi?"
"Kama ni hivyo Dk.Makete ameshazungumza. Yuko wapi Chox?"
"Amekwenda hospitali kumshughulikia huyo daktari. Kwani vipi?"
"Ni kazi bure. Tunachotaka kumzuia mzee huyo asikiseme ameshakisema."
"Yaani yule School Boy hakuwa akizungumza utumbo? Yaani Bwana Kessy ndiye Kassim Hashir?"
"Achana na hayo." Kembo alisema kwa karaha. Akauliza, "Umezungumza nini na huyo kijana?"
"Hatukuzungumza mengi. Eti anataka tukabiliane. My God, laiti angejua mimi ni nani!" Chiko akatikisa kichwa. "Acha tu, nitaikomesha balehe yake."
"Wapi saa ngapi?"
"Saa kumi na moja jioni. Kiwanda cha zamani cha sukari."
"Chiko unaweza kuwa mtego!"
"Mimi wa kunaswa katika mtego wa kijinga? Bos, unanionaje? Hivi sasa Fensy yuko huko anavinjari. Anapiga simu ya mfukoni kama hii niliyonayo. Akiona kitu chochote zaidi ya huyo School Boy ataniarifu na kuyeyuka. Tutampata huyo 'Rambo' wakati mwingine, mahala pengine."
Kembo akakubali kwa kichwa, akasema, "Kuweni waangalifu."
"Usiwe na wasiwasi bos. Mwingine huyo School Boy kwenye orodha ya marehemu. Ikiwezekana angeshauriwa apitie kwanza kanisani akajiombea kabisa misa ya wafu kabla hajaenda huko kiwanda cha sukari."
**********************************
Mama Denny aliufungua mlango Na. 13 akaingia ndani.Kachero Koplo Koba aliyekuwa ameketi akainuka. akasema, "Karibu, Bi mkubwa. Shikamoo."
"Asante mwanangu," Aliitikia Mama Denny. "Anaendeleaje mgonjwa?"
"Vizuri, ningekushauri usimchoshe sana kwa mazungumzo marefu."
"Nafahamu."
"Nanyosha miguu kwenye korido." Aliendelea Koplo Koba." Nauacha wazi mlango, ukiwa na shida yoyote niite. Kama jina umelisahau, ni Koplo Koba."
"Vizuri mwanangu."
Mama Denny akaenda kando ya kitanda na kukifumbata kiganja cha mumewe kwenye viganja vyake. Mzee Makete akafumbua macho. Akasema kwa sauti dhaifu, "Ooh, ni wewe mama Denny!"
"Ndiyo mpenzi. Unajisikiaje?"
"Uchovu tu."
"Vumilia mpenzi, ndiyo hali ya dunia. Dk.Beka amesema atakuruhusu baada ya siku chache tu."
Baada ya kimya kifupi Mzee Makete akasema, "Mpenzi, Kassim Hashir angali hai. Ndiye aliyenigonga."
"Nafahamu. Polisi tiyari wanamtafuta."
"Huoni kuwa ni wajibu wetu kumweleza Denny ukweli?"
"Nimekwisha mueleza."
"Asante sana. Umenipunguzia mzigo mkubwa sana."
"Nimemweleza kila kitu, tangu mwanzo hadi mwisho. Hata jinsi alivyopata yale makovu."
"Akasemaje?"
"Unamjua jinsi Denny alivyo. Hakubadilika. Kama vile nimemsimulia kisa cha mtu mwingine kabisa."
"Kuna wakati huyu mtoto hunishangaza na kunitia wasiwasi."
"Si peke yako."
"Kama vile ana kasoro." Aliendelea Mzee Makete. "Kama vile si mtu wa kawaida!"
"Yaani taahira?"
"Hapana. Hapana, Denny ni mzima kabisa. Ana akili kama mtu wa wastani. Isipokuwa ana tofauti kidogo na mtu wa kawaida. Hupenda kuishi porini, kufanya mazoezi magumu, kwake hakuna kinachomstua na haogopi kitu hata kama kwa wengine kitaonekana ni kigumu na cha hatari kiasi gani. Inatokana na viini chimbuko bila shaka. Yaani jenetiki."
"Tulifanya makosa kumchukua hali tukijua anaweza kuwa na jenetiki za Kassim Hashir?"
"No. Hapana. Hatukufanya kosa hata kidogo. Tusingemchukua sisi angechukuliwa na mtu mwingine. Au pengie angepelekwa kwenye makazi ya watoto yatima. Pengine asingepeta malezi kama tuliyompa. Hapana, hatukufanya kosa hata kidogo kumchukua."
Bi mkubwa akashusha pumzi. Akasema, "Sijui ningejisikiaje ungesema tulifanya kosa. Unajua tumejizuia kuzaa kwa kuogopa kuja kugawa upendo. Hakuna wa kuthubutu kuninyang'anya Denny wangu. Hakuna."
"Mpenzi,mpenzi,mpenzi - hakuna wa kukunyang'anya Denny wako. Awe taahira, zuzu, awe na bongo au la ni wako. Kihaki, kisheria na Kimungu."
Kachero Koplo Koba alimuona daktari tangu alipozimaliza ngazi na kuingia kwenye korido. Alikuwa mgeni kabisa kwake, lakini tena, hakuwa akiwafahamu madaktari wote wa hospitali hii kubwa. Isitoshe, hakuwa na tofauti yoyote na madaktari wengine. Kama ilikuwepo, basi ni ya huyu kuonekana ni daktari aliyekamilika.
Alivaa kidaktari, pamoja na pima moyo shingoni, Na hata tembea yake ilikuwa ni ya kidaktari.
"Habari za hapa kijana?" Chox alitamka kwa sauti nzito, ya uhakika.
"Salama tu Dokta."
"Good. Very good." Chox alisema akiridhika kwa kichwa. "Dk.Makete yuko peke yake au kuna mtu mwingine ndani?"
"Yuko na mkewe. Amewasili sasa hivi."
"Good. Good. Very good."
Chox akapenya kwenye mlango uliokuwa wazi. Akasema, "Shikamoo Mama Makete."
"Marahaba Dokta. Karibu."
"Asante." Alijibu Chox. Akavichukua vyeti vya matibabu kitandani. Akauliza, "Anajisikiaje mgonjwa wetu?"
"Hajambo. Yuko macho."
"Good. Very good."
Chox akavirudisha vyeti na kumkaribia mgonjwa. Akamuuliza, "How do you feel Doctor?"
"Still very weak." Alijibu Mzee Makete.
"Expected. Most expected. You'll be as good as a new born in no time. You'll see."
Chox akakichukua kipimamoyo na kuanza kumpima mgonjwa. Akasema, "Good. Very good. Very normal. Utahitaji sindano hii moja kwa jioni ya leo." Akaingiza mkono mfukoni na kutoa sindano na kichupa cha dawa. Mzee Makete akasema, "Mpe mke wangu anidunge."
Chox akasita.
"Ooh, usiwe na wasiwasi Dokta." Alisema mama Denny akiinuka. "Mimi ni nesi kamili. Wajua, ni mimi ninayemdunga sindano nyumbani."
"Good. Very good. Very good."
"Chox akampa Mama Denny sindano na kichupa kile cha dawa. Akasema, "Just 2cc"
Mama Denny akaijaza sindano dawa, akakiweka kichupa mezani. Akainua sindano na kupunguza dawa, akitafuta usawa wa 2cc.
"Good. Very good. Exllent. Chox aliafiki akiiangalia sindano.
Itaendelea ...