Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 39
Walipogeukiana na kuonana ana kwa ana, kila mmoja alikuwa na ghadhabu na mwenzie.
Patrick akaanza kurudi akimfata Maiko akiwa amejiaminisha kabisa, Maiko akajua hapo si mahala pema kwani aliweza kuiona vizuri hasira ya Patrick.
Ndipo Maiko alipoanza kukimbia, ila hakufika mbali akawa amepigwa mtama na Patrick, Maiko akaanguka chini.
Patrick akamnyanyua Maiko kwa nyuma na kumgeuza huku akimpiga ngumi usoni, Maiko akaona kuwa ataonekana mzembe asipo pambana na Patrick, alichofanya ni kumpiga teke Patrick. Hasira ikamzidi Patrick, akainuka na kumrukia Maiko akampiga teke ambalo Maiko alikwepa, nae akarusha ngumi ambayo Patrick aliikwepa.
Pambano likaanza sasa, walipigana sana na kuumizana ila Maiko ndiye aliyeumia zaidi, alikuwa chini na Patrick juu huku akishambuliwa kwa ngumi, akabahatika kumpiga Patrick teke sehemu za siri, hapo ndipo akapata upenyo wa kukimbilia gari lake na kuondoka.
Patrick alionekana kuwa na hasira sana hadi mishipa ya sura ilimsimama.
Mashaka akaingia kwenye kile chumba alichowekwa Tina, akamkuta Tina akiwa amelala.
Akamfata karibu na kuanza kumpapasa, Tina akashtuka na kuanza kuogopa huku akitoa mikono ya Mashaka ila hakuacha, aliendelea kumpapasa papasa Tina.
Akataka kumuingilia, Tina akawa anakataa na purukushani kati yao zikafatia, ikawa kama mtafutano wa jogoo na kuku jike.
Mashaka akaona asisumbuliwe sana na huyu binti, akaamua kutumia nguvu sasa. Naye akampiga na kumbaka.
Alipomaliza akamuangalia Tina na kumwambia "asante kwa huduma ingawa nimetumia nguvu kuipata" halafu akatoka nje.
Tina akalia sana, akajiuliza maswali mengi "yani ofa ya bia mbili ndio nafanyiwa hivi! Jamani mimi! Maskini Tina mie. Mungu nisaidie nitoke humu."
Tina akawa analia tu bila msaada wowote.
Maiko aliondoka moja kwa moja hadi kwa wenzie walipo.
Mashaka akamshangaa Maiko kuwa na damu na alama za kupigwa mwilini.
MASHAKA: Vipi tena Maiko?
MAIKO: Hivi tumekuja huku Mwanza kumtafuta Patrick au Patrick kututafuta sisi?
MASHAKA: Kivipi Maiko?
MAIKO: Nimekutana na Patrick na ndiye aliyenifanya hivi, alikuwa na hasira sana hata nashangaa kwanini amekuwa vile.
MASHAKA: Dah! Yani Patrick ndo kakufanya hivi!! Hako ka Patrick nikikapata nakanyonga kabisa, yani yeye ndo mwenye makosa halafu anatuletea hasira sisi!
MAIKO: Umeona hapo! Hata mi namshangaa, angekuwa mwingine angekimbia kuniona eti yeye ndo akanikimbilia na kuanza kupigana nami.
MASHAKA: Madai yake imemuuma sana hiyo ya Tusa, ngoja sasa tutamchinja huyo Tusa mbele ya macho yake. Nimechukizwa sana kwakweli.
Maiko alishindwa kumuelewa kabisa Patrick kuwa ana matatizo gani hadi kumvamia yeye kiasi kile.
Deborah bado aliendelea kumtafakari Patrick.
DEBORAH: Nashindwa kumuelewa mwenzenu, kaondoka kimya kimya hadi leo hajarudi.
PAMELA: Ninachowaza mimi ni kuwa, kama Adamu amefika Mwanza basi itakuwa tabu kwamaana hanipati kwenye ile simu yako.
DEBORAH: Haya majanga mbona mmh! Sijui hata tufanyaje! Au labda niende mjini kununua line.
PAMELA: Nadhani hilo litakuwa jambo la busara sana.
DEBORAH: Basi hakuna tatizo nitaenda hata leo au kesho.
Deborah akajipanga kwenda kununua namba nyingine ili aweze kuwasiliana.
Patrick akaenda alipomuacha Yuda.
PATRICK: Nimekutana na Maiko leo, bora hukuwa pamoja nami.
YUDA: Bora tena!! Wakati ndio tungesaidiana kulipa kisasi!
PATRICK: Sitaki ajue mapema hivi kama tunafahamiana, kwasasa wewe unatakiwa ufanye kazi moja.
YUDA: Kazi gani hiyo?
PATRICK: Uwasiliane na wakina Maiko ili ujue walipo, halafu uwafuate. Hapo ndio tutacheza mchezo mzuri bila ya wao kujua. Si wamejileta wenyewe kwenye mji wetu bhana.
YUDA: Na je vipi haturudi nyumbani?
PATRICK: Hakuna kurudi hadi tukamilishe hili swala kwanza.
Yuda akaanza kutambua jinsi gani Patrick anawajua wakina Maiko na kundi lake.
Mashaka akapanga mkakati na Maiko.
MASHAKA: Hakuna kubweteka Maiko, hapa tumtafute Tusa kwa gharama yoyote ile kwanza tutafaidika na pili tutamkomesha Patrick.
MAIKO: Kwahiyo tuanze na msako wa Tusa kwanza?
MASHAKA: Ndio, tuanze na Tusa.
MAIKO: Vipi kale karembo ndani kapo!
MASHAKA: Kapo ndio, kale ndio katakuwa kutuburudisha baada ya kazi.
MAIKO: Yani na wewe unakatumia!
MASHAKA: Ndio kwani kuna ubaya gani?
MAIKO: Tafuta wako bhana, hapa Mwanza wamejaa kibao. Yule mrembo niachie mimi. Tafadhari sana sitaki tuingiliane kwa warembo, nawe tafuta wako bhana.
MASHAKA: Tujadili ya maana hapa, tukianza kujadili kuhusu hao wanawake tunaweza kugombana bure mwanangu. Hebu achana nao kwanza tuwaze ya muhimu hapa.
MAIKO: Hata na yao ni muhimu, sawa bhana. Tujadili sasa namna ya kumpata Tusa.
Wakaanza kupanga mipango ya kuweza kumpata Tusa.
Adamu alishakata tamaa kabisa.
ADAMU: Hivi tutakaa hapa Mwanza hadi lini jamani?
FAUSTA: Hata sielewi, Tina ametuletea mambo jamani.
ADAMU: Yani huyo Tina angekuwepo tungesharudi Dar. Ametuchanganya kweli huyo Tina.
FAUSTA: Mdogo wangu Pamela nae ni magumashi tu, tangu tuingie Mwanza kile kinamba chake hakipatikani wala namba aliyokupigia haipatikani hata sijui anafikiria nini.
ADAMU: Kwakweli wananichanganya sana hawa watu, alianza Tusa, akaja mama yake na sasa ni Tina. Wote namba zao hazipatikani tunabaki kukadilia tu kuwa ni wazima, ila haya ni mateso kwakweli.
FAUSTA: Sasa kaka itakuwaje?
ADAMU: Kama hadi kesho mambo hayaeleweki basi turudi tu Dar tukatafute njia ya kuwapata. Hapa Mwanza hatuna makazi wala nini, kwa kifupi hapatufai, asije akapotea na mwingine bure.
Adamu akatoka tena kwenda kujaribu kuwatafuta hawa watu wa tatu kama atapata taarifa zao zozote.
Adamu akiwa mjini anashangaa kumuona mtu ambaye hakumtarajia kabisa.
Walipogeukiana na kuonana ana kwa ana, kila mmoja alikuwa na ghadhabu na mwenzie.
Patrick akaanza kurudi akimfata Maiko akiwa amejiaminisha kabisa, Maiko akajua hapo si mahala pema kwani aliweza kuiona vizuri hasira ya Patrick.
Ndipo Maiko alipoanza kukimbia, ila hakufika mbali akawa amepigwa mtama na Patrick, Maiko akaanguka chini.
Patrick akamnyanyua Maiko kwa nyuma na kumgeuza huku akimpiga ngumi usoni, Maiko akaona kuwa ataonekana mzembe asipo pambana na Patrick, alichofanya ni kumpiga teke Patrick. Hasira ikamzidi Patrick, akainuka na kumrukia Maiko akampiga teke ambalo Maiko alikwepa, nae akarusha ngumi ambayo Patrick aliikwepa.
Pambano likaanza sasa, walipigana sana na kuumizana ila Maiko ndiye aliyeumia zaidi, alikuwa chini na Patrick juu huku akishambuliwa kwa ngumi, akabahatika kumpiga Patrick teke sehemu za siri, hapo ndipo akapata upenyo wa kukimbilia gari lake na kuondoka.
Patrick alionekana kuwa na hasira sana hadi mishipa ya sura ilimsimama.
Mashaka akaingia kwenye kile chumba alichowekwa Tina, akamkuta Tina akiwa amelala.
Akamfata karibu na kuanza kumpapasa, Tina akashtuka na kuanza kuogopa huku akitoa mikono ya Mashaka ila hakuacha, aliendelea kumpapasa papasa Tina.
Akataka kumuingilia, Tina akawa anakataa na purukushani kati yao zikafatia, ikawa kama mtafutano wa jogoo na kuku jike.
Mashaka akaona asisumbuliwe sana na huyu binti, akaamua kutumia nguvu sasa. Naye akampiga na kumbaka.
Alipomaliza akamuangalia Tina na kumwambia "asante kwa huduma ingawa nimetumia nguvu kuipata" halafu akatoka nje.
Tina akalia sana, akajiuliza maswali mengi "yani ofa ya bia mbili ndio nafanyiwa hivi! Jamani mimi! Maskini Tina mie. Mungu nisaidie nitoke humu."
Tina akawa analia tu bila msaada wowote.
Maiko aliondoka moja kwa moja hadi kwa wenzie walipo.
Mashaka akamshangaa Maiko kuwa na damu na alama za kupigwa mwilini.
MASHAKA: Vipi tena Maiko?
MAIKO: Hivi tumekuja huku Mwanza kumtafuta Patrick au Patrick kututafuta sisi?
MASHAKA: Kivipi Maiko?
MAIKO: Nimekutana na Patrick na ndiye aliyenifanya hivi, alikuwa na hasira sana hata nashangaa kwanini amekuwa vile.
MASHAKA: Dah! Yani Patrick ndo kakufanya hivi!! Hako ka Patrick nikikapata nakanyonga kabisa, yani yeye ndo mwenye makosa halafu anatuletea hasira sisi!
MAIKO: Umeona hapo! Hata mi namshangaa, angekuwa mwingine angekimbia kuniona eti yeye ndo akanikimbilia na kuanza kupigana nami.
MASHAKA: Madai yake imemuuma sana hiyo ya Tusa, ngoja sasa tutamchinja huyo Tusa mbele ya macho yake. Nimechukizwa sana kwakweli.
Maiko alishindwa kumuelewa kabisa Patrick kuwa ana matatizo gani hadi kumvamia yeye kiasi kile.
Deborah bado aliendelea kumtafakari Patrick.
DEBORAH: Nashindwa kumuelewa mwenzenu, kaondoka kimya kimya hadi leo hajarudi.
PAMELA: Ninachowaza mimi ni kuwa, kama Adamu amefika Mwanza basi itakuwa tabu kwamaana hanipati kwenye ile simu yako.
DEBORAH: Haya majanga mbona mmh! Sijui hata tufanyaje! Au labda niende mjini kununua line.
PAMELA: Nadhani hilo litakuwa jambo la busara sana.
DEBORAH: Basi hakuna tatizo nitaenda hata leo au kesho.
Deborah akajipanga kwenda kununua namba nyingine ili aweze kuwasiliana.
Patrick akaenda alipomuacha Yuda.
PATRICK: Nimekutana na Maiko leo, bora hukuwa pamoja nami.
YUDA: Bora tena!! Wakati ndio tungesaidiana kulipa kisasi!
PATRICK: Sitaki ajue mapema hivi kama tunafahamiana, kwasasa wewe unatakiwa ufanye kazi moja.
YUDA: Kazi gani hiyo?
PATRICK: Uwasiliane na wakina Maiko ili ujue walipo, halafu uwafuate. Hapo ndio tutacheza mchezo mzuri bila ya wao kujua. Si wamejileta wenyewe kwenye mji wetu bhana.
YUDA: Na je vipi haturudi nyumbani?
PATRICK: Hakuna kurudi hadi tukamilishe hili swala kwanza.
Yuda akaanza kutambua jinsi gani Patrick anawajua wakina Maiko na kundi lake.
Mashaka akapanga mkakati na Maiko.
MASHAKA: Hakuna kubweteka Maiko, hapa tumtafute Tusa kwa gharama yoyote ile kwanza tutafaidika na pili tutamkomesha Patrick.
MAIKO: Kwahiyo tuanze na msako wa Tusa kwanza?
MASHAKA: Ndio, tuanze na Tusa.
MAIKO: Vipi kale karembo ndani kapo!
MASHAKA: Kapo ndio, kale ndio katakuwa kutuburudisha baada ya kazi.
MAIKO: Yani na wewe unakatumia!
MASHAKA: Ndio kwani kuna ubaya gani?
MAIKO: Tafuta wako bhana, hapa Mwanza wamejaa kibao. Yule mrembo niachie mimi. Tafadhari sana sitaki tuingiliane kwa warembo, nawe tafuta wako bhana.
MASHAKA: Tujadili ya maana hapa, tukianza kujadili kuhusu hao wanawake tunaweza kugombana bure mwanangu. Hebu achana nao kwanza tuwaze ya muhimu hapa.
MAIKO: Hata na yao ni muhimu, sawa bhana. Tujadili sasa namna ya kumpata Tusa.
Wakaanza kupanga mipango ya kuweza kumpata Tusa.
Adamu alishakata tamaa kabisa.
ADAMU: Hivi tutakaa hapa Mwanza hadi lini jamani?
FAUSTA: Hata sielewi, Tina ametuletea mambo jamani.
ADAMU: Yani huyo Tina angekuwepo tungesharudi Dar. Ametuchanganya kweli huyo Tina.
FAUSTA: Mdogo wangu Pamela nae ni magumashi tu, tangu tuingie Mwanza kile kinamba chake hakipatikani wala namba aliyokupigia haipatikani hata sijui anafikiria nini.
ADAMU: Kwakweli wananichanganya sana hawa watu, alianza Tusa, akaja mama yake na sasa ni Tina. Wote namba zao hazipatikani tunabaki kukadilia tu kuwa ni wazima, ila haya ni mateso kwakweli.
FAUSTA: Sasa kaka itakuwaje?
ADAMU: Kama hadi kesho mambo hayaeleweki basi turudi tu Dar tukatafute njia ya kuwapata. Hapa Mwanza hatuna makazi wala nini, kwa kifupi hapatufai, asije akapotea na mwingine bure.
Adamu akatoka tena kwenda kujaribu kuwatafuta hawa watu wa tatu kama atapata taarifa zao zozote.
Adamu akiwa mjini anashangaa kumuona mtu ambaye hakumtarajia kabisa.