Abtali mwerevu
JF-Expert Member
- May 5, 2013
- 665
- 515
- Thread starter
- #21
Sehemu ya 14
Hatimaye Mako alimaliza darasa la saba. Akaomba kusoma ‘pre-form one’ nje kidogo ya mji ambako kulikuwa na kituo cha masomo hayo tena kilichotoa huduma ya bweni. Alisema alitaka afurahie kukaa nje ya nyumbani kwa miezi japo mitatu ili ajifunze changamoto mpya. Kwa sababu Baba alimwamini kijana wake na alishampa mbinu mbili tatu za kukabiliana na dunia na mambo yake, alimruhusu.
Hatimaye ilifika siku ya mwisho ya mafunzo. Baba akafunga safari kwenda kumrejesha nyumbani kijana wake. Alipofika alielezwa kwamba mtoto yule aliandikishwa lakini alitoweka siku tatu tu baada ya masomo na hakuonekana tena. “Kwa nini hamkunijulisha. Atakuwa wapi sasa?” alihoji Baba aliyepatwa na mshituko.
“Hukutuachia namba ya simu.”
“Nilimpa awape.”
“Hakutupa.”
Baada ya mabishano ya muda, Baba aliamua kurudi nyumbani akiwa kachanganyikiwa. Alipofika alipitiliza katika ofisi yake, hakutaka kuongea na Mama aliyekuwa chumbani, hakuwa na jibu la swali lake.
Alipofungua mlango wa ofisi alitabasamu alipomuona kijana wa miaka 13 akiwa kakaa nyuma ya kompyuta, mikono kaweka kichwani naye anatabasamu.
“Umesoma wapi pre form one, hukuonekana shule miezi yote mitatu,” Baba aliuliza akivua kofia na kuiweka juu ya msumari katika pembe ya mlango.
“Password ya kompyuta ulibadili… nimeshindwa kufungua,” Mako aliuliza Akilikwepa swali la kwanza.
“Ulisoma wapi pre form one?” Aliuliza tena Baba, akiangaza huku na kule bila shaka akitafuta bakora yake, endapo angeikosa, yangetumika makofi.
“Kuna joto sana humu ndani… Oooooh… marafiki, nilinasa katika mtego wa marafiki. Marafiki zangu wote hawakuwa kituo kile, lakini wote walikuwa Bahari School. Hivyo nikaenda kusoma huko.”
“Ada tulilipa huku, kule ulilipa nini?”
“Hivi hujui kwamba Bahari School inamilikiwa na mama ya rafiki yangu Dan? Nilisoma bure.”
“Kwa nini hukunipa taarifa?”
“Vipi kama ungekataa, ilikuwa salama. Nilithubutu katika njia salama.”
“Nipe ushahidi kwamba umesoma.”
Mako alinyanyuka katika kiti. Akaelekea chumbani kwake na kurudi na begi. “Tazama hili, daftari la physics limeandikwa angalia na vema hizo. Hili la Mathematics, the study of number, hili la Biology, study of living things… hili la History, study of past, present and future events… angalia madaftari… unaona hii, hiki cheti cha heshima nimepewa, nimeongoza katika mitihani… angalia mitihani hiyo. Tisini, mia, sabini na nane… hilo ndiyo pekee nilianguka, zingine ni mia kwa tisini.”
Baba alikosa swali la kuuliza japo kichwani hakuwa na majibu. Aulize nini kama ushahidi upo mezani. Akamkaribisha kijana nyumbani.
Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp. Kujiunga, Gusa Hapa
Tupate Wadhamini:
Soma: Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi
Soma: Jinsi ya Kuandika CV
Hatimaye Mako alimaliza darasa la saba. Akaomba kusoma ‘pre-form one’ nje kidogo ya mji ambako kulikuwa na kituo cha masomo hayo tena kilichotoa huduma ya bweni. Alisema alitaka afurahie kukaa nje ya nyumbani kwa miezi japo mitatu ili ajifunze changamoto mpya. Kwa sababu Baba alimwamini kijana wake na alishampa mbinu mbili tatu za kukabiliana na dunia na mambo yake, alimruhusu.
Hatimaye ilifika siku ya mwisho ya mafunzo. Baba akafunga safari kwenda kumrejesha nyumbani kijana wake. Alipofika alielezwa kwamba mtoto yule aliandikishwa lakini alitoweka siku tatu tu baada ya masomo na hakuonekana tena. “Kwa nini hamkunijulisha. Atakuwa wapi sasa?” alihoji Baba aliyepatwa na mshituko.
“Hukutuachia namba ya simu.”
“Nilimpa awape.”
“Hakutupa.”
Baada ya mabishano ya muda, Baba aliamua kurudi nyumbani akiwa kachanganyikiwa. Alipofika alipitiliza katika ofisi yake, hakutaka kuongea na Mama aliyekuwa chumbani, hakuwa na jibu la swali lake.
Alipofungua mlango wa ofisi alitabasamu alipomuona kijana wa miaka 13 akiwa kakaa nyuma ya kompyuta, mikono kaweka kichwani naye anatabasamu.
“Umesoma wapi pre form one, hukuonekana shule miezi yote mitatu,” Baba aliuliza akivua kofia na kuiweka juu ya msumari katika pembe ya mlango.
“Password ya kompyuta ulibadili… nimeshindwa kufungua,” Mako aliuliza Akilikwepa swali la kwanza.
“Ulisoma wapi pre form one?” Aliuliza tena Baba, akiangaza huku na kule bila shaka akitafuta bakora yake, endapo angeikosa, yangetumika makofi.
“Kuna joto sana humu ndani… Oooooh… marafiki, nilinasa katika mtego wa marafiki. Marafiki zangu wote hawakuwa kituo kile, lakini wote walikuwa Bahari School. Hivyo nikaenda kusoma huko.”
“Ada tulilipa huku, kule ulilipa nini?”
“Hivi hujui kwamba Bahari School inamilikiwa na mama ya rafiki yangu Dan? Nilisoma bure.”
“Kwa nini hukunipa taarifa?”
“Vipi kama ungekataa, ilikuwa salama. Nilithubutu katika njia salama.”
“Nipe ushahidi kwamba umesoma.”
Mako alinyanyuka katika kiti. Akaelekea chumbani kwake na kurudi na begi. “Tazama hili, daftari la physics limeandikwa angalia na vema hizo. Hili la Mathematics, the study of number, hili la Biology, study of living things… hili la History, study of past, present and future events… angalia madaftari… unaona hii, hiki cheti cha heshima nimepewa, nimeongoza katika mitihani… angalia mitihani hiyo. Tisini, mia, sabini na nane… hilo ndiyo pekee nilianguka, zingine ni mia kwa tisini.”
Baba alikosa swali la kuuliza japo kichwani hakuwa na majibu. Aulize nini kama ushahidi upo mezani. Akamkaribisha kijana nyumbani.
Kuwa wa Kwanza Kupokea mwendelezo wa Riwaya hii Kwa kujiunga katika Group la bure WhatsApp. Kujiunga, Gusa Hapa
Tupate Wadhamini:
Soma: Jinsi ya Kuandika Barua ya Maombi ya Kazi
Soma: Jinsi ya Kuandika CV