Riwaya: Paspoti ya Gaidi

Riwaya: Paspoti ya Gaidi

PASPOTI YA GAIDI.
MTUNZI, Richard MWAMBE
SEHEMU ya 13
Hayuko peke yake, wako kama wane hivi, wote lazima washughulikiwe,” Briston akiajbu huku akifungua mlango kutoka. Nje ya hoteli hiyo kila mmoja alichukua gari yake na kuondoka. Lakini Kubrah aliitazama sana gari ya Amata na akaiona ikiwa palepale, ina maana huyu mshenzi bado yupo humu ndani? Akajiuliza. Na taratibu akaondosha gari yake pale hotelini huku akimwagiza mmoja wa vijana wake kuiangalia ile gari mpaka itakapoondoka.
Ile gari aliyopanda Amata iliingia ndani ya majengo yasiyokwisha ambayo bado yalikuwa yakiendelea na ujenzi, ikaingia na kufika mahali ndani ya kitu kama chumba hivi. Ikasimama na milango ikafunguliwa huku wale jamaa wakiteremka hai hai.
“Vipi huko?” mtu mmoja aliyeonekan kama mlinzi aliuliza.
“Jamaa kauawa bwana na tunayemsaka inaonekana katoroka eneo lile,” akajibu mmoja wa walioshuka kwenye ile gari.
“Kwa hiyo tunafanyaje?”
“Mpango ni uleule, kesho asubuhi, tunaondoka na Malkia na kuelekea kisiwani kwani mpango mwingine unatakiwa kuchukua nafasi, weka kila kitu sawa kama mpango ulivyo,” akatoa maagizo ambayo Amata alikuwa akiyasikia vyema. Kwa kutumia simu yake akatuma ujumbe mfupi kumpa Madam S juu ya hayo anayoyasikia. Kisha akatulia palepale kusubiri watu hao watoke eneo hilo ili naye aweze kujitokeza na kufanya yake.
IKULU
USIKU UOHUO
SIMU YA RAIS iliita kwa fujo, mheshimiwa bado alikuwa hajalala na wala hakuwa hata na lepe la usingizi, alipoitazama akajua ni ile simu nyeti ambayo huweza kukaa zaidi ya siku tatu bila kuita isipokuwa kwa jmabo muhimi na la kiusalama tu, akaitazama na kuona kwenye kioo TSA, akaiweka sikioni mara moja.
“Taarifa kutoka TSA juu ya usalama wa taifa usiku huu, naomba kikao cha dharula kama inawezekana,” upande wa pili ukasubiri jibu. Bila kusita Mheshimiwa Rais akakubali kikao hicho usiku huo akakata simu na kutoa taarifa kwa wanausalama wachache juu ya ujio wa Selina ndani ya jingo hilo jeupe.
Saa tisa usiku, mwanamama huyo aliwasili Ikulu na kupokelewa na mtu alioyeandaliwa na moja kwa moja alifikishwa kwenye ofisi ya Rais kwa mazungumzo.
“Kwanza samahani kukukatisha usingizi,” akaanza kwa kusema hivyo.
“Hapana Sellina, siwezi kupata usingizi kwa hali hii ambayo inanikabili, na najua ni wewe tu kwa sasa unaeweza kunipa jibu ambalo litanifariji, nipe maendeleo ya kazi niliyowapa,” Rais akamwambia kisha akatulia kitini.
“TSA tupo kwenye uchunguzi wa hali ya juu sana katika swala la uvamizi wa Ikulu uliofanyika hapa na tumeshagundua mambo mengi sana kuliko unavyotarajia kusikia…”
“Enhe…”
“Kwanza kabisa, mkuu umezungukwa na maadfua kila kona ndani ya idara zako na nchi yako kwa ujumla. Uvamizi wa Ikulu ulipangwa na watu walio chini yako kwenye idara nyeti za uslama…” akamweleza kila kitu lakini hakutaja wahusika wa tukio hilo. Mheshimiwa Rais alikuwa katika hali ya hasira na uchungu alipokuwa akipokea taarifa hiyo fupi lakini iliyojaa utaalam wa kikachero wa hali ya juu, moyoni mwake alimshukuru aliyekuwa na wazo la kuanzisha idara hii ambayo sasa anaielewa umuhimu wake.
“Sasa kuna watu ambao wapo chini ya jicho letu na tunahitaji kuwakamata mara moja ikiwezekana kwa amri yako usiku huu, hawa watatueleza vyema juu ya mpango mzima tangu mwanzo na nani anahusika,” Madam Sellina akaeleza na Rais akalipokea kwa kutikisa kichwa akiashiria kuwa amekubaliana naye. Lakini mpaka hapo hakuwa anajua ni nani na nani.
“Nani na nani?” akauliza.
“Wa kwanza ni Kepteni Benzilahagi…”
“Kepteni? Wa jeshi au wa meli?” akauliza kwa hamaki.
“Bora angekuwa wa meli, ni wa jeshi tena JW, tunamshuku kutokana na nyendo zake siku hizi, baadae nitakujulisha nyendo hizo lakini sio leo kwa sababu za kiusalama. Mbaya zaidi mtu huyu yupo kwenye kitengo nyeti sana ndani ya jeshi letu, nikiwa na maana kuwa anajua kila kitu, kila siri, kila mpango wa jeshi letu. Ni msaliti…”
“Akamatwe na ahojiwe mara moja!” Rais akatoa amri na kupiga ngumi juu ya meza baada ya kutajiwa kitengo cha mtu huyo.
“Na wa pili nani? Nataka kumjua!” akang’aka mheshimiwa.
“Wa pili ni afisa ubalozi wa Nduruta anaitwa Kimosa Kabalege, sasa kwa huyu tulisita kwa sababu za kidiplomasia,” Madam S akaeleza.
“Kamata, weka ndani ahojiwe. Sellina unataka kunambia hii ni njama kutoka Nduruta?” akauliza Mheshimiwa Rais huku akionekana wazi kuhamanika kwa mpango huo.
“Ndiyo Mheshimiwa, kumbuka umeamuru vikosi vyako vya JW kuvaa kofia ya UN na kwenda kuendesha operesheni dhidi ya waasi wa X65, waasi hawa kwa uchunguzi wetu ni watu wa Rais Sebutunva wa Nduruta na washirika wake ambao siku hizi umeona wakikutenga katika mambo mengi ya ki-kanda. Tumegundua kwamba wafadhili wakubwa wa waasi hawa ni vyama vyenye mlengo wa kushoto huko Ughaibuni, kwa biashara ya mabadilishano wa vitu wao hupeleka Almasi na kupewa silaha nzito na za kisasa. Hivyo basi kama kisasi kutoka kwa jirani yao Sebutunva ndiye aliyefanya mipango yote ya kutekwa kwa First Lady akishirikiana na watu ambao ni mapandikizi ambao kila siku unakula na kunywa nao…”
“Stop!!! Ishia hapohapo Sellina. Sasa nimeielewa TSA na kazi yake, mmefanya kazi kubwa sana na je habari zozote juu ya mke wangu?” akauliza kwa shauku.
“Ninavyoongea na wewe hapa tupo kazini, na kwa kuwa tulikwambia ni saa sabini na mbili tutakuwa na jibu, nakuhakikishia tuko mbioni kumpata First Lady katika saa zizi hizi,” Madam S alimhakikishia Sellina hayo asemayo. Baada ya dakika chache zilizofuata waliagana huku…
Oda ya kukamatwa Kepteni Benzilahagi ilifika makao makuu ya jeshi, Upanga. Usiku huohuo polisi wa jeshi, sita walikuwa ndani ya Nissan Patrol ya kijani wakielekea nyumbani kwa Kepteni huyo, walitumwa kazi moja tu, kumkamata Benzilahagi na kumpeleka walikoamriwa.
Scoba alisthuliwa na simu iliyokuwa ikifanya fujo mfukoni mwake alipoikwapua alikutana na TSA 2.
“Sema namba 2,” akaitikia.
“Kuna jamaa wanakuja hapo, waache wafanye kazi, kutoka ulipo hakikisha tu operesheni imekwenda sawa wala usitie nguvu yoyote,” Chiba akamaliza.
“Copy!”
Alipoishusha simu hiyo aliona taa za gari zilizowashwa full zikicheza na kuyumbayumba akajua moja kwa moja kuwa hiyo gari iko kasi sana kupita maelezo.
Kepteni Benzilahagi aliiweka vizuri bastola yake ikiwa full, akaipachika kiunoni mwake na kuvaa fulana yake pull neck pamija na jinzi yake nyeusi. Akaketi kitako akinywa pombe kali makusudi kusubiri kile anachokitarajia. Muungurumo wa gari ulimuondoa pale kitini, akasimama na kujiweka vizuri kitini huku simu yake iliyokuwa sikioni. Kengele ya mlango ikafuatia, akasimama na kuelekea mlangoni hapo, macho kwa macho akakutana na MP waliovalia kijeshi wakiwa kamili na barua yao mkononi ya kumkamata.
“Mmetumwa kunikamata mimi?” akawauliza huku akiwarudishia ile karatasi.
“Ndiyo, tunavyoongea hivi sasa unatakiwa kuondoka nasi,” wakamwambia.
“Kwa kosa gani hasa?”
“Kosa utalijua hukohuko ukifika,” wakamueleza.
“Sawa hakuna tabu, nipeni dakika moja tu nimuage mama watoto kisha nakuja,” akawaambia, nao wakamruhusu na kumsubiri palepale. Benzilahagi akatembea kwa mikogo huku akipiga mluzi kuelekea chumbani.
“Suzi! Suuuuzi! Mi naondoka Suzi naenda kazini…” akaongea huku akiingia chumbani na kuufunga mlango nyuma yake. Pumbavu sana, subirini hapohapo narudi, akasema kwa sauti ya kujisikia mwenyewe moyoni. Akavuta kabati kubwa na kulisukuma pembeni kisha akatoa funguo zake na na kufungua mlango uliokuwa nyuma ya kabati hilo, alipoingia ndani ya kijichumba hicho, akarudisha lile kabati palepale na kuufunga mlango kisha akateremka ngazi zinazokwenda chini kisha akapita kwenye kitu kama andaki na kutokea nje ya ukuta kulikokuwa na kitu kama chemba ya maji taka. Alipomaliza kuurudishia ule mfuniko wa chuma, akajipukuta vumbi na kutokomea katika majumba ya jirani.
“Asee huyu jamaa anaaga kwa maneno au kapanda kitandani kabisa?” MP mmoja akauliza.
“Ah kweli hebu tumfatilie hukohuko dakika kumi sasa,” mwingine aliyekuwa kiongozi wao akawaambia kisha akawaongoza kuingia ndani ya jumba lile, walipoufikia lango wa chumbani, wakagonga, kimya, hakuna jibu wakagonga tena na tena, kimya kilekile kikaendelea. Alipousukuma, ukafunguka, wakaingia chumbani, wakatanabahi hakuna mtu, kitanda tupu.
“Unataka kusema kaondoka hapa hapa?” mmoja akauliza huku akitupa godoro upande wa pili, hakuna mtu. Mwingine alikuwa akipekuwa makabati bila mafanikio.
“Jamaa katoroka, lakini kapitia wapi? Mbona hakuna mlango humu? Atakuwepo tu mumu humu. Dakika ishiririni ziliwachukua kupekua chumba hicho lakini hawakuona mtu wala nyau.
“Ni aibu, tumewezwa!” Yule kiongozi wao akaongea huku mikono ikiwa kichwani na wakati huo akitoka nje ya chumba kile, “Hebu zunguka nyumba muifanyie ukaguzi huko nje,” akaamuru na vijana wake wakafanya hivyo.
Scoba akiwa ndani ya gari yake ametulia tuli, aliona kitu kama kivuli kikipita nyuma ya ga ri hiyo, alipogeuka akamwona mtu, mwanaume anayeishia kizani. Machale yakamcheza, akainuka na kuufungua mlango taratibu kisha akafuata njia ile ambayo yule kijana aliingia. Kona ya kwanza nay a pili akasikia mlio wa injini ya gari iliyokuwa ikiwashwa na gari ile ikaondoka zake. Scoba akajikuta anashindwa la kufanya kwa wakati ule, akarudi haraka kwenye gari yake na alipoiwasha na kuigeuza akasimamishwa na wale MP.
“Teremka chini ukiwa mikono kichwani,” akaamuriwa. Scoba akateremka na kusimama akiwa mikono kichwani. Wakampekua harakaharaka na kumwacha pembeni.
“Unafanya nini hapa usiku huu?” mmoja akauliza.
“Kuna mtu namsubiri,” akajibu.
“Haujaona mtu kapita hapa sasa hivi?”
“Nimemwona, alitokea upande huu!” akajibu.
“Kaenda wapi?”
“Kapita hapa hivi kaingia upande wa pili,” akawaelekeza na wale MP wakalekea upande ule, alipohakikisha wamepotelea kizani akawasha gri na kuondoka kwa kasi kuelekea upande ule ambao Benzilahagi amekwenda na gari, akajaribu kuifuata bila mafanikio, Kepteni Benzilahagi alikuwa ametoweka.
Itaendelea.
 
PASPOTI YA GAIDI.
MTUNZI, Richard MWAMBE
SEHEMU ya 13
Hayuko peke yake, wako kama wane hivi, wote lazima washughulikiwe,” Briston akiajbu huku akifungua mlango kutoka. Nje ya hoteli hiyo kila mmoja alichukua gari yake na kuondoka. Lakini Kubrah aliitazama sana gari ya Amata na akaiona ikiwa palepale, ina maana huyu mshenzi bado yupo humu ndani? Akajiuliza. Na taratibu akaondosha gari yake pale hotelini huku akimwagiza mmoja wa vijana wake kuiangalia ile gari mpaka itakapoondoka.
Ile gari aliyopanda Amata iliingia ndani ya majengo yasiyokwisha ambayo bado yalikuwa yakiendelea na ujenzi, ikaingia na kufika mahali ndani ya kitu kama chumba hivi. Ikasimama na milango ikafunguliwa huku wale jamaa wakiteremka hai hai.
“Vipi huko?” mtu mmoja aliyeonekan kama mlinzi aliuliza.
“Jamaa kauawa bwana na tunayemsaka inaonekana katoroka eneo lile,” akajibu mmoja wa walioshuka kwenye ile gari.
“Kwa hiyo tunafanyaje?”
“Mpango ni uleule, kesho asubuhi, tunaondoka na Malkia na kuelekea kisiwani kwani mpango mwingine unatakiwa kuchukua nafasi, weka kila kitu sawa kama mpango ulivyo,” akatoa maagizo ambayo Amata alikuwa akiyasikia vyema. Kwa kutumia simu yake akatuma ujumbe mfupi kumpa Madam S juu ya hayo anayoyasikia. Kisha akatulia palepale kusubiri watu hao watoke eneo hilo ili naye aweze kujitokeza na kufanya yake.
IKULU
USIKU UOHUO
SIMU YA RAIS iliita kwa fujo, mheshimiwa bado alikuwa hajalala na wala hakuwa hata na lepe la usingizi, alipoitazama akajua ni ile simu nyeti ambayo huweza kukaa zaidi ya siku tatu bila kuita isipokuwa kwa jmabo muhimi na la kiusalama tu, akaitazama na kuona kwenye kioo TSA, akaiweka sikioni mara moja.
“Taarifa kutoka TSA juu ya usalama wa taifa usiku huu, naomba kikao cha dharula kama inawezekana,” upande wa pili ukasubiri jibu. Bila kusita Mheshimiwa Rais akakubali kikao hicho usiku huo akakata simu na kutoa taarifa kwa wanausalama wachache juu ya ujio wa Selina ndani ya jingo hilo jeupe.
Saa tisa usiku, mwanamama huyo aliwasili Ikulu na kupokelewa na mtu alioyeandaliwa na moja kwa moja alifikishwa kwenye ofisi ya Rais kwa mazungumzo.
“Kwanza samahani kukukatisha usingizi,” akaanza kwa kusema hivyo.
“Hapana Sellina, siwezi kupata usingizi kwa hali hii ambayo inanikabili, na najua ni wewe tu kwa sasa unaeweza kunipa jibu ambalo litanifariji, nipe maendeleo ya kazi niliyowapa,” Rais akamwambia kisha akatulia kitini.
“TSA tupo kwenye uchunguzi wa hali ya juu sana katika swala la uvamizi wa Ikulu uliofanyika hapa na tumeshagundua mambo mengi sana kuliko unavyotarajia kusikia…”
“Enhe…”
“Kwanza kabisa, mkuu umezungukwa na maadfua kila kona ndani ya idara zako na nchi yako kwa ujumla. Uvamizi wa Ikulu ulipangwa na watu walio chini yako kwenye idara nyeti za uslama…” akamweleza kila kitu lakini hakutaja wahusika wa tukio hilo. Mheshimiwa Rais alikuwa katika hali ya hasira na uchungu alipokuwa akipokea taarifa hiyo fupi lakini iliyojaa utaalam wa kikachero wa hali ya juu, moyoni mwake alimshukuru aliyekuwa na wazo la kuanzisha idara hii ambayo sasa anaielewa umuhimu wake.
“Sasa kuna watu ambao wapo chini ya jicho letu na tunahitaji kuwakamata mara moja ikiwezekana kwa amri yako usiku huu, hawa watatueleza vyema juu ya mpango mzima tangu mwanzo na nani anahusika,” Madam Sellina akaeleza na Rais akalipokea kwa kutikisa kichwa akiashiria kuwa amekubaliana naye. Lakini mpaka hapo hakuwa anajua ni nani na nani.
“Nani na nani?” akauliza.
“Wa kwanza ni Kepteni Benzilahagi…”
“Kepteni? Wa jeshi au wa meli?” akauliza kwa hamaki.
“Bora angekuwa wa meli, ni wa jeshi tena JW, tunamshuku kutokana na nyendo zake siku hizi, baadae nitakujulisha nyendo hizo lakini sio leo kwa sababu za kiusalama. Mbaya zaidi mtu huyu yupo kwenye kitengo nyeti sana ndani ya jeshi letu, nikiwa na maana kuwa anajua kila kitu, kila siri, kila mpango wa jeshi letu. Ni msaliti…”
“Akamatwe na ahojiwe mara moja!” Rais akatoa amri na kupiga ngumi juu ya meza baada ya kutajiwa kitengo cha mtu huyo.
“Na wa pili nani? Nataka kumjua!” akang’aka mheshimiwa.
“Wa pili ni afisa ubalozi wa Nduruta anaitwa Kimosa Kabalege, sasa kwa huyu tulisita kwa sababu za kidiplomasia,” Madam S akaeleza.
“Kamata, weka ndani ahojiwe. Sellina unataka kunambia hii ni njama kutoka Nduruta?” akauliza Mheshimiwa Rais huku akionekana wazi kuhamanika kwa mpango huo.
“Ndiyo Mheshimiwa, kumbuka umeamuru vikosi vyako vya JW kuvaa kofia ya UN na kwenda kuendesha operesheni dhidi ya waasi wa X65, waasi hawa kwa uchunguzi wetu ni watu wa Rais Sebutunva wa Nduruta na washirika wake ambao siku hizi umeona wakikutenga katika mambo mengi ya ki-kanda. Tumegundua kwamba wafadhili wakubwa wa waasi hawa ni vyama vyenye mlengo wa kushoto huko Ughaibuni, kwa biashara ya mabadilishano wa vitu wao hupeleka Almasi na kupewa silaha nzito na za kisasa. Hivyo basi kama kisasi kutoka kwa jirani yao Sebutunva ndiye aliyefanya mipango yote ya kutekwa kwa First Lady akishirikiana na watu ambao ni mapandikizi ambao kila siku unakula na kunywa nao…”
“Stop!!! Ishia hapohapo Sellina. Sasa nimeielewa TSA na kazi yake, mmefanya kazi kubwa sana na je habari zozote juu ya mke wangu?” akauliza kwa shauku.
“Ninavyoongea na wewe hapa tupo kazini, na kwa kuwa tulikwambia ni saa sabini na mbili tutakuwa na jibu, nakuhakikishia tuko mbioni kumpata First Lady katika saa zizi hizi,” Madam S alimhakikishia Sellina hayo asemayo. Baada ya dakika chache zilizofuata waliagana huku…
Oda ya kukamatwa Kepteni Benzilahagi ilifika makao makuu ya jeshi, Upanga. Usiku huohuo polisi wa jeshi, sita walikuwa ndani ya Nissan Patrol ya kijani wakielekea nyumbani kwa Kepteni huyo, walitumwa kazi moja tu, kumkamata Benzilahagi na kumpeleka walikoamriwa.
Scoba alisthuliwa na simu iliyokuwa ikifanya fujo mfukoni mwake alipoikwapua alikutana na TSA 2.
“Sema namba 2,” akaitikia.
“Kuna jamaa wanakuja hapo, waache wafanye kazi, kutoka ulipo hakikisha tu operesheni imekwenda sawa wala usitie nguvu yoyote,” Chiba akamaliza.
“Copy!”
Alipoishusha simu hiyo aliona taa za gari zilizowashwa full zikicheza na kuyumbayumba akajua moja kwa moja kuwa hiyo gari iko kasi sana kupita maelezo.
Kepteni Benzilahagi aliiweka vizuri bastola yake ikiwa full, akaipachika kiunoni mwake na kuvaa fulana yake pull neck pamija na jinzi yake nyeusi. Akaketi kitako akinywa pombe kali makusudi kusubiri kile anachokitarajia. Muungurumo wa gari ulimuondoa pale kitini, akasimama na kujiweka vizuri kitini huku simu yake iliyokuwa sikioni. Kengele ya mlango ikafuatia, akasimama na kuelekea mlangoni hapo, macho kwa macho akakutana na MP waliovalia kijeshi wakiwa kamili na barua yao mkononi ya kumkamata.
“Mmetumwa kunikamata mimi?” akawauliza huku akiwarudishia ile karatasi.
“Ndiyo, tunavyoongea hivi sasa unatakiwa kuondoka nasi,” wakamwambia.
“Kwa kosa gani hasa?”
“Kosa utalijua hukohuko ukifika,” wakamueleza.
“Sawa hakuna tabu, nipeni dakika moja tu nimuage mama watoto kisha nakuja,” akawaambia, nao wakamruhusu na kumsubiri palepale. Benzilahagi akatembea kwa mikogo huku akipiga mluzi kuelekea chumbani.
“Suzi! Suuuuzi! Mi naondoka Suzi naenda kazini…” akaongea huku akiingia chumbani na kuufunga mlango nyuma yake. Pumbavu sana, subirini hapohapo narudi, akasema kwa sauti ya kujisikia mwenyewe moyoni. Akavuta kabati kubwa na kulisukuma pembeni kisha akatoa funguo zake na na kufungua mlango uliokuwa nyuma ya kabati hilo, alipoingia ndani ya kijichumba hicho, akarudisha lile kabati palepale na kuufunga mlango kisha akateremka ngazi zinazokwenda chini kisha akapita kwenye kitu kama andaki na kutokea nje ya ukuta kulikokuwa na kitu kama chemba ya maji taka. Alipomaliza kuurudishia ule mfuniko wa chuma, akajipukuta vumbi na kutokomea katika majumba ya jirani.
“Asee huyu jamaa anaaga kwa maneno au kapanda kitandani kabisa?” MP mmoja akauliza.
“Ah kweli hebu tumfatilie hukohuko dakika kumi sasa,” mwingine aliyekuwa kiongozi wao akawaambia kisha akawaongoza kuingia ndani ya jumba lile, walipoufikia lango wa chumbani, wakagonga, kimya, hakuna jibu wakagonga tena na tena, kimya kilekile kikaendelea. Alipousukuma, ukafunguka, wakaingia chumbani, wakatanabahi hakuna mtu, kitanda tupu.
“Unataka kusema kaondoka hapa hapa?” mmoja akauliza huku akitupa godoro upande wa pili, hakuna mtu. Mwingine alikuwa akipekuwa makabati bila mafanikio.
“Jamaa katoroka, lakini kapitia wapi? Mbona hakuna mlango humu? Atakuwepo tu mumu humu. Dakika ishiririni ziliwachukua kupekua chumba hicho lakini hawakuona mtu wala nyau.
“Ni aibu, tumewezwa!” Yule kiongozi wao akaongea huku mikono ikiwa kichwani na wakati huo akitoka nje ya chumba kile, “Hebu zunguka nyumba muifanyie ukaguzi huko nje,” akaamuru na vijana wake wakafanya hivyo.
Scoba akiwa ndani ya gari yake ametulia tuli, aliona kitu kama kivuli kikipita nyuma ya ga ri hiyo, alipogeuka akamwona mtu, mwanaume anayeishia kizani. Machale yakamcheza, akainuka na kuufungua mlango taratibu kisha akafuata njia ile ambayo yule kijana aliingia. Kona ya kwanza nay a pili akasikia mlio wa injini ya gari iliyokuwa ikiwashwa na gari ile ikaondoka zake. Scoba akajikuta anashindwa la kufanya kwa wakati ule, akarudi haraka kwenye gari yake na alipoiwasha na kuigeuza akasimamishwa na wale MP.
“Teremka chini ukiwa mikono kichwani,” akaamuriwa. Scoba akateremka na kusimama akiwa mikono kichwani. Wakampekua harakaharaka na kumwacha pembeni.
“Unafanya nini hapa usiku huu?” mmoja akauliza.
“Kuna mtu namsubiri,” akajibu.
“Haujaona mtu kapita hapa sasa hivi?”
“Nimemwona, alitokea upande huu!” akajibu.
“Kaenda wapi?”
“Kapita hapa hivi kaingia upande wa pili,” akawaelekeza na wale MP wakalekea upande ule, alipohakikisha wamepotelea kizani akawasha gri na kuondoka kwa kasi kuelekea upande ule ambao Benzilahagi amekwenda na gari, akajaribu kuifuata bila mafanikio, Kepteni Benzilahagi alikuwa ametoweka.
Itaendelea.

Sehr gut [emoji106]
 
wa
PASPOTI YA GAIDI.
MTUNZI, Richard MWAMBE
SEHEMU ya 13
Hayuko peke yake, wako kama wane hivi, wote lazima washughulikiwe,” Briston akiajbu huku akifungua mlango kutoka. Nje ya hoteli hiyo kila mmoja alichukua gari yake na kuondoka. Lakini Kubrah aliitazama sana gari ya Amata na akaiona ikiwa palepale, ina maana huyu mshenzi bado yupo humu ndani? Akajiuliza. Na taratibu akaondosha gari yake pale hotelini huku akimwagiza mmoja wa vijana wake kuiangalia ile gari mpaka itakapoondoka.
Ile gari aliyopanda Amata iliingia ndani ya majengo yasiyokwisha ambayo bado yalikuwa yakiendelea na ujenzi, ikaingia na kufika mahali ndani ya kitu kama chumba hivi. Ikasimama na milango ikafunguliwa huku wale jamaa wakiteremka hai hai.
“Vipi huko?” mtu mmoja aliyeonekan kama mlinzi aliuliza.
“Jamaa kauawa bwana na tunayemsaka inaonekana katoroka eneo lile,” akajibu mmoja wa walioshuka kwenye ile gari.
“Kwa hiyo tunafanyaje?”
“Mpango ni uleule, kesho asubuhi, tunaondoka na Malkia na kuelekea kisiwani kwani mpango mwingine unatakiwa kuchukua nafasi, weka kila kitu sawa kama mpango ulivyo,” akatoa maagizo ambayo Amata alikuwa akiyasikia vyema. Kwa kutumia simu yake akatuma ujumbe mfupi kumpa Madam S juu ya hayo anayoyasikia. Kisha akatulia palepale kusubiri watu hao watoke eneo hilo ili naye aweze kujitokeza na kufanya yake.
IKULU
USIKU UOHUO
SIMU YA RAIS iliita kwa fujo, mheshimiwa bado alikuwa hajalala na wala hakuwa hata na lepe la usingizi, alipoitazama akajua ni ile simu nyeti ambayo huweza kukaa zaidi ya siku tatu bila kuita isipokuwa kwa jmabo muhimi na la kiusalama tu, akaitazama na kuona kwenye kioo TSA, akaiweka sikioni mara moja.
“Taarifa kutoka TSA juu ya usalama wa taifa usiku huu, naomba kikao cha dharula kama inawezekana,” upande wa pili ukasubiri jibu. Bila kusita Mheshimiwa Rais akakubali kikao hicho usiku huo akakata simu na kutoa taarifa kwa wanausalama wachache juu ya ujio wa Selina ndani ya jingo hilo jeupe.
Saa tisa usiku, mwanamama huyo aliwasili Ikulu na kupokelewa na mtu alioyeandaliwa na moja kwa moja alifikishwa kwenye ofisi ya Rais kwa mazungumzo.
“Kwanza samahani kukukatisha usingizi,” akaanza kwa kusema hivyo.
“Hapana Sellina, siwezi kupata usingizi kwa hali hii ambayo inanikabili, na najua ni wewe tu kwa sasa unaeweza kunipa jibu ambalo litanifariji, nipe maendeleo ya kazi niliyowapa,” Rais akamwambia kisha akatulia kitini.
“TSA tupo kwenye uchunguzi wa hali ya juu sana katika swala la uvamizi wa Ikulu uliofanyika hapa na tumeshagundua mambo mengi sana kuliko unavyotarajia kusikia…”
“Enhe…”
“Kwanza kabisa, mkuu umezungukwa na maadfua kila kona ndani ya idara zako na nchi yako kwa ujumla. Uvamizi wa Ikulu ulipangwa na watu walio chini yako kwenye idara nyeti za uslama…” akamweleza kila kitu lakini hakutaja wahusika wa tukio hilo. Mheshimiwa Rais alikuwa katika hali ya hasira na uchungu alipokuwa akipokea taarifa hiyo fupi lakini iliyojaa utaalam wa kikachero wa hali ya juu, moyoni mwake alimshukuru aliyekuwa na wazo la kuanzisha idara hii ambayo sasa anaielewa umuhimu wake.
“Sasa kuna watu ambao wapo chini ya jicho letu na tunahitaji kuwakamata mara moja ikiwezekana kwa amri yako usiku huu, hawa watatueleza vyema juu ya mpango mzima tangu mwanzo na nani anahusika,” Madam Sellina akaeleza na Rais akalipokea kwa kutikisa kichwa akiashiria kuwa amekubaliana naye. Lakini mpaka hapo hakuwa anajua ni nani na nani.
“Nani na nani?” akauliza.
“Wa kwanza ni Kepteni Benzilahagi…”
“Kepteni? Wa jeshi au wa meli?” akauliza kwa hamaki.
“Bora angekuwa wa meli, ni wa jeshi tena JW, tunamshuku kutokana na nyendo zake siku hizi, baadae nitakujulisha nyendo hizo lakini sio leo kwa sababu za kiusalama. Mbaya zaidi mtu huyu yupo kwenye kitengo nyeti sana ndani ya jeshi letu, nikiwa na maana kuwa anajua kila kitu, kila siri, kila mpango wa jeshi letu. Ni msaliti…”
“Akamatwe na ahojiwe mara moja!” Rais akatoa amri na kupiga ngumi juu ya meza baada ya kutajiwa kitengo cha mtu huyo.
“Na wa pili nani? Nataka kumjua!” akang’aka mheshimiwa.
“Wa pili ni afisa ubalozi wa Nduruta anaitwa Kimosa Kabalege, sasa kwa huyu tulisita kwa sababu za kidiplomasia,” Madam S akaeleza.
“Kamata, weka ndani ahojiwe. Sellina unataka kunambia hii ni njama kutoka Nduruta?” akauliza Mheshimiwa Rais huku akionekana wazi kuhamanika kwa mpango huo.
“Ndiyo Mheshimiwa, kumbuka umeamuru vikosi vyako vya JW kuvaa kofia ya UN na kwenda kuendesha operesheni dhidi ya waasi wa X65, waasi hawa kwa uchunguzi wetu ni watu wa Rais Sebutunva wa Nduruta na washirika wake ambao siku hizi umeona wakikutenga katika mambo mengi ya ki-kanda. Tumegundua kwamba wafadhili wakubwa wa waasi hawa ni vyama vyenye mlengo wa kushoto huko Ughaibuni, kwa biashara ya mabadilishano wa vitu wao hupeleka Almasi na kupewa silaha nzito na za kisasa. Hivyo basi kama kisasi kutoka kwa jirani yao Sebutunva ndiye aliyefanya mipango yote ya kutekwa kwa First Lady akishirikiana na watu ambao ni mapandikizi ambao kila siku unakula na kunywa nao…”
“Stop!!! Ishia hapohapo Sellina. Sasa nimeielewa TSA na kazi yake, mmefanya kazi kubwa sana na je habari zozote juu ya mke wangu?” akauliza kwa shauku.
“Ninavyoongea na wewe hapa tupo kazini, na kwa kuwa tulikwambia ni saa sabini na mbili tutakuwa na jibu, nakuhakikishia tuko mbioni kumpata First Lady katika saa zizi hizi,” Madam S alimhakikishia Sellina hayo asemayo. Baada ya dakika chache zilizofuata waliagana huku…
Oda ya kukamatwa Kepteni Benzilahagi ilifika makao makuu ya jeshi, Upanga. Usiku huohuo polisi wa jeshi, sita walikuwa ndani ya Nissan Patrol ya kijani wakielekea nyumbani kwa Kepteni huyo, walitumwa kazi moja tu, kumkamata Benzilahagi na kumpeleka walikoamriwa.
Scoba alisthuliwa na simu iliyokuwa ikifanya fujo mfukoni mwake alipoikwapua alikutana na TSA 2.
“Sema namba 2,” akaitikia.
“Kuna jamaa wanakuja hapo, waache wafanye kazi, kutoka ulipo hakikisha tu operesheni imekwenda sawa wala usitie nguvu yoyote,” Chiba akamaliza.
“Copy!”
Alipoishusha simu hiyo aliona taa za gari zilizowashwa full zikicheza na kuyumbayumba akajua moja kwa moja kuwa hiyo gari iko kasi sana kupita maelezo.
Kepteni Benzilahagi aliiweka vizuri bastola yake ikiwa full, akaipachika kiunoni mwake na kuvaa fulana yake pull neck pamija na jinzi yake nyeusi. Akaketi kitako akinywa pombe kali makusudi kusubiri kile anachokitarajia. Muungurumo wa gari ulimuondoa pale kitini, akasimama na kujiweka vizuri kitini huku simu yake iliyokuwa sikioni. Kengele ya mlango ikafuatia, akasimama na kuelekea mlangoni hapo, macho kwa macho akakutana na MP waliovalia kijeshi wakiwa kamili na barua yao mkononi ya kumkamata.
“Mmetumwa kunikamata mimi?” akawauliza huku akiwarudishia ile karatasi.
“Ndiyo, tunavyoongea hivi sasa unatakiwa kuondoka nasi,” wakamwambia.
“Kwa kosa gani hasa?”
“Kosa utalijua hukohuko ukifika,” wakamueleza.
“Sawa hakuna tabu, nipeni dakika moja tu nimuage mama watoto kisha nakuja,” akawaambia, nao wakamruhusu na kumsubiri palepale. Benzilahagi akatembea kwa mikogo huku akipiga mluzi kuelekea chumbani.
“Suzi! Suuuuzi! Mi naondoka Suzi naenda kazini…” akaongea huku akiingia chumbani na kuufunga mlango nyuma yake. Pumbavu sana, subirini hapohapo narudi, akasema kwa sauti ya kujisikia mwenyewe moyoni. Akavuta kabati kubwa na kulisukuma pembeni kisha akatoa funguo zake na na kufungua mlango uliokuwa nyuma ya kabati hilo, alipoingia ndani ya kijichumba hicho, akarudisha lile kabati palepale na kuufunga mlango kisha akateremka ngazi zinazokwenda chini kisha akapita kwenye kitu kama andaki na kutokea nje ya ukuta kulikokuwa na kitu kama chemba ya maji taka. Alipomaliza kuurudishia ule mfuniko wa chuma, akajipukuta vumbi na kutokomea katika majumba ya jirani.
“Asee huyu jamaa anaaga kwa maneno au kapanda kitandani kabisa?” MP mmoja akauliza.
“Ah kweli hebu tumfatilie hukohuko dakika kumi sasa,” mwingine aliyekuwa kiongozi wao akawaambia kisha akawaongoza kuingia ndani ya jumba lile, walipoufikia lango wa chumbani, wakagonga, kimya, hakuna jibu wakagonga tena na tena, kimya kilekile kikaendelea. Alipousukuma, ukafunguka, wakaingia chumbani, wakatanabahi hakuna mtu, kitanda tupu.
“Unataka kusema kaondoka hapa hapa?” mmoja akauliza huku akitupa godoro upande wa pili, hakuna mtu. Mwingine alikuwa akipekuwa makabati bila mafanikio.
“Jamaa katoroka, lakini kapitia wapi? Mbona hakuna mlango humu? Atakuwepo tu mumu humu. Dakika ishiririni ziliwachukua kupekua chumba hicho lakini hawakuona mtu wala nyau.
“Ni aibu, tumewezwa!” Yule kiongozi wao akaongea huku mikono ikiwa kichwani na wakati huo akitoka nje ya chumba kile, “Hebu zunguka nyumba muifanyie ukaguzi huko nje,” akaamuru na vijana wake wakafanya hivyo.
Scoba akiwa ndani ya gari yake ametulia tuli, aliona kitu kama kivuli kikipita nyuma ya ga ri hiyo, alipogeuka akamwona mtu, mwanaume anayeishia kizani. Machale yakamcheza, akainuka na kuufungua mlango taratibu kisha akafuata njia ile ambayo yule kijana aliingia. Kona ya kwanza nay a pili akasikia mlio wa injini ya gari iliyokuwa ikiwashwa na gari ile ikaondoka zake. Scoba akajikuta anashindwa la kufanya kwa wakati ule, akarudi haraka kwenye gari yake na alipoiwasha na kuigeuza akasimamishwa na wale MP.
“Teremka chini ukiwa mikono kichwani,” akaamuriwa. Scoba akateremka na kusimama akiwa mikono kichwani. Wakampekua harakaharaka na kumwacha pembeni.
“Unafanya nini hapa usiku huu?” mmoja akauliza.
“Kuna mtu namsubiri,” akajibu.
“Haujaona mtu kapita hapa sasa hivi?”
“Nimemwona, alitokea upande huu!” akajibu.
“Kaenda wapi?”
“Kapita hapa hivi kaingia upande wa pili,” akawaelekeza na wale MP wakalekea upande ule, alipohakikisha wamepotelea kizani akawasha gri na kuondoka kwa kasi kuelekea upande ule ambao Benzilahagi amekwenda na gari, akajaribu kuifuata bila mafanikio, Kepteni Benzilahagi alikuwa ametoweka.
Itaendelea.
bheja mkuu
 
RIWAYA; PASIPOTI YA GAIDI
Hujuma na uzandiki
MTUNZI: richard MWAMBE
“Unataka kusema kaondoka hapa hapa?” mmoja akauliza huku akitupa godoro upande wa pili, hakuna mtu. Mwingine alikuwa akipekuwa makabati bila mafanikio.
“Jamaa katoroka, lakini kapitia wapi? Mbona hakuna mlango humu? Atakuwepo tu mumu humu. Dakika ishiririni ziliwachukua kupekua chumba hicho lakini hawakuona mtu wala nyau.
“Ni aibu, tumewezwa!” Yule kiongozi wao akaongea huku mikono ikiwa kichwani na wakati huo akitoka nje ya chumba kile, “Hebu zunguka nyumba muifanyie ukaguzi huko nje,” akaamuru na vijana wake wakafanya hivyo.
SEHEMU YA 14
Scoba akiwa ndani ya gari yake ametulia tuli, aliona kitu kama kivuli kikipita nyuma ya ga ri hiyo, alipogeuka akamwona mtu, mwanaume anayeishia kizani. Machale yakamcheza, akainuka na kuufungua mlango taratibu kisha akafuata njia ile ambayo yule kijana aliingia. Kona ya kwanza nay a pili akasikia mlio wa injini ya gari iliyokuwa ikiwashwa na gari ile ikaondoka zake. Scoba akajikuta anashindwa la kufanya kwa wakati ule, akarudi haraka kwenye gari yake na alipoiwasha na kuigeuza akasimamishwa na wale MP.
“Teremka chini ukiwa mikono kichwani,” akaamuriwa. Scoba akateremka na kusimama akiwa mikono kichwani. Wakampekua harakaharaka na kumwacha pembeni.
“Unafanya nini hapa usiku huu?” mmoja akauliza.
“Kuna mtu namsubiri,” akajibu.
“Haujaona mtu kapita hapa sasa hivi?”
“Nimemwona, alitokea upande huu!” akajibu.
“Kaenda wapi?”
“Kapita hapa hivi kaingia upande wa pili,” akawaelekeza na wale MP wakalekea upande ule, alipohakikisha wamepotelea kizani akawasha gri na kuondoka kwa kasi kuelekea upande ule ambao Benzilahagi amekwenda na gari, akajaribu kuifuata bila mafanikio, Kepteni Benzilahagi alikuwa ametoweka.
Ukimya ukatawala, Amata akasukuma juu mfuniko wa buti lile, kwa uwazi mdogo akatazama nje hakuona kitu zaidi ya giza. Wameondoka, akawaza na kufungua lile buti kisha akatoka na kulifunga taratibu, akanyata na kujibanza kando ya pipa moja lililojaa zege ndani yake. Hakukuonekana kitu kingine zaidi ya giza lile na miale hafifu ya taa za nje iliyokuwa ikipenya kati ya uwazi na uwazi. Ijapokuwa kulikuwa na giza lakini Amata aliweza kuona kwa taabu mlango wa bati uliokuwa umerudishiwa tu, akavuta hatua mbili tatu na kuufikia alipotaka tu kuugusa akasikia michakacho ya hatua za binadamu kutoka upande wa pili wa mlango ule ambao ulikuwa haujafunga kabisa na kuruhusu nafasi kama ya milimita tano hivi kuwa wazi, akarudi na kujificha nyuma yake, akasubiri.
“Tizo!” sauti ikaita kutoka ndani.
“Sema we!” Tizo akaitikia. Amata akatikisa kichwa baada ya kujua kuwa jina la huyo kijana ni Tizo.
“Usichelewe kaka, digala anatia timu sasa hivi ili tucheki mpango wa kesho,” ile sautin ikatoa maagizo.
“Poa poa,” akajibu huku akiufungua ule mlango, akatoka na kuurudisha tena nyuma yake kisha akavuta hatua kuelekea kwenye lango kubwa la chumba kile.
Kutoka alipojificha Kamanda Amata akapiga mruzi wa taratibu uliomfanya Tizo asimame pale alipo, kabla hajajua nini kinaendelea, alijikuta akipata pigo zito lililotua katikati ya paji lake la uso, kisha Amata akamdaka kabla hajafika chini. Tizo alikuwa hana fahamu, Amata akamburuza taratibu na kumpakia kwenye ile gari, ndani ya buti na kumfungia. Kisha moja kwa moja akauendea ule mlango na kuufuangua, kelele za ule mlango zilimfanya Amata kuganda kama kapigwa shoti ya umeme. Sekunde kadhaa mbele, akateremka ngazi zilizokuwa zikielekea chini ya jingo hilo na huko akakutana na mlango mwingine mzuri tena isitoshe ni wa kisasa. Akautazama kwa jicho lake la kikachero, kwa maana mlango huu haukuwa na kitasa. Chini yake kulikuwa na zuria zito, akalikanyaga na ule mlango ukafunguka, Amata alipitisha jicho harakaharaka na kuona ndani kile chumba kuna nini. Watu wawili walikuwa wamekati katik sebule safi, mmoja mwafrika na mwingine alikuwa na asili ya kichina si kichina, kifilipino si kilipino, alikuwepokuwepo tu. Akiwa katika kutafakari, akaona mtu wa tatu akiongezeka akiwa na vinywaji mkononi. TSA 1 akaitazama saa yake, saa zinayoyoma, karibu alfajiri itanikuta, akawaza kisha akapenyeza mkono katika mlango huo na kuupeleka upande wa kushoto kuitafuta swichi ya taa hiyo maana alijuwa kuwa kaatika sheria za mafundi umeme za kimataifa swichi ya taa huwekwa upande tofauti na ule ambao mlango hufungukia. Akaipata na kuibofya.
“Ta!” mlio huo wa swichi ukafuatiwa na giza nene.
“Aaaaa shittt! Tanesco! Hili shirika bora wabinafsishe tu, namna hii!” mmoj wa wale jama akapiga makelele. Amata kama umeme akajirusha ndani na bastola mkononi, akajibiringisha na kutua kwenye kona aliyoitaka. Risasi ya kwanza haikufanya kosa, ikavunja bega la mmoja wao, ile ya pili ikafumua kichwa cha mwingine. Taa zikawaka, Amata akageuza macho mlangoni na kuona domo la bastola likimtazama, akajikunja na kuruka back akiziacha risasi za bastola hiyo zichimbe ukuta wakati yeye keishatua upande mwingine.
“Ah! Ah! Ah! Umejiingiza kwenye domo la mamba siyo?” Yule kijana aliyeonekana kujazia mwili wake akamwambia Amata, “Nilijua hutoweza kupafahamu hapa kumbe wewe mtundu sana kama nilivyopewa taarifa, sasa leo utaishia humu humu,” akaongeza huku bastola yake bado ikiwa mkononi.
“Nini kimekuleta kama si kifo chako?” akauliza.
“Nimemfuata First Lady,” Amata akajibu akiwa bado nyuma ya meza alikojificha baada ya ile sarakasi maridadi.
“First Lady! Unajua sisi tulivyomchukua tulikuwa wangapi? Na unajua mbinu tuliyoitumia? Halafu wewe uje peke yako ukiamini kumpata. Kwa taarifa yako na alfajiri hii anaondoka anapelekwa hukooooo akale honeymoon!” Yule jamaa mawnye asili isiyo rasmi akasema. Amata kwa jicho lake la kikachero aligundua kuwa huyo jamaa aliyesimama kama mita tano hivi mbele yake alikuwa hatazami upande ule isipokuwa mwingine, akageuza jicho kwa chati na kumuona Yule aliympiga risasi ya bega akiwa anachomoa bastola yake taratibu, akasubiri mkono wake ukae sawa kiunoni na lilipotimia hilo, alijirusha na kumtandika teke la usoni, mguno wa uchungu ukasikika, kwa kasi ya ajabu Amata akaiweka sawa bastola yake na kuifumua taa, giza likarudi tena na milio ya risasi ikasikika huku na huko.
“Umeniua bro!” sauti ilisikika kutoka pale chini, Amata akajua tayari washauana wenyewe kwa wenyewe.
“Nikikutia mkononi wewe nyau utajua kilichomtoa kanga manyoya,” Yule jamaa akaunguruma kwa hasira.
“Huwezi, na sasa nataka unieleze ni wapi alipo First Lady!”
“Ha! Ha! Ha! Ha! Kweli huna akili nah ii ndiyo kwa heri yako,” baada ya ile sauti kumaliza maneno yale, Yule jamaa akaanza kupiga risasi ovyo ndani ya ile sebule huku akipiga na kelele za kutisha. Amata alijikunyata kimya kwenye moja ya kuta ambapo palikuwa na kabati kubwa la vitabu, risasi nyingine zilichimba kuta, nyingine zikapita karibu na kabati hilo, Amata alikuwa akiomba dua tu zisifike pale alipo. Risasi zile zilipotulia, harufu ya baruti ilitawala.
“Aaaaaaaa hauna ujanja ushakufa wewe!” ile sauti ya Yule jamaa ikaendelea kutamba huku Amata akiskia hatua nzito zikivutwa kwa upole, akaendelea kutulia kuona kama mtu huyo atafika eneo lile. Punde tu mwanga wa kurunzi ukapiga pale alipo Amata, akaendelea kujibanza kiasi kwamba Yule jamaa hakuweza kumuona. Akasimama, akachukua simu yake na kuiweka sikioni.
“Windo letu limejileta lenyewe, liko huku fikeni haraka tumalize kazi…” Yule jamaa aliongea kwa simu na mtu wa upande wa pili, kabla hajaishusha ile simu, Amata akajitokeza na bastola mkoni lakini kabla hajafyatua guu la Yule bwana likatua juu ya mkono wa Amata na kumpoka ile bastola, konde zito likatua shavuni, Amata akaenda chini.
“Aaaaahhhh utanitambua leo,” lile jamaa lilikoroma huku likimfuata Amata na mikono yake likikunja ngumi. Likamdaka shingo, likamwinua.
“Aaaaaaiiihhhhh!” Amata alijaribu kupiga kelele na kujitikisa, wapi, alijikuta pumzi ikizidi kumwishia. Akajitahidi na kuinua mikono yake akaukamata uso wa Yule jamaa, vidole gumba vya kamanda vikatua machoni pa Yule bwana, akaanza kukandamiza. Jasho lilikuwa likimtoka Amata kwa mkabo ule lakini na yeye hakumwachia alikandamiza macho kwa nguvu na alikuwa akiongeza mkandamizo mpaka Yule bwana akaona isiwe tabu akamwacha na Kamanda akabwagika chini. Wakati jamaa anajipapasa macho yake kama yapo au la, alijikuta akipokea makonde mazito mazito ya siyo na hesabu ya liyompeleka chini.
“Na sasa utanieleza vyema yuko wapi First Lady?” Amata akang’aka huku mishipa ya hasira ikimdinda kwenye paji la uso. Akamtandika teke moja lililotua shavuni na jamaa akajibwaga upande wa pili, akajaribu kujiinua na kutambaa kwa magoti huku Amata akimfuata kwa pembeni taratibu.
“Niambie First Lady yuko wapi?” Amata akazidi kuuliza. Mara ghafla, Yule jamaa akaidaka miguu ya kamanda na kumnyayua hewani, Amata aliruka sarakasi na miguu yake ikapiga kwenye paa la juu, akahisi maumivu kwenye moja ya kisigino chake, lakini alivumilia. Yule jamaa aliokota kiti cha mbao na kumtandika mgongoni Amata akapepesuka, huku kile kiti kikitawanyika vipande vipande.
Saa ya Chiba ikapiga ukulele, akaiinua na kuangalia kwenye kioo, kijitaa chekundu kilikuwa kikiwaka, haraka akaivuta kompyuta yake ndogo na kuifungua. Kamanda Amata, akawaza, punde tu ile saa ikamfinya, akaibofya kwa juu na kuruhusu ujumbe ule uingie, kijimkanda chembamba kikajitokeza.
“Rescue First Lady…TSA 1”
Chiba aliuelewa ujumbe ule, haraka akampigia Scoba na Gina wote walikuwa tayari katika kona tofauti za jiji, akawataka kuelekea Masaki haraka, nao ila kupinga waliitii amri ya TSA2 na kuelekea pande hizo.
Chiba aliingia garii na kuondoka kwa kasi kuelekea eneo la tukio. Usiku huo hakukuwa na gari yoyote barabarani hivyo ilikuwa ni kupiga mwendo kadiri ya injini yako itakavyo.
Briston Kalangila aliicha barabara ya Oysterbay na kuikamata ile inayoelekea Sea Cliff, mwendo wa gari yake ulikuwa wa kasi kiasi kwamba kila lilipokata kona tairi zilipiga kelele. Huku akiwa kauma meno moyoni mwake kulikuwa na jambo moja. Huyu jamaa anastahili akatwe vipande vipande, aliwaza huku akiendelea kuliweka guu lake zito kwenye pedeli ya mafuta na kuifanya gari hiyo kukimbia isivyo kawaida.
Akili ya kikachero ya Briston alaifanya kazi, alipofika katika yale majengo, akapitiliza kwa kasi ileile na kwenda kusimama mbele kisha akateremka na kuziweka tayari bastola zake.
Kazi moja tu, kwanza jamaa wameshaharibu mpango, iliyobaki ni kutoroka nchi, akajiongelea moyoni mwake huku akipachika sawia zile bastola na kuyafuata yale majengo kwa mlango wa nyuma ambao ni wachache waliujua.
Scoba alikuwa wa kwanza kuwasili eneo lile akitokea upande wa Coco beach, mkononi akiwa na kitu kama simu alichokivaa kilikuwa kikimwonesha wapi mahala alipokuwa akitakiwa kufika, akaiinua na kuisogeza karibu na kinywa.
“Nimetua salama uwanjani!” akasema na kushusha mkono huku nusu akikimbia na nusu akitembea.
“Copy, nipo jirani,” Chiba akajibu na wote wakasikia kupitia vidubwasha vyao vidogo vilivyopachikwa sikioni.
Dakika chache jumba lile lilizingirwa na watu watatu; Chiba, Scoba na Gina aliyeingia na kuegesha gari yake nyuma ya jingo lingine kabisa. Yeye ndiye aliyemwona Briston tangu aliposhuka kwenye gari yake na kuingia kupitia mlango mdogo wa nyuma ya majengo yale. Akatikisa kichwa kwa kuwa sasa alihakiki juu uhusika wa mtu huyo, anafata nini huku? Akajiuliza na kuinua mkono wake wenye saa akaizungusha pete ile ya pembeni mwa saa yake kisha akabonyeza kitufe cha pembeni na kuisogeza kinywani.
“Briston Kalangila ameingia kwa mlango wa nyuma!” akapeleka ujumbe wa maneno ulioweza kuwafikia wote kwa wakati mmoja. Aliposhusha mkono wake na kuichomoa bastola tayari kwa lolote akauendea ule mlango aliyoingilia Briston, akasimama pindi tu alipoufikia, akatulia tuli! Akisikiliza nini kinaendelea ndani, kimya. Alipouweka mkono wake juu ya komeo ili kuufungua akasikia muungurumo wa gari nyingine, ilikuwa Land Cruiser ikasimama jirani kabisa na ile gari ya Kalangila, akashuka kijana mmoja mfupi aliyekomaa na kushupaa misuli. Gina akamkumbuka mtu huyo, alimwona kule New Afrika alipokuwa na Scoba, hakuwa mwingine, ni Kubrah Khaleb. Naye akauelekea ule mlango, Gina akajibanza nyumba ya pipa kubwa la takataka, akamtazama Yule kijana akiingia katika ule mlango kisha akaufunga nyuma yake. Gina akatuma taarifa nyingine kwa mtindo uleule na wote wakapata ujumbe huo. Kisha akachukua simu yake na kuingiza namba za siri akampa taarifa Madam S ya kuwa wapi wapo kwa wakati huo, alipoizima na kuipachika mahala pake, akauendea ule mlango na na kuusukuma taratibu nao ukasukumika, akajitoma ndani na kujificha nyuma ya simtank kubwa la maji.
“He! He! He! We unafanya nini hapa! Na imeingilia wapi, le utachezea Masai,” sauti ya kimasai ilisikika nyuma ya Gina, hakutoa nafasi ya kusikiliza sentensi ya pili wala inayofuati, aligeuka na pigo moja la maana liliotua shingoni mwa Yule Masai na kumpelaka chini, kimya. Utaamka baadae! Akajisemea moyoni kisha akavuta hatua nyingine chache na kujificha kwenye kibaraza kilichokuwa na mlango wa kuingilia ndani. Kutoka ndani alisikia vipigo vya kimya kimya na miguno vikiendelea.
Kutoka pale chini Amata alinyakua mguu wa kiti na kuurusha kwenda kwa Yule jamaa, akaudaka na kuuvunja kwa goei lake kisha akavitupa vile vipande huku na kule, akavua shati lake na kulitupa kando hukun akiuma meno kwa hasira. Aliiruka meza na kwa minajiri ya kutua pale alipo Amata, kosa! Amata akajizungusha na nyayo la guu lake likatua kwenye korodani, Yule jamaa alitoa yowe la uchungu, Amata akainuka na kuruka tik tak na miguu yake yote miwili ikapiga usoni na kumwinua wima kisha akajibwaga juu ya meza. Kwa haraka Yule jamaa akainuka na kukutana na Amata uso kwa uso, kwa mikono yake miwili akampiga Amata huku na huku kwenye masikio kisha konde moja zito likatua kwenye chembe, Amata akarudi nyuma na kugumia maumivu. Yule bwege akachomoa kisu kikali kutoka kwenye travota yake na kumjia Amata kwa kasi.
“Aaaaaaaaggggghhhhhh! Im killliiinngggg yyyooooouuu!” pigo moja kisu kile lililikosa sikio la Amata, akaepa, pigo la pili likachana fulana aliyovaa kwa ubavuni na kuipapasa ngozi ya eneo hilo, damu zikaanza kuvuja. Pigo la tatu likatua kwenye nyama ya mkono kati ya kiganja na kiwiko. Akaitunisha misuli ya mkono, kile kisu kikatua na kuchoma sentimeta kama mbili ndani ya nyama ya mkono huo, Yule jamaa akakichomoa na kukiinua juu. Akakishusha kwa lengo la kupiga pembeni mwa shingo. Alipokishusha kwa nguvu, Amata aksogea kando na kupeleka pigo moja kali la karate likatua mbavuni na kuvunja ubavu mmoja.
Mapigo ya kifo, akawaza akilini mwake huku akipeleka pigo la kung fu lililotanguliza vidole viwili vilivyoachama, pigo lila likatua tena mbavuni na vidole vile vikakamata mbavu, kwa hasira aliyokuwa nayo, Amata aligeuka mnyama, alivuta na kufyatua mbavu nyingine, akachomo mkono na kumtandika pigo kali la paji la uso, lililomzungusha Yule jamaa kisha bila kuchelewa Amata alaongeza pigo la mwisho lililotua katikati ya uti wa mgongo na kukamata vertebra, akafuta juu na kuzifyatua kisha kwa teke lake moja akamtandika mgongoni na kumwabwaga upande wa pili akiwa hana uhai, macho yamemtoka.
“Wasalimie kuzimu!” akamwambia huku akisimama wima baada ya pigo lile la nguvu. Taa za akiba zikawaka ndani ya chumba kile. Mbele ya Amata kulikulikuwako watu watatu; Briston, Khubrah na mtu mwingine.
“Nilisikia habari zako kumbe unaweza ee?” Briston alimwambia Amata aliyekuwa kasimama imara tayari kwa lolote.
“Naweza sana kuliko unavyofikiria, siamini kabisa kama wewe, Bristona Kalangila, namba 301 TNS unaweza kusaliti kazi yako. Lakini sio kosa lako, wewe ni pandikizi na dawa ya pandikizi kama wewe ni kung’olewa ili maoteo yasipate nafasi,” Amata alinguruma huku akisimama kawaida.
Briston aliusukuma mwili wa Yule jamaa, akaitazama na ile mingine miwili, kisha akamwangalia Amata.
“TSA 1 !” akatamka kwa sauti ndogo.
“Niite Kamanda Amata, unstoppable! Kama ulikuwa hunijui ndio mimi,” Amata akainua kidole chake cha shahada na kumnyoshea mtu huyo mwenye tambo kubwa.
“Umetudhalilisha, umeidhalilisha idara, nakwambia leo hii utaeleza kila siri iliyo moyoni mwako…”
“Keleleeee!!!!” Briston akapiga ukulele na kufyatua risasi iliyopita milimita kadhaa kwa Amata.
“Wewe unaweza kuniambia mimi maneno kama hayo, wewe ni motto mdogo sana kwangu, na leo nitakuchinja kama kuku. Mlete huyo!” Briston akaongea kwa hasira na mara kijana mmoja akatokea akiwa kamkamata nywele mke wa Rais na kusukuma kwa nguvu sakafuni.
“Sasa atakatwa kichwa mbele ya macho yako!” Briston akamwambia Amata.
“Kamwe hilo haliwezi kutokea, huyo atakayemkata kichwa atakata roho sekunde tano kabla hajatekeleza hilo,” Amata akajibu na kusimama huku kajishika kiuno na damu bado zikimvuja polepole kwenye jeraha lake la mkono. Yule kijana aliyemsukuma First Lady sakafuni akauvuta upanga mkali mwembamba mkononi mwake na taratibu akamwendea Yule mwanamke na kuuinua juu.
“Na upanga huu ndiyo utakaokukata na wewe!” Briston akamwambia Amata.
“Mchinje basi, mbona unaniangalia mimi?” Amata akamwambia Yule kijana, na alipoona anaanza kushusha ule mkono, Amata akapiga kisigino cha kiatu chake chini, kisu kisodo chembamba kikafyatuka mbele ya kiatu hicho na kikadidimia kwenye koromeo la Yule jamaa mwenye upanga. Akauacha upanga na kujichika koo huku akianguka chini na kukoroma vibaya. Kamanda Amata aliruka kutoka pale alipo na risasi za Briston zakachimba tiles za sakafu.
Mara hiyo mlango ulifunguliwa kwa pigo moja la nguvu, Gina akabingirika ndani na miguu yake ikatua kifuani mwa Khaleb, kijana huyo akayumba lakini akasimama imara na kuikunja mikono yake kwa namna ya ajabu, pigo alililolipiga likapanguliwa na Gina kwa ustadi lakini mwanmke huyu alihisi maumivu kwenye mifupa yake kutokana na jinsi Khaleb alivyokomaa mwili. Pigo la pili lilimsukuma Gina na kujibamiza kwenye kabati.
“Freeeza!” Scoba na Chiba wakaingia kwa mara moja ndani ya chumba hicho na mtupiano wa risasi haukuwa wa kawaida. Khaleb akaona wazi kuwa hapo mambo yameishaharibika, alitazama huku na huko na kufungua mlango wa kuingia ndani zaidi lakini kabla hajapotelea, Gina alikuwa tayari wima, aliruka sarakasi moja maridadi na kutua mgongoni mwa kijana huyo, akaenda chini na kuporomoka ngazini. Khaleb akainuka kwa haraka na kurudi juu, katikati ya ngazi hizo akakutana na Gina aliyefura kwa hasira. Gina akaruka hewani na kumchapa teke maridadi lililompotezea mwelekeo kijana huyo lakini haraka alijiweka sawa na kumdhibiti Gina kwa mapigo ya kimbunga, mwanamke huyo akajikuta anashindwa kuhimili kasi hiyo huku akivuta hatua kurudi alikotoka, Khaleb alimchapa teke moja matata la kifua lililomsukuma mpaka sebuleni ambako sasa mapigano ya risasi yalikuwa yametulia.
Khaleb alipojitokeza tu akakutana uso kwa uso na Amata, pigo la kwanza lilitua mbavuni, Khaleb alipotaka kujishika kwa maumivu Amata akaruka teke kali na kumtwanga sikioni, majanga. Kijana huyo alipeleka mapigo kama kumi na tano ya karate kwa Amata lakini yote yalipanguliwa kwa ustadi, akajikuta anaishiwa.
Khaleb akatumia hila, akajikunja na kujiweka tayari kwa mapigano, akamtisha Amata kama anampelekea pigo na Amata alipoepa, mwenzake akaruka sarakasi na kujipiga kwenye kioo kikubwa cha dirisha, kikapasuka naye akatoka nje, akainuka haraka na kukimbia. Chiba na Scoba bastola mkononi wakapita palepale dirishani na kuanza kumtoa mbio huku wakirusha risasi lakini Khaleb alikuwa mwepesi zaidi yao, alikwea ukuta kwa jinsi ya ajabu na kujitupa nje.
Taa za gari za polisi zilipendezesha anga la nje ya majengo hayo, vijana walioongozwa na Inspekta Simbeye waliwasili dakika chache baada ya Madam S na Hosea Mkurugenzi wa idara ya Usalama wa Taifa (TNS) kuwasili.
Ndani ya sebule hiyo walikuta hali mbaya ya vifo na mapigano. Madam S alielewa kuwa ni dakika chache tu zilizopita mirindimo ya risasi ilisitishwa kutokana na harufu kali ya baruti. Bwana Hosea alipoingia tu alikutana macho kwa macho na Briston Kalangila, mtu wake katika idara namba 301 aliyemoa jukumu la kuongoza wana intelijensia ndani ya jengo la tukufu la Ikulu. Akatikisa kichwa na kumtazama kwa makini.
“Huyu ni nani Briston?” akamtupia swali huku mkono wake ukimwoneshea mke wa Rais ambaye alikuwa ameketi na kuuegemea ukuta.
“First Lady! Nimemkuta humu ndani,” akajibu huku akisimama.
“Amekujaje?” swali la pili.
“Ametekwa, na mimi kama mdau wa usama nilikuwa katika kumwokoa kutokana na kazi na cheo change nilipaswa kufanya hivyo nikiwa undercover,” Briston akaeleza, “Na hawa vijana nahisi majambazi ndiyo waliyokuwa wakinizuia mimi kufanya kazi yangu kama mwanausalama,” akaongeza.
“Acha uongo Briston!” Madam S aling’aka, “Hivi unatufaya sisi hatuna akili siyo? Nani asiyejua uliyoyafanya? Na utaenda kueleza yote leo, tuliku suspect tangu siku za mwanzo, tutakuhiji zaidi na tutaujua ukweli,” Madam akang’aka.
“Umeniuzi, umenisaliti, mchukueni!” Hosea akamwambia Madam S. inspekta Simbeye aliingia ndani ya sebule hiyo, na mara moja wakamtia pingu Briston na kutoka nae. Polisi wengine wakachukua miili ya marehemu na kuibeba machelani kuiondoa eneo lile.
“Pole sana mama!” Madam S alimpa pole First Lady huku akimwinua kutoka pale alipoketi, “Amata, pekua nyumba hii mwanzo mwisho. Simbeye majengo haya yaw echini ya ulinzi wa polisi mpaka amri nyingine itakapotolewa, ujenzi usimamishwe kwanza ili uchunguzi uchukue nafasi yake,” akamaliza na kuvua koti lake kubwa alilovaa na kumvika First Lady kwa kuwa nje kulikuwa na manyunyu mazito ya mvua.
MWISHO
 
a
RIWAYA; PASIPOTI YA GAIDI
Hujuma na uzandiki
MTUNZI: richard MWAMBE
“Unataka kusema kaondoka hapa hapa?” mmoja akauliza huku akitupa godoro upande wa pili, hakuna mtu. Mwingine alikuwa akipekuwa makabati bila mafanikio.
“Jamaa katoroka, lakini kapitia wapi? Mbona hakuna mlango humu? Atakuwepo tu mumu humu. Dakika ishiririni ziliwachukua kupekua chumba hicho lakini hawakuona mtu wala nyau.
“Ni aibu, tumewezwa!” Yule kiongozi wao akaongea huku mikono ikiwa kichwani na wakati huo akitoka nje ya chumba kile, “Hebu zunguka nyumba muifanyie ukaguzi huko nje,” akaamuru na vijana wake wakafanya hivyo.
SEHEMU YA 14
Scoba akiwa ndani ya gari yake ametulia tuli, aliona kitu kama kivuli kikipita nyuma ya ga ri hiyo, alipogeuka akamwona mtu, mwanaume anayeishia kizani. Machale yakamcheza, akainuka na kuufungua mlango taratibu kisha akafuata njia ile ambayo yule kijana aliingia. Kona ya kwanza nay a pili akasikia mlio wa injini ya gari iliyokuwa ikiwashwa na gari ile ikaondoka zake. Scoba akajikuta anashindwa la kufanya kwa wakati ule, akarudi haraka kwenye gari yake na alipoiwasha na kuigeuza akasimamishwa na wale MP.
“Teremka chini ukiwa mikono kichwani,” akaamuriwa. Scoba akateremka na kusimama akiwa mikono kichwani. Wakampekua harakaharaka na kumwacha pembeni.
“Unafanya nini hapa usiku huu?” mmoja akauliza.
“Kuna mtu namsubiri,” akajibu.
“Haujaona mtu kapita hapa sasa hivi?”
“Nimemwona, alitokea upande huu!” akajibu.
“Kaenda wapi?”
“Kapita hapa hivi kaingia upande wa pili,” akawaelekeza na wale MP wakalekea upande ule, alipohakikisha wamepotelea kizani akawasha gri na kuondoka kwa kasi kuelekea upande ule ambao Benzilahagi amekwenda na gari, akajaribu kuifuata bila mafanikio, Kepteni Benzilahagi alikuwa ametoweka.
Ukimya ukatawala, Amata akasukuma juu mfuniko wa buti lile, kwa uwazi mdogo akatazama nje hakuona kitu zaidi ya giza. Wameondoka, akawaza na kufungua lile buti kisha akatoka na kulifunga taratibu, akanyata na kujibanza kando ya pipa moja lililojaa zege ndani yake. Hakukuonekana kitu kingine zaidi ya giza lile na miale hafifu ya taa za nje iliyokuwa ikipenya kati ya uwazi na uwazi. Ijapokuwa kulikuwa na giza lakini Amata aliweza kuona kwa taabu mlango wa bati uliokuwa umerudishiwa tu, akavuta hatua mbili tatu na kuufikia alipotaka tu kuugusa akasikia michakacho ya hatua za binadamu kutoka upande wa pili wa mlango ule ambao ulikuwa haujafunga kabisa na kuruhusu nafasi kama ya milimita tano hivi kuwa wazi, akarudi na kujificha nyuma yake, akasubiri.
“Tizo!” sauti ikaita kutoka ndani.
“Sema we!” Tizo akaitikia. Amata akatikisa kichwa baada ya kujua kuwa jina la huyo kijana ni Tizo.
“Usichelewe kaka, digala anatia timu sasa hivi ili tucheki mpango wa kesho,” ile sautin ikatoa maagizo.
“Poa poa,” akajibu huku akiufungua ule mlango, akatoka na kuurudisha tena nyuma yake kisha akavuta hatua kuelekea kwenye lango kubwa la chumba kile.
Kutoka alipojificha Kamanda Amata akapiga mruzi wa taratibu uliomfanya Tizo asimame pale alipo, kabla hajajua nini kinaendelea, alijikuta akipata pigo zito lililotua katikati ya paji lake la uso, kisha Amata akamdaka kabla hajafika chini. Tizo alikuwa hana fahamu, Amata akamburuza taratibu na kumpakia kwenye ile gari, ndani ya buti na kumfungia. Kisha moja kwa moja akauendea ule mlango na kuufuangua, kelele za ule mlango zilimfanya Amata kuganda kama kapigwa shoti ya umeme. Sekunde kadhaa mbele, akateremka ngazi zilizokuwa zikielekea chini ya jingo hilo na huko akakutana na mlango mwingine mzuri tena isitoshe ni wa kisasa. Akautazama kwa jicho lake la kikachero, kwa maana mlango huu haukuwa na kitasa. Chini yake kulikuwa na zuria zito, akalikanyaga na ule mlango ukafunguka, Amata alipitisha jicho harakaharaka na kuona ndani kile chumba kuna nini. Watu wawili walikuwa wamekati katik sebule safi, mmoja mwafrika na mwingine alikuwa na asili ya kichina si kichina, kifilipino si kilipino, alikuwepokuwepo tu. Akiwa katika kutafakari, akaona mtu wa tatu akiongezeka akiwa na vinywaji mkononi. TSA 1 akaitazama saa yake, saa zinayoyoma, karibu alfajiri itanikuta, akawaza kisha akapenyeza mkono katika mlango huo na kuupeleka upande wa kushoto kuitafuta swichi ya taa hiyo maana alijuwa kuwa kaatika sheria za mafundi umeme za kimataifa swichi ya taa huwekwa upande tofauti na ule ambao mlango hufungukia. Akaipata na kuibofya.
“Ta!” mlio huo wa swichi ukafuatiwa na giza nene.
“Aaaaa shittt! Tanesco! Hili shirika bora wabinafsishe tu, namna hii!” mmoj wa wale jama akapiga makelele. Amata kama umeme akajirusha ndani na bastola mkononi, akajibiringisha na kutua kwenye kona aliyoitaka. Risasi ya kwanza haikufanya kosa, ikavunja bega la mmoja wao, ile ya pili ikafumua kichwa cha mwingine. Taa zikawaka, Amata akageuza macho mlangoni na kuona domo la bastola likimtazama, akajikunja na kuruka back akiziacha risasi za bastola hiyo zichimbe ukuta wakati yeye keishatua upande mwingine.
“Ah! Ah! Ah! Umejiingiza kwenye domo la mamba siyo?” Yule kijana aliyeonekana kujazia mwili wake akamwambia Amata, “Nilijua hutoweza kupafahamu hapa kumbe wewe mtundu sana kama nilivyopewa taarifa, sasa leo utaishia humu humu,” akaongeza huku bastola yake bado ikiwa mkononi.
“Nini kimekuleta kama si kifo chako?” akauliza.
“Nimemfuata First Lady,” Amata akajibu akiwa bado nyuma ya meza alikojificha baada ya ile sarakasi maridadi.
“First Lady! Unajua sisi tulivyomchukua tulikuwa wangapi? Na unajua mbinu tuliyoitumia? Halafu wewe uje peke yako ukiamini kumpata. Kwa taarifa yako na alfajiri hii anaondoka anapelekwa hukooooo akale honeymoon!” Yule jamaa mawnye asili isiyo rasmi akasema. Amata kwa jicho lake la kikachero aligundua kuwa huyo jamaa aliyesimama kama mita tano hivi mbele yake alikuwa hatazami upande ule isipokuwa mwingine, akageuza jicho kwa chati na kumuona Yule aliympiga risasi ya bega akiwa anachomoa bastola yake taratibu, akasubiri mkono wake ukae sawa kiunoni na lilipotimia hilo, alijirusha na kumtandika teke la usoni, mguno wa uchungu ukasikika, kwa kasi ya ajabu Amata akaiweka sawa bastola yake na kuifumua taa, giza likarudi tena na milio ya risasi ikasikika huku na huko.
“Umeniua bro!” sauti ilisikika kutoka pale chini, Amata akajua tayari washauana wenyewe kwa wenyewe.
“Nikikutia mkononi wewe nyau utajua kilichomtoa kanga manyoya,” Yule jamaa akaunguruma kwa hasira.
“Huwezi, na sasa nataka unieleze ni wapi alipo First Lady!”
“Ha! Ha! Ha! Ha! Kweli huna akili nah ii ndiyo kwa heri yako,” baada ya ile sauti kumaliza maneno yale, Yule jamaa akaanza kupiga risasi ovyo ndani ya ile sebule huku akipiga na kelele za kutisha. Amata alijikunyata kimya kwenye moja ya kuta ambapo palikuwa na kabati kubwa la vitabu, risasi nyingine zilichimba kuta, nyingine zikapita karibu na kabati hilo, Amata alikuwa akiomba dua tu zisifike pale alipo. Risasi zile zilipotulia, harufu ya baruti ilitawala.
“Aaaaaaaa hauna ujanja ushakufa wewe!” ile sauti ya Yule jamaa ikaendelea kutamba huku Amata akiskia hatua nzito zikivutwa kwa upole, akaendelea kutulia kuona kama mtu huyo atafika eneo lile. Punde tu mwanga wa kurunzi ukapiga pale alipo Amata, akaendelea kujibanza kiasi kwamba Yule jamaa hakuweza kumuona. Akasimama, akachukua simu yake na kuiweka sikioni.
“Windo letu limejileta lenyewe, liko huku fikeni haraka tumalize kazi…” Yule jamaa aliongea kwa simu na mtu wa upande wa pili, kabla hajaishusha ile simu, Amata akajitokeza na bastola mkoni lakini kabla hajafyatua guu la Yule bwana likatua juu ya mkono wa Amata na kumpoka ile bastola, konde zito likatua shavuni, Amata akaenda chini.
“Aaaaahhhh utanitambua leo,” lile jamaa lilikoroma huku likimfuata Amata na mikono yake likikunja ngumi. Likamdaka shingo, likamwinua.
“Aaaaaaiiihhhhh!” Amata alijaribu kupiga kelele na kujitikisa, wapi, alijikuta pumzi ikizidi kumwishia. Akajitahidi na kuinua mikono yake akaukamata uso wa Yule jamaa, vidole gumba vya kamanda vikatua machoni pa Yule bwana, akaanza kukandamiza. Jasho lilikuwa likimtoka Amata kwa mkabo ule lakini na yeye hakumwachia alikandamiza macho kwa nguvu na alikuwa akiongeza mkandamizo mpaka Yule bwana akaona isiwe tabu akamwacha na Kamanda akabwagika chini. Wakati jamaa anajipapasa macho yake kama yapo au la, alijikuta akipokea makonde mazito mazito ya siyo na hesabu ya liyompeleka chini.
“Na sasa utanieleza vyema yuko wapi First Lady?” Amata akang’aka huku mishipa ya hasira ikimdinda kwenye paji la uso. Akamtandika teke moja lililotua shavuni na jamaa akajibwaga upande wa pili, akajaribu kujiinua na kutambaa kwa magoti huku Amata akimfuata kwa pembeni taratibu.
“Niambie First Lady yuko wapi?” Amata akazidi kuuliza. Mara ghafla, Yule jamaa akaidaka miguu ya kamanda na kumnyayua hewani, Amata aliruka sarakasi na miguu yake ikapiga kwenye paa la juu, akahisi maumivu kwenye moja ya kisigino chake, lakini alivumilia. Yule jamaa aliokota kiti cha mbao na kumtandika mgongoni Amata akapepesuka, huku kile kiti kikitawanyika vipande vipande.
Saa ya Chiba ikapiga ukulele, akaiinua na kuangalia kwenye kioo, kijitaa chekundu kilikuwa kikiwaka, haraka akaivuta kompyuta yake ndogo na kuifungua. Kamanda Amata, akawaza, punde tu ile saa ikamfinya, akaibofya kwa juu na kuruhusu ujumbe ule uingie, kijimkanda chembamba kikajitokeza.
“Rescue First Lady…TSA 1”
Chiba aliuelewa ujumbe ule, haraka akampigia Scoba na Gina wote walikuwa tayari katika kona tofauti za jiji, akawataka kuelekea Masaki haraka, nao ila kupinga waliitii amri ya TSA2 na kuelekea pande hizo.
Chiba aliingia garii na kuondoka kwa kasi kuelekea eneo la tukio. Usiku huo hakukuwa na gari yoyote barabarani hivyo ilikuwa ni kupiga mwendo kadiri ya injini yako itakavyo.
Briston Kalangila aliicha barabara ya Oysterbay na kuikamata ile inayoelekea Sea Cliff, mwendo wa gari yake ulikuwa wa kasi kiasi kwamba kila lilipokata kona tairi zilipiga kelele. Huku akiwa kauma meno moyoni mwake kulikuwa na jambo moja. Huyu jamaa anastahili akatwe vipande vipande, aliwaza huku akiendelea kuliweka guu lake zito kwenye pedeli ya mafuta na kuifanya gari hiyo kukimbia isivyo kawaida.
Akili ya kikachero ya Briston alaifanya kazi, alipofika katika yale majengo, akapitiliza kwa kasi ileile na kwenda kusimama mbele kisha akateremka na kuziweka tayari bastola zake.
Kazi moja tu, kwanza jamaa wameshaharibu mpango, iliyobaki ni kutoroka nchi, akajiongelea moyoni mwake huku akipachika sawia zile bastola na kuyafuata yale majengo kwa mlango wa nyuma ambao ni wachache waliujua.
Scoba alikuwa wa kwanza kuwasili eneo lile akitokea upande wa Coco beach, mkononi akiwa na kitu kama simu alichokivaa kilikuwa kikimwonesha wapi mahala alipokuwa akitakiwa kufika, akaiinua na kuisogeza karibu na kinywa.
“Nimetua salama uwanjani!” akasema na kushusha mkono huku nusu akikimbia na nusu akitembea.
“Copy, nipo jirani,” Chiba akajibu na wote wakasikia kupitia vidubwasha vyao vidogo vilivyopachikwa sikioni.
Dakika chache jumba lile lilizingirwa na watu watatu; Chiba, Scoba na Gina aliyeingia na kuegesha gari yake nyuma ya jingo lingine kabisa. Yeye ndiye aliyemwona Briston tangu aliposhuka kwenye gari yake na kuingia kupitia mlango mdogo wa nyuma ya majengo yale. Akatikisa kichwa kwa kuwa sasa alihakiki juu uhusika wa mtu huyo, anafata nini huku? Akajiuliza na kuinua mkono wake wenye saa akaizungusha pete ile ya pembeni mwa saa yake kisha akabonyeza kitufe cha pembeni na kuisogeza kinywani.
“Briston Kalangila ameingia kwa mlango wa nyuma!” akapeleka ujumbe wa maneno ulioweza kuwafikia wote kwa wakati mmoja. Aliposhusha mkono wake na kuichomoa bastola tayari kwa lolote akauendea ule mlango aliyoingilia Briston, akasimama pindi tu alipoufikia, akatulia tuli! Akisikiliza nini kinaendelea ndani, kimya. Alipouweka mkono wake juu ya komeo ili kuufungua akasikia muungurumo wa gari nyingine, ilikuwa Land Cruiser ikasimama jirani kabisa na ile gari ya Kalangila, akashuka kijana mmoja mfupi aliyekomaa na kushupaa misuli. Gina akamkumbuka mtu huyo, alimwona kule New Afrika alipokuwa na Scoba, hakuwa mwingine, ni Kubrah Khaleb. Naye akauelekea ule mlango, Gina akajibanza nyumba ya pipa kubwa la takataka, akamtazama Yule kijana akiingia katika ule mlango kisha akaufunga nyuma yake. Gina akatuma taarifa nyingine kwa mtindo uleule na wote wakapata ujumbe huo. Kisha akachukua simu yake na kuingiza namba za siri akampa taarifa Madam S ya kuwa wapi wapo kwa wakati huo, alipoizima na kuipachika mahala pake, akauendea ule mlango na na kuusukuma taratibu nao ukasukumika, akajitoma ndani na kujificha nyuma ya simtank kubwa la maji.
“He! He! He! We unafanya nini hapa! Na imeingilia wapi, le utachezea Masai,” sauti ya kimasai ilisikika nyuma ya Gina, hakutoa nafasi ya kusikiliza sentensi ya pili wala inayofuati, aligeuka na pigo moja la maana liliotua shingoni mwa Yule Masai na kumpelaka chini, kimya. Utaamka baadae! Akajisemea moyoni kisha akavuta hatua nyingine chache na kujificha kwenye kibaraza kilichokuwa na mlango wa kuingilia ndani. Kutoka ndani alisikia vipigo vya kimya kimya na miguno vikiendelea.
Kutoka pale chini Amata alinyakua mguu wa kiti na kuurusha kwenda kwa Yule jamaa, akaudaka na kuuvunja kwa goei lake kisha akavitupa vile vipande huku na kule, akavua shati lake na kulitupa kando hukun akiuma meno kwa hasira. Aliiruka meza na kwa minajiri ya kutua pale alipo Amata, kosa! Amata akajizungusha na nyayo la guu lake likatua kwenye korodani, Yule jamaa alitoa yowe la uchungu, Amata akainuka na kuruka tik tak na miguu yake yote miwili ikapiga usoni na kumwinua wima kisha akajibwaga juu ya meza. Kwa haraka Yule jamaa akainuka na kukutana na Amata uso kwa uso, kwa mikono yake miwili akampiga Amata huku na huku kwenye masikio kisha konde moja zito likatua kwenye chembe, Amata akarudi nyuma na kugumia maumivu. Yule bwege akachomoa kisu kikali kutoka kwenye travota yake na kumjia Amata kwa kasi.
“Aaaaaaaaggggghhhhhh! Im killliiinngggg yyyooooouuu!” pigo moja kisu kile lililikosa sikio la Amata, akaepa, pigo la pili likachana fulana aliyovaa kwa ubavuni na kuipapasa ngozi ya eneo hilo, damu zikaanza kuvuja. Pigo la tatu likatua kwenye nyama ya mkono kati ya kiganja na kiwiko. Akaitunisha misuli ya mkono, kile kisu kikatua na kuchoma sentimeta kama mbili ndani ya nyama ya mkono huo, Yule jamaa akakichomoa na kukiinua juu. Akakishusha kwa lengo la kupiga pembeni mwa shingo. Alipokishusha kwa nguvu, Amata aksogea kando na kupeleka pigo moja kali la karate likatua mbavuni na kuvunja ubavu mmoja.
Mapigo ya kifo, akawaza akilini mwake huku akipeleka pigo la kung fu lililotanguliza vidole viwili vilivyoachama, pigo lila likatua tena mbavuni na vidole vile vikakamata mbavu, kwa hasira aliyokuwa nayo, Amata aligeuka mnyama, alivuta na kufyatua mbavu nyingine, akachomo mkono na kumtandika pigo kali la paji la uso, lililomzungusha Yule jamaa kisha bila kuchelewa Amata alaongeza pigo la mwisho lililotua katikati ya uti wa mgongo na kukamata vertebra, akafuta juu na kuzifyatua kisha kwa teke lake moja akamtandika mgongoni na kumwabwaga upande wa pili akiwa hana uhai, macho yamemtoka.
“Wasalimie kuzimu!” akamwambia huku akisimama wima baada ya pigo lile la nguvu. Taa za akiba zikawaka ndani ya chumba kile. Mbele ya Amata kulikulikuwako watu watatu; Briston, Khubrah na mtu mwingine.
“Nilisikia habari zako kumbe unaweza ee?” Briston alimwambia Amata aliyekuwa kasimama imara tayari kwa lolote.
“Naweza sana kuliko unavyofikiria, siamini kabisa kama wewe, Bristona Kalangila, namba 301 TNS unaweza kusaliti kazi yako. Lakini sio kosa lako, wewe ni pandikizi na dawa ya pandikizi kama wewe ni kung’olewa ili maoteo yasipate nafasi,” Amata alinguruma huku akisimama kawaida.
Briston aliusukuma mwili wa Yule jamaa, akaitazama na ile mingine miwili, kisha akamwangalia Amata.
“TSA 1 !” akatamka kwa sauti ndogo.
“Niite Kamanda Amata, unstoppable! Kama ulikuwa hunijui ndio mimi,” Amata akainua kidole chake cha shahada na kumnyoshea mtu huyo mwenye tambo kubwa.
“Umetudhalilisha, umeidhalilisha idara, nakwambia leo hii utaeleza kila siri iliyo moyoni mwako…”
“Keleleeee!!!!” Briston akapiga ukulele na kufyatua risasi iliyopita milimita kadhaa kwa Amata.
“Wewe unaweza kuniambia mimi maneno kama hayo, wewe ni motto mdogo sana kwangu, na leo nitakuchinja kama kuku. Mlete huyo!” Briston akaongea kwa hasira na mara kijana mmoja akatokea akiwa kamkamata nywele mke wa Rais na kusukuma kwa nguvu sakafuni.
“Sasa atakatwa kichwa mbele ya macho yako!” Briston akamwambia Amata.
“Kamwe hilo haliwezi kutokea, huyo atakayemkata kichwa atakata roho sekunde tano kabla hajatekeleza hilo,” Amata akajibu na kusimama huku kajishika kiuno na damu bado zikimvuja polepole kwenye jeraha lake la mkono. Yule kijana aliyemsukuma First Lady sakafuni akauvuta upanga mkali mwembamba mkononi mwake na taratibu akamwendea Yule mwanamke na kuuinua juu.
“Na upanga huu ndiyo utakaokukata na wewe!” Briston akamwambia Amata.
“Mchinje basi, mbona unaniangalia mimi?” Amata akamwambia Yule kijana, na alipoona anaanza kushusha ule mkono, Amata akapiga kisigino cha kiatu chake chini, kisu kisodo chembamba kikafyatuka mbele ya kiatu hicho na kikadidimia kwenye koromeo la Yule jamaa mwenye upanga. Akauacha upanga na kujichika koo huku akianguka chini na kukoroma vibaya. Kamanda Amata aliruka kutoka pale alipo na risasi za Briston zakachimba tiles za sakafu.
Mara hiyo mlango ulifunguliwa kwa pigo moja la nguvu, Gina akabingirika ndani na miguu yake ikatua kifuani mwa Khaleb, kijana huyo akayumba lakini akasimama imara na kuikunja mikono yake kwa namna ya ajabu, pigo alililolipiga likapanguliwa na Gina kwa ustadi lakini mwanmke huyu alihisi maumivu kwenye mifupa yake kutokana na jinsi Khaleb alivyokomaa mwili. Pigo la pili lilimsukuma Gina na kujibamiza kwenye kabati.
“Freeeza!” Scoba na Chiba wakaingia kwa mara moja ndani ya chumba hicho na mtupiano wa risasi haukuwa wa kawaida. Khaleb akaona wazi kuwa hapo mambo yameishaharibika, alitazama huku na huko na kufungua mlango wa kuingia ndani zaidi lakini kabla hajapotelea, Gina alikuwa tayari wima, aliruka sarakasi moja maridadi na kutua mgongoni mwa kijana huyo, akaenda chini na kuporomoka ngazini. Khaleb akainuka kwa haraka na kurudi juu, katikati ya ngazi hizo akakutana na Gina aliyefura kwa hasira. Gina akaruka hewani na kumchapa teke maridadi lililompotezea mwelekeo kijana huyo lakini haraka alijiweka sawa na kumdhibiti Gina kwa mapigo ya kimbunga, mwanamke huyo akajikuta anashindwa kuhimili kasi hiyo huku akivuta hatua kurudi alikotoka, Khaleb alimchapa teke moja matata la kifua lililomsukuma mpaka sebuleni ambako sasa mapigano ya risasi yalikuwa yametulia.
Khaleb alipojitokeza tu akakutana uso kwa uso na Amata, pigo la kwanza lilitua mbavuni, Khaleb alipotaka kujishika kwa maumivu Amata akaruka teke kali na kumtwanga sikioni, majanga. Kijana huyo alipeleka mapigo kama kumi na tano ya karate kwa Amata lakini yote yalipanguliwa kwa ustadi, akajikuta anaishiwa.
Khaleb akatumia hila, akajikunja na kujiweka tayari kwa mapigano, akamtisha Amata kama anampelekea pigo na Amata alipoepa, mwenzake akaruka sarakasi na kujipiga kwenye kioo kikubwa cha dirisha, kikapasuka naye akatoka nje, akainuka haraka na kukimbia. Chiba na Scoba bastola mkononi wakapita palepale dirishani na kuanza kumtoa mbio huku wakirusha risasi lakini Khaleb alikuwa mwepesi zaidi yao, alikwea ukuta kwa jinsi ya ajabu na kujitupa nje.
Taa za gari za polisi zilipendezesha anga la nje ya majengo hayo, vijana walioongozwa na Inspekta Simbeye waliwasili dakika chache baada ya Madam S na Hosea Mkurugenzi wa idara ya Usalama wa Taifa (TNS) kuwasili.
Ndani ya sebule hiyo walikuta hali mbaya ya vifo na mapigano. Madam S alielewa kuwa ni dakika chache tu zilizopita mirindimo ya risasi ilisitishwa kutokana na harufu kali ya baruti. Bwana Hosea alipoingia tu alikutana macho kwa macho na Briston Kalangila, mtu wake katika idara namba 301 aliyemoa jukumu la kuongoza wana intelijensia ndani ya jengo la tukufu la Ikulu. Akatikisa kichwa na kumtazama kwa makini.
“Huyu ni nani Briston?” akamtupia swali huku mkono wake ukimwoneshea mke wa Rais ambaye alikuwa ameketi na kuuegemea ukuta.
“First Lady! Nimemkuta humu ndani,” akajibu huku akisimama.
“Amekujaje?” swali la pili.
“Ametekwa, na mimi kama mdau wa usama nilikuwa katika kumwokoa kutokana na kazi na cheo change nilipaswa kufanya hivyo nikiwa undercover,” Briston akaeleza, “Na hawa vijana nahisi majambazi ndiyo waliyokuwa wakinizuia mimi kufanya kazi yangu kama mwanausalama,” akaongeza.
“Acha uongo Briston!” Madam S aling’aka, “Hivi unatufaya sisi hatuna akili siyo? Nani asiyejua uliyoyafanya? Na utaenda kueleza yote leo, tuliku suspect tangu siku za mwanzo, tutakuhiji zaidi na tutaujua ukweli,” Madam akang’aka.
“Umeniuzi, umenisaliti, mchukueni!” Hosea akamwambia Madam S. inspekta Simbeye aliingia ndani ya sebule hiyo, na mara moja wakamtia pingu Briston na kutoka nae. Polisi wengine wakachukua miili ya marehemu na kuibeba machelani kuiondoa eneo lile.
“Pole sana mama!” Madam S alimpa pole First Lady huku akimwinua kutoka pale alipoketi, “Amata, pekua nyumba hii mwanzo mwisho. Simbeye majengo haya yaw echini ya ulinzi wa polisi mpaka amri nyingine itakapotolewa, ujenzi usimamishwe kwanza ili uchunguzi uchukue nafasi yake,” akamaliza na kuvua koti lake kubwa alilovaa na kumvika First Lady kwa kuwa nje kulikuwa na manyunyu mazito ya mvua.
MWISHO
[/Qasante mkuu umetisha
 
Kazi kwenu wakuu tukutane kwenye kigongo kingine.
 
Kwa mahitaji ya Riwaya nyingine kali kutoka kwa Richard Mwambe kama vile
TUFAA JEKUNDU
CRONOC 7
KITISHO
HARUFU YA KIFO
MPATANISHI n.k
Walisiana nae kwa namba
+255 766 974 865
 
RIWAYA; PASIPOTI YA GAIDI
Hujuma na uzandiki
MTUNZI: richard MWAMBE
“Unataka kusema kaondoka hapa hapa?” mmoja akauliza huku akitupa godoro upande wa pili, hakuna mtu. Mwingine alikuwa akipekuwa makabati bila mafanikio.
“Jamaa katoroka, lakini kapitia wapi? Mbona hakuna mlango humu? Atakuwepo tu mumu humu. Dakika ishiririni ziliwachukua kupekua chumba hicho lakini hawakuona mtu wala nyau.
“Ni aibu, tumewezwa!” Yule kiongozi wao akaongea huku mikono ikiwa kichwani na wakati huo akitoka nje ya chumba kile, “Hebu zunguka nyumba muifanyie ukaguzi huko nje,” akaamuru na vijana wake wakafanya hivyo.
SEHEMU YA 14
Scoba akiwa ndani ya gari yake ametulia tuli, aliona kitu kama kivuli kikipita nyuma ya ga ri hiyo, alipogeuka akamwona mtu, mwanaume anayeishia kizani. Machale yakamcheza, akainuka na kuufungua mlango taratibu kisha akafuata njia ile ambayo yule kijana aliingia. Kona ya kwanza nay a pili akasikia mlio wa injini ya gari iliyokuwa ikiwashwa na gari ile ikaondoka zake. Scoba akajikuta anashindwa la kufanya kwa wakati ule, akarudi haraka kwenye gari yake na alipoiwasha na kuigeuza akasimamishwa na wale MP.
“Teremka chini ukiwa mikono kichwani,” akaamuriwa. Scoba akateremka na kusimama akiwa mikono kichwani. Wakampekua harakaharaka na kumwacha pembeni.
“Unafanya nini hapa usiku huu?” mmoja akauliza.
“Kuna mtu namsubiri,” akajibu.
“Haujaona mtu kapita hapa sasa hivi?”
“Nimemwona, alitokea upande huu!” akajibu.
“Kaenda wapi?”
“Kapita hapa hivi kaingia upande wa pili,” akawaelekeza na wale MP wakalekea upande ule, alipohakikisha wamepotelea kizani akawasha gri na kuondoka kwa kasi kuelekea upande ule ambao Benzilahagi amekwenda na gari, akajaribu kuifuata bila mafanikio, Kepteni Benzilahagi alikuwa ametoweka.
Ukimya ukatawala, Amata akasukuma juu mfuniko wa buti lile, kwa uwazi mdogo akatazama nje hakuona kitu zaidi ya giza. Wameondoka, akawaza na kufungua lile buti kisha akatoka na kulifunga taratibu, akanyata na kujibanza kando ya pipa moja lililojaa zege ndani yake. Hakukuonekana kitu kingine zaidi ya giza lile na miale hafifu ya taa za nje iliyokuwa ikipenya kati ya uwazi na uwazi. Ijapokuwa kulikuwa na giza lakini Amata aliweza kuona kwa taabu mlango wa bati uliokuwa umerudishiwa tu, akavuta hatua mbili tatu na kuufikia alipotaka tu kuugusa akasikia michakacho ya hatua za binadamu kutoka upande wa pili wa mlango ule ambao ulikuwa haujafunga kabisa na kuruhusu nafasi kama ya milimita tano hivi kuwa wazi, akarudi na kujificha nyuma yake, akasubiri.
“Tizo!” sauti ikaita kutoka ndani.
“Sema we!” Tizo akaitikia. Amata akatikisa kichwa baada ya kujua kuwa jina la huyo kijana ni Tizo.
“Usichelewe kaka, digala anatia timu sasa hivi ili tucheki mpango wa kesho,” ile sautin ikatoa maagizo.
“Poa poa,” akajibu huku akiufungua ule mlango, akatoka na kuurudisha tena nyuma yake kisha akavuta hatua kuelekea kwenye lango kubwa la chumba kile.
Kutoka alipojificha Kamanda Amata akapiga mruzi wa taratibu uliomfanya Tizo asimame pale alipo, kabla hajajua nini kinaendelea, alijikuta akipata pigo zito lililotua katikati ya paji lake la uso, kisha Amata akamdaka kabla hajafika chini. Tizo alikuwa hana fahamu, Amata akamburuza taratibu na kumpakia kwenye ile gari, ndani ya buti na kumfungia. Kisha moja kwa moja akauendea ule mlango na kuufuangua, kelele za ule mlango zilimfanya Amata kuganda kama kapigwa shoti ya umeme. Sekunde kadhaa mbele, akateremka ngazi zilizokuwa zikielekea chini ya jingo hilo na huko akakutana na mlango mwingine mzuri tena isitoshe ni wa kisasa. Akautazama kwa jicho lake la kikachero, kwa maana mlango huu haukuwa na kitasa. Chini yake kulikuwa na zuria zito, akalikanyaga na ule mlango ukafunguka, Amata alipitisha jicho harakaharaka na kuona ndani kile chumba kuna nini. Watu wawili walikuwa wamekati katik sebule safi, mmoja mwafrika na mwingine alikuwa na asili ya kichina si kichina, kifilipino si kilipino, alikuwepokuwepo tu. Akiwa katika kutafakari, akaona mtu wa tatu akiongezeka akiwa na vinywaji mkononi. TSA 1 akaitazama saa yake, saa zinayoyoma, karibu alfajiri itanikuta, akawaza kisha akapenyeza mkono katika mlango huo na kuupeleka upande wa kushoto kuitafuta swichi ya taa hiyo maana alijuwa kuwa kaatika sheria za mafundi umeme za kimataifa swichi ya taa huwekwa upande tofauti na ule ambao mlango hufungukia. Akaipata na kuibofya.
“Ta!” mlio huo wa swichi ukafuatiwa na giza nene.
“Aaaaa shittt! Tanesco! Hili shirika bora wabinafsishe tu, namna hii!” mmoj wa wale jama akapiga makelele. Amata kama umeme akajirusha ndani na bastola mkononi, akajibiringisha na kutua kwenye kona aliyoitaka. Risasi ya kwanza haikufanya kosa, ikavunja bega la mmoja wao, ile ya pili ikafumua kichwa cha mwingine. Taa zikawaka, Amata akageuza macho mlangoni na kuona domo la bastola likimtazama, akajikunja na kuruka back akiziacha risasi za bastola hiyo zichimbe ukuta wakati yeye keishatua upande mwingine.
“Ah! Ah! Ah! Umejiingiza kwenye domo la mamba siyo?” Yule kijana aliyeonekana kujazia mwili wake akamwambia Amata, “Nilijua hutoweza kupafahamu hapa kumbe wewe mtundu sana kama nilivyopewa taarifa, sasa leo utaishia humu humu,” akaongeza huku bastola yake bado ikiwa mkononi.
“Nini kimekuleta kama si kifo chako?” akauliza.
“Nimemfuata First Lady,” Amata akajibu akiwa bado nyuma ya meza alikojificha baada ya ile sarakasi maridadi.
“First Lady! Unajua sisi tulivyomchukua tulikuwa wangapi? Na unajua mbinu tuliyoitumia? Halafu wewe uje peke yako ukiamini kumpata. Kwa taarifa yako na alfajiri hii anaondoka anapelekwa hukooooo akale honeymoon!” Yule jamaa mawnye asili isiyo rasmi akasema. Amata kwa jicho lake la kikachero aligundua kuwa huyo jamaa aliyesimama kama mita tano hivi mbele yake alikuwa hatazami upande ule isipokuwa mwingine, akageuza jicho kwa chati na kumuona Yule aliympiga risasi ya bega akiwa anachomoa bastola yake taratibu, akasubiri mkono wake ukae sawa kiunoni na lilipotimia hilo, alijirusha na kumtandika teke la usoni, mguno wa uchungu ukasikika, kwa kasi ya ajabu Amata akaiweka sawa bastola yake na kuifumua taa, giza likarudi tena na milio ya risasi ikasikika huku na huko.
“Umeniua bro!” sauti ilisikika kutoka pale chini, Amata akajua tayari washauana wenyewe kwa wenyewe.
“Nikikutia mkononi wewe nyau utajua kilichomtoa kanga manyoya,” Yule jamaa akaunguruma kwa hasira.
“Huwezi, na sasa nataka unieleze ni wapi alipo First Lady!”
“Ha! Ha! Ha! Ha! Kweli huna akili nah ii ndiyo kwa heri yako,” baada ya ile sauti kumaliza maneno yale, Yule jamaa akaanza kupiga risasi ovyo ndani ya ile sebule huku akipiga na kelele za kutisha. Amata alijikunyata kimya kwenye moja ya kuta ambapo palikuwa na kabati kubwa la vitabu, risasi nyingine zilichimba kuta, nyingine zikapita karibu na kabati hilo, Amata alikuwa akiomba dua tu zisifike pale alipo. Risasi zile zilipotulia, harufu ya baruti ilitawala.
“Aaaaaaaa hauna ujanja ushakufa wewe!” ile sauti ya Yule jamaa ikaendelea kutamba huku Amata akiskia hatua nzito zikivutwa kwa upole, akaendelea kutulia kuona kama mtu huyo atafika eneo lile. Punde tu mwanga wa kurunzi ukapiga pale alipo Amata, akaendelea kujibanza kiasi kwamba Yule jamaa hakuweza kumuona. Akasimama, akachukua simu yake na kuiweka sikioni.
“Windo letu limejileta lenyewe, liko huku fikeni haraka tumalize kazi…” Yule jamaa aliongea kwa simu na mtu wa upande wa pili, kabla hajaishusha ile simu, Amata akajitokeza na bastola mkoni lakini kabla hajafyatua guu la Yule bwana likatua juu ya mkono wa Amata na kumpoka ile bastola, konde zito likatua shavuni, Amata akaenda chini.
“Aaaaahhhh utanitambua leo,” lile jamaa lilikoroma huku likimfuata Amata na mikono yake likikunja ngumi. Likamdaka shingo, likamwinua.
“Aaaaaaiiihhhhh!” Amata alijaribu kupiga kelele na kujitikisa, wapi, alijikuta pumzi ikizidi kumwishia. Akajitahidi na kuinua mikono yake akaukamata uso wa Yule jamaa, vidole gumba vya kamanda vikatua machoni pa Yule bwana, akaanza kukandamiza. Jasho lilikuwa likimtoka Amata kwa mkabo ule lakini na yeye hakumwachia alikandamiza macho kwa nguvu na alikuwa akiongeza mkandamizo mpaka Yule bwana akaona isiwe tabu akamwacha na Kamanda akabwagika chini. Wakati jamaa anajipapasa macho yake kama yapo au la, alijikuta akipokea makonde mazito mazito ya siyo na hesabu ya liyompeleka chini.
“Na sasa utanieleza vyema yuko wapi First Lady?” Amata akang’aka huku mishipa ya hasira ikimdinda kwenye paji la uso. Akamtandika teke moja lililotua shavuni na jamaa akajibwaga upande wa pili, akajaribu kujiinua na kutambaa kwa magoti huku Amata akimfuata kwa pembeni taratibu.
“Niambie First Lady yuko wapi?” Amata akazidi kuuliza. Mara ghafla, Yule jamaa akaidaka miguu ya kamanda na kumnyayua hewani, Amata aliruka sarakasi na miguu yake ikapiga kwenye paa la juu, akahisi maumivu kwenye moja ya kisigino chake, lakini alivumilia. Yule jamaa aliokota kiti cha mbao na kumtandika mgongoni Amata akapepesuka, huku kile kiti kikitawanyika vipande vipande.
Saa ya Chiba ikapiga ukulele, akaiinua na kuangalia kwenye kioo, kijitaa chekundu kilikuwa kikiwaka, haraka akaivuta kompyuta yake ndogo na kuifungua. Kamanda Amata, akawaza, punde tu ile saa ikamfinya, akaibofya kwa juu na kuruhusu ujumbe ule uingie, kijimkanda chembamba kikajitokeza.
“Rescue First Lady…TSA 1”
Chiba aliuelewa ujumbe ule, haraka akampigia Scoba na Gina wote walikuwa tayari katika kona tofauti za jiji, akawataka kuelekea Masaki haraka, nao ila kupinga waliitii amri ya TSA2 na kuelekea pande hizo.
Chiba aliingia garii na kuondoka kwa kasi kuelekea eneo la tukio. Usiku huo hakukuwa na gari yoyote barabarani hivyo ilikuwa ni kupiga mwendo kadiri ya injini yako itakavyo.
Briston Kalangila aliicha barabara ya Oysterbay na kuikamata ile inayoelekea Sea Cliff, mwendo wa gari yake ulikuwa wa kasi kiasi kwamba kila lilipokata kona tairi zilipiga kelele. Huku akiwa kauma meno moyoni mwake kulikuwa na jambo moja. Huyu jamaa anastahili akatwe vipande vipande, aliwaza huku akiendelea kuliweka guu lake zito kwenye pedeli ya mafuta na kuifanya gari hiyo kukimbia isivyo kawaida.
Akili ya kikachero ya Briston alaifanya kazi, alipofika katika yale majengo, akapitiliza kwa kasi ileile na kwenda kusimama mbele kisha akateremka na kuziweka tayari bastola zake.
Kazi moja tu, kwanza jamaa wameshaharibu mpango, iliyobaki ni kutoroka nchi, akajiongelea moyoni mwake huku akipachika sawia zile bastola na kuyafuata yale majengo kwa mlango wa nyuma ambao ni wachache waliujua.
Scoba alikuwa wa kwanza kuwasili eneo lile akitokea upande wa Coco beach, mkononi akiwa na kitu kama simu alichokivaa kilikuwa kikimwonesha wapi mahala alipokuwa akitakiwa kufika, akaiinua na kuisogeza karibu na kinywa.
“Nimetua salama uwanjani!” akasema na kushusha mkono huku nusu akikimbia na nusu akitembea.
“Copy, nipo jirani,” Chiba akajibu na wote wakasikia kupitia vidubwasha vyao vidogo vilivyopachikwa sikioni.
Dakika chache jumba lile lilizingirwa na watu watatu; Chiba, Scoba na Gina aliyeingia na kuegesha gari yake nyuma ya jingo lingine kabisa. Yeye ndiye aliyemwona Briston tangu aliposhuka kwenye gari yake na kuingia kupitia mlango mdogo wa nyuma ya majengo yale. Akatikisa kichwa kwa kuwa sasa alihakiki juu uhusika wa mtu huyo, anafata nini huku? Akajiuliza na kuinua mkono wake wenye saa akaizungusha pete ile ya pembeni mwa saa yake kisha akabonyeza kitufe cha pembeni na kuisogeza kinywani.
“Briston Kalangila ameingia kwa mlango wa nyuma!” akapeleka ujumbe wa maneno ulioweza kuwafikia wote kwa wakati mmoja. Aliposhusha mkono wake na kuichomoa bastola tayari kwa lolote akauendea ule mlango aliyoingilia Briston, akasimama pindi tu alipoufikia, akatulia tuli! Akisikiliza nini kinaendelea ndani, kimya. Alipouweka mkono wake juu ya komeo ili kuufungua akasikia muungurumo wa gari nyingine, ilikuwa Land Cruiser ikasimama jirani kabisa na ile gari ya Kalangila, akashuka kijana mmoja mfupi aliyekomaa na kushupaa misuli. Gina akamkumbuka mtu huyo, alimwona kule New Afrika alipokuwa na Scoba, hakuwa mwingine, ni Kubrah Khaleb. Naye akauelekea ule mlango, Gina akajibanza nyumba ya pipa kubwa la takataka, akamtazama Yule kijana akiingia katika ule mlango kisha akaufunga nyuma yake. Gina akatuma taarifa nyingine kwa mtindo uleule na wote wakapata ujumbe huo. Kisha akachukua simu yake na kuingiza namba za siri akampa taarifa Madam S ya kuwa wapi wapo kwa wakati huo, alipoizima na kuipachika mahala pake, akauendea ule mlango na na kuusukuma taratibu nao ukasukumika, akajitoma ndani na kujificha nyuma ya simtank kubwa la maji.
“He! He! He! We unafanya nini hapa! Na imeingilia wapi, le utachezea Masai,” sauti ya kimasai ilisikika nyuma ya Gina, hakutoa nafasi ya kusikiliza sentensi ya pili wala inayofuati, aligeuka na pigo moja la maana liliotua shingoni mwa Yule Masai na kumpelaka chini, kimya. Utaamka baadae! Akajisemea moyoni kisha akavuta hatua nyingine chache na kujificha kwenye kibaraza kilichokuwa na mlango wa kuingilia ndani. Kutoka ndani alisikia vipigo vya kimya kimya na miguno vikiendelea.
Kutoka pale chini Amata alinyakua mguu wa kiti na kuurusha kwenda kwa Yule jamaa, akaudaka na kuuvunja kwa goei lake kisha akavitupa vile vipande huku na kule, akavua shati lake na kulitupa kando hukun akiuma meno kwa hasira. Aliiruka meza na kwa minajiri ya kutua pale alipo Amata, kosa! Amata akajizungusha na nyayo la guu lake likatua kwenye korodani, Yule jamaa alitoa yowe la uchungu, Amata akainuka na kuruka tik tak na miguu yake yote miwili ikapiga usoni na kumwinua wima kisha akajibwaga juu ya meza. Kwa haraka Yule jamaa akainuka na kukutana na Amata uso kwa uso, kwa mikono yake miwili akampiga Amata huku na huku kwenye masikio kisha konde moja zito likatua kwenye chembe, Amata akarudi nyuma na kugumia maumivu. Yule bwege akachomoa kisu kikali kutoka kwenye travota yake na kumjia Amata kwa kasi.
“Aaaaaaaaggggghhhhhh! Im killliiinngggg yyyooooouuu!” pigo moja kisu kile lililikosa sikio la Amata, akaepa, pigo la pili likachana fulana aliyovaa kwa ubavuni na kuipapasa ngozi ya eneo hilo, damu zikaanza kuvuja. Pigo la tatu likatua kwenye nyama ya mkono kati ya kiganja na kiwiko. Akaitunisha misuli ya mkono, kile kisu kikatua na kuchoma sentimeta kama mbili ndani ya nyama ya mkono huo, Yule jamaa akakichomoa na kukiinua juu. Akakishusha kwa lengo la kupiga pembeni mwa shingo. Alipokishusha kwa nguvu, Amata aksogea kando na kupeleka pigo moja kali la karate likatua mbavuni na kuvunja ubavu mmoja.
Mapigo ya kifo, akawaza akilini mwake huku akipeleka pigo la kung fu lililotanguliza vidole viwili vilivyoachama, pigo lila likatua tena mbavuni na vidole vile vikakamata mbavu, kwa hasira aliyokuwa nayo, Amata aligeuka mnyama, alivuta na kufyatua mbavu nyingine, akachomo mkono na kumtandika pigo kali la paji la uso, lililomzungusha Yule jamaa kisha bila kuchelewa Amata alaongeza pigo la mwisho lililotua katikati ya uti wa mgongo na kukamata vertebra, akafuta juu na kuzifyatua kisha kwa teke lake moja akamtandika mgongoni na kumwabwaga upande wa pili akiwa hana uhai, macho yamemtoka.
“Wasalimie kuzimu!” akamwambia huku akisimama wima baada ya pigo lile la nguvu. Taa za akiba zikawaka ndani ya chumba kile. Mbele ya Amata kulikulikuwako watu watatu; Briston, Khubrah na mtu mwingine.
“Nilisikia habari zako kumbe unaweza ee?” Briston alimwambia Amata aliyekuwa kasimama imara tayari kwa lolote.
“Naweza sana kuliko unavyofikiria, siamini kabisa kama wewe, Bristona Kalangila, namba 301 TNS unaweza kusaliti kazi yako. Lakini sio kosa lako, wewe ni pandikizi na dawa ya pandikizi kama wewe ni kung’olewa ili maoteo yasipate nafasi,” Amata alinguruma huku akisimama kawaida.
Briston aliusukuma mwili wa Yule jamaa, akaitazama na ile mingine miwili, kisha akamwangalia Amata.
“TSA 1 !” akatamka kwa sauti ndogo.
“Niite Kamanda Amata, unstoppable! Kama ulikuwa hunijui ndio mimi,” Amata akainua kidole chake cha shahada na kumnyoshea mtu huyo mwenye tambo kubwa.
“Umetudhalilisha, umeidhalilisha idara, nakwambia leo hii utaeleza kila siri iliyo moyoni mwako…”
“Keleleeee!!!!” Briston akapiga ukulele na kufyatua risasi iliyopita milimita kadhaa kwa Amata.
“Wewe unaweza kuniambia mimi maneno kama hayo, wewe ni motto mdogo sana kwangu, na leo nitakuchinja kama kuku. Mlete huyo!” Briston akaongea kwa hasira na mara kijana mmoja akatokea akiwa kamkamata nywele mke wa Rais na kusukuma kwa nguvu sakafuni.
“Sasa atakatwa kichwa mbele ya macho yako!” Briston akamwambia Amata.
“Kamwe hilo haliwezi kutokea, huyo atakayemkata kichwa atakata roho sekunde tano kabla hajatekeleza hilo,” Amata akajibu na kusimama huku kajishika kiuno na damu bado zikimvuja polepole kwenye jeraha lake la mkono. Yule kijana aliyemsukuma First Lady sakafuni akauvuta upanga mkali mwembamba mkononi mwake na taratibu akamwendea Yule mwanamke na kuuinua juu.
“Na upanga huu ndiyo utakaokukata na wewe!” Briston akamwambia Amata.
“Mchinje basi, mbona unaniangalia mimi?” Amata akamwambia Yule kijana, na alipoona anaanza kushusha ule mkono, Amata akapiga kisigino cha kiatu chake chini, kisu kisodo chembamba kikafyatuka mbele ya kiatu hicho na kikadidimia kwenye koromeo la Yule jamaa mwenye upanga. Akauacha upanga na kujichika koo huku akianguka chini na kukoroma vibaya. Kamanda Amata aliruka kutoka pale alipo na risasi za Briston zakachimba tiles za sakafu.
Mara hiyo mlango ulifunguliwa kwa pigo moja la nguvu, Gina akabingirika ndani na miguu yake ikatua kifuani mwa Khaleb, kijana huyo akayumba lakini akasimama imara na kuikunja mikono yake kwa namna ya ajabu, pigo alililolipiga likapanguliwa na Gina kwa ustadi lakini mwanmke huyu alihisi maumivu kwenye mifupa yake kutokana na jinsi Khaleb alivyokomaa mwili. Pigo la pili lilimsukuma Gina na kujibamiza kwenye kabati.
“Freeeza!” Scoba na Chiba wakaingia kwa mara moja ndani ya chumba hicho na mtupiano wa risasi haukuwa wa kawaida. Khaleb akaona wazi kuwa hapo mambo yameishaharibika, alitazama huku na huko na kufungua mlango wa kuingia ndani zaidi lakini kabla hajapotelea, Gina alikuwa tayari wima, aliruka sarakasi moja maridadi na kutua mgongoni mwa kijana huyo, akaenda chini na kuporomoka ngazini. Khaleb akainuka kwa haraka na kurudi juu, katikati ya ngazi hizo akakutana na Gina aliyefura kwa hasira. Gina akaruka hewani na kumchapa teke maridadi lililompotezea mwelekeo kijana huyo lakini haraka alijiweka sawa na kumdhibiti Gina kwa mapigo ya kimbunga, mwanamke huyo akajikuta anashindwa kuhimili kasi hiyo huku akivuta hatua kurudi alikotoka, Khaleb alimchapa teke moja matata la kifua lililomsukuma mpaka sebuleni ambako sasa mapigano ya risasi yalikuwa yametulia.
Khaleb alipojitokeza tu akakutana uso kwa uso na Amata, pigo la kwanza lilitua mbavuni, Khaleb alipotaka kujishika kwa maumivu Amata akaruka teke kali na kumtwanga sikioni, majanga. Kijana huyo alipeleka mapigo kama kumi na tano ya karate kwa Amata lakini yote yalipanguliwa kwa ustadi, akajikuta anaishiwa.
Khaleb akatumia hila, akajikunja na kujiweka tayari kwa mapigano, akamtisha Amata kama anampelekea pigo na Amata alipoepa, mwenzake akaruka sarakasi na kujipiga kwenye kioo kikubwa cha dirisha, kikapasuka naye akatoka nje, akainuka haraka na kukimbia. Chiba na Scoba bastola mkononi wakapita palepale dirishani na kuanza kumtoa mbio huku wakirusha risasi lakini Khaleb alikuwa mwepesi zaidi yao, alikwea ukuta kwa jinsi ya ajabu na kujitupa nje.
Taa za gari za polisi zilipendezesha anga la nje ya majengo hayo, vijana walioongozwa na Inspekta Simbeye waliwasili dakika chache baada ya Madam S na Hosea Mkurugenzi wa idara ya Usalama wa Taifa (TNS) kuwasili.
Ndani ya sebule hiyo walikuta hali mbaya ya vifo na mapigano. Madam S alielewa kuwa ni dakika chache tu zilizopita mirindimo ya risasi ilisitishwa kutokana na harufu kali ya baruti. Bwana Hosea alipoingia tu alikutana macho kwa macho na Briston Kalangila, mtu wake katika idara namba 301 aliyemoa jukumu la kuongoza wana intelijensia ndani ya jengo la tukufu la Ikulu. Akatikisa kichwa na kumtazama kwa makini.
“Huyu ni nani Briston?” akamtupia swali huku mkono wake ukimwoneshea mke wa Rais ambaye alikuwa ameketi na kuuegemea ukuta.
“First Lady! Nimemkuta humu ndani,” akajibu huku akisimama.
“Amekujaje?” swali la pili.
“Ametekwa, na mimi kama mdau wa usama nilikuwa katika kumwokoa kutokana na kazi na cheo change nilipaswa kufanya hivyo nikiwa undercover,” Briston akaeleza, “Na hawa vijana nahisi majambazi ndiyo waliyokuwa wakinizuia mimi kufanya kazi yangu kama mwanausalama,” akaongeza.
“Acha uongo Briston!” Madam S aling’aka, “Hivi unatufaya sisi hatuna akili siyo? Nani asiyejua uliyoyafanya? Na utaenda kueleza yote leo, tuliku suspect tangu siku za mwanzo, tutakuhiji zaidi na tutaujua ukweli,” Madam akang’aka.
“Umeniuzi, umenisaliti, mchukueni!” Hosea akamwambia Madam S. inspekta Simbeye aliingia ndani ya sebule hiyo, na mara moja wakamtia pingu Briston na kutoka nae. Polisi wengine wakachukua miili ya marehemu na kuibeba machelani kuiondoa eneo lile.
“Pole sana mama!” Madam S alimpa pole First Lady huku akimwinua kutoka pale alipoketi, “Amata, pekua nyumba hii mwanzo mwisho. Simbeye majengo haya yaw echini ya ulinzi wa polisi mpaka amri nyingine itakapotolewa, ujenzi usimamishwe kwanza ili uchunguzi uchukue nafasi yake,” akamaliza na kuvua koti lake kubwa alilovaa na kumvika First Lady kwa kuwa nje kulikuwa na manyunyu mazito ya mvua.
MWISHO

Safi sana.. Bonge la story...

Chapter Closed...



Cc: mahondaw
 
Mimi ni mgeni, lakini nimefurahia riwaya sana😄😍..ni simulizi tamu
 
Back
Top Bottom