Riwaya: Senyenge

SEHEMU YA SITA
Reacher alikuwa amesimama eneo la wanaosafiri kuondoka hapo uwanja wa ndege. Kulikuwa na watu wakizungumza lugha tofautitofauti. Wengine kihispania. Wengine kichina nakadhalika. Reacher hakuwajali sana, macho yake yalikuwa kwenye runinga inayoonesha ratiba za safari. New York ndiyo ilikuwa ya kwanza kwenye orodha kama alivyohisi tangu awali. Alielekea kwenye dawati la tiketi akaulizia bei ya tiketi ya New york. Alipojibiwa akatikisa kichwa na kuondoka.

Alienda bafuni na kusimama mbele ya kioo. Akaingiza mkono mfukoni na kutoa pesa alizokuwa amezifungafunga na kuhesabu idadi ya pesa alizokuwa ameambiwa kwenye dawati la mapokezi. Aliporudisha zile zilizobaki mfukoni alirudi hadi kwenye lile dawati la kuuzia tiketi na kumkabidhi pesa zote dada aliyekuwepo.

"Jina lako, mheshimiwa?" Yule dada aliuliza.

"Truman," Reacher alijibu. "Kama jina la Rais."

Yule msichana alipigwa butwaa. Inaonesha hakuwa anamfahamu Nickson Truman. Reacher hakujali na wala hakuanza kumuelezea. Yule dada akaanza kuliandika jina na tiketi ikatoka kwenye mashine. Aliichukua na kuiweka kwenye jarada mojawapo lililokuwa hapo mezani.

"Acha nimalizie," Yule dada alisema.

Reacher alitikisa kichwa kukubali. Hata hivyo alijua tatizo la kununua tiketi ya ndege kwa pesa taslimu, haswa kwenye mji wa Miami, unaweza ukafanya watu wakuhisi wewe ni msafirishaji wa madawa ya kulevya. Ilikuwa ni kanuni tu. Walionunua kwa kadi zao za benki waliaminiwa zaidi. Na ndiyo maana alienda bafuni kuhesabu hela zake huko ili kuepusha kuzua mashaka. Maana yule dada angeziona tu angebofya kitufe kidogo cha siri chini ya dawati lake kuwashtua askari. Halafu angepoteza muda kwa kuigiza anabofyabofya kompyuta yake hadi polisi watakapotokea. Askari wangefika na kukuta mtu mwenye mwili mkubwa wa kutisha akiwa na hela nyingi kiasi kile lazima wangemhisi ni jambazi. Wangeanza kumchukua maelezo ambayo yangeleta tu usumbufu na kumchelewesha kwenda alipotaka kwenda. Hivyo alihakikisha anashughulikia hilo suala vyema. Alihakikisha anavaa muonekano wa mtu asiyejua chochote kuhusu teknolojia na ndiyo maana yule dada wa dawati la tiketi hakuhisi kitu kingine.

"Geti namba sita B, mheshimiwa." Yule mhudumu alimwambia Reacher. "Nimekupa siti ya dirishani na ni matumaini yangu safari yako itakuwa nzuri."

"Nashukuru." Reacher alimwambia huku akianza kuondoka. Alitembea hadi lilipokuwa geti namba sita B. Dakika kumi na tano baadae alikuwa angani kuitafuta Atlanta kisha New York.

Chester Stone aliyatoa macho yake kwenye dari ilipohitimu saa kumi na mbili kamili alfajiri. Alitoka kitandani na kuzima saa yake ya alamu kabla haijalia ili asimshtue Marilyn. Alielekea jikoni na kupasha kahawa ambayo aliinywa harakaharaka. Alipomaliza alielekea bafuni kwenye chumba cha wageni kwaajili ya kuoga. Hakutaka kumwamsha Marilyn ambaye alikuwa bado amelala. Alitaka kile anachokipitia iwe ni siri yake tu na si vinginevyo. Ilivyo ni kwamba yeye aliamini Marilyn hafamu lolote. Na alifarijika kuona hali iko hivyo. Aliamini pia mambo yangeenda mrama zaidi kama Marilyn angegundua nini kilikuwa kinaendelea.

Alitumia muda mwingi bafuni kuwaza kuliko kuoga. Alikuwa akiwaza atavaa nini na atazungumza vipi mbele ya huyu mtu anayeenda kuonana naye. Au ampigie magoti? Maana huyo jamaa ndiye alikuwa kimbilio lake la mwisho. Ndiye mtu ambaye alishika hatma ya maisha yake. Kwahivyo aende vipi? Kupiga magoti isingekuwa jambo zuri. Hivyo sivyo mchezo wa biashara ulivyotaka - Ukionesha unahitaji sana mkopo, haupewi. Utapewa pale ambapo utaonesha haujali kama watakupa au watakunyima. Ndiyo biashara ilivyotaka.

Aliamua shati jeupe na tai isiyo na rangirangi. Lakini avae suti ipi? Akivaa mishono ya Italia zitamwonesha yeye ni mtu anayejisikia sana. Hivyo hizo hapana. Armani je? Hapana. Armani ingeonesha ana uwezo mzuri wa fedha, lakini hana matumizi mazuri ya fedha. Aliamua atavaa Brooks Brothers.

Aliitoa kwenye kabati lake na kuipimisha kwa juu ya mwili. Ilikuwa nzuri, lakini kuna kitu ilikosa. Aliamua kuirudisha. Akajaribu Savile kutoka London. Hiyo ilimkaa vyema. Ilimpa mwonekano alioutaka - Ulikuwa mwonekano wa mtu mwenye busara na anayeweza kuaminika. Alipoivaa na tai akajiangalia kwenye kioo tena. Alikuwa amependeza na muonekano alioutaka ulikuwa mbele yake. Akaridhika na kutoka nje kimyakimya bila kumwamsha Marilyn na kuelekea alipoegesha magari yake. Hapo akachagua gari lake alilolipenda ainza ya Benz. Akakanyaga mafuta tayari kwenda kuonana na mwokozi wake. Muda ulikuwa ni saa kumi na mbili na dakika arobaini na tano alfajiri.

SEHEMU YA SABA
 
Mzee baba inaonesha umesoma sana tamaduni za hao watu, si kidogo
 
Riwaya nzuri tayari nimeshajifunza vitu muhimu hadi sasa
 
SEHEMU YA SABA
Ndege aliyokuwa amepanda Reacher ilitumia dakika arobaini na tano kupumzika Atlanta, halafu ikaendelea na safari kuitafuta New York. Reacher alikuwa anakunywa kahawa. Mhudumu wa ndege alikuwa amependekeza ampe maji, lakini Reacher aliomba kahawa. Alikuwa anaitumia kuuamsha ubongo wake ambao ulikuwa na maswali lukuki yasiyo na majibu. Swali la kwanza lilikuwa Mrs. Jacob ni nani? Swali la pili lilikuwa ni kwanini alimtuma Costello amtafute yeye?

Walianza kuutafuta uwanja wa ndege La Guardia. Reacher alivutiwa sana na eneo hili. Majengo mengi ambayo watu huyaona tu kwenye filamu yalikuwa mbele yake yakipigwa jua la asubuhi. Ndege ilikuwa inashuka kwaajili ya maegesho.

Mkutano wake ulikuwa umepangwa kufanyika saa tatu asubuhi na hii ilimkera. Sio kwasababu ya muda, hapana. Kilichomchukiza ni kwamba alitakiwa kuonana na mtu. Ulikuwa umepita muda mrefu bila yeye kuomba kuonana na mtu. Na katika kumbukumbu zake hakumbuki kama aliwahi kuomba kuonana na mtu yeyote. Labda babu yake ndiye aliwahi kuomba kuonana na watu, lakini tangia hapo Chester Stone wote walikuwa wakiombwa kuonwa na watu na ilikuwa ni jukumu la katibu muhtasi kushughulika na kazi ngumu ya kuwasubirisha watu kwa masaa au siku kadhaa bila kuonana na Chester yeyote. Lakini leo meza zilikuwa zimegeuka juu chini. Hii ilikuwa zamu yake kusubirishwa na ilimkera kuliko kitu chochote.

Alikuwa amewahi kwasababu ya shauku. Alikuwa ametumia zaidi ya dakika arobaini na tano akitafakari machaguzi yake. Hakuwa na chaguzi lingine lolote. Kila njia aliyoifikiria ilimtaka apate dola milioni moja nukta moja. Na hilo pia lilimkera kuliko chochote.

Saa tatu kamili jengo la WTC ni kama New York nyingine. Eneo lenyewe lina ukubwa wa hekari kumi na tatu, lakini asubuhi tu huwa linazungukwa na idadi ya watu wasiopungua laki moja na elfu thelathini.

Aliitazama saa yake na kuingia ndani. Akapanda lifti hadi ghorofa namba themanini na nane. Alipofika huko akatoka kwenye lifti kuingia kwenye korido iliyomuongoza hadi kwenye vyumba vya ofisi aliyoelekezwa. Korido ilikuwa tupu na kimya kama jangwa. Aliutafuta mlango alioelekezwa na kubofya kidude ambacho kilitii amri na mlango ukafunguka. Aliingia kwenye chumba kilichoonekana ndiyo sehemu ya mapokezi. Mpangilio wa ile ofisi ulimuacha na mshangao. Haikuwa inaonekana kama ofisi iliyostahili kuwepo kwenye hili jengo. Kulikuwa na meza na kiti tu. Hakuna mapambo. Hakuna samani za aina yeyote. Kwenye kiti alikuwa amekaa mwanaume.

Chester alisimama kidogo halafu kama aliyeshtushwa akaanza kumsogelea yule mwanaume aliyekuwa amekaa.

"Naitwa Chester Stone," Alianza kujitambulisha. "Nina appointment na Bwana Hook Hobie saa tatu asubuhi."

Uwepo wa mwanaume pale mapokezi kilikuwa kitu cha kushangaza kwa Chester. Kichwani mwake alitegemea atakuta mwanamke. Lakini si hivyo tu, jambo lingine lilomshangaza ni kwamba alielekezwa aende moja kwa moja kwenye ofisi ya Hobie. Hakuambiwa subiria kidogo.

Ofisi alipoelekezwa ilikuwa kubwa tofauti na chumba cha mapokezi. Kuta zake zilikuwa zimepakwa rangi nyeusi isipokuwa ukuta mmoja ambao ulikuwa na dirisha lililozibwa kwa blaindi. Kulikuwa na dawati kubwa liliotazamana na Sofa tatu kubwa. Na kila mwisho wa sofa kulikuwa na meza ndogondogo. Ofisi ilikuwa na muonekano wa sebule.

Nyuma ya lile dawati kulikuwa na mwanaume mwingine amekaa. Chester alitembea kuzivuka meza na sofa hadi alipofika karibu na ile meza alipokaa yule mwanaume na kunyoosha mkono kwaajili ya salamu.

"Bila shaka wewe ndiye Bwana Hobie." Alisema na kuongeza, "Mimi naitwa Stone, Chester Stone."

Yule mwanaume nyuma ya dawati alikuwa na kovu kubwa la kuungua lililokula upande mmoja wa uso wake. Hii ilifanya nusu ya uso wake uonekana kama ngozi ya kenge au mamba. Chester alitazama pembeni kwa uoga. Alimkadiria yule mwanaume kuwa na umri kati ya miaka arobaini na tano au hamsini. Alikuwa amekaa tu huku mikono yake ikiwa kwenye mapaja. Chester alijikaza kumtazama tena huku akiwa bado kanyoosha mkono wake kwaajili ya salamu.

Huu ulikuwa wakati mgumu sana. Hakuna kitu kinakera na kuumiza kama kutoa ishara ya kusalimia halafu unayemsalimia anakupuuza tu. Hapo huwa kuna mambo mawili: Kwanza unaoneka mjinga na pili utaonekana mjinga zaidi kama ukiurudisha mkono wako. Kwahivyo Chester alibaki amenyoosha tu mkono.

Yule mwanaume akarudisha kiti nyuma kwa mkono wa kushoto na kunyanyua mkono wa kulia kumsalimia chester. Haukuwa mkono. Ilikuwa ni chuma kilichong'aa. Sio mkono wenye mfano wa chuma, hapana. Ilikuwa ni chuma tu yenye muundo wa herufi 'J.' Mwanzo Chester alitaka kukishika lakini uoga ukamvaa akaurudisha mkono wake nyuma. Yule mwanaume akatabasamu.

"Wananiita Hook Hobie." Alisema.

Chester alimeza mate kujiweka sawa. Akawaza pengine amsalimie kwa mkono wa kushoto, lakini hakupata jibu mawazo yake yakaingiliwa.

"Karibu uketi." Hobie alimwambia.

Chester alifarijika na kwenda kuketi kwenye sofa. Hobie alikuwa anamuangalia huku akishusha mkono wake kwenye meza ambayo ilitoa mlio wa kulalamika kutoka na uzito wa ile chuma.

"Unataka mkopo?" Hobie aliuliza.

Upande wa uso wake ulioungua ulikuwa kama sanamu tu iliyoganda alipoongea. Ni upande mmoja ambao ulionesha uhai usoni kwake. Chester alihisi kutapika lakini alijikaza akatikisa kichwa kukubali huku akijaribu kuchagua maneno yake kwa umakini.

"Ni kweli. Nahitaji dola milioni moja nukta moja."

"Umejaribu kwenda benki?"

Chester aliinamisha kichwa chake kwenye sakafu. "Sijataka kuwafuata," Alianza kueleza. "Tayari wananidai hela na siwezi kuruhusu wajue nina tatizo la upungufu wa hela. Bado ni mapema."

Hobie aliuburuza mkono wake wa kulia hapo mezani.
"Bullshit." Aling'aka.

Chester hakujibu. Alikuwa bado kainamisha kichwa chake.

"Wewe ulihudumu?"

"Kuhudumu?"

"Namaanisha kipindi cha vita na wa-Veitnam ulichukuliwa kwenda kwenye vita?"

Chester alimeza mate. Alikuwa ameanza kuelewa makovu na chuma ya Hobie vilitokana na nini.

"Hapana." Alijibu. "Wakati vita inaisha ndiyo nilikuwa namaliza chuo hivyo sikupata nafasi ya kwenda vitani."

Hobie alitikisa kichwa kukubali. "Mimi nilienda vitani." Alisema na kuongeza, "Na moja kati ya vitu nilivyojifunza nikiwa huko ni ukusanyaji wa taarifa. Hili ni somo zuri sana kama utalitumia kwenye biashara."

Ukimya ukatawala. Chester akatikisa kichwa kukubali halafu akabadilisha mpango wa maelezo yake. Kitu pekee ambacho kingemuokoa ni ukweli tu.

"OK," Alisema. "Lakini najua ninachokifanya."

"Kusema kweli upo kwenye wakati mgumu sana," Hobie alimwambia. "Benki yako inakudai pesa nyingi na haiwezi kumudu kukuongeza pesa nyingine na biashara yako inahitaji pesa. Lakini umefanya maamuzi mazuri kuja kuonana na mimi."

"Kweli." Chester alijibu. "Nahitaji milioni moja nukta moja tu."

"Naelewa." Hobie alisema. "Na kesi kama zako ndiyo shughuli zangu. Mimi naziokoa kampuni ambazo benki inazipuuza wakati ambao kampuni zinazihitaji benki."

Hobie alitulia kuona kama Chester anamuelewa halafu akaendelea, "Na ndiyo niko tofauti sana na wakopeshaji wengine. Riba zangu ni ndogo na ni sawa na sijakukopesha kwa riba kabisa. Asilimia sita ya mkopo kila baada ya wiki sita."


Chester alianza kupiga hesabu. Asilimia sita kwa wiki sita? Ni sawa na dola ngapi kwa mwaka? Karibu asilimia 52 ya mkopo wenyewe. Leo atakopeshwa dola milioni moja nukta moja halafu kila baada ya wiki sita atatakiwa kulipa dola elfu sitini na sita ambayo ni sawa na dola elfu kumi na moja kila wiki. Sio mbaya, aliwaza.

"Na utataka nini kama dhamana." Chester aliuliza baada ya kutafakari.

"Utanipa sehemu ya hisa zako."

Chester akamtazama kwa jicho la mshangao. Pengine huu ulikuwa ni mtego.

"Hisa hazina thamani kwa sasa." Chester alisema ukweli.

Hobie alitikisa kichwa chake kukubali. "Nafahamu hilo," Alisema. "Lakini najua zitakuwa na thamani siku sio nyingi kutoka leo."

"Hio itakuwa ni baada ya kukulipa. Kabla sijakulipa sidhani kama zitapanda bei." Chester alieleza.

"Ndiyo maana nasema nitafaidikia." Hobie alimwambia. "Dhamana ninayotaka uweke sio ya muda mfupi bali hisa zako utakazonipa zitakuwa zangu."

"Kama unanunua?" Chester aliuliza sauti yake ikiwa imejawa mshangao. Yaani alipe riba ya asilimia hamsini na mbili na atoe baadhi ya hisa zake?

"Ndivyo huwa ninafanya." Hobie alisema. "Najua ni suala gumu, lakini huwa napenda kumiliki sehemu ndogo ya biashara ninazozisaidia."

Chester alimeza mate. Akatazama tena sakafuni kutafakari machaguzi aliyonayo. Hakukuwa na uchaguzi mwingine, ila kukubali. "OK," Alisema. "Ni sawa."

Hobie alitumia mkono wake wa kushoto kufungua droo na kutoa makaratasi na kuyaweka mezani.

"Niliandaa hii fomu na unaweza ukaipitia." Alisema.

Chester aliichukua kuitazama. Ulikuwa ni mkataba wa mkopo. Dola milioni moja nukta moja kwa riba ya asilimia sita kila baada ya wiki sita na kuhamisha umiliki wa baadhi ya hisa.

"Natamani sana kukusaidia, lakini hiyo ndiyo njia pekee iliyopo." Hobie alisema. "Kama nilivyokuambia hauwezi ukapata sehemu wakakupa mkopo wako huo haraka na kwa masharti rahisi kama ya kwangu."

Chester alitikisa kichwa kukubali. Halafu akaingiza mkono mfukoni kutoa kalamu na kuanza kuweka sahihi. Hobie alikuwa akimtazama huku akitikisa kichwa.

"Nadhani utataka hii pesa nikuwekee kwenye akaunti ambayo benki yako haitagundua?" Hobie aliuliza.

Chester alitikisa kichwa kukubali. "Itapendeza sana ikiwa hivyo."

Hobie aliandika kitu kwenye kikaratasi kwa mkono wake wa kushoto halafu akasema, "Suala lako litashughulikuwa baada ya lisaa limoja."

"Nitashukuru sana." Chester alisema.

"Lakini nimejiweka kwenye wakati mgumu hauoni?" Hobie alisema. "Nakupa dola milioni moja nukta moja bila dhamana yenye hiyo thamani."

"Usijali," Chester alisema. "Hakuna jambo lolote litakalotokea nikashindwa kukulipa."

"Ninakuamini." Hobie alisema halafu akanyanyua simu yake na kubofya vitufe kadhaa kabla ya kuongea maneno kwenye maiki ya simu.

"Naomba kabrasha la Stone tafadhali."

Alipoweka simu chini ukimya ulitawala hadi mlango ulipofunguka na yule mwanaume aliyekuwepo mapokezi kuingia akiwa na faili jekundu mkononi. Alifika na kuliweka mezani kwa Hobie.

"Angalia kilichomo," Hobie alimwambiwa Chester ambaye alinyanyuka na kulichukua faili.

Alilifungua akiwa amesimama. Ndani kulikuwa na picha tofautitofauti. Ya kwanza ilikuwa ni picha ya nyumba yake. Ilionekana imepigwa na mtu akiwa ndani ya gari. Picha ya pili ilikuwa ni picha ya mke wake. Marilyn. Ya tatu ilikuwa ni ya mke wake pia akiwa anatoka kwenye mahemezi. Picha ya nne ilikuwa ni picha ya gari aina ya BMW ya mke wake huku namba za kwenye sahani ya namba zikionekana vyema.

Picha ya tano ilikuwa ni picha ya Marilyn pia. Ilikuwa imepigwa usiku kupitia dirisha la bafuni wakati akiwa kajifunga taulo. Chester alishangaa - ili mtu aipate hiyo picha jinsi ilivyo ilikuwa ni lazima aingine hadi nyuma kabisa ya nyumba kilipo chumba chake. Lakini hakuhoji. Alikuwa amekwisha weka sahihi kwenye mkataba aliopewa. Masikio yalimuuma kwa ukimya uliokuwemo mule ndani. Taratibu akalirudisha lile faili na kuliweka mezani bila kusema kitu.

Hobie alikuwa anamtazama tu.

"Hiyo ndiyo dhamana yako kwangu, bwana Stone na ninaamini hakutakuwa na shida yeyote."

Chester Stone hakujibu chochote. Alikuwa bado amesimama tu kwa sekunde kadhaa. Nguvu zilipomuijia kwa kasi alianza kutoka nje. Akaipita ile ofisi ya mapokezi, akatokea kwenye ile korido aliyoipita wakati wa kuingia. Ilikuwa bado ipo tupu na kimya. Akapanda lifti kushuka ghorofa themanini na nane chini hadi nje ambako jua la asubuhi kwenda mchana lilimpokea kama ngumi ya kushtukiza.

SEHEMU YA NANE
 
SEHEMU YA NANE
Jua hilohilo lilikuwa mgongoni kwa Reacher aliyekuwa akielekea yalipo maegesho ya taxi baada ya kushuka kwenye ndege. Alipanda Taxi moja na kumwelekeza dereva ampeleke Roosevelt Square, Manhattan. Walipofika Reacher alitulia kama anayetafakari jambo. Alikuwa anawaza ni wapi atapata hoteli ya gharama nafuu, lakini iwe na huduma ya kupiga simu. Na iwe na kitabu cha namba ya simu. Jibu moja lilikuwa wazi: Asingepata hoteli yenye sifa zote hizo tatu. Hata hivyo alishuka na kimlipa dereva wa Taxi. Alikuwa ameamua atatembea kwa safari iliyobaki.

Wanaume wengine wawili waliokuwa wamevalia suti zao vizuri walisubiri hadi Chester Stone alipoondoka ndipo wakaingia ofisi ya ndani na kusimama mbele ya meza. Hobie aliinua kichwa kuwatazama. Bila kusema jambo alifungua droo yake na kuweka lile faili jekundu pamoja na mkataba. Halafu akatoa kikaratasi kingine cha njano.

"Nawasikiliza." Alisema.

"Tumefika muda huu." Mwanaume wa kwanza aliongea.

"Mmepata taarifa niliyowatuma?" Hobie aliuliza.

Mwanaume wa pili alitikisa kichwa kukubali halafu akaketi kwenye sofa na kuongea, "Costello alikuwa anamtafuta mtu anaitwa Jack Reacher."

Hobie aliandika lile jina kwenye kile kikaratasi cha njano.

"Huyo Jack Reacher ni nani?"

"Hatufahamu." Yule mwanaume aliyekuwa amesimama alijibu.

Hobie alitikisa kichwa, "Na huyo Costello alikuwa ametumwa na nani kwenda huko?"

Ukapita ukimya kidogo.

"Hatufahamu pia." Yule mwanaume aliyekuwa amesimama alijibu tena.

"Hayo ni maswali ambayo yapo wazi kabisa," Hobie alisema. "Inamaana hamkumuuliza Costello hata moja wapo."

Yule mwanaume aliyekuwa amekaa akajibu, "Tulimuuliza, mkuu."

"Lakini?"

"Hakutujibu."

"Hakuwajibu?"

"Alifariki kwa mshtuko," Yule mwanaume aliyekuwa amekaa alijibu na kuongeza. "Tusamehe sana, boss."

Hobie alitikisa kichwa chake taratibu. "Kuna uwezekano pengine mwili wake ukagundulika alikuwa nani?"

"Hapana," Yule jamaa aliyekuwa amesimama alijibu. "Tumehakikisha huo uwezekano unakuwa ni mdogo."

"Na kisu kipo wapi?"

"Tumekitupa baharini." Yule mwanaume aliyekuwa amekaa alijibu.

Hobie alitembeza mkono wake kuipapasa chuma yake. Alikuwa anafikiria kabla hajasema jambo.

"Basi sawa." Aliwaambia. "Sio kosa lenu, ni kosa la moyo wake mbovu. Lakini mmefikiria cha kufanya?"

Yule mwanaume aliyekuwa amesimama alipungukiwa wasiwasi akaenda kukaa kwenye sofa. Alikuwa ameponea chupuchupu!

"Tunatakiwa kumpata aliyemtuma Costello huko."Hobie alisema.

Wale wanaume wawili walitikisa vichwa vyao kukubali.

"Costello lazima alikuwa na katibu mhtasi, sio?" Hobie alijiuliza kwa sauti. "Basi huyo ndiye atatupeleka kwa tunayemtafuta. Hakikisha mnamleta huyu katibu muhtasi."

Hawakujibu kitu na walibaki wamekaa kwenye sofa.

"Hamkunisikia?" Hobie aliuliza.

"Tatizo ni huyu Jack Reacher," Yule mwanaume wa kwanza kuketi alisema. "Tuliambiwa jamaa ana mwili mkubwa na anafanya kazi baa - Costello pia alisema hivyohivyo. Tulivyoenda baa tulimkuta lakini alisema hilo sio jina lake."

"Kwahivyo?"

"Tulipofika uwanja wa ndege kulikuwa na ndege ya moja kwa moja kuja New York na ndege inayopitia Delta, Atlanta hadi New York."

"Na?"

"Tulimuona Jack Reacher akiwa anakata tiketi kwenye dirisha la ndege ya pili."

"Una uhakika?"

"Kwa zaidi ya asilimia tisini na tisa, mkuu. Ni kweli tulikwa mbalimbali, lakini nina uhakika yule alikuwa ni yeye."

Hobie alianza kugusagusa chuma yake akiwa kwenye dimbwi la mawazo.

"OK, Anaitwa Reacher." Alisema. "Baada ya kutafutwa anaamua kukimbilia New York, sio?

Yule mwanaume wa kwanza kuketi alijibu, "Ndiyo. Ila ni kama hajashukia Delta au Atlanta na basi lazima atakuwa yupo New York."

"Kwanini?" Hobie aliuliza na kuongeza, "Mmekwishafahamu yeye ana shughuli gani?"

Hakuna aliyejibu. Alitafakari kwa muda na kujijibu swali lake mwenyewe.

"Katibu muhtasi wa Costello atatuambia mteja wao alikuwa ni nani, sio?"

Halafu akatabasamu tena.

"Huyo mteja atatuambia Reacher ni nani na Reacher atatuambia anashughulika na nini."

Wale wanaume wawili walitikisa vichwa vyao kwa pamoja kukubaliana na Hobie. Halafu wakanyanyuka kutona nje ya ile ofisi.

Reacher alikuwa anatembea kusini mwa barabara ya mitaa ya Manhattan. Alikuwa anajaribu kuwaza ugumu na ukubwa wa shughuli iliyokuwa mbele yake. Mambo mawili yalikuwa wazi. Kwanza alikuwa yupo sehemu sahihi na kwa muda sahihi. Lakini New York ni jiji kubwa lenye idadi ya watu wengi. Watu zaidi ya milioni saba na nusu kwa mjini. Ukijumlisha na kijijini unaongelea watu zaidi ya milioni kumi na nane. Hisia zake zilimuwambia pia Costello alikuwa mtu wa Manhattan lakini mteja wake hakuwa mtu wa Manhattan. Kama wewe ni mwanamke na unataka mpelelezi wa kujitegemea sehemu pekee ya kumpata ni kwenye kitabu cha namba za makampuni na watoa huduma mbalimbali.

Aliamua hatoanzia kwenye hoteli. Hakuwa na muda wa kupoteza. Hivyo alihitaji apate kitabu cha namba za simu. Lakini pia hakuwa tayari kulipa gharama kubwa wanazotoza wenye mahoteli kwaajili ya kupiga simu. Kazi ya kuchimba mabwawa haikuwa imemfanya tajiri.

Kwahivyo alianza kutafuta maktaba kuu ya mji. Ambayo duniani ni maktaba ya kwanza kwa ukubwa. Labda ndiyo au labda hapana, hakuwa na uhakika. Lakini aliamini itakuwa kubwa kiasi cha kutosha kumpatia vitabu kadhaa vya namba za simu. Alitumia mwendo wa lisaa limoja hadi kufika hapo maktaba. Kilichofanya atumue muda mwingi ni pale aliposimama kununua kalamu na kidaftari kidogo.

Aliyekuwa ameingia kwenye ofisi ya Hobie muda huu alikuwa ni yule mwanaume wa mapokezi. Aliingia ndani na kuufunga mlango kwa funguo. Alitembea na kwenda kukaa kwenye sofa karibu kabisa na Hobie. Hapo alimtazama machoni.

"Nini?" Hobie aliuliza.

"Unatakiwa uondoke," Yule mwanaume wa mapokezi alisema. "Ni hatari sana wewe kuendelea kukaa hapa."

Hobie hakujibu. Alikuwa anaishikashika chuma yake kwa vidole vya mkono wa kushoto.

"Huo ndiyo ulikuwa mpango wetu," Yule mwanaume alisema tena. "Na uliniahidi sasa nashangaa imekuwaje?"

Hobie aliinua mabega juu na kuguna bila kusema kitu.

"Makubaliano ilikuwa kama tukipata dokezo kutoka Hawaai utaondoka."

"Costello hakufika Hawaai," Hobie alijitetea. "Ushahidi tunao."

"Na hicho ndicho kinafanya nikuambie mambo hayako sawa. Kama Costello hakufika inamaana kuna mtu mwingine anafuatilia pia."

"Umesahau mipango yetu," Hobie alijitetea tena. "Hebu fikiria kwanini upande wa pili hawajasema kitu chochote? Kama taarifa itatoka huko pia ndiyo tutaingia hatua inayofuata."

"Lakini uliniahidi..." Yule mwanaume wa mapokezi alisema tena.

"Bado ni mapema," Hobie alijitetea tena. "Hebu fikiria. Ni kama umemuona mtu amenunua bunduki na boksi la risasi halafu akakuweka chini ya ulinzi, utaogopa?"

"Ndiyo nitaogopa."

"Mimi siataogopa," Hobie alianza kueleza. "Sitaogopa kwasababu huyo mtu hajaweka risasi kwenye hiyo bunduki yake. Alinunua bunduki na boksi la risasi, lakini hakuweka risasi. Kwahivyo hadi tusikie kutoka upande wa pili ndipo tukae kwenye mpango. Vinginevyo dokezo la Hawaai ni kama bunduki isiyokuwa na risasi."

Yule mwanaume aliegemea sofa na kuinua kichwa kutazama dari.

"Kwanini unafanya huu ujinga?" Aliuliza.

Hobie alifungua kabati lake na kutoa kabrasha la Chester. Akautoa ule mkata uliosaniwa na kumuonesha yule mwanaume., "Nahitaji wiki sita tu."

Yule mwanaume wa mapokezi akaguna, "Wiki sita za nini?"

"Hii ndiyo nafasi yangu ya dhahabu," Hobie alianza kueleza. "Chester amenipa kampuni yake burebure. Kazi ya vizazi vyake vitatu naipata kiulaini sana."

"Mimi naona kama umepoteza dola milioni moja nukta moja kwaajili ya makaratasi tu."

Hobie alitabasamu. Nusu ya uso wake mmoja ilikuwa imenunua kama sanamu.

"Acha nikuambie ninachofikiria," Hobie alianza kuongea. "Chester anamiliki kiwanda kikubwa cha uzalishaji na jumba kubwa tu la kifahari. Kiwanda chake kina eneo kubwa sana na takribani nyumba mia tano."

"Hizo nyumba sio zake." Yule mwanaume aliingilia.

"Ni za kwake lakini zipo kwenye dhamana."

"Kwahiyo?"

"Hebu fikiria nini kitatokea kama nikiingiza hisa anazonipa sokoni."

"Hautopata kitu kwa sababu hazina thamani kwa sasa hivi."

"Ni kweli. Na ndiyo maana akaja kwangu. Hataki benki zilizomkopesha zijue hilo. Sasa waza benki zikijua hicho kitu?"

"Watahaha." Yule mwanaume alijibu.

"Safi," Hobie alisema na kuendelea, "Watahaha. Halafu watakurupuka kunifuata mimi ambaye tayari nitakuwa nazimiliki kwahivyo nitawalipi senti ishirini kwa kila dola wanayomdai Chester."

"Watakubali."

"Kwanini wakatae. Ni bora wapate kidogo kuliko kukosa kabisa." Hobie alisema huku akitabasamu.

"Na kuhusu hizo nyumba... Utazifanyia nini?"

"Kwakuwa nitakuwa mmiliki kamili nitakifunga kiwanda kufanya marekebisho. Hapo nitakodisha magari ya kuja kusawazisha eneo lote libaki wazi. Tutapata zaidi ya hekari elfu tatu. Jumlisha jumba lake?
Pengine gharama nitakazotumia zitafika dola milioni sita, lakini faida itakuwa ni lukuki. Zaidi ya dola milioni mia."

Yule mwanaume wa mapokezi alikuwa anamshangaa Hobie. "Ndiyo maana unahitaji wiki sita?"

Hobie alitikisa kichwa kukubali halafu chumba kikaingiwa ukimya kidogo.

"Hauwezi kufanikiwa." Yule mwanaume wa mapokezi alisema na kuongeza, "Hiyo ni biashara ya familia. Lazima kuna hisa ambazo Chester hajaziweka dhamana. Kwahivyo umiliki wako wa kampuni hautakuwa asilimia mia moja."

Hobie alitikisa kichwa kupinga, "Ataniuzia kila kitu chake. Subiria uone."

"Hawezi kufanya hivyo hata iwe vipi!"

"Ninao mpango. Niamini mimi ataniuzia kila kitu chake."

SEHEMU YA TISA
 
Kwahyo dhamana ni mke au nyuma au gari, naona mke kaonekana mara nyingi kuliko vingine, huenda ndo dhamana yenyewe
 
Kwahyo dhamana ni mke au nyuma au gari, naona mke kaonekana mara nyingi kuliko vingine, huenda ndo dhamana yenyewe
Kwa binadamu, binadamu ana thamani kuliko vitu vingine. In that sense, Chester ataguswa sana na hili suala kama mke wake akiwa matatizoni kuliko vitu tu ndiyo vikiwa matatizoni na ndiyo maana Hobie alitumia picha za mke wake ili kumuomesha anafahamu mambo mengi kumhusu. Ukusanyaji wa taarifa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…