Riwaya: SIN

SIN 159


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188





ILIPOISHIA


Akachukua begi lake na kutoa baibui lake, akachomoa bastola yake aliyo iweka chini ya siti ya gari lake ambapo sio rahisi kwa mtu kuweza kuiona. Akalivua baibui hilo na kujifunika uso wake na kitambaa cha baibui hilo. Akafunga kiwambo cha kuzuia sauti kwenye bastola yake kisha akaichomeka kiunoni. Alipo hakikisha kwamba amejikamilisha kwa kila kitu. Akashuka kwenye gari lake na kuanza kutembea kwenye mtaa huo ulio tulia na hauna hata watu wanao katika katiza. Akafika katika geti la Magreth na kulitazama kwa sekunde kadhaa kisha akarudi nyuma kwa sekunde kadhaa kisha kwa kasi ya ajabu akakimbia na kuupanda ukuta huo kwa kasi hiyo ambayo, kwa uwezo wake wa mazoezi haikuwa kazi ngumu kuuruka ukuta huo na kutua ndani ya nyuma ya Magreth.





ENDELEA


Jackline akaanza kunyata kwa umakini huku bastola yake akiwa ameishika kwa umakini mkubwa sana. Akalisogela dirisha hilo la kioo, taratibu akalisogeza, kitendo cha kufunua pasia. Magreth akastuka na kutazmaa dirishani hapo kwani alihisi kama kuna mtu ameingia katika nyumba yake ila alihisi ni ndoto. Jackline hakutaka kufanya makosa akaanza kufyatua risasi zilizo mfanya Magreth kujirusha upande wa pili wa sofa na risasi hizo kwa bahati nzuri hazikuweza kumpata. Magreth akajikagua kiononi mwake na kukuta hana bastola yake, akakumbuka kwama bastola yake hiyo ameiacha ndani ya gari lake lililopo nje hapo alipo adui. Jackline akatulia kwa sekunde kadhaa huku akisikilizia kama risasi hizo alizo zifyatua kama zita kuwa zime zaa matunda. Mapigo ya moyo ya Magreth yakazidi kumuenda kasi kwani kama mtu amemfwata hadi nyumbani kwake kwa ajili ya kumuua basi mtu huyo ana jiamini sana. Simu ya Magreth iliyopo mezani ikaanza kuita na kumstua Jackline ambaye bado amejibanza dirishani. Jackline akafyatua risasi mbili ambazo moja iliipiga simu hiyo na ikapasuka hapo hapa huku risasi nyingine ikipasua meza hiyo ya kioo na ikachanguka vipande vipande.


Magreth akashusha pumzi yake kwa sekunde kadhaa kuhakikisha kwamba ana punguza wasiwasi na kufikiria nini cha kufanya ili kupambana na adui yake huyo.


‘Nina bastola ndani’


Magreth alijisema kimoyo moyo. Akaiona rimoti ya redio ikiwa karibu naye, akaivuta kwa umakini kisha akawasha redio hiyo na kuweka mziki mkubwa jambo lililo mchanganya Jackline ambaye kitendo cha kuitazama redio hiyo, ikampa nafasi Magreth kunyanyuka kwa kasi na kukimblia ndani kwake. Akafungua droo ya dreasing table na kutoa bastola yake pamoja na magazine. Akaichomeka magazine hiyo iliyo jaa risasi. Akafungua kabati lake na kutoa nguo zake za kufanyia kazi na uzuri wa nguo hizo haziingii risasi kwa maana zime tengenezwa kwa utaalamu mkubwa unao weza kumlinda mtu anaye zivaa. Magreth akatoka sebleni kwa kujiamini, Jackline akanza kufyatua risasi mfululizo ambazo zote zilimpiga magreth kifuani mwake, jambo lililo muacha mdomo wazi Jackline ni jinsi risasi hizo zinavyo dunda na kuanguka chini. Magreth akaanza kufyatua risasi zilizo toka na milio mikubwa kwa maana bastola yake hajaifunga kiwambo cha kuzuia risasi. Jackline alipo ona mambo yama muwia ugumu akaona isiwe shida. Akaanza kukimbilia getini kwa uharaka akafungua na kuanza kukimbia kwa kasi kuelekea kwenye gari lake. Magreth akaanza kuitafuta fungua yake na kuikuta ikiwa katika sehemu alipo angukia, akaichukua na kufungua mlango wa mbele na kukimbilia nje. Akamuona mtu huyo aliye valia baibui akiwa ana ingia kwenye gari nyeusi. Magreth akarudi ndani na kuchukua funguo ya pikipiki yake, akatoka nje na kupanda pikipiki hiyo, akaigeuza kwa utaalamu wa hali ya juu na kutoka nje. Akalishuhudia gari hilo lilikunja kona ya kushoto inayo ingia mtaani kwao. Akavuta mafuta ya kutosha huku akiwa ameihimili vizuri pikipiki hiyo. Akaliona gari hilo likiwa lina endeshwa kwa mwendo wa kasi saha na yeye akazidi kuendesha gari hilo kwa mwendo wa kasi.


Kwa kupitia kioo cha pembeni, Jackline akamuona Magreth akiwa katika pikipiki na akimfukuzia kwa kasi ya ajabu sana.


“Shitii”
Jackline alizungumza huku akizidi kukanyaga mafuta ya gari lake hili aina ya BMW SERIES 7 yenye speed 260 KM/H. Uwezo wa pikipiki ya Magreth nayo haitofautiani sana na gari hilo kwani kadri jinsi Jackline anavyo ongeza mwendo kasi wa gari hilo ndivyo jinsi Magreth anavyo zidi kumsogelea. Jackline akaichukua simu yake na kuitafuta namba ya nabii Sanga. Akampigia na simu ikapokelewa.


“Vipi?”
“Aisee huyu mtu wako ni jini?”
“Nani?”
“Huyu Magreth”
“Kwa nini?”
“Nimekwenda kumvamia nyumbani kwake, ila nikimpiga risasi hafi”
“Hafi ina kuwaje hafi?”
“Sijajua na hapa ninavyo kuambia ana nifukuzia kwa pikipiki?”
“Ohoo upo wapi kwani?”
“Kigamboni?”
“Ila si una mmudu?”
“Nita mmudu vipi mtu ambaye hata risasi haiingia mwilini mwake na amevalia zile nguo ambazo ulisema kwamba una nishonea”
“Duuu kwa hiyo itakuwaje?”
“Hapa cha msingi ni kutafuta namna ya kujiokoa tu”
“Fanya hivyo Jack nina kuaminia”
“Poa”
Jackliene akakata simu na kuiweka pembeni, mshale wa speed kwenye dashboard ina elekea kwenye namba 240. Speed iliyo sababisha gari hilo kuanza kutoa mlio wa kumuashiria dereva apunguze mwendo kwani akizidi kwenda kasi zaidi basi kuna uwezekano mkubwa wa kupata ajali. Maandishi ya alama nyekundu yanayo onekana kwenye tv ndogo iliyopo ndani ya gari hilo, yana zidi kumsisitizia Jackline kupunguza mwendo. Magreth akachomo bastola yake kwenye eneo alipo ichomeka katika paja lake na kuanza kufyatua risasi kuelekea kwenye gari hilo. Wananchi walio isikia milio hiyo ya risasi na jinsi gari na pikipiki hiyo zinavyo pita kila mtu alijihami kwa kutafuta sehemu ya kuokoa maisha yake kwa maana ni wananchi wengi wana hofu kwani toka kutokee milipuko ya mabomu kila mmoja haamini usalama kabisa wa nchi yake.


***


“Mkuu njoo uone”


Mmoja wa vijana wa kitengo cha NSA, alimuambia bwana Msangi video inayo rekodiwa kutokea juu kwa kupitia sattelaite.


“Itume kwenye screan kubwa”
Bwana Msangi alizungumza huku akiyahamishia macho yake kwenye screan kubwa iliyopo ndani ya chumba hicho. Kila mmoja akashangaa kuona jinsi pikipiki inavyo ifukuzia gari hiyo.


“Ni Magreth”
Bwana Msangi alizungumza huku akitoa simu yake mfukoni na kuanza kumpigia simu Magreth, kwa bahati mbaya akakuta simu yake ikiwa haipatikani.
“Shitt hapatikani. Ana hitaji kupatiwa msaadaa. Timu D7 ondokeni na helicopter hakikisheni muna izuia hiyo gari”
Bwana Msangi alizungumza kwa kinasa sauti. Vijana watano walio valia nguo nyeusi, ambazo ndio sare kuu ya kitengo hicho cha NSA, pamoja na majaketi ya kuzuia risasi, yenye maandishi makubwa meupe mngononi na kifuani yanayo someka NSA. Wakaingia kwenye helicopter huku kila mmoja akiwa ameshika bundiki yake pamoja na kuvalia kinasa sauti. Rubani wa helicopter hiyo ya kitengo cha NSA. Akaanza kuipaisha juu taratibu na ikaanza kuelekea eneo wanapo elekea Magreth na mtu huyo ambaye hawamfahamu hadi sasa. Halikuwa jambo gumu helicopter hiyo kufika katika barabara hiyo wanayo fukuzana Magreth na Jackline.
“What’s fuc**”
Jackline alitukana mara baada ya kuoan helicopter ya kitengo cha NSA ikipita juu yake. Magreth akatabasamu kwa maana amepata msaada huo. Jackline akashusha kioo cha upande wake taratibu kidogo kisha akaanza kushambulia helicopter hiyo.


“Mkuu tumshambulie?”
Kijana mmoja alizungumza kwa kupitia kinasa sauti chake huku wakisubiria amri ya kulishambulia gari hilo kwa manaa sehemu walipo wana liona vizuri na hata dereva wana uwezo wa kumpiga risasi.
“Hapana ina bidi tumpate hai”
Bwana Msangi alizungumza na vijana hao walio jipanga vizuri ndani ya helicopter hiyo wana hakikisha wana mzuia mtu huyu pasipo madhara yoyote. Magreth akautazama mkono wa Jackline ambaye akili yake yote kwa sasa ina izingatia helicopter hiyo. Akafyatua risasi moja iliyo mpiga Jackline mkononi na kusababisha bastola yake kuanguka barabarani.
“Fuc**”
Jackline alilia kwa maumivu makali huku akiurudisha mkono wake huo wa kulia ndani ya gari. Damu zinazo mtoka kwa wingi zikamfanya ahisi kuchanganyikiwa. Amefanya kazi nyingi sana za ujasusi ila hakuwahi kupigwa sirasi hata siku moja na wala hayajui maumivu ya risasi.
“No siwezi kufa”
Jackline alilalama huku akiendelea kuongeza mwendo. Jackline macho yakaanza kumtoka mara baada ya gari lake kuanza kupungua mwendo taratibu huku alama zinazo muashiria kwamba gari hilo lime kwisha mafuta zikianza kuoenkana.


“Mother fuc*. Fuc* me”


Jackline alilalama huku akipiga piga mskani wa gari lake kwa kutumia mkono wa kulia. Taratibu gari hilo likasimama katikati ya barabara, Magreth akasimisha pikipiki yake mita chache kutoka sehemu lilipo gari la Jackline, akashuka kwenye pikipiki huku bastola yake ikiwa mkononi. Helicopter hiyo ya NSA, taratibu ikatua katikati ya barabara hiyo na askari wa kitengo cha NSA, wakashuka huku bunduki zao wakizielekezea kwenye gari hilo.


“No siwezi kufa”
Jackline alizungumza huku jasho likimwagika mwili mzima. Damu nazo hazikuacha kumwagika kwa maana risasi hiyo ime piga katika mshipa una safirishia damu na ime toboa na kutoke upande wa pili wa mkono. Simu yake ikaanza kuita, akaitazama na kukuta ni nabii Sanga. Akaichukua na kuiweka sikioni mwake.
“Vipi ume fikia wapi?”
“Nime zingirwa. NSA na yule malaya wame zingira gari langu. Bye”
Jackline mara baada ya kukata simu hiyo akaiweka pembeni na ndani ya sekunde kumi na tano simu hiyo ika jifunga kwa namba za siri ambazo ni yeye pekee tu ndio ana zifahamu na ubaya ni kwamba simu yake ni Iphone X ambazo zime tengenezwa katika ubora wa hali ya juu, zinazo muwezesha mtumiaji wa simu hiyo kuweka neno la siri ambalo hata watundu wa mambo ya I.T wajaribu kuifungua hawato weza, tofauti na simu nyingine ambazo ulinzi wake ni mdogo hata kama mtu ame ingiza neno la siri. Magreth akavunja kioo cha dereva kwa kutumia kitako cha bastola yake na kwa ishara akamuomba Jackline kushuka kwenye gari.


Jackline akawatazama askari wa kitengo cha NSA ambao wame simama mbele ya gari hilo huku banduki zoa wakimuelekezea yeye, akamtazama Magreth aliye mnyooshea bastola yake.


‘Sihitaji kufa’


Jackline alijisema kimoyo moyo huku akinyoosha mkono wa kushoto juu na kushuka kwenye gari hili akiashiria kwamba ame sarenda. Magreth akamvua kitambaa cha usoni mwake, macho yakamtoka mara baada ya kumkuta ni mtu ambaye wana mtafuta kwa udi na uvumba kuhakikisha kwamba wana mzuia katika kusitisha zaoezi la kumuua makamu wa raisi wa nchi ya Marekani.


***


Nabii Sanga akahisi kichwa kina mpasuka kwa maumivu. Akamtazama Julieth ambaye naye tumbo la woga lina mkata kisawa sawa.


“Baba tuna fanyaje sasa?”
“Yaani hata sijui na nina hisi ata kuwa amekamatwa”
“Akikutaja baba si familia nzima tuta chinjwa sisi?”
“Yaani sielewi mwanangu ita kuwaje”


Nabii Sanga alihahaa huku ajsho likimwagika mithili ya mtu aliye toka kuoga.
“Nenda ikulu”
“Wapi!!?”
Julieth aliuliza kwa mshangao mkubwa sana.


“Ikulu”
“Kufanya nini baba?”
“Nenda kahakikishe una jua wapi alipo pelekewa Jackline na tuta jua jinsi gani ya kutumia nguvu ya pesa katika kumuachia”
“Baba hivi una mjua vizuri yule mzee? Nimkali hana masihara na toka mke wake afe ame kuwa ni mtu asiye hitaji hutani hata kidogo na majambazi”
“Sasa una taka kukaa hapa ili iweje, tuje kukamatwa au?”
Nabii Sanga alizungumza kwa kufoka huku akimkazia macho Julieth aliye jikuta akikaa kimya.


“Usisahau ume kwenda ikulu kufanya kitu gani, nina hitaji uhakikishe una jua kila kinacho endelea juu ya huyo msichana”
“Sawa baba”
“Fanya hivyo sasa hivi”
Nabii Sanga alizungumza kwa kukoroma huku wasiwasi wake ukiwa ni kwenye simu zake alizo piga na kupigiwa na Jackline.


‘Siwezi kushikwa kirahisi namna hii’


Nabii Sanga alizungumza huku akijaribu kutafakari nini cha kukifanya. Akapata wazo, kwa haraka akaingia bafuni, akaoga kwa haraka na kurudi chumbani, akatafuta suti moja kali sana na kuiva. Akatoka nje na kumfwata msaidizi wake wa kanisani kwake.


“Nina omba uwatangazie waumini wetu kwamba tuna kongamano la kuiombea nchi litakalo anza leo saa kumi kanisani pale”
“Sawa nabii”
“Pia waambie watu wa dini zote wana karibishwa. Nime pewa maono sasa hivi na Mungu, ina bidi kuliombea taifa na kulitoa kwenye hali ya matatizo tunayo kabiliwa”
“Sawa sawa mtu wa Mungu”
Msaidizi wake huyo alizungumza kwa upole na unyenyekevu wa hali ya juu. Laiti kama engefahamu upande wa pili wa kiongozi wake huyo wala asinge thubutu kufungua kinywa chake na kumuita mtu wa Mungu.
“Baade tuta wasiliana”
Julieth alimuambia baba yake huku akipanda kwenye gari lake na wakaondoka nyumbani hapo na walinzi hao ikulu na kuianza safari ya kuelekea ikulu.


***


“Kazi nzuri sana Magreth”
Raisi Mtenzi alizungumza na Magreth kwa kupitia video call.


“Shukrani sana muheshimiwa”
“Nina kupa mamlaka ya kumuhoji huyo mtuhumiwa. Tumia kila aina ya uwezo na nguvu ulizo nazo kuhakikisha kwamba una muhoji na ana wataja walio muagiza”
“Sawa muheshimiwa. Tume ipata simu yake hapa nina imani kupitia hii simu tuna weza kujua ni nani ambaye alimtuma”
“Sasa chochote mutakacho kihitaji basi nipo tayari kuwapa ushirikiano wa asilimia mia moja”
“Nashukuru kwa hilo muheshimiwa”
Magreth akaka simu hiyo na raisi Mtenzi akamtazama Josephine aliye tawaliwa na tabasamu pana usoni mwake.


“Hakika Mungu aliyemo ndani yako ni Mungu wa kweli”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akiwa na furaha kubwa sana.


“Nina shukuru sana muheshimiwa. Nipo kwa ajili ya kuisaidia hii nchi, nina imani kwamba hapata kuwa na jambo lolote baya litakalo jitokea endapo nita kuwa hai”
“Mungu ni mwema ata kupa maisha marefu. Hata kipindi changu cha uongozi kitakapo kwisha basi nina imani hata huyo raisi ajaye uta shirikiana naye vizuri katia kuiongoza hii nchi iende katika mstari mzuri na unao faa”
“Amen”
“Basi nenda kaendelee na kazi na endapo kuta kuwa na jambo lolote utakalo lihitaji nina omba uni fahamishe”
“Sawa muheshimiwa”
Josephine akatoka ofisini hapo na kuaelekea ofisini kwake, kwenye kordo akakutana na Julieth anaye tembea kwa mwendo wa haraka huku akionekana ana wahi jambo fulani.


“Hei Julieth”
Josephine alizingumza huku akimsimamisha Julieth.
“Nini?”
Julieth alijibu kwa hasira kidogo huku akimpita Josephine ambaye hakuhitaji kujisumbua kuhisi chochote kwa maana alimshuhudia Jery akiingia ofisini kwa baba yake asubuhi hiyo akiwa katika hali ya hasira. Julieth akasimama kwenye mlango wa kuingia ofisini kwa raisi Mtenzi. Akavuta pumzi nyingi na akazishusha taratibu, akaingia ofisini hapo kwa mwendo wa taratibu huku usoni mwake akiwa na furaha hafifu ambayo moja kwa moja raisi Mtenzi alitambua ni kutokana na kukosana kwake na Jery.


***


Magreth akakabidhi bastola yake mapokezi na kuingia katika chumba cha mahojiano alipo wekwa Jackline ambaye tayari amesha patiwa matibabu ya mkono wake ulipo pigwa risasi. Magreth akavuta kiti na kukaa mbele ya Jackline aliye fungwa pingu mikononi na nyororo miguuni mwake. Katikati yao wame tenganishwa na meza ya chuma mbayo ime jengwa chini na haiwezi kusogea. Magretg akatazama kamera nne zilizo fungwa kwneye kila kona ya chumba hicho na zina rekodi kiloa kitu kinacho zungumzwa ndani hapo.


“Najua aliye kuagia uniue, sasa hivi ata kuwa ana pata tabu sana akiwaza ni kwa nini ume kamatwa”
Magreth alizungumza huku akiweka simu ya Jackline juu ya meza hiyo. Jackline hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kuendelea kumtazama Magreth ambaye amevua kofia ya juu ya nguo yake hiyo aliyo ivaa na kumfanya sura yake kuonekana vizuri sana.
“Mdada mzuri, mwenye kipaji chake kizuri, una hadaika na pesa kwa ajili ya kuhitaji kunia mimi na kumuua makamu wa raisi wa nchi ya Marekani. Hivi huyo aliye kutuma kwa nini usinge mueleza aifanye kazi hiyo peke yake kama kweli ana kupenda?”
Maneno ya Magreth yaka mstua sana Jackline kwa maana ana tambua kwamba dili hilo la nabii Sanga hakuna mtu mwengine anaye lifahamu zaidi yake.
“Jackline ume salitiwa na mtu aliye kupa hii kazi. Jiulieze, tulikujuaje kama upo Tanzanai, jiulize nime juaje kama una mpango wa kunia mimi na kumuua makamu wa raisi kesho kutwa. Huyo aliye kutuma ame kudanganya na hana mpango wa kukulipa hata kiasi hicho cha pesa mulicho kubaliana. Niambie ni nani huyo aliye kuagiza ili tujue jinsi ya kukusaidia kwa maana huna hatia yoyote, aliyopo nyuma yako ndio mwenye makosa”
Magreth alizungumza kwa upole sana kiasi cha kumfanya Jackline moyo wake kumuua na kuamini kwa asilimia kadhaa kwamba nabii Sanga ame muuza kwenye dili hilo.
“Nipo tayari kumtaja aliye niagiza ila kwa sharti moja”
Magreth na kila mtu anaye fwatilia mahojiano hayo katika chumba cha pili chenye tv nne akastuka kwani ime kuwa rahisi sana kwa binti huyo kuzungumza ukweli tofauti na vile walivyo kuwa wame tarajia.


****************************************************************************************************************


***


ITAENDELEA


Haya sasa, Jacklinea ameingia mikononi mwa vyombo vya ulinzi. Amesema yupo tayari kumtaja yule aliye muagiza kwa sharti moja tu. Sasa sijui ni sharti gani hilo ambalo ana kwenda kulitaja ikiwa ame hisi kwamba nabii Sanga ame msaliti kwenye kazi hiyo? Usikose sehemu ya 160.
 
Sasa chief umeambiwa ni uhalisia hii??

Sent using Jamii Forums mobile app
 
umelazimishwa kusoma?Acha ukuda basi!
 
Nafikiri ungetupia uachane na wakuda@Brodre
 
Ukisema hivo Misukule yake inawaka maana riwaya haina uhalisia kabisa
 
Ukisema hivo Misukule yake inawaka maana riwaya haina uhalisia kabisa
Tatizo watu wajinga kama ninyi kubishana nanyi LAZIMA uwe umekunywa Konyagi kama mimi Sasa hivi. Hadithi imeishasemwa ni ya kutunga na sio ya uhalisia, halafu kwa ujinga wako unakuja humu unaloloma na ushamba wako wa Kikurya kama Umughaka eti hii hadithi ya kufikirika! Ujinga mtupu! Kama ni ya kweli uliishawahi kusikia Tanzania kuna Rais anaitwa Mpanzi? KUMBAVU!!!
 
SIN 160


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188




ILIPOISHIA


“Jackline ume salitiwa na mtu aliye kupa hii kazi. Jiulieze, tulikujuaje kama upo Tanzanai, jiulize nime juaje kama una mpango wa kunia mimi na kumuua makamu wa raisi kesho kutwa. Huyo aliye kutuma ame kudanganya na hana mpango wa kukulipa hata kiasi hicho cha pesa mulicho kubaliana. Niambie ni nani huyo aliye kuagiza ili tujue jinsi ya kukusaidia kwa maana huna hatia yoyote, aliyopo nyuma yako ndio mwenye makosa”
Magreth alizungumza kwa upole sana kiasi cha kumfanya Jackline moyo wake kumuua na kuamini kwa asilimia kadhaa kwamba nabii Sanga ame muuza kwenye dili hilo.
“Nipo tayari kumtaja aliye niagiza ila kwa sharti moja”
Magreth na kila mtu anaye fwatilia mahojiano hayo katika chumba cha pili chenye tv nne akastuka kwani ime kuwa rahisi sana kwa binti huyo kuzungumza ukweli tofauti na vile walivyo kuwa wame tarajia.





ENDELEA


“Sharti gani hilo?”
Magreth aliuliza hukua akiwa amejawa na shahuku kubwa sana ya kusikia shari hilo.


“Nahitaji umuue makamu wa raisi wa nchi ya Marekani. Baada ya hapo nita zungumza kila kitu ni nani ambaye yupo nyuma ya hili tukio na ana hitaji kitu gani kwa ajili ya hii nchi. Ila hata munikate kate vipande vidogo vidogo vya mwili wangu sinto weza kutaja ni nani aliye nipa hii kazi kwa maana sheria namba moja ya kazi yangu, ni kuhakikisha una mlinda mteja wako no matter what’s happen”
Jackline alizungumza kwa kujiamini sana huku uso wake ukiwa umetawali na tabasamu kubwa sana. Magreth akashusha pumzi huku akimtazama, Jackline akaitazama simu yake iliyo shikwa na Magreth.


“Ohoo una hisi kwamba muna weza kupata kitu. No no no….hamuto weza kuifungua simu yangu na baada ya masaa ishirini na nne PUUUUUUUU……!!”
Magreth akaka kimya kwa sekunde kadhaa kisha akanyanyuka na kutoka katika chumba hicho na kuingia chumba cha pili ambapo yupo bwana mzee Mbogo na wapelelezi wengine wanao fwatilia mahojiano hayo kupitia video zinazo rekodiwa na kamera zilizo fungwa ndani hapo.


“Vipi mbona ume toka?”
“Nahitaji kufanya kitu cha tofauti”
“Kitu gani?”
Mzee Mbogo alizungumza huku akimtazama Magreth usoni mwake. Magreth akatoka ndani hapo na moja kwa moja akaelekea eneo la jiko.


“Jamani muna weza kuniazima kisu kikali sana?”
Magreth aliwaambia wapishi hapo.


“Ndio”
Mpishi mmoja alizungumza huku akimuonyesha Magreth eneo linalo hifadhiwa visu. Magreth akavitazama visu hivyo kwa sekunde kadhaa kisha akachukua kisu chenye ncha kali na kilicho na makali. Akaona mashine ya kunolea visu, akaiwasha na kukinoa kisu hicho kwa sekunde kadha kisha akatoka ndani hapo. Magreth akarudi katika chumba alicho muancha mzee Mbogo na wapelelezi wengine.


“Una taka kufanya nini?”
“Zimeni hizo kamera zisirekodi hili tukio”
“Ila kumbuka ana paswwa kuwa hai?”
“Ndio nna liatambua hilo”
Magretg alimjibu mzee Mbogo kisha akaingia ndani hapo.


“Ume sema kwamba hata tkukate vipande vidogo vidogo hoto zungumza chochote. Naomba unisikilize dada, wewe ni mzui sana ila nina kwenda kukutoa jicho moja baada ya jengine nina imani hata huyo aliye kupa pesa kwa ajili ya kuniua huto muona tena kwenye maisha yako”
Magreth alizungumza kwa msisitizo huku akimkaba Jacklien shingo yake na kukibenua kichwa chake kwa nyuma na kuanza kukishusha kisu hicho kwenye jicho la upande wa kushoto wa Jackline ambaye alianza kutetemeka mwili mzima kwa woga.
“Acha”
Sauti ya ukali ya mzee Mbogo ikamfanya Magreth kusitisha zoezi hilo ambalo amelikusudia kulifanya na laiti kama mzee Mbogo ange chelewa kuingia ndani hapo Magreth ange ling’ofoa jicho hilo la Jackline.


“Nita muhoji mimi”
“Ila raisi amenipa mamlaka ya kumuhoji na ameniambia nitumie kila liwezekanalo kuhakikicha nina pata information kutoka kwa huyu malaya”
“Nalijua hilo ila mahojiano hayaendi hivyo. Nakuomba ukapumzike”
Magreth akamtazama mzee Mbogo kwa macho yaliyo jaa hasira. Akamtazama na Jackline ambaye uso wake umejawa hofu na mashaka mengi. Mzee Mbogo akamnyooshea Magreth mkono wa kushoto akimaanisha kwamba ana iomba simu ya Jackline. Magreth akaingiza mkono mfukoni na kuitoa simu hiyo na kumkabidhi mzee Mboho na akatoka ndani hapo huku akiwa amejawa na hasira kwani lengo lake lime zuiwa na mzee huyo.


***


Ukimya wa sekunde kadhaa ukatawala ndani ya ofisi ya raisi Mtenzi huku akimtazama Julieth usoni mwake.
“Ni kweli una mahusiano na yule kijana?”
“Hapana baba, siwezi kuwa na mahusiano na mwanaume mwengine tena ndoa yangu ikiwa change kiasi hichi”


Julieh alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaaa simanzi. Raisi Mtenzi akajiweka vizuri kwenye kiti chake, kisha akavua miwani yake na kuifuta futa na kitambaa kisha akaivaa tena.


“Jery mwanangu ni mgonjwa.”
Julieth aka stuka kidogo.


“Usistuke, ila ina bidi wewe ndio uwe msaada mkubwa sana wa kumponya ugonjwa wake huo kama alivyo kuwa ana fanya marehemu mama yake. Toka alipo kuwa mdogo alikuwa ana sumbuliwa na tatizo la hasira, jambo la kumshukuru Mungu hasira yake ya leo haja weza kukudhuru. Mama yake aliongeza upendo wake na kuwa naye karibu hadi hilo tatizo lilimuosha. HIvyo kuwa karibu sana na Jery mpe kile anacho kipenda kwa wakati husika wala hato weza kuwa kama alivyo kuwa leo sawa mkwe?”
“Ndio baba nime kuelewa, ila hato nipiga kwa maana jinsi alivyo kuwa leo nilihisi ana weza kuniua?”


Julieth alizungumza kwa sauti ya kudeka kidogo na kumfanya raisi Mtenzi kutabasamu.
“Kama alishindwa kukupiga leo, basi hata siku nyingine akiwa na hasira hawezi kukudhuru. Kuwa naye karibu isitoshe ana kupenda sana. Jambo la msingi mpatie kile anacho kihitaji”
Raisi Mtenzi alizungumza kima fumbo kwa maana hawezi kumuambia mkwewe moja kwa moja kwamba ampatie penzi mtoto wake.
“Sawa baba, je kazi uta nifuta?”
“Hapana siwezi kufanya hivyo na nina imani hakuto kuwa na safari ya kwenda Marekani pale utakapo mtapa kile alicho kuaomba sawa mkwe?”
“Sawa baba”
“Nenda kaonane naye nahita atakuwa nyumbani”
“Sawa”
Julieth akatamani kumuuliza raisi Mtenzi juu ya kukamatwa na Jackline ila akaona kwamba ina weza kumleta sinto fahamu kwa maana yeye hakuwepo hapo ikulu, ina kuwaje ana fuhamu mambo yanayo endelea ndani ya ikulu. Akaingia katia chumba cha Jery na kumkuta akiwa amejilaza kitandani huku akiwa amevalia boksa tu. Taratibu Julieth akavua nguo zake zote na kubaki kama vile alivyo zaliwa. Akamsogela Jery na kuanza kumpapasa mgongoni mwake. Jery akakurupuka hukuakigeuka, akashusha pumzi mara baada ya kumkuta ni Julieth ambaye kidogo amejawa na wasiwasi.
“Hei baby”


Jery alizungumza kwa sauti ya upole ambayo kidogo ilimfanya Julieth kuondoa wasiwasi wake unao mkabili.


“Am sorry”
“For what?”
“For everything.”
Julieth alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa mahaba mengi sana.
“Usijali mke wangu”
Jery alizungumza kwa sauti ya kugugumia kwani tayari Julieth alisha anaza kumchezea jogoo wake. Julieth akazidi kwenda mbali na kuongeza maujuzi, akaanza kumnyonya taratibu na kumfanya Jery kuzidi kusisimkwa kwa furaha hiyo anayo ipata. Jery alipo jiridhisha kwa huduma hiyo, akamlaza chali Julieth kisha na yeye akaanza kumnyonya kitumbua chake na kumfanya Julieth kuanza kumkumbuka mwanaume wa kwanza kumfanya hivyo ambaye ni Evans na jambo hilo likamfanya hisia zake zote kuanza kumbukumbuka Evans ambaye kwa sasa hatambui ni wapi alipo.


***


Evans akamshika Baby Al, mkono wake huku helicopter hiyo ikishuka taratibu kwenye kiwanja cha jumba moja la kifahari lililopo katika mji wa Moscow nchini Rusia.


“Usiwe na hofu”
Baby Al alizungumza huku akimtazama Evans usoni mwake. Safari yao iliyo chukua masaa kadhaa hewani kutoka bara la Afrika hadi kufika Russia kwa ndege binafsi inayo milikiwa na baba yake Baby Al, hakika ni safari ndefe. Wakashuka kwenye helicopter hiyo ambavyo walipanda kutokea unaja wa ndege wa hapo jijini Moscow na kufikishwa katika jumba hilo. Wakaanza kutembea kuelekea kwenye mlango wa kuingilia kwenye jumba hilo la kifahari. Ulinzi ulipo eneo hilo hakika kidogo uka mtisha Evans. Macho yake hakakusita kutazama kila eneo la jumba hilo, walinzi walio valia suti nyeusi na miwani nyeusi huku wakiwa na bunduki mikononi mwao hakika ina dhihirisha kwamba eneo hilo lina ulinzi mkali sana.
“Karibu Baby”
Mzee mmoja mwenye ndevu zenye mvi huku usoni mwake akiwa amevibana kwa nyuma nywele zake hizo nyingi alikumbatiana na Baby Al huku akimbusu shavuni mwake.


“Nashukuru babu. Kutana na huyu ni mpenzi wangu ana itwa Evans. Evans huyu ni babu yangu ana itwa Rusev”
“Nashukuru kukufahamu mzee”
“Karibu sana Russia”
“Asante sana”
Wakakaribishwa sebleni hapo na wakakaa huku wakimtazama mzee huyo.


“Nime toka kuzungumza na baba yako nusu saa lililo pita”
“Ana semaje?”
“Ana hitaji siku hii ya leo uelekee nchini Ufaransa”
Baby Al akashusha pumzi huku akimtazama babu yake huyo ambaye ni baba wa mama yake.
“Sawa baba kama tulivyo zungumza kwenye simu. Huyu kijana ana hitaji kupewa msaada wa mfunzo ya kijasusi. Amesha jiandaa kisaikolojia hivyo yupo tayari kwa kila jambo”
“Una mfahamu vizuri?”
“Ndio babu”
Mzee Rusev akamtazama kwa sekunde kadhaa Evans kisha akatingisha kichwa akimaanisha ame kubaliana na hilo.
“Kesho alfajiri ata pelekwa kambini”
“Sawa babu shukrani kwa hilo. Ila nina kuomba usimueleze baba juu ya hili jambo”
“Usijali siwezi kufanya hivyo”
“Evans kuanzia sasa uta kuwa chini ya babu yangu. Hivyo nina kuomba utulivu mzuri sawa”
“Sawa”
“Babu acha niendelee na safari”
“Sawa”
Evans hakuamini kama Baby Al ana ondoka kwa uharaka wa namna hiyo. Baby Al akapanda helicopter hiyo na kurudi kiwanja cha ndege, akapanda ndege walio kuja nayo na kuelekea nyumbani kwao nchini Ufaransa.


***


“Nini?”
Josephie aliuuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa huku simu yake akiwa ameishika mkononi mwake huku wakitazamana na Magreth aliyopo kitengo cha NSA.


“Ndio nahitaji kuacha hii kazi. Najiona nita kuwa kuwa mtu mbaya zaidi ya hapa Jose. Kumbuka nina hofu ya Mungu ndani yangu. Ila katika kipindi hichi nime kuwa ni muuaji, kumwaga damu ya mtu kwangu ni jambo rahisi sana. Hivyo ni heri nika endelea na biashara yangu ya kuuza chakula kwenye mgahawa”
Magreth alizungumza kwa sauti ya upole kwenye masiliano hayo ya video. Josephine akashusha pumzi nyingi huku akimtazama rafiki yake huyo anaye onekana kukata tamaa kabisa kwa kazi hiyo.


“Mage”
“Bee”
“Nchi bado ina kutegemea na watu wengi wana kutegemea. Kumbuka kwamba nchi kwa sasa ina endeshwa kwa maono ambayo Mungu ata tupatia. Laiti kama ingekuwa sio kupata yale maono, leo hii nasi si tunge kuwa kwenye lile janga la mlipuko?”
Josephine alizungumza kwa sauti ya upole sana.
“Natambua hilo Jose, ila sipendi kuona damu zina endelea kumwagika. Nime fikia umri ambao nahitaji kuitwa mama na nina hitaji kuwa na familia yangu. Ona Juma amekufa kwa ajili yetu, alikuwa na kosa gani hadi afe”
Magreth alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Kitendo hicho nacho kikamfanya Josephine kumwagikwa na machozi.
“Jose mimi sikupata haya mafunzo kwa ajili ya kuua watu. Nilipata kwa ajili ya kujilinda mwenyewe na niwapendao. Sasa ona hata niwapendao siwezi kuwalinda, huoni hilo lina weza kuwa ni tatizo kubwa kwa familia zetu za baadae”
“Mungu ata tusaidia Mage ila acha kwanza tupate hii hadhina kisha mambo mengine yata fwata”
Magreth anaye tumia kuwasiliana kwa kupitia laptop akamtazama Josephine kwa sekunde kadhaa kisha akafuta machozi yake.


“Nime kubali ila nina kuomba tukipata hiyo hadhinabasi tuna acha hizi kazi sisi wote niahidi kwenye hilo”
“Nakuahidi tuta acha”
Josephine alizungumza huku naye akijifuta machozi.
“Sawa nakuamini Josephine”
“Nakuamini pia Mage. Baadae”
“Poa”


Josephine akashusha pumzi nyingi. Gafla kichw achake kikaanza kumuua, na akaanza kuonyeshwa maono mengine ambayo hakumaliza hata dakika tano akaanguka chini na kuzimia.


****************************************************************************************************************





ITAENDELEA


Haya sasa, Josephine ame onyeshwa maono mengine makubwa hadi amepekekea kuzimia, je ni maono gani ambayo ameonyesha? Usikose sehemu ya 161.
 
SIN 161


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188





ILIPOISHIA


“Mungu ata tusaidia Mage ila acha kwanza tupate hii hadhina kisha mambo mengine yata fwata”
Magreth anaye tumia kuwasiliana kwa kupitia laptop akamtazama Josephine kwa sekunde kadhaa kisha akafuta machozi yake.


“Nime kubali ila nina kuomba tukipata hiyo hadhinabasi tuna acha hizi kazi sisi wote niahidi kwenye hilo”
“Nakuahidi tuta acha”
Josephine alizungumza huku naye akijifuta machozi.
“Sawa nakuamini Josephine”
“Nakuamini pia Mage. Baadae”
“Poa”


Josephine akashusha pumzi nyingi. Gafla kichw achake kikaanza kumuua, na akaanza kuonyeshwa maono mengine ambayo hakumaliza hata dakika tano akaanguka chini na kuzimia.





ENDELEA


Mlio wa simu inayo itwa kwa sauti ya juu kiasi kidogo, ikaanza kupenda masikioni mwa Josephine. Taratibu akafumbua macho yake na kuangaza angaza kila eneo la ofisi yake. Hapakuwa na mtu yoyote zaidi yake. Mlio wa simu hiyo ya mezani ukamfanya kunyoosha mkono wa kulia na kuchukua mkonga wa simu hiyo na kuuweka sikioni mwake.


“Haloo”
Josephine alizungumza kwa sauti ya upole huku akijitahidi kunyanyuka na akaketi kwenye kiti chake.


“Josephine nime kupigia mara kadhaa huja pokea vipi kwema”


Sauti ya nabii Sanga ikamfanya akae vizuri kwenye kiti chake.


“Shikamoo mtumishi”
“Marahaba. Namba yako ya ofisini nime weza kupatiwa na muheshimiwa raisi, kuna jambo nilianza kumuomba hivyo nawe nikaona niweze kukuomba kama huto jali”
“Usijali mtumishi, niombe tu”
“Leo nina anzisha kongamano la kuiombea nchi. Nakujua wewe ni mtu wa Mungu hivyo ninge penda leo kwenye ufunguzi wa kongamano hilo”
“Ahaa ni saa ngapi?”
“Saa kumi kuwasili na saa kumi na moja lina anza. Pale pale kanisani kwetu”
“Sawa mtumishi nita fika”
“Hakuna shaka basi nikutakie siku njema?”
“Nashukuru nawe pia”
Josephine akakata simu, kisha akanyanyuka huku akijinyoosha viongo vyake kwani uchovu utokanano na kuzimia kwake.
***


Nabii Sanga akaishusha simu yake kutoka sikioni mwake na kumgeukia mtu aliyekaa siti ya nyuma ya gari lake.


“Huyu binti ndio kivuruge wa kila jambo. Huyu ndio anaye sababisha mipango yangu yote kwenda vibaya. Sasa nina hitaji umshuhulikie una nielewa?”
Nabii Sanga alizungumza huku akimuonyesha mtu huyo picha ya Josephine kwenye simu yake.


“Usijali mzee”
“Narudi hakikisha huyu msichana una mshuhulikia ipasavyo ila sinta hitaji tu afe hadi pale nitakapo kuambia kwamba afe”
“Hakuna shaka”
Nabii Sanga akaingiza mkono kwenye mfukowe wa suti na kutoa kibunda cha dola za kimarekani.
“Ni dola elfu tano. Hakikisha una maliza hiyo kazi leo hiii”
“Usiwe na shaka sijawahi kukosea”
“Sawa una weza kwenda”
Mwana mama huyo mrefu aliye valia suti nyeusi akashika kitasa cha mlango, kabla ya kushuka nabii Sanga akamzuia.


“Jackline ana endeleaje?”
“Hajazungumza chochote ila bado yupo chumba cha mahojiano”
“Nani anaye muhoji?”
“Kuna yule binti mpya ambye ameingia ingia kwenye kitengo cha NSA. Ndio alikuwa ana muhoji ila sasa hivi jukumu hilo ana lifanya mkuu mwenyewe mzee Mbogo”
“Mbogo ana msimamo sana. Sasa je una weza kumtorosha mule ndani?”
“Hilo jambo halipo nabii Sanga na halito wezekana”
“Nina kuongezea pesa?”
“Nisiwe muongo kuna ulinzi mkubwa sana. Jambo la pekee ambalo lina wezekana kufanyika ni kumuua ndani ya jengo lile”
Nabii Sanga akashusha pumzi huku akimtazama mwana mama huyo ambaye naye ni mfanyakazi wa kitengo cha NSA tenaa ana yupo katika ngazi za juu za upelelezi.
“Nita kupatia jibu”
“Sawa, ila kuwa makini sana Sanga. Usiitumie vibaya nafasi ya ukaribu wako na raisi, laiti akija kufahamu mzunguko wa haya uta potea”
“Nashukuru kwa ushauri wako. Hivyo nifanyie hilo tu niliko kupatia pesa”
“Sawa”
Mwana mama huyo akashuka kwenye gari la nabii Sanga na kungia kwenye gari lake na kuondoka hapo.


‘Mpango wangu hauwezi kwenda lazima nikuweke kizuizini wewe mjinga’


Nabii Sanga alizungumza huku akitazama picha ya Josephine, akawasha gari lake na kuondoka eneo hilo.


***


“Kongamano”
Mrs Sanga alishangaa mara baada ya kuona tangazo hilo kwenye ukurasa wa mume wake wa mtandao wa Instergram.


“Nini baby?”
Tumaini aliuliza huku hukia amekaa pembeni ya mrs Sanga.


“Hapana ngoja mara moja”
Mrs Sanga akaichukua simu yake na kuitafuta namba ya mume wake, akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akampigia.


“Vipi?”
“Nimeona kuna kongamano una litangaza ni la nini?”
“Kwani hujaona maelezo yake?”
Nabii Sanga alijibu kwa kurudisha swala kwa mke wake.
“Hivi una nguvu gani za kuendesha kongamano ikiwa tupo kwenye kipindi cha kuadhimisha misiba ya watoto wetu?”
“Huna jipya”
Nabii Sanga alijibu kwa dharau na kukata simu kitendo kilicho mfanya mrs Sanga kuachia msunyo mkali sana.
“Baby kuna nini?”
“Kuna mtu ana nichefua tu hapa”
“Nani?”
“Ahaa huiswe na wasiwasi. Una jisikia njaa?”
“Kiasi”
“Sawa ngoja nijiandae niende chini nika chukua chakula”
“Poa poa”
Mrs Sanga akaiweka simu yake mezani, na kuingia bafuni. Tumaini kwa haraka akaichukua simu hiyo na kutazama ni namba gani ya mwisho kupigwa na mwana mama huyo aliye jikuta akianza kumuwekea wivu kutokana na pesa ambazo ana pewa. Akainakili namba hiyo kwenye simu yake kwa uharaka kisha akairudisha simu kama ilivyo wekwa.


“Baby”
“Naam”
“Tanga ni maeneo gani yame tulia sana tuka weza kukaa bila buguza ya mtu yoyote?”
“Kwa Tanga hapa wachawi wengi na wengi wana nijua. Labda sehemu nzuri ni Lusthoto au Pangani”
“Lushoto si hakuna bahari?”
“Ndio ila kuna ukijani mzuru ambao kwa kweli una furahisha ukiutazama. Pia hali ya hewa kule ni safi sana, sio kama huku, hadi tutegemee A/C.


“Ila ni mbali sana na hapa?”
“Ndio ni mwendo wa masaa sita au saba”
“Basi huko tuta kwenda kesho. Nahitaji kutanua wiki nzima na wewe, sina haja ya kurudi Dar es Salaama kwa sasa”


“Nashukuru mpenzi wangu”
“Hivi simu yake ime sajiliwa Tigopesa?”
“Ndio”
“Ngoja nikuingizie pesa ya vocha alafu hiyo simu ikiwezekana leo uka nunue nyingine nzuri sitaki kukuona na kasimu kabaya kama hako”
Mrs Sanga alizungumza kwa kujiamini akashika simu yake na kumuingizia Tumaini kiasi cha pesa kilicho mfanya aduwae kwa sekunde kadhaa huku akiwa haamini kabisa Kiwango cha milioni mbili na nusu alicho kipokea hakika hajawahi kukiona kwenye laini yake hiyo na hata maisha yake toka kuzaliwa kwake.


“Mbona una duwaa?”
“Sija wahi shika pesa kama hii mpenzi wangu”
“Ndio yako sasa. Nenda kanunua simu mpya sasa hivi, si una weza kuendesha gari?”
“Ndio naweza”
“Leseni unayo?”
“Ndio”
“Basi kanunue simu urudi hapa. Nataka leo uni** hadi nizimie”
Maneno ya mrs Sanga yakampagawisha sana Tumaini akanyanyuka na kumkumbatia mrs Sanga kwa furaha huku akimpiga mabusu mfululizo.


“Vaa uende sasa hivi sawa”
“Sawa”
“Funguo hiyo hapo”
Mrs Sanga akamkabidhi Tumaini fungu ya gari lake, akajindaa baraka haraka na kuondoka hotelini hapo. Akafika kwenye moja ya duka ambalo siku zote kuna simu alikuwa ana itamani kuinunua ila hakuwa na pesa za kuweza kufanya.


“Hapa si nina weza kulipa kwa tigopesa?”
“Ndio”
“Nahitaji hii iphone 8 plus”
Tumaini alizungumza kwa kuchachawa. Akailipia simu hiyo milioni mbili na laki tatu kisha akarudi nayo ndani ya gari huku akiwa amejawa na furaha sana, akatamani kuputa maskani kwa washakaji wake ili kuwaringishia ila akahisi kwamba ana weza kuvuruga mipango yake. Hakutaka kuchelewa akaiingiza laini yake kwenye simu hiyo, akajisajili vizuri kisha akarudi hotelini. Akamkuta mrs Sanga akiwa amesha nunua chakula cha mchana.


“Nilihisi kwamba huto rudi”
“Kwa nini?”
“Basi tu?”
“Siwezi kukufanyia hivyo mpenzi wangu”
Tumaini alizungu huku akiipanua mihuu ya mrs Sanga, akailufunua taulo alilo jifunga na kuanza kunyonya kitumbua chake.


“Baby tule kwanza?”
Mrs Sanga alilalama huku akihisi raha ya kumuahamisha katika ulimwengu wa kwake peke yake.


“Chakula hakina faidi kwa saa”
Tumaini alizunguma huku akiongeza mautundu ambayo yamekuwa ni mara dufu na yale yote aliyo wahi kumfanyia mrs Sanga toka walipo kutana.
***


Jery aliendelea kuchachawa na mauno yanayo katwa na Julieth. Kitendo cha kuziona damu chache alipo kuwa ana anza kufanya tendo hilo, zikamfanya Jery aamini moja kwa moja kwamba ame itoa bikra ya mke wake huyo wa ndoa.


Vilio vya kimahaba zinazo tokea chumbani kwa Jery zikamfanya Shani kusogelea mlango huo huku mapigo yake yakimuenda kasi sana. Kumbatio la Jery alilo fanyiwa masaa kadhaa yaliyo pita hakika linamtesa sana Shani akilini mwake. Japo ana mwanaume wake, ila moyo wake tayari ulisha vutiwa na Jery mtoto wa raisi. Kwa bahahi nzuri Shani akakuta mlango huo ukiwa haujabanwa vizuri, kijinafasi kinacho onekana hapo mlango, kina onyesha kioo cha dreasing table ambayo ina onyesha kitanda hicho cha Jery. Shani akahisi mapigo yake ya moyo yana kwenda kupasua kifua chake, viuno vinavyo katwa na mke wa Jery hakika vikamfanya asisimkwe, akamuona Jery akimgeuza mke wake na kumuinamisha mkao wa mbuzi kagoma kwenda. Jery akamshika mke wake mikono yake yote miwili, kisha akaanza kumshulikia kwa nguvu zake zote. Shani akameza fumba zito la mate huku jasho likimtoka, taratibu akajikuta akiingiaza mkono wake kwenye suruali yake aliyo ivaa na kuanza kukipapasa kitumbua chake. Shani akaona haburudiki kwa kusimama hapo, akakimbilia katika chumba chake, akavua nguo zake na kufunga mlango kwa ndani, kisha akajitupa kitandani na kuanza kujichezea kitumbua chake huku akivuta hisia za Jery na mke wake jinsi wanavyo pesa haki ya tendo la ndoa.


Magreth akaingia ofisini kwa Josephine na kumkuta akiminya minya compture yake.


“Hei”
Magreth alimsalimia huku akikaa kwenye kiti.
“Mage karibu”
“Asante. Vipi hauendi nyumbani kupumzika”
“Tena nilikuwa nina imalizia hii kazi nikupigie ili twende wote kanisani”
“Kanisani, wapi?”
“Kwa nabii Sanga”
“Jose!! Una taka kwenda kwa yule muhuni anaye tumia muamvuli wa dini kujiaminisha kwa watu kwamba ni mwema?”
“Sawa Mage ila kumbuka tuna kwenda pale kuungana na watu wengine kwa ajili ya kumuabudu Mungu. Kama yeye sio mtu mwema au hamtumikii Mungu, sisi hayo hayatuhusu. Pia ngoja nikuulize mara ya mwisho wewe kwenda kanisani ni lini?”
“Sikumbuki kwa kweli?”
“Twende lao tuka muombe ombe Mungu”
“Sawa leo huja onyeshwa jambo lolote?”
“Nime onyeshwa jambo kubwa ila nimelisahau. Natambua Mungu ana makusudi maalumu ya kunifanya nisahau juu ya hili alio nionyesha. Nahisi kwa kutokea tukio lolote ana weza kunifungulia mwanga wa kile kitu ambacho amenionyesha”
“Sawa kama ni hivyo”
Josephine akamalizia kazia yake, kisha wakamuaoga raisi Mtenzi na kuondoka. Wakafika katika nyumba ya Magreth wakafanya usafi kwani toka uvamizi utokee hana hata mmoja wao aliye rudi nyumbani. Walipo maliza kila kitu, wakapata chakula cha mchana wakajiandaa na kuelekea kanisani kwa nabii Sanga. Wingi watu walio jitokeza ukamfanya Magreth kukaa kiti cha nyuma huku Josephine akienda kukaa mbele kabisa kama alivyo pewa maelekezo na mzee wa kanisa hilo kwamba kuna kiti chake mbele. Ibada ikaanza huku nyimbo za kumsifu Mungu na kumuabudu zikifanyika. Nabii Sanga akaanza kupiga maombi ya nguvu huku watu wenye mapepo wakianza kutokwa na mapepo yao. Nabii Sanga akamtazama mwana mama aliye kaa kiti cha nyuma na Josephine na ana tambua kabisa jukumu la kazi aliyo mpatia ni kuhakikisha ana mteka Josephine ambaye naye kwa wakati huo yupo kwenye maombi makubwa sana. Mwana mama huyo kwa umakini mkubwa akatoa kisindano kidogo chenye dawa yakali ya usingizi. Akanijanya na yeye ana sali huku akirusha mikono yake hapa na pale kama mtu anaye kemea mapepo. Akamchoma kisindano hicho Josephine shingoni mwake pasipo mtu yoyote kuona.


“Aiiisssiii”
Josephine aligugumia muamivu kidogo, akajaribu kugeuka ila akajikuta akishiwa nguvu na akaanguka chini na kuzimia jambo lililo wafanya watumishi wanao watoa wenye mapepo na kuwaingiza katika chumba cha maombi, wakambeba Josephine wakisaidiana na mwana mama huyo na wakamtoa kanisani hapo pasipo Magreth kufahamu chochote kinacho endelea.


****************************************************************************************************************



ITAENDELEA


Haya sasa, Josephine ameondolewa ndani ya kanisa na mwana mama huyo ambaye amepewa jukumu la kumteka, Magreth hafahamu chochote kinacho endelea, watu walipo hapo kanisani ni wengi sana, je Magreth ata weza kweli kumsaidia rafiki yake huyo? Usikose sehemu ya 162.
 
SIN 162


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188






ILIPOISHIA


Nabii Sanga akaanza kupiga maombi ya nguvu huku watu wenye mapepo wakianza kutokwa na mapepo yao. Nabii Sanga akamtazama mwana mama aliye kaa kiti cha nyuma na Josephine na ana tambua kabisa jukumu la kazi aliyo mpatia ni kuhakikisha ana mteka Josephine ambaye naye kwa wakati huo yupo kwenye maombi makubwa sana. Mwana mama huyo kwa umakini mkubwa akatoa kisindano kidogo chenye dawa yakali ya usingizi. Akanijanya na yeye ana sali huku akirusha mikono yake hapa na pale kama mtu anaye kemea mapepo. Akamchoma kisindano hicho Josephine shingoni mwake pasipo mtu yoyote kuona.


“Aiiisssiii”
Josephine aligugumia muamivu kidogo, akajaribu kugeuka ila akajikuta akishiwa nguvu na akaanguka chini na kuzimia jambo lililo wafanya watumishi wanao watoa wenye mapepo na kuwaingiza katika chumba cha maombi, wakambeba Josephine wakisaidiana na mwana mama huyo na wakamtoa kanisani hapo pasipo Magreth kufahamu chochote kinacho endelea.





ENDELEA


Taratibu wakamuweka chini Josephine kisha watumishi hao wawili wakanisa wakaondoka ndani hapo na kurudi ndani ya kanisa. Mwanamama huyo kwa haraka akatoa simu yake mfukoni na kumpigia kijana wake anaye shirikiana naye kwenye jambo hilo. Kijana huyo akalisogeza gari karibu kabisa na chumba hicho. Mwanamama huiyo akambeba Josephine na kumuingiza ndani ya gari hilo pasipo mtu yoyote kuona. Taratibu wakaondoka eneo hilo pasipo mtu yoyote kustukia juu ya utekaji huo. Maombezi yakaendelea ndani ya kanisa na baada ya dakika hamsini watu wakaruhusiwa kukaa.


Magreth kila anavyo mtazama nabii Sanga ana jihisi kujawa na hasira kwa maana ana mchukia na yeye ndio mtu aliye yasababisha maisha yake kuyumba kwa asilimia kadhaa. Magreth akanyanyuka na kutoka nje, akatoa simu yake mfukoni na kumtumia ujumbe Josephine kwamba ana kaa ndani ya gari kwani kuendelea kukaa kanisani hapo kuna weza kumfanya akamvamia nabii Sanga. Josephine hakujibua meseji hiyo na wala Magreth hakupata wasiwasi wa aina yoyote kwa maana naa tambua rafiki yake huyo akiwa katika maoembezi siku zote ana kuwa ni mtu wa kuzima simu yake au kutoa kabisa mlio wa simu. Magreth akaa ndani ya gari lake hadi ibada hiyo ikaisha majira ya saa mbili usiku. Watu wakaanza kutawanyika huku wenye magari yao wakiondoka kwenye maegesho hayo ya kanisa.


“Mmmm mbona haji huyu?”
Magreth alizungumza huku akitazama saa yake ya mkononi. Mshale wa saa yake una onyesha ni saa tatu kasoro usiku. Idadi ya watu kanisani hapo ina zidi kupungua. Magreth akashuka kwenye gari na kuanza kuanga eneo la mlango wa kutokea kanisa hilo.
“Samahani”
Magreth alimsimamisha mzee mmoja ambaye ana mtambua kwamba ni mmoja wa wapambe wa karibu wa nabii Sanga.


“Ohoo binti yangu. Bwana Yesu asifiwe”
“Amen shikamoo mzee Kiondo”
“Marahaba, hoonekani siku hizi kwenye huduma za kinanisa?”
“Ni kweli mzee wangu mambo yamekuwa ni mengi sana”
“Ila Mungu pia ana umuhimu sana binti yangu”
“Ni kweli mzee wangu. Nina muulizia Josephine huja muona?”
“Mmmmm nilimuona kipindi muna fika hapa kasinani ile jioni, ila sasa hivi sija weza kumuona kabisa. Labda jaribu kumpigia simu”
“Sawa mzee wangu”
Magreth akaipiga namba ya Josephine na kwa bahati mbaya akakuta haipatikani hewani.


“Uko wapi Jose”
Magreth alihaha huku akianza kupita pita kwenye vikundi vya watu wachache wachache walio simama wakipiga stori za hapa na pale. Baada ya kumtafuta ndani hapo pasipo mafanikio yoyote, Magreth akaingia ndani ya kanisa hilo na kuwakuta wazee wa kanisa wachache wakipanga viti vizuri.
“Jamani hamjamuona Josephine?”
“Hapana”
Mzee mmoja wa kanisa alijibu.
“Labda uka mtazame ofisini kwa mtumishi”
“Nashukuru”
Magreth akapiga hatua za haraka huku akipita katia siti za mbele za kanisa hilo. Magreth akasimama kwa sekunde kadhaa kisha akarudi nyuma hatua kadhaa na kuangalia kiti alicho kuwa amekalia Josephine. Chini ya kiti hicho akaiona simu ya Josephine, kwa haraka akaisogelea na kuishika. Akaitazama na kukuta ikiwa imezima.


“Hii huyu amedosha simu?”
Magreth alizungumza huku akiiwasha simu hiyo. Akaendelea na lengo lake la kwenda ofisini kwa nabii Sanga, akaingia ofisini hapo pasipo kubisha hodi na akamkuta nabii Sangaa akizungumza na wamama wawili.
“Samahani jamani, nina muulizia Josephine”
“Magreth ni utaratibu wa wapi huo kuingia ofisini kwa mtu pasipo kubisha hodi?”
Nabii Sanga alilalama huku akimtazama Magreth, ambaye alijishauri kwa sekunde kadhaa kabla hajafikiria ni nini amjibu nabii Sanga.
“Samahani nabii, ila rafiki yangu ndio nina muulizia”
“Hayupo hapa ofisini”
“Ila……”
Magreth akakatisha sentensi yake hiyo huku akimtazama nabii Sanga.
“Nashukuru”
Magreth akatoka ndani hapo huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana, kiasi cha kumfanya ajawe na wasiwasi mwingi sana kwani sio jambo la kawaida kwa rafiki yake huyo kuondoka pasipo kumuaga. Akiwa anakatiza nje ya chumba cha kupumzishia watu wanao lipukwa na mapepo wakati wa maombezi. Akaona kiatu kimoja cha Josephine hapo ndipo akili kengele ya hatari ikamgonga kichwani mwake na kujua kwamba rafiki yake ata kuwa ametekwa na watu wasio julikana. Magreth akatoa simu yake mfukoni kwa haraka na kumpigia raisi Mtenzi.
“Magreth habari yako”
“Muheshimiwa kuna tatizo”
“Tatizo gani?”
“Josephine ameweza kutekwa tukiwa hapa kanisani.”
“Nini?”
“Ndio ametekwa muda na wakati ambao haujulikani?”
“Kivipi na ime kuwaje atekwe katika kanisani?”
“Muheshimiwa nina imani kwamba watekaji walitumia akili ya hali ya juu na ubaya ni kwamba tulikaa maeneo tofauti. Yeye alikaa siti ya mbele na mimi nilikaa siti ya nyuma”
“Shiti, hapo kanisani hakuna kamera?”
Magretha akaangaza angaza eneo hilo.
“Hapana muheshimiwa hakuna kamera”
“Ngoja nimpigie Sanga sasa hivi”
“Sawa muheshimiwa”
Magreth akakata simu hukua kianza kutembea na kurudi ofisini kwa nabii Sanga. Akapishana na wana mama hao mlangoni mwa ofisi ya nabii Sanga. Magreth akaingia ndani na kumkuta nabii Sanga akipokea simu yake na kuiweka sikioni mwake.


“Ndio ndugu yangu”
“Kuna mfanyakazi wangu ana itwa Josephine ame tekwa hapo kanisani kwako. Hivyo nina kuomba unipatie ushirikiano wako ndugu yangu”
“Ametekwa hapa kanisani kwangu?”
“Ndio, nime zungumza na rafiki yake ana itwa Magreth amenidhibitishia kwamba atakuwa maetekwa. Hivyo ndugu yangu nisaidie katika hilo kwa maana kama vile ulivyo muomba binti huyo aje kusali kanisani kwako ndivyo jinsi ninavyo kuomba aweze kupatikana kwa maana jukumu la ulinzi wa waumini wako wote lina paswa kuwa mikononi mwako. Tumelewana ndugu yangu?”
Raisi Mtenzi alizungumza kwa msisitizo.
“Nime kuelewa ndugu yangu nita fanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba nina mpata msichana huyo”
“Nashukuru, na vijana wangu wa upelelezi wata kuja kuanza kuifanya upelelezi hapa kanisani”
“Sawa sawa nita wasubiria”
“Nashukuru’
Simu ikakatwa, nabii Sanga akamtazama jinsi Magreth alivyo shika kiatu mkonini mwake.
“Ame tekwaje?”
Nabii Sanga alijifanya kuuliza kana kwamba hajui kitu chochote.
“Nahitaji mkanda mzima wa video zilizo rekodiwa na makamera man wako katika ibada ya leo”
“Sawa”
Nabii Sanga alizungumza kwa kujiamini. Akampigia produser wa vipindi vya kanisani hapo na akaingia akiwa na flash yenye video ya mahubiri ya siku nzima ya siku hiyo. Wakaichomeka kwenye tv na wakaanza kufwatilia kuanzia ibada ilivyo anza. Hadi wanafikia mwisho Magreth hakuona sehemu aliyo kuwa amekaa Josephine jambo lililo mfanya azidi kuchanganyikiwa kwa woga.


***


Taratibu Josephine akafumbua macho yake, akajikuta akiwa amelala kitandani, jambo lililo mfanya kuvuta kumbukumbu yake ya mwisho iliyo mueleza kwamba alikuwa kanisani katika kipindi cha maombi na baada ya hapo hafahamu ni kitu gani kinacho endelea. Akajitazama mavazi yake na kujikuta akiwa amevaa vile vile alivyo kuwa kanisani. Taratibu akaka kitako na kuangaza ndani ya chumba hicho ambapo kuna tv kubwa, meza ya mbao pamoja na kitanda hicho. Hakuna kabati wala kochi. Akasimama na kuanza kutembea kwa mwendo wa taratibu na kuchungulia dirishani. Mapigo ya moyo yakaanza kumuenda kasi mara baada ya kuona kuna bahari tu.


‘Mungu wangu nipo wapi hapa?’


Josephine alijiuliza huku akiendelea kuangaza angaza. Akatembea hadi mlangoni akashika kita na kujaribu kufungua ila akakuta mlango huo ukiwa ume fungwa kwa nje. Akaanza kugonga mlango huo huku akiomba kufunguliwa, ila hapakuwa na mtu yoyote aliye weza kumsaidia kufungua.


“Ehee Mungu ni nini hichi?”
Josephine alijikuta akisali ila hakuweza kupewa majibu yoyote na Mungu wake. Gafla mlango ukafunguliwa, akaingia mwanaume mrefu mwenye madevu mengi usoni mwake na kwa kumtazama kwa haraka haraka asili yake ni mzungu, japo Josephine hatambui ni mzugu wa wapi. Mwanaume huyo mkononi mwake, ameshika sahani ambayo ina vipande vya soseji viwili, mkate slesi nne, yai moja la kuchemsha. Kipande cha samaki wa kukaanga pamoja na glasi iliyo jaa maziwa.


“Wee ni nani?”
Josephine aliuliza huku akiwa ana tetemeka kwa woga. Mwanaume huyo hakuzungumza chochote zaidi ya kuweka sahani hiyo pamoja na glasi juu ya meza na kuanza kutembea kulekea nje.


“Nime kuuliza wewe ni nani?”
Mwanaume huyo akafunua tisheti yake eneo la kiunoni na kumfanya Josephine aione bastola ya mwanaume huyo, jambo lililo muashiria Josephine kwamba eneo hilo alipo sio salama kabisa na maisha yake. Mwanaume huyo akaufunga kwa nguvu mlango huo wa chuma na kumfanya Josephine kustuka. Akafunga kwa nje mlango huo kisha akaondoka.


Machozi yakaanza kumbubujika Josephine, jambo alilo kuwa ameonyesha mchana wa siku hiyo sasa taratibu akaanza kulikumbuka kwa maana mara baada ya kuonyesha alisahaulishwa kila kitu ili asiweze kujitoa kwenye jambo hilo.
***


Nabii Sangaa akaendelea kutoa ushirikiano kwa wapelelezi hao walio fika kanisani kwake kujaribu kuchunguza tukio la kupotea kwa Josephine chief staff wa ofisi ya raisi ya raisi. Upepelezi wao wote hakuweza kujua ni nani ame husika na utekaji wa Josephine. Mwanana mama ambaye ndio aliifanya kazi hiyo, ndio kiongozi anaye ongoza vijana wake katika kupeleleza tukio hilo.Muda wote Magreth alikuwa kama mtu aliye shikwa na bumbuwazi, sehemu aliyo kaa hakunyanyuka huku mkononi mwake akiwa na kiatu cha rafiki yake huyo.


“Mage”
Nabii Sanga alimuita Magreth kwa sauti ya upole huku akikaa pembeni yake.
“Mungu wetu tunaye muabudu nina imani ata muokoa Josephine hujo alipo”
Maneno ya nabii Sanga yakamfanya Magreth kumtazama kwa sekunde kadhaa pasipo kumjiubu chochote.
“Mage nina omba unisamehe”
“Nini?”
“Nina kuomba unisamehe. Mimi na wewe tume kuwa ni watu wa kupishana sana kauli. Tume ingia kwenye mgogoro ambao kwa kweli sihitaji uendelee. Ya nyuma yaliyo pita yapite na tugange yajayo”
Nabii Sanga aliendelea kuzungumza kwa sauti ya ushawishi.
“Nisikilize wewe, nina kuchukia na laiti inge kuwa sio hii sheria ya nchi, ni siku nyingi sana ninge kuwa nimesha kuua wewe”
“Mage Mage”
“Niache bwana”
Magreth alizungumza kwa hasira na kunyanyuka kwenye kiti hicho. Akaingia kwenye gari lakena kuelekea moja kwa moja makao makuu ya kitengo cha NSA.


“Mkuu nahitaji kuonana na yule Jackline”
“Kwa nini?”
“Mkuu nina hitaji kumuhoji, kama waliweza kujaribu kuniua mimi asubuhi, sasa hivi wame mteka rafiki yangu. Huoni kwamba hapa kuna kajimtandao?”
“Magreth upo kwenye hasira siwezi kukupa ruhusa ya kuonana na yule msichana”
“Sikuelewi mkuu, mbona una mlinda sana yule binti au kwa kuwa ni mzuri?”
“Sio hivyo”
“Ila?”
“Yeye kama mtu humiwa ana haki zake za msingi”
Magreth akatoa simu yake mfukoni na kumpigia raisi Mtenzi na kumuomba ruhusu ya kumuhoji Jackline. Raisi Mtenzi akaomba azungumze na mzee Mbogo na Magreth akampatia simu.


“Ndio muheshimiwa”
“Mpatie ruhusa ya kumuhoji huyo biti. Acha atumie uwezo wake wote katika kumuhoji, tuna paswa kujua ni nani ana husika na haya matukio. Asubuhi ni yeye, usiku huu ni mfanyakazi wangu tena ametekewa kanisani huoni kama hilo ni jambo ambalo halipo sawa?”
“Ila muheshimiwa huyu binti tuna paswa kumuhoji kwa akili sana”
“Ni amri Mbogo nina kupatia”
“Sawa muheshimiwa”
Mzee Mbogo akampatia simu Magreth na akaiweka sikioni mwake.


“Ndio muheshimiwa”
“Tumia silaha yoyote kuhakikisha ana zungumze ukweli na hakikisha tu hafi”
“Usijali muheshimiwa”
Magreth akakata simu huku akimtazama mzee Mbogo anaye onekana kuto kuridhishwa na amri hiyo, ila hana jinsi zaidi ya kufwata amri ya mkuu wake wa nchi. Magreth moja kwa moja akaelekea kwenye chumba alicho fungiwa Jackline.


“Sijakuja kiwema nime kuja kwa jambo moja tu. Niambie ni nani ambaye alikutuma kuniua mimi?”
Magreth alizungumza kwa sauti ya kukoroma. Taratibu Jackline akaka kitako kitandani kwake huku akiwa amefunga pingu mkono mmoja kwenye kitanda hicho huko miguu yake ikiwa ime fungwa cheni inayo muwezesha kupiga hatua moja.


“Nilisha kueleza kwamba siwezi kutaja mtu hadi utimize nililo kuambia”
Magreth kwa hasira kaampiga teke la kifua Jackline na kumfanya ajibamize ukutani, akamshika mkono wake ambao haujafungwa pingu na kuuvunja kwa nguvu na kumfanya Jackline alie kwa sauti ya juu kwani maumivu hayo ni makali sana.
“NIAMBIE NI NANI ALIYE KUTUMAAAAAAA”
Magreth alizungumza kwa ukali huku akishika vidole viwili vya Jackline ambaye bado anaendelea kulia kwa uchungu. Magreth akavunja vidole hivyo vya mkono huo huo alio uvunja na kumfanya Jacklien achachamae kwa kulia kwa uchungu sana kwani kwenye maisha yake hajakutana na adhabu kama hizo anazo pewa na Magreth,
***


“Sanga”
Mwnaa mama huyo alimuita nabii Sanga na wakasogea pembeni ili wazungumze.


“Kazi yako imesha kamilika na tulimkabidhi yule binti kwa vijana wako kule baharini nina imani kwamba wame kupatia ripoti sehemu walipo mpeleka?”
“Ndio nina shukuru sana kwa hilo na hongera sana kwa kazi nzuri”
“Usijal…..”
Mwana mama huyo akatoa simu yake mfukoni na kusoma ujumbe huo mfupi wa maseji aliyo tumiwa na kijana wake.
“Shitiii”
“Nini?”
Nabii Sanga alimuuliza mwana mama huyo huku macho yakiwa yamemtoka kwa maana ana onenyesha kuchanganyikiwa na meseji hiyo aliyo tumia.


“Yule binti aliye ondoka hapa, amekwenda kwenye kitengo cha NSA na sasa hivi ana muhiji Jackline na ana mpatia mateso makali sana. Mzee usipo angalia Magreth ana kuunguza”
Nabii Sanga mapigo yake ya moyo yakanza kumuenda kasi sana huku akiwa ana tafakari ni nini cha kufanya.
“Nina omba msaada mmoja”
“Msaada gani?”
“Niulie Magreth na Jackline. Nita kupatia dola milioni tano, nina imani umasikini uta kwenda kuuga, tafadhali ifanye kazi hiyo”
Maneno ya nabii Sanga yakamfanya mwana mama huyo kujitafakari kwa dakika moja nzima kisha akatabasamu huku akimtazama Sanga usoni mwake. Akampatia mkono ikiwa ni ishara ya kukubali kuifanya kazi hiyo ambayo ana amini endapo ata ifanikisha basi umasikini uta muondokea kwenye maisha yake.


****************************************************************************************************************


ITAENDELEA


Haya sasa, Jackline ana vunjwa vunjwa viongo vya mwili wake je ata mtaja muhusika aliye mtuma. Josephine ana weza kutoka kwenye eneo hilo alilo fungiwa. Je mwana mama huyo ata weza kumuua Jackline na Magreth? Usikose sehemu ya 163.
 
SIN 163


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188



ILIPOISHIA


“Shitiii”
“Nini?”
Nabii Sanga alimuuliza mwana mama huyo huku macho yakiwa yamemtoka kwa maana ana onenyesha kuchanganyikiwa na meseji hiyo aliyo tumia.


“Yule binti aliye ondoka hapa, amekwenda kwenye kitengo cha NSA na sasa hivi ana muhiji Jackline na ana mpatia mateso makali sana. Mzee usipo angalia Magreth ana kuunguza”
Nabii Sanga mapigo yake ya moyo yakanza kumuenda kasi sana huku akiwa ana tafakari ni nini cha kufanya.
“Nina omba msaada mmoja”
“Msaada gani?”
“Niulie Magreth na Jackline. Nita kupatia dola milioni tano, nina imani umasikini uta kwenda kuuga, tafadhali ifanye kazi hiyo”
Maneno ya nabii Sanga yakamfanya mwana mama huyo kujitafakari kwa dakika moja nzima kisha akatabasamu huku akimtazama Sanga usoni mwake. Akampatia mkono ikiwa ni ishara ya kukubali kuifanya kazi hiyo ambayo ana amini endapo ata ifanikisha basi umasikini uta muondokea kwenye maisha yake.





ENDELEA


“Jambo moja kabla sijaifanya hiyo kazi”
“Ehee”
“Hii kazi nina imani kwa asilimia kubwa haito niacha salama mimi na familia yangu. Ningependa kupata nchi ambayo mimi na familia yangu tuta kwenda kuishi au kuitanguliza familia yangu ikaishi huko, ili ikitokea la kutokea basi nijue ni wapi kwa kukimbilia.”
“Wewe una kwenda nchi gani?”
“Nita kupatia jibu ni nchi gani ambayo itakuwa ni rafiki kwangu na familia kwenda kuishi”
“Unijulishe mapema kwa maana hili swala ni nyeti sana”
“Sawa nabii Sanga”
Mwana mama huyo akaagana na nabii Sanga kisha akaondoka kanisani hapo. Wapelelezi hao walipo kusa kitu cha kuwasiaida kwenye kazi yao ya kumtafuta Josephine wakaondoka kanisani hapo na kumuacha nabii Sanga akiwa na baadhi ya watumishi wake.


***


Maumivu makali anayo yapata Jackline yakamfanya ashindwe kuyahimili na kujikuta akizimia. Jambo hilo halikumuogopesha Magreth ambaye ana vujwa na jasho mwili mwizma. Kupotea kwa Josephine hakika kume mfanya kuwa kama mtu aliye changanyikiwa.


“Nahitaji mumchome sindano ya kumuamsha”
Magreth aliwaambia madaktari wawili walio ingia ndani hapo kwa ajili ya kumpatia huduma Jackline.


“Mkuu ila hali yake sio nzuri kabisa”
“Hana faida kwenye hili taifa, nasema mchomeni sindano ya kumzindua”
Magreth alizungumza kwa ukali na madaktari hao wakatii, Jackline akazinduka mara baada ya kuchomwa sindano hiyo.


“Bado hatujamaliza, nahitaji kufahamu ni nani ambaye amekutuma kuniua mimi?”
Jackline akamtazama Magreth kwa macho ya dharua kisha akatabasamu.
“Go fuc** your as**”
Tusi hilo likamfanya Magreth kuanza kumshambulia kwa kumpiga Jackline kila mahali ya mwili wake. Kitendo hicho kikawafanya askari walipo ndani nje ya mlango huo kuingia na kumshika Magreth ili kuacha kufanya kitendo hicho ambacho hakiwezi kumfanya mtuhumiwa kuzungumza.


“Niachieni?”
Magreth alizungumza huku akijitutumia mikononi mwa askari hao walio jazia kwa misuli ila hakuweza kujichomoa kwa maana wana nguvu kubwa sana.Wakamtoa ndani hapo na kuwaacha madaktari wakiwa na kazi ya kuanza kumuhudumia Jackline aliye vunjika mkono, vidole pamoja na majeraha mengine kagtuka mwili wake.
“Magreth najutia ni kwa nini nime kupatia hiyo hii kazi. Una tumia nafasi yako vibaya ya ukaribu wako na raisi Mtenzi. So nikiwa kama mkuu wa hichi kitua kuanzia hivi sasa, nime kusimamisha kazi kwa muda usio julikana. Nipatie bastola yako pamoja na kitambulisho chako”


Mzee Mbogo alizungumza huku akimtazama Magreth aliye simama hapo huku akiwa na hasira kali. Magreth akatoa kitambulisho hilo mfukoni mwake.
“Bastola njooni muichukue kwenye gari”
Askari hao wakaongozana na Magreth hadi kwenye gari lake, akawakabidhi bastola aliyo kabidhiwa na kitengo hicho kisha akaondoka makao makuu ya kitengo hicho majira ya saa sita usiku.


“Hali yake ipo vipi?”
Mzee Mbogo aliuliza huku pambeni yake akiwa amesimama mwana mama aliye pewa kazi ya kumuua Jackline na Magreth.


“Hali yake sio nzuri kabisa mkuu”
“Hakikishenii ana kuwa salama”
“Sawa”


“Ila muheshimiwa endapo huyu bunti akifariki ita kuwaje?”
Mwana mama huyo aliuliza swali.
“Tuta kuwa tume poteza pointi za muhimu. Wasimamie madaktari hadi hii kazi itakapo kamilika, nina kwenda kumuandikia ripoti raisi juu ya vitendo vilivyo nifanya nimsimamishe kazi Magreth”
“Sawa mkuu”
Mzee Mbogo akapiga hatua mbili mbele kisha akageuka.


“Alafu Sia mume fanikiwa kujua chochote kwenye kanisa la nabii Sanga, kuonyesha watekaji ni kina nani?”
“Hapana muheshimiwa hatukufanikiwa kupata ushahidi wowote wa video zaidi ya kiatu kimoja cha biti huyo?”
“Daaa mambo yana ingiliana sana jamani. Haya baadae”
Mwana mama huyo aitwaye Sia akamtazama Jackline jinsi alivyo mrembo na kujikuta akimuoea huruma sana kwa maana makano ya Jackline ni sawa na binti yake wa kwanza. Akatafakari miaka zaidi ya ishirini na tisa amekuwa ni mpelelezi kwenye kitengo hicho na hakuwahi kukuta na kosa la aina yoyote. Akawafikiria wanae wanao ishi kwenye maisha ya raha na starehe kutokana na kazi yake hiyo, akajifikiria endapo serikali ita anza kumsaka kama muhalifu, furaha ya familia yake hiyo ita kuwa wapi.


‘No siwezi kufanya hii kazi, nilicho kifanya leo ina tosha’


Sia alizungumza na kuondoka chumbani hapo huku moyoni mwake akidhamiria kuhakikisha kwamba ana mueleza nabii Sanga juu ya kushindwa kwake kuifanya kazi hiyo.


***


Magreth akasimamisha gari nje ya nyumba yake huku hasira bado ikiwa ume ukamata moyo wake unao kwenda kasi na kusababisha maumivu makali. Akazidi kutafakari ime kuwaje Josephine akatekwa kanisani na alitekwa muda gani.


‘Ni nani mwenye chuki na Josephine? Au ni yule X wake?’


Magreth alijiuliza maswali kichwani mwake ila akakosa jibu ka kujipatia.


‘Hapana X wake toka nimpige kipindi kile hakurudi tena’


‘Au ni Evans ndio ana endeleza huu mpango wake?’


‘Yaa ni Evans nahisi wamemkamata Josephine ili kunishinikiza kumuachia mtu wao. Magreth akaitoa simu ya Josephine mfukoni mwake, akachukua waya wa chaji, akauchomeka ndani ya gari hilo kisha akaiwasha simu hiyo, akaingiza neno la siri ambalo ana lifahamu na simu hiyo ikafunguka Akaanza kukagua majina ya watu walio mpigia na mtu wa mwisho kabisa ni nabii Sanga.


‘Sanga sana sanga ana weza kumteka Josephine?’


Magreth mawazo yake yakahamia tena kwa nabii Sanga.


‘Hapana laiti angekuwa ame mteka ange kuwa na wasiwasi mwingi ila, alikuwa hajui nini kinacho endelea.’


‘Ila kama Magreth angetoka pale kanisani ninge muona kwa maana mlango ni mmoja na isitoshe nilikaa siti ya nyuma karibu na mlangoni.’


Magreth aliendelea kujishauri. Akaanza kukumbuka kipindi cha maombezi watu wengi walisimama huku watu kadhaa wakianguka na mapepo.


‘Au ni kipndi kile cha mapepo ndio alitoka nje?’


‘Yaaa kiatu nilikikuta nje ya kile chumba cha kuwawekea watu wenye mapepo.’


‘Josephine ana mtindo wa kuzimia akisali sana. Kama walimpeleka kule nina uhakika wa asilimia mia moja kuna watu walio mbeba.’


Magreth aliendelea kuchanganua kichwa chake. Jambo la kumshukuru Mungu watumishi karibia wote wa kanisa la nabii Sanga ana wafahamu na sehemu zao wanapo ishi. Magreth akashuka kwenye gari lake kwa haraka akaingia ndani kwake, akaoga na kubadilisha nguo zake kisha akachukua kiasi cha pesa na kutoka ndani hapo, akafunga nyumba yake na kuanza kwenda kwenye nyumba ya mtumishi mmoja baada ya mwengine. Japo ilikuwa ni usiku, ila watumishi hao waliweza kumfungulia milango na kumsikiliza na jambo zuri zaidi ni kwamba wana mfahamu Magreth alikuwa ni miongoni mwa watumishi wezao hapo kanisani kwa kipindi kirefu sana. Magreth akafika kwa mtumishi wa tano iatwaye John Manguruwe.


“Bwana Yesu asifiwe mtumishi”
“Amen, mbona usiku kuna tatizo?”
“Kwanza nikuombe msamaha kwa kuja kwako usiku huu. Nina imani sio taratibu nzuri kufika nyumbani kwa mtu usiku kama huu”
“Usijali, sisi ni wanajeshi wa Mungu, muda wowote kwetu tumejiandaa na vita. Niambie una tatizo gani Magreth”
“Leo nilikuja kanisani na Josephine”
“Yaa nilimuona Josephine alikaa siti ya mbele pale”
“Ni kweli, ila huwezi amini Josephine hatumuoni hadi sasa hivi?”
“Hamumuoni muna maanisha nini?”
“Naweza kutumia hili neno japo sio rasmi. Josephine ame tekwa na watu ambao hatuwajui kabisa”
“Mmmm hapana bwana Magreth. Mimi, mtumishi Luka na mwana mama mmoja hivi tuliweza kumbeba Josephine na kumpeleka katika chumba cha watu wanao hitaji huduma ya maombi kisha tukamuacha ndani hapo na kwenda kuwachukua wengine”
“Alianguka kwa mapepo?”
“Hapana una jua mtu anaye anguka kwa mapepo ana kuwa ana ruka ruka, ila yeye alikuwa kama mtu aliye zimia vile”
“Ahaa kwa hiyo mulimbeba watatu?”
“Ndio tulisaidiana na yule mwana mama”
“Una mkumbuka sura yake huyo mama?”
Bwan John Manguruwe akaka kimya kwa sekunde kadhaa huku akivuta taswira ya mwana mama huyo aliye saidiana naye.


“Ngoja kwanza”
Bwan John akaingia ndani kwake na kuchukua simu yake kisha akatoka nayo sebleni hapo. Akaitafuta namba ya Luka.
“Ngoja nimpigie Luka ana weza kuwa na kumbu kumbu nzuri”
Bwana John akaiweka simu yake loud speaker, na simu hiyo ikaanza kuita. Baada ya sekunde kadhaa ika pokelewa.


“Mtumishi bwana Yesu asifiwe?”
“Amen ndugu yangu nina shukuru kwa kuniamsha bwana nifanye maombi ya usiku”
“Yaa muda ume fika ni saa nane usiku sasa. Ila nipo na Magreth yule aliye kuwa ni muimbaji kwaya”
“Ohoo Mage ndio ndio mtumishi. Vipi kuna tatizo?”
“Ndio hivi una kumbuka muda tuna mbeba yule binti Josephine?”
“Ndio nina kumbuka?”
“Una mkumbuka yule mwana mama tuliye saidiana naye kumbeba na kumuingiza mule ndani?”
“Yaa naikumbuka sura yake vizuri sana. Alafu yule mama ni mara yangu ya kwanza kumuona pale kanisani, japo kanisa letu kila siku lina pokea watu wapya”
Magrteth akashusha pumzi huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.


“Sawa hembu zungumza na Magreth hapa umuelezee sifa za muonekano wa yule mwana mama”
Magreth akaishika simu hiyo na kuisogeza mdomoni mwake. Bwana Luka akaanza kueleza sifa za mwana mama huyo jinsi anavyo onekana. Hadi ana fika mwishoni Magreth akaanza kujiuliza ni wapi aliwahi kumuona mwana mama huyo.


“Ni maji ya kunde?”
“Ndio alafu tulimuacha mule ndani, ya kile chumba”
“Sawa ngoja kuna kijana nina mpigia simu sasa hivi alafu nina kuomba sana umuelezee hizi sifa”
“Sawa”
Magreth kwa kutumia simu ya Josephine akampigia Samson.
“Sister upo salama?”
Samson aliwahi kuzungumza mara baada ya kupokea simu hiyo.


“Ni mimi Mage”
“Ohoo Magreth, heshima yako”
“Nashukuru sasa Samson kuna yule mchoraji yupo bado ikulu?”
“Ndio”
“Hembu niunganishe naye kwenye simu”
“Sawa”
Baada ya dakika mmoja mchoraji wa katuni na mambo mengine, akaunganishwa kwenye simu na Magreth.


“Habari yako kaka”
“Salama dada”
“Kuna mchoro nina hitaji uweze kuuchora muda huu ili kumtambua huyo mtu. Je una nafasi ya kuifanya hiyo kazi?”
“Ni ishu ya kiserikali au binafsi?”
“Serikali”
“Sawa”
“Nina kuunganisha na mtu atakaye kuelezea sifa za mtu tunaye muhitaji”
“Hakuna shaka”
Magreth akakata simu ya bwana Luka iliyo pigwa na bwana John kisha akampigia yeye bwana Luka.


“Ndio mtumishi”
“Upo hewani na mchoraji wa ikulu, sasa una weza kumuelezea hizo sifa”
Bwana Luka akaanza kueleza sifa za mwana mama huyo muonekano wake wa sura na jinsi alivyo vaa.


“Tayari nimesha zi master baada ya muda mchache mchoro wako uta kuwa tayari dada Magreth”
“Nina shukuru sana, nina fika hapo ikulu muda si mrefu na hakikisha humuelezi mtu yoyote juu ya huo mchoro kabla yangu”
“Sawa”
Magreth akakata simu na kuanza kumshukuru bwana John Manguruwe. Akampatia kiasi cha laki mbili kisha akamuachia laki moja ambayo ata mkabidhi bwala Luka, kwani ushirikiano wao katika majira hayo ya usiku wa saa nane hakika ni jambo linalo mpa moyo sana. Magreth moja kwa moja akaelekea ikulu, akasimamisha gari lake kwenye maegesho na kuelekea katika ofisi ya mchoraji.
“Habari za muda”
“Salama mchoro wako upo tayari”
Mcharaji alizungumza huku akiuweka mchoro huo kwenye computer yake kubwa iliyopo mbele yake.
“Una mfahamu huyo mwana mama?”
“Hapana labda Samson ngoja nimtumie hii picha”
“Hembu muite Samson aje hapa”
Mchoraji akanyanyua mkonga wake wa simu, na kumpigia Somson.


“Dogo hembu njoo ofisini kwangu mara moja”
“Sawa kaka”
Baada ya dakika tano Samson akaingia ndani hapo. Kuiona sura ya mwana mama huyo akastuka kidogo.
“Huyo ndio mulikuwa muna mchora?”
Samson aliuliza.


“Ndio una mfahamu?”
“Ndio si mkuu wa kitengo cha upelelezi cha NSA. Ana itwa Sia Kamara”
“Ahaa ndio maana nilikuwa nina jiuliza hii sura nime iona wapi kumbe ni mfanyakazi wa kitengo cha NSA?”
“Ndio tena yupo nafasi ya juu sana”
Magreth akakaa kimya kwa sekunde kadha akisha akamkumbuka mwana mama huyo aliweza kufika kanisani hapo wakati akika katika uchunguzi wa kulichunguza tukio la kutekwa kwa Josephine.


“Una namba yake?”
“Nahisi ila ngoja nikachukue laptop yangu”
Samson akatoka ndani hapo na baada ya dakika kadhaa akarudi akiwa na laptop yake. Akatafuta profile ya mwana mama huyo na kuipata, katika profile hiyo kuna jina halisi, miaka ya kuzaliwa, barua pepe pamoja na namba yake ya simu.
“Je muna weza ku hack namba ya huyu mwana mama?”
“Eheheee…..Mage sihitaji kwenda jela na umri huu aisee. Demu wangu ana ujauzito baada ya miezi kadhaa tu ata jifungua. Hilo swala kwa kweli haliwezekani”
Samson alizungumza huku akimtazama Magreth usoni mwake.
“Dada Mage una jua maswala ya kumchunguza mpelelezi wa serikali hayo una takiwa kupata kibali maalumu kutoka kwa raisi mwenyewe. Usije kumshinikiza dogo akaifanya hiyo kazi ni hatari sana”
“Nime waelewa, ila ikitokea nime pata hicho kibali je una weza kudukua mazungumzo yake ya simu?”
“Ndio ila watu kama hao, ufanyaji wao wa kazi hawawi na laini moja. Yaani hii utakuta ni laini inayo julikana na watu kadhaa, ila wana kuwa na namba za siri ambazo sifa namba moja haziwezi kabisa kurekodiwa na makampuni ya simu hivyo ili kupata mazunugumzo yao ya siri ni kuweka kudukua simu zao. Kuna app fulani hivi ni ya siri sana, ukiingiza ndani ya simu hiyo basi kila simu na meseji anazo piga na kupigiwa zina ingia kwenye simu yako.”
“Ina itwaje hiyo app?”
“Siwezi kukuambia kwa sasa hivi kwa maana hiyo app hata playstore haipo. Tunayo sisi tu watu wa mitandao tunao fanya kazi na serikali”
“Sawa nita lifwatilia hili jambo kisha nita omba tushirikiane. Ila tafadhali nina waomba sana hili jambo lisiweze kutoka kati ya sisi watu watatu”
“Swali la mwisho dada Mage. Kwa nini una mfwatilia huyo mwana mama?”
Mchoraji aliuliza swali huku akimtazama Magreth usoni mwake.
“Chief staff wa ikulu ametekwa?”
“Weee Josephine ametekwa?”
Mchoraji aliuliza huku akiwa na mshangao mkubwa sana.
“Ndio ametekwa ndio maana muna niona nina hangaika hivi”
“Duu sina habari kabisa, wapi ame tekwa?”
“Ilikuwa ni kanisani. Ila bado nina endelea kufanya uchunguzi kwa kutumia akili sana, nina waomba kwa pamoja tuweze kushirikiana kwa pamoja katika hili”
“Sawa dada ila pole sana”
“Nashukuru.”
“Sister ukihitaji msaada wowote, wewe niambie nina imani tuta mpata tu Josephine”
“Nashukuru Samson”
Magreth akaagana nao kisha akaelekea ofisini mwa Josephine. Akasimama kwa sekunde kadhaa huku akitazama jinsi vitu vilivyo pangana vizuri ndani hapo. Taratibu akaka kwenye sofa, kisha akajilaza huku akitafakari.


‘Sasa inabidi kutumia akili, hili jambo ni la kwenda nalo taratibu sana, nikienda kwa papara hakika nita mpoteza rafiki yangu na mimi nita kufa pia’


Magreth alizugumza kimoyo moyo huku akiendelea kutafakari juu ya upelelezi wake huo mpya ambao ana amini kwenda taratibu basi ata wapata maadui zake.


****************************************************************************************************************



ITAENDELEA


Haya sasa, Magreth ameanza upalelezi wake wa kimya kimya je ata fanikiwa kweli kujua chochote juu ya mwana mama huyo kama ndio muhusika wa utekaji wa rafiki yake kipenzi Josephine? Usikose sehemu ya 164.
 
“Mage”
Nabii Sanga alimuita Magreth kwa sauti ya upole huku akikaa pembeni yake.
“Mungu wetu tunaye muabudu nina imani ata muokoa Josephine hujo alipo”
Huyu nabii anaweza kwenda mbinguni kweli?
 
SIN 164


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188




ILIPOISHIA


“Duu sina habari kabisa, wapi ame tekwa?”
“Ilikuwa ni kanisani. Ila bado nina endelea kufanya uchunguzi kwa kutumia akili sana, nina waomba kwa pamoja tuweze kushirikiana kwa pamoja katika hili”
“Sawa dada ila pole sana”
“Nashukuru.”
“Sister ukihitaji msaada wowote, wewe niambie nina imani tuta mpata tu Josephine”
“Nashukuru Samson”
Magreth akaagana nao kisha akaelekea ofisini mwa Josephine. Akasimama kwa sekunde kadhaa huku akitazama jinsi vitu vilivyo pangana vizuri ndani hapo. Taratibu akaka kwenye sofa, kisha akajilaza huku akitafakari.


‘Sasa inabidi kutumia akili, hili jambo ni la kwenda nalo taratibu sana, nikienda kwa papara hakika nita mpoteza rafiki yangu na mimi nita kufa pia’


Magreth alizugumza kimoyo moyo huku akiendelea kutafakari juu ya upelelezi wake huo mpya ambao ana amini kwenda taratibu basi ata wapata maadui zake.





ENDELEA


Usingizi wa mang’amu ng’amu ukampitia Magreth. Alafajairi na mapema akwazinduka huku akiangaza angaza ndani ya ofisi hiyo ya Josephine. Hakika kupotea kwa rafiki yake kuna mfanya ajihisi vibaya. Akanyanyuka na kujinyoosha viongo vyake vya mwili kisha akatoka ndani hapo. Akasalimiana na baadhi ya wafanyakazi huku lengo lake ni kuhakikisha kwamba ana kuwa wa kwanza kuwea kuonana na raisi kwa ajili ya kumshirikisha katika mpango wake wa upelelezi kwa maana hana mamlaka yoyote kwa sasa.


“Habari muheshimiwa raisi”
Magreth aliwahi kumsalimia raisi Mtenzi mara baada ya kumona akiwa ameongozana na walinzi weka wawili kwenye kordo ya kuelekea ofisini kwake.
“Salama tu, tena nilikuwa nina kuwazia. Twende ofisini”
Wakaingia ofisini, na moja kwa moja raisi Mtenzi akaka kwenye kiti chake na Magreth akaka kwenye kiti cha wageni.
“Ume fikia wapi mchakato wa kumtafuta Josephine?”
“Muheshimiwa bado sija mpata ila nina dalili fulani za kumpata. Ila kazi yangu ina kuwa ngumu kwa sasa kutokana na kufukuzwa kazi?”
“Umefukuzwa kazi na nani na kwa nini?”
Raisi Mtenzi alionekana kushangaa huku akiwasha computer yake.


“Mkuu wa kitengo cha NSA.”
Raisi Mtenzi akamtazama Magreth kwa sekunde kadhaa kisha akafungua computer yake na kukutana na ujumbe wa barua pepe kutoka kwa mkuu wa kitengo cha NSA, mzee Mbogo. Akaifungua barua pepe hiyo na kuanza kuisoma, maelezo yanayo onyesha makosa aliyo yafanya Magreth.
“Wame kuonea.”
Raisi Mtenzi alizungumza huku akinyanyua mkonga wa simu yake ya mezani.
“Muheshimiwa ila mimi sihitaji kurudi tena kwneye kile kitengo”
Kauli hiyo ya Magreth ikamfanya raisi Mtenzi kurudisha mkonga huo wa simu sehemu alipo utoa.
“Kwa nini?”
“Nahitaji kumsaidia Josephine, nikifanikiwa kumpata basi nita ifanya kazi yangu moja ya mwisho ya kumtafuta Evans Shika, kisha baada ya hapo nita endelea na maisha yangu ya upishi. Nahitaji kuwa mama, nahiaji kuwa na mume hivyo nikiendelea kuwa katika kazi hii hakika sinto weza kupata hivyo vitu viwili au nina weza kuvipata vyote ila nina weza kuwasababishia waishi kwakuto kuwa na amani katika maisha yao yote kutokana na maadui nitakao watengeneza”
Hoja ya Magreth ikamfanya raisi Mtenzi kuka kimya kwa sekunde kadha huku akionekana kuitafakari.
“Natambua muheshimiwa una nihitaji kwenye majukumu yako. Ila nimesha fanya kazi vya kutosha. Nimejitahidi pale nilipo weza kutokana na uwezo wangu huu nilio nao. Sihitaji kutengeneza matatizo zaidi ya viongozi wako ambao una saidiana nao. Tafadhali muheshimiwa nina kuomba sana unisaidie kwenye hili jambo la mwisho tu”
“Niambie jambo gani?”
“Kuna huyu mwana mama ana itwa Sia, ni mmoja wa viongozi wa kitengo cha NSA. Jana usiku nilipo endelea na upelelezi wangu kwa kuwahoji watu walio saidiana kumbebea Josephine na kumuingiza kwenye chumba cha mapumziko waka daiwa kwamba walisaidiana na mwana mama huyo kumuingiza Josephine kwenye hicho chumba”
“Ngoja kwanza Magreth, una sema walisaidiana kumbebaba kivipi?”
“Jana kanisani maombezi yalivyo kuwa yana endelea. Josephine aliweza kuangua, huwa ni kawaida yake pale anapo kuwa ana pata maono nina imani hili jambo ulisha wahi kulishuhudia?”
“Yaa nilisha wahi kuliona”
“Hivyo baada ya jambo hilo kutokea, akabebwa na watumishi wawili wa kanisa pamoja na huyo mwana mama na kumuingiza katika hicho chumba. Pale kanisani kwa nabii Sanga kuna chumba maalumu cha maombia ambacho wale wanao anguka kwa mapepo huwa wana ingizwa hapo kwa ajili ya kupumzishwa.”
“Hapo nime kuelewa. Ehee endelea?”
“Sasa wale watumishi wawili waliniambia mwana mama huyo anaye itwa Sia walimuacha ndani ya hicho chumba. Sasa hapo ndipo ninapo anza kupata mashaka, imekuwaje Josephine akapotea na mbaya zaidi nilikuta kiatu chake kikiwa nje ya chumba hicho”
“Kwani kuna mlango wa kutokea katika hicho chumba tofauoti ya na mlango wa kuingilia kanisani?”
“Ndio upo”


Raisi Mtenzi akashusha pumzi taratibu.


“Ile yule mwana mama nina mfahamu vizuri sana. Hana matatizo na ni mtendaji mzuri sana wa kazi”
“Ni kweli muheshimiwa, ila hili swala muheshimiwa hatupaswi kumuamini mtu yoyote hadi pale tutakapo pata uhakika wa nani ana husika. Isitoshe asubuhi nilishambuliwa mimi, jioni akatekwa Josephine. Huyu mtu anaye tekeleza haya mama atakuwa ni mtu anaye tufahamu kwa undani kabisa na ameweza kutufwatilia nyendo zetu na akajua kabisa kwamba sasa tupo kanisani ndio maana akaamua kutekeleza hilo jambo lake hapo hapo kanisani na kama mtu wa mwisho alikuwa ni yule mama na alimbeba Josephine basi nina weza kumuhoji maswali isitoshe naye usiku wa jana alikuja pale kanisani kuchunguza hilo tukio”
Raisi Mtenzi akakaa kimya kwa sekunde kadhaa huku akiendelea kutafakari nini cha kufanya.


“Mage”
“Ndio muheshimiwa”
“Kumchunguza mpelelezi ni jambo ambalo lina hitaji umakini sana kwa maana na yeye ana mbinu nyingi sana za kumchunguza mtuhumiwa”
“Ni kweli?”
“Kama alikuwa ndio wa mwisho kumbeba Josephine na kumuingiza ndani hapo na akaachwa peke yake na baadae aka rudi kuchunguza jambo hilo hilo na hapakuwa na majibu yoyote mazuri, basi kuna ulanikini, hata mimi nina anza kumshuku kwenye hilo”
“Ume ona ehee?”
“Ndio, nami nina mshuku kwenye hilo jambo. Sasa fanya hivi, japo ni jambo gumu ila tutumie njia hii, endapo kuta uwa na dalili yoyote ya yeye kuhusika na jambo hilo basi tuna weza kupata jibu la uharaka. Ana kijana yake wa mwisho ana mpenda sana ana itwa Mathayo. Ana miaka kumi na mbili ana soma shule ya Fedha Boys. Kwa kumtumia kijana huyo basi tuna weza kujua kama mama yake ana husika kwa jambo hilo au laa”
“Ina maana nimteke mwanaye?”
“Ndio, hii oparesheni nina hitaji uifanye wewe mwenyewe, usimshirikishe mtu zaidi ya sisi wawili. Nita jua jinsi gani ya kukulinda kwenye hilo. Ume nielewa?”
“Ndio muheshimiwa”
“Angalizo yule mwana mama ni hatari sana, ana uwezo wa kila aina katika maswala ya upelelezi hivyo kuwa makini sana”
“Usijali muheshimiwa. Ila nina kuomba nimuazime kijana wako mmoja?”
“Nani?”
“Samson”
Raisi Mtenzi akaka kimya kwa sekunde kadhaa, kisha akakubaliana na ombi la Magreth. Akampigia simu Samson ana akaingia ndani hapo, akashirikishwa mapango mzima walio upanga raisi na Magreth kisha kazi ya kuanza kumfwatilia kijana huyo ikaanza mara moja.


***


“Ume pendeza mke wangu”
Jery alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana, akamtazama mke wake jinsi alivyo valia nguo hizo kwa ajili ya kuingia kazini asuhuhi hiyo.
“Nashukuru mume wangu, vipi ume enjoy?”
“Ndio nime enjoy yaani ume nifanya nijisikie ni kidume. Hakika mke wangu nita kupenda maisha yangu yote na sinto kuacha hata iweje kwa maana ume nitunzia usichana wako ambao toka tukiwa sekondari nilikuwa nina uwinda niupate ila uliweka msimamo. Hakika wewe ni chagua kutoka kwa Mungu wangu”
Jery alimwaga sifa nyingi huku akiwa na furaha kubwa sana.


“Nashukuru mume wangu. Natambua ulikuwa huniamini ndio maana jana uliamua kunikasirikia”
“Ni wivu mke wangu”
“Natambua hilo mume wangu ila una paswa kuniamini na mimi siku moja moja. Siwezi kuw ana mwanaume mwengine tofauti na wewe. Pia hii ninayo ifanya ni kazi hivyo nina paswa kujua kila kitu kinacho endelea hapa ikulu, kumbuka mimi ni msaidizi wa baba yako”
“Usijali hilo mke wangu, sinto kufwatilia kwenye mambo yako ya kazi na mambo ya kwenda Marekani hayato kuwepo”
“Kweli mume wangu”
“Ndio hayato weza kuwepo”
“Basi nina shukuru mume wangu. Acha niwahi ofisini”
“Sawa mke wangu”
Julieth akambusu Jery kwenye lipsi zake kisha akatoka ndani hapo na kuelekea ofisini kwake.


“Za asubuhi bosi”
Shania alimsalimia Jery huku akimtazama jinsi alivyo simama mlangoni kwake akiwa na bukta tu.


“Safi aisee, hivi uliniambia una itwa nani kwa maana jina lako nilisha lisahau”
“Naitwa Shani”
“Ohoo sawa sawa Shani ehee ume amkaje kwanza?”
“Namshukuru Mungu nime amka salama”
Shani alizungumza kwa sauti laini huku macho yake yakiwa yame mlegea, ukiwa ni mtego wake wa kumpata Jery ambaye aliweza kumshuhudia jinsi anavyo mshuhulikia mke wake kitandani.


“Vipi leo macho yako yana nini, una umwa?”
Jery alizungumza huku akimshangaa Shani pasipo kujua kwamba ana yafanya macho hayo kwa ajili ya kumlegezea.


“Yana niuma?”
“Ohoo pole sana, hembu sogea hapa, mimi ni dokta”
Shani akamsogelea Jery ambaye yupo kifua wazi. Garden love iliyo jaa kifuani mwa Jery ikazidi kumpagawisha Shani ambaye muda wote alijikuta akitamani kupata kumbatio kama la jana usiku. Jery akaanza kumtazama tazama Shani macho yake huku akiwa ameyafunua moja baada ya jingine. Shani akausogeza mkono wake karibu na jogoo wa Jery na kumgona kidogo huku akijifanya ni bahati mbaya.


“Ohoo samahani”


“Usijali, ila macho yako hayana tatizo lolote mbona.”
“Ila nina hisi yana niuma”
Shani alizungumza kwa sauti ya kudeka kiasi cha kumfanya Jery aanze kuhisi jambo juu ya msichana huyo ambaye kwa kumtazama tu ni mzuri na ana kila sifa ya kusifiwa kama ni mwana mke mzuri. Jery akamtazama kwa dekunde kadhaa Shani, kisha akamvuta karibu yake na kumkumbatia kwa nguvu na kuanza kumsikilizia mapigo yake ya moyo. Jinsi mapigo ya moyo ya Shani yanavyo kwenda kwa kasi kubwa sana, yakamfanya Jery kuweza kutambua kwamba msichana huyo ana hisia kali sana za kimapenzi.
“Shani”
“Bee”
“Una tamba mimi ni mume wa mtu?”
Swahi la Jery likampa Shani kiguhumizi, akajaribu kujitoa mikoni mwa Jery ila Jery akaikaza mikobo yake na kujikuta akiendelea kugugumia kifuani mwa Jery.


“Nd..io..”
“Una taka kumuibia mke wangu penzi lake”
“Ha…ha…a.ha…p…..a…..n….a bo…s….s…”
Shani alizungumza kwa woga pasipo kujua kwamba Jery ana tabasamu kimoyo moyo. Akamuachia Shani na kumtazama kwa sekunde kadhaa.


“Hatuwezi kufanya mapenzi kwenye kitanda ninacho lala na mke wangu, wala humu ikulu. Nina iheshimu sana nyumba hii eneo. Sasa fanya hivi, kwako ni wapi?”
“Kwangu ni Kimara?”
“Ume panga nyumba nzima?”
“Hapana nina chumba na sebule”
“Sawa, nita kuambia ni wapi uje sawa, ikremishe namba yangu”
Jery akamtajia Shani namba yake ya simu kisha, Shani naye akamtajia Jery namba yake ya simu na Jery akaingia chumbani kwake na Shani akaendelea na majukumu yake ya kawaida huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana moyoni mwake. Jery akajilaza kitandani huku akitafakari mambo mengi sana, akaitafakari ndo yake ambayo ndio kwanza bado ni mpya.


‘Ila huyu demu ni mzuri aisee, siwezi kumukosa’


Jery alijisema kimoyo moyo. Akashuka kitandani, akaingia bafuni na kuaoga kwa haraka, akavaa nguo zake kisha akatoka chumbani hapo na kumkuta Shani,akifuta futa meza ya hapo sebleni, akamsogelea na kumshika kidevu chake, akamtazama macho yake malegevu kisha akaanza kumnyonya lipsi zale kwa sekunde kadhaa na kumfanya Shani ahasi kama mwili wake una nyong’onyea kwa furaha.


“Usimuambie mtu”
Jery mara baada ya kuzungumza hivyo akatoka ndani hapo. Akampigia simu mlinzi wake ambaye alikwa naye kipindi chote toka alipo kuwa masomoni Marekani, japo alipata matatizo kwa kumsaidia bosi wake huyo kwenye maswala ya kutumtumia Evans majambazi ila, hakuacha kuwa mnyenyekevu kwa Jery na siku zote ame kuwa ni mtunza siri mzuri sana wa Jery.


“Niambie Devi”
“Safi kaka”
“Hivi una fahamu dalali ambaye ana weza kunisaidia kutafuta nyumba nzima, eneo ambalo lime tulia na lisilo na mambo mengi kwa siku hii hii ya leo?”
“Ndio madalali wapo wengi sana. Je una hitaji kuhama hapa ikulu?”
“Hapana sihami”
“Ila nyumba ya nini tena kaka?”
“Nahitaji kumpangishia mmoja wa wasichana hapa ikulu nahitaji awe mke wangu wa pembeni”
“Jery Jery Jery ndugu yangu, bado huja acha hizo tabia rafiki yangu. Kumbuka kwamba ume oa tena mwanamke mkali sana, why una taka kuhangaika na wasichana kama ulivyo kuwa Marekani kule”
“Kaka huyu ata kuwa ni mwanamke wangu wa mwisho kabisa”
“Hapana huwezi kumfanyia hivyo mke wako. Kumbuka ni mambo mangapi tuliyafanya juu ya yule manzi, ilibakia kidogo nipoteze ajira yangu. Hembu tulia kwanza achana na huyo manzi”
Jery akaka kimya kwa sekunde kadha huku akimtazama Devi usoni mwake.


“Namuhitaji yule msichana, una nisaidia au hutaki?”
Jery alizungumza kwa jazba kidogo na kumfanya Devi akubali kishingo upande. Wakatafuta dalali mzuri na mwenye sifa nzuri katika utendaji wake wa kazi, wakaona picha jumba moja la gorofa lililopo Mbezi Lous Dar es Salaam.


“Mpigie simu”
“Kaka hii nyumba ni milioni mia sita una taka kuichukua”
“Fanya hivyo Devi, pesa yangu ipo nyingi na haina kazi, acha ninunua hii nyumba”
Devi akafwata maelekezo ya mkuu wake huyo ambaye ana mjua A to Z, na ana mtambu kwamba Jery ni king’ang’anizi na endapo ata amua kufanya jambo lake lolote basi hawezi kusikiliza jambo la mtu ni lazima alitimize kwa wakati anao uhitaji yeye. Dalali huyo aka wahakikishia kwmaba jumba hilo lipo na walicho kifanya ni kuondoka na kueleka lililo hilo. Jumba, wakiwa wawili tu. Wakakutana na dalali na kuanza kulikagua hilo jumba.


“Mwenye hili jamba ni mzungu, muda wake wa kuondoka nchini ume kwishi hivyo ana iuza kwa uharaka sana.”
Dalali alizungumza huku akiwatazama Jery na mlinzi wake huyo.


“Una weza kuwasiliana na muhusika?”
“Ndio”
Dalali huyo akawasiliana na mzungu huyo ambaye baada ya dakika ishirini akafika hapo wakakubaliana na Jery katika kuinunua jumba hilo la kifahari, Jery akafanya malipo kwa njia ya benki na wakaandikishiana na mzungu huyo kisha akakabidhiwa hati za jumba hilo na kuanza hapo akawa ni mmiliki halali wa juma hilo.


“Sasa kaka yule demu akija kuishi kwenye hili jumba nina imani lita mfaa sana. Jambo la kwanza nina mpiga mimba anizali mtoto kabla ya mke wangu ambaye kuna mambo nina hisi kwake”
“Mambo gani?”
“Nina hisia mbaya na mke wangu na nina hisi ana hitaji kutumia ndoa yetu kama daraja la kufanikishia mambo yake na familia yake”
“Mmmm mambo gani hayo kaka?”
“Bado sijayajua, ila kwa sasa nina jifanya ni mjinga kwake, ila nina mpeleleza taratibu endapo nikipata uhakika wa kile ninacho kihisi PUUUUUUU, nita muua”
Devi akastuka sana huku akimtazama Jery usoni mwake kwa maana endapo Jery ana sema jambo la kumuua mtu huwa ana dhamiria kufanya hivyo na sio mtu muoga wa kumuua mtu kwa maana ana roho mbaya na ngumu kumpita hata baba yake japo amepewa sura nzuri, yenye ucheshi na tabasamu la plastiki.


****************************************************************************************************************


****


ITAENDELEA


Haya sasa, Jery ana mpelelezi Julieth na ana amini kwamba ana mambo ana yafanya kwa ajili ya kujinufais
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…