Riwaya: SIN

Riwaya: SIN

SIN 112


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188





ILIPOISHIA


Magreth kwa haraka akafungua mlango wa gari hilo na kuwafanya nabii Sanga na mke wake kupiga makelele ya woga.
“KIMYA”
Sauti nzito ya Magreth ikawafanya nabii Sanga na mke wake kuacha kupiga kelele na kukaa kimya huku haja ndogo ikaanza kumtoka.


“Muna hisi huyu mtu ana weza kupambana na mimi?”
Magrerth alizungumza huku akikirushia kichwa cha Tyson ndani ya gari na kikatua mapajani mwa mrs Sanga mstuko walio upata wa kukiona kichwa cha Tyson ndani ya gari lao kika mfanya mrs Sanga kuzimia kwani hawakutarajia kama Tyson ambaye walikuwa wame mpa kazi hiyo ame uwawa kikatili namna hiyo.





ENDELEA


Nabii Sanga mwili mzima ukazidi kumtetemeka kwa woga. Swali alilio ulizwa hakuweza hata kulijibu, ujanja wote ukamuisha.
“Nimekuuliza una hisi ana weza kuni ua?”
“Ha..h…a…p….ana”
“Nahitaji pesa”
Magreth alizungumza kwa ukali sana na kumfanya nabii Sanga kujibu kwa kutingisha kichwa kwamba ana ingiza kiasi hicho. Nabii Sanga akachukua laptop yake iliyopo siti ya nyuma, akaiwasha na kuingia kwenye tovuti ya moja ya akauti ya benki iliyopo inchini Afrika kusini.


“Kwa kosa kama hili nahitaji dola milioni 25”
Nabii Sanga macho yakamtoka, jasho la woga likazidi kulowanisha mwili wake. Hakika alihisi kwamba hili jambo ni la kawaida sana ila mambo yame kuwa tofauti saba, Nabii Sanga akaanza kujaza fomu ya uhamisho wa pesa kwa njia ya mtandoa. Alipo kamilisha fumo hiyo ambayo ameandika namba ya akaunti inayo onyesha jina la Tomas, akaminya neno lililo andikwa ‘SEND’


Nabii Sanga akaanza kushuhudia jinsi asilimia za uhamishaji wa pesa zinavyo kwenda taratibu taratibu.


“Mage pesa ina aanza kuingia”
Levina alizungumza na kumfanya Magreth kujawa na tabasamu pana usoni mwake, japo nabii Sanga haioni sura yake halisi. Gari moja aina ya defender ililiyo jaza askari kumi ikakatiza kwenye barabara iliyopo eneo hilo la Coco beach. Ila gafla gari hilo likasimama.
“Jamani mume ona lile gari pale?”
Mkuu wa kikosi hicho cha oparesheni alizungumza huku akimuuliza dereva wake.
“Ndio mkuu”
“Usiku huu ina fanya nini?”
“Sijafahamu”
“Heii tuichekini gari hiyo”
Mkuu huyo alizungumza na kumfanya dereva wa gari hiyo kuirudisha nyuma gari hiyo kwa kasi. Kitendo cha gari hiyo kusimama, askari wote waka ruka huku wakiwa na bunduki zao. Magreth aliweza kushuhudia jinsi askari hao wanavyo kuja.
“Zimebaki asilimia ngapi ikamilike?”


Magreth alimuuliza nabii Sanga kwa ukali, nabii Sanga akamgeuzia Magreth laptop na akaona zime baki asilimia thelathini na tano kabla ya pesa hizo kuhama. Magreth taratibu akaanza kuukunjua mnyororo wake ambao kwa mbele una kisu kikali na kinacho kata pande zote mbele.


“Mage uta weza kupambana na hao askari!!?”
Levina aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana kwa maana askari hao wapo wengi.


“Wangapi wapo?”
“Kumi na wana smg mikononi mwao”
“Wana kufa”
“Eheee?”
Magreth akampiga nabii Sanga eneo la shingoni mwake na akazimia. Magreth akaichukua laptop hiyo na kuiweka siti ya nyuma ya gari hilo, ili kama ni zoezi hilo lisiweze kukatishwa na mtu yoyote. Magreth kwa haraka akapanda juu ya gari hilo huku akiwa ameshika mnyororo huo unayo ng’aa hata kama kuna giza. Askari wote wakashangaa kuona mtu wa aina hiyo.


“Ime fika asilimia ya ngapi?”
Magreth alizungumza kwa sauti ya chini.


“Asilimia sabini”
“Poa hakikisha isikatike”
Magreth akachuchumaa huku akiandaa nyota nne huku akiwatazama askari walio tangulia mbele.
“Muna nafasi ya kuondoka eneo hili kabla hamjapata madhara?”
Magreth alizungumza kwa sauti kubwa na kuwafanya askari wanne walio tangulia mbele kusimama kidogo huku wakijiuliza juu ya sauti mbaya na nzito ya mtu huyo.


“Mkuu ume sikia?”
“Ndio nime sikia, sijawahi kuona mtu wa aina hii”
“Moja…..Mbili….”
Magreth alizungumza ili kuwapa onyo askari hao.


“Mage usiue askari, una jua ukiiua askari wata kusaka dunia nzima”
Levina alisiitiza kwani hali ilipo fikia ni lazima askari wafanye mashambulizi kwa Magreth. Mkuu wa kikosi hicho kwa wenge akafyatua risasi moja, iliyo tua kifuani mwa Magreth. Risasi hiyo haikuweka kuingia mwilini mwa Magreth, kitendo hicho kikazidi kuwachanganya na kuwashangaza askari hao.


“Shambulia”
Mkuu wao alizungumza na kuwafanya askari wake kuanza kufyatua risasi kuelekea eneo alipo Magreth. Magreth kwa kasi ya ajabu akaruka sarakasi kadhaa huku akishuak kutoka juu ya gari hio. Magreth akaanza kurusha nyota hizo zilizo anaza kutua kwenye miili ya askari hao. Kila askari aliye kutana na silaha hiyo iliyo kaa kwenye umbo la nyota alianguka chini na mwili wake ukazizima na kushindwa kufanya chochote. Magreth kwa kutumia cheni hiyo akaanza kuwashambulia askari hao huku akiwajeruhu kwa kuwakata baadhi ya sehemu za miili yao kwa kisu hicho. Japo askari wana bunduki ila wakashindwa kabisa kumuhimili Magreth ambaye ana onekana kuwa ni mwiba kwao. Ndani ya dakika mona na sekunde hamsini, askari wote wapo chini wakiugulia maumivu makali sana. Magreth hakuhitaji kuwaua wala kuwapunguza viongo vyao kwani ana tambua jukumu la askari hao ni kulinda raisi. Magreth kwa haraka akarudi kwenye gari la nabii Sanga akaifungua laptop hiyo na kuona zikiwa zime baki asilimia mbili.


Akampapasa nabii Sanga mifukoni mwake na kuichukua simu yake. Akaivunja simu hiyo vipande vipande kisha akavitupia ndani ya gari lao. Ilipo fika asilimia mia mia moja, tiki la kijani lililo ambatana na neno complete, vikaonekana kwenye laptop hiyo. Magreth akaivunja laptop hiyo vipande vipande na kuirushia ndani ya gari la nabii Sanga.


“Waoo zime ingia”
Levina alizungumza kwa furaha sana.


“Salio lipo kweli?”
“Ndio”
“Poa”
Magreth akaanza kuondoka eneo hilo kwa kukimbia. Akafika sehemu alipo iacha pikipiki yake, akapanda na kuondoka eneo hilo.
“Ondokeni eneo hilo na tukutane Morogoro”
“Tuondoke na magari yote”
“Ndio”
“Poa”
Magreth hakuwa na mpango wa kurudi kwenye nyumba hiyo kwani kama ni kazi amesha ikamilisha na kilicho baki ni yeye kutoka nje ya mji huo.


***


“Beba kila kitu”
Levina alizungumza na wakaanza kukusanya kila kitu na Josephine na kuviingiza kwenye gari la Levina. Josephine akaingia kwenye gari la Magreth, akaliwasha na kulitoa ndani hapo. Levina naye akalitoa gari lake na wakazima taa za nyumba nzima, wakafunga geti na kuanza kuondoka kuelekea mkoani Morogoro.


“Mume fikia wapi?”


Magreth aliwauliza wezake.
“Sisi tuna itafuta kibaha”
“Mimi nimesha fika Moro”
“Ume fika?”
Josephine aliuliza kwa mshangao mkubwa sana.
“Ndio nime fika”
“Acha utani bwana Mage”
“Haki ya Mungu, kwani Levina ukiniangalia location yangu una ona nipo wapi?”
Levina akafunua laptop yake na kweli eneo ambalo lina someka alipo Magreth ni Morogoro.
“Hiyo pikikipi ume iendeshaje jamani?”
“Nime izoea tayari ina spidi kubwa sana”
“Je kuna askari njiani?”
“Hapana, barabara ipo nyeupe”
“Poa sasa tuna fikizia wapi?”
“Hoteli ile ile, ila wahini kuna sehemu nina wasubiria nahitaji muni patie nguo”
“Sawa”
Levina na Magreth wakazidi kuongeza mwendo wa magari hayo. Wakafika kwenye msitu mmoja na kusimama, Magreth akatoka ndani ya msitu huo alipo jificha, wakampatia nguo za kwaida, akabadilisha haraka haraka, kisha Magreth akaongoza msafara wa wezake wakiwa na gari hizo. Majira ya saa kumi na moja alfajiri wakafika kwenye hoteli waliyo panga. Wakashuka na kuelekea kwenye chumba chao, hapakuwa na muhudumu aliye wahofia huku wahudumu hao wakiamini kwamba mabinti hao walikwenda disko kama wafanyavyo baadhi ya wateja wao pangisha ndani ya hoteli yao.
“Mage wewe ni mtu wa ajabu sana”
Levina alizungumza huku akiwa amejawa na furaha kubwa sana.
“Kwa nini?”
“Cheki hizi video jinsi ulivyo kuwa una pambana na huyu Tyson. Hembu angalia jinsi ulivyo kuwa una pambana na hawa askari. Yaani your so amaizing”
Levina alizungumza huku akimuonyesha Magreth video hizo. Magreth hata yeye mwenyewe akajishangaa kwani alikuwa ana jichukulia ni mtu wa kaiwada tu, ila kumbe ana uwezo mkubwa namna hiyo.


“Ila Mage wewe huja ogopa kumkata huyo jaa kichwa?”
Josephine aliuliza huku akimtazama Magreth usoni mwake.
“Niogope nini sasa. Endapo ninge muacha ange nidhuru mimi”
“Mmmm ila kwa kweli una ujasiri. Ehee ime kuwaje kwa nabii Sanga na mke wake kwa maana tulikuwa tuna sikia makelele tu”
“Ohoo mrs Sanga alikata moto mara baada ya kumrushia kichwa cha jamaa kwenye mapaja yake.”
Josephine na Levina wakajikuta wakicheka kana kwamba walicho kifanya ni kitu cha kawaida sana.


“Weee”
“Ohoo wee acha tu”
“Naona kuna gari za polisi zime fika Coco”


Levina alizungumza na wote wakaanza kutazama gari nne za polisi zikisimama eneo la Coco beach kwani ndege hiyo isiyo na rubani bado ipo eneo hilo.


***


Kila askari aliye waona wezake wakiwa wame lala chini huku wakiwa wame jeruhiwa maeneo mbalimbali ya miili yao wakajawa na mshangao sana. Wakaanza kuwasaidia wezao na kuwapatia huduma ya kwanza.


“Mzee, mzeee”
Askari mmoja alimuamcha nabii Sanga ambaye yeye na mke wake wote wame zimia. Nabii Sanga aka kurupuka huku akipiga makelele.
“Tulia tulia mzee”
Askari huyo alizungumza huku akimshikilia nabii Sanga. Askari huyo akawaita wezake na wakashangaa kuona kichwa cha mtu kikiwa mapajani mwa mrs Sanga.
“Ime kuwaje mzee?”
“Mmmmm?”
“Ime kuwaje?”
Nabii Sanga akakosa hata cha kujibu.


“Kwa sasa hawezi kuelewa ime kuwaje ana wenge. Kitoeni hicho kichwa hapo”
Askari mmoja alizungumza, mmoja wao akavaa gloves na kukitoa kichwa hicho mapajani mwa mrs Sanga. Mrs Sanga akamtingisha mke wake naye akakurupuka huku akiwa na mawenge.


“Tuna kufa mume wangu tuna kufa.”
Mrs Sanga alizungumza huku akibabaika.


“Hayupo ame ondoka mke wangu”
Nabii Sanga alizungumza huku akimkumbatia mke wake. Mrs Sanga alilia kwa uchungu sana kwa maana hakuwahi kushuhudia tukio la kikatili kama hilo japo kuwa amefanya matukio mengi ya mauaji ila hakuwahi kumkata mtu yoyote kichwa chake. RPC na mlinzi wake wakafika eneo hilo.


“Mume jua ni kitu gani kilicho tokea?”
“Hapana muheshimiwa, ila tume mkuta nabii Sanga na mke wake wakiwa aneo hili”
RPC Karata akashtuka kidogo kwa maana watu hao walipaswa wae majumbani kwao kwa maana leo hii ndio siku ya harusi ya mtoto wao. RPC Karata akatembea hadi kwenye gari la nabii Sanga. Akatazama tairi ya nyuma jinsi ilivyo chomwa na silaha ambayo kwa Tanzania sio maarufu sana kutumiwa na wahalifu.


“Pigeni picha hapa ni ushahidi huu”
RPC Karata alizungumza huku akimuonyesha kijana wake mmoja. Akasimama kwenye mlango wa nabii Sanga. Akawatazama jinsi walivyo kumbatiana na mke wake huku mrs Sanga akilia kama mtoto mdogo.


“Nabii Sanga habari yako?”
RPC Karata alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama nabii Sanga. Taratibu nabii Sanga akamuachia mke wake na kumtazama RPC Karata ambaye kwa sasa hawapatani kabisa.


“Kime wakuta nini waheshimiwa?”


“Karata tusaidie tusaidie baba”
Mrs Sanga alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu na kumfanya RPC Karata kujawa na mshangao kwa maana watu mashuhuri na matajiri kama hao ambao hapo awali walikuwa wana mpa vitisho ime kuwaje leo hii wana muomba msaada tena kwa machozi mengi sana.


ITAENDELEA


Haya sasa, nabii Sanga na mke wake wame zikdi kuchanganyikiwa je RPC Karata ata wasaidia ikiwa watu hao walisha mnyanyasa kwa pesa zao na ukaribu wao na raisi Mtenzi? Usikose sehemu ya 113.
 
SIN 113


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188





ILIPOISHIA


Akasimama kwenye mlango wa nabii Sanga. Akawatazama jinsi walivyo kumbatiana na mke wake huku mrs Sanga akilia kama mtoto mdogo.


“Nabii Sanga habari yako?”
RPC Karata alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama nabii Sanga. Taratibu nabii Sanga akamuachia mke wake na kumtazama RPC Karata ambaye kwa sasa hawapatani kabisa.


“Kime wakuta nini waheshimiwa?”


“Karata tusaidie tusaidie baba”
Mrs Sanga alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu na kumfanya RPC Karata kujawa na mshangao kwa maana watu mashuhuri na matajiri kama hao ambao hapo awali walikuwa wana mpa vitisho ime kuwaje leo hii wana muomba msaada tena kwa machozi mengi sana.





ENDELEA


“Wazee wangu shukeni kwenye gari. Tuelekee kituoni”
Nabii Sanga na mke wake wakashuka kwenye gari huku wakitetemeka kwa woga. Wakatazama damu za askari walio jeruhiwa zikiwa zime tapakaa chini, huku askari hao wakiwa wame wahishwa hospitalini.


“Mkuu tume kuta mwili wa mtu kule juu ya jiwe, tuna imani kwamba mwili huo ndio wa kichwa kike”
Kijana huyo alizungumza na kumfanya nabii Sanga na mke wake kuzidi kuogopa.
“Uchukueni huo mwili na muupeleke hospitali kuu ya taifa”
“Sawa muheshimiwa, ila tume mkuta akiwa na bunduki mbili. Ina onekana ni mdunguaji”
“Sawa pigeni picha kisha muelekee naye mochwari. Hili eneo nahitaji lisafishwe, sinto hitaji wananchi wala waandishi wa bahari wafahamu ni kitu gani ambacho kime tokea.”
“Sawa mkuu”


RPC Karata akwafungulia mlango wa siti za nyuma nabii Sanga na mke wake. Wakaingia ndani ya gari hilo aina ya Toyota land cruiser V8. RPC Karata na dereva wake ambaye ndio mlinzi wake, wakaondoka eneo hilo.


“Tuelekee nyumbani kwa nabii Sanga”
“Sawa muheshimiwa”


RPC Karata akageuka nyuma na kumtazama nabii Sanga na mke wake ambao wame jawa na hofu kubwa sana. Simu ya mrs Sanga aikaanza kuita, akaitazama na kukuta ni Julieth ndio anaye mpigia.


“Pokea simu”
RPC Karata alizungumza huku akimtazama mrs Sanga usoni mwake. Taratibu mrs Sanga akapoke simu hiyo na kuiweka sikioni mwake.


“Haloo”
“Mama mupo wapi jamani. Tume jaribu kuwapigia toka jana mulipo ondoka hampokei simu zenu”
“Tuna kuja”
“Mbona simu ya baba haipatikani”
“Ime zima chaji”
Mrs Sanga aliongopea huku akizungumza kwa sauti ya upole sana.
“Sawa mama wahini si muna jua maandalizi ya harusi yana anza asubuhi hii”
“Ndio”
Mrs Sanga akakata simu. Akajitazama damu zilizo tapakaa kwenye suruali yake ya jinzi aliyo ivaa.
“Jamani naombeni nikatafute nguo nyingine”
Mrs Sanga alizungumza na RPC Karata akakubaliana na jambo hilo. Wakasimama kwenye moja ya dula la nguo.


“Una vaa size gani kiuno?”
RPC Karata alimuuliza mrs Sanga huku akimtazama.
“Kuino arobaini na mbili”
“Sawa”
RPC Karata akashuka kwenye gari lake na kuingia ndukani hapo. Akanunua suruali ya jinzi pamona na tisheti na kurudi navyo kwenye gari. Akamkabidhi mrs Sanga nguo hizo kisha dereva wake akashuka ili wabadilishe nguo.


“Mkuu hivi una hisi ni kitu gani kilicho wapata?”
“Yaani hata mimi sielewi, ilikuwaje na wala sijui kulikuwa na tukio gani pale.”
“Daa una jua ina ogopesha. Askari wote wale hakuna aliye pigwa risasi, ila wame katwa katwa kiasi kwamba sijui ili kuwaje waka shindwa kujitetea”
“Ndio hivyo upelelezi uta tusaidia katika kufahamu ni kitu gani kinacho endelea”


Nabii Sanga akashusha kioo kidogo.
“Tayari ame maliza”
Mara baada ya nabii Sanga kuzungumza hivyo. RPC Karata na kijana wake wakaingia ndani ya gari hilo na kuendelea na safari hiyo. Wakafika nyumbani kwa nabii Sanga na kukuta watu wakiwa katika heka heka za maandalizi ya harusi hiyo.


“Mzee tuna weza kuzungumza”
RPC Karaka alizungumza huku akimtazama nabii Sanga. Wakashuka kwenye gari na kukaa kwenye moja ya kibanda cha kupumzikia.
“Ehee mzee niambie ni kitu gani kimetokea?”
Nabii Sanga akashusha pumzi taratibu huku akimtazama RPC Karata.
“Akili yangu kwa sasa haipo sawa. Una weza kunipa muda na hayo maswali uka nihoji baadae”
“Ila mzee kumbuka wewe na mke wako mume kutwa eneo la tukio na mbaya zaidi mume kutwa na kichwa cha marehemu ndani ya gari lenu”
Julieth akafika eneo hilo, akamsalimia baba yake kisha akamsalimia RPC Karata.
“Baba raisi ana kupigia simu yako haipo hewani”
“Ime zima chaji”
“Ngoja nimpigie kwangu ana hitaji kuzungumza nawe.”
Julieth alizungumza na akampigia raisi Mtenzi. Simu ikapokelewa.
“Baba mkumkwe mzee huyu hapa”
Julieth alizungumza kisha akampatia baba yake simu.
“Ndio muheshimiwa”
“Habari za asubuhi ndugu yangu”
“Salama tu muheshimiwa”
“Ratiba ya kufungisha ndoa kanisani ime badilika. Nilizungumza na mchungaji na ame tuambia saa sita mchana ibada ifanyike, Hivyo nina omba muweze kujiandaa kwa hilo na muwapatie taarifa ndugu na jamaa mbao walijiandaa kwa ajili ya saa tisa alasifi”
“Sawa ndugu yangu nime kuelewa”
“Ila samahani bwana kwa kutengua ratiba”
“Hakuna tabu ndugu yangu kwa maana ripoti ime kuja asubuhi basi nina weza kuwasiliana na watu na wakafahamu hilo”
“Nashukuru sana kwa kunielewa ndugu yangu”
“Sawa sawa”
Nabii Sanga akakata simu na kumrudishia Julieth.


“Naamini ume ambiwa muda wa harusi ni saa ngapi?”
“Saa tisa au?”
“Ni saa sita. Waambie na watu wengine sawa”
“Sawa baba”
Julieth akaondoka eneo hilo huku akiwa na furaha sana moyoni mwake.


“Naamini kwamba ume ona ratiba ime badilika hivyo nakuomba niweze kujianda akwa ajli ya shuhuli ya mwangu”
“Sawa, je una weza kuniambia aliye sababisha mauaji yale na kuwajeruhia askari wangu yupo vipi?”
“Sio mtu wa kawaida. Mtu ambaye mwili wake haingizi risasi ana zungumza sauti mbaya. Basi sio mtu wa kaiwada. Nahisi mke wangu ata kuwa hayupo sawa, acha nika ungumze naye. Nitafute kesho akili yangu ikiwa ime tulia”
Nabii Sanga alizungumza kwa sauti ya upole sana huku akimtazama RPC Karata usoni mwake. RPC Karata akamtazama nabii Sanga kwa sekunde kadhaa kisha akatingisha kichwa kwamba ame mkubalia.
“Hakikisha una wasiliana na mimi pale utakapo ona jambo la tofauti”
“Sawa”
Nabii Sanga akanyanyuka kwenye kiti na kuelekea chumbani kwake. Akasikia maji yakiwa yana mwagika bafuni, akafungua mlango na kumkuta mke wake akiwa amekaa kwenye sakafu huku maji ya mbomba la mvua yakimwagikia mwilini mwake. Taratibu nabii Sanga na yeye akakaa pembeni ya mke wake na kumkumbatia.
“Sijawahi kukutana na tukio la ajabu maishani mwangu kama hili”
Mrs Sanga alizungumza kwa sauti ya upole sana.
“Hata mimi, nime shindwa kumfahamu mtu huyo ni wa aina gani”


“Ila niliona ukimpiga risasi, kwa nini hakufa?”
“Hilo ndio swali ninalo jiuliza na wanavyo dai ni kwamba hata askari wenyewe wame shambuliwa kiasi cha lile eneo kujaa damu”
“Mmmmm sasa ina kuwaje mume wangu kama akirudi tena?”
“Hilo ni jambo gumu. Ila ngoja tuangalie itatavyo kuwa, ila kwa sasa ina bidi tubadilishe namba zetu za simu. Sawa”
“Sawa mume wangu”
“Jiandae muda wa harusi ume badilika. Sio saa tisa tena ni saa sita”
“Kwa nini?”
“Sijamuuliza muheshimiwa, ila kutokana wao ndio wenye harusi wana mamlaka ya kuzungumza chochote wanacho jisikia. Sisi tuta fwata”
“Sawa yaani nikikumbua kile kichwa cha yule kijana. Yaani mwili wangu una ishiwa nguvu kabisa”
“Usiwe hivyo, jikaze mke wangu”
“Mmmmm”
“Ndio jikaze mke wangu. Polisi nina imani kwamba wata kuwa wana tufwatilia ila tuwe na kauli moja. Wakituhoji tuwaeleze kwamba tulipigiwa simu ya mtu asiye julikana. Alitupa vitisho vya kutuvamia kwenye harusi ya binti yetu na alihitaji kiasi cha pesa cha milioni hamsini za kitanzania. Hivyo muda huo tulikuwa tume kwenda kuonana naye. Sawa”
“Mmmm hilo mume wangu lita tupeleka mbali sana. Tuwaambie hivi polisi, tulikuwa tuna toka kwenye hoteli yetu. Njiani tuliweza kutekwa na watu wasio julikana, wakatupeleka pale Coco na wakataka kutua.”
“Hilo nalo halijaa vizuri. Jambo la msingi tusubirie akili zetu zikae sawa kisha tuta jua nini cha kufanya”
”Sawa”
Nabii Sanga akamvua mke wake nguo kisha na yeye akavua nguo zake na wakaanza kuoga kwa pamoja.


***


“Muheshimiwa raisi tukio hizi ndio picha za tukio lililo tokea Coco beach”
RPC Karata alizungumza huku akiweka picha hizo za askari wake kujeruhiwa na maiti ya mtu mmoja aliye katwa picha. Raisi Mtenzi akaanza kutazama picha moja baada ya nyingine.


“Hizi star si zina tumiwa na manija wa Kijapani?”
“Ndio muheshimiwa. Ndio muheshimiwa na tume jaribu kufanya mahojiano na askari wetu walio jeruhiwa na waka dai kwamba mtu aliye wavamia kwanza ana sauti mbaya nzito mithili ya radi na tatu mtu huyo haja mwili wake hauingii risasi”
“Mwili wake hauingii risasi?”
“Ndio, vijana wetu walimshambulia kwa risasi za kutosha, ila uwezi amini muheshimiwa kitu walicho kutana nacho ndio hichi”
“Mmmmm!!”
Raisi Mtenzi aliguna huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana usoni mwake.
“Je wame sema mtu hiyo ana tumia silaha gani tofauti na hizi nyota”
“Ana tumia mnyororo ambao kwa mbele una kisi kikali sana. Kiufupi huyu mtu ni muhalifu mpya Tanzania na ana uwezo mkubwa sana kwani kupambana na askari zaidi ya kumi tena wakiwa na silaha sio jambo rahisi muheshimi”
“Ni kweli. Je hii habari ime wafikiwa waandishi wa habari?”
“Hapana haija wafikia kwani niliwaeleza vijana waweze kufuta kila kitu kilicho tokea, ili waandishi wa habari wasije waka leta hofu kwa watu wa jiji letu”
“Ni kweli, hapo ume fanya jambo la maana. Sasa hakikisheni kwamba mtu huyu ana sakwa na akipatikana nahitaji nimshuhudie kwa macho yangu”
“Sawa muheshimiwa”
“Hili gari ni la nani?”
Raisi Mtenzi aliuliza huku akitazama picha ya gari la nabii Sanga.
“Hilo gari mkuu ni la wakwe wezako na wao tuliwakuta eneo la tukio wakiwa wame zimia”
Raisi Mtenzi alishangaa.
“Wamezimia?”
“Ndio tena na mbaya zaidi, maiti ya mtu huyu aliye katwa kichwa. Kichwa chake kilikuwa kimetupiwa mapajani mwa mrs Sanga.”
“Ohoo Mungu wangu. Una taka kuniambia mtu huyu aliwateka?”
“Kitu kama hicho, nime jaribu kuzungumza nao, kidogo wana onekana kwamba hawapo sawa hivyo nime waacha harusi hii ipite kisha tuta kaa nao chini na kuzungumza. Pia kwenye gari lao tume kuta laptop ikiwa ime funjwa, simu ya mzee ikiwa ime vunjwa na bastola ya mzee ikiwa ime tumika risasi moja. Tairi zikiwa zime chomwakwa hizi star”
“Ila wao ni wazima na hawajeruhiwa?”
“Yaa ni wazima hakuna mwenye jeraha mwilini mwake na hali tuliyo ikuta ni wao kuzimia”
“Mmmm kwa mtazomo wako wana weza kusherekea hii harusi kwa furaha?”
“Naamini wana weza”
“Sawa Karata, hakikisha kwamba ulinzi una kuwa ni imara, nikipata muda nita watembelea vijana wako walio jeruhiwa”
“Sawa muheshimiwa”
RPC Karata akatoka ofisini kwake. Akaingia kwenye gari lake huku akitafakari ni kitu mtu wa aina gani ambaye ana weza kufanya mashambulizi kama hayo. Akampigia simu Magreth na ikapokelewa.


“Mage habari yako”
“Salama muheshimiwa”
“Tuna weza kuonana?”
“Lini?”
“Muda huu?”
“Hapana muheshimiwa kwa maana nipo nje ya mkoa wa Dar es Salaam. Vipi kwema?”
“Sio kwema. Adui zako jana usiku walivamiwa na mtu wa ajabu aisee. Ila haya mazungumzo sio mazuri kuzungumzia kwenye simu. Ni heri tukutane na kuzungumza kwa kina”
“Usijali, ila nina jambo moja nahitaji kukueleza kabla ya kukutana”
“Jambo gani?”
“Kama mke wako na familia yako ipo bado jiji la Dar es Salaam nina kuomba uweze kuwahamisha na uwaondoke kabisa ndani ya jiji la Dar”
“Kwa nini?”
RPC Karata alizungumza kwa mshangao wa hali ya juu.
“Al-Shab wana vamia jiji la Dar saa tisa alasiri. Nime kuambia kama kaka yangu ambaye nina penda kukuona una ishi maisha marefu. Tafadhali nina kuomba unisikilize na kuniamini”
RPC Karata akaka kimya kwa muda kidogo huku akianza kujiuliza ni kwa nini muda wa harusi ya mtoto wa raisi Mtenzi ime badilishwa kutoka saa tisa alasiri na kuwa saa sita mchana.


‘Ina maana raisi ana jua hili ndio maana ame badilisha na haja nifahamisha’


RPC Karata alijiuliza kimoyo moyo huku akitazama jengo hilo la ikulu. Taswira ya mke wake ika mjia usoni mwake na kujikuta akimuamrisha mlinzi wake kuwasha gari na kuelekea nyumbani kwake kuhakikisha ana ondoka na familia yake, kama majanga yakitokea, basi asiwepo ndani ya jiji hilo la Dar es Salaam lililo pangwa kuvamiwa.


ITAENDELEA


Haya sasa, RPC Mtenzi ame gundua siri hiyo ambayo ni viongozi wacache tu wa juu walio elezwa kuhusiana na siri hiyo je ata waagiza vijana wake kuimarisha ulinzi? Usikose sehemu ya 114.
 
SIN 114


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188






ILIPOISHIA


“Al-Shab wana vamia jiji la Dar saa tisa alasiri. Nime kuambia kama kaka yangu ambaye nina penda kukuona una ishi maisha marefu. Tafadhali nina kuomba unisikilize na kuniamini”
RPC Karata akaka kimya kwa muda kidogo huku akianza kujiuliza ni kwa nini muda wa harusi ya mtoto wa raisi Mtenzi ime badilishwa kutoka saa tisa alasiri na kuwa saa sita mchana.


‘Ina maana raisi ana jua hili ndio maana ame badilisha na haja nifahamisha’


RPC Karata alijiuliza kimoyo moyo huku akitazama jengo hilo la ikulu. Taswira ya mke wake ika mjia usoni mwake na kujikuta akimuamrisha mlinzi wake kuwasha gari na kuelekea nyumbani kwake kuhakikisha ana ondoka na familia yake, kama majanga yakitokea, basi asiwepo ndani ya jiji hilo la Dar es Salaam lililo pangwa kuvamiwa.





ENDELEA


“Halooo”
Magreth alizugumza mara baada ya kusikia ukimya wa dakika moja.
“Ndio Mage”
“Ume nielewa?”
“Ndio nime kuelewa. Nashukuru kwa taarifa”
“Asante”
RPC Karata akakata simu na kumuhimiza dereva wake wawahi kuelekea nyumbani kwake. Ndani ya dakika arobaini na tano wakafika nyumbani kwa RPC Karata.
“Nisikilize Basesa kama una ndugu yako au rafiki yako na mademu zako. Waambie waondoke jiji la Dar es Salaam sasa hivi Umenielewa”
RPC Karata alizungumza huku akimtazama mlinzi wake huyo ambaye pia ni dereva wake.
“Kuna nini muheshimiwa?”
“Dar es Salaam ifikapo saa tisa ita shambuliwa na Al-Shabab hatujui wata shambulia kwa anga au kujitoa muhanga ila ni lazima wata shambulia. Ndio maana jana iliendeshwa oparesheni ya kusaka mabomu na maumbwa. Mbaya zaidi niliagizwa tu vijanawafanye kazi ila hatukuambiwa sababu ya kitu gani kinacho endelea. Ume nielewa?”
“Ndio mkuu”
“Chukua gari yangu ile nyeusi na ondoka nayo. Tukutane Morogoro”
“Sawa mkuu”
RPC Karata akaingia ndani na kumkuta mke wake akiwa jikoni akiandaa chakula cha mchana.
“Mke wangu acha kupika na ninahitaji ukusanye nguo, pesa na watoto wapo wapi? Tuna ondoka ndani ya jiji la Dar es Salaam”


“Kuna nini mume wangu?”
“Al-Shabab wana kwenda kushambulia jiji hili. Hivyo nahitaji wewe na wanangu muwe nje ya jiji hili. Umenielewa”
RPC Karata alizunguma kwa akimtazama mke wake usoni kwa msisitizo.
“Sawa, watoto wapo wana cheza huko uwani”
“Kawaite”
Mrs Karata akazima jiko hilo la gesi na kukimbilia eneo la nyumba hiyo ambapo kuna uwanja mdogo wa mpira. RPC Karata, akafungua shelf yake akatoa vibunda vya pesa kisha akatoa na bastola yake ambayo ina kaa nyumbani hapo. Mke wake akaingia ndani hapo akiwa na watoto wake wawili.
“Waandae haraka haraka”
Mrs Karata akaanza kuwaandaa waneye huku RPC Karata akihakikisha ana kusanya nguo zao watakazo zitumia wakiwa nje ya mkoa. Wakaingiza mizigo kwenye gari hilo la serikali na kuanza kuondoka Mkoa Dar Es Salaam na kuelekea mkoani Tanga.
***


“Jamani bado tu bibi harusi hajamaliziwa kupambwa?”
Nabii Sanga alizungumza huku akiwa amesimama mlangoni mwa chumba cha Julieth.
“Tuna mmalizia baba”
Mpambaji alizungumza, nabii Sanga akamtazama mwanaye jinsi alivyo mrembo na akajikuta akitabasamu. Maandalizi yote ya kumuandaa bi harusi yakakamiika. Bi harusi na wana familia wote wakaingia kwenye gari za kifahari zipatazo ishirini na kuondoka nyumbani hapo. Mrs Sanga akamshika mkono mume wake huku wakiwa wame kaa siti ya nyuma kwenye gari lao aina ya Range Rover Sport.


“Vipi mbona kama una wasiwasi?”
Nabii Sanga alimuuliza mke wake huku akimtazama usoni.


“Yaani nina kumbuka yale ya usiku, kila nikifumba macho nakiona kile kichwa”
“Usijali mke wangu, yata kishwa na hii harusi ikiisha nita hakikisha kwamba nina imarisha ulinzi kwa familia yangu na hapato kuwa na mtu ambaye ana weza kutu gusa”
“Sawa mume wangu”
Julieth akaifungua picha aliyo tumiwa na Jery. Akaanza kuitazama huku akiwa amejawa na furaha kwani ni picha inayo muonyesha akiwa ame valia suti yake.


‘Nitumie basi na wewe picha yako mke wangu’


Julieth aliisoma meseji hiyo huku akiwa amejawa na tabasamu.


‘Sikutumii uta niona kanisani’


‘Mmm acha hizo mke wangu, nitumie bwana’


‘Kweli vile sikutumia. Vipi mume sha toka ikulu?’


‘Ndio tuna jiandaa si una jua raisi kutoka kwake ni kwa maandalizi’
‘Ni kweli, sisi ndio tupo njiani kuelekea kanisani’
‘Sawa mke wangu nita kukuta huko. Natamani nikuone sema ndio hivyo ume nibania’


‘Usijali mume wangu uta niona tu na nitakuwa wako milele na milele’


Nafurahi kusikia hivyo, nina kupenda sane mke wangu’


Julieth akafurahi sana kuziona meseji hizo. Wakafika kanisani na bi harusi moja kwa moja akeleekea katika ofisi ya mchungaji akiwa na waziazi wake, kuwasubiria wakwe zao kufika..


***


Ulinzi wa barabarani ulipo kamilishwa. Raisi Mtenzi na wana familia yake wakaanza kuondoka ikulu. Waandishi wa habari nao hawakucheza mbali juu ya kurusha matangazo yao ya moyo kwa moja kwenye vituo vyao vya televishion. Wananchi wengi walishangazwa juu ya linado;ola lwa ratiba ya harusi hiyo.


“Jery mwanangu una kwenda kuoa. Jana sikupata muda wa kuzungumza na wewe”
Mrs Mtenzi alizungumza huku akiwa ana mtazama Jery usoni.


“Nina kuomba sana mwanangu ukawe ni kielelezo cha maisha ambayo tulikulea mimi na baba yako. Una muona baba yako, nilikuwa naye toka yupo askari wa kawaida. Ila leo hii ame kuwa ni raisi, kwenye ngazi zote za vyeo nilipanda naye. Una weza kugundua nguvu ya mwanamke kwa mwanaume. Laiti kama baba yako angekuwa ni mtu wa starehe kama wanaume wengine basi leo hii nina imani hata yale maombi yangu ya kufunga na kuomba kwa ajili yake yasinge fanya kazi”
Raisi Mtenzi akatabasamu tu huku wakiendelea kumsikiliza mke wake kwa umakini.
“Najua nyinyi nyote mume toka kwenye familia za kitajiri. Wotte muna ujua utajiri, isitokee mmoja wenu akajigamba kisa pesa za wazazi wake, hakuto kuwa na ndoa”
“Hili mama halito weza tokea”


“Nami nina ombea lisije likatoka. Pili hakikisha muwe muna chukuliana mapungufu. Ifikie hatua kila mmoja awe ana weza kujishusha kwa mwenzake. Wewe ukikosea, usisite kumuomba mke wako msamaha, hivyo hivyo na yeye akikosea asisite kukuomba msamaha. Mukiyamuda hayo, nina imani mwanangu uta fanikiwa zaidi ya haya mafanikio tulio kuwa nayo sisi wazazi wako”
“Nashukuru mama kwa nasaha zako nzuri”
“Jery sisi wawili tulisha malizana jana usiku”
“Ndio baba”
“Basi ukiyashika maneno yetu tuliyo kueleza basi nina kuhakikishia kwamba uta kuwa na ndoa yenye furaha na mfano kwa watu wengine”
“Asanteni sana wazazi wangu”
Wakafika kanisani, ulinzi ukaendelea kuimarishwa. Wakashuka kwenye gari hilo na moja kwa moja wakaelekea ofisini kwa mchungaji na kuwakuta wakwe wezao pamoja na mkwe woa. Wakasalimiana kwa furaha kisha wazazi waka omba kutoka nje ili kuwapisha wana ndoa wakiwa na mchungaji.
“Utaratibu wetu wa kanisa, huwa tuna wauliza wana ndoa kabla ya kufika pale madhabauni. Je kuna mtu yoyote kati yenu ambaye ame lazimishwa kuingia kwenye ndoa hii?”
“Hapana”
“Hapana”


“Je kuna mmoja kati yenu ambaye amewahi kuzini huku nyuma au muliwahi kuzini?”
“Hapana”
“Hapana mchungaji”
Julieth alijibu kwa kujikaza tu ila ukwelia na ufahamu kwani hata hiyo bikra aliyo kuwa nayo hivi sasa ni ya bandia.
“Sawa je muna penda na kweli au mume kuwa kwenye mahusiano kwa ajili ya matamanio ya kihisia?”
“Nina mpenda sana mume wangu”
“Bwana harusi”
“Hata mimi nina mpenda sana mke wangu kwani nilikuwa naye kwa kipindi cha mahusiano toka tulipo kuwa tuna soma na niliweza kumsubiria na kumvumilia hadi sasa tuna kwenda kufunga ndoa”
“Nafurahi kusikia hivyo na nina shukuru kwa wote kuwa wavumilivu. Leteni mikono yenu niwaombee”
Wakamkabidhi mchungaji mikono yao ya upande wa kulia na akaanza kuwaombe taratibu. Sala ilipo malizika akawaachia mikono.
“Sasa ni wakati wa kuelekea kwenye ibada”
Julieth na Jery wakanyanyuka. Jery akamtazama mke wake kuanzia chini hadi juu, uzuri wa Julieth ume zidi kuongezeka mara dufu. Mchungaji akatanguli mbele kutoka ofisini hapo na wao wakamfwata kwa nyuma huku wakijumuika na wasimmizi wao wa kike na wakiume.


***


“Shitii tume pigwa chenga ya mwili”
Omary alizungumza huku akiwasa tv iliyopo chumbani hapo. Vijana wote wa Al-Shabab wakashuhudia jinsi harusi ya mtoto wa raisi ikiendelea kanisani.


“Sasa tuna fanyaje mkuu ikiwa mabomu yote tuliyo yagega kwenye simu yana lipuka saa tisa kamili alasiri”
Omary akatazama saa yake ya mkononi na ina muonyesha ni saa saba na dakika moja.


“Yamebaki masaa mawili kabla ya kufika saa tisa, hatuwezi kuzikusanya simu zote na kufanya mashambulizi”
“Sasa ita kuwaje?”
“Saa tisa hiyo hiyo tuta fanya mashambulizi, haijalishi ni nani ata kufa ila ni lazima tufanye mashambulizi”
“Ni muda wa sisi kuondoka na kusambaa kila eneo la jiji la Dar es Salaam sawa”
“Sawa mkuu”
“Tuta toka moja mmoja”


Omary alizungumza kwa msisitizo na wakaanza kutoka kijana mmoja baada mwengime. Omary akawa wa mwisho kutoka eneo hilo. Akakodisha pikipiki na kuomba impelekea kwenye kanisa inapo fungishwa ndoa ya mmtoto wa raisi.


Muendesha pikipiki akmtazama Omary kwa sekunde kadhaa kisha akamruhusu apande. Wakaondoka na kufika karibu kabisa na kanisa hilo.
“Dogo ulinzi ume imarishwa hapo. Wewe shuka utembee kwa miguu”
“Sawa”
Omary akalipa kiasi alicho kubaliana naye, kisha dereva huyo akaondoka. Omary akaungana na wana nchi wengien kuingia kanisani hapo. Aka kaa kwenye benchi la mwisho huku akishuhudia ibada hiyo jinsi inavyo endelea.


Omary akaendelea kutazama jinsi ulinzi ulivyo imarishwa ndani ya kanisa hilo. Muda wa maharusi kula kiapo cha kuishi milele ikawadia. Akaanza Jery kiapo cha kumpokea Julieth kuwa mke wake hadi kifo kitakapo watengenisha kisha akamvisha pete. Julieth naya alaka kiapo hicho na akamvisha pete mume wake. Shangwe zikazidi kutawala ndani ya kanisa hilo huku wazazi na ndugu wa pande zote wakiwa wamejawa na furaha.


***


“Josephine hivi hao Al-Shabab watavamia au maono ni ya siku nyingine?”
Levina aliuliza huku akimtazama Josephine usoni mwake.
“Kwani saa tisa imesha fika?”
“Bado”
“Subiri uone”
“Naona harusi ina kwenda kwisha na ndio tayari wamesha kuwa mume na mke”
“Jery kumuona Julieth hilo mimi sikuonyeshwa, nilicho onyeshwa ni Dar es Salaam kulipuka”
“Levima una onekana una hamu sana ya kushuhudia maono ya Josephine ehee?”
“Ndio nina hamu ya kuona kama alicho kizungumz ani kweli au laa”
“Usijali, uta ona”
Wakaendelea kutazama matangazo hayo ya kurushwa moja kwa moja kwenye tv. Maharusi wakaelekea kwenye hoteli moja ya hadthi tano kwa ajili ua mapumziko kabla ya kuelekea ukumbini. Josephine akatazaama saa yake ya mkononi na ina onyesha ni saa tisa kasoro ishirini.
“Ehee Mungu wangu!!!”
Josephine alihamaki.
“Kuna nini?”
“Zime baki dakika ishirini kabla ya kile jambo kukamilika”
“Acha likamilieke tu, sisi si tupo mbali”
Levina alizungumza kana kwamba kitu kinacho kwenda kutokea ni cha kawaida kabisa.


“Levina kumbuka kuna watoto na wana wake ambao wana kwenda kufa pasipo hatia ya aina yoyote”


Josephine alizungumza kwa msisitizo huku machozi yakimlenge lenga usoni mwake. Magreth akashusha pumzi na kumuona jinsi rafiki yake anavyo pata maumivu ya moyo. Josephine akaanza kusali na kumuomba Mungu kama ikiwezekana basi kisasi hicho cha Al-Shabab aweze kukiepusha kwenye ardhi ya Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.


ITAENDELEA


Haya sasa, Josephine ana jitahidi kuomba je maombi yake yata fanikiwa kuepusha balaa lililopo mbele yao? Usikose sehemu ya 115.
 
SIN 115


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188







ILIPOISHIA


“Ehee Mungu wangu!!!”
Josephine alihamaki.
“Kuna nini?”
“Zime baki dakika ishirini kabla ya kile jambo kukamilika”
“Acha likamilieke tu, sisi si tupo mbali”
Levina alizungumza kana kwamba kitu kinacho kwenda kutokea ni cha kawaida kabisa.


“Levina kumbuka kuna watoto na wana wake ambao wana kwenda kufa pasipo hatia ya aina yoyote”


Josephine alizungumza kwa msisitizo huku machozi yakimlenge lenga usoni mwake. Magreth akashusha pumzi na kumuona jinsi rafiki yake anavyo pata maumivu ya moyo. Josephine akaanza kusali na kumuomba Mungu kama ikiwezekana basi kisasi hicho cha Al-Shabab aweze kukiepusha kwenye ardhi ya Dar es Salaam na Tanzania kwa ujumla.





ENDELEA


Gafla Josephine akaanza kuhisi kizungu zungu, akajaribu kusimama ila akastukia akiaanguka chini na akazimia. Magreth na Levina wakajikuta wakishangaa sana kwani hali kama hiyo hawajawahi kumuona nayo Josephine. Wakamnnyanyua kwa haraka na kumlaza kitandani, wakafungua vifungo vya shati lake pamoja na suruali ailiyo ivaa.
“Amezimia hiyu”
Levina alizungumza huku akiwa ana mpima Josephine mapigo yake ya moyo.
“Vipi tumpelekea hospitali?”
“Hapana ata kaa sawa tu”
Levina alizungumza kwa kujiamini kwa maana ana ujuzi kidogo kwenye maswala ya udaktari kwani marehemu mama yeke elikuwa ni dokta.


***


Omary hakucheza mbali sana na hoteli ambayo maharusi na familia zao wamekusanyika eneo hilo. Wapambe pamoja na waandishi wa habari nao pia wapo hotelini hapo kuhakikisha wana shuhudia kila kinacho endelea katika sherehe hiyo. Omary akaitazama saa yake ya mkononi na ima bakisha dakika tano kabla ya mambo waliyo tatege kwenye simu zaina za Nokia, kulipuka.
“Hii hoteli ni nzuri sana”
Julieth alizungumza huku akitazama tazama eneo la hoteli hiyo.


“Baba aliichagua hoteli hii kw amaana ni mpya na pia upo pazuri sana”
“Hei baby una jua ni watu wengi wapo nje wana tusubiria. Njoo uone”
Jery akasogea dirishani hapo na kutazama nje, akaona jinsi watu walivyo kusanyika wakiwa wana wasubiria japo wawaone tu kwa macho.
“Harusi yetu ime weka historia Tanzania”
“Ni kweli ime weka historia.”
“Mke wangu una weza kunipa kidogo?”
“No baby acha totoke ukumbini, nitakupa hadi uchoke mwenyewe. Tambua zime baki dakika mbili tu tuelekee eneo la kupiga picha”


Mlango wa chumba chao uka gongwa. Jery akatembea hadi mlangoni na kuufungua.
“Baba”
“Ahaa nina weza kuingia?”
“Ndio”
Raisi Mtenzi akaingia ndani hapo.


“Nina imani mume pumzika vya kutosha?”
“Ndio baba”
“Basi twendeni kuna viongozi nina hitaji kuwatambulisha kwao”
Jery akamshika mkono Julieth kisha wakatoka chumbani hapo. Wakaingia ndani ya lifti wakiwa na walinzi wao wawili. Galfa mtikisiko mkubwa ukatokea katika jengo hilo, umeme uka katika na kusababisha hofo kubwa kwa raisi Mtenzi pamoja watu wote.


Mlipuko mkubwa ulio tokea eneo alilo kuwa amesimama Omary na kumgawanyisha vipande vipande, ukawadhuru watu wote walipo eneo hilo. Magari na kila kitu kilichopo eneo hilo kiliweza kulipuka vibaya sana. Maeneo mbali mbali ndani ya jiji la Dar es Salaam ambapo zilitupwa simu na maeneo ambayo vijana hao wa Al-Shabab walisambaa maeneo yote yalilipuka kwa mabomu hayo ambayo ni makubwa sana. Vilio vilizidi kutanda na kutawala maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam. Majengo mengi yalivunjika mithili ya biskuti zinavyo vunjwa vunjwa. Hapakuwa na eneo la kukimbilia kwani milipuko hiyo ni mikubwa sana na ime dhuru eneo kubwa sana.
***


Mzee Mbogo na vijana wake wote macho yamewatoka. Kila mmoja alihisi kwamba habari za mashambulizo hizo ni propaganda tu katika mitandoa ya kijamii. Wengi wao machozi yalianza kuwamwagika, video inayo rekodiwa na satelati, ina onyesha milipuko mbalimbali jinsi inavyo tokea ndani ya jiji la Dar es Salaam.


“Mkuu”
John alimuuita Mzee Mbogo huku akimtazama usoni mwake.
“Mmmm”
“Hali ime tokea kama hivyo. Tuna fanyaje?”
“Hatuna la kufanya ila kusema katika hili”
Mzee Mbogo akaondoka ndani hapo na kuingia chumbani kwake. Kila akifumba macho ana ona jinsi milipuko hiyo ikiendelea kulipuka katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam. Mzee Mbogo akatoa simu yake, akaitafuta namba ya Evans, akaitazama kwa sekunde kadhaa kisha akampigia. Simu ya Evans ikapokelewa.
“Kijana”
Mzee Mbogo alizungumza kwa sauti ya upole na iliyo jaa unyonge ndani yake.
“Ndio muheshimiwa”
“Wewe ni nani?”
“Kivipi mzee wangu mbona sija kuelewa?”
“Ulijuaje kama Al-Shabab wata shambulia leo?”
“Kama nilivyo kuambia nilipewa maono na Mungu ndio maana niliweza kukupa habari hiyo. Niliyo yazungumza yame timia”
“Malaki wa watu wame teketea na moto ndani ya jiji la Dar es Salaam, kwa nini hii habari hukuizungumza toka wiki iliyo pita ili hili janga lisiangamize watu wengi”
“Mzee wangu ilipaswa kutokaa hivi ili raisin aye aweze kujifunza. Kazi yangu mimi ni kutabiri tu na siwezi kuzia mambo kama hayo kutokea”
“Nahitaji kuonana na wewe. Niambie upo wapi?”
“Nita kufwata wewe ulipo ila usije nilipo.”
“Sawa nipo Morogoro”
“Natambua upo shambani kwako”
“Ume juaje?”
“Mungu akiwa na uwezo wa kumfunilia mtumishi wake basi ana uwezo wa kuona hata yaliyo jificha. Kama nina uwezo wa kuwaona mizimu, vibwengo ma majini basi nina weza kukuona hata wewe”
“Sawa nina kusubiria”
Mzee Mbogo akakata simu huku akiwa na huzuni kubwa sana. Kwenye maisha yake yote aliyo wahi kuishi duniani hajawahi kuona shambulizi kama hilo na baadhi ya mashambulizi ambayo kidogo yana endana na hilo, aliyashuhudia Iraq kipindi alipo kuwa chini ya jeshi la umoja wa mataifa, UN.


***


“Sasa ni wakati wa wewe jina lako kukua na huduma yako pia kukua”
Jini Maimuna alizungumza huku akimtazama Evans usoni mwake.


“Nini nina paswa kufanya?”
“Una paswa kupona wagonjwa, una paswa kutoa misaada kwa watu na una paswa kuanzisha taasisi yako ambayo ita tambulika kitafita na uta wajengea watu wote nyumba zao zilizo bomoka. Ukifanya hivyo uta pata wafuasi wengi na wata kusujudia na hato kuwa Evans huyu wa sasa, bali uta kuwa ni Evans mwenye nguvu na mamlaka hata ndani ya serikali”
Jini Maimuna alizungumza msisitizo.
“Nina imani uta kuwa nami kwenye kila hatua?”
“Ndio sinto weza kukuacha”
“Sawa ina bidi leo hii niondoke na nielekee Morogoro nikaonane na mzee Mbogo.”
“Hakuna shaka tuta ondoka wote”
Mlango wa chumba cha Evans uka fungulia na akaingia mdogo wake.


“Kaka una zungumza na nani?”
“Kuna rafiki yangu nilikuwa nina zungumza naye kwenye simu”
“Ahha…..ume ona kilicho tokea leo Dar es Salaam?”
“Rafiki yangu ndio alikuwa ana nina taarifa hiyo”
Evans alizungumza huku akimtazama jina Maimuna ambaye mdogo wake hawezi kuomuona zaidi yake yeye pake yake.
“Daa yaani kuna ogopesha. Watu wame kufa hao, mabomu yame lipuka”
“Ndio hivyo mdogo wangu nina shukuru Mungu nilisha ondoka”
“Ni kweli?”
“Mama yupo wapi?”
“Mama yupo sebleni ana tazama habari hiyo”
“Sawa mimi nina hitaji kuondoka leo na kuelekea Morogoro”
“Mmmm kaka Morogoro na Dar si karibu, usije uka lipuka na wewe?”
“Hakuna kitu kama hicho siwezi kulipuka”
“Mmm sijui kama mama ana weza kukubalia”
“Usijali nita zungumza naye. Hakikisha una simamia mafundi wana maliza kujenga hiyo gorofa ya mwisho pamona na ukuta uta jengwa vizuri”
“Sawa, je hakuna fundi ambaye ana tudai?”
“Mafundi wote nilisha walipa hakuna anaye dai”
“Sawa kaka”
Mdogo wa Evans akatoka ndani hapo.
“Jiandae sasa tuondoke”
Evans akaingiza nguo kadhaa kwenye kibegi chake kisha akatoka ndani hapo. Akamueleza mama yake juu ya safari hiyo na hakuweza kupinga kwa lolote. Evans na jini Maimuna wakaingia kwenye gari jipya la Evans aina ya Toyoter Harrier new model na wakaianza safari ya kuelekea mkoani Morogoro


***


Magreth na Levina nao wakawa kama watu walio shikwa na bumbuwazi. Walihisi mlipuko una weza kuwa ni mmoja ila hawakuamini kuona jiji ambalo lilikuwa na magorofa makubwa na majumba ya kifahari kwa sasa lina teketea kwa moto huku magorofa hayo yakiwa yame katika katika. Levina akajaribu kuminya japo batani moja kwenye laptop yake hiyo ila akajikuta mikono yote ikimtetemeka kwa woga.


Hadi sasa rafiki yao Josephine bado jaja zinduka na wakaanza kuhisi kitu kilicho mfanya azimie ni hii hali wanayo iona hivi sasa.


“Levina”
“Mmmmm”
“Sa…sa…aa tuna fanya nini?”
“Sijui rafiki yangu. Nime amini Josephine ana tumiwa na Mungu. Piga picha na sisi tunge kuwepo eneo hilo”
“Ila hawa Al-Shabab wame wau watu wasio na hatia kwa nini wame fanya hivi?”
“Sijui”
“Nahitaji kukiteketeza kikosi chote cha Al-Shabab”
Magreth alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake.
“Una hisi ni jambo rahisi kama hivyo”
“Ita wezekana tu nilazima niwewe kufanya jambo”
“Mage usije uka sababishia watu balaa jengine.”
“Haijalishi ila nikiwa kama mtanzani ni lazima niwe na uchungu. Wale walio kufa pale sio panya au kuku, ni watu wale Levina. Kuna ndugu zetu pale, kuna rafiki zetu pale na pia kuna watoto na vichanga ambavyo havina hatia yoyote. Kwa nini wawaue, kwa nini wasinge lipiza kisasi kwa raisi Mtenzi mwenyewe na serikali yake”
Magreth alizungumza huku akilia kwa uchungu sana. Levina naye machozi yakaendelea kumwagi. Josephine akakurupuka na kuwakuta weake wakiwa katika haliya huzuni kubwa.


“Jose Jose ime tokea kweli”
Levina alizungumza huku naye akilia. Josephine kwa haraka akashuka kitandani na kusogea ilipo laptop ya Levina, akashika mdomo wake kwani dakika za mwisho hali hiyo ndio aliyo weza kuiona kwenye maombi yake na ilimstua sana hadi akazimia.
“Josephine muombe huyo Mungu wako na akuonyeshe ni wapi lilipo kundi la Al-Shabab nina taka kwenda kuwaua wote. Nina taka kwenda kuchinja kundi zima la Al-Shabab na kiongozi wao nina hitji kumleta hapa nchini Tanzania na kumkabidhisha kwa wananchi waweze kumtandika mawe hadi afe”
Magreth alizungumza huku akimshika Josephine mikono yake. Josephine hakuzungumza kitu chochote zaidi ya kuendelea kuduwaa mithili ya mtu anaye anza kupandwa uwenda wazimu.


***


Gorofa ya hoteli waliyopo raisi Jery pamoja na familia yake, japo ime tengeneza kwa uimara wa hali ya juu, ila haikuweza kuhimili mlipuko huo wa bumo kubwa. Gorofa hilo likaanza kukatika vipande vipande huku rais, Jery, Julieth na walinzi wawil wakipigizw a pigizwa ndani ya lifti hiyo na kila mtu aliweza kumuomba Mungu wake aweze kumsaidia.


“Mungu wangu ni nini kimetokea ume usikia huo mtikisiko?”
Mrs Sanga ali hamaki huku wakiwa wamo ndani ya boti ya kifahari ambayo walikuwa wana ifanyia majaribio kabla ya kuinunua.
“Ndio, sijui hembu turudi”
Nabii Sanga alimuambia nahodha wa boti hiyo, kugeuza kwani hapo walio ni mbali na fukwe ya hoteli hiyo. Nahonda wa boti hiyo taratibu akaigeuka na wakaanza kurudi eneo lilipo hoteli.


“Mapigo yangu ya moyo yana nienda kasi mume wangu”
Mrs Sanga alizungumza huku akiwa amejawa na wasiwasi mkubwa sana.
“Usijali labda ita kuwa ni tetemeko la ardhi”
“Baharini?”
“Ndio”
Nabii Sanga alimtia matumaini mke wake, ila na yeye ame tawaliwa na wasiwasi mkubwa sana. Kila jinsi walivyo karibia nchi kavu ndivyo jinsi walivyo weza kushuhudia moshi mwingi mweusi ukiwa ume tanda kwenye anga la hoteli hiyo.


“Ohoo Mungu wangu”
Nahonda wa boti hiyo ambayo nabii Sanga walipanga kuinunua na kumpatia mtoto wao zawadi katika sherehe ya usiku, alizungumza huku akiwa ana tazama eneo la fukweni kwa kutumia darubini yake. Nabii Sanga kwa haraka akampokonya darubini hiyo na kuiweka machoni mwake. Nabii Sanga akajawa na mstuko mkubwa sana kwani hoteli ya gorofa hamsini, ime katika na zime baki gorofa tatu tuu huku kipande chote cha juu kikiwa kimetapakaa chini.


ITAENDELEA


Haya sasa, nabii Sanga na mke wake bahati ime kuwa upande wao. Wame salimika na hawakuwepo ndani ya hoteli hiyo je watoto wao watatu wata fanikiwa kuwa hai, ita kuwaje kwa upande wa raisi Mtenzi na familia yake? Usikose sehemu ya 116.
 
SIN 116


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188








ILIPOISHIA


“Usijali labda ita kuwa ni tetemeko la ardhi”
“Baharini?”
“Ndio”
Nabii Sanga alimtia matumaini mke wake, ila na yeye ame tawaliwa na wasiwasi mkubwa sana. Kila jinsi walivyo karibia nchi kavu ndivyo jinsi walivyo weza kushuhudia moshi mwingi mweusi ukiwa ume tanda kwenye anga la hoteli hiyo.


“Ohoo Mungu wangu”
Nahonda wa boti hiyo ambayo nabii Sanga walipanga kuinunua na kumpatia mtoto wao zawadi katika sherehe ya usiku, alizungumza huku akiwa ana tazama eneo la fukweni kwa kutumia darubini yake. Nabii Sanga kwa haraka akampokonya darubini hiyo na kuiweka machoni mwake. Nabii Sanga akajawa na mstuko mkubwa sana kwani hoteli ya gorofa hamsini, ime katika na zime baki gorofa tatu tuu huku kipande chote cha juu kikiwa kimetapakaa chini.





ENDELEA


Nabii Sanga hakurusubiria nahonda wa boti hiyo kutua nanga. Akajirusha ndani ya maji kwa haraka na kuanza kuogelea kuelekea nchi kavu. Akafanikiwa kutoka ndani ya maji na akaanza kukimbilia eneo la hoteli hiyo ambalo uzuri wake ume badilika na kuwa kama jehanamu ya moto.


”Oooohhh Mungu wangu”
Nabii Sanga alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Hakuelewa ni kitu gani kilicho tokea kwani miili ya watu iliyo katika katika viungo ime tapakaa kila mahali. Nahodha wa boti hiyo akamsaidia mrs Sanga kushuka kwenye boti hiyo na wakakimbilia alipo nabii Sanga. Kila mmoja alihisi kama ana ota ndoto isiyo isha kwenye upeo wa macho yao.


Mrs Sanga akajikuta akikaa chini huku akiendelea kulia kwa uchungu sana kwani hatambui wana familia wake wata kuwa wapi kwani eneo hilo lina onyesha hakuna mtu aliye weza kusalia.


***


“Ohoo Mungu wangu”
Makamu wa raisi bwana Madenge Jr alijikuta akitahamaki huku akitazama tv iliyopo chumbani kwake akiwa katika ziara ya kikazi nchini China. Msaidizi wake naye macho yame mtoka kwani shambulizi linazo lililo tokea jijini Dar es Salaam lime washangaza wote.


“Muheshimiwa raisi kwa sasa si yupo kwenye hiyo hoteli?”
“Ndio muheshimiwa”
“Ohoo Mungu wangu kwa hiyo ata kuwa ame fariki dunia?”
“Hatuwezi kukadiria hilo muheshimiwa, ina bidi tuwasiliane na mkuu wa majeshi”
“Basi fanya hivyo”
Kijana huyo kwa haraka, akachukua simu yake na kumpigia mkuu wa majeshi. Simu ya mkuu wa majeshi nayo kwa bahati mbaya haipatikani.


“Hapatikani mkuu”
“Niandalie ndege yangu, nahitaji kurudi nchini Tanzania sasa hivi”
“Sawa muheshimiwa”
Kijana akawasiliana marubabi wa ndege ya makamu wa raisi, kisha akawasiliana na raisi wa nchi ya chini ambaye ndio mwenyeji wao.
“Raisi Jing Hoo ana hitaji kuzungumza nawe”
Bwana Madege Jr akaichukua simu hiyo na kuiweka sikioni mwake.


“Ndio muheshimiwa”
“Nimeona shambulizi la kigaidi lililo tokea hapo nchini kwako. Kwakeli nime fadhaika kuona maelfu ya watu wakiteketea. Hivyo mimi na serikali yangu tupo tayari kukupa full support utakayo hitaji, ikiwemo ujenzi mpya wa jiji la Dar es Salaam”
“Nina shukuru sana muheshimiwa. Nami nina omba niweze kuikatisha ziara yangu nirudi nchini kwa maana hadi sasa hivi hatutambu kama raisi yupo hai au laa”
“Sawa nafanya mawasiliano na uwaja wa ndege ili ndege yako ipewe kipambele katika kupaa”
“Nashukurus ana muheshimiwa”
“Pole sana rafiki yangu”
“Nina shukuru”
Bwana Madenge Jr akakata simu huku macho yote yakiwa mekundu. Wakatoka hotelini hapo na walinzi wake pamoja na walinzi wa kichina. Moja kwa moja wakaelekea uwanja wa ndege, raisi Madenge na wasidizi wake pamoja na walinzi wake wakangia kwenye ndege yake na wakaondoka nchini China huku kila mmoja akiwa amejawa na mawazo ya ni kitu gani ambacho kime zipata familia zao zinazo ishi jijini Dar es Salaam.
“Muheshimiwa, waziri mkuu yupo kwenye laini namba moja”
Bwana Madenge Jr akanyanyua mkonga wa simu ya mezani iliyopo pembeni yake.
“Ndio bwana Makongoro?”
“Muheshimiwa nime tuma vikosi vya jeshi na zima moto kwa njia ya anga kufika katika jiji la Dar es Salaam kwa maana miundo mbinu ime haribika vibaya sana na milipuko”


“Kabla hawajafanya jambo lolote hakikisheni kwamba wana fika katika kwenye hoteli aliyopo raisi na wana hakikisha wana mpata akiwa hai au ame kufa”
“Sawa muheshimiwa na ndio agizo ambali tume wapatia?”
“Je mume weza kufahamu ni kina nani ambao wame husika na shambulizi hilo?”
“Hadi sasa hivi muheshimiwa hatuja weza kufahamu ni kina nani na hakuna kikundi hata kimoja na kigaidi ambacho kime andika statmente yoyote ya shambulizi hilo”
“Sawa nipi njiani nina kuja Tanzania, nita tua kwneye uwanja wa KIA kisha nita elekea Dar es Salaam”
“Sawa mueshimiwa”
Bwana Madenge Jr akakata simu huku picha ya milipuko ya mabomu hayo ikiendelea kumtawala kichwnai mwake. Akawatazama wasaidizi wake alio kuwa nao ndani ya ndege hiyo na kila mmoja ana onekana kujawa na wasiwasi mwingi sana huku wengie wakishindwa kuzuia machozi yao.


***


Nabii Sanga, nahodha wa boti pamoja na mrs Sanga wakaanza kuona helicopter nyingi zikikatiza eneo hilo. Helicopter hizo zikaanza kumwaga maji mengi kwenye gorofa hillo linalo teketea kwa moto. Vikosi maalumu vya ukozi vya wanajeshi vikaanza kushuka kwenye helicopter hizo huku wakitumia kamba.


“Nabii Sanga, nina itwa captain Homba. Eneo hilo kwa sasa sio salama, ina bidi tuwaondoe”
Kaptain Homba alizungumza huku akimtazama nabii Sanga usoni mwake.


“Siwezi kwenda popote kampteni, watoto wangu watatu wote wapo ndani ya hicho kifusi hapo. Siwezi kuwaacha na kuondoka. Nahitaji kusaidiana nayi”
Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo huku machozi yakiendelea kumwagika. Kapteni Homba akamtazama mrs Sanga aliye jichokea, na akawaagiza madaktari wa jeshi alio ambatana nao kumuondoa mrs Sanga aneo hilo kwani ana weza kufa kwa presha. Shuhuli ya kutoa vifusi vya jengo hilo ikaanza huku wanajeshi wangine wakijaribu kuondoa miili ya watu walio poteza katika eneo hilo. Waandishi wa bahari wa jeshi wakaanza kurusha matangazo ya kufukua kifusi hicho kwenye chaneli tofauti tofauti za nchi ya Tanzania. Zoezi hilo halikuwa jepesi kwani madhara yaliyo tokea ni makubwa sana.


Waziri mkuu naye na walinzi wake wakafika eneo hilo majria ya saa mbili usiku. Akakuta wana jeshi pamoja na polisi wakiendelea kujitahidi katika kutoa vifusi hivyo. Kapteni Homba akamfwata waziri mkuu, akampigia saluti kisha wakapeana mikono.


“Karibu muheshimiwa”
“Nashukuru je kuna mtu yoyote ambaye ame patikana?”
“Hapana muheshimiwa. Hatujafanikiwa kupata mtu aliye hai hivyo pia hatujui kama raisi na familia yake kama wapo hai”
Waziri mkuu akashusha pumzi huku akitazama vijana wanavyo jitahidi kufunua vifusi hivyo kwa kutumia vifaa visivyo na uwezo wa kuifanya hiyo kazi iende haraka haraka.
“Kapteni hakuna uwezekano wa kuleta Matinga tinga kuja kufukua hili eneo?”
“Hapana muheshimiwa. Barabara zime haribika hapa nime weza kuwasiliana na mkuu wa jeshi la majini. Nime muagiza kutumia boti zake kubwa kuleta japo vikoko viwili viweze kusaidia na kika hili swala”
“Sawa jambo zuri. Makamu wa raisi ata fika eneo hili muda si mrefu”
“Hakuna shaka muheshimiwa”
Wziri Mkuu akaanza kukatiza katiza eneo la hoteli hiyo na kuangalia uharibifu mkubwa ulio weza kutokea eneo hilo.


‘Nashukuru Mungu sikuwepo eneo hili’


Waziri mkuu alizungumza kimoyo moyo moyo kwani bomu hilo halijamucha mtu salama.


***


Evans akasimamisha gari lake aneo la kuingilia katika shamba kubwa la mzee Mbogo. Akatoa simu yake na kumpigia mzee huyo.
“Nime fika njia ya kuingilia shambani kwako”
“Ingia tu”


Evans akakata simu huku akimtazama jini Maimuna amabaye muda wote ame kuwa naye ndani ya gari hilo.
“Hawato kuona kweli?”
“Wewe pekee ndio mwenye uwezo wa kuniona mimi.”
Evans akaanza kuifwata barabara hiyo inayo ingia ndani ya shamba hilo na akafika katika nyumba ya mzee Mbogo na kukuta ulinzi ukiwa ume imarishwa. Evans akashuka kwenye gari, akakagulia na walinzi wa mzee Mboo kisha akasindikizwa ndani hadi sebleni alipo mzee huyo.
“Heshima yako mzee”
“Nashukuru. Una weza kukaa”
Evans akaka kwenye moja ya sofa linalo tazamana na mzee Mbogo.
“Ndio mzee nime kuja”
“Nime kuita hapa nahitaji kufahamu mambo mengi kutoka kwako. Ulicho kizungumza ndio kitu kilicho tokea”


“Ndio ni maono niliyo onyeshwa.”
“Je ni kitu gani kinacho kwenda kutokea sasa”
“Wapi?”
“Kwenye nchi”
“Kilichopo hivi sasa ni kuhakikisha una jengwa mji mpya wa Dar es Salaam”
“Vipi raisi na familia yake ipo salama”
Evans akamtazama jini Maimuna aliye simama pembeni yake, akatingisha kichwa.
“Swala hilo kwa siwezi kulijibu kabisa kwa maana ni jambo gumu kulitabiri”
“Nahitaji umuombe Mungu wako huyo na akuonyeshe”
“Siwezi kufanya hivyo kwa sasa”
“Nahitaji”
Mzee Mbogo alizungumza kwa kufoka na kuwafanya hadi wasaidizi wake kumshangaa.
“Kama hili ndio ulilo niitia nina ondoka”
“Huwezi kuondoka. Nahitaji uweze kunifahamisha kila kitu. Au wewe una shirikiana na hao Al-Shaba?”
“Ninge kuwa nina shirikiana nao basi nisinge kuambia jambo la iana yoyote kuhusiana na tukio ambalo lingetoka, pia kama ume kuja kunifokea, basi acha niondoke. Sina haja ya kuendelea kukaa hapa kwako”
Evans mara baada ya kuzungumza kanyanyuka na kuanza kueleeka mlangoni. Mzee Mbogo akamtazama Evans kwa macho makali sana yaliyo jaa hasira na uchungu.


“Hivi wewe ni mtanzania kweli?”
Swali la mzee Mbogo likamfanya Evans kusimama na kugeuka.


“Wewe una nionaje?”
“Uso wako una onysha dhahiri kwamba huna uchungu kwa yale yaliyo tokea”
“Una hisi kwamba sina uchungu. Wale walio kufa pale ni ndugu zangu na rafiki zangu na nilazima niwe na uchungu. Jambo jengine haya yote yaliyo tokea ni kwa ajili ya raisi wako na una jua kabisa kwamba ni raisi wako ndio alikuwa ana lipiziwa kisasi. Maamuzi yake ndio yame mponza, kwa heri”
Evans akatoka eneo hilo, akaingia kwenye gari lake na kuaianza safari ya kuelekea Morogoro mjini.
“Hivi raisi ni kweli yupo hai?”
Evans alimuuliza jini Maimuna.


“Sifahamu kwa kweli”
Evans akamtazama jini Maimuna kisha akaweka umakini wake barabani.
***


Josephien akaanza kushika kichwa chake huku huku akianza kuona giza lililo mfanya kutingisha kichwa chake na kuwafanya Magreth na Levina kumshangaa. Josephine akaanza kuona eneo ambalo raisi Mtenzi, Jery, Julieth na walinzi wawili walipo. Akayafumbua macho yake huku akihema sana, akatazama kwenye tv na kuona watu wakiendelea kufukua sehemu ambazo sio ambayo wana weza kumkuta raisi.
“Ina tubidi kwenda Dar sasa hivi?”
Josephine alizungumza kwa msisitizo.


“Kufanya nini?”
Levina aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao.
“Nime fahamu sehemu raisi alipo na yakipita masaa kumi yeye na watu wote waliomo ndani ya lifti hiyo wata kufa”
Magreth aliweza kumuelewa kwa uharaka Josephine anacho kizungumza.


“Ahaa kwa mabomu hayo mimi kwa kweli siwezi kurudi Dar”
Levina alizungumza huku akiwa amejawa na woga.
“Ina bidi kwenda kweli”
Magreth alitilia msisitizo.
“Tuna kwendaje, ikiwa barabara zitakuwa zime haribika, muna hisi mabomu hayo ni madogo kweli?”
“Levina kama huitaji kwenda, kaa hapa hatujakulazimisha”
Magreth alizungumza kwa kufoka na kumfanya Levina kushusha pumzi nyingi huku akijishauri juu ya kwenda au kuto kwenda.
“Tuta kwenda na pikipiki. Vaa nguo zako”
Magreth alizungumza huku akichukua fungua ya pikipiki hiyo.
“Msaada tunao omba kwako. Uweze kutuelekeza sehemu gani ya kupita, sawa”
Magreth alizungumza huku akimtazama Levina usoni mwake.
“Sawa hilo nita fanya kwa roho moja”
Magreth na Josephine wakajiandaa na kutoka nje ya hoteli hiyo. Wakapanda kwenye pikipi hiyo.
“Naomba unishikilie”
“Sawa”
Magreth akavaa kofia ngumu(helment) kisha waianza safari ya kuelekea jijini Dar es Salaam. Gafla Magreth akafunga breki za gafla mara baada ya gari ndogo kukatiza mbele yake. Gari hiyo ikasimama na kumfanya Magret kujawa na hasira kubwa sana kwani mwenye gari huyo ame mchomekea na asinge kuwa makini basi ange wasababishia ajali mbaya sana. Mageth akazima pilikipi yake na wakashuka na wakatembea hadi kwenye gari hiyo. Magreth akagonga kioo cha pembeni cha dereva huyo na kumfanya ashushe kioo cha gari hilo.
“Samahani sana dada yangu”
Magreth akastuka sana mara baada ya kumuona Evans ndio dereva wa gari hiyo. Hasira zote alizo kuwa nazo zikamshuka na kujikuta akivua helment hiyo na kumfanya Evans kujawa na mshangao mkubwa sana.


ITAENDELEA


Haya sasa, Magreth na Evans baada ya muda mrefu sana sasa lelo wame kutana kwa mara nyingine tena. Je ita kuwaje? Usikose sehemu ya 117.
 
SIN 117


Muandishi…………………………………………….EDDAZARIA G.MSULWA(G.Authour)


Age ……………………………………………………18+


Simu………………………………………………… 0657072588(whatsapp) au 0768516188





ILIPOISHIA


Gari hiyo ikasimama na kumfanya Magret kujawa na hasira kubwa sana kwani mwenye gari huyo ame mchomekea na asinge kuwa makini basi ange wasababishia ajali mbaya sana. Mageth akazima pilikipi yake na wakashuka na wakatembea hadi kwenye gari hiyo. Magreth akagonga kioo cha pembeni cha dereva huyo na kumfanya ashushe kioo cha gari hilo.
“Samahani sana dada yangu”
Magreth akastuka sana mara baada ya kumuona Evans ndio dereva wa gari hiyo. Hasira zote alizo kuwa nazo zikamshuka na kujikuta akivua helment hiyo na kumfanya Evans kujawa na mshangao mkubwa sana.





ENDELEA


“Evans!!?”
Magreth aliita huku akiwa amejawa na mshangao. Evans akamtazama jini Maimuna aliye kaa pembeni yake, jini Maimuna muda wote macho yake yana tazamana na Josephine aliye simama upande wake. Magreth akazunguka na kumshika mkono Magreth.
“Waache waondoke”
“Jose una jua ni jinsi gani nilivyo kuwa nina mpatuta Evans”
“Hapana sio Evans yule ambaye una mjua”
Josephine alizungumza huku akimkazia macho jini Mariam ambaye hana uwezo wa kumdhuru Josephine kwa lolote kwani Josephine ana ulinzi wa Mungu.
“Kwa nini?”
“Nita kuambia sio leo”
Josephine akamshika mkono Magreth na wakarudi kwenye pikipiki yao. Taratibu Evans akafunga kioo cha gari lake na kuondoka eneo hilo huku akimtazama jini Mariam ambaye muda wote amekuwa kimya. Magreth akaikremisha namba ya gari la Evans kisha taratibu akapanda kwenye pikipiki hiyo.
“Jose niambie ni kwa nini ume nizuia kuzungumza na Evans ikiwa una jua nina mpenda?”
“Ana tumiwa na jini”
“Jini?”
“Ndio na pale alipo Evans hawezi kuwa na mahusiano na mwamke ambaye sio bikra”
“Ume juaje?”
“Ume sahau nina uwezo gani?”
Magreth hakutaka kubishana au kuuliza swali jengine, akavaa kofia ya pikipiki yake. Josephine akapanda na wakaendelea na safari yao. Wakafanikiwa kufika maeneo ya Kihaba, hakika ni sehemu kubwa ya jiji la Dar es Salaam lime weza kuathiri kwa asilimia kubwa sana.


“Tuna elekea wapi?”
“Kwenye hoteli ambayo alikuwepo raisi na familia yake”
Magreth akajitahidi kuendesha pikipi yake katika meneo yaliyo kungoroka hadi wakafanikiwa kufika tika hoteli hiyo.Wakakuta ulinzi mkubwa ukiwa ume imarishwa katika eneo hilo huku taa kuwa zikiwa zime fungwa eneo hilo ili kuhakikisha kazi ya kuokoa walio fukiwa na kifusi hicho ina endelea kama kawaida.


“Hamruhusiwi kuingia hili eneo?”
Mwanajeshi mmoja aliwazuia Magreth na Josephine kuingia eneo hilo.
“Nani ambaye ni kiongozi wenu”
Magreth alimuuliza mwana jeshi huyo.


“Una muhitaji wa nini?”
“Kuna jambo muhimu sana nina hitaji kumuambia”
“Dada kama una shindwa kuzungumza kilicho waleta basi ondokeni”
“Kaka nime kuja hapa nina tambua ni wapi raisi alipo. Tuonyeshe nani ni mkuu wako tuzungumze”
Josephine alizungumza kwa msisitizo na kumfanya mwanajeshi huyo kustuka kidogo. Akatwazama kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kuongoza sehemu alipo kapteni wa kikosi chake hicho.
“Mkuu kuna hawa wasichana wana hitaji kuzungumz ana wewe”
“Ehee mabinti jitambulisheni”
“Mimi nina itwa Magreth”
“Mimi nina itwa Josephine nina fahamu sehemu raisi Mtenzi alipo”
Kauli ya Josephine kidogo ika mstua kapteni Homba. Akamtazama Josephine kwa umakini huku akimkazia macho.
“Ndio nina fahamu sehemu raisi Mtenzi alipo. Yame baki masaa matano tu, mukishindwa kumukoa basi ana weza kufa na watu wote walipo ndani ya lifti hiyo”
Kapteni Homba kabla hajafanya maamuzi yoyote akamuita kijana wake kumuita waziri mkuu. Waziri mkuu akafika eneo hilo.
“Muheshimiwa kuna hawa wasichana hapa, huyu ana itwa Josephine ana dai kwamba ana fahamu ni sehemu gani raisi Mtenzi yupo”
“Ume muona wapi raisi Mtenzi?”
Waziri mkuu aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao.


“Nifwateni”
Josephine akaanza kutembea na kuwafanya watu kumfwata kwa nyuma. Josephine akapanda kwenye moja ya kifusi na akasimama.
“Eneo hili kwa chini ndipo alipo raisi”
Watu wote wakashangaa kitu anacho kizungumza Josephine, wengi walihisi ata waonyesha eneo tofauti na gorofa hilo.


“Hapa ndipo alipo raisi?”
Waziri mkuu aliuliza huku akiwa amejawa na mshangao mkubwa sana.
“Ndio, tena ina bidi mutoa kifusi hichi”
Kapteni Homba akamuamini Josephine kitu anacho kizungumza na shuhuli ya kuanza kupasua kifusi hicho ika anza.
“Wewe kenge upo hapa?”
Sauti ya nabii Sanga ika mstua sana Magreth, akageuka nyuma kwa haraka na kumkumta nabii Sanga akiwa amejawa na vumbi jingi usoni mwake.


“Mzee samahani ume changanyikiwa au?”
Magreth alizungumza kana kwamba hamfahamu nabii Sanga.
“Ume fwata nini hapa?”
“Samahani dada mzee kidogo hayupo sawa. Muheshimiwa tuna kuomba uka pumzike kule”
Mwanajeshi mmoja alizungumza huku akimtoa nabii Sanga kwenye eneo hilo. Nabii Sanga akamtazama Magreth huku akiwa na hasira kali sana.


“Ume muona nabii wako?”
Magreth alimuuliza Josephine.


“Yupo wapi?”
“Yule kule anaye pelekwa. Naona ame ponea chupu chupu”
“Masikini ana tia huruma”
Josephine alizungumza kwa sauti ya upole huku akimtazama nabii Sanga. Mwanajeshi huyo akamkalisha nabii Sanga kwenye moja ya eneo lililo tulia. Nabii Sanga machozi yakaendelea kumwagika usoni mwake kwani hadi sasa hatambu ni wapi walipo. Simu yake ikaanza kuita, akaitoa mfukoni mwake na kukuta ni mke wake ndio anaye mpigia.
“Ndio”
Nabii Sanga alizungumza kwa sauti iliyo jaa huzuni kubwa.
“Vipi mume wangu kuna lolote?”
“Hakuna mke wangu”
“Ohoo Mungu wangu, tuna fanyaje?”
“Sijui nina endelea kusikilizia. Vipi nyumba yetu?”
“Ipo salama”
“Upo na nani?”
“Peke yangu”


Nabii Sanga akafumba macho kwani katika kundi kubwa la watu alio kuwa nao nyumbani kwake hapo lime teketezwa na mabomu hayo.
“Sawa usitoke pumzik”
“Uni fahamishe kile kinacho tokea mume wangu”
“Sawa”
Nabii Sanga akakata simu huku akimtazama Josephine aliye simama mbele yake.
“Mtumishi”
Josephine alizungumza huku akichuchumaa mbele ya nabii Sanga.
“Jose una fanya nini hapa?”
“Nime kuja kuwaonyesha eneo ambalo raisi yupo”
“Wa….w….a.aaa..nang…u je?”
“Sehemu atakayo patikana raisi ndipo alipo Julieth na mume wake”
“Je na wanangu wa kiume?”
Nabii Sanga alizungumza huku akimkodolea macho Josephine kwa maana ana utambua uwezo wake. Taratibu Josephine akafumba macho yake, Josephine akafumbua macho yake na kumtazama nabii Sanga huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana.
“Nini?”
“Samahani kwa kuzungumza haya”
Josephine alizungumza kwa sauti ya upole huku malengo yakimlenga lenga usoni mwake.
“Zungumza tu”
“Watoto wako wote wa kiume wame fariki dunia”
Nabii Sanga macho yakamtoka huku mapigo yake ya moyo yakimuenda kasi sana kwani habari hiyo sio nzuri hata kidogo kwake.


***


Ndege ya makamu wa raisi bwana Madenge Jr, ikatua katika kiwanja cha kimataifa KIA. Akapanda kwenye helicopter na moja kwa moja safari ya kuelekea jiji la Dar es Salam ikaanza.


“Wama patikana watu wangapi hai hadi sasa?”
Bwana Madenge alimuuliza mkuu wa mkoa wa Moshi aliye mpokea katika kiwanja hicho.
“Bado hatuja pata taafira mkuu”
“Daa hawa washenzi ni lazima tushuhulike nao kisawa sawa”
“Ni kweli muheshimiwa, wame tuharibia sana sifa ya nchi yetu”
Helicopter hiyo ikatua katika eneo la hoteli hiyo na makamu wa raisi akapokelewa na waziri mkuu.
“Karibu sana muheshimiwa”
Waziri mkuu alizungumza huku wakipenda mkono na makamu wa raisi.


“Nashukuru, aisee hii gorofa ndio ime kuwa hivi?”
“Ndio muheshimiwa na lile eneo pale kuna bintu ametueleza kwamba ndipo alipo raisi Mtenzi”
“Binti!! Binti gani?”
“Yule msichana yupo wapi?”
Mwanajeshi mmoja akaenda eneo alipo Josephine.


“Sinte una hitajika”
Josephine akamtazama nabii Sanga anaye weweseka kwa uchungu wa kufiwa na watoto wake wa kiume. Akasimama na kuanza kumfwata mwanajeshi huyo huku Magreth naye akiambatana naye. Wakafika katika eneo walipo viongozi hao.


“Binti mwenyewe ndio huyo hapo”
Makamu wa raisi akamtazama Josephine kuanzia juu.
“Shikamoo”
Josephine alizungumza huku akimpa mkono makamu wa raisi”
“Marahaba ume tambuaje kwamba raisi yupo eneo hilo?”
“Ni maono yangu”
“Maono?”
“Ndio”
“Je uliweza kufahamu juu ya hili shambulizi?”
Josephine akamtazama Magreth ambaye alishindwa kumpa ishra yoyote kwa maana viongozi wote wana mtazama yeye.


“Ndio, nilionyeshwa juu ya shambulizi hilo na nilitambua muda na saa ambalo lita tokea”
Watu wote wakamshangaa Josephine.


“Kwa nini sasa usiwaambie watu au ulitoa ripoti kwenye chombo gani?”
“Hata ninge zungumza nisinge aminika. Hakuna mtu ambaye anaweza kuamini, yamebaki masaa manne endapo muta shindwa kumtoa raisi, mwanaye, mkwe wake pamoja na walinzi wake wawili waliomo ndani ya lifti basi wote wata kufa”
Kauli za Josephine zikazidi kuwashangaza watu wote hapo na hawakuna na namna ya kufanya zaidi ya kuendelea kuongeza juhudi za kuifukua sehemu hiyo walio onyeshwa na Josephine kwamba ndipo alipo raisi Mtenzi.



***


“Mbona una mawazo mengi”
Jini Maimuna alimuuliza Evans aliye jilaza kwenye sofa huku akimfikiria Magreth aliye kutana naye.
“Hei Evans”
“Mmmm”
“Nakuuliza mbona una mawazo mengi kiasi hicho, au una muwaza Mgareth?”
“Yaa nina muwaza yeye”
“Kumbuka kwa sasa wewe ni nani, hupaswi kumuwaza na wala hupaswi kumpenda kabisa”
“Maimuna tambua kwamba mimi ni binadamu. Endapo ninapo kutana na hali kama hizo basi nina kuwa katika hali kama hiyo”
Taratibu jini Maimuna akakaa pembeni ya Evans, akamtazama kwa sekunde kisha taratibu akamshika mashavu yake na kumnyonya lipsi zake na kumfanya Evans kushangaa sana.
“Sihitaji umfikirie tena Magreth”
Jinsi Maimuna mara baada ya kuzungumza hivyo, akampulizia Evans pumzi ailiyo ingia hadi ndani ya moyo wake na kusabaisha chuki kubwa sana juu ya Magreth na hata mawazo yake mazuri yakabadilika na kuwa mabaya.
“Magreth ni adui yako nauna paswa kumuua yeye na yule rafiki yake”
Jini Maimuna alizidi kumpandikiza Evans chuki hadi akatamani kumuua Magreth wakati huo huo.
“Nita muua Magreth na rafiki yake sehemu yoyote nitakayo muona”
Evans alizungumz akwa msisitizo huku akimtazama jini Maimuna usoni mwake na kumfanya atabasamu kwa maana uwezo alio kuwa nao rafiki wa Magreth ni mkubwa sana na una weza kumkwamisha kwenye mipango yake mingi.


ITAENDELEA


Haya sasa, Evans amepandikizwa chuki juu ya kuwadhuru Magreth na Josephine je ata weza kuwaangamiza? Usikose sehemu ya 118.
 
Back
Top Bottom