RIWAYA: Tai kwenye mzoga

RIWAYA: Tai kwenye mzoga

Gentries watu tunakosea bt try kukosoa kwa staha ndugu yangu. Wengine ni watu na heshima zetu kabisa na we are just doing things for hobby with no any personal gains. Namsaidia mtunzi kutangaza kazi zake na pia nasaidia member kupata burudani. It is a voluntary work.
Pole mkuu chukulia kama moja ya changamoto
 
Gentries watu tunakosea bt try kukosoa kwa staha ndugu yangu. Wengine ni watu na heshima zetu kabisa na we are just doing things for hobby with no any personal gains. Namsaidia mtunzi kutangaza kazi zake na pia nasaidia member kupata burudani. It is a voluntary work.
Msamehe buree Kakaa, tupia burudani
 
Mkuu kama ungeelwa content ya post yangu sikumaanisha kukutukana kabisa It was a joke..

BTW Sorry sana mkuu kwa kukuudhi
Gentries watu tunakosea bt try kukosoa kwa staha ndugu yangu. Wengine ni watu na heshima zetu kabisa na we are just doing things for hobby with no any personal gains. Namsaidia mtunzi kutangaza kazi zake na pia nasaidia member kupata burudani. It is a voluntary work.
 
Mkuu kama ungeelwa content ya post yangu sikumaanisha kukutukana kabisa It was a joke..

BTW Sorry sana mkuu kwa kukuudhi
Hamna shida kaka Amani na itawale narudia tena kuomba radhi kwa kutopost jana lakini leo nataka niwasindikizie weekend yenu
 
Pamoja sana mkuu..

yaani nipo nazurura humu tu kuona kama ushashusha mzigo..

Tujazie mzigo wa Heavy weight..
Hamna shida kaka Amani na itawale narudia tena kuomba radhi kwa kutopost jana lakini leo nataka niwasindikizie weekend yenu
 
Nadhani mpaka hapo the banker utakuwa ushamwelewa Gentries!!ndo uzur wa wanaume!kusameheana ni chap tu,mambo zingine zinasonga!!haya the banker fanya mambo unazingua ujue!
 
Nadhani mpaka hapo the banker utakuwa ushamwelewa Gentries!!ndo uzur wa wanaume!kusameheana ni chap tu,mambo zingine zinasonga!!haya the banker fanya mambo unazingua ujue!
Yaaa mkuu uanaume sio kufuga ndevu na kuvaa suruali..
Attitude & personality make you to be a Gentleman
 
“Mna hakika kuwa hamkumchukua mtu yoyote njiani?
“Hatujamchukua mtu yoyote kwani tunajua hata sheria za barabarani haz-
ituruhusu kufanya hivyo” yule dereva akaongea kwa msisitizo huku akioneka-
na kuwa mwenye mashaka.
Wale askari waliochepuka kuja kukagua nyuma ya lile tela walipekua kila
mahali huku wakifunua turubai lililokuwa limefunika ile mifuko ya sukari
hata hivyo hawakuwa watundu katika kufanya upekuzi hivyo hawakuyagun-
dua maficho yangu. Baadaye niliwaona wakiondoka na kuelekea kule mbele
na sikuweza kuwaona tena kwani walikuwa wamehamia upande mwingine.
Mimi niliendelea kujibanza mle ndani ya lile tela nikisikilizia huku bastola
yangu ikiwa tayari mkononi.
Haukupita muda mrefu mara niliwaona yule dereva wa lori na utingo wake
wakiingia ndani ya ile kibini ya lori kisha milango ikafungwa na haukupita
muda mrefu baada ya pale nikaanza kuisikia injini ya lile lori ikianza kuungu-
ruma. Muda mfupi baadaye lile lori lilianza kuondoka na kuingia tena baraba-
rani na hapo safari ikaanza tena.
Niliendelea kujibanza mle ndani ya tela hadi pale nilipohisi kuwa tuliku-
wa tumesafiri umbali mrefu wa safari yetu ndiyo nikaanza kutoka mle ndani
nikielekea kwenye ile kibini huku nikiwa makini kutazama nyuma kama lile
gari Nissan Patrol lilikuwa bado likitufuatilia. Sikuliona tena lile gari na hali
ile ilinipa furaha sana. Nilipofika kwenye ile kabini nikasimama juu ya lile
gunia la mkaa huku nikiufungua ule mlango mdogo wa dharura na baada ya
muda mfupi nikawa nimefanikiwa kurudi mle ndani ya kibini na kukaa ma-
hali pangu. Macho yenye hofu na mashaka ya utingo na yule dereva wa lori
yalinipokea bila kusema neno kisha yakageuka na kutazama mbele na hapo
nikafahamu kuwa ile hali ya urafiki ilishatoweka mle ndani na isingekuwa
rahisi kuirudisha haraka.
“Wale watu ni kama waliokuwa wakikutafuta wewe bwana kwani una shida
gani? yule dereva aliniuliza huku akionekana mwenye mashaka na mimi.
“Nilitarajia hivyo” nilimwambia yule dereva na jibu langu bila shaka lili-
washtua wote na hivyo kuwapelekea wageuke tena kunitazama kwa tuo kisha
wakageuka tena kutazama mbele.
“Kwa sababu gani unasema hivyo bwana? yule utingo aliniuliza
“Unajua kabla ya kuharibikiwa na basi letu kuna kituo kimoja cha njiani
nilisimamishwa na askari wa barabarani na hawakunikuta na kosa lolote hata
hivyo walikataa kuniruhusu eti mpaka niwape kitu kidogo. Sikuwapa pesa
yoyote na kwa hasira nikawasha gari na kuondoka nikiendelea na safari hivyo
nilijua tu askari wale wangenifuatilia. Nahisi watakuwa wameambiwa na wale
abiria kuwa mimi nimeelekea jijini Kigali kutafuta msaada hivyo wakaona
wanifuatilie na kunibana huku huku njiani wakiamini kuwa kwa vyovyote nina
pesa. Nimemkumbuka yule askari uliyeingia naye humu ndani kuwa alikuwa
miongoni mwa wale askari walionisimamisha kule njiani” nilimaliza kuongea
huku nikiupima uzito wa uwongo wangu kama ungekuwa rahisi kukubalika
hata hivyo sikuona kama uwongo wangu uliwaingia yule dereva na utingo
wake kwani nilikuwa ni kama ninayejiongelesha mwenyewe.
“Wanasema wewe ni mtu hatari unayesakwa kile pembe ya hii nchi” yule
utingo alidakia
“Toka lini mtu anayekataa kutoa rushwa akawa ni mtu hatari katika nchi?,
achana nao wale wana njaa zao. Ni kawaida kwa askari wa barabaani wa nchi
hii kudai rushwa hususani kwa madereva wasio wazawa” nilijaribu kujitetea
huku nikifahamu kuwa sikuwa na hoja ya msingi ya kujitetea lakini kukaa
kimya sikuona kama ingefaa, hata hivyo hakuna aliyeunga mkono utetezi
wangu.
“Ulikuwa umejificha wapi ?, nilikuwa na wasiwasi sana wakati yule askari
alipotaka kuingia humu ndani ili ajiridhishe kuwa hakukuwa na mtu tuliyem-
chukua” yule dereva aliniuuliza akiingiza gia na kukanyaga mafuta.
“Nilijua tu kuwa kwa vyovyote wale watu wangetaka kujiridhisha kwa ku-
fanya upekuzi humu ndani ndiyo maana niliwahi kutoka kwa kupitia mlango
wa dharura wa hii kibini na kwenda kujificha nyuma kwenye tela huku nikiji-
funika kwa ile mifuko ya sukari”
Niliendelea kuongea na wakati huu pia si utingo wala yule dereva aliyeo-
nekana kuvutiwa na maelezo yangu na hapo ukimya ukachukua nafasi yake
na mimi sikupenda tuendelee na maongezi yale. Niligeuka kutazama dirishani
nikaona kuwa kulikuwa na wingu zito limetanda angani na hapo nikajua kuwa
muda si mrefu mvua kubwa ingeanza kunyesha. Safari iliendelea na lile lori
lilikuwa likitimua mbio sana.
Mle ndani hakuna aliyekuwa na hamu ya maongezi yangu tena na mimi
nilipenda tuwahi kufika jijini Kigali ili kila mtu ashike hamsini zake. Nilitaka
kuuliza kuwa muda gani ungekuwa umesalia kabla ya kufika jijini Kigali la-
kini nilisita kufanya hivyo kwani huenda swali langu lingenifanya nionekane
kuwa sikuwa dereva niliyeifahamu vizuri barabara ile hivyo niliegemea siti
yangu vizuri nikawa nikitazama nje huku usingizi ukiwa mbali na mimi.
WALINISHUSHA PEMBENI YA KITUO kikubwa cha kujazia mafuta kili-
chokuwa katikati ya jiji la Kigali ikiwa tayari imekwishatimia saa kumi na
mbili jioni. Manyuyu hafifu ya mvua yalikuwa bado yakianguka toka angani
na giza nalo lilikuwa mbioni kushika hatamu. Niliwashukuru sana yule dereva
na utingo wa lile lori huku nikiwaahidi kuwa ningewatafuta baada ya kurudi
nchini Tanzania, na wakati nikiwaaga niliziona nyuso zao zikirudiwa na fura-
ha iliyotoweka kwa muda mrefu. Hapo nikajua furaha yao ilikuwa si kwa kwa
sababu walitaka tuonane tena hapo baadaye ila ni kwa sababu hawakupenda
kuwa na mimi na hilo halikunipa shida kwani mpaka pale walikuwa wameni-
saidia sana na sikuwa nahitaji msaada wao tena.
Baada ya kushuka kwenye lile lori na kuagana na yule dereva na utingo
wake nilisimama kando ya barabara ile nikiliacha lile lori likitoweka mbele
yangu kisha nikavuka barabara nikiwa mwenye tumaini jipya katika harakati
zangu. Sasa nilikuwa nimefika jijini Kigali.
Nikiwa na hakika kuwa hakuna mtu yeyote eneo lile aliyekuwa akizifuatilia
nyendo zangu tangu niliposhuka kwenye lile lori nilivuka barabara nyingine
upande wa kushoto na hapo nikaingia kwenye njia ya watembea kwa miguu.
Sikufahamu hasa ni wapi nilipaswa kuelekea ambapo ningeweza kutuliza
kwanza fikra zangu na kujipanga vizuri kabla ya kuanza tena harakati zangu
hata hivyo niliamini kuwa ingekuwa rahisi kupata jibu la swali hilo huku niki-
wa bado natembea kuliko nikiwa bado nimesimama eno lile.
Wakati nikiendelea kutembea nilijikuta nikifikiria kurudi kule chumbani
kwangu Hotel des Mille Colline hata hivyo nilipozidi kufikiria nilijikuta niki-
liweka wazo hilo kando kwanza kwani niliamini kuwa wale watu walioniteka
hadi wakati huu wangekuwa wakifahamu kila kitu kuhusu mimi ikiwemo ho-
teli niliyofikia na hata namba ya chumba changu na kwa kuwa nilikuwa nime-
watoroka kwa vyovyote sehemu ya kwanza ambayo wangenisubiri ingekuwa
ni kule chumbani kwangu hotelini. Hivyo sikuona kama ningekuwa nikifanya
uamuzi sahihi endapo ningeamua kufikia kule hotelini.
Nilifikiria niende kule Kigali Casino nikaonane na Mutesi hata hivyo wazo
hilo nalo pia sikuliona kuwa kama lingekuwa muafaka kwa kipindi kile hasa
nilipoanza kuhisi kuwa upo uwezekano kuwa huenda nisingemkuta Mutesi
wakati ule kwani nilikuwa sizifahamu vizuri ratiba zake na vilevile sikuwa na
hata pesa kidogo mfukoni ambayo ingeniwezesha kununua mzinga mmoja wa
pombe ambao ungetumika kuyasindikiza maongezi yetu. Hivyo wazo hilo pia
nililiweka kando huku nikifikiria mpango mwingine mzuri zaidi.
Wakati nikiendelea kufikiria nikajikuta nikiyakumbuka maelezo ya Ros-
ine wakati ule tulipokuwa pamoja kule kwenye ili nyumba katikati ya msitu.
Nikiwa nayakumbuka vizuri maelezo yake Rosine kuwa yeye na dada yake
aliyekuwa akiitwa Diane walikuwa wakiishi kwenye nyumba moja miongoni
mwa nyumba za shirika la nyumba la taifa la Rwanda eneo liitwalo Block C
nyumba namba 11 na nyumba hiyo ilikuwa ikimilikiwa na mume wa dada
yake aitwaye Jean Felix Akaga. Pia nilikumbuka kuwa huyo Diane na huyo
mumewe Jean Felix Akaga walikuwa wameuwawa hivyo katika familia hiyo
mtu pekee aliyesalia alikuwa Rosine. Na hadi wakati huu nilikuwa sifahamu
kuwa Rosine alikuwa wapi tangu tulipopoteana kule msituni, huenda angeku-
wa ametekwa na kuuwawa au labda angekuwa ametoroka, sikufahamu.
Kwa tathmini hiyo niliona kuwa sehemu salama ya kukimbilia kwanza in-
gekuwa ni huko Block C nyumba namba 11 na uamuzi wangu ukanipa faraja
kiasi huku nikiamini kuwa kama Rosine angekuwa amepata nafasi nzuri ku-
toroka toka kwa wale watu hatari kule msituni basi sehemu ya kwanza ambayo
angefikia ingekuwa ni kwenye hiyo nyumba. Na kwa maana nyingine hiyo
ingekuwa sehemu nzuri ya kuonana naye kwa mara nyingine huku tukiwa ni
wenye furaha na amani na mambo mengine yote yangefuatia baada ya hapo.
Mpango huu ukanipelekea nitabasamu na kuingiza mkono mmoja mfukoni
mwa suruali na sasa kilichobaki ilikuwa ni kupeleleza na kulijua hilo eneo la
Block C na sehemu ilipo nyumba namba11.
Niligeuka nyuma kutazama nikaona hakuna mtu yeyote aliyekuwa akini-
fuatilia kwani kila mtu alionekana kupita na hamsini zake hivyo nikaendelea
kufarijika huku nikizitupa hatua zangu ndefu kuifuata ile barabara ya watem-
bea kwa miguu. Nilifika mbele kidogo sehemu kulipokuwa na jengo dogo
la shirika la posta na hapo nikakunja kona na kuifuata barabara iyelekeayo
upande kushoto huku nikifurahishwa na namna jiji la Kigali lilivyojengwa
kwa mpangilio unaovutia. Kwa wakati huu kila sehemu ya jiji ilionekana
kuchangamka na watu walionekana kukusanyika katika baadhi ya sehemu
za starehe. Biashara ndogo ndogo za barabarani zilikuwa zikiendelea kama
kawaida na hata maduka makubwa yalikuwa wazi huku yamerembwa kwa
mabango makubwa ya taa za aina tofauti zinazopendeza. Jiji la Kigali lilikuwa
limechangamka na pilikapilika za watu zilikuwa mbioni kushamiri.
Niliendelea kutembea katika barabara ile huku nikipishana na watu wa aina
tofauti hata hivyo nilikuwa makini sana kuzichinguza nyuso za watu nili-
opishana nao. Nilipofika mwisho wa barabara ile nikawa nimetokezea kwenye
kituo cha mabasi madogo yanayoelekea maeneo tufauti ya jiji la Kigali. Ku
likuwa na kundi kubwa la abiria waliokuwa wakisubiri usafiri wa kuelekea
maeneo yao. Kufikia hapo nikakumbuka kuwa sikuwa na pesa yoyote mfukoni
na pia nilikuwa silifahamu hilo eneo la Block C lilikuwa wapi toka pale nili-
pokuwa.
Nilifika sehemu fulani na kusimama pale kwenye kituo cha mabasi madogo
huku nikijaribu kumtafuta mtu wa kumuuliza ambaye angekuwa tayari ku-
nielekeza. Baada ya kuchunguza chunguza nikawa nimemuona mzee moja
aliyeonekana kuwa muungwana na mwenye ufahamu mzuri wa jiji la Kigali
hivyo nikaaza kumsogelea lakini kabla sijamfikia nikapata wazo jingine baada
ya teksi fulani kuja na kusimama pembeni yangu.
Dereva wa teksi ile alikuwa kijana wa miaka ishirini na kitu hivi, aliposim-
amisha teksi pembeni yangu akatoa kichwa dirishani na kuniuliza kwa lugha
ya kinyarwada
“Amakuru? sikuweza kumjibu kwani nilikuwa siifahamu lugha ya kinyar-
wanda ingawaje nilikuwa nimehisi kuwa alikuwa akiniuliza “Habari za saa
hizi”. Nikamtumbulia macho kijana yule na nilipomuona kuwa hanielewi
nikaongea kwa lugha yangu mama ya kiswahili.
“Nipeleke eneo liitwalo Block C, unapafahamu?
“Ugiyehe? akaniuliza kwa kinyarwanda yaani “Unaenda wapi?” kama am-
baye hajanisikia vizuri.
“Block C” nikarudia kusema kwa sauti ya juu kidogo yenye msisitizo.
“Uri umushyits? akaniuliza akimaanisha “Wewe ni mgeni hapa?”
“Block C” nikasisitiza huku nikimwona ananichanganya na kinyarwanda
chake.
“Uri u mtanzania? akaniuliza tena yaani akimaanisha “Wewe ni mtanzania?”
“Ndiyo” nikamjibu “Nataka unipeleke eneo liitwalo Block C” nilimwambia
tena huku nikianza kukata tamaa.
“Ufite kibazoki? yule dereva wa teksi akatabasamu na kuniuliza tena
akimaanisha “Unashida gani?” Sikumjibu tena yule dereva wa teksi kwani
nilianza kumuona ni kama anayenipotezea muda wangu hivyo nikaacha kum-
tazama na kugeuka nikitazama upande mwingine huku nikijaribu kuchunguza
kama kulikuwa na teksi nyingine jirani na pale. Yule dereva wa teksi akawa
ameishtukia dhamira yangu hivyo haraka akapenyeza mkono wake kwa nyu-
ma na kufyatua kabari ya mlango.
“Ingia ndani my friend” yule kijana akaniambia kwa kiswanglish cha kin-
yarwanda, sikutaka kujivunga kwani sikupenda kuendelea kupoteza muda pale
na kuvuta macho ya watu. Nikafungua mlango na kuingia nyuma ya ile teksi
na muda uleule ile teksi ikaanza safari ikielekea sehemu ya kutokea magari ya
kituo kile cha mabasi madogo.
Tulipotoka nje ya kituo kile cha mabasi madogo tukaingia barabara ya
upande wa kulia na muda mfupi baadaye tukawa tukiuacha mtaa mmoja na
kuingia mwingine tukiendelea na safari yetu na mimi sikusahau wajibu wangu
hivyo kila mara nikawa nikigeuka nyuma kutazama kama kulikuwa na gari
lolote lililokuwa likitufungia mkia. Safari ilikuwa poa kwani sikuweza kuliona
gari lolote likitufungia mkia nyuma yetu na hivyo safari yetu iliendelea
Tuliwasili eneo la Block C dakika tano zikiwa mbele ya nusu saa kwa muji-
bu wa majira ya saa iliyokuwa kwenye dashibodi mle ndani ya gari. Tulikuwa
ndiyo tunaiingia eneo la Block C wakati nilipomtaka dereva asimame kando
ya barabara ile sehemu kulipokuwa na giza lilofanywa kwa vivuli vya miti ya
barabarani na teksi iliposimama tu nikafungua mlango na kushuka.
“Pesa yangu vipi ndugu? yule dereva aliniuliza kwa mshangao baada ya
kuniona nikishuka bila kumlipa. Sikumjibu badala yake nikaingiza mkono
wangu mfukoni na nilipoutoa nilikuwa nimeshika bastola, yule dereva alipoo-
na vile akawa naye ameshtuka na kunitazama kwa woga. Nikamsogelea karibu
na kumgusagusa shavuni kwa mtutu wa ile bastola na hapo akazidi kutetemeka
kwa hofu.
“Siku moja moja jifunze kujitolea”nilimuonya.
“Sawa ndugu” akanijibu kwa kihoro kama anayepigania roho yake usiuache
mwili.
“Potea!” nikamwambia na muda uleule akatia moto gari na kutokomea
mbele yangu. Nilitabasamu kidogo kisha nikairudisha bastola yangu mfukoni
na kupotelea kwenye vivuli vya miti iliyokuwa eneo lile na muda mfupi baa-
daye nikawa nimetokezea kwenye barabara ya mtaa wa pili.
Kulikuwa na bango kubwa katika barabara ile na bango hilo lilikuwa na
maandishi yaliyoandikwa kwa lugha ya kifaransa yakisomeka “Bien venu au
rendroir C” yaani “Karibu eneo la Block C” na hapo nikatabasamu taratibu
baada ya kuwa na hakika kuwa nilikuwa sijapotea. Sikuwa mgeni sana wa
lugha ya kifaransa kwani nilikuwa nimesoma kwenye shule ya sekondari ya
Milambo iliyopo mkoani Tabora nchini Tanzania. Shule hiyo ilikuwa ni mion-
goni mwa shule chache za serikali zilizokuwa zikifundisha somo la lugha ya
kifaransa nchini Tanzania ukiachilia mbali zile shule za watu binafsi ambazo
kwa idadi zilikuwa chache sana.
__________
ENEO LA BLOCK C LILIKUWA MIONGONI mwa maeneo yenye makazi
ya kisasa kabisa jijini Kigali, nyumba zake zilijengwa kwa mpangilio unaovu-
tia na barabara za lami zenye nguzo za taa pembeni. Wakatinikitembea katika
barabara ya mtaa ule nilihisi kama niliyekuwa nikionekana kwenye nyumba za
jirani hata hivyo suala hilo halikuyumbisha msimamo wangu.
Macho yangu yalizunguka kutazama kila nyumba ya mtaa ule na hadi nafika
mwisho wa ule mtaa geti la nyumba hiyo lilikuwa limeandikwa kwa lugha ya
kifaransa “Maison numero dix” yaani nyumba namba kumi, nikajua nyumba
namba kumi na moja ingekuwa ipo nyuma ya nyumba ile katika mtaa unao-
fuata. Hivyo nilikatisha kwenye uchochoro kuingia mtaa wa nyuma na safari
hii sikuhangaika kwani nyumba namba kumi na moja ilikuwa mbele. Hata
hivyo nilishangaa kuiona kuwa ilikuwa ni nyumba pekee eneo lile isiyokuwa
na uzio pia taa zake zilikuwa zimezimwa lakini hilo halikunishangaza kwani
nilifahamu kuwa wenyeji wa nyumba ile hawakuwepo.
Nilipofika nilizunguka nyumba ile nikaichunguza kama kulikuwa na dalili
za uwepo wa kiumbe chochote mle ndani. Niliporidhika kuwa mle ndani haku
wa na mtu yoyote nikazunguka nyuma na kuingia ndani kwa kupitia dirisha
la jikoni baada ya kukiharibu kitasa chake. Niliingia sehemu ya jikoni nika-
tokezea katika sebule ndogo yenye chumba cha kulia chakula pembeni yake.
Ile nyumba ilikuwa na samani za kisasa na hali hiyo ilinifahamisha kuwa
Jean Felix Akaga, mpelelezi wa kikosi maalumu kilichikuwa kikishughulika
na usalama wa rais wa Rwanda alikuwa ni mtu mwenye kipato cha kudhirisha.
IIikuwa ni nyumba yenye vyumba vitatu vya kulala, choo, maliwato, sebule
na sehemu ya jiko. Kwa muda mfupi nikawa nimeyazoea manzingira ya mle
ndani na kuridhika na usalama wake na hapo nikavua fulana yangu na kuitupa
sakafuni kisha nikaelekea vyumbani.
Nilianza kufanya upekuzi kwenye ile nyumba mle ndani na katika chumba
cha pili niligundua mle ndimo alimokuwa akiishi Rosine kwani mle ndani
nilifanikiwa kupata picha yake na zaidi ya hapo hapakuwa na kitu kingine cha
maana isipokuwa kabati moja liliyokuwa na nguo na lukuki ya vipodozi vya
kila namna. Chumba cha tatu na cha mwisho nilipowasha taa niligundua hara-
ka kuwa huenda kingekuwa ni chumba alichokuwa akiishi Jean Felix Akaga
na Diane. Ndani ya chumba kile sakafuni kulikuwa na zulia maridadi, kitanda
kipana na kizuri, makabati mawili ya nguo, seti moja ya runinga, meza ya
kusomea na kochi moja kubwa la sofa.
Niliyazungusha macho yangu mle ndani nikaziona picha mbili zilizokuwa
zimetundikwa ukutani, picha ya mwanamke na ya mwanaume. Nilianza kwa
kuitazama ile picha ya yule mwanamke na sikutaka kujiuliza kuwa yule aliku-
wa Diane yaani dada wa Rosine kwa namna walivyofanana. Kwa kweli Diane
alikuwa mzuri sana kama aliyokuwa mdogo wake, tabasamu lililochomoza
usoni mwake lilinifanya nijihisi ni kama ninayetazamana naye pale ukutani.
Niliitazama vizuri ile picha ya yule mwanaume nikaona ni kama niliyelinga-
na naye kwa umri, alikuwa amevaa suti nadhifu ya kijivu, shati jeupe na tai
shingoni.
Alikuwa mwanaume mwenye mvuto katika macho ya mwanamke yoyote
na sikuwa na mashaka kuwa ile picha ilikuwa ya Jean Felix Akaga. Kabla ya
kuendelea na udadisi zaidi niliyasogelea yale makabati na kulifungua mojawa-
po. Ndani ya kabati lile niliziona nguo za kiume zilizopangwa kwa unadhifu,
nilitabasamu kidogo baada ya kufikiria kuwa nilikuwa nimepata nguo za kuba-
dilisha. Nilisogea karibu na kioo cha kabati lile nikajitazama na kuridhika kwa
namna nywele na ndevu zangu zilivyokuwa na kuubadilisha kidogo ule mu-
onekano wangu wa wakati nilipokuwa nikiingia hapa jijini Kigali.
Kwa kitambo kidogo nilisimama mbele ya kioo kile nikijitazama bila akili
yangu kuwepo pale kwani mawazo juu ya Rosine yalikuwa yakianza kupita
upya kichwani mwangu na wakati huu nilianza kuhisi kupungukiwa na kitu
moyoni mwangu. Sijui ni kwanini nilikuwa nimetokea kumpenda sana Rosine
ingawa hapo nyuma niliwahi kukutana na wasichana wazuri wa kila sampuli
katika nchi tofauti tofauti nilizowahi kufika wakati nilipokuwa katika harakati
zangu za kijasusi.
Nilikumbuka wakati ule nilipokuwa na Rosine katika ile nyumba ya ma-
ficho kule msituni nikiwa nimelala juu ya kitanda kimoja na mrembo huyo
huku akiniruhusu kukitomasa tomasa kiuno chake na kuzifikicha chuchu zake
kifuani bila pingamizi lolote. Loh! kwa kweli hisia juu ya Rosine zilikuwa
zikinitafuna moyoni na sasa nilikuwa ndani ya nyumba hii bila yeye. Roho
iliniuma sana kwani sikufahamu kama Rosine alikuwa hai au mfu, na kama
alikuwa hai alikuwa wapi kwa wakati huu. Kwa kweli nilihisi upungufu wa
kitu fulani katika nafsi yangu.
Kwa muda wote ambao ningeendelea kuwepo nchini Rwanda nilikuwa
nimeazimia kuwa nyumba hii ingekuwa maskani yangu kwani sikuona sababu
ya kuingia gharama za kukaa kule hotelini, tena katika sehemu nisiyokuwa na
hakika ya usalama wake. Kitu cha kwanza nilichofikiria ilikuwa ni kuoga na
kubadilisha zile nguo zangu mwilini ambazo mpaka sasa zilikuwa chafu na
zinazonuka jasho. Hivyo nilivua nguo nikajifunga taulo nililolichukuwa mle
kabatini na kuingia bafuni.
Muda mfupi baadaye nilitoka bafuni na kujiandaa vizuri nikiwa na nguo
mpya na safi mwilini, nilipomaliza nilielekea kule jikoni na kufungua jokofu
lililokuwa na vyakula lakini vingi vikiwa vya kutoka kwenye maduka makub-
wa ya kisasa ama super market. Nikachukua pakiti mbili za soseji ya ng’ombe,
mayonaizi, vinega na karoti. Kulikuwa na trei moja ya mayai juu ya kabati la
vyombo lililokuwa mle jikoni hivyo nilichukuwa mayai mawili na kwa pamo-
ja nikatengeneza mlo kupitia jiko la gesi lilokuwa pale jikoni.
Ilikuwa imetimia saa nne kasoro usiku wakati nilipokuwa nimeketi mezani
kula. Nilijipatia mlo na kushiba vizuri kisha nikasukumia kwa mzinga mmoja
wa mvinyo mwekundu uliokuwa kwenye kabati la vinywaji lililokuwa mle
ndani pale sebuleni na wakati huo nilikuwa nimewasha runinga kubwa iliy-
okuwa pale ndani sebuleni nikitafuta stesheni inayorusha habari za nchi ya
Rwanda. Niligundua kuwa stesheni nyingi zilizokuwa zikipatikana kwenye
ile runinga zilikuwa zikirusha matangazo yake kwa lugha ya kifaransa huku
baadhi ya stesheni chache zikirusha matangazo yake kwa lugha ya kinyar-
wanda.
Hakukuwa na habari yeyote ya maana iliyonivutia katika stesheni niliyoi-
fungua isipokuwa stesheni moja tu iliyokuwa ikirusha habari kuwa rais wa
Rwanda Juvenal Habyarimana alikuwa amesafiri kwenda nchini Tanzania ku-
kutana na marais wengine wa nchi za ukanda wa maziwa makuu kuzungum-
zia masuala mbalimbali likiwemo suala la amani ya kudumu katika nchi ya
Rwanda na Burundi na masuala mengine ya kiuchumi. Taarifa zile ziliendelea
kueleza kuwa katika msafara huo wa rais kwenye ndege yake Falcon 50 Jet
angeambatana na mkuu wake wa majeshi Deogratias Nsabimana na mkuu wa
usalama wa rais Kanali Elie Sagatwa.
Nilipoitafakari taarifa ile nikajikuta nikifurahi kwa namna viongozi wetu
wa Afrika walivyokuwa wakishirikiana kama ndugu wa familia moja katika
kuziletea maendeleo nchi zao. Kisha vikafuatia vipindi vingine vya runinga
ambavyo havikuonekana kunivutia hivyo niliamua kuizima ile runinga pale
sebuleni. Nilihisi kuwa akili yangu ilikuwa imepata utulivu wa kutosha wa
kuweza kutafakari hili na lile na kutengeneza hoja zenye msingi na wakati nili-
pokuwa nikitafakari nikaikumbuka ile bahasha ya kaki niliyoichukua chini ya
godoro kwenye kile chumba cha mwenyeji wetu ndani ya ile nyumba iliyoku-
wa kule katikati ya ule msitu. Wazo hilo likanifanya ninyanyuke na kuelekea
kule chumbani nilipoiacha ile suruali yangu niliyotokanayo kule msituni am-
bamo ile bahasha ilikuwa ndani ya mfuko wa suruali hiyo.
Muda mfupi baadaye nikawa nimerudi na ile bahasha pale sebuleni na hapo
nikaketi kwenye kochi. Kabla ya kuifungua ile bahasha niliyapitisha macho
yangu nikiichunguza kwa juu hata hivyo sikufanikiwa kuona kitu chochote
mle ndani kwani ile bahasha ilifungwa kwa gundi kali na karatasi yake hai-
kuruhusu macho yangu kupenya na kuona ndani. Hivyo nikaichana ile baha-
sha kwa juu na kuchungulia ndani na hapo nikaiona karatasi yenye rangi ya
samawati. Mwanzoni nilipoichunguza ile karatasi haikuwa na maana yoyote
kwangu kwani sikuweza kuona chochote kilichoandikwa kwenye karatasi ile.
Hata hivyo mimi sikuwa mshamba wa karatasi za namna ile hasa pale nili-
pofikiria kuwa hakuna binadamu mwenye akili timamu ambaye angetumbuki-
za karatasi isiyo na kitu ndani ya bahasha na kuifunga kwa gundi kali namna
ile.
Baada ya kuigeuzageuza ile karatasi na kuichunguza vizuri nikajikuta niki-
tabasamu. Ilikuwa ni aina fulani ya karatasi inayotumiwa sana na majasusi ka-
tika kupashana habari. Karatasi ambayo ili kuweza kuyasoma maelezo ndani
yake nilihitajika niwe na kalamu ya grafati. Kupitia kalamu hiyo ningeilaza
ile karatasi juu ya meza au juu ya kitu chochote kilichonyooka vizuri halafu
baada ya hapo ningeanza kuichorachora ile karatasi huku nikiwa nimeilaza
kalamu hiyo ya grafiti katika pembe isiyozidi nyuzi ishirini na tano ili niweze
kupata taswira nzuri ya kilichoandikwa ndani ya karatasi husika. Kwa kawaida
karatasi ya namna hii zinapotumwa kwa mhusika hutumwa pamoja na kalamu
yake maalumu.
Kwa kulikumbuka hili nilizidi kuifungua ile bahasha na muda si marefu
kweli nikaiona kalamu ndogo ya grafiti iliyochongwa vizuri. Niliichukua ile
kalamu kisha nikachukua kitabu fulani kilichokuwa kwenye rafu pale sebuleni
na juu ya kitabu hicho nikailaza ile karatasi kisha nikaanza kuichorachora ile
karatasi kwa ule wino wa ile kalamu ya grafiti.
Mwanzoni nilidhani kuwa ile karatasi ingekuwa na mchoro fulani wa siri
ambao zingehitajika jitahada za kipekee katika kuutafsiri ili kuweza kuuele-
wa maana yake kwani mara nyingi karatasi za namna hii hutumika kupeleka
ujumbe kwa njia ya mchoro. Lakini kadiri nilivyokuwa nikizidi kuichorachora
karatasi ile nikawa naanza kuona herufi, nilipozidi kuchora zaidi herufi zile
zilianza kuunganika na kutengeneza sentensi fulani.
Niliendelea kuichora ile karatasi hadi mwisho na nilipomaliza nikaona mu-
unganiko wa sentensi kamili inayoleta maana ingawaje sentensi hiyo haikuwa
na maana kamili kwangu. Sentensi yote kwenye karatasi ile ilikuwa imeandik-
wa kwa lugha ya kifaransa ikisomeka,
“Mecred recontre avec elle en Halfmoon bar à 22:00hrs avant de nous com-
mencer, chaque chose est soyez bien”
Kwa kutuumia karatasi ileile nikaigeuza nyuma na kuanza kutafsiri neno
moja baada ya jingine kwa lugha yangu ya kiswahili na nilipomaliza nikawa
nimepata tafsiri kamili ya maneno yale ambayo yalimaanisha kuwa,
“Jumatano onana naye ndani ya Halfmoon bar saa nne usiku kabla hatu-
jaanza. Kila kitu kipo tayari”
Nilipomaliza kusoma sentensi hiyo moyo ulikuwa ukinienda mbio sana
na sikuweza kufahamu ni kwanini hali ile ilikuwa ikinitokea. Niliendelea
kuichunguza chunguza tena ile karatasi hata hivyo sikuweza kuliona jina la
mwandishi wala mtumiwaji wa ujumbe ule. Ila kwa kuwa nilikuwa nime-
ichukua ile bahasha toka chumbani kwa yule mwenyeji wetu aliyejinadi kwa
jina la Innocent Gahizi kwenye ile nyumba kule msituni hivyo niliamini kwa
vyovyote mtumiwaji angekuwa ni yeye.
Niliendelea kutafakari ujumbe ule kwenye ile karatasi bila kupata maana
yoyote kamili inayonipa picha ya nini kilichokuwa kikiendelea. Nilitembe-
za macho yangu kuitazama kalenda iliyokuwa imetundikwa pale sebuleni na
hapo moyo wangu ukapiga kite kwa nguvu kwani siku ile ilikuwa ni siku ya
jumatano kwa mujibu wa kalenda ile ilivyoonesha, yaani siku ambayo ujumbe
ule ilikusudiwa kufanyiwa kazi. Nikageuka kuitazama saa ya ukutani pale se-
buleni, tayari ilikwisha timia saa tatu na robo usiku hivyo zilikuwa zimesalia
dakika arobaini na tano tu kutimia saa nne usiku muda wa miadi.
Nikavuta pumzi nyingi na kuitoa taratibu huku nikianza kuhisi kuwa kuliku-
wa na hatari kubwa iliyo kuwa mbele yangu endapo ningeamua kujitumbukiza
katika mkasa huu usioeleweka. Hata hivyo kulikuwa na kitu kilichokuwa kiki-
nisukuma moyoni kuwa nisimame na kuanza kuitafuta Halfmoon Bar. Kingine
kilichonisukuma kutaka kufuatilia mkasa huu ni pale nilipowaza kuwa kwa
vyovyote mtu aliyekusudiwa kuupata ujumbe huu hadi wakati huu alikuwa
bado hajausoma na kuuelewa maana yake kwani mimi ndiye niliyekuwa mtu
wa kwanza.
Hivyo nilikuwa na hakika kuwa ndani ya hiyo Halfmoon Bar huo muda wa
saa nne usiku kungekuwa na mtu fulani anayemsubiri huyo mtu mwingine am-
baye bila shaka mtu huyo anayesubiriwa ndiye huyo ambaye ujumbe huu uli-
kusudiwa kwake. Na kwa kuwa mhusika huyo alikuwa bado hajaupata ujumbe
huu asingeweza kufika kwenye miadi na badala yake mimi ndiyo ningeitumia
nafasi hiyo. Niliendelea kuwaza nikapiga moyo konde na kusimama. Akili
yangu yote sasa ilikuwa ni wapi ambapo ningeipata hiyo Halfmoon Bar hapa
jijini Kigali.
__________
 
NILIIACHA NYUMBA ILE NIKIWA NIMEZIMA TAA zote na kuweka
kila kitu mahali pake kama nilivyokuta. Mbali na hayo pia nilikuwa nime-
andika ujumbe mfupi kwenye karatasi ndogo niliyoiweka chini ya sabuni ya
kuogea bafuni. Karatasi hiyo ikimuuleza Rosine kuwa kama angefika mle
ndani ajue kuwa mimi pia nilikuwa pale kwenye ile nyumba hivyo aendelee
kunisubiri. Vilevile nilikuwa nimechukua namba ya simu ya ile nyumba ili
ikitokea kuwa endapo ningechelewe niweze kupiga simu kuuliza kama Ros-
ine angekuwa amefika. Sikujua ni kwanini nilisukumwa kuichukua namba ya
simu ya nyumba ile lakini bado nilikuwa na imani kuwa ningeonana tena na
Rosine kabla ya kifo changu hapa duniani.
Nilikuwa na kiasi kidogo cha pesa nilizozichukua toka katika droo ya kabati
kwenye kile chumba nilichohisi kuwa huenda walikuwa wakiishi dada yake
Rosine yaani Diane na mumewe ambaye sasa nilikuwa nikimfahamu kwa jina
Jean Felix Akaga. Wakati nikiiacha ile nyumba na kuingia mtaa wa pili nilir-
idhika na muonekano wangu mpya wa mavazi ya kawaida usioweza kuyavuta
macho ya mtu yoyote. Nywele na ndevu zangu zilikuwa zimekua kiasi cha
kuweza kuubadilisha muenekano wangu mbele ya macho ya mtu yoyote anay-
enifahamu na kofia niliyokuwa nimeivaa nilikuwa na hakika kuwa mtu yeyote
asingenigundua kirahisi.
Nilitembea kwa muda wa zaidi ya dakika kumi kutoka barabara ya mtaa wa
kwanza hadi ile ya mtaa wa pili kisha nilikunja kona kuelekea upande wa kulia
na mwisho wa barabara hiyo nikachepuka kuingia upande wa kushoto mah-
ali kulipokuwa na kichochoro kidogo chenye giza hafifu. Wakati nikitembea
niliweza kuziona baadhi ya nyumba zikiwaka taa kwa ndani kuashiria kuwa
wenyeji wa nyumba hizo walikuwa bado hawajalala.
Kichochoro nilichoingia kilinichukua hadi upande wa pili kulipokuwa na
barabara kubwa ya lami na nilipofika kwenye barabara hiyo niligundua kuwa
muda ulikuwa umesonga kutokana na uchache wa magari katika barabara ile.
Hali hiyo ilinitahadharisha kuwa ingekuwa vigumu kidogo kupata usafiri wa
mabasi ya umma wa kunifikisha maeneo ya katikati ya jiji ambapo niliami-
ni kuwa hiyo Halfmoon bar ingekuwa rahisi kujulikana. Hata hivyo sikukata
tamaa hivyo nilivuka barabara ile na kuanza kutembea kandokando nikiufuata
ule uelekeo wa barabara inayoelekea katikati ya jiji la Kigali.
Baada ya mwendo mfupi wa miguu nikawa nimefika eneo moja lililokuwa
na bar fulani kando ya barabara. Nje ya bar hiyo kulikuwa na teksi chache
zilizoegeshwa hivyo niliiendea taksi moja iliyokuwa imejitenga kidogo na
eneo lile. Dereva wa teksi ile alinipokea kwa bahasha zote na kunifungulia
mlango.
“Nipeleke ilipo Halfmoon bar? nilimwambia yule dereva bila kudadisi
kuwa alikuwa akielewa lugha ya kiswahili au lah!. Dereva ayatuliza macho
yake kama anayefikiria jambo kisha akatamka
“Sina hakika sana kama naifahamu hiyo bar lakini hilo jina siyo geni ma-
sikioni mwangu, nahisi hiyo bar ipo katikati ya jiji sehemu fulani, twende
tutauliza hatuwezi kupotea” yule dereva aliniambia katika lugha ya kiswahili
chenye lafudhi ya kikongomani, nikajua alikuwa ni mtu mwenye asili ya nchi
ya Congo. Hapakuwa na maongezi tena baina yetu wakati teksi ile ilipokuwa
akiymtia maegesho yake na kuingia barabarani kuufuata uelekeo wa mjini.
__________
TEKSI ILISIMAMA KIASI CHA UMBALI WA HATUA ISHIRINI kab-
la ya ilipo Halfmoon Bar eneo la Remera jijini Kigali. Wakati nilipoitupia
macho saa ndogo iliyokuwa kwenye dashibodi ya gari mle ndani nilifurahi
kuona kuwa zilikua zimesalia dakika kumi na mbili kabla ya kutimia saa nne
usiku. Moyoni nilimshukuru sana yule dereva wa teksi kwa kuwa mjanja wa
kuvijua vitongoji vingi vya jiji la Kigali. Hadi kufikia mtaa ule tulishavipita
vitongoji vingi vya jiji la Kigali kama vile Nyamirambo, Kicukiro, Kacyiru,
Kwa Rubangura, Nyabugogo, Jali, Nyarutama na vinginevyo vingi. Na tuli-
kuwa tumetumia muda mfupi mno kutokana na dereva yule kuwa na ufahamu
mzuri wa maeneo yale na vichochoro vyake. Ni katika kuulizauliza hatimaye
tukaelekezwa na mtu mmoja aliyekuwa akiifahamu vizuri Bar ile.
Nilimlipa dereva wa teksi pesa yake nikamshukuru na kushuka huku nikii-
acha teksi ile ikipotelea mitaani. Mtaa ule ulikuwa upo miongoni mwa mitaa
iliyokuwa ikithaminiwa vizuri na Meya wa jiji la Kigali. Ulikuwa ni mtaa
uliochangamka na wenye afya njema kama barabara pana ya lami iliyokatisha
katikati ya majengo marefu ya ghorofa, migahawa ya kisasa, maduka ya nguo
na ofisi za benki.
Halfmoon Bar ilikuwa kando ya jengo la benki ya taifa ya Rwanda hivyo
nilitembea nikalipita jengo lile la benki na kuelekea ilipo Bar ile na wakati
nikiikaribia ile Bar niliyaona magari mawili madogo yakiwa yameegeshwa
nje ya Bar hiyo. Sikuwa na shaka yoyote kuwa Halfmoon Bar ilikuwa ipo
kwenye orodha ya Bar za kisasa kabisa zilizokuwa jijini Kigali kutokana na
muonekano wake wa nje. Bango kubwa lenye maandishi yanayowaka taa
yakisomeka “Halfmoon Bar–Bien venu”-neno la kifaransa lenye maana ya
“Karibu Halfmoon Bar” liliamsha hisia mpya moyoni mwangu kuwa niliku-
wa nimefika eneo sahihi kabisa.
Wakati nilipokuwa nukiusukuma mlango na kuingia ndani ya Halfmoon
Bar nilipishana na watu wawili wapenzi, mwanamke na mwanaume waki-
wa wamekumbatiana viunoni. Niligeuka kidogo nikawatazama na hapo nik-
agundua kuwa walikuwa wamelewa sana kutokana mwendo wao wa kuyum-
bayumba na harufu kali ya pombe iliyopenya toka vinywani mwao baada ya
jaribio lao la kunisalimia kilevilevi kutofanikiwa vizuri.
Niliingia mle ndani ya Bar huku nikiuacha mlango ukijifunga taratibu nyu-
ma yangu na hapo nikajikuta nikitazamana na macho ya mhudumu mmoja
wa Bar ile aliyekuwa amesimama pembeni ya kaunta ya vinywaji. Sikupenda
kuonesha ugeni wa namna yeyote mle ndani hivyo nilichagua meza moja iliy-
okuwa nyuma ya mlango na kuketi. Mhudumu alipokuja nikamuagiza aniletee
kinywaji baridi kisicho na kilevi na wakati akiondoka nikapata wasaha mzuri
wa kuyatembeza taratibu macho yangu mle ndani.
Ile bar ilikuwa ya kisasa sana na yenye meza kumi na mbili kila meza moja
ikizungukwa na viti vitano vya mbao aina ya mkangazi. Ndani ya Bar ile
upande wa kulia kulikuwa na ukumbi mdogo wa muziki uliotenganishwa na
sehemu hii niliyokaa kwa pazia kubwa lililotengenezwa kwa simbi nyingi za
baharini zilizotungwa kamba nyembamba katikati. Taa za rangi tofauti zili-
kuwa zikimulika mle ndani na muziki laini wa rumba ya kilingala uliokuwa
ukitumbuiza taratibu.
Katika sehemu ile niliyokaa hapakuwa na watu wengi kwani ni meza saba
tu ndiyo zilizokuwa na wateja ambao wengi wao walionekana kuwa wapenzi
na meza mbili tu ndiyo zilionekana kukaliwa na mtu mmoja mmoja, zaidi ya
hapo sikuona sura yoyote ya kuitilia mashaka mle ndani.
Niliyazungusha macho yangu tena kwenye kuta za Bar ile nikitarajia kuiona
saa ya ukutani lakini sikufanikiwa kwani hakukuwa na saa yoyote mle ndani
na hali hiyo ikanifanya niikumbuke ile saa yangu ya mkononi iliyochukuliwa
na wale wanajeshi wa Kanali Basco Rutaganda kule mapangoni. Nilikilaani
sana kitendo kile kwani miongoni mwa vitu nilivyokuwa nikivijali sana katika
maisha yangu basi muda ulikuwa miongoni mwavyo. Hivyo nilibaki nimetulia
pale kwenye ile meza huku nikitafakari hili na lile hata hivyo niliendelea kuji-
fariji kuwa bado nilikuwa ndani ya ule muda wa miadi.
Mawazo yangu yakakatishwa na sinia dogo lililowekwa mbele yangu juu ya
meza likiwa na chupa moja ya kinywaji na bilauri moja ndefu. Mhudumu yule
akatabasamu kidogo na kunifungulia kinywaji
“Are you waiting for someone? yule mhudumu aliniuliza kwa lugha ya kiin-
gereza
“No” nikamjibu na kabla hajaondoka nikawahi kutumbukiza mkono mfu-
koni na kuchukua noti moja kisha nikampa kama malipo ya kinywaji kile.
Yule mhudumu aliipokea ile noti ya fedha ya kinyarwanda huku akionesha
kila dalili za kutaka kuendeleza maongezi na mimi lakini nilijitahidi kwa kila
namna kumkwepa kwani maongezi yangeweza kunoga na kunipotezea umak-
ini wa kazi yangu. Hivyo yule mhudumu alipoona kuwa sielekei kutengeneza
urafiki naye akachukua lile sinia la vinywaji na kuondoka zake na hapo mimi
nikamimina kinywaji kile kwenye bilauri na kuanza kunywa taratibu huku
macho yangu yakiweka kituo kwenye ule mlango kutazama kila mtu aliyeku-
wa akiingia ndani ya Bar ile.
Alikuwa ni mtu wa tano kuingia nyuma ya watu wanne waliotangulia kuingia
mle ndani tangu mimi nilipoingia ndani ya Bar ile wakati nilipoyazungusha
macho yangu na kumtazama msichana mzuri na mrembo ajabu aliyeongeza
idadi ya wasichana wachahe niliyowahi kuwaona katika harakati zangu. Msi-
chana yule alikuwa amevaa suruali nyeusi ya jeans iliyolichora vema umbo
lake la msichana wa kiafrika mwenye kiuno chembamba, mzigo wa makalio
ya wastani unaopendeza kwa mtazamaji na mapaja yenye minofu ya kutosha.
Matiti yake madogo yasiyokuwa na uwiano mzuri na umbo lake yalihifadhi-
wa vyema kifuani mwake kwa blauzi nyepesi na nyeupe iliyozionesha vizuri
chuchu zake nyeusi zilizotuna. Mkufu wake unaometameta uliizunguka vizuri
shingo yake ndefu na nyembamba ukipotelea katikati ya matiti yake. Mkufu
huo ulinishtua na kunifanya nimtazame usoni yule mrembo ambaye sasa nil-
ianza kuhisi kuwa hakuwa mgeni sana machoni mwangu. Nikajitahidi kukum-
buka sehemu nilipowahi kumuona hata hivyo akili yangu ilishindwa kuniletea
majibu ya haraka.
Mara baada ya kuingia ndani ya ile Bar yule msichana alisimama na
kuyatembeza macho yake taratibu kutazama kila meza iliyokuwa mle ndani na
wakati alipogeuka upande wangu mimi niliwahi kuishusha kofia yangu chini
kisha nikaikamata bilauri ya kinywaji na kugida mafunda kadhaa nikikiacha
kinywaji kile kikiteleza taratibu kooni mwangu kama mtu ambaye nimezama
katika hamsini zangu. Nilipoinua kichwa tena kumtazama yule mrembo ali-
kuwa tayari amegeukia upande mwingine wa Bar ile na hapo ndiyo nikapata
nafasi nzuri ya kuendelea kumchunguza. Miwani nyeusi aliyoivaa ikaninyima
nafasi nzuri ya kumdadisi ingawaje mara hii pia moyo wangu ulipiga kite kwa
nguvu ukunikumbusha kuwa sura yake haikuwa ngeni sana kwangu.
“Ni wapi vile nimemuona huyu mrembo? nilinong’ona kama bwege na
wakati huu zile kumbukumbu chache zilizosalia kichwani mwangu kuhusu
yeye ziliyeyuka kabisa na kuniacha katika mduwao wa kizembe. Nywele zake
halisi za kipilipili alikuwa amezikata katika mtindo wa kipekee kwa msichana
wa kiafrika uitwao Low cut ambao kwa kweli mtindo ule ulikuwa amezidi
kuupalilia uzuri wake wa urefu wa wastani, huku pochi yake nzuri ya ngozi
ikiongeza zaida katika mwonekano wake.
Kama mtu aliyeitarajia ishara fulani kutoka kwa mmoja wa watu walioke-
ti mle ukumbini hilo halikutokea na kwa namna moja au nyingine hali hiyo
ilionekana kumshangaza sana. Hisia tofauti zikaanza kuumbika kichwani
mwangu kuwa mtu niliyekuwa nikimsubiri huenda angekuwa ndiye yule mr-
embo aliyeingia.
Yule mrembo aliendelea kutazamatazama huku na kule mle ndani na ali-
poona kuwa kila mtu alikuwa akiendelea na hamsini zake akachagua meza
moja ya jirani na kuketi. Mhudumu alikuja na kumsikiliza na muda mfupi
baadaye niliona akipelekewa kinywaji lakini sikutaka kuamini kuwa kinywaji
kile ndiyo kitu kilichokuwa kimemleta ndani ya ile Bar. Wakati yule mrem-
bo akijipatia kinywaji taratibu nilimuona mara kwa mara akinyanyua mkono
wake kuitazama saa yake ya mkononi na kisha akigeuka na kutazama katika
ule mlango wa kuingia mle ndani ya ile Bar huku akionekana mwenye haraka
na wasiwasi.
Kulikuwa na watu waliokuwa wakiendelea kuingia mle ndani ya Bar na
vilevile walikuwepo pia watu wengine walioonekana kutosheka na starehe
zao na hivyo kuamua kuondoka, na suala hilo halikuonekana kutiliwa maanani
hata kidogo na mrembo yule. Badala yake aliendelea kuitazama saa yake ya
mkononi na baadaye kutazama pale mlangoni mara kwa mara.
Ulipita muda mrefu yule mrembo akiendelea na zoezi hilo na nilianza kuhisi
kuwa alikuwa mbioni kukata tamaa na hali ile. Mwishowe nilimuona akisi-
mama kisha akaelekea pale kaunta na wakati akielekea kaunta aliyatembeza
tena macho yake kuwatazama watu waliokuwa mle ukumbini. Muda mfupi
baadaye nilimuona akirudi kutoka kule kaunta huku akiufuata ule uelekeo wa
mlango wa kutokea na hapo nikatambua kuwa alitoka kule kaunta kulipa bili
ya kinywaji na sasa alikuwa akiondoka. Nikapata nafasi nyingine nzuri ya
kumchunguza wakati akitembea kuelekea nje na bado hisia zangu ziliendelea
kunieleza kuwa hakuwa mtu mgeni machoni mwangu.
Nilimalizia funda la mwisho la kinywaji kilichosalia kwenye bilauri yan-
gu na nilipoiweka bilauri ile mezani nikasogeza kiti nyuma na kusimama na
hapo nikaanza kuufuata ule mlango wa kutokea nje. Yule msichana mrembo
alikwishatoka nje na sikutaka aniache mbali sana hivyo nilipotoka tu nje nik-
agundua kuwa usiku ulikuwa umeshamiri. Kulikuwa na giza zito lililoashiria
kuwa mvua ilikuwa mbioni kunyesha tena hata hivyo kwa msaada wa taa za
barabarani zilizokuwa kando ya barabara kwenye nguzo ndefu, giza lile zito
liligeuka mchana kwa baadhi ya sehemu.
Nilishangaa kutomuona yule msichana pale nje hivyo nikawahi kuvuka
barabara upande wa pili uliotazamana na ile Bar na hapo nikumuona. Yule
mrembo alikuwa akitembea haraka haraka katika mtindo wa mashindano ya
urembo yaani Catwalk na sasa alikuwa ameshalipita lile jengo la benki ya taifa
la Rwanda. Nilimuona mara kwa mara akigeuka nyuma kutazama na mimi si-
kutaka kupoteza muda hivyo kwa haraka nikavuka tena ile barabara na kuanza
kumfuatilia kwa nyuma lakini katika namna ambayo nilikuwa na hakika kuwa
asingeweza kunishtukia. Alikuwa akijua namna ya kutembea haraka na aliku-
wa mwangalifu sana katika nyendo zake lakini hakuwa zaidi yangu. Alikuwa
zaidi ya umbali wa mita thelathini mbele yangu, umbali mzuri ulionifanya
niweze kujificha haraka kila alipokuwa akijiandaa kugeuka nyuma.
Alipofika mwisho wa barabara ya mtaa ule akaingia upande wa kulia akii-
fuata barabara nyingine ya lami iliyokatisha katikati ya mtaa mwingine wenye
maduka mengi ya nguo na baadhi ya sehemu nyingine za starehe. Alipofika
karibu na jengo la ukumbi wa sinema akasimama kidogo na kugeuka tena nyu-
ma akitazama katika namna ya kujiridhisha kuwa hakukuwa na mtu yoyote
aliyekuwa akimfuatilia nyuma yake.
Aliporidhika kuwa hakukuwa na mtu nyuma yake akavuka barabara upa-
nde wa pili na wakati akifanya hivyo ghafla nililiona gari dogo aina ya Volvo
likiacha maegesho ya ukumbi ule wa sinema uliokuwa pale jirani na kuufuata
ule uelekeo wa yule msichana mrembo alipokuwa. Gari lile lilienda kusimama
hatua chache pembeni ya yule msichana mrembo na hapo nikaelewa ni nini
kilichokuwa kikiendelea mbele yangu. Lile gari liliposimama tu yule msicha-
na akafungua mlango wa nyuma na kuingia ndani na hapo safari ikaanza lile
gari likiufuata uelekeo wa barabara iendayo kando ya mji.
Lilikuwa tukio ambalo sikulitarajia na lilikuwa limeniacha katika mduwao
usioelezeka huku nikihisi kuwa nilikuwa nimezidiwa ujanja hata hivyo sikuta-
ka kukubaliana mapema na hali ile hivyo nikaharakisha kuyaendea maegesho
ya magari ya ule ukumbi wa sinema. Nilimkuta dereva mmoja wa teksi akiwa
tayari kwani alikuwa ameniona tangu nilipokuwa mbali nikiharakisha kuja
eneo lile.
Nilipoifikia teksi ile nikafungua mlango wa nyumba na kuingia na kabla
yule dereva hajaniuliza uelekeo wangu nikamwambia aifuate ile gari aina ya
Volvo iliyoondoka pale kwenye yale maegesho muda mfupi uliyopita. Dereva
yule alinielewa na bila shaka kumbukumbu ya uelekeo wa lile gari ilikuwa
bado ipo vizuri kichwani mwake kwani muda uleule akayaacha yale maegesho
na kuingia barabarani akiufuata ule uelekeo wa lile gari. Na wakati tukiondoka
eneo lile nilimuonya yule dereva kuwa awe mwangalifu ili watu waliokuwa
ndani ya lile gari mbele yetu wasiweze kutushtukia kuwa tunawafuatilia.
Muda mfupi baada ya safari yetu kuanza nikagundua kuwa nilikuwa nimem-
pata dereva mjanja na mwerevu anayevitambua vizuri vitongoji na vichochoro
vya jiji la Kigali. Nilifahamu hivyo baada ya kumuona akiiacha ile barabara
niliyoiona ile gari aina ya Volvo ikielekea kisha akakunja kona kuingia upande
wa kushoto. Nikataka kumuuliza ni kwanini alikuwa akifanya vile na wakati
nikijiandaa kumuuliza tukawa tumikwisha tokezea upande wa pili wa mtaa
mwingine katika barabara iliyokatisha katikati ya majengo marefu ya ghorofa.
Tulipofika kwenye mtaa huo yule dereva akakatisha tena kwenye barabara
hafifu iliyoonekana kutotumika sana. Barabara hiyo ilikatisha katika ya kituo
kidogo cha kujazia mafuta halafu mbele kidogo tukachepuka upande wa kulia
wa barabara hiyo ikituchukua moja kwa moja hadi mbele ya jengo la ofisi za
wizara ya mambo ya ndani ya nchini Rwanda. Tukawa kama tunaotaka kuto-
kezea mbele ya jengo hilo lakini tulipokuwa tukilikaribia dereva alichepuka
tena upande wa kushoto na barabara hiyo ikatuchukua muda mfupi tu kuto-
kezea mbele ya barabara nyingine ya lami ielekeayo kando ya mji, na wakati
tukikaribia kuifikia barabara hiyo mara tukaiona ile gari aina ya Volvo iliyom-
chukua yule msichana ikikatisha mbele yetu.
Nikashangaa sana na kumuuliza yule dereva kuwa alijuaje kama gari lile
Volvo lingetokezea maeneo yale. Dereva alitabasamu kidogo na kuniambia
kuwa barabara ile iliyopita lile gari aina Volvo haikuwa na sehemu nyingine ya
kukatishia. Ilikuwa ni barabara ya moja kwa moja hivyo yule dereva alikuwa
na hakika kuwa angekuja kukutana na lile gari sehemu ile. Yule dereva alipun-
guza mwendo akisubiri lile gari lipite kisha akaiingia kwenye ile barabara na
kulifungia mkia kwa nyuma.
Tulikuwa tumesafiri umbali wa maili kama tatu tukiliacha jiji la Kigali nyu-
ma yetu wakati tulipoliona lile gari mbele yetu likiwasha taa kuashiria kuwa
lilikuwa linataka kukata kona kuingia upande wa kulia. Nikamtaka yule dere-
va wa teksi apunguze mwendo na hapo tukaliona lile gari mbele yetu likiingia
upande wa kulia kuifuata barabara chakavu ya lami yenye mashimo mashimo.
Barabara ile ilipakana na vichaka na mapori ya hapa na pale hali iliyopelekea
barabara ile itawaliwe na giza nene. Tukio lile likanipelekea nimwambie dere-
va wangu kuwa azime taa za gari na kuendesha taratibu kulifuata lile gari.
Lile gari mbele yetu liliendelea kusafiri kwenye barabara ile yenye mashi-
mo na madimbwi ya mji na dereva wangu alikuwa makini sana kulifuatilia.
Baada ya umbali mfupi kiasi mara tuliliona tena lile gari likipunguza mwendo
na hatimaye kukata kona likiingia upande wa kushoto. Kiasi cha umbali wa
hatua hamsini mbele yetu lile gari lilipunguza mwendo na hatimaye kusimama
mbele ya geti kubwa jekundu lililoshikiliwa na kuta ndefu zilizojengwa kuizu-
nguka nyumba ya ghorofa tatu.
Tukiwa tumesimama umbali mfupi toka pale lilipokuwa lile gari mbele yetu
nilimwambia dereva wangu azime injini ya gari. Dereva alikuwa mwepesi ku-
nielewa akafanya kama nilivyomwagiza na hapo nikamuuliza kuwa ni pesa
kiasi gani alikuwa akinidai kama malipo ya umbali wa kutoka kule nilikom-
kodi. Yule dereva akaniambia kiasi cha pesa na bila kupoteza muda nikamlipa
na kumzidishia kidogo nikijenga uaminifu kwake. Akazipokea zile pesa na
kunishukuru huku nikimtaka ageuze gari lake na aende akanisubiri kule kando
ya barabara ile ya lami kabla ya kuchepuka na kuingia kwenye barabara hii ya
vumbi iliyotufikisha pale.
Nilikuwa nimemuahidi dereva yule kuwa ningerudi baada ya muda wa
nusu saa na kuwa endapo angeona muda huo umepita bila ya mimi kutokea
basi alikuwa huru kuondoka. Sote tulisubiri mpaka pale lile gari mbele yetu
liingie ndani ya ile nyumba na haukupita muda mrefu dereva wa lile gari
mbele yetu alipiga honi na muda mfupi baadaye tuliliona lile geti la ile nyum-
ba likifunguliwa na lile gari likaingia ndani. Ingawaje ulikuwa usiku lakini lile
geti lilipokuwa likifunguliwa ili kuliruhusu lile gari aina ya Volvo kuingia nili-
pata nafasi ya kuona mle ndani ya lile geti. Ilikuwa nyumba ya kisasa yenye
mazingira mazuri ya kuvutia ingawaje kitendo cha kufungwa haraka kwa geti
lile mara baada ya lile gari kuingia ndani kuliniacha katikati ya udadisi wangu.
Kwa kuhofia kukutwa eneo lile nilishuka haraka nikiiacha ile teksi ikigeuza
na kurudi kule tulipotoka. Moyo wangu ulikuwa ukienda mbio sana na si-
kuweza kuhisi nini ambacho kingenitokea mbele yangu hata hivyo hilo ha-
likunizuia kuendelea na harakati zangu. Mara baada ya kushuka kwenye ile
teksi nilianza kutembea taratibu kuifuata ile nyumba amabayo lile gari Volvo
lilipoingia huku nikiwa tayari nimeishika bastola yangu mkononi.
Ile nyumba ya ghorofa ilikuwa imezungukwa na miti mirefu na mikubwa
na wakati nikitembea niliweza kuzisikia sauti za ndege toka juu ya miti hiyo.
Nilijiuliza ni kwanini nyumba ile ilikuwa imejengwa mafichoni katika eneo
lililojitenga na makazi ya watu kama lile na sikuweza kupata majibu. Niligeu-
ka kutazama nyuma na pembeni yangu na sikuweza kumuona mtu yoyote eneo
lile ingawaje mwanga wa taa kubwa zilizopandwa juu ya ukuta wa ile nyumba
uliniwezesha kwa kiasi fulani kuyasoma mazingira ya eneo lile. Niliendelea
kutembea kwa tahadhari nikielekea mbele ya lile geti huku nikitazama huku
na kule kuutathmini usalama wa eneo lile.
Hatua tatu tu nilizoziputa mbele yangu kulikaribia geti la nyumba ile nil-
ishtukia kuwa kulikuwa na kamera mbili zilizokuwa zimepandwa juu ya geti
lile zenye uwezo wa kunasa picha ya kitu chochote mbele ya jengo lile. Kwa
kushtukia hilo nikachepuka na kupotelea gizani kwenye mti mkubwa uliyoku-
wa jirani na geti lile. Kupitia giza lililofanywa na matawi ya miti iliyoizunguka
ile nyumba niliweza kuzunguka taratibu kwa nje nikiuchunguza ukuta mrefu
uliyoizunguka ile nyumba.
Ulikuwa ni ukuta mrefu na wenye seng’enge maalumu juu yake inazomzuia
mtu yoyote kupenya kwa urahisi endapo mtu huyo angefanikiwa kufika juu ya
ukuta huo, na kwa kweli hali hiyo ilinikatisha tamaa juu ya namna ya kuingia
ndani ya nyumba ile. Niliendelea kuzunguka huku nikiuchunguza ule ukuta na
nilipoona kuwa hapakuwa na mwanya wowote wa kuniruhusu kuingia ndani
ya nyumba ile nikapata wazo jipya.
Niliichunguza ile miti mirefu na mikubwa iliyoizunguka ile nyumba nikiwa
nimepata wazo lenye tija baada ya kugundua kuwa baadhi ya matawi ya ile
miti yalikuwa yameinga ndani ya ule ukuta mrefu wa ile nyumba. Hali ile ika-
nipa faraja kiasi kwani nilianza kupata tumaini la kuyatumia matawi yale ku-
penya na kuingia mle ndani ya ile nyumba. Wazo hilo likanifanya nianze tena
kuizunguka ile nyumba na baada ya muda mfupi nikagundua kuwa kulikuwa
na mti mmoja ulioonekana kuwa rahisi kidogo kuupanda nyuma ya nyumba
ile. Nilipoufikia ule mti nilichunguza usalama wa eneo lile na niliporidhika
kuwa hali ilikuwa poa nikaanza kuukwea ule mti.
Haikuwa kazi ngumu kuukwea mti wa namna ile kwangu kwani tayari nil-
ishawahi kukwea miti mingi ya namna ile katika harakati zangu za kijasusi pia
mafunzo mengi ya kijeshi niliyowahi kuyapitia yalikuwa yamenifunza vizuri
namna rahisi zaidi ya kukwea mti kwa muda mfupi. Hivyo kwa muda mfupi
nikawa nimefanikiwa kuukwea ule mti lakini katika namna isiyoweza kukish-
tua kiumbe chochote ambacho kingekuwa eneo lile.
Nilipofika juu ya ule mti nilichagua tawi moja zuri lililoning’inia ndani ya
ukuta wa ile nyumba lakini kabla sijafanya maamuzi ya kulitumia tawi lile
nilitulia kwanza pale juu nikiichanguza vizuri ile nyuma na mazingira yake. Il-
ikuwa ni nyumba ya ghorofa ya kifahari sana iliyozungukwa kwa bustani nzuri
ya maua na nyasi zilizokatiwa vizuri. Nikiwa pale juu ya mti niliweza kuliona
lile gari aina ya Volvo nililokuwa nikilifuatilia toka kule Halfmoon Bar pia
kulikuwa na magari mengine mawili. Gari moja aina ya Nissan Patrol nyeupe
na gari nyingine aina ya Benz. Magari yale yote yalikuwa yameegeshwa mbele
ya nyumba ile chini ya banda maalumu la kuegeshea magari.
Niligundua kuwa pia kulikuwa na walinzi waliokuwa wakilinda eneo lile na
wote walikuwa na bunduki zao mikononi huku wakipeana zamu kuzunguka
ile nyumba. Mbali na hayo niligundua pia vyumba viwili vilikuwa vikiwaka
taa katika ghorofa ya juu ya nyumba ile kwani ule mti nilioukwea urefu wake
ulilingana na kimo cha ghorofa ile ya juu. Tofauti na hapo hapakuwa na kitu
kingine cha ziada.
Nikiwa nimejiridhisha na uchunguzi wangu nilijilaza juu ya tawi lile na
kuanza kusota kwa tumbo taratibu nikishuka kuelekea mle ndani ya ule ukuta.
Tawi lile refu lilikuwa limeelekea katika chumba kimoja cha ghorofa lile na
chumba hicho kilikuwa miongoni mwa vile vyumba viwili vilivyokuwa viki-
waka taa. Hata hivyo sikuweza kuona chochote ndani ya kile chumba kutoka-
na na pazia zito lililokuwa dirishani.
Nikiwa juu ya tawi lile niliendelea kusota kwa tumbo kuelekea ule uelekeo
wa lile dirisha la kile chumba kilichokuwa kikiwaka taa na wakati huo wote
bastola yangu ilikuwa mkononi tayari kufanya shambulizi lolote na macho
yangu yalikuwa yakijitahidi kuzunguka huku na kule kujaribu kuchunguza
kama kulikuwa na mtu yoyote mwingine eneo lile kwani wale walinzi wote
walikuwa wamesimama mbele ya ile nyumba kwa wakati huu.
Wakati nikiwa nimefika nusu ya lile tawi nililazimika kusitisha kwa muda
mjongeo wangu baada ya kusika sauti fulani ikitokea kwenye pembe ya ile
nyumba. Nikatulia kimya juu ya tawi lile huku nikiyatembeza macho yangu
kutazama upande ule ile sauti ilipotokea. Nilipoyatuliza vizuri macho yangu
nikamuona mlinzi mmoja akiwa na mbwa. Nilimtazama mlinzi yule nikagun-
dua kuwa hawakuwa na hisia zozote za uwepo wangu eneo lile, na bunduki
yake alikuwa ameining’iniza begani huku mkono wake mwingine akiwa ume-
shikilia sigara. Yule mbwa aliyeongozana naye alikuwa akimrukiarukia na
yule mlinzi hakuonekana kushughulika naye.
Nikiwa nimejibanza pale juu ya lile tawi nilimuona yule mlinzi akisogea
taratibu kuja usawa ule niliokuwepo na alionekana kwa kila namna kuzama
katika starehe yake ya kuvuta sigara. Yule mlinzi aliendelea kuzitupa hatua
zake taratibu mpaka alipofika chini ya usawa wa lile tawi ndiyo akasimama na
kugeuka akitazama kule nyuma kabla ya kuirudisha tena sigara yake mdomoni
akivuta taratibu kisha kipisi cha sigara kilichosalia akakitupa chini na kukizima
kwa kiatu chake. Baadaye nilimuona yule mlinzi akiinama na kuanza kumpa-
pasa yule mbwa shingoni. Nikiwa nimejibanza juu ya tawi lile nilianza kuhisi
kuanza kuchoka kulikumbatia lile tawi hivyo nilianza kuhisi kuwa endapo hali
ile ingeendelea vile nisingeweza kuhimili zaidi hivyo nilianza kufikiria namna
ya kumfanyia shambulizi la kushtukiza yule mlinzi.
Lakini wakati nikijipanga kufanya hivyo nilimuona yule mlinzi pale chini
akianza kuondoka pamoja na yule mbwa wake na tukio hilo likanipa faraja
kidogo. Nilimsubiri yule mlinzi hadi pale alipokunja kona na kupotelea mbele
ya ile nyumba na hapo ndiyo nikaanza kuendelea na safari yangu. Nilipofika
mwisho wa lile tawi nikaning’inia kwenye bomba moja lililokuwa likitumika
kupitishia maji ya mvua toka sehemu ya juu ya paa la ghorofa lile. Kwa ku-
tumia bomba lile nikajivuta kwa mikono yangu hadi pale nilipoufikia ukuta
wa ile nyumba sehemu kulipokuwa na nafasi kidogo ya kujishikiza.
Nilipofika pale nikaanza kuambaa na ule ukuta taratibu kwa uangalifu hadi
pale nilipokifikia kile chumba kilichokuwa kikiwaka taa. Nikiwa kwenye di-
risha la chumba hicho niliweza kuona ndani kupitia uwazi mdogo ulioachwa
na pazia na wakati huu macho yangu yalijikuta yakiweka kituo kwenye umbo
zuri la msichana fulani aliyekuwa ndani ya kile chumba. Nilipomchunguza
vizuri msichana yule nikagundua kuwa alikuwa ni yule msichana mrembo
niliyemwona kule Halfmoon Bar, na wakati huu alikuwa amevua nguo zake
zote na kubaki kama alivyozaliwa. Nilimtazama msichana yule akiwa katika
muonekano mpya kabisa wenye kuvuta hisia zangu na wakati huu yule msi-
chana hakuwa na ile miwani nyeusi machoni kama kipindi kile nilipomuona
kule Halfmoon Bar.
Ni katika mtazamo huo mpya nikajikuta nikikumbuka kitu fulani na kuki-
kumbuka kitu hicho kikanipelekeanianze kuhisi kuwa damu yangu ilikuwa
ikaanza kuchemka mwilini huku nikiachama mdomo kwa mshangao. Msicha-
na yule aliyekuwa mbele yangu sasa nilikuwa na kila hakika kuwa alikuwa
ni yule msichana niliyeonana naye kule uwanja wa ndege wa Kigali nikim-
fahamu kwa jina la Marceline wakati nilipokuwa nikifika hapa nchini Rwan-
da. Kwa kweli nilishtuka sana na kwa namna moja au nyingine hisia tofauti
zikaanza kuumbika upya kichwani mwangu. Kwa kweli nilijisikia kuchang-
anyikiwa pale nilipoikumbuka ile barua yenye ujumbe wa siri niliyoiiba kule
chumbani katika ile nyumba ya maficho kule msituni.
“Mercelina...” nilijikuta nikitamka jina lile bila kujielewa na kama aliye-
shtuka baada ya kulisikia jina lake likitamkwa nilimuona Marceline akigeuka
kutazama pale dirishani nilipokuwa na hapo nikajihisi ni kama niliyepigwa
shoti kali ya umeme na kuacha moyo wangu ukiwa umesimama kwa sekunde
kadhaa kama mfu. Ingawaje nilikuwa na kila hakika kuwa pamoja na Marce-
line kutazama pale dirishani lakini alikuwa hanioni lakini bado akili yangu
ilishindwa kabisa kukubaliana na tukio lile. Nikayasimamisha macho yangu
kukabiliana naye huku nikiwa na ujasiri wa kipekee kabisa, hata hivyo aliku
wa hanioni.
Uzuri wake ulikuwa umechangia kwa kiasi kikubwa kuniduwaza mbele ya
dirisha lile. Nilianza kwa kukitathmini kifua chake kilichobeba matiti mado-
go yanayofanana na umbo lake yenye chuchu ndogo zilizosimama. Kitovu
chake kilichotumbukia ndani na kuacha kishimo kidogo tumboni kiliungana
na mstari hafifu ulioshuka chini na kupotelea katikati ya mapaja yake huku
ukikiacha kiuno chake laini kikicheza taratibu kwa kadiri alivyokuwa akijari-
bu kupiga hatua moja mbele yake.
Nilimuona Marceline ni kama aliyekuwa akija pale dirishani halafu mara
nilimuona akikunja kona kuelekea upande wa kushoto na hapo nikagun-
dua kuwa alikuwa akielekea kujitazama kwenye kioo kikubwa kilichokuwa
kwenye kabati la nguo pembeni ya kitanda mle chumbani. Na wakati akitem-
bea kuelekea kwenye lile kabati niliweza kuliona umbo lake vizuri na kwa
haraka sana niliweza kukubali moyoni kuwa sikuwahi kumuona mwanamke
mwenye umbo linalotamanisha na kuziteka haraka hisia za mwanaume kama
yeye.
Kiuno chake chembamba kilicheza taratibu pande huu na ule sambamba na
mtikisiko wa makalio yake laini yaliyopishana taratibu wakati akizitupa hatua
zake. Alipofika kwenye lile kabati alisimama kwenye kile kioo na kujishika
kiunoni akijitazama kwa kujizungusha zungusha na baadaye alipandisha juu
mikono yake na kuanza kujitomasa tomasa matiti yake. Hata hivyo nilipom-
chunguza usoni niligundua kuwa hakuwa na furaha.
Simu iliyoanza kuita sebuleni ilimshtua Marceline na kumpelekea aache ku-
jitazama kwenye kile kioo na hapo akafungua lile kabati haraka na kuanza ku-
chagua nguo. Muda mfupi baadaye nilimuona akivaa bikini kisha akavaa suru-
ali nyepesi ya jeans na fulana nyeusi na alipomaliza akaharakisha kuelekea
kule sebuleni simu ilipokuwa ikiita.
Wakati Marceline akikiacha kile chumba kuelekea kule simu ilipokuwa
ikiita nikawa nimepata wazo la kuingia mle ndani ya ile nyumba kupitia diri-
sha la chumba kile. Hivyo bila ya kupoteza muda nilifungua kioo cha dirisha
lile baada ya kupata upenyo mdogo wa kupenyeza mkono na kufyatua komeo
la dirisha na muda mfupi baadaye nikafanikiwa kuingia ndani ya kile chum-
ba. Niliyazungusha macho yangu mle ndani na hapakuwa na chochote cha
kunivutia hivyo sikutaka kupoteza muda kwani nilikuwa na kila hakika kuwa
mwenyeji wa chumba kile angerudi muda si mrefu mara baada ya kumaliza
maongezi yake kwenye ile simu.
Ile simu iliendelea kuita na muda mfupi baadaye niliisikia ikipokelewa.
Niliusukuma mlango wa kile chumba taratibu na kutoka nje na hapo nika-
jikuta nimetokezea kwenye korido pana iliyokuwa na uzio mfupi wa vyuma
vilivyopindwa katika mtindo wa kupendeza. Uzio huo ulikuwa pembeni ya
ngazi zilizokuwa zikishuka sehemu ya chini ya ghorofa lile. Nilitazama upa-
nde wa kushoto kwangu nikaviona vyumba viwili vikiwa vimefungwa mbele
yangu na mbele ya vyumba hivyo kulikuwa na ukumbi mpana nilioufananisha
na sebule ya juu ya ghorofa lile.
Katika ukumbi ule kulikuwa na seti mbili za makochi ya sofa, meza pana ya
fomeka na seti moja ya runinga vilevile kulikuwa na kabati kubwa lililoshe-
heni vinywaji vya aina tofauti kwenye kona ya ukumbi ule. Nilitazama katika
ukumbi ule na sikumuona mtu yoyote hivyo nikajua kuwa Marceline alikuwa
ameshuka sehemu ya chini ya jengo lile ambapo sasa nilikuwa na hakika kuwa
simu ile ndipo ilipokuwa ikiita. Sauti ya maongezi ya kwenye ile simu ikanifa-
nya niukaribie ule uzio wa zile ngazi za kushuka kule chini na hapo nikaanza
kupiga hatua zangu taratibu nikinyata kushuka zile ngazi.
Nilikuwa nimefika nusu ya safari yangu pale nilipotupa macho yangu upa-
nde wa kulia na kupata picha nzuri ya sebule pana ya kifahari iliyokuwa seh-
emu ya chini ya ghorofa lile. Sebule ile ilipambwa kwa zulia la kifahari la
rangi nyekundu, seti tatu za makochi ya kisasa ya sofa yaliyozunguka meza
fupi za vioo, mapazia marefu dirishani, jokofu kubwa lililokuwa pembeni ya
kaunta kubwa ya vinywaji, seti moja ya runinga iliyokuwa mbele ya sebule ile
na sistimu moja ya muziki.
Niliyazungusha macho yangu upande wa kushoto na hapo nilimuona Marce-
line akiwa ameketi kwenye kochi moja lililokuwa jirani na meza iliyokuwa
na simu juu yake. Alikuwa ameketi kwa utulivu huku mkonga wa simu hiyo
ukiwa sambamba na mdomo wa sikio lake. Mwonekano wake usoni ulikuwa
na kila dalili za mashaka na wasiwasi ambao bila shaka ulitokana na taarifa za
upande wa pili wa simu ile.
Toka pale nilipokuwa nimesimama niliweza kuyasikia maongezi baina yake
na mtu wa pili kwenye simu ile hata hivyo sikuweza kuambulia kitu kutokana
na maongezi hayo kutumia lugha ya kinyarwanda ambayo mimi sikuifaha-
mu. Katika maongezi yale kuliibuka mabishano na mabishano hayo yalipozidi
nilimuona Marceline akikata simu na kuirudisha mahala pake kisha akasima-
ma na kuanza kuufuata uelekeo wa zile ngazi ili apande na kuja kule juu.
Alikuwa hajapiga hata hatua mbili katika safari yake pale ile simu ya mezani
ilipoanza kuita tena pale mezani. Marceline aligeuka na kuitazama ile simu ki-
sha tusi zito likamponyoka huku akionekana kuwa hana mpango wa kuipokea
tena na badala yake aligeuka na kuzitupa hatua zake kwa haraka akiendelea
na safari yake.
Niliwahi kurudi kule juu kabla ya Marceline hajaanza kupanda zile ngazi
na hapo nikaingia kwenye kile chumba nilichotoka na kujibanza nyuma ya
mlango nikimsubiri. Muda mfupi uliofuata niliouna ule mlango wa kile chum-
ba ukisukumwa kwa pupa na kisha Marceline akaingia na kwenda kujitupa
kitandani. Niliyatega vizuri masikio yangu na kuzisikia zile kelele za ile simu
ikiendelea kuita kule sebuleni na muda si mrefu ile simu iliacha kuita.
Marceline alikuwa amejilaza kifudifudi pale kitandani huku akihema kwa
hasira kama mtu aliyegombana na mwenzake na bila ya kupoteza muda nili-
jitoa kule nyuma ya mlango mafichoni na kuanza kumsogelea taratibu pale
kitandani. Na kama aliyehisi uwepo wa kiumbe kingine mle ndani Marceline
akashtuka na kugeuka na macho yetu yalipokutana akashikwa na taharuki am-
bayo sikumbuki kama niliwahi kuiona kwenye sura ya kiumbe chochote hapa
duniani.
“Wewe ni nani na unafanya nini humu ndani? aliniuliza kwa mshangao huku
uso wake umejawa na hofu.
“Patrick Zambi, mara hii tu umenisahau Marceline?
“Toka nje sasa hivi kabla sijakuitia walinzi’’
“Hebu keti tuzungumze mpenzi uite walinzi wa nini? nilimwambia kwa utu-
livu huku nikitabasamu na taharuki aliyokuwanayo usoni ni kama mwanamke
aliyefumaniwa na mume wa mtu. Nilipomtazama usoni nikaisoma akili yake
namna ilivyokuwa ikifanya kazi na kufumba na kufumbua Marceline akajitu-
pa upande wa pili wa kile kitanda huku mkono wake mmoja ukipotelea chini
ya mto mmoja wa kuegemea uliokuwa pale kitandani na alipoutoa ulikuwa
umeshika bastola.
Hata hivyo hakupata muda wa kuitumia ile bastola kwani kwa wapesi wa
ajabu niliipangua kwa teke jepesi lililoitupa ile bastola chini ya kabati. Marce-
line alikuwa hodari kuliko nilivyomdhania na pigo moja alilotupa la kareti
ilibakia kidogo liitengue shingo yangu kama nisingekuwa makini kulikwe-
pa. Akalitupa pigo lingine la teke lililolenga korodani zangu lakini niliwahi
kuliona nikalidaka na kulizungusha katika namna ya kulipoteza shabaha.
Ulikuwa ni mtindo hatari sana wa mapambano ya ana kwa ana uliotumika
kwa mashambulizi ya namna ile kwani Marceline alizunguka hewani kama pia
na kutua juu ya kile kitanda akiwa hajielewi. Nikamfuata lakini wakati huu
aliniwahi na kwa wepesi wa ajabu akarusha pigo moja la teke lililotua bila
pingamizi tumboni mwangu na kunitupa ukutani nikiwa na maumivu makali
sana.
Nilishikwa na mshangao sana kwani sikuamini kuwa msichana yule an-
gekuwa ni yule Marceline niliyemuona kule uwanja wa ndege wa Kigali seh-
emu ya mapokezi ya wasafiri akiwa na haiba nzuri ya kazi yake na tabasamu
la kibiashara. Wakati nikijiandaa kusimama Marceline aliniwahi hata hivyo
nilikuwa makini zaidi kwani pigo la teke jingine alilolirusha nililiona na hapo
nikatumia jitihada kidogo kuinama chini nikiliacha pigo lile likipita hewani
na kukikosa kidogo kichwa changu. Na kabla teke lile halijafika mwisho wa
safari yake niliwahi kujibetua na hapo nilimtandika Marceline mapigo mawili
ya ngumi kavu za mgongo na hapo nikamsikia akipiga yowe kali la maumivu
huku akipepesuka kama mlevi.
Sikutaka kumsubiri hivyo kabla hajasimama nikamtandika pigo jingine la
teke la mgongoni na wakati huu sikutaka kumchukulia tena kama msichana
wa kawaida kwani dhana iliyoanza kujengeka kichwani mwangu ni kuwa nili-
kuwa nikipambana na msichana hatari na si yule Marceline niliyemuona kule
kiwanja cha ndege cha Kigali.
Mapigo niliyomtandika Marceline yalikuwa madhubuti na yenye uhakika
kwani pamoja na jitihada zake za kujizuia hakufanikiwa badala yake alien-
da kujipigiza kwenye kile kioo cha kabati. Kile kioo kikavunjika na kum-
chanachana Marcelina mikononi na usoni huku akipiga yowe la hofu na kisha
kuanguka chini. Alipotaka kusimama nilikuwa tayari nimekwisha muwahi
hivyo alijikuta akitazamana na mtutu wa bastola yangu wenye uchu na roho
yake.
“Sikupenda tufikishane huku Marceline tambua kuwa ni wewe ndiye uli
yenipelekea nifanye haya yote mpenzi”
“Si umepania kuniua basi endelea na kwa bahati mbaya sana hujui mtu un-
ayemfanyia hivi ni nani”
“Mimi sina lengo la kukuua Marceline na kama ningetaka kufanya hivyo
ningefanya tangu kipindi kile ulipokuwa uchi ukijishikashika matiti na kiuno
chako mbele ya kioo cha kabati humu ndani” nilimwambia Marceline na hapo
nilimuona akitaharuki na kunitazama kwa mshangao kisha akageuka kutaza-
ma upande ule wenye lile dirisha la kile chumba huku uso wake ukiwa tayari
umesawajika.
“Umeniambia kuwa kwa bahati mbaya nakufanyia haya yote pasipo kuku-
jua kuwa wewe ni nani. Kwani wewe ni nani mimi mbona nakutambua kama
Marceline” nilimuuliza
“Ungekuwa na shida ya kinifahamu usingenifanyia haya uliyonifanyia”
“Basi naomba unisamehe mpenzi”
“Wewe niue tu nadhani hicho ndicho kilichokuleta humu ndani” Marceline
alifoka kwa hasira.
“Marceline!...” nilimuita kwa upole na utulivu huku nikimshika begani
kama mpenzi wangu wa siku nyingi. Kwa kweli nilikuwa hodari sana wa ku-
cheza na hisi za viumbe wa sampuli ile kwani Marceline aligeuka taratibu na
kunitazama pasipo kuonesha ukaidi wa aina yoyote.
“Nimetumwa” hatimaye nilimwambia kwa utulivu huku mtutu wa bastola
yangu bado ukiwa unamtazama.
“Umetumwa nini na nani? Marceline aligeuka tena na kunitazama huku
ameshikwa na mshangao.
“Nimetumwa na Bolos!”
Marceline alishikwa na mshangao huku akinitazama kwa hofu akionekana
kuchanganyikiwa na maelezo yangu.
“Bolos amekutuma wewe!...kwa nini asije mwenyewe? Marceline alinuliza
huku akionekana kuzidi kustaajabu.
“Amepata dharura” nilimjibu kwa utulivu huku moyoni nikitabasamu kwani
kitendo cha yeye kunisikiliza zilikuwa dalili nzuri sana kwangu “...Leo usiku
ana kikao cha dharura na wageni muhimu hivyo ndiyo alivyoniambia na kuni-
taka nifike kwako na kuchukua taarifa ulizonazo” nilimdanganya Marceline
na nilipomtazama usoni nilimuona jinsi alivyozidi kuchanganyikiwa na kwa
dalili nilizoziona kwake niligundua haraka kuwa Marceline alikuwa mwana-
funzi mzuri wa kijasusi.
“Taarifa zipi na wewe ni nani mpaka akutume?
Nilitabasamu kidogo ingawaje tabasamu langu halikutokana na furaha bali
mlolongo wa maswali mengi yasiyokuwa na majibu kichwani mwangu.
“Mimi ni rafiki wa Bolos vilevile unaweza kuniita Patrick Zambi, mwandi-
shi wa habari wa kujitegemea kutoka nchini Tanzania. Bila ya shaka sasa ume-
nikumbuka” nilimwambia Marceline huku nikiivua ile kofia yangu kichwani
taratibu na kutabasamu kidogo kabla ya kuirudisha tena kichwani” hofu nili-
yoiona usoni kwa Marceline mimi mwenyewe naijua. Akabaki ameachama
mdomo wake kwa mshango kama anayetaka kuzungumza neno fulani ambalo
hakuwa na nguvu ya kutosha kuliongea.
“Bila shaka sasa umenikumbuka vizuri” nilizungumza taratibu huku niki-
tabasamu. Marceline alijitahidi tena kuzungumza neno lakini hata hivyo sauti
yake ilikuwa hafifu sana na yenye kila dalili za woga hivyo akaishia kumu-
munya maneno kama mtoto anayejifunza kuongea. Nilipomuona anakawia
kunijibu nikaendelea,
“Mimi na wewe ni kitu kimoja Marceline bahati mbaya sana hatuna muda
wa kutosha wa kukaa na kufahamiana na hii ni kutokana na usiri wa mipango
yenyewe ulivyo. Ninachohitaji sasa ni hizo taarifa nilizoagizwa kwako na Bo-
los kwani ni lazima nionane naye usiku huu kabla hakuja pambazuka halafu
baada ya hapo mimi na wewe tutapanga namna ya kuonana kwa nafasi yetu
mpenzi” nilimdanganya Marceline huku nikijiuliza kama uongo wangu uliku-
wa na ushawishi wowote kichwani mwake.
“Nani mpenzi wako? Marceline alinikana “Mimi sina taarifa zozote za kuk-
upa”
“Hebu tulia kwanza mpenzi hivi unadhani ninaweza kupoteza muda wangu
bure kwa kufuatilia kitu nisicho na hakika nacho?. Unazo taarifa Marceline na
taarifa hizo zinatakiwa kwa haraka sana kuliko unavyodhani. Hakuna haja ya
kupoteza muda kwani nahitaji kurudi usiku huu huu kabla ya hakujapamba-
zuka” Marceline aliinua macho yake kunitazama na hapo nilipata nafasi tena
kuuona uso wake namna ulivyoharibiwa na kile kioo cha kabati kisha akayak-
wepesha macho yake pembeni akitazama upande mwingine wa kile chumba.
Nilikuwa na imani sasa kuwa Marceline alikuwa akijiandaa kuniambia
kitu fulani hali iliyonipelekea nitabasamu kidogo huku nikijitahidi kum-
shawishi kwa macho yangu anieleze hicho kitu. Nikiwa nimeanza kujiandaa
kumsikia Marceline ghafla nilishangaa kumuona Marceline akianza kuangua
kicheko, alinitazama usoni kama mwehu kisha akaendelea kuangua kicheko.
Kwa kweli nilistaajabu sana kwani sikuweza kukufahamu kuwa Marceline
alikuwa akicheka nini.
“Huna ujanja Luteni Venus Jaka, unadhani na safari hii pia utafanikiwa ku-
toroka kwa kunihadaa kitoto kama hivi?. Pole sana mpenzi kwani mwisho
wako sasa umefika” Merceline aliendelea kuongea huku akicheka. Kwa kwe-
li nilishindwa kumuelewa vizuri Marceline kuwa alikuwa akimaanisha nini
kusema vile. Wakati Marceline akiendelea kucheka vile nikamuona akiangalia
nyuma yangu ikabidi na mimi nigeuke kutazama kule alipokuwa akitazama na
hapo ndiyo nikajua kwa nini alikuwa akicheka vile.
“Tupa bastola yako chini Luteni” sauti nzito ya kiume yenye amri ilinion-
ya toka nyuma yangu na kwa kweli nilihisi kuchanganyikiwa na kwa mara
nyingine nilianza kuona kuwa roho yangu haikuwa kwenye mikono salama
tena. Kipande cha mwanaume mrefu na mweusi aliyevaa gwanda za kijeshi
alikuwa amesimama nyuma yangu na mtutu wa bastola yake mkononi ukini-
tazama tayari kufanya kazi. Sura ya mtu yule ilikuwa ngeni kabisa machoni
ya mwangu na alikuwa na mwili uliojengeka vizuri kwa mazoezi na hata
alipotabasamu bado tabasamu lake lilimfanya aonekane kama mtu aliyetaka
kupiga chafya.
 
Back
Top Bottom