Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sura ya Tatu
Sura ya Tatu
Hazifunguki zoteSura ya 18
Nilliachana nayo, nikafuatwa nbox na watu wa Mkuki na Nyota wanasema sina haki ya kuirusha kazi yao.Hazifunguki zote
Nimesoma mpk nimeanza kusinzia hakuna nikichoona kimeingia akiliniSura ya Pili
Yasmin alifika Unguja kwa meli kiasi cha saa kumi na mbili na nusu za
magharibi, jua lilikuwa linapotea upande wa magharibi na mbingu zilikuwa
zimepambika kwa mawingu ya rangi ya dhahabu yaliyochanganyikana
na rangi ya zambarau. Abiria wote walikuwa washateremka melini na
kila mmoja alikwenda alikokwenda isipokuwa Yasmin ambaye alibakia
nje ya mlango wa kuelekea gatini, amesimama, amepigwa na bumbuwazi
hana zaidi isipokuwa kikapu alichokuwa nacho mkononi. Wachukuzi
namba walimzonga kama nzi wanapouzongea mzoga, kila mmoja katika
wachukuzi wale akitaka kujua mizigo ya Yasmin ilipo ili akamchukulie.
Yasmin hakushughulika na yeyote katika wachukuzi wale ila aliwaona
kama wendawazimu tu. Mawazo yake yalikuwa mbali na pale kilipo
kiwiliwili chake na alikuwa akiwaza na kujiuliza, “Nende wapi saa hizi?”
Alijiuliza na kujishauri moyoni mwake, “Nende kwa mama? Nikenda kwa
mama atanitukana asinibakishe. Nende kwa mjomba? Ah! Nikenda kwa
mjomba anaweza kunifukuza kwa kashfa ikawa aibu mtaa mzima.”
Yasmin alijiuliza masuali kem-kem lakini jawabu linalofaa hakuligundua
ng’o. Alianza safari yake ya kutokea bandarini kidogo kidogo akiwa na
kikapu chake mkononi lakini wapi alikokuwa akienda hata yeye mwenyewe
hakujua. Madereva wa teksi walizirambaza gari zao chini ya miguu yake
lakini kwa wakati ule rasilimali yote ya Yasmin ilikuwa shilingi tano na
kupanda teksi ilikuwa ni hasara asiyoweza kuimiliki ijapokuwa alikuwa
amechoka na njaa kali imemshika.
Alijikongoja mpaka senema ya Malindi. Alikwenda moja kwa moja
mpaka “Passing Show.” Alipinda mkono wa kulia na kutokezea kwa Amar
Waga. Hapo tena aliingia ndani ya barabara nyembamba za mtaa wa
Malindi mpaka akafika kwa Rasam na alipofika hapo alitamani kupumzika
lakini baada ya kujishauri aliona bora aendelee na safari yake. Moja kwa
moja aliendelea mpaka “Dagger Club” na baada ya hatua chache alifika
mbele ya mlango wa nyumba ya mjomba wake. Alijishauri kwanza kabla ya
kubisha hodi. Alipogonga mlango alifunguliwa na mke wa mjomba wake
ambaye kwa sauti ya mshtuko iliyochanganyikana na mshangao aliita,
“Yasmin.”
“Mjomba yupo?” aliuliza Yasmin hata bila ya kusalimu.
“Hayupo, kenda Jamatini. Mbona ghafla? Habari za Mombasa?”
“Mbaya.
Kwa nini?”
“Kwanza usiniulize maswali mengi, njaa imenishika tena nimechoka,
kama kipo chakula nigaiye kwanza nile halafu tutazungumza.”
Yasmin alikaa juu ya kiti na kukiweka kikapu chake chini. Palepale mke
wa mjomba wake aliingia jikoni na kuanza kukaangakaanga. Kinywa cha
Yasmin kilivuja mate kwa harufu nzuri iliyokuwa ikitokea jikoni na alihisi
kwamba baada ya muda mfupi atakula kikomo cha shibe yake.
Kabla ya karamu aliyokuwa akiandaliwa haikuwa tayari mlango
ulingongwa na alipokwenda kufungua alimkuta mjomba amemsimamia
mbele.
“Mbona upo hapa saa hizi? Umerudi lini? Mume wako yuko wapi?”
Yasmin hakujua ajibu lipi katika maswali aliyoulizwa. Alinyamaza kimya
kama mtu aliyepigwa na bumbuwazi.
“Nakuuliza mume wako yuko wapi?” aliuliza tena mjomba wa Yasmin.
“Yuko Mombasa, mimi nimerudi nimeshindwa kuishi naye.”
“Unasemaje? Umeshindwa kuishi na Raza?”
Mjomba wa Yasmin aliondoka pale mlangoni alipokuwa amesimama.
Aliingia ukumbini na kukaa juu ya kiti. “Enhe, hebu nieleze vizuri.”
Yasmin aliinamisha uso chini hofu imemjaa, “Mjomba, kusema kweli
thawabu, mimi nimeshindwa kuishi na Bwana Raza. Kwa hakika mimi
sikumpenda wala sikumtaka. Nilikubali kuolewa naye kwa kukuridhini
nyinyi wazee wangu tu.”
“Kama hukuweza kuishi na Raza basi na sisi hatuna pa kukuweka,”
mjomba wake Yasmin alisema kwa kelele. Kelele zilikuwa kubwa mpaka
majirani wakaanza kuchungulia madirishani. “Tena upesi tuondokee
mbele ya macho yetu utafute pa kwenda. Toka!” alifoka mjomba.
Yasmin alisita kidogo na kumtazama mjomba wake, matone ya machozi
yakianza kuteleza taratibu kutoka kwenye macho yake mazuri.
“Nakwambia toka! Nenda zako! Nenda kamtafute huyo unayempenda.”
“Niondoke nende wapi na hapa ndiyo kwetu?” alisema Yasmin kwa
unyonge.
“Hapa palikuwa kwenu kabla hujaolewa. Sisi tulikupa mume ili
tupungukiwe na mzigo. Sasa madhali umemkimbia mumeo, tafuta pa
kwenda.”
Yasmin mabega yalimporomoka, asijue la kufanya. Alitoka nje taratibu
na alipofika nje mjomba wake aliufunga mlango kwa nguvu huku akilaani
na kutukana. Majirani walikwishajaa madirishani wanamwangalia Yasmin akitoa na kikapu chake mkononi, amenywea kama aliyemwagiwa maji ya
baridi. Aliwaza na kujiuliza, “Nende kwa mama?” alifikiri, “Aa, nikenda
huko mambo yatakuwa mabaya zaidi.”
Aliendelea na safari yake mpaka Darajani na alipofika hapo alisita
kidogo. Alitia mkono sidiriani na kuzichomoa shilingi tano alizokuwa
amezifutika na kuzitazama, akiwaza ni chakula gani atakachoweza kupata
kwa pesa zile. Alikwenda mpaka kwa mchoma muhogo akanunua wa
shilingi mbili. Alijibanza pembeni na kuanza kuula, akiula huku akifikiri
na machozi kutaka kumtoka, zamani alikuwa akila muhogo wa kuchoma
kwa kuutamani tu, leo anaula kwa njaa. Aliula wote na kupangusa midomo.
Sasa alizidi kufikiri pa kwenda. Alihisi balaa limemfika na janga
limemwangukia hajui la kufanya. Palepale ilimjia fikra, “Bora nende kwa
Mwajuma, labda ataweza kunisaidia.” Alikwenda moja kwa moja mpaka
kwa Mwajuma. Alipofika hapo aligonga mlango na sauti ya Mwajuma
ilimjibu kumkaribisha. Mwajuma alipofungua mlango na kumwona
Yasmin alishangaa na kuuliza, “Yalikuwaje shoga yangu?”
“Ah, mambo makubwa, hata sijui nikwambie nini.”
“Karibu jikoni basi tupike.” Mwajuma alimsogezea Yasmin mbuzi na
kumkaribisha akae yeye mwenyewe akiendelea na mapishi.
“Enhe! Khabari za Mombasa?”
“Khabari shoga yangu mbaya. Maisha na Bwana Mkubwa yule
yamenishinda. Sina raha sina starehe, mwisho nimeona bora nirejee
kwetu kwa wazee wangu. Nimekwenda kwa mjomba nimetimuliwa kama
mbuzi na kwa mama naogopa kwenda manake maneno yake nayajua.”
Yasmin alisita kidogo na kupumua. “Sasa hata sijui la kulifanya usiku huu,”
aliendelea huku akikiweka kikapu chake alichokuwa amekikumbatia.
Alikihisi kizito ijapokuwa bidhaa zote zilizokuwemo ndani ya kikapu kile
ilikuwa ni kanzu moja na nguo za ndani mbili tatu alizogawiwa na jirani
yake kule Mombasa. Labda kilichozidi ni mswaki na dawa ya meno.
“Maskini shoga yangu. Sasa una shauri gani?” Mwajuma aliuliza kwa
huruma za dhati.
“Sina shauri lolote, nimekuja kwako kukusikiliza utaniambia nini.
Tafadhali nisitiri, nisitiri aibu yangu!”
Mwajuma alimtazama Yasmin akatikisa kichwa. “Basi karibu shoga,
tutajibana hapa hivyohivyo, ijapokuwa kitanda chenyewe kimoja,”
alimwambia na kumwongoza chumbani akipangusa mikono kwa kanga
aliyokuwa amejifunga kifuani.
Yasmin alikaribishwa chumbani. Baada ya kuingia ndani tu alikaa
juu ya kitanda na kupumua kwa nguvu kwa machofu aliyokuwa nayo
na wasiwasi uliokuwa umeyatawala maisha yake wakati ule. Mwajuma
alimwacha Yasmin akipumzika na haraka haraka alimaliza kupika. Baada
ya muda mfupi aliandaa wali mzuri uliokolea nazi, mchuzi wa chukuchuku
na mboga ya mtoriro kidogo. Ilikuwa ni bahati tu kuwa siku ile Mwajuma
hakuwa na nyendo za usiku, na baada ya kula tu walilala. Yasmin alilala
usingizi mzito kwa machofu aliyokuwa nayo. Labda alizindukana mara
mojamoja tu kujikuna mbu au kunguni aliyemtafuna, lakini alipokuja
kuzindukana hasa kulikuwa kushakucha. Huko jikoni alimsika Mwajuma
akihangaika kukosha vyombo alivyopikia jana usiku na huko nje alisikia
mlio wa kinu kilichokuwa kikitwangwa na watu wawili.
Haukupita muda, chai ilikuwa tayari na walipokuwa wakinywa
Mwajuma alionekana ana haraka. Baada ya kumaliza tu alilitafuta baibui
lilipo. Alivaa baibui, akasimama mbele ya kioo kirefu kiliomo chumbani
mwake. Alijipaka podari, akajiremba wanja machoni. Alizichana nywele
zake fupi ambazo leo hakuzisuka na baadaye aligeuka na kumtazama
mgeni wake. “Mimi natoka mara moja. Nafika hapo Mbuyuni kwa mshoni
wangu kusikiliza kama kanzu yangu iko tayari, nitarudi saa hivi.”
“Mimi utanikuta hapahapa ukirudi,” Yasmin alisema kwa unyonge
wenye kutia huruma.
Mwajuma alitoka na kumwacha Yasmin peke yake. Hapo tena Yasmin
alikabiliwa na kimya tu. Sauti za pekee alizoweza kuzisikia zilikuwa labda
zile za mwuza samaki au mwuza mboga wakitangaza biashara zao kwa
kelele.
Kwa Yasmin kimya kile kilikuwa cha sauti tu, kwani kichwani mwake
mlikuwa mmejaa mawazo yaliyokuwa yakisokotana na kumfanyia kelele
ambazo mtu yeyote hakuweza kuzisikia ila yeye mwenyewe. Aliondoka
juu ya kiti alichokuwa amekikalia na kulala kitandani. Kitanda kilikuwa
kimetandikwa vizuri kwa shuka ya rangi ya waridi iliyofumwa maua
katikati. Wakati akigaragara juu ya kitanda kile, aliuchukua mmoja wa
mito miwili iliyovikwa foronya rangi moja na ya lile shuka na kuukumbatia
halafu akajilaza kifudifudi. Hapo tena fikra zilianza kutembea kichwani
mwake na kuaza kujiuliza vipi ataweza kuyakabili maisha ilhali yu
peke yake na yeye bado yu ngali mtoto hata ubwabwa wa shingo bado
haukomtoka. Alijiuliza vipi ataweza kujiendesha? Mpaka lini ataishi kwa
Mwajuma, mtu aliyemjua kwa mazungumzo tu? Nini jamaa zake watasema wakisikia anaishi Uswahilini na Waafrika. Almureadi fikra namna kwa
namna zilikuwa zinaranda na kupigana vikumbo ndani ya kichwa chake.
Alipogeuka alikikabili kile kioo kirefu kilichotundikwa ukutani na kama
kioo kile kilikuwa kikimtua, aliinuka na kukisogelea. Sasa mawazo yote
aliyokuwa nayo yalipeperuka kwa muda na kuanza kujianglia kioni namna
alivyoumbika. Alijitazama na kujitazama tena, halafu akachukua kitana
kilichokuwepo juu ya meza ndogo iliyokuwemo chumbani mle akaanza
kuchana nywele zake na kuzilazia nyuma. Alijiona akizichana namna ile
hapendezi. Alizichana tena na kuzilazia pembeni. Aligeuka na kujitazama
huku na huku na alipohisi hajajifaidi bado, alifunga mlango. Alisimama
mbele ya kioo akavua kanzu na kubakia na nguo za ndani tu.
Alijishika kiunoni kwa mikono yake na kujitazama tena huku na huku.
Alijigeuza nyuma na kujiangalia lakini aliona bado hajajifaidi. Alivua sidiria
na kujiangalia matiti yake na kuyainuainua huku akiyachezea. Alijigeuza
tena mbele na nyuma na mara kwa ghafla, kama mtu aliyesituliwa,
aliondoka mbele ya kioo na kuvaa nguo zake kwa haraka. Alipomaliza
alijitupa kitandani na kulala kifudifudi na mara machozi yalianza kumtoka.
Zilimjia fikra za kwamba mtoto mzuri kama alivyo, mwenye mwili mzuri
kama ule, leo anaishi maisha ya dhiki na unyonge vipi atakosa kupendwa
na kijana mwenzake aliye mzuri kama yeye, tena aliye Mhindi. Kijana
ambaye angelifuatana naye wakatia ngosho njiani huku vijana wenzake
wakimhusudu. Alijiuliza, “Vipi?” Alifikiri labda Bwana Raza amemtia
kisirani au labda amekaa ndani sana hata vijana hawakuwahi kumjua.
Lakini kabla hakupata majibu ya maswali aliyokuwa akijiuliza, zilirudi
kichwani mwake fikra juu ya maisha yaliyomkabili. Aliendelea kufikiri
mpaka fikra zikamwisha, usingizi ukamchukua, akalala.
Hivi sasa Yasmin alikabiliwa na maisha mapya kabisa, maisha ambayo
hakupata kuishi kwani ijapokuwa alikuwa akiishi Ng’ambu, lakini alikuwa
haishi king’ambu. Alijuana na jirani zake wa Mtendeni kwa kuja kwao
dukani kwa Bwana Raza tu, zaidi hapana. Ilikuwa ni bahati nzuri tu
kujuana na Mwajuma, na hii ni labda kwa sababu tabia zao zimelingana.
Mwajuma, ijapokuwa ni mtoto wa kimaskini, alikuwa na roho nzuri ya
ajabu na roho nzuri yake ilichanganyika na ukarimu usiokuwa na mfano.
Alikuwa yuko tayari kumkirimu mtu chochote kidogo alichokuwa nacho.
Alikuwa mwingi wa huruma na siku zote alikuwa tayari kumsaidia yeyote
aliyemweleza shida zake, pindi akiwa na uwezo wa kumsaidia mtu huyo.
Kadhalika, alikuwa ni msichana asiyependa kujikera nafsi yake na
aliutumilia uhuru wake wa maisha kama alivyopenda. Alikuwa tayari
kufanya lolote lile ambalo alihisi litamletea furaha bila ya kujali wengine
watasema nini. Kila Jumamosi alikuwa hakosi densini na alikuwa mpenzi
mkubwa wa taarabu. Katika bahari ya muziki wa aina hiyo, alikuwa na
sifa kubwa katika chama chake cha “Cheusi Dawa” kwa ajili ya sauti yake
nyororo, kali wakati anapoimba. Asionyeshwe bi-harusi pahala popote
pale, utamkuta Mwajuma amekwisha fika, amejitia kizoro pamoja na
wasichana wenzake. Na hapo kwake, ingia toka ya vijana wa kike na wa
kiume ilikuwa haishi. Yeye alikuwa hajali kusemwa na majirani ikiwa kwa
wema au kwa ubaya, bali hufanya vile anavyopenda yeye mwenyewe.
Kiasi cha saa saba za mchana, Mwajuma alirejea kutoka safari yake
ya randaranda mitaani na alimkuta Yasmin bado amelala. Ijapokuwa
hakupenda kumwamsha, vishindo alivyovifanya wakati akibadili nguo
vilimwamsha.
“Nimekukatia usingizi wako?” Mwajuma aliuliza, akihisi amemkera
Yasmin.
“Ah, tokea hapo nilikuwa sina haja ya kulala, lakini usingizi umeniiba
tu, “Yasmin alisema akijinyoosha. “Je usharudi safari yako?” aliuliza.
“Nimesharudi lakini yule mshoni sikumkuta. Nitakwenda kumsikiliza
tena kesho.”
Baada ya kubadili nguo, Mwajuma aliingia jikoni na kutayarisha mlo na
alipomaliza walikula. Baada ya hapo alifanya kazi ndogondogo za kusafisha
nyumba. Kisha ndipo likaanza gumzo baina yake na Yasmin.
“Mimi nilikuwa nikikuhisi kwamba humtaki Bwana Raza,” Mwajuma
alianza akiwa na hakika kwamba Yasmin atazungumza sana.
“Ah, yule alikuwa si mume wa kumtaka mimi mwenyewe niliozeshwa
tu na wazee wangu na mimi sikuweza kuwavunja,” alisema Yasmin
akitabasamu na kuonyesha meno yake yaliyokuwa yaking’aa kama marmar.
Hapo tena liliendelea porojo baina ya Yasmin na Mwajuma kwa muda
mrefu akizungumzwa Bwana Raza. Walimuumba na kumuumbua mzee
huyo na mara mojamoja soga hilo lilistawishwa na hadithi za jiji la
Mombasa. Hapo ulizungumzwa uzuri wa jiji hilo, jia pana la Kilindini lenye
mataa mengi, maduka chungu nzima ya Mtaa wa Salim Road na harakati
zinazokuwapo katika jia hilo usiku na mchana. Vitambaa na mapambo kila
aina yaliyojaa ndani ya maduka yenye kupendeza. Na zinapoanza hadithi
hizo ndipo Yasmin anapopata uwanja wa kuzungumza.
Aliyakumbuka mengi juu ya mji wa Mombasa, lakini katika kuhadithia
kwake kote mwisho huangukia juu ya maisha yake na Bwana Raza na hapo
soga juu ya Bwana Raza huendelea. Mwajuma na Yasmin walizungumza
sana utafikiri hawakuonana kwa muda wa miaka kumi iliyopita. Ilipofika
jioni wakati bado wamo katika starehe yao ya kupiga soga, waliingia vijana
wawili. Walibisha hodi mara moja tu na hata kabla hawajawahi kujibiwa
walijitoma ndani moja kwa moja mpaka chumbani kwa Mwajuma.
“Halo shem! Habari za kushinda?” aliuliza Salum, amesimama
mlangoni mkono wake mmoja amekamata ubao wa mlango, mkono
mwingine ameutia ndani ya mfuko wa suruali ya kaki aliyoivaa. Mwenzake
amesimama karibu na pembe ya kitanda alichokalia Yasmin. Yasmin alikaa
katikati ya kitanda amekumbatia mto mikononi mwake.
“He! Leo umepata mgeni wa Kihindi?” aliuliza Salum bado yungali
amesimama mlangoni. Hakuonyesha heshima wala staha kwa mgeni yule
ambaye hakupata kumwona hata siku moja.
“Aaaaa! Wacha maneno yako njoo ukae huku.” Bila ya kuonyesha kwamba
amekasirika au kuonyesha dalili yoyote ya furaha, Mwajuma alimkaribisha
Salum kukaa juu ya kiti lakini badala ya kukaa pale alipokaribishwa
alikwenda moja kwa moja mpaka kitandani na kujipweteka karibu na
Yasmin.
Salum alimtumbulia macho Yasmin akaanza kumchungua tokea utosini
hadi dole gumba halafu akamwuliza, “Hujambo dada?”
Yasmin alijibu kama aliyelazimishwa kusema akishangazwa na viroja
vipya asivyopata kuviona. Aliondoka kwa haraka pale alipokuwa amekaa
na kusogea mpaka pembe ya kitanda. Salum hakumshughulikia tena ila
aligeuka upande wa pili na kumwangalia mgeni wake aliyemwandalia
matembezi kwa Mwajuma siku ile.
“Roger pita ukae, usiwe na wasiwasi.”
Halafu Salum alimgeukia Mwajuma na kumwambia, “Shem, huyu rafiki
yangu kutoka Dar es Salaam. Tulikutana mwaka jana nilipokwenda huko
kwa sherehe za Pasaka.”
“Karibu Roger,” Mwajuma alimkaribisha.
“Mbona mgeni wako kanikimbia?” Salum aliuliza akiingilia katikati ya
mazungumzo ya kujuliana hali kati ya Roger na Mwajuma.
“Eh! Basi wewe umeingia kama shetani moja kwa moja mpaka kitandani
na kuanza kumwangalia mtoto wa watu kama umeona ajabu gani sijui.”
Kama umezaliwa mkoani huwezi elewa mambo hizi za Pwani,Nimesoma mpk nimeanza kusinzia hakuna nikichoona kimeingia akilini
Kanda ya ziwa vumbi tuna lijua linachapa hiloKama umezaliwa mkoani huwezi elewa mambo hizi za Pwani,
Myself huwa naenjoy mno
Mbona kuanzia Sura ya tatu hamna kitu?Sura ya Tatu