Robert Knepper: Muigizaji aliyepata umaarufu mbaya kwa kucheza kama T-Bag, hadi leo watu wengi hudhani ana roho mbaya

Robert Knepper: Muigizaji aliyepata umaarufu mbaya kwa kucheza kama T-Bag, hadi leo watu wengi hudhani ana roho mbaya

Wote hao wanamkubali T bag, uzuri au ubaya wa t bag ni kuwa hana adui wa kudumu na hana rafiki wa kudumu yeye urafiki unakuja kwenye mchongo tuu na ukikaa vibaya anakutapeli mchongo wenyewe ikitiki
 
JamiiForums-533867264.gif
 
Scofield ana degree ya kuingiza na masters ya literature,Wana vyuo vya uigizaji,hapo Mara moja moja vina udwanzi,maana nasikia Denzel Washington alifeli chuo Cha uigizaji

Wanaigiza utafikiri kweli kabisa
Bongo movie wakasome jamani
 
Scofield alikuwa hamkubali Tbag wala nini ila tu wakati wa vurugu gerezani kwenye season ya kwanza alikuwa anampiga yule afande mbaya wake akajikuta anaingia kwenye chumba cha Scofield akagundua Scofield anachimba shimo la kutorokea,akataka kupiga kelele "they're digging the hole" alivyoona hajasikika akataka kupiga tena kelele ndio John Abruzzi akamuwahi kumfunga mdomo na kumwabia asiseme na yeye atakuwepo kwenye part ya escaping team ila hawakumkubali wala nini kutokana na mitabia yake mibaya!

Ila mwishoni alizalilika vibaya! Nilikuwa namkubali sana mwamba t-bag kwanza ni vituko vyakufa mtu.....
 
T bag kuonyesha hakuna anayemwamin

Walipotoroka wakiwa nje kila mtu njia yake kuna kipande kina Sucre(Sugar) wakiwa na michel na kaka yake wakakutana na T bag barabaran wakamkimbiza na kutaka kumpiga kawauliza kwa nn wakasema haaminiki amekaa kishari shar tu na wanahs anawafata
 
T bag noma Kuna kipind alikua haongei na mtu anajifanya bubu Kama tazani mara akamuona Joti acha achekeeee ila jamaaa katiliii sana....
 
Wanaigiza utafikiri kweli kabisa
Bongo movie wakasome jamani
Bongo muvi wanalazimisha tuangalie muvi zao, na wakati hawana jipya! Ubunifu 0! Teknolojia yao ya kuigizia ni ile ya mwaka 1947!

Hivi awamu hii ya huyu mama wamepewa mikopo isiyo na riba, utashangaa wataitumia hiyo mikopo kufanyia mambo ya kipuuzi tu, badala ya kujiimarisha kwenye hiyo tasnia yao!

Kiufupi Bongo Muvi wanasikitisha na kutia huruma.
 
Nataka bio series ikiwa Na subtitles za kibongo msaada Tafadhali
 
Toka mwezi wa pili umeanza nilikua nairudia hii series after kama 6 years bila kuiangalia... kiukweli tbag alicheza sana mule.... enzi inatoka nilikua sekondari huko ndo ilikua story za shule hizo kujadili episodes tu kuna muhuni akawa ndo anatusimulia akishacheki dstv kabla sisi hatujapata cd za buku buku kkoo
 
Back
Top Bottom