Robertinho ni kama ameingia kwenye mtego mkubwa sana Simba

Robertinho ni kama ameingia kwenye mtego mkubwa sana Simba

Bwana Bima

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2014
Posts
429
Reaction score
929
Ukijaribu kuangalia sajili za simba nadiriki kusema kwamba angalau wako vizuri japo nadhani walikua wanahitaji angalau wapate beki mmoja ambaye anaweza kumpa changamoto Inonga.

Nasema hivyo kwasababu, viongozi wa simba wamesajili kwa maelekezo ya kocha. Ukiangalia kikosi chao asilimia kubwa kuanzia kwenye kiungo, wote ni aina ya viungo ambao wanawaza kushambulia zaidi. Bila shaka huo ndo mfumo wa soka la brazil na soka analolipenda Robertinho.

Swali ni Je, ataweza kuwajenga wachezaji wake hasa wapya waingie kwenye mfumo? Je atafikia malengo ya klabu ya kubeba makombe? Huu ni mtihani mzito sana kwake na ninavyowajua mashabiki wa simba safari hii sijui kama wataweza kuvumilia. Mtihani mzito zaidi kwake ni ngao ya jamii.

Asipobeba hili au ikatokea simba akacheza na yanga then labda simba ikafungwa, naona kabisa jamaa akifurushwa virago.
 
Simba Wamesajili kwa KUKURUPUKA na MIHEMUKO.

Wamesajili kwa LENGO la kuwafurahisha Mashabiki.

Simba hawana Beki
Hawana kiungo mkabaji.

WANARUDIA MAKOSA Kila wakati.
Mwaka 2020 walikuwa na mawinga 11.
1. Perfect CHIKWENDE.
2. BENARD MORISON.
3. Dunkan Nyoni.
4. Pape sakho.
6 peter Banda.
7. Hassan Dilunga.
8. Ibrahim Ajibu.
9. Hassan Dilunga.
10. Muhilu.

MWAKA 2023 WANARUDIA YALE YALE.

1. KIBU Denis.
2.Saido ntibazonkiza.7 to 10.
3 CLOTUS chama 10 to 11.
4. Essomba Onana.
5. Aubin Kramo.
6.jimyson mwinuke.
7. Luis Miguisson

( Peter Banda )

ALEX FERGASON KOCHA BORA WA DUNIA ANASEMA.

"Safu Bora ya ushambuliaji itafunga MAGOLi. Safu Bora ya ulinzi itakupa Mataji.".

MSIMU uliopita Simba Alikuwa na MAGOLi zaidi ya 100.
Mataji 0.

LIGI KUU 75.
CAF CL.
AZAM FC

WAMECHAGUA MAGOLI NA SI MATAJI.
 
Simba Wamesajili kwa KUKURUPUKA na MIHEMUKO.

Wamesajili kwa LENGO la kuwafurahisha Mashabiki.

Simba hawana Beki.
Hawana kiungo mkabaji.

WANARUDIA MAKOSA Kila wakati.
Mwaka 2020 walikuwa na mawinga 11.
Kabisa
 
Simba Wamesajili kwa KUKURUPUKA na MIHEMUKO.

Wamesajili kwa LENGO la kuwafurahisha Mashabiki.

Simba hawana Beki.
Hawana kiungo mkabaji.

WANARUDIA MAKOSA Kila wakati.
Mwaka 2020 walikuwa na mawinga 11.
Upo sahihi hasa nafasi ya beki wa kati na hata wa pembeni... Sioni nafasi ya Mwenda na duchu dhidi ya kapombe na zimbwe. Mbaya zaidi Robertinho naona kama hapendi kufanya rotation kama alivyokua Nabi. Ndomana nasema kama simba ngao hatabeba sidhani kama watamvumilia jamaa
 
Upo sahihi hasa nafasi ya beki wa kati na hata wa pembeni... Sioni nafasi ya Mwenda na duchu dhidi ya kapombe na zimbwe. Mbaya zaidi Robertinho naona kama hapendi kufanya rotation kama alivyokua Nabi. Ndomana nasema kama simba ngao hatabeba sidhani kama watamvumilia jamaa
Anaweza akabeba kutokana na makosa ya wapinzani.
 
Anaweza akabeba kutokana na makosa ya wapinzani.
Wapinzani wepi mkuu? Kwa azam hii? Au singida fountain gate? Au yanga ambao kila position uwanjani ina watu haswa? Au labda aendelee na kikosi chake cha mwaka jana
 
Kitendo cha Simba kushindwa ku hakikisha wanabaki na Kakolanya ambaye kipa mwenye ubora mkubwa na kumwacha aende Singida.
Huitaji elimu ya juu kutambua ni watu wa masihara katika mambo muhimu.
Itachukua miaka mingi mpaka Simba kuja kutwaa kombe lolote la maana kutokana na mtazamo wa viongozi walionao kwa sasa.
 
Tusubri ligi ianze, me naona wako vzr japo heri namtakia yanga
Iko vizur sana ttzo litakuja kwenye machaguzi and second selection pale player mmoja anapoumia au kua na kadi... Kuna sehemu zina shida bado
 
Kitendo cha Simba kushindwa ku hakikisha wanabaki na Kakolanya ambaye kipa mwenye ubora mkubwa na kumwacha aende Singida.
Huitaji elimu ya juu kutambua ni watu wa masihara katika mambo muhimu.
Itachukua miaka mingi mpaka Simba kuja kutwaa kombe lolote la maana kutokana na mtazamo wa viongozi walionao kwa sasa.
Kosa kubwa sana hili
 
Iko vizur sana ttzo litakuja kwenye machaguzi and second selection pale player mmoja anapoumia au kua na kadi... Kuna sehemu zina shida bado
Yah hili ndio kosa ligi msimu huu itakuwa na ushindani sana kadi injury zinaweza kuwa nyingi
 
Kikubwa waifunge Yanga Ila ikiwa kinyume chake Moto Utawaka
 
Back
Top Bottom