Rodrigo Duterte Rais wa Zamani wa Ufilipino ahojiwa na ICC Juu ya Kuamrisha Mauaji Dhidi ya Watuhumiwa wa Madawa ya kulevya

Dikteta mwingine anapelekwa the Hague rasmi akajibu tuhuma zake, alifanana sana na mwendazake.

Naamini ipo siku mauaji ya halaiki iliyofanyika Rufiji wakati wa mwendazake yatakuja kujibu tu! Roho za mamia ya vijana zilizotupwa mtoni zikaliwa na mamba zinaililia hii nchi na kuna siku tu zitasikilizwa na muumba (kama yupo) ili haki itendeke.
 
πŸš¨πŸ‡΅πŸ‡­ RAIS WA ZAMANI WA UFILIPINO DUTERTE NJIANI KWENDA THE HAGUE KWA KESI YA VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA ICC

Rais wa zamani wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, yuko njiani kuelekea The Hague baada ya kukamatwa kwa hati ya ICC kwa tuhuma za uhalifu dhidi ya ubinadamu zinazohusiana na vita vyake vikali dhidi ya dawa za kulevya.

Mawakili wamewasilisha ombi kwa Mahakama Kuu kuzuia uhamisho huo, wakidai kuwa ni "utekaji nyara."

Familia za waathiriwa zinasema kuwa kukamatwa kwake ni haki iliyocheleweshwa kwa muda mrefu.

Chanzo: AFP
 
Pamoja na haki kwa Ben Saanane
 
Unaligalise vipi sembe?Magari barabarani siyatakuwa yakipita juu ya migongo yamateja yaliyolala barabarani.?
Uki legalise bei ya madawa itashuka sana na hivyo kuua soko la madawa kabisa maana supplier watakua wengi mnoo.
 
NINI KILICHOSABABISHA KUKAMATWA KWA RAIS WA ZAMANI WA UFILIPINO

Rodrigo Duterte, aliyekuwa akijulikana kama "The Punisher," alikamatwa kwa tuhuma za uhalifu unaohusiana na vita vyake vikali dhidi ya dawa za kulevya.

Uongozi wake (2016–2022) ulighubikwa na maelfu ya mauaji ya kiholela.

Takwimu rasmi zinaripoti vifo 6,248, lakini mashirika ya haki za binadamu yanasema idadi halisi ni kubwa zaidi.

Uchunguzi ulibaini kuwa waathiriwa wengi - mara nyingi watumiaji wa dawa za kulevya kutoka maeneo duni mijini - waliuawa katika mazingira ya kutatanisha, huku baadhi wakipewa vyeti vya kifo vilivyofanyiwa udanganyifu.

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) ilianza kuchunguza msako wa Duterte mnamo 2018, lakini aliondoa Ufilipino katika mamlaka ya mahakama hiyo haraka.

Hata hivyo, ushahidi uliendelea kuongezeka, ikiwa ni pamoja na miili iliyofukuliwa upya ikiwa na majeraha ya risasi lakini ikiwa imeripotiwa kama vifo vya kawaida, hali iliyodumisha shinikizo la kimataifa.

Uchunguzi huo ulisitishwa mwaka 2021 baada ya serikali ya Ufilipino kudai kuwa ingeweza kushughulikia uchunguzi wake yenyewe, lakini mnamo 2023, ICC ilifufua kesi hiyo ikidai kukosekana kwa mashtaka ya kuaminika.

Kufikia mwishoni mwa 2024, utawala wa Rais wa sasa, Marcos Jr, ulionyesha kuwa utatekeleza hati ya kukamatwa, hatua iliyosababisha anguko la Duterte.
 
Nini matokeo ya uwepo wa suppliers wengi halafu?
Demand inashuka, kwahiyo kilo moja ya cocaine inakua mfano Tsh.100 unadhani tajiri gani atauza tena? So wale matajiri wakubwa wakishaondoka sokoni ndio unakuja kuyaondoa tena madawa hapo tayari unakua umeondoa wale cartels wakubwa, hawa wadogo dogo kuwadaka ni masaa machache tu.

Si umeona Mexico serikali ilipowapa uhuru tu kwa kutowaingilia sana, wauzaji wamekuwa wengi hadi bei kushuka hadi sasa wamehamia biashara ya parachichi.

Mambo yanahitaji akili tu sio nguvu
 
ICC itaamua hatma yake.
 
Vipi kuhusu kizazi utakachoangamiza kwa uwepo wa hiyo biashara ?
Mfano sahivi madawa si yamepigwa marufuku ila bado watu wanatumia ila ndio wananunua kwa bei kubwa, sasa watu hao hao 100 wakiruhusiwa kutumia ila kodi ni say 100% per teaspoon ina maana serikali itavuna pesa nyingi zilizokuwa zinaenda kwa cartels na wauzaji watakua wengi so madawa yatasambaa ndani ya mwaka or so then cartels wakifilisika unaanza kurudisha mfumo wa zamani kuyapiga marufuku.

Na kwa sababu watakaouza ni "vipanya" kwenye perfect competition wengi ni rahisi kuwakamata kuliko sasa ambapo soko ni duopoly hivyo kuwang'oa ni ngumu maana wana fedha kuliko wizara kadhaa.
 
Wauzaji wakiwa wengi na biashara ikiwa halali ni rahisi kupata watumiaji wapya wengi wao vijana (mtaongeza idadi ya mateja), itabidi muongeze pia 'Sober house' na mjiandae kwa matukio mengi ya kihalifu na uvunjifu wa usalama.

Kiufupi mtatengeneza balaa jipya.
 
Hata isipokuwapo hiyo biashara ya ngada, kizazi kitaangamia kwa sababu nyingine tofauti
Kwa hiyo bora kiangamie kwa 'ngada' maana kuangamia ni kuangamia tu ?
 
cartels wakifilisika unaanza kurudisha mfumo wa zamani kuyapiga marufuku.
Kuna baadhi ya nchi zimehalalisha baadhi ya madawa (mfano bangi) tena kwa ajili ya shughuli za kitabibu au tafiti tu na hata watumiaji ni marufuku kutumia hadharani hii maana yake sio 'madawa yote' yanayofaa kuhalalishwa.

Mkuu haya madawa ni adui na janga kwa Dunia, kuhalalisha ndio anguko la nchi
 
Demand and supply haifanyi kazi hivyo, unajua kitu kikiwa haramu ndio kina wateja wengi maana demand inakua kubwa kuliko supply. Ila ukihalalisha madawa hata ukipandisha kodi kama sigara au pombe kali bado ni ushindi maana serikali ndio itaingiza mabilion compared to Cartels hivyo hata kuiharibu biashara ni wiki moja tu maana mnufaika anakuwa serikali sio tena cartels.

Hata sasa biashara ni haramu ila bado madawa yanapatikana tu mimi binafsi nmeshuhudia hata nliposoma high school watu walikua wanapata supply ya "unga" ndio sembuse uraiani?
 
Mkuu naona kama kuna double standard sana kwenye serikali zetu. Mfano zile pombe kali zinaua Figo mbona hazizuiwi kama tu Sigara nazo zinaua mapafu ila zinaruhusiwa. Sasa kama pombe kali zina madhara na unga una madhara kwanini moja inaruhusiwa na nyingine ndio izuiwe?
 
Si kweli ,data na experiment iliyofanyika Portugal ins suggest kinyume ,Portugal Ndio nchi pekee iliyoruhusu kila aina ya dawa ya kulevya kutumika ila result ya kwamba mateka wameongezeka au violence za drug cartels and gangs Hamna , na actually wanapata positive results Kwa kila angle ambayo nimegusia hapo tofauti na nchi ambazo zinakimbizana na wauza madawa na kufanya prohibition ya madawa duniani humu , hii experiment ni kama kipindi kile cha miaka ya 1920 enzi za alcohol prohibition kule Marekani ,hivi una jua kwamba Marekani miaka hiyo alcohol au pombe zilipigwa marufuku ? ,Unajua effects zake kilichotokea baada ya hapo ?
Walizaliwa magangwe na wahalifu wakubwa waliokuja kusumbua sana hiyo nchi enzi hizo akina Al capone na mamafia wengine wa kiitaliano na kiyahudi kama murder Inc ,Cosa nostra nk kutokana na utajiri mkubwa wa pesa za faster zilizopatikana kutokana na kazi ya kutengeneza na kuuza pombe kinyemela , nenda kasome historia ya Akina Capone na mamafia wengine miaka hiyo na hii issue ya uzuiaji wa pombe humo Marekani , ilikuwa ni shida kubwa .
Walivyo achia pombe kuuzwa na kutumiwa na raia hayo matatizo yote yakapotea ,cartels zikafilisika na kupotea na addiction ,violence na crimes nyingine zilizohusiana na hiyo shughuli ya kutengeneza na kuuza liquor au pombe zinapungua na kutokomea kwa kiasi kikubwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…