Roma bado inatawala dunia

Naomba, kuelimishwa kwa nukuu moja ya bibilia iliyo badilishwa na papa, aliyesema hakosei n nani ktk roma, pia thibitisha.
Hiyo Ufu:13 ni muham mad ibn abd allah..[emoji53]

Ilipoandikwa MNYAMA WA NNE , UFALME WA NNE. hizo nne zinamaanisha nini?. yaani 1,2,3 ni wakina nani hadi kufikia roma 4 ? Tuanzie hapo
 
Nithibitishe nini..?!
Ulicho kisema, shika bibilia yako vizuri na uisome usiokote vipeperushi ukatupia alafu ukashidwa kiuitetea.
Ni kweli!; ndio sababu waisilamu wanasali ijumaa wakisherehekea kwamba Yesu kafa...wasabato wanasali jumamosi wakifurahia Yesu yupo kaburini...Wakristo tunasali JPili tunasherehekea Bwana wa Mabwana kashinda kifo ni limbuko letu [emoji123] [emoji106]
 
Tatizo lako hujijui kama hujui, ni heri mjinga kuliko mpumbavu,

Wewe mwenye kujuwa nijibu swali moja tu: Jee, Mahakama ipi leo hii duniani inayokubali kuwa utumwa (slavery) ni halali?

Hapo sasa.
 
Naomba, kuelimishwa kwa nukuu moja ya bibilia iliyo badilishwa na papa, aliyesema hakosei n nani ktk roma, pia thibitisha.
Amri ya 4 ya Mungu inasema "Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote. Lakini siku ya saba ni sabato ya Bwana Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana kwa siku 6 Bwana alifanya mbingu na nchi na bahari na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba, kwa hio Bwana akaibarikia siku ya sabato akaitakasa. Kutoka 20:8-11.
Hio ni amri ya Mungu iliopindishwa na papa... Kanisa Katoliki hawaisomi jinsi ilivyo ktk Biblia Takatifu
 

Uongo mtupu. Hii ni tafsiri inayotokana na fikra za waliotafsiri hivyo kwa kufananisha matukio, hakuna uthibitisho wowote hata kwenye Biblia yenyewe. Natoa sababu zifuatazo:
1. Miaka yote hii uliyorodhesha kwenye maelezo yako haijaandikwa popote kwenye Biblia.
2. Isipokuwa tu kwa dola ya Babeli, nyingine zote ulizoorodhesha hazizungumziwa kwenye Biblia.
3. Unapotaja dola zilizotawala dunia wakati Nebuchadnezzar alipoota ndoto yake, unamaanisha dunia ipi? Unazungumziaje Ancient China (600BC), Ancient India (ambayo ilikuwa na strong urban kingdoms tangu 700BC), Falme za Mesoamerica na himaya staarabu za Maya, America Kusini (tangu 7,000BC)? Hao unaowataja walitawala himaya hizi pia? Kumbe si kweli, dunia unayozungumzia ni ya eneo la mashariki ya kati, sehemu kiasi ya ulaya na afrika ya kaskazini. Dola unazotaja hazikutawala dunia, zilitawala maeneo hayo machache.
4.Sehemu ya dunia unayokwepa kuizungumzia (Uchina, Japan, Korea, na mashariki ya mbali) ndiyo yenye mifumo tofauti ya kiutamaduni na kimaendeleo inayoshindana sana na ya kimagharibi. Haiko kwenye maelezo yako kwa kuwa umejikita kwenye 'dunia' ndogo ya mashariki ya kati.

Bisha.
 

Typical paranoia. Usijichanganye ndugu. Hivi kweli unaamini kuwa Mungu anayetajwa kuwa mwenyezi, mwenye uwezo wote, aliumba kiumbe (shetani) halafu akakipa uwezo wa kushindana naye kwa kiwango cha vita hizi mnazosema hapa? Kwamba Mungu mwenye uwezo wote anaumba kiumbe halafu kinamgeuka na kumsumbua kiasi hiki? Hujamwelewa Mungu.
 
Mackie nimetambua kwamba mimi na wewe tupo kwenye spiritual horizons 2 tofauti. Kwangu mimi biblia inajitosheleza, ni kila kitu. Kwa hiyo mjadala na wewe nimefunga. I have nothing any more to debate with u!
Another confused poor soul. Unamaanisha kuwa Mungu ni mdogo kiasi cha habari zake zote kutoshea kwenye kitabu kidogo kama Biblia? Fani yako uliyosomea peke yake ukikusanya vitabu ulivyosoma shahada ya kwanza tu mkusanyiko utazidi ukubwa wa Biblia mara nyingi. Na unajua kuwa fani yako uliyosomea haiwezi kumzidi Mungu, sasa vipi maelezo ya Mungu yatoshe kwenye Biblia pekee? Unazungumziaje watu walioishi kabla Biblia haijakusanywa (rejea historia ya Biblia ujue ni lini vitabu hivyo vilikusanywa katika mfumo unaouona sasa), hiyo habari ya "Biblia ni kila kitu" iliwahusuje, au walikuwa na Mungu mwingine? Na je waumini wa Buddhism na Hinduism ambao vitabu vyao vina umri mrefu kuliko Biblia, wanahusikaje na kauli yako ya 'Biblia ni kila kitu', au nao wana Mungu wao? Na wewe hiyo dini ya "Biblia ni kila kitu" ulizaliwa huko au uliitafuta kwa bidii mpaka ukaipata? Najua mlio wengi mlizaliwa katika dini zenu, inabidi tu mzitetee maana huwezi kukana identity yako, ni kama kabila lako au utaifa wako, lakini kumbuka hakuna aliyechagua kuzaliwa Macca (kwa waislamu) au Roma (kwa wakatoliki) au India (kwa wahindu) au Japan na China (kwa wabuddha), walijikuta huko na wakajifunza tamaduni hizo zilizowalea, sasa huwezi kubeza yote hayo unless unataka tuamini kuwa wote hao katika tofauti zao kila mmoja ana mungu wake tofauti na huyo wa kwako wa "Biblia ni kila kitu".

Mwisho, napenda nikubaliane nawe kuhusu msimamo wako, kwa matarajio kuwa nawe pia utaheshimu misimamo ya wengine. Na kama unaheshimu hivyo, basi usipinge wanachoamini wenzako. Ukitaka kufahamu ni sawa, lakini huna haki ya kukosoa kwa sababu huna objective reference ya kilicho sahihi dhidi ya kisicho sahihi. Fuata yako, waache wenzio pia wafuate yao. Tutofautiane hivyo.
 

Duh! Vituko vitupu! Kwa kujitungia udaku tu hujambo! Kwahiyo haya yote yako kwenye biblia ipi? Au na wewe umeandika ya kwako?
Na hiyo biblia unayosoma wewe, unajua ilikotoka? Ni Mungu aliiandika, eti? Hebu tafiti kidogo tu kuhusu maana na asili ya biblia (Biblia ni nini, ilianzaje, ikakua vipi hadi kufikia hiyo unayokariri?)
 
Mkuu! Unapoteza muda wako...wote hao na mpeleta mada ni vi.laza....hakuna wanachojua
 
Propaganda ya anayejifunza propaganda. Eti ulikuwa mroma (sijui ndio kabila gani hii inaitwa hivi), halafu eti ukasikia habari ya "siku ya ibada ni ipi", kwani huko ulikosema kanisani ulikuwa unakaa karibu na padri (kwanza hakuna seat ya namna hiyo katika makanisa yenye mapadri) siku ya ibada haikuwepo? Kwa hiyo ulikuwa unaenda kufanya nini kanisani? Acha uongo ndugu. Amini unachoamini, ni hiari yako, lakini acha uzushi.
Na hiyo biblia uliyosoma ikakueleza kuhusu sabato, uliipata wapi? Unajua historia yake? Kariri tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…