Roma bado inatawala dunia

Roma bado inatawala dunia

Roma bado inatawala dunia: ingawa ilianguka mwaka 476 AD ila athari zake zilikula dunia yote, ndo maana primary tulisoma no. za Kirumi na hata saa na Kalenda tunatumia za Kirumi na mataifa mengi yana sheria za Roma mpaka lugha zao tunazitumia. Roma haikuanguka kama inavyosemwa bali ilisambaratika na kuwa nchi za Ulaya ambazo zilikuja kuwa zenye nguvu na kutawala karibu dunia yote na kusambaza utamaduni wao. Mfano Uingereza imetawala bara Asia mpaka bara Arabu, hata ufalme wa Yordan, Saudia, Qatar zimewekwa na Uingereza. Kwaiyo ukisikia jumuiya ya madola tambua hizo ni nchi zilizotawaliwa na the greater Britain. Na Ufaransa, Spain, Portugal nazo hivo hivo.
Ulaya(Roma ya zamani) bado ina mkono mkubwa juu ya nchi za dunia hii. Ndo maana wameweka mahakama yenye sheria za Roma(The hague) ambayo daima ikiwahukumu viongozi wa nchi maskini, utake usitake ukiitwa hapo utaenda tu, na ukibisha utatolewa kwa bunduki.
Nabii Daniel alisema hivi juu ya Roma.
23 Akanena hivi, Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande. Daniel 7
Huu utawala wa Roma utadumu mpk Kuja kwa Yesu. Roma imeathiri dunia kisiasa, kidini, kisheria na kitamaduni na nchi yeyote inayokataa hoja za Roma lazima iangamizwe. Sadamu, Gadafi waliangamizwa sababu walipingana na utawala wa Roma, na sahivi Assad anakinywea kisha # Iran itapotezwa. Nabii aliona jinsi wana wa Ishmael(waarabu) wanavyopinduliwa na Roma maana hao waliifukuza Roma karne ya 7 na Roma ikajirudi tena kwa namna ya kuwaweka vibaraka wao ktk falme za Kiarabu kama ufalme wa Saudia, Qatari, UEA na Jordan hao wote ni puppet wa Roma. Na wote watakao pinga watafanyiwa hivi:-
Naye ataunyosha mkono wake juu ya nchi hizo, hata na nchi ya Misri haitaokoka. Daniel 11:42
Utawala wa Roma utaziangusha nchi zote pinzani zikiwemo nchi za Kiarabu na dunia itamstajabiwa mnyama yule(ufalme huo) na kuufata. Ufunuo 13:3 NIV
ROMA itatengeneza utawala wa dini na kulazimisha dunia yote kufata dini hiyo na watakao pinga watauawa.
Akapewa kutia pumzi katika ile sanamu ya mnyama, hata ile sanamu ya mnyama inene, na kuwafanya hao wote wasioisujudu sanamu ya mnyama wauawe. Ufunuo 13:5
Roma haitaangushwa na wanadamu......
......wakisema, Ni nani afananaye na mnyama huyu? Tena ni nani awezaye kufanya vita naye? Ufunuo 13:4
Roma itaangushwa na Mungu tu.
Kwa sababu hiyo mapigo yake yatakuja katika siku moja, mauti, na huzuni, na njaa, naye atateketezwa kabisa kwa moto. Kwa maana Bwana Mungu aliyemhukumu ni mwenye nguvu. Ufunuo 18:8
Take care usije anguka na Roma

a1175df048e7c5de0a0fe3db44ef801f.jpg
Bila shaka Mleta Uzi ni Msabatho, sasa mtafanyaje Kama Binadamu hawezi kuiangusha Roma, zaid Ya Mungu pekee kwa mujib wa maelezo yako.
Nakushauri bora uungane nao tu maana kuna msemo unasema kama huwezi kushndana nao bas ungana nao ukiwa Unamsubri Mungu wako kuja kuiangusha Roma
 
Hakuna mahali Biblia imetaja Rumi kwenye unabii wa siku za mwisho bali Biblia imetaja falme zingine kabisa....

Hili suala la Rumi ni assumtion zenu tu...

Hata suala la Papa kuwa mnyama ni assumtion zenu vile vile....

Hakuna ushahidi wowote wa kiunabii wa jambo hili.....
Mkuu bora umefika na uku uongeze nyama
 
Mungu yupo naamini,alieumba hii dunia..ila am very sure atakua anastaajab sana na kushangaa hiv hawa watu hiki wanachoamin sasa wamekitoa wapi?..kwenye jiolojia tunasoma mambo meng sana ikiwemo historia ya ulimwengu..tunasoma kua dunia hii ina apriximately miaka bil4.5,..na hii ni proven kisayansi,kwasabab kama waweza pima umri wa mwanadam exactly bas inawezekana hata umri wa miamba iliyotengeneza dunia inapimwa kwa muktadha uleule,point yangu ni hiv,hata ukienda mkoa kule kwenye asili ya ukoo wenu halisi kabsa bas kuna stor nyiiing sana za eneo lile,..same thing kwa ukienda uyahudin utakuta stor nyiiing za eneo lile ila tuu wenzetu waliamua stor yao kuiweka kwenye maandish,sasa nachoshangaa kwa mswahil ngoz nyeus kujifanya naye et stor yake ni ya wale wayaud,..y?mi naamin Mungu huyu wa kwel aliumba dunia kwa style yake anayoijua mwenyew na siri nying anazo yeye,haya mambo yakukisia kisia sjui nin mi naona ni ya binadam tuu kutaka kujua ukwel ndo ina result kwenye stor zoote hiz mara likaenda hili mara lile,maneno meengi,alieumba huu ulimwengu aliuumba perfectly kabsaa kwa habitat ya binadam kuish na wanyama na mimea na bacteria etc,sasa mtu kujifanya maisha ya dunian ni kama laana vile kutwa kudream heaven,Alietuumba atakua anashangaa sana kwamba yeye kutupa yote haya amekosea au?
 
Hakuna utawala uliotawala wala utakaotawala dunia. Wamasai wengi hawajui rais wa Tanzania ni nani. True stori tembea Arusha vijijini. Ndio maana North Korea ni ndimu. Je utawala wa Roma una athari gani kwa wachina wachina na ndio wengi duniani.

Na unaposema Anglican wanatawaliwa na Roma kwa sababu asili yao ni waroma hapo umechemsha kwa sababu uroma ulipingwa watu wakaanzisha makanisa yao yanayojitegemea.
Leo hii Vatican haitawali kisiasa hata Italy kwenyewe na kidini ndio kabisaaa.
 
Mada zinazojadiliwa kwenye mlengo wa kidini huwa zinawafanya watu wa mjadala kuwa wafungwa kimawazo kwa kuwa wote mawazo yanafanana au kuzungukia humo humo...kwenye kiboksi cha maandiko hivyo kukosa mawazo huru na kukosa elimu stahiki.....
 
Sasa Mimi nilikua mroma roma sugu familia nzima ...kanisani nilikua nakaa karibu na padri nadhan mnaelewa ....,....ila nilisikia tu habari ya siku ya ibada ni IPI ???? nikaanza kusoma maandiko na kuuliza baadhi ya watu wadini ...lakini kila nilipokua nikimuuliza padri Wangu alikua akinambia nitakujibu jumapili ijayo hatimae nikaanza kukata tamaa nikawa sionekan tena pale mbele ...Kwa kusoma na kudadisi Nikagundua kua Sabato ya Mungu ni Juma mosi ...Nabiblia pekee ndio inayotoa jibu ....nampaka sasa Familia nzima tu wasabato kasoro Baba yangu lakini naye nikipata muda narudi huwa nazidi kumpa somo ..naniaamini mauti hayatomfika kabla naye hajawa msabato.

Somen Biblia mjue ukuu Wa Mungu ...ujanja na porojo zakubisha bisha alafu biblia hujawahi hata kuigusa pengine hujui inauzwa shilingi ngapi no way zaidi ya kupotea tu.
Ulijua kama ni jumamos maana hii calendar imebadilishwa sana
 
Bila shaka ndugu wewe ni msomaji wa vitabu vya Danieli na Ufunuo!
Ukisoma vizuri Danieli 9:20-27, utaelewa kwamba utawala wa Roma utatawala juma la 70 (wiki 1). Kinabii wiki 1 = miaka 7. Kipindi hicho kitaanza baada ya unyakuo wa kanisa (waliompokea Yesu Kristo kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yao walipokuwa duniani). Wakati huo serikali zote duniani zitakuwa chini ya serikali kuu moja zikipokea amri za kiutawala kutoka kwa mkuu mmoja ambaye ni serikali ya Roma (mfano wa utawala huo ni kama Raisi Magulifuli alivyo na mamlaka kwa wakuu wote wa mikoa yote ya Tanzania). Huyo Rumi (Kaisari) atatawala kwa kushirikiana na mataifa mengine 10 (rejea Danieli 2:33, 41 - sanamu aliyoota Nebukadreza). Wakati huo hakuna atakayekiuka amri hata moja ya mtawala huyo yaani Rumi. Huyo Rumi (Kaisari) atakuwa na nguvu sana, na ndiye Mpinga Kristo.
Tujiulize, kama Roma ndiyo inatawala dunia kwa sasa je, kila serikali iliyoko duniani inatii kila amri kutoka kwa huyo mkuu (Kaisari=mpinga kristo)? Je hizo serikali zinatekeleza policy za huyo Mrumi? Jibu ni hapana. Kipindi hicho bado hakijafika ila hakiko mbali (2Thesolanike 2:1-10). Wateule kuweni macho!
70% right
 
Hapa alieandika biblia alikuwa na IQ kubwa mpaka watu mnabishana kwa stor za kusadikika kutojielewa sisi ni kitu gani ndo kunasababisha kuwepo kwa sintofahamu kama hizi za mleta uzi
Kuna hasara kubwa walioturetea hawa watu hadi hatuwezi kujadili kujihusu sisi badala tunapigania assumption zao sisi zetu zi nalala
Hivi kwann mmelala kiasi hicho kwann amfikirii chochote zaidi kariri za vitabu kwann lakini
Mna macho hamuoni mna masikio hamsikii mna pua hamnusi kila mlango wa fahamu hamtumiii
Badilikeni badilikeni khaaaa. Sio siri mnakera
 
Pengine ufalme utakao tawala milele na milele ni wa mungu jehova,yeye aliesema yupo ambae yupo,Neno aliekuwepo tangu mwanzo,ambae bila yeye hakuna chchote kitakachofanyika.
 
HIVI KANISA LA SABATO LILIANZA LINI?
MISINGI YAKE NI IPI?

WANASIMANIA NINI HASA?
 
Mi sio.msabato wewe tatizo.la wakatoliki.na ugomvi wenu na wasabato.mnadhani kila.mtu msabato...Poor You. Ni kama waislamu wanavyohubiri mfumo kristo kuwa serikali imeingia mkataba na wakristo ilihali ni mikataba ya wakatoliki. Wanachanganya wote. Wake up!
Plus Mungu hana Dini. So toa porojo zako hapa za ukatoliki na usabato. Mleta mada alileta mada kutoka kwenye bible hakutoa kwenye kitabu cha sabato au catholic so bora ubishane na hiko kitabu
Mikataba??? To a uthibitisho
 
Jibu swali ,ni wap unapata ushahidi au andiko kuwa kufufuka kwa Yesu ndio siku ya ibada?
Soma Biblia katika sehemu tano zifuatazo, zinatosha kabisa: Isa 1: 13, Hos 2 :11, Ebr 4: 4-10, Kol 2: 16-17 na Rum 14: 1-10
 
Amri ya 4 ya Mungu inasema "Ikumbuke siku ya sabato uitakase. Siku sita fanya kazi, utende mambo yako yote. Lakini siku ya saba ni sabato ya Bwana Mungu wako, siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe wala mwana wako, wala binti yako, wala mtumwa wako, wala mjakazi wako, wala mnyama wako wa kufuga, wala mgeni aliye ndani ya malango yako. Maana kwa siku 6 Bwana alifanya mbingu na nchi na bahari na vyote vilivyomo, akastarehe siku ya saba, kwa hio Bwana akaibarikia siku ya sabato akaitakasa. Kutoka 20:8-11.
Hio ni amri ya Mungu iliopindishwa na papa... Kanisa Katoliki hawaisomi jinsi ilivyo ktk Biblia Takatifu
Yesu alipoulizwa amri iliyo kuu alijibu IPI???
 
Back
Top Bottom