Ronaldinho alikuwa zaidi ya Messi Barcelona

mchezaji bora ni ibrahimovic zlatan tu,ambaye hucheza anavyotaka,hufunga anavyotaka,na anapiga carrate,he is a reaay superstar
 
Well written Sikonge, nilisoma maelezo ya Deco kuhusiana na Barca hii ya sasa, yeye alisema Barca hii haina tofauti na ile ya kwao kwani game approach ni ileile na wana maintain-philosophy-ileile isipokuwa tofauti kubwa ni Messi.
Kwa miaka mingi Barca wana maintain philosophy yao na ukifuatilia utaona huwa inaundwa kupitia wachezaji ambao huibeba timu.

kwa mfano Fernando Daucick aliijenga Barca kupitia Ladislau Kubala, Herenio Herera yeye aliunda barca kupitia Luis Suarez, ikaja Barca iliyoundwa kupitia Johan Cruyf na pia Cruyf aliunda timu yake kupitia Hristo Stoichkov, Van Gaal yeye alikuwa na RIVALDO na Figo, ikaja Barca ya Ronaldinho na Eto'o chini ya Rijkaardt.

Kila mtu anajua kuwa Pep Guardiola aliunda Barca kupitia Messi, Tito yeye anafikiria sana La Masia, lakini all in all Barca remains the same
 
Hakunaga kama DINHO. Yule ni mtakatifu katika soka. MSIJARIBU KUMFANANISHA NA MESSI JAMANI. Dinho anajua sana, yule jamaa hata akileta kanisa au msikiti bongo mimi nitakua muumini wa kwanza. Daaah mzee wa back and away.
 
Ongeeni tu ila unapomzungumzia Lionel Messi ni habari nyingine kabisa. Anajua majukumu yake uwanjani.

MKuu, Mesi ni mzuri, lakini Gaucho ni shughuli nyingine kabisa, Messi nje ya viungo wa Barca (Xaxi, Iniesta nk) si kitu kabisa na ndio maana hana mafanikio yoyote kwenye timu yake ya taifa, na hapo ndipo Gaucho anapomzidi Messi
 
Kombe la dunia lililofanyika SA, sports commentators waliweka wazi kuwa Lione Messi amepwaya na michuano imekosa msisimko kutokana na kukosekana kwa Ronaldinho. Hakukuwa na mchezaji aliyewaza kuonyesha umahiri wa GAUCHO, licha ya wapambe (waandishi uchwara) kumwita Messi -The Megician kabla hajaingia uwanjani na kuchemsha vibaya mno.

Messi ni mfungaji bora ni makosa makubwa ambayo fifa wamefanya na hizo kamati feki zinazoundwa na waandishi wa habari kumpa Messi uchazaji bora wa dunia. Msimu uliopita hakupata mafaniko yoyote kupelekea team alizochezea kuanzia timu ya taifa mpaka BARCA . Iweje watu waliopelekea timu zao kupata mafanikio msimu uliopta kama Ronaldo ama Drogba wasiwekwe kwenye list wampe mtu aliyestahli ufungaji bora na si uchezaji bora.
 


Mwana mtoka patamu umemsoma kamanda hapo juu?
 
mwmabie mnazi wa messi huyo mtoka kupaya......na alaaniwe dunga mpumbavu sana huyu kocha aliniuzi sana....
 
Mwana mtoka patamu umemsoma kamanda hapo juu?

Bado siamini kuwa wewe na huyo mwalimu wako ndio mna akili saaaana kuliko jopo la makocha 193 waliomchagua Messi kuwa mchezaji bora.

Huyu mwenzako ndio ameenda mbali na ku-suggest Drogba ndio angekuwa mchezaji bora....kwa ukweli ni kichekesho. Mtu timu yake ikidifensi 90mins na kufunga kagoli kamoja basi aliyefunga hako kagoli ndio mchezaji bora wa dunia tehe tehe tehe. kweli mwaka wenu huu, mtaongea sana.

Eti FIFA wamefanya makosa, tuzo haitolewi na FIFA ni makocha na makapteni wa timu za taifa ndio wanapiga kura kumchagua mchezaji bora na si kwamba Blatter na mkewe wanakaaa na kuamua kama mnavyofikiri
 
mwmabie mnazi wa messi huyo mtoka kupaya......na alaaniwe dunga mpumbavu sana huyu kocha aliniuzi sana....

Punguza jazba. Huyo Mwakalinga hata hajui tuzo inatolewaje. Anafikiri kibongobongo zaidi ndio maana anasema FIFA ilikosea.

Messi kupewa tuzo si pendekezo la FIFA, ni jopo la makocha na manahodha wa timu za Taifa ndio hupiga kura, upo hapo? Kwa hiyo kama nyinyi watatu mnajua zaidi yao, sawa.
 
Tell me braza

Kila Team inataman kumpata Messi, Trust me Bro Hakuna Pesa ya Kumtoa Lionel Messi pale Barcelona. Ndio maana Team yoyote ikitaka kumsajil kwenye mazungumzo hata wiki moja haichukui, unapomzungumzia Messi basi unazungumzia Habar nyingine katika SOKA, nenda pale Madrid kauze wachezaji wote rudi na uingereza ukauze wachezaji wa Team kubwa wote na bado usipate ela ya kumnunua. Nkwambie kitu kingine tena!!!???
 
MKuu, Mesi ni mzuri, lakini Gaucho ni shughuli nyingine kabisa, Messi nje ya viungo wa Barca (Xaxi, Iniesta nk) si kitu kabisa na ndio maana hana mafanikio yoyote kwenye timu yake ya taifa, na hapo ndipo Gaucho anapomzidi Messi

Shame on you.


Mpira hauchambuliwi kupitia magazeti ya sh mia tatu ya bongo, kama unataka kuuchambua ingia maktaba na angalia mechi.

Messi ana medali ya dhahabu ya Olympic ya mwaka 2005. Kwa taarifa yako, kwenye michuano hiyo yeye ndie alikuwa mfungaji bora (6 goals)

Kama ni Xavi na Iniesta hata Gaucho alicheza nao, mbona na yeye asiwe mchezaji bora mfululizo?

La tatu, (hii ni kwa faida yako na mama Yo Yo, Gang Chomba na wengineo) Messi kwa muda wote aliochezea timu ya Taifa ya Argentina amekuwa akicheza kama Playmaker (namba 8) ukiondoa mwaka 2012 ambapo kwa mara ya Kwanza amecheza kama Namba 10 na kudhihirisha kuwa hakabiki, mechi yake ya kwanza tu kucheza kama mshambuliaji alipiga Hat-Trik. Kumbuka hapo mwanzo jukumu la kufunga lilikuwa kwa Tevez na Higuan (Fuatilieni mpira sio majungu tu)

Kwa kuongezea, magoli 4 kati ya 12 aliyoifungia Argentina mwaka 2012 ameyafunga baada ya kumaliza beki zote kwa chenga za maudhi
 

Tell me braza
 
Messi is overrated........
He is what i call a media sensation
For me Gaucho hands down

Kama ulivyosema, FOR YOU.

Lakini kwa mujibu wa makocha wa vilabu na manahodha wa timu za taifa, Messi ndio bora zaidi.

Na hata kama ni kumshindanisha basi Ronaldinho sio saizi yake, yupo mtu mmoja tu: Ronaldo de Lima 'The Phenomenon Boy'. Haya anayobebewa mbeleko Gaucho hata Gervinho na Kanu wamefanya
 
usisahau pia kuwa Messi ndiye aliyeongoza kwa kufunga magoli mengi kwenye timu za taifa mwaka 2012, alifunga magoli 12, akifuatiwa na Neymar magoli 11.
 
haya mambo ya kuangalia mpira ukifika DSM ndio haya matatizo yake kila mchezaji akisifiwa wewe ukiambiwa alikuwa anacheza kama Messi,hivi hukuwahi kuona mchezaji zaidi ya Messi?
kama Gaucho anacheza sasa basi Messi haoni ndani kweli Messi amefunga magoli mengi hakuna ubishi lakini mpira alikuwa anacheza Gaucho wewe umekuja leo Dar unataka watu wote wajue kuwa Messi ndio mchezaji mzuri sasa kwani nani kakubishia, umeambiwa Gaucho alikuwa zaidi ya Messi
haya mambo ya kuangalia mpira kwenye TV ukubwani yana taabu kweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…