Ronaldo de Lima abatizwa na kuwa Mkristo!

Ronaldo de Lima abatizwa na kuwa Mkristo!

Duh! Sijasoma comments za akina FaizaFoxy na wenzake wale wa nyuzi zile. Ni mnyukano wa wakristo wenyewe kwa wenyewe, wengine hawaelewi kitu kuhusu ubatizo, wanapita kimya kimya. Ubatizo wa maji kidogo ulianza pale yule mfalme wa rumi alipokubali kuwa mkristo, wakambatiza kistarabu kwa maji kidogo kama kumuheshimu badala ya kumpeleka mtoni kumzamisha. Ikawa ni mapokeo hadi leo ingawa kuna madhehebu hayakubaliani na ubatizo wa maji ya kunyunyuziwa kidogo kichwani. Ubatizo halali ni kuzamishwa na kuibuliwa katika maji mengi. Maana yake ni kuuzika utu wa kale na kuibuka utu mpya, yaani unakuwa mtu mpya katika maisha mapya ya kikristo, sawa na kufa na kufufuka kwa Yesu Kristo.
 
Mshambuliaji mashuhuri duniani Ronaldo de Lima amebatizwa katika Kanisa la Sao Jose do Jardim Europa Parish huko Sao Paulo.

Ronaldo de Lima ame post picha kwenye Instagram page yake na kusema "Imani ya Kikristo imekuwa msingi muhimu wa maisha yangu toka utoto ingawa nilikuwa sijabatizwa. Kwa sakramenti hii najisikia kuzaliwa upya kama mtoto wa Mungu kwa namna mpya, kihisia na kwa undani kabisa."

Hongera kwake kuamua kujikabidhi kwa Kristo.

Sio ubatizo huo
 
Umekalili vibaya mnoo


Ngoja nikuulize maswali matatu ya ubatizo afu nyie wote mnaofanana mnijibu.


Kwanza ni kweli ubatizo ni neno la kigreek lenye maana ya kuzamishwa- kwa kiswahili kisicho fasaha sana.

Hata neno pentecoste mnalodhania ni siku ya Roho Mtakatifu maana ake ni siku ya 50.
Eti kanisa la kipentekoste, kanisa la kihamsini guys amkeni. Anyways hili tuliache.

Ubatizo wa maji mengi au machache ulianza kuwa practiced lini? Hapa kama hujui historia ya kanisa hutakaa uje ujibu hili swali. Hapa ni lazima usome Church Fathers au Apostolic Father lazma tena uwasome Apologetic Fathers. Otherwise huwezi jibu hilo swali.

Twende kibiblia maana utasema hayo ni mapokeo ila naomba twende polepole tujibu huu ubatizo ulikuwa wa aina gani.


1. Kuongoka kwa Sauli/ Paulo na kubatwa kwake. Nitanukuu...

Ukiweza soma Matendo 9 yote upate context.

Kisha Anania akaenda kwenye ile nyumba, akaingia ndani. Akaweka mikono yake juu ya Sauli akasema, “Ndugu Sauli, Bwana Yesu aliyekutokea njiani amenituma kwako ili upate kuona tena na ujazwe Roho Mtakatifu.” Ghafula vitu kama magamba vikaanguka chini, kutoka machoni mwa Sauli, akapata kuona tena. Akasimama, akabatizwa.
Matendo 9:17‭-‬18


Mwenye akili aniambie huyu Mtume Paulo alibatizwa mto gani hapo kwenye nyumba? Na je kama ubatizo ulifanyika kwenye nyumba maji yalikuwa madogo au mengi?

Kama ubatizo wa maji ya mtoni ungekuwa lazma huyu Anania angeongozana na wenzake kwenda mtoni na huyo kipofu sauli akambatize huko ila hilo halionekan apo.


2. Ubatizo wa Mrumi Kornelio

Na nukuu kama ilivoandikwa.


Kwa kuwa waliwasikia wakinena kwa lugha mpya na kumwadhimisha Mungu. Ndipo Petro akasema, “Je, kuna mtu yeyote anayeweza kuzuia watu hawa wasibatizwe kwa maji? Wamempokea Roho Mtakatifu kama sisi tulivyompokea.” Kwa hiyo akaamuru wabatizwe kwa jina la Yesu Kristo. Wakamsihi Petro akae nao kwa siku chache.
Matendo 10:46‭-‬48



Naomba jina la huu mto nyumban kwa huyu mtu wa mataifa.


3. Paulo na Sila kumbatiza askari wa gereza walimokuwa wamefungwa.

Wakamjibu, “Mwamini Bwana Yesu Kristo, nawe utaokoka, pamoja na watu wa nyumbani mwako.” Wakamwambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwako nyumbani mwake. Wakati ule ule, yule mkuu wa gereza akawachukua, akawaosha majeraha yao, kisha akabatizwa yeye pamoja na wote waliokuwa nyumbani mwake bila kuchelewa.
Matendo 16:31‭-‬33


Hii familia ya huyu askari walienda kubatizwa mto gani?
Je. Maji yalikua mengi au madogo/machache?

Swali chokonozi. Ubatizo wa watoto wa dogo ni ruksa au sio? Maana hapo walibatizwa yeye na familia yake yote [emoji38] au hii familia haikuwa na watoto? Au kama walikuwepo mbona hatusikii wakisema watoto waliachwa hawakubatizwa?


Zingatia Jeografia ya Israel haina mito mingi tangu zamani hadi leo

Basi hii ni mifano michache kibiblia ambayo majibu unayo wewe msomaji
Asante sana Mkuu... Nimejifunza jambo hapa maana ilikua inanipa ukakasi.. kumbe kuna jamii ina refer zaidi ubatizo wa Yesu kule mtoni na wanasahau kuwa mitume walipo pewa uweza waliendelea kubatiza hata nje ya hiyo mito

Thanks Brother [emoji120]
 
Wewe unataka battle za dini, kwenye ubatizo maji ni ishara tu na sio yanayotakasa. Hakuna andiko lolote linaloelekeza ubatizo uwe wa maji kiasi gani zaidi wengi mnakimbilia ku refer Yesu kubatizwa mtoni na maana ya ubatizo yaani kuzamishwa!

Kiasi cha maji hakijawahi kuwa issue toka enzi za mitume. Mkitoka kusema lazima yawe maji mengi itabidi tuulizane kiasi gani? Kwa maelekezo ya mapokeo au maandiko gani? Mkitoka hapo wengine watasema Yesu alibatizwa mtoni hivyo lazima ukabatizwe kwenye mto tu! Wengine watasema lazima uende mto jordan penyewe! n.k

Christianity sio imani ya juzi, tumepokezana miaka 2000 sasa kuanzia utaratibu wa ibada hadi masakramenti, you can't teach the church my friend! Hili sio Kanisa liloanzishwa na mtu tu.
Inafikirisha sana.Ni sawa sawa na mtu anaposema kuongelea alafu akasema hata ukiingiza mguu mmoja tu kwenye maji ni kuogelea.Wakati maana na amntiki nzima ya mtu anayepiga mbizi lazima awe kwenye maji
Suala la ubatizo tukiacha ushabiki wa kidini liko wazi sana.Hata ishu ya kilevi inaweza kuwa debatable ila siyo ubazo.Kwanza neno lenyewe tu ubatizo.Ni kitu kilichotowezwa au zamishwa.
Shida moja tunapenda sanadini zetu kuliko uhalisia na ukweli wa mambo.Tuache ukatoliki,uprotestanti au upentekoste.Tuache maandiko yaongee.
 
Back
Top Bottom