Rula ya Mafisadi
JF-Expert Member
- Dec 28, 2024
- 404
- 852
Huyu Rose Mayemba Mjumbe wa Kamati kuu ya CHADEMA namfananisha na Kamala Harris wa Marekani hapa Mdee na Bulaya wakasome
Nimesikiliza wanasiasa wengi sana hapa Tanzania na Africa huyu binti ni tunu na hazina ya Taifa.
Rose Mayemba nimempenda bure huyu dada.
===
Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA Rise Mayemba , amesema kuwa kampeni ya No Reforms No Election siyo tu harakati za madai ya uchaguzi huru na haki, bali ni mapambano ya kurejesha rasilimali za nchi mikononi mwa Watanzania.
Akihutubia kwenye mapokezi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, wilayani Ikungi mkoani Singida, Mayemba alisisitiza kuwa kampeni hiyo inalenga kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na utajiri wa nchi kwa usawa.
"Hii ni kampeni ya kuondoa nchi kutoka mikononi mwa wachache na kuirejesha kwa wananchi wengi. Ni mapambano ya kuzinusuru bandari zetu, madini yetu na rasilimali za taifa ambazo zimeporwa na wachache," alisema Mayemba huku akishangiliwa na wafuasi wa chama hicho.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Aliongeza kuwa mchakato huo hautakuwa rahisi kwa sababu mfumo uliopo unanufaisha wachache, lakini akasisitiza kuwa Watanzania wakisimama kwa umoja wanaweza kufanikisha mabadiliko hayo.
"Kama keki ya taifa itagawanywa sawa, kila mmoja atapata haki ya kutibiwa hospitali wanazotibiwa wao na watoto wao, kusomesha watoto wao kwenye shule bora wanazosomesha watoto wao, na kufaidika na rasilimali za nchi hii," aliongeza.
Kampeni ya No Reforms No Election inahamasisha mageuzi ya mfumo wa uchaguzi ili kuhakikisha haki na usawa kwa vyama vyote vya siasa kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu. CHADEMA na viongozi wake wameendelea kusisitiza kuwa bila mabadiliko hayo, hawatashiriki uchaguzi ujao.
Mapokezi ya Tundu Lissu wilayani Ikungi yamevutia maelfu ya wananchi na wafuasi wa CHADEMA, wakidhihirisha kuongezeka kwa mwamko wa kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.
Nimesikiliza wanasiasa wengi sana hapa Tanzania na Africa huyu binti ni tunu na hazina ya Taifa.
Rose Mayemba nimempenda bure huyu dada.
===
Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA Rise Mayemba , amesema kuwa kampeni ya No Reforms No Election siyo tu harakati za madai ya uchaguzi huru na haki, bali ni mapambano ya kurejesha rasilimali za nchi mikononi mwa Watanzania.
Akihutubia kwenye mapokezi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Lissu, wilayani Ikungi mkoani Singida, Mayemba alisisitiza kuwa kampeni hiyo inalenga kuhakikisha kila Mtanzania ananufaika na utajiri wa nchi kwa usawa.
"Hii ni kampeni ya kuondoa nchi kutoka mikononi mwa wachache na kuirejesha kwa wananchi wengi. Ni mapambano ya kuzinusuru bandari zetu, madini yetu na rasilimali za taifa ambazo zimeporwa na wachache," alisema Mayemba huku akishangiliwa na wafuasi wa chama hicho.
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Aliongeza kuwa mchakato huo hautakuwa rahisi kwa sababu mfumo uliopo unanufaisha wachache, lakini akasisitiza kuwa Watanzania wakisimama kwa umoja wanaweza kufanikisha mabadiliko hayo.
"Kama keki ya taifa itagawanywa sawa, kila mmoja atapata haki ya kutibiwa hospitali wanazotibiwa wao na watoto wao, kusomesha watoto wao kwenye shule bora wanazosomesha watoto wao, na kufaidika na rasilimali za nchi hii," aliongeza.
Kampeni ya No Reforms No Election inahamasisha mageuzi ya mfumo wa uchaguzi ili kuhakikisha haki na usawa kwa vyama vyote vya siasa kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu. CHADEMA na viongozi wake wameendelea kusisitiza kuwa bila mabadiliko hayo, hawatashiriki uchaguzi ujao.
Mapokezi ya Tundu Lissu wilayani Ikungi yamevutia maelfu ya wananchi na wafuasi wa CHADEMA, wakidhihirisha kuongezeka kwa mwamko wa kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.