Rostam Aziz of New Habari Corporation: The facts

Hoja ya Rostam Aziz Bungeni


Source: MwanaHALISI
 
TAHARIRI YA MwanaHALISI KUHUSU VITISHO VYA ROSTAM

TUMESOMA katika vyombo vingine vya habari kwamba mfanyabiashara kigogo na Mbunge wa Igunga, Rostam Azizi, amefungua kesi dhidi ya gazeti hili la wananchi-MwanaHALISI.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, kwa kuwa sisi hatujapewa taarifa rasmi, madai ya Rostam Azizi ni kwamba gazeti hili "limemchafua" jina lake. Anataka gazeti limlipe Sh 3 bilioni (3,000,000,000) kama fidia ya kusafisha" jina lake.

Zaidi ya hayo, Rostam anaiomba mahakama iamuru tusiandike habari zake. Wakati tunasubiri taarifa rasmi kuhusu kushitakiwa kwa gazeti hili, tunapenda kusisitiza kwamba kwetu, hiki ni kitisho kingine.

Anachojaribu kufanya Rostam Azizi, ni kufunga mdomo wa wananchi wanaommulika yeye kama mfanyabiashara na mwanasiasa, ambaye matendo yake yanagusa moja kwa moja maslahi ya wananchi wa Tanzania.

Ifahamike wazi kuwa Rostam naye ni mmiliki wa vyombo vya habari, vinavyofanya kazi kama inayofanywa na MwanaHALISI, ingawa kwa viwango na malengo tofauti.

Lengo la MwanaHALISI linafahamika. Gazeti hili ni mdomo wa wananchi maskini wa Tanzania. Ni kioo cha kuwamulika wote walio na dhamana katika jamii, wanaozitumia vizuri na vibaya – Rostam akiwamo. Ni kauli ya wanyonge wanaonyanyasika kutokana na uroho wa wakubwa na wafanyabiashara wasio waaminifu.

Inawezekana Rostam Azizi alidhani nasi tungeingizwa katika mkumbo wa vyombo vya habari vilivyoanzishwa au kununuliwa kwa ajili ya kulinda majina ya viongozi wa serikali ya awamu ya nne na maswahiba wao. Amekosea!

Kinachomsibu Rostam Azizi kimeshawasibu wengine pia walio katika mkondo mmoja naye. Kinafahamika. Faraja kubwa tuliyo nayo ni kwamba walau sasa jamii inaanza kuwajua watu wasiopendezwa na kazi yetu, wanaotutisha na kutudhulumu.

Kwa muda mrefu, baadhi ya wanasiasa walijifunika utukufu wa kisiasa ambao walidhani wangeendelea kuwa nao kwa sababu wanazozijua. Hawakutarajia kumulikwa na kukosolewa, kazi ambayo tumeifanya vema.

Kwa hatua hii ya sasa ya Rostam Azizi ni dhahiri hataki kukosolewa. Lakini hatutaki kuamini kwamba Rostam Azizi amesahau wasifu wake katika jamii ya Watanzania.

Na hatutaki kuamini kwamba hajui kuwa hata haya yaliyoandikwa juu yake anayolalamikia sasa ni matone tu katika bahari ya mengi ambayo sasa anajaribu kuyazuia kwa kitisho cha mahakama.

Rostam si maskini. Lakini hilo halikumzuia kuwadai maskini Sh. 3 bilioni, ambazo kwake ni thamani ya jina lake. MwanaHALISI halina pesa ya kuwagawia matajiri.

Pesa kidogo inayopatikana ni kwa ajili ya kuwaunga mkono Watanzania wazalendo na maskini katika vita dhidi ya mafisadi kwa kutumia uhuru wao wa kuhabarishana na kuwasiliana.

Tunaamini kwamba vitisho hivi vya Rostam Azizi na "amri" anazoipa mahakama, havina nia njema kwa taifa, bali vina lengo la kuficha ukweli kwa umma kuhusu siasa na biashara zake.

Rostam anataka wananchi wafungwe mdomo, macho na masikio dhidi yake. Yeye ana pesa, na anadhani atazitumia pesa hizo hizo kutunyamazisha, na kuwadhulumu wananchi maskini tunaowatetea.

Tungependa kumweleza wazi wazi kwamba vitisho vyake havitawazuia wananchi kufikiri, kuchunguza, kusema na kujadili kuhusu ufisadi unaofanywa na vigogo na maswahiba wao.

Tuna hakika kwamba gazeti hili halijamkashifu Rostam, bali limeandika habari asizopenda zijulikane kwa umma. Tuna hakika kwamba shida ya Rostam- katika suala hili si pesa, kwani anazo nyingi kuliko hizi, bali anataka kulifilisi na kuliua gazeti hili.

Gazeti hili halipo tayari kuwasujudia mafisadi. Kama ambavyo tumekuwa tunafanya huko nyuma, licha ya vitisho kadhaa tunavyoendelea kukabiliana navyo. Tutaendelea kuandika bila kumwonea, kumpendelea au kumwogopa mtu yeyote.

Tutasimamia ukweli na haki na tutafichua ufisadi kwa maslahi ya taifa. Katika hili, hatutarudi nyuma; na kama Rostam Azizi anataka kutupeleka mahakamani, atangulie tutamkuta huko; na asubiri matokeo.
 
Haya maelezo yake na vielelezo vyote aende navyo maakamani, huko ndo njia nzuri zaidi ya kufanikiwa kujitetea na kuwaeleza vizuri Richmond ni ya nani.
 
Tutasimamia ukweli na haki na tutafichua ufisadi kwa maslahi ya taifa. Katika hili, hatutarudi nyuma;

Yes I said JF we Stand Before You coz we dare talk Openly.
 
That is the spirit Kubenea, watanzania wanakuthamini sana maana through you RA ataongea openly bila kukatazwa na ibara ya 15:1
 
Wapendwa naomba kuongeza hoja binafsi, is it true that ROST-TAMU A-ZEE is all alone in all these ? ninavyo muelwa mimi huyu bwana ana visenti vingi kama alivyosema yule msukuma. Je ni kweli hizi fedha ni zake au anamtumnzia mtu ? na kama anamtunzia mtu je ni nani? Nasikia eti yeye ndio Hazina ya kile chama chetu cha wenyewe ndio sisi? eti ndio hutumika kama production or money generation unit yao? mhhh just a comment.
 
Haya maelezo yake na vielelezo vyote aende navyo maakamani, huko ndo njia nzuri zaidi ya kufanikiwa kujitetea na kuwaeleza vizuri Richmond ni ya nani.

Jamco_za;

Nani alikuambia mambo yakijadiliwa bungeni yanaweza kupelekwa tena mahakamani?

Elimu ya uraia ndugu!

Umezoea kusikiliza upande mmoja!!! sasa wa pili huooo!!!!!!!!!!!
 
Tuna asili na rekodi ya kusema kweli, tena kweli tupu. Tunaamini katika kutenda na kutendewa uadilifu.

Hivi Rostam ana matatizo ya akili,Kwanini ametutusi watanzania..Rekodi ya kusema ukweli ameitoa wapi,ameshindwa kutuambia wamiliki wa RDc ni kina nani??Je ni mkweli huyu??
Mheshimiwa Spika, sisi wengine hatuna kawaida ya kuja na mbwembwe nyingi za kujisifu hata kama ni kwa gharama ya kulipotosha Taifa na kuwapotosha wananchi.
Kauli yake ,Ya sisi wengine ina maana alikuwa anaogelea watu wangapi??Yeye Lowassa,Karamagi,Dr Msabdaha na au???ina maana hii hoja ilikuwa imeandaliwa na watu wangapi?

Kwani wakati Lowassa anatoa hoja yake ya kuachia ngazi,Je zile siyo Mbwembwe??

angalia na alichosema hapa juu na hapa chini uone viroja na uongo mtupu
"Nadhani ni rafiki yangu Rostam Aziz".Mheshimiwa Spika, ni juu ya Ndugu Salva mwenyewe kuweka sawa kumbukumbu zake na kujua kwa uhakika ni nani aliyemtambulisha na Richmond badala ya kusema "anadhani".
Huu ni mchezo Mchafu na naomba Mungu atuepushe na hawa watu wabaya na wanyang'anyi wa nchi yetu.Mwanakijiji Read between s the lines.


Yesa I said,Rostam tangulia Mahakamani na tutakukuta huko!
 
kama mambo ndio haya mwanahalisi hajapelekewa taharifa rasmi, basi nimegundua huyu jamaa anaogopa kama MAFISADI wengine.

Anaogopa kuumbuliwa. Rostamu tia timu tu ujimalize mwenyewe.
 
Kumbe, Rostamu anaweza kufungwa hivi hivi.

Anyway labda kwa kuwa hatukupata book lake.
 
Nimewahi kusoma humu kuwa malipo kwa Dowans yanapochelewa mfuatiliaji huwa ni Rostam. Nilikuwa nashindwa kuelewa uhusiano mpaka niliposoma maelezo yake kuwa hiyo huwa ni hospitality arrangement baina ya wafanyabiashara kitu ambacho sisi tusio na uelewa wa uendeshaji biashara tunakiona cha ajabu. Hayo siyo matusi kwa watanzania ?
 
Nadhani naweza kuungana na Spika kuwa ilikuwa ni upuuzi kuleta hoja kama hii kwenye bunge. Naona kama Spika alifanya jambo la maana!
 
Nadhani naweza kuungana na Spika kuwa ilikuwa ni upuuzi kuleta hoja kama hii kwenye bunge. Naona kama Spika alifanya jambo la maana!

Mkuu kweli kabisa spika alikuwa na kila haja ya kuzuia hoja hii katika kulinda heshima ya bunge. haya yanaweza kusemwa kwenye mitaa wakati wa kunywa kahawa, na bia siyo bungeni.
 
ndiyo maana waliizima haina maana yoyote. Mimi nifikiri imewataja wamiliki wa RDL kuwa ni Mtoto wa EL an JK. Bravo camati ya maadili kuzima huyu fisadi asiseme huu utumbo mbele ya Bunge.
 
Harafu unashangaa kwa nini taifa letu halisongi mbele! Tunaweza kusonga mbele kweli na wabunge (eti wanaitwaga wawakilishi wa wananchi) wa namna hii? This ushahidi is just a crap hata kwa darasa la saba atajua kabisa!
Huyu bwana sijui alifutia ujinga wapi...au si atafute spinning machines wazuri basi? otherwise hao spinning doctors wake kama ndo waliandika hii barua ya ushahidi..wanakula mshahara wa bure...
 
The ball is on Rostam's court. It is his move now! Lets wait and see what follows next.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…