Rostam, Msabaha, Kikwete and Richmond - Yes I said it again!

Rostam, Msabaha, Kikwete and Richmond - Yes I said it again!

a. RDC iliingia nchini kwa ushirika wa Mhe. Msabaha (Mbunge - Waziri wa Madini)
b. RDC iliingia nchini kwa ushirika wa Jakaya Kikwete (Mbunge)
c. RDC (USA) wametoa mchango mkubwa katika kampeni ya Kikwete na Msabaha
d. Rostam Aziz ndiye mfanyabiashara aliyetengeneza mazingira ya wao RDC kujikita kwenye biashara hiyo ya energy. Yeye mwenyewe akiwa ni shemeji ya Kikwete.
e. Naeem Gire waliingia na asilimia 75 ya RDC (tanzania) na asilimia 25 zilizobakia zikigawanywa miongoni mwa wahusika wakuu.


so, now you know.

Hili la ushemeji lilinipita? Nani kaoa kaoa au kuolewa?
 
Kwa kweli ni vigumu kuona wapi JK anaingia kwenye hili la RDC moja kwa moja, maana mtiririko wa matukio ulikuwa unaonyesha kama vile na yeye alikuwa hapewi habari zilizokamilika, kitu ambacho share holder angetakiwa awe anajua mapema zaidi.

Lakini labda hii ziara ya Balozi Andrew Daraja, kule Houston, ni ya kudadisi zaidi maana bosi wake wakati ule alikuwa JK. Kwa mtazamo wangu ni kuwa, labda JK alifahamu yote kuhusu RDC kwa kupitia kwa best wake, Lowassa, lakini hakuwa among the key players.

Balozi Daraja kauli yake kwenye hili suala kama angehojiwa ingekuwa ni muhimu sana ili kuelezea huyo aliyemtuma kwenda kuipandisha chati RDC.

KUBWA JINGA HAYO NDIYO MANENO!

Ni kama ninayosema tuuuu!

Haya..Kuna wale wanaotaka kuwasafisha mafioso!

NO WAY!

MBONA HAWAULIZI KUWA KUNA WATENDAJI WAKUU AMBAO NDIO WASHAURI WA RAIS NA WALIANGUKA MASAINI NA KUMPA USHAURI KUHUSU RICHMOND?

Ok ilianza toka JK akiwa MBUNGE...Hii ina maana kuwa ukweli ndiyo usiwekwe wazi?

Na kama ni hivyo...Then mkataba wa Richmond ulikuwa facilitated na MKAPA!

WAMEMTEGA JK WA WATU NA SASA ANAKODOA MIMACHO TU HUKU MITI IKIENDELEA KUTELEZA!

Hao waliotajwa wakamatwe...Na hiyo mikataba IFUTWE!

ALIYEIPITIA HIYO MIKATABA NA KUMSHAURI RAIS KUWA KUWA INAFAA NDIYO RESPONSIBLE!

MBONA WALE WANAJESHI WA ABU GRAIB KULE IRAKI WALIOFANYA VITENDO VICHAFU VYA UDHALILISHAJI HAWAKUAMBIWA WAMETUMWA NA RAIS LICHA YA KWAMBA NI KWELI WALITUMWA VITANI?

Kama washauri hao walitumwa kufuatilia MIKATABA YA KULINUFAISHA TAIFA NA WAKAFANYA MAMBO YA TOFAUTI...

HATA KAMA RAIS MWENYEWE ALINUNULIWA HISA NDANI YA KAMPUNI HIYO BADO ANA HAKI YA KUWAGEUKA WATENDAJI WAKE WOTE WALIOSHIRIKI NA PIA HATA KUMFIKISHA MAHAKAMANI RAIS WA AWAMU YA TATU ALIYEYAJENGA MAZINGIRA HAYO MABOVU!

Wameutumia UDHAIFU HUO NA SASA WANAMFANYA JK AONEKANE NI KITUKO!

KAMA NA YEYE HASIKILIZI USHAURI THEN INA MAANA AMEKULA KIAPO NA MAFIA...NA KWA HIYO BASI ATALIINGILIZA TAIFA LETU MATATIZONI KWANI HANA MAAMUZI YEYOTE NA KAMA ANAYO..BASI YUKO HAPO KAMA PUPPET!

Mimi namwambia wazi kuwa bado mpango wa kesi upo pale pale!

Huko Bongo watafunguwa kesi lakini kama anafikiri hizi hapa ninazopiga ni kelele basi atafakari mara mbili!

Najuwa yeye keshafanya hivyo ila WAPAMBE WAKE BADO WANAMSHAURI VIBAYA!
SHAURI YAKE!
 
MKJJ: Sasa utaona ni wapi Rostam anapata nguvu.

Mimi hoja yangu imekuwa kwa nini tumekuwa tukiwakwepa wengine, na hasa JK, kwenye hili sakata la Richomond? Au ndio tunasubiri atoke madaraka ndio tumbebee bango kama tunavyofanya sasa kwa Mkapa? Huoni kama huu utamaduni hautasaidii sana kwenye haya mapambano yetu?


Kumkwepa Kikwete ni strategic move, huwezi kumuacuse Jaji ambaye ndio anamamlaka ya kutoa uamuzi katika kundi moja na watuhumiwa kwani kuwatia hatiani maana yake na yeye hafai, hivyo atajilinda kwa vyovyote, kinachofanyika sasa na kumchochea awachukulie hatua halafu akiishafanya tunamgeukia na yeye. wapinzani walikosea sana kumuweka JK kwenye list of shame, kwani alitakiwa aachwe ili a act against them ndio wamgeukie na yeye. Hivyo mambo ya ufisadi yangekuwa yameisha siku nyingi.
 
Mimi nilisema hapa siku nyingi kuwa haingii hakilini subordinate afanye kitu ambacho hamjakubaliana na superior akae kimya kusubiri report ya bunge. JK anausika moja kwa moja na RDC na ndo maana EL amekasirika kiasi kikubwa kuona ametoswa wakati mwenye mzigo anatesa.

Mkakati wa EL kurudi utafunua mengi kama JK mwenyewe hakujitokeza na kusema jinsi gani haliusika kwani wananchi hawatamwelewa JK kuona anamwachia EL arudi bila maelezo ya kutosha.

Anayefikiri kuwa wananchi hawatauliza swala la RDC amekosea kwani wananchi hivi sasa wako makini mfano ni Masha kuulizwa ushiriki wake na Deep Green Finance na akaamua kusema ukweli kwa kuitosa serikali na kusema walielekezwa na serikali kuanzisha deep green na kuifirisi.

Kikwete anafaamu issue zote za RDC, EPA, Deep Green na mengineyo yanayoendelea kutokea hivi sasa na ndo maana hakuna hata fisadi mmoja atayepelekwa mahakamani.
 
Mimi nilisema hapa siku nyingi kuwa haingii hakilini subordinate afanye kitu ambacho hamjakubaliana na superior akae kimya kusubiri report ya bunge. JK anausika moja kwa moja na RDC na ndo maana EL amekasirika kiasi kikubwa kuona ametoswa wakati mwenye mzigo anatesa.

Mkakati wa EL kurudi utafunua mengi kama JK mwenyewe hakujitokeza na kusema jinsi gani haliusika kwani wananchi hawatamwelewa JK kuona anamwachia EL arudi bila maelezo ya kutosha.

Anayefikiri kuwa wananchi hawatauliza swala la RDC amekosea kwani wananchi hivi sasa wako makini mfano ni Masha kuulizwa ushiriki wake na Deep Green Finance na akaamua kusema ukweli kwa kuitosa serikali na kusema walielekezwa na serikali kuanzisha deep green na kuifirisi.

Kikwete anafaamu issue zote za RDC, EPA, Deep Green na mengineyo yanayoendelea kutokea hivi sasa na ndo maana hakuna hata fisadi mmoja atayepelekwa mahakamani.


Kwa huu wa RDC, bado sijaona kiunganishi zaidi ya kile cha Balozi Daraja. Sidhani kama JK ni smart kuliko EL kwenye mambo ya kudokoa kiasi kwamba ashiriki na asiache trails zozote. Let'd dig deeper tusijepotea kwa kulazimishia mambo tusiyo na ushahidi nayo.
 
Mimi nilisema hapa siku nyingi kuwa haingii hakilini subordinate afanye kitu ambacho hamjakubaliana na superior akae kimya kusubiri report ya bunge. JK anausika moja kwa moja na RDC na ndo maana EL amekasirika kiasi kikubwa kuona ametoswa wakati mwenye mzigo anatesa.

Mkakati wa EL kurudi utafunua mengi kama JK mwenyewe hakujitokeza na kusema jinsi gani haliusika kwani wananchi hawatamwelewa JK kuona anamwachia EL arudi bila maelezo ya kutosha.

Anayefikiri kuwa wananchi hawatauliza swala la RDC amekosea kwani wananchi hivi sasa wako makini mfano ni Masha kuulizwa ushiriki wake na Deep Green Finance na akaamua kusema ukweli kwa kuitosa serikali na kusema walielekezwa na serikali kuanzisha deep green na kuifirisi.

Kikwete anafaamu issue zote za RDC, EPA, Deep Green na mengineyo yanayoendelea kutokea hivi sasa na ndo maana hakuna hata fisadi mmoja atayepelekwa mahakamani.

Inabidi AMTOSE KILA MTU!

Na pia akumbuke kuwa hata mikataba hiyo aliletewa na kuelezwa mazuri yake na kama angejuwa kuwa ina mabaya haya sidhani kama mtu mwenye akili timamu angekubali.

Hivyo kama unadai hatafanya kitu...Basi na sisi tutaomba afanyiwe MENTAL EVALUTATION ILI TUWE NA UHAKIKI KUWA RAIS WETU ANA AKILI TIMAMU!

Hadi sasa nina wasi wasi sana na uwezo wake wa Kufikri kwani na yeye anaona nafasi aliyonayo hata Mr Nice angeweza kuwa nayo bila wasi wasi!

Kwa maana hiyo basi...Yeye anaudharau Urais na haoni kama una maana yoyote ile...Kaufananisha na USANII!

Huyu kama ana mawazo hayo hafai hata kuitwa Rais!

Na hata huo uwaziri wa mambo ya nje sijuwi ni vigezo gani vilitumika akapewa cheo hicho!

Nafikiri vigezo vilivyotumika vya kumpa uwaziri wa mambo ya nje na kupewa Urais ni vigezo vile vile vilivyotumika kumyima urais pale mwalimu alipokuwa hai...Sasa mwanafunzi wa Mwalimu akajuwa kuwa yule amabaye hakutakiwa kuwa rais wakati mwalimu akiwepo..Basi ndiye huyo anayetakiwa kuwa rais wakati huu kwani ni kweli hana hata chembe ya ubinadamu na uwezo wa kufikiri kama binadamu wa kawaida!

Najiuliza sana...Baada ya mwalimu kufa...Mkapa akamalizia kuiuza nchi na wakati bado kila kitu hakijakaa sawa muda wake wa urais ukapita!

Sasa kwasababu Mkapa na yeye ni mwanamtandao...Basi akampa tafu mwanamtandao mwenzake ambaye alikataliwa na mwalimu.

Sasa ile nafasi amabayo hata mwalimu alifikiri inamtosha jk ya uwaziri wa mambo ya nje...Ndiyo hiyo Mkapa aliyompa na yeye bado kuendelea kutawala taifa!
 
...Anayefikiri kuwa wananchi hawatauliza swala la RDC amekosea kwani wananchi hivi sasa wako makini mfano ni Masha kuulizwa ushiriki wake na Deep Green Finance na akaamua kusema ukweli kwa kuitosa serikali na kusema walielekezwa na serikali kuanzisha deep green na kuifirisi.

Jamco, Masha ameweza kuulizwa maswali kwa sababu ni yeye mwenyewe anakubali maswali yoyote. Anaitisha vikao mbele ya wananchi.

Japo nae yuko under a cloud na law firm yake, lakini kwa hili nampongeza mno, na ni mfano wa kuigwa.

Kikwete anapoitisha press conference kuna ka understanding ka nidhamu fulani ya uoga kwamba huwezi kumuuliza chochote unachotaka. Mimi nishakuwepo Kikwete akiulizwa maswali anapokwenda Marekani ambapo vijana huwa wanakuwa na ka freedom fulani ka kuuliza. Lakini bado huwa wanakusanya maswali kwenye vikaratasi halafu wanayapiga panga kwanza. Na huwa hakuna such thing as a follow up once he starts obfuscating.

Masha is a trailblazer when it comes to having the balls to face public inquiry into his dealings. It may be tied to his upbringing in America, a more open society, and being of a later generation . That's why I say once that old guard of the ruling elite fades away there will be seismic changes, almost overnight overhaul of the way we run things. The Makamba's of the world will, one day, pave way for the new guard.
 
Muungwana aliwaamini sana Usalama, kwa sababu alimuonya mara nyingi sana Msabaha kuwa hii kampuni isipokuwa kweli atakiona cha moto,

Ninaamini kuwa muungwana hakujua michezo yote iliyochezwa na kina Lowassa, aliamini kuwa kampuni ni nzuri na hasa kwa kuhakikishiwa sana na usalama, ambao walikuwa wakipewa order za what to say kwa rais na mkurugenzi mstaafu ambaye ni rafiki wa karibu sana na lowassa na Rostam, ingawa tayari kulikuwa na mkurugenzi mpya, lakini nasikia yule wa zamani bado ana-run the show, yule ana mkono mzito sana kwenye hili soo la Richimonduli,

Muungwana hakujua kuhusu uhuni walioufanya hawa kina Lowassa, na hakuhusika na wizi wa hili deal, labda tatizo lake hapa ni kama Commander-In-Chief wa taifa letu na ndiye the Chief Law Enforcer, amefanya nini baada ya kujua kuhusu huu uhuni wa kina Lowassa na Richimonduli?
 
FMES... tafuta link ya Kikwete, Msabaha na kina Gire kabla ya uchaguzi Mkuu 2005. Utaelewa JK is not a bystander in this.
 
Muungwana aliwaamini sana Usalama, kwa sababu alimuonya mara nyingi sana Msabaha kuwa hii kampuni isipokuwa kweli atakiona cha moto,

Hiki kitu sikiamini.

Kikwete hajulikani kwa integrity ya hali ya juu hivyo.

Hakuna serious commentator in the country anaeweza kusema hayo hapo juu.

Bila substantiation, hiyo taarifa iimekaa kama imepikwa pikwa. Watu wazima tunashtukia!
 
Muungwana aliwaamini sana Usalama, kwa sababu alimuonya mara nyingi sana Msabaha kuwa hii kampuni isipokuwa kweli atakiona cha moto,

Ninaamini kuwa muungwana hakujua michezo yote iliyochezwa na kina Lowassa, aliamini kuwa kampuni ni nzuri na hasa kwa kuhakikishiwa sana na usalama, ambao walikuwa wakipewa order za what to say kwa rais na mkurugenzi mstaafu ambaye ni rafiki wa karibu sana na lowassa na Rostam, ingawa tayari kulikuwa na mkurugenzi mpya, lakini nasikia yule wa zamani bado ana-run the show, yule ana mkono mzito sana kwenye hili soo la Richimonduli,

Muungwana hakujua kuhusu uhuni walioufanya hawa kina Lowassa, na hakuhusika na wizi wa hili deal, labda tatizo lake hapa ni kama Commander-In-Chief wa taifa letu na ndiye the Chief Law Enforcer, amefanya nini baada ya kujua kuhusu huu uhuni wa kina Lowassa na Richimonduli?


Mkuu FMES,
Hapa nakubaliana na wewe kabisaa.

Inawezekana JK alijua kuwepo kwa uhusiano wa Lowasa na RDC, kama biashara zake Lowassa, lakini ukiangalia kabisa tokea pale alipochemsha kuahidi umeme wa RDC kuwaka, inaelekea kabisa hakuwa mshiriki wa moja kwa moja. Kufahamu inawezekana lakini nafikiri Lowassa alimficha mwenzake details.

FMES... tafuta link ya Kikwete, Msabaha na kina Gire kabla ya uchaguzi Mkuu 2005. Utaelewa JK is not a bystander in this.

Mkuu MMJJ,
Hapa inabidi kuwa makini tusijepoteza mwelekeo.

Hadi hivi sasa hatuna kiunganishi chochote hata cha kimazingira mwenye nacho akiweke. Ni muhimu tupate data angalau kiduchu kuliko tukamzulia wakati anayo mengi tu yaliyo yake, EPA, Meremeta n.k.
 
Kama Kikwete alihusika katika haya yote inakuwaje huyu mtu anajitenga kama vile hakushiriki kwenye kitu chochote?Hivi Tanzania hii kweli hamna vitu kama Orange Revolution ya Ukraine iliyomuondoa madarakani Victor Yanukovich alipoiba kura na kukaa madarakani.Yaani hamna mtu influential wa kuinfluence such a revolution?


Jamani wana JF ni kweli tuna uhuru wa kuongea hapa katika kijiwe chetu, lakini ni vyema kuwa na ushaidi. Mpaka sasa sijaona ushaidi wa Kikwete kushiriki katika hili la RDC tafadhali naomba mwenye huo ushaidi aumwage hapa kijiweni.
 
Bado,

Analysis za Mwanakijiji... ni za kufikirika kumuweka ubaya RA kama muhusika... narudia... kumuweka mtu/taasisi kama fisadi au mwizi... u must have clear evidence without doubt? Hayo mambo ya kutumia logic etc. ni uzandiki tu kama magazeti yanavyofanya watanzania wasijadili mambo ya maendelea bali wajadili mambo ya uchawi.

Hili la evidence... mwanakijiji ana-spin tu! nothing new....

Kwa mara nyingine naungana na Kitila... kwamba vita ya ufisadi.. inaelekea kutushinda maana hatufuati mafisadi tunafuata victim wa mafisadi...
 
Kwa wale ambao wanasema kwamba JK hakujua kitu kinachoendelea ama alidanganywa/shauriwa vibaya na wasaidizi wake kuhusu Richmond, mimi sikubaliani nao.

Kuna siku aliongea na waandishi wa habari, sikumbuki ni lini lakini alikuwa Ikulu, alisema mbele ya waandishi wa habari kwamba swala la Richmond akasema aliita FILE la Richmond na kulipitia lote na alijiridhisha kwamba Richmond haikuwa kampuni ya mtoto wa mkubwa! Swali la kujiuliza, alikuwa anaangalia vitu gani kwenye hilo file? Kwamba ni kampuni ya mtoto wa mkubwa ama mchakato mzima?

Kama akina Mwakyembe waliona uchafu kwenye mchakato mzima, ina maana yeye na wasaidizi wake hawakuona huo uchafu? Achilia mbali legality ya Richmond, bali the whole process mpaka tenda kuja kutolewa.

Kama alidanganywa na wana UWT na wasaidizi wengine, je, baada ya hayo mambo kuwekwa wazi amefanya nini? Maana hii ni aibu, haiwezekani Rais mzima useme ulidanganywa ama ulipewa wrong information na bado hapo hapo anasema kilichotokea kwa Lowassa ni ajali ya kisiasa. Kweli mtu aliyeku-mislead unaweza kusema amepata ajali ya kisiasa?

Kuna viashiria vingi sana kuonyesha kwamba JK knew a lot kuhusu hili swala labda alijipa matumaini kwamba after some time lingeweza ku-fade away na watu wakaendelea na mengineyo. Lakini likaja likawa kinyume na ndiyo maana Lowassa akapata ajali ya kisiasa!

Akina Mwakyembe kuna mambo hawakuyasema ili kulinda heshima ya serikali ya CCM, ni yepi hayo ambayo yalikuwa yanailinda serikali? Na by the way nani ni serikali ya CCM?
 
Hiki kitu sikiamini. Kikwete hajulikani kwa integrity ya hali ya juu hivyo.

Wewe kutoamini haina maana kuwa hakipo, Kikwete ana matatizo mengine mengi ya integrity lakini la wizi sio lake, lakini still ni haki yako kuamini as you wish. Hatuko hapa kurusha tu mawe bikla sababu au angalau ukweli kidogo, Kikwete mpaka leo bado ni masikini tu kama alivyoingia labda huko mbele ya safari.

Hakuna serious commentator in the country anaeweza kusema hayo hapo juu.
Bila substantiation, hiyo taarifa iimekaa kama imepikwa pikwa. Watu wazima tunashtukia!

Mkuu hapa tunajadili kwa hoja, sio hadithi za mitaani za kupika nani anaweza kupika hapa wakati ukweli wote uliotolewa kuhusu hii ishu tunaujua? Kupika ili iwe nini? Ripoti imetolewa wote tumeiona, maneno yote ya Kikwete during hii deal yapo clear tena wazi, kuwa kila mara alikuwa akimhoji Msabaha mambo yanaendeleaje, sasa mkuu akisema hoja ambayo haikubaliani na mawazo yako basi imepikwa, imepikwa na nani? Kwa nini hoja zako hazijapikwa au huwa hazipoikwi? Mbona hili la kupika kupika habari unalielewa sana?

Acha hizo mkuu, hapa tunajadili ishu nzito na muhimu sana kwa taifa, kumhusisha rais wa Jamhuri katika ufisadi unatakiwa kuwa na more evidence kuliko hivi, kwa sababu kuna some of us ambao bado tunaamini kuwa some integrity kwenye serikali yetu ingawa sio ya kuridhisha,

Unless kuna ukweli ambao haujawekwa wazi, uliopo so far haiumuhusishi Rais na Richimonduli, unasema commentators wa bongo na wewe kila siku unasema kuwa bongo hakuna press sasa hawa wapya unaowasema sasa wametoka wapi? Ushahidi hata wa mdomo tu between viongozi haupo kabisa wa kumuunganisha Rais na hii deal, Mkapa alimfundisha tabia ya kuwaamini usalama, na ndio walikuwa wakimhadaaa kwenye hii deal ambapo Rostam na Lowassa walikuwa wakimtumia mstaafu kumhadaa Rais, I believe that,

Lakini at the same token ninaamini kabisa kwa 100%, kuwa Rais alijua deal zote za kuchota hela za kampeni ya uchaguzi kule BOT kupitia makampuni ya ujanja ujanja, hili ninaamini kwamba ndio hasa kinachomfanya awe na aibu na Mkapa, ambaye ndiye aliyekuwa akisaini mpaka dakika za mwisho alipokuwa anenda Uwanja wa Taifa kukabidhi urais, alikuwa bado anasain watu kuchukua hela kule, kumuhusisha Rais na Richimonduli eti kwa sababu huwa hana integrity nafikiri ni too strong of a political language, au tu kwa sababu commentators wa bongo hawawezi kusema haya, basi ina maana Rais anahusika, hapana inahitajika more proof hata za mdomo bado kuzisikia,

Tungeshawasikia hata kwenye private wakionong'ona, ninaamini sehemu zote ambazo Rais anahusika haziguswi, na ninaamini sana kuwa ana something to na Chenge na deals zake, lakini Richimonduli sijaona angalau ushahidi kidogo tu!

Haya ni maoni yangu na ni haki ya wengine kuwa na maoni tofauti, lakini hina maana kuwa kwa sababu ni tofauti na yangu basi yatakuwa yamepikwa.
 
Keil,

Ni kwa bahati mbaya watanzania tuna matatizo mengi sana... hebu angalia... Mh. Lowassa alithubutu kutaka kuvunja mkataba wa Richmond mara mbili, kila moja akiambiwa kwamba ukivunja taifa litapata hasara zaidi... na mshauri mkuu hapa ni Taasisi inayoitwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali chini ya Mh. Mwanyika. Baadaye hili lilisababisha waziri Mkuu kumwaga unga...

Sawa Mh. Lowassa alifuata ushauri wao akijua anashauri vizuri kwa manufaa ya taifa... juzi juzi serikali hiyo hiyo ikaweza kuona vifungu ambavyo wameamua kuvitumia kuvyunja mkataba ule ule ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliosema tusivunje....

Sasa angali Mwanasheria Mkuu wa Serikali Anakula Kuku hadi leo... wakati yeye ndio source ya matatizo yote...

Ambayo hawako direct na uvundo huo... ndio wanaathirika... Mh. Lowassa amejiuzulu, Mh. Rostam anasakamwa...

Ninyi watanzania muna matatizo gani... kwa nini hafuati kwenye matatizo munasumbuka na watu wengine?
 
Ni kwa bahati mbaya watanzania tuna matatizo mengi sana... hebu angalia... Mh. Lowassa alithubutu kutaka kuvunja mkataba wa Richmond mara mbili, kila moja akiambiwa kwamba ukivunja taifa litapata hasara zaidi... na mshauri mkuu hapa ni Taasisi inayoitwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali chini ya Mh. Mwanyika. Baadaye hili lilisababisha waziri Mkuu kumwaga unga...Sawa Mh. Lowassa alifuata ushauri wao akijua anashauri vizuri kwa manufaa ya taifa... juzi juzi serikali hiyo hiyo ikaweza kuona vifungu ambavyo wameamua kuvitumia kuvyunja mkataba ule ule ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iliosema tusivunje....

Sasa angali Mwanasheria Mkuu wa Serikali Anakula Kuku hadi leo... wakati yeye ndio source ya matatizo yote...Ambayo hawako direct na uvundo huo... ndio wanaathirika... Mh. Lowassa amejiuzulu, Mh. Rostam anasakamwa...
Ninyi watanzania muna matatizo gani... kwa nini hafuati kwenye matatizo munasumbuka na watu wengine?

Waziri Mkuu hakufuata ushauri wa kiongozi yoyote kwenye hili la Richimonduli, alikuwa akifuata ushauri wake tu, ni yeye aliyeivunja kamati ile yenye wataalamu na kuunda mpya yenye watu wake kina Mwakapugi, na Mwanasheria Mkuu ambaye hata kamati ya Mwakyembe imeshauri afukuzwe kazi mara moja,

Lowassa ndiye aliyekuwa mhusika mkuu wa hii deal, kama hakuwa basi alikua na nafasi zote za kusema maneno yake bungeni akasikilizwa, hata Rais alimkatalia kumsikiliza tena nyumbani kwa Rais, sasa huyu ulitaka apone halafu Mwanasheria Mkuu ndiye aondoke? Kama una hoja za kuwatetea jaribu kuziweka hapa tuzione acha kurusha hizi insult kwa sababu na wewe ni M-Tanzania kama wengine na pia kodi yako imehusika na kuibiwa hapa, sasa sioni sababu ya kurusha personal attacks mkuu wewe weka hoja zikiwa nzito ziatonekana,

Kampuni ya Dowans ni ya Rostam na sasa ameihamishia kwa Manji, sasa hapa unasema tatizo ni Mwanasheria Mkuu? Eti Lowassa hakuamua uamuzi wake kwa sababu ya kuzuiwa na Mwanasheria Mkuu, lini hiyo? Huyu Mwansheria mkuu kila mahali alipowahi kupita kikazi kuna rushwa tu, tena ni aibu hata kusema kwa wanaomjua vizuri, sasa mbona husemi na mtoto wake Lowassa aliingiaje humu kwenye dela za serikali na yeye sio mfanyakazi wa serikali wala mmiliki wa Dowans au Richimonduli?

I mean kama umeamua kuwatetea watete kwa hoja lakini acha kurusha hizi personal insult kwamba tunaoamini kutokana na ushahidi uliowekwa tayari kuwa hawa ni wezi, na kwamba wewe usiyeamini basi sio M-Tanzania kama sisi, hawa kina Lowassa na Rostam ni wezi, Mwanasheria Mkuu pia ni mwizi tena hatari sana.

ahsante mkuu!
 
Keil,

Ni kwa bahati mbaya watanzania tuna matatizo mengi sana...

Ninyi watanzania muna matatizo gani... kwa nini hafuati kwenye matatizo munasumbuka na watu wengine?

Ndugu unaishi wapi? usiye yaona matatizo ya Tanzania?..kila kukicha ni scandal mpya, ma vijisenti mengi yetu yamebebwa....halafu muungwana tuliyemzoea,ambaye kila kukitokea shida alikuwepo pale(kumbuka alipotembelea masoko ya chakula)...sasa leo kilio chote hiki,Muungwana amekaa kimya badala yake awatuma kina Salva na Pinda.

Je ina maana sasa amekuwa bora zidi kuliko hapo mwanzoni? au haya matatizo yanamgusa?
 
Samahani kwa kutoka nje ya mada...Lakini nitaeleza ni kwanini.

Hiyo hotuba hapo chini...Mtanzania kama atakumbuka niliyasema maneno yote hayo hapo chini kwenye mjadala mmoja juzi kama sikosei pale nilipogusia kuhusu AGOA.

Kuhusu sisi kuuza raw materials na pia kutotumia mpango wa AGOA na EPZ.

Sasa ndugu zangu ni kweli huyu mtu hana washauri!

Haya anayoyasema hapo chini ni mambo ambayo wasaidizi wake wangetakiwa kuyafanya...Lakini badala yake wanamwachia yeye kila kitu? Tena hata kuwaambia wananchi kuhusu opportunities zilizoko?

Sasa kama kweli wangekuwa wanafanya kazi zao vizuri...Mipango hiyo ingeshatekelezwa na si kusubiri rais awakumbushe kila siku majukumu yao!

Hawa watu hadi Ngurdoto kwenye seminar lakini hawakuingiza AKILI!

Sasa na hii mikataba waliyosaini badala ya kuwachungulisha dili wananchi wao wako kwenye maslahi yao na ndio maana ni NOMA!

Kwenye highlights ndipo haswa palipogusiwa PAMOJA NA MENGINE KAMA NILIVYOSEMA KWENYE MJADALA ULE WA VIWANDA KUWA KINACHOTUKWAMISHA NAMBA MOJA NI UMEME.

JK: Wafanyabiashara msiuze bidhaa ghafi, ziongezeeni thamani

2008-07-14 09:31:31
Na Joseph Mwendapole


Rais Jakaya Kikwete, amewataka wafanyabiashara Watanzania, kuziongezea thamani bidhaa wanazozalisha badala ya kuziuza zikiwa ghafi.

Aliyasema hayo jana wakati wa kutoa tuzo ya Rais ya wazalishaji bora wa mwaka 2008, iliyoandaliwa na Shirikisho la Wenye Viwanda Nchini (CTI).

Alisema tabia ya kuuza bidhaa zikiwa ghafi, ndiyo inaifanya Tanzania kuendelea kuwa maskini na wanaonunua bidhaa hizo ghafi kutajirika baada ya kuziongezea thamani.

Rais Kikwete alitoa mfano wa watu wanaouza pamba nje wanawanufaisha zaidi wanaonunua kwani hutengeneza bidhaa na kuzirejesha tena nchini ambapo huuzwa kwa bei kubwa.

``Badala ya kuuza pamba nje kwa nini usiuze nguo, maana kilo moja ya pamba inaweza kutengeneza mashati mawili, tanzanite ghafi yenye thamani ya Sh. milioni 20 wenzetu wanaiongezea thamani na wanapata zaidi ya Sh. milioni 300,`` alisema.

Aliwataka pia wafanyabiashara kutangaza bidhaa zao nje ya nchi kwani kwa kufanya hivyo watapata masoko mengi na aliwashauri wasiogope gharama za kujitangaza.

``Tuache tabia ya kunung`unika bila sababu na tufanye mambo, kujitangaza wengine wanasema ni ghali sasa hakuna cha bure, na mkiendekeza vya bure nawaambia hamtakua, mtabaki hivyo hivyo,`` alisisitiza Rais Kikwete.

Aliwataka pia kufanya mambo yao kwa malengo na kwamba bila kufanya hivyo wanaweza kudhani wamefanikiwa kumbe hakuna walichopata.

Aliwashauri wajitahidi kuongeza mauzo ya bidhaa zao nje ya nchi angalau kwa asilimia kumi kila mwaka na kuongeza kuwa nchi zote zilizoendelea uchumi wake umekua kutokana na kuuza zaidi nje ya nchi.

Alisema hata soko la Afrika Mashariki ni kubwa la wafanyabiashara wanaoingiza bidhaa zao hawatozwi ushuru na kwamba hata vikwzo vilivyokuwepo awali vimeshaondolewa.

``Masoko yapo jamani, Ulaya, Marekani wametupa fursa kupitia mpango wa Agoa tunaingiza bidhaa zaidi ya 5,000 bila ushuru, kinachotakiwa tuongeze thamani bidhaa zetu tuzitangaze na tuache tabia ya kunung`unika nung`unika haitatusaidia chochote,`` alisema.

Aidha, aliongeza kuwa, serikali inatambua kero ya miundombinu ya barabara na umeme na kwamba inajitahidi kuhakikisha inaiboresha ili wenye viwanda wafanye biashara zao katika mazingira mazuri.

Alisema anatambua kuwa umeme ni kilio kikubwa kwa wenye viwanda nchini na serikali itajitahidi kutumia rasilimali zilizopo kuhakikisha umeme unazalishwa kwa bei nafuu.

``Hii Sheria mpya ya umeme italeta ushindani mkubwa katika uzalishaji umeme, wawekezaji watakuwa na uwezo wa kuzalisha, kusambaza na kuuza umeme hivyo ni dhahiri gharama zitashuka,`` alisema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda CTI, Bw. Reginald Mengi, naye alizungumzia umuhimu wa wafanyabiashara Watanzania kuongezea thamani bidhaa zao badala ya kuziuza zikiwa ghafi, ambapo hupata bei ya chini.

Bw. Mengi alisema alitoa mfano kuwa bei ya kilo moja ya kahawa ambayo haijaongezewa thamani ni Dola za Marekani 1.5 , wakati ile iliyoongezewa thamani inaweza kuuzwa hadi Dola 15 za Marekani.

Alimshukuru kipekee Rais Kikwete kutokana na busara na hekina anazotumia kutatua changamoto mbali za kisiasa na kiuchumi ambazo zimekuwa zikitokea hapa nchini na hata nje ya nchi.

``Mheshimiwa Rais sisi wafanyabiashara hatuna wasiwasi na wewe hata kidogo, kutokana na busara ulizonazo tunaamini utaendelea kutuongoza vizuri na utatuvusha,`` alisema Bw. Mengi ambaye pia ni Mwenyekiti Mtendaji wa IPP.

Mkurugenzi Mkuu wa NBC, ambayo ni mmoja wa wafadhili wa tuzo hiyo, Bw. Christo De Vries, aliipongeza CTI kwa maandalizi mazuri ya utoaji wa tuzo hiyo na aliahidi kuwa benki yake itaendelea kushirikisha na shirikisho hilo.

``Kama Mheshimiwa Rais ulivyosema sekta binafsi ndiyo injini ya ukuaji wa uchumi, injini haiwezi kwenda bila mafuta kwa hiyo mafuta ya injini ni NBC nyote mnakaribishwa kufungua akaunti,`` alisema na kuwafanya wageni waalikwa kuangua kicheko.

Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi wa Celtel, ambao nao walifadhili utoaji wa tuzo hiyo, Bw. Chirui Walingo, alisema lengo la kampuni hiyo ni kuyafanya maisha ya watanzania kuwa mazuri kwa kuhakikisha mawasiliano yanakuwa mazuri nchini kote.

Alitoa mfano kuwa mteja wa Celtel anaweza kupiga simu akiwa Kenya, Uganda na nchi zingine 15 za Afrika kwa kiwango kile kile cha fedha anachotozwa akiwa hapa nchini.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha na Utawala ya CTI, Bw. Yogesh Manek, alisema CTI imepokea changamoto zilizotolewa na Rais Kikwete na watazifanyia kazi ili kusaidia jitihada za kuondokana na umaskini.

Alisema watafanya kila linalowezekana kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa hapa nchini zinaongezewa thamani ili wafanyabiashara wapate fedha zaidi.

Mshindi wa jumla alikuwa kampuni ya bia Tanzania TBL.




Makampuni mengine yaliyopatiwa tuzo ya uzalishaji bora ni Allieance Insurance , Alaf Ltd, Simba Plastics Ltd, Shely Pharmaceuticals, 21 Century textiles Ltd, Said Salim Bakhresa and Company, DPI Simba Ltd na Nyanza mine Ltd.
  • SOURCE: Nipashe
 
Kuna mtu mmoja muhimu ambaye angeweza kutusaidia sana kwenye hili jambo na sina hakika sana kama alihojiwa na Kamati ya Mwakyembe. Huyu ni aliyekuwa Balozi wetu Marekani naye si mwingine ila ni Balozi Andrew Daraja. Nakumbuka jinsi nyakati hizo mkurugenzi wa RDC alijitapa sana kwenye tovuti yake alivyoweza kum'host' Balozi wetu ikiwa ni pamoja na kumtembeza, kumtambulisha na kumfanyia tafrija ya mwaka.

Kama sijakosea sana baadaye Mzee wa Kaya alitembelea Marekani na sehemu mojawapo aliyohakikisha amefika ni Houston, Texas.
Haukupita sana muda na RDC wakapewa tenda. Sikumbuki vizuri mtiririko wa mambo na niko kwenye harakati kuzitafuta data lakini sidhani niko mbali na ukweli hata kidogo.

Hata hivyo kwenye tovuti ya RDC mpaka elo wanasema hivi:

RECENT PROJECTS

In 2006, we completed the Ubungo Emergency Supply Power Plant Project in Dar es Salaam, Tanzania. We provided full project development and engineering, procurement and commissioning (EPC) for the first 25MW, and all preparatory work for the second phase, of a 100MW ISO gas-based generation plant.

Sasa, kuliko wakati wowote ule, kuna ulazima mkubwa wa kumbebesha mzigo wa RDC mhusika mkuu na sio mabungusilo.

EVENTS

Richmond Development Company of Houston (RDEVCO) which is developing several projects in the East African nation of Tanzania hosted The Tanzanian Ambassador to USA, The Honorable Andrew M. Daraja to Houston, Texas, from July 20 through to July 22, 2003.

During his visit, Ambassador Daraja was introduced to the leaders of the business community of Houston, which also included alliance partner companies of RDEVCO.


Ambassador Daraja acknowledged that the African region is becoming prominent with regard to the economic and strategic interests of United States as evidenced by President Bush's recent trip to the region.

"With some of our Tanzanian projects approaching financial close, RDEVCO will add new high caliber jobs in Houston" said Dr. Huque, a principal at RDEVCO.

"The fact that Ambassador Daraja came to Houston demonstrates the commitment of The Government of Tanzania to extend business cooperation of Houston based companies" added Mr. Gire, another principal at RDEVCO.

The highlight of The Ambassador's visit to Houston was a Gala Dinner attended by Dr. Lee P. Brown, Mayor of Houston.

The Mayor awarded an honoree citizenship to The Ambassador.


Je,na mkono wa Mkapa upo hapa


In fact Daraja alipokuja pale Houston hakutaka kuonana na watanzania wengine. Aliishia kwa huyu Bwana Gire tu, wakati ziara ile ilikuwa ni ya Balozi kukutana na watanzania waishio Houston. Kitendo cha Daraja kujificha kwa Gire wakati wa ziara ile kweli kinatia wasiwasi sana
 
Back
Top Bottom