Yakki Kadaf
Member
- Jan 8, 2023
- 29
- 107
Wasaalam wanajamvi naendelea na namna maskari Eli eli, afande zawadi na mgambo ajulikanae kwa jina Samwel wanavyoharibu sifa nzuri ya jeshi la polisi wilayani Bunda.
Huyu mgambo ambaye vijana wa mjini wanamuita "Mundu" wa afande li eli kapewa mamlaka ya kutembea na pingu ambazo amekuwa akizitumia kwa maslahi yake pamoja na wanufaikaji wengine eli eli na zawadi kama ifuatavyo:
Wilayani Bunda hasa halmashauri ya mji wa Bunda kuna kundi maarufu la vijana ambao hurusha mabunda ya pesa feki "mrimba" ambapo mtu wa kuja anapoliokota lile bunda vijana wapatao wawili au zaidi wanakuwa eneo la karibu humfuata aliyeliokota na kujifanya wote wameliona ambapo hujifanya kumshawishi kwenda pembeni ili wagawane ambapo mhusika huishia kutapeliwa.
Sasa Mgambo Samweli anahusikaje hapa? Jibu ni kwamba mgambo huyu ana orodha yote ya vijana hawa na maeneo ambayo huenda kufanya uhalifu ikiwemo kuuza dhahabu feki nk. Mgambo huyu ana ratiba za hawa vijana zote za wiki nzimana alishawapa utaratibu hawa vijana ambapo kila kijana anayefanikisha dili lake humpatia ten percente(10%)ambapo mhusika huipeleka kwa eli eli ambaye huigawanyisha.
Njia nyingine anayoitumia huyu mgambo ni pale anapomuona mtu au kusikia ana kitu cha thamani mfano Godoro, Tv, radio, woofer nk atamfuata na kumuomba amuonyeshe risti(kiuhalisia ni ngumu kutunza risti kwa kila mali unayoimiliki) inapotokea mhusika akadai hana risti huwekwa chini ya ulinzi na endapo akieleweka kutoa hongo ataachiwa huru na mali itataifishwa. Nguvu ya kuidai hatakuwa nayo maana hana risti. Akikosa risti na wakati huo huo hataki kutoa hongo atapelekwa "lock up" ambapo akiwa huko kuna uwezekano mkubwa wa kubambikiwa kesi za uvunjaji na uporaji!
Yapo mambo mengi sana ya kuudhi yanayofanywa na hawa wahusika ila naliomba jeshi la polisi kupitia RPC Mara, OCD Bunda kufuatilia hizi tuhuma maana wanatumia mamlaka yao vibaya sana! Jeshi linachafuliwa na watu wachache wasio na maadili ya kazi!
Huyu mgambo ambaye vijana wa mjini wanamuita "Mundu" wa afande li eli kapewa mamlaka ya kutembea na pingu ambazo amekuwa akizitumia kwa maslahi yake pamoja na wanufaikaji wengine eli eli na zawadi kama ifuatavyo:
Wilayani Bunda hasa halmashauri ya mji wa Bunda kuna kundi maarufu la vijana ambao hurusha mabunda ya pesa feki "mrimba" ambapo mtu wa kuja anapoliokota lile bunda vijana wapatao wawili au zaidi wanakuwa eneo la karibu humfuata aliyeliokota na kujifanya wote wameliona ambapo hujifanya kumshawishi kwenda pembeni ili wagawane ambapo mhusika huishia kutapeliwa.
Sasa Mgambo Samweli anahusikaje hapa? Jibu ni kwamba mgambo huyu ana orodha yote ya vijana hawa na maeneo ambayo huenda kufanya uhalifu ikiwemo kuuza dhahabu feki nk. Mgambo huyu ana ratiba za hawa vijana zote za wiki nzimana alishawapa utaratibu hawa vijana ambapo kila kijana anayefanikisha dili lake humpatia ten percente(10%)ambapo mhusika huipeleka kwa eli eli ambaye huigawanyisha.
Njia nyingine anayoitumia huyu mgambo ni pale anapomuona mtu au kusikia ana kitu cha thamani mfano Godoro, Tv, radio, woofer nk atamfuata na kumuomba amuonyeshe risti(kiuhalisia ni ngumu kutunza risti kwa kila mali unayoimiliki) inapotokea mhusika akadai hana risti huwekwa chini ya ulinzi na endapo akieleweka kutoa hongo ataachiwa huru na mali itataifishwa. Nguvu ya kuidai hatakuwa nayo maana hana risti. Akikosa risti na wakati huo huo hataki kutoa hongo atapelekwa "lock up" ambapo akiwa huko kuna uwezekano mkubwa wa kubambikiwa kesi za uvunjaji na uporaji!
Yapo mambo mengi sana ya kuudhi yanayofanywa na hawa wahusika ila naliomba jeshi la polisi kupitia RPC Mara, OCD Bunda kufuatilia hizi tuhuma maana wanatumia mamlaka yao vibaya sana! Jeshi linachafuliwa na watu wachache wasio na maadili ya kazi!