RPC Ruvuma: Mwanamke Aliyekutwa Ofisi za TANESCO Hana Uhusiano na Uchawi, Ana Tatizo la Akili

RPC Ruvuma: Mwanamke Aliyekutwa Ofisi za TANESCO Hana Uhusiano na Uchawi, Ana Tatizo la Akili

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Hali ya gumzo imetanda kwa baadhi ya Wananchi wa Manispaa ya Songea mjini Mkoani Ruvuma baada ya Mwanamke mmoja katika Ofisi za Shirika la Umeme TANESCO Mkoani humo akiwa hana nguo huku baadhi ya Mashuhuda wakisema alianguka na ungo wa kichawi wakati akipita juu ya Ofisi hizo.

Soma Pia: Apata 'ajali' angani akiwa kwenye ungo aangukia TANESCO

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Ruvuma Marco G Chilya ambaye ndiye alikuwa wa kwanza kupigiwa simu na Meneja wa TANESCO baada ya Mwanamke huyo kukutwa kwenye Ofisi hizo ambapo hata hivyo RPC Chilya amekanusha taarifa za ungo na kusema Mwanamke huyo sio Mchawi bali ana tatizo la akili.

 
Back
Top Bottom