RPC Wankyo Nyigesa ni kielelezo cha kuzorota kwa kiwango cha utumishi na nidhamu ndani ya Jeshi la Polisi

Madudu ya kiutendaji, uhuni na ujambazi sasa yanafnywa na MAAFISA WA POLISI!!!!
Hatuna jeshi la polisi.
 
Labda mtoa mada nikukumbushe tu, kwamba vyombo vya dola vya Tanzania havijawahi kuwa na maadili tangu nchi hii imepata uhuru.

Vinakosa maadili kwasababu havikutengenezwa kuwasaidia raia bali kukitumikia kikundi fulani cha viongozi wa nchi, kuanzia ngazi ya chama hadi taifa.

Mnaweza kukataa ukweli, lakini Polisi, JWTZ na USALAMA ni vyombo vya chama tawala. Maslahi ya chama kwanza, halafu nchi baadae. Kusema kwamba wameanza kukosa weredi siku hizi nakataa.

Huko nyuma kipindi cha awamu ya kwanza na ya pili, kuna matukio yaliwahi kufanywa na vyombo vya dola ukisikia unaweza sikitika. Mbaya zaidi kulikuwa hakuna uhuru wa kusema, kama siku hizi.

Hivi umewahi kujiuliza kwanini watanzania ni waoga kupitiliza : State Terrorism has conditioned rational Tanzanians into subservient mindless drones.

In this Fiasco, the malevolent IGP is just a symptom not a disease. We all know that, a major cancer to this country lies deep within the heart of CCM and its perpetual failing governments.

Ukweli ambao mnakimbia kuusema ni kwamba, bila watu waovu kama Sirro, Makonda, Sabaya, Mahita, Kingai, Kipilimba n.k kufanya hayo wanayoyafanya CCM haiwezi kubaki madarakani.
 
Nakubaliana na wewe kwa kiasi kidogo tu.
Inabidi vile vile tuelewane kuwa vyombo vya Dola mara zote ni mali ya Dola.

Na hali hii ni kwa nchi yoyote duniani, iwe Magharibi au Mashariki.
Vyombo vikuu vya Dola ni The executive(serikali), Judiciary(Mahakama na Sheria) na Legislative(Bunge).
Kwa muundo uliopo sasa, Serikali imevipiku kimadaraka hivi vyombo viwili yaani Mahakama na Bunge.
Hivyo basi Serikali inakuwa na a Free Ride kufanya kile inachokitaka iwe mchana iwe usiku.
Checks and balances ni hafifu.

Kuna mifano halisi ya nguvu ya serikali juu ya vyombo vingine.
Watendaji waandamizi wote huteuliwa na mhimili wa Serikali na Rais.
Watendaji nawakuu wote wa mhimili wa Mahakama wanateuliwa na Rais. Kimtazamo Mahakama haiko huru 100%.
Spika wa Bunge anaweza kuondolewa na Rais kupitia chama chake, hivyo nalo Bunge haliko huru 100%.

Sasa hapo ndio tunapata hiyo laiszez faire ya vyombo ndani ya serikli, vyombo ambavyo havipitii checks za aina yoyote.
Zile kamati za Bunge zinazo oversee vyombo vya Ulinzi na Usalama havina impact ya aina yoyote katika kusimamia vyombo hivi.
Tumeona Mahakama zilivyotekwa na serikali, wakati mwingine hata kuagizwa kutoa maamuzi ya kesi.

Na niwe muwazi, checks and balances si za kukomoana kisiasa , bali zinatakiwa ziwe kuona Sheria na Haki zinatendeka kama ilivyo katika Katiba,
Hili halifanyiki.

Kw hali ilivyo sasa ndio tunaona , kwa maoni yangu, vyombo vya Dola vinatumika kisiasa, na vimezoea kutumika hivyo utafikiri ndiyo kazi waliyotumwa kuifanya na Taifa.
 

Kama dola ilivyo mali ya wananchi kwa ujumla wake, hata vyombo vyake ni mali ya wananchi. Kuvitumia vyombo hivi kwa manufaa ya kikundi fulani ni jambo lisilo na afya kwa taifa.

Dola inabidi iwajibike kwa raia, iwalinde raia na mali zao, pamoja na maslahi mengine ya taifa husika. Ulilolisema hapo juu kwamba dola ni mali ya watawala wenzetu Ulaya walishaachana nalo karne za 18 na 19 huko.

Tukishaanza kufikiri kwamba dola ni mali ya waendesha dola, basi safari yetu itakuwa ni ndefu sana.
 
Nilianzia mbali kueleza hali halisi ilivyo kwa maana ya kueleza in Theory kuwa Dola ni mali ya wananchi, lakini in pratice Dola ni mali ya serikali.
Serikali ina toa funds za kuendesha vyombo vyote, na havijiendeshi automatically.

Hata kwa wenzetu Dola bado inaendeshwa na serikali, kwa mlengo wa cham kichoshinda uchaguzi.
Hilo liko wazi.
Trump alipoingia madarakani aliwaondoa wale wote waliowekwa kuongoza FBI, CIA, na hata Federal organs zote kuwa watu watakao endana na siasa zake.
Biden alipoingia mafdarakani aliwaondoa viongozi wote waliowekwa na Trump na kuweka wa kwake.
Lakini tukubaliane kwamba wenzetu wana weledi wa kufuata sheria zilizowekwa , hata kama si zote.
 
Pengine Sirro bado haelewi kuwa Taasisi yake iko compromised.
Na haelewi kuwa tatizo si lake bali Taasisi yenyewe ilivyotumika kisiasa na kudharau PGO.

IGP anaongoza mafisa wanaopika na kubambika kesi nyingi.
IGP anaongoza maafisa wanaoua wananchi kwa kuwaibia madini
IGP anaongoza maafsa wasiojua wajibu wao utendaji kwa kutumia sheria zinazoongoza polisi, PGO

Kuna mengine mengi tu, sasa ambayo si dhahiri kama rushwa.
Sasa Taasisi hii ya Polisi imeshindwa kujichukulia sheria na kujisafisha, lazima mtu au chombo nje ya Polisi kifanye kazi hiyo.
 

Bila wanasiasa kubadilika, juhudi zozote za kufanya reform ya TPF zitakuwa ndoto isiyotimia. Uharibifu uliofanywa (na unaoendelea kufanywa) na wanasiasa kwenye hii taasisi ni mkubwa sana!
 
Hiyo no 4 ikisomwa na watu makini kama ilivyo,inafubaza hoja zako zote za msingi katika bandiko hili.

Kifupi utawapa polisi kiburi na ujasiri wa kukujibu kwamba huna unalolijua.
 
Nilianzia mbali kueleza hali halisi ilivyo kwa maana ya kueleza in Theory kuwa Dola ni mali ya wananchi, lakini in pratice Dola ni mali ya serikali.
Serikali ina toa funds za kuendesha vyombo vyote, na havijiendeshi automatically.
Nakukumbusha tena, kufanya teuzi na kuweka watu unaowataka hilo liko kisheria na halimaanishi kwamba vyombo vya dola ni mali ya serikali. Hivyo mfano wako hauko sawa hapa. Unachoshindwa kukielewa hapa ni kwamba vyombo vya dola nchini Marekani na Magharibi vinawajibika kwa bunge na siyo kikundi cha watu au mtu. Huyo Donald Trump unayemtaja hapa mwenyewe ameajibishwa mara kibao tu na bunge, mwishowe wakampiga chini. Hii siyo nadharia (Theory) ambayo nimeitoa hewani tu. Nchi za wenzetu wametuacha mbali kwasababu raia zake wanajielewa, siyo kama hapa Tanzania.

Pili, kuhusu kuviwajibisha vyombo vya dola nadhani wewe umejisahaulisha au umeamua kupuuza. Idara ya Usalama wa Taifa imewahi kufumuliwa, maafisa wengi waandamizi kustaafishwa na kusukwa upya siyo chini ya mara mbili, lakini hujiulizi kwanini matatizo hayaishi tu. Bado wana kashfa zilezile za uonevu dhidi ya raia, rushwa, utesaji, utekaji, uuaji na kuchanganya siasa na utaalamu. Jeshi la polisi nalo lishawahi kufumuliwa miaka ya huko nyuma, lakini kwanini unadhani matatizo hayaishi tu.

Narudia tena, tatizo siyo polisi peke yao, tatizo wote tunalifahamu lakini tumeamua kufumbia kwasababu za maslahi.
 
Kwa mfumo wa sasa kikatiba, haiwezekani jeshi hili kubadilika. Katiba mpya ndilo suluhisho.
 
Jeshi la polisi huwezi kuelewa nini kinaendelea mpaka ukutane na jambo linalowahusu. Kuna mitihani mizito sana kule.
Haya ya huyu kamanda ni dalili mojawapo tu.
Ukiona moshi unafuka, jua kuna moto
 
Hiyo no 4 ikisomwa na watu makini kama ilivyo,inafubaza hoja zako zote za msingi katika bandiko hili.

Kifupi utawapa polisi kiburi na ujasiri wa kukujibu kwamba huna unalolijua.
Tatizo kubwa katika hoja no 4 ni kile kisemwacho mitaani kutokana na tukio lenyewe.
Mtu unaweza kusema hakuna ninalojua ambapo ni kweli, lakini masikio hayana pazia na dalili za moto ni moshi.

Suala la Hamza hakuna independent investigation.
Kwa wasioiamini polisi wanasema uchunguzi wao una matokeo ya kupikwa.
Gaidi yeyote ana handlers wake na affiliation na vikundi wanavyoshirikiana.
Polisi hawajawahi kulieleza hili hadharani, kwamba Hamza alishirikiana na nani.
Polisi wamekaa na kuwahoji familia yake na nahisi hakuna cha maana wamekipata.

Hali hii inaipa uzito hoja ya Hamza kulipiza kisasi kwa wale vijana waliompora madini yake kama inavyoelezwa mitaani.

Unless unaoushahidi ulio wazi mkuu uweke hadharani.
 
Wakenya walishaliona kama hili letu na hatimae kati ya mambo walioyaona Wakenya kuondoa kuitwa Jeshi la police na sasa ni Police service.
Mbona magereza inaitwa "Tanzania Prison service " na bado hali sio ya kuridhisha?
 
Wakenya walishaliona kama hili letu na hatimae kati ya mambo walioyaona Wakenya kuondoa kuitwa Jeshi la police na sasa ni Police service.
maaana ya service bado ni jeshi .
JKT- National service
jeshi la maji-Naval service
Special Air Service- kikosi maalum cha jeshi la anga UK

nakushauri usitafsiri neno service kama huduma
 
Jeshi la polisi huwezi kuelewa nini kinaendelea mpaka ukutane na jambo linalowahusu. Kuna mitihani mizito sana kule.
Haya ya huyu kamanda ni dalili mojawapo tu.
Ukiona moshi unafuka, jua kuna moto
Jeshi limeoza kwa rushwa.
Jamaa aliyekamatwa majuzi akiwakaanga kwa mafuta yao wenyewe.
Kawatoa upepo ma RPC, OCD na wengine wengi wanaotoa rushwa ili wapande vyeo na upendeleo mwingine.

Polisi imeoza.
 
Ni ngumu chama fulani na vyombo fulani vya dola kujinasua katika mahusiano ya mahaba ni mpaka pale ubwabwa upikwe na Wana wa nchi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…