Ave Ave Maria
JF-Expert Member
- Apr 22, 2011
- 10,707
- 5,678
tafazali Kipipi,nyumba nijenge mimi kulala nilale kwa jirani? Arrrrrrrrooooo tena usirudie kusema maneno hayo!
Nyumba ni yako umeacha wafanyakazi wako humo ndani? Au umekodi mtu wa kukulindia chumba? Nani anapenda kujiwa usiku wa manane kila siku, mfanyakazi wa kufua suruali, kutandika kitanda na kufungua mlango?? Unamlipa sh. ngapi? Kama we jeuri badilisha kitasa uwe na funguo yako......upoo!!
IMO nafikiri ni hasira mara nyingi... na mwanaume akikuta kua Mkewe anamuambia hivo ajue kabisa hamtendei haki for yaonesha wazi huyo mwanamke bado anampenda... For angekua hampendi angefungua mlango kimya kimya bila hata lawama... na lawama yaweza kua more of kumsumbua kumtoa kitandani kuliko sababu ya kuchelewa... hapa mume asishangae mkewe akichongesha funguo na kumkabidhi ili walau asisumbuliwe usiku....
Kuhusu why wanaume wanachelewa siku zoote kurudi... hapa sababu ni lukuki kwa kweli tokana na kwamba matatizo ya ndoa hu-vary from one to another... sababu ya kuchelewa yaweza kua sababu ya Mke ama Mme ama Wooote.
kwani hata kuna haja ya ugomvi basi?!we unakataa kufungua mi nageuza kimya kimya kurudi 'nilikokuwa'!siku nyingine nikichelewa kurudi nakupigia simu nikiwa 'huko huko' ili kama 'unajisikia' kufungua siku hiyo ndo nianze safari ya kurudi home.hii haijalishi kama nyumba ni 'yako','yangu' au 'yetu'!
Pole sana kama yalikukuta mzee, we nakuamini najua ulibanwa na
kazi ukachelewa kurudi. Bora tu usinzie hapohapo mlangoni kuliko
kwenda hukohuko.
kwani hata kuna haja ya ugomvi basi?!we unakataa kufungua mi nageuza kimya kimya kurudi 'nilikokuwa'!siku nyingine nikichelewa kurudi nakupigia simu nikiwa 'huko huko' ili kama 'unajisikia' kufungua siku hiyo ndo nianze safari ya kurudi home.hii haijalishi kama nyumba ni 'yako','yangu' au 'yetu'!
Safi sana kijana manake hapo utakuwa umenidhihirishia kuwa ulisogeza mtu wa kukufanyia kazi na haukuoa mke!! Kwa sababu kama ungekuwa umeoa basi ungeithamini ndoa na kuuona umuhimu kupunguza/kuondoa tatizo kuliko kuliongeza mara 10 tena kwa makusudi!! Na hayo unayoyasema ndugu, utayafanya kama huna shida ya ndoa!
hahahaaaah! katika wanaume huyo ndio mwenyewe!!!Mwanakijiji,ngoja nikupe kisa cha ukweli.Jamaa yangu kuna siku alirudi usiku sana,mkewe akaleta hizo 'kalale huko huko'akagoma kufungua mlango.Jamaa alikuwa na landrover,all he did alichukua mnyororo akafunga kwenye mlango wa mbele akatia gia,vruuuuuuuu akaung'oa,mama akashtuka kishindo kutoka chumbani mlango wa mbele aliukuta barazani.Kilichofuata ni kibondo.Kesho yake namuuliza jamaa kulikoni,akasema 'nyumba yangu unifungie nje?'
shida ninakuwa nayo na nakuwa nakupenda kiukweli kabsa kipipi,ila mara nyingine nyie visirani vyenu tukiviendekeza maisha yatasimama kabisa aisee!sasa kama huyo jamaa alieamua kuruka ukuta baadae akavunjika na kupelekea kifo ni upuuzi wa mke tu!fungua mlango tuzungumze mama,wewe kunifungulia mlango sio kwamba ndo mfanyakazi wangu bana,ndo hata maji ya kuoga hamweki siku hizi eti 'kuna shower'!,sasa kwenye shower mdalasini unawekaje!?hebu kuweni wanawake bwana na mtumie nguvu kubwa ya 'uanamke'(bado kidogo nikosee hapa,wallah.ningekula ban refu!)wenu kulinda na kutulea sisi wanafamilia jamani!!