Uchaguzi 2020 Rufaa 557 za Tume ya Uchaguzi, tunataka Matokeo

Uchaguzi 2020 Rufaa 557 za Tume ya Uchaguzi, tunataka Matokeo

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imekiri kupoke rufaa za wagombea nafasi ya ubunge na udiwani zipatazo 557. Tume iliahidi kuanza kuzifanyia kazi kuanzia tarehe moja mwezi wa tisa na kutoa majibu japo hatujasikia jibu kwa mkata rufaa hata mmoja.

Kwakuwa kampeni zimeanza kushika kasi tungependa kupata majibu ili wagombea waweze kujipanga Kama wameshinda rufaa zao. Ikiwezwkana tume itoe matokeo ya Kila rufaa iliyotolewa uamuzi bila kusubiri zoote 557 zikamilike.

Kuchelewesha rufaa kutahesabika Kama mbinu za kupima hali ya ushindani ili kujua rufaa ipi ikubaliwe na ipii ikataliwe. Hapa NEC itakuwa sehemu ya siasa. Chondechonde vyama visijisahau virudi kutazama namna ya kushinikiza mapitio ya hizo rufaa.

Sidhani Kama rufaa zote zinahitaji muda mrefu kujadiliwa ukizingatia sababu zilizotolewa na wasimamizi kuwaengua wagombea.

NEC isije kujifungia ofisini ikipanga Nani awe mbunge na nani asiwe. Nafasi 557 nyingi sana . Ukiengua hata nusu tu itakuwa umehujumu uchaguzi kwa kiwango kikubwa.

Sisi wananchi tungependa majina yarudi na kuturudishia haki yetu ya kuchagua badala ya NEC kutuchagulia kwa kivuli Cha ameandika herufi kubwa badala ya ndogo , hakuweka picha nk


Nadhani ni wakati muafaka matokeo hayo kuambatana na majina. Tutajuaje ni kweli au figisu tu!
 
huyo aliyeandika DSM alipotakiwa aandike jina kamili alishindwa, sasa unataka tume ipitishe mambumbu wakagombee watupe shida wananchi kumsomea barua zake.
Katika hili mbumbumbu ni wewe. Sifa mojawapo ya kugombea ubunge ni kujua kusoma na kuandika. Sifa hiyo ipo wakati Kayumba zinazalisha kidato cha nne wasiojua kusoma na kuandika! Mwenye sifa ya kusoma na kuandika ataandika Dar es Salaam akikutana na Dar au DSM hajui. Wa chuo kikuu mpaka anamaliza shahada ya uzamivu mara zote huandika UDSM. Darasa la saba ( Msukuma) labda apige ramli kwanza ndio atajua hili ni nini! Wengine hatuna shida na hilo. Hata we don't give it a second thought. Ni dhahiri shayiri kulingana na muktadha. Hapa mbumbumbu ni wewe na NEC! Hawa NEC wanasema Lissu kakosea kwa kuandika CDM sehemu ya chama kinachomdhani. Kwa Msajili wa Vyama hakuna chama kama hicho. Lakini wanatoa taarifa kuwa mgombea wa CCM kateuliwa na wagombea wa CDM na ACT-W hawakuteuliwa! Tanzania nchi ya vi-wonder.
 
Back
Top Bottom