Ok!
Kwanza nikwambie tu kuwa mimi ndio Gang ''Matherf*cken'' Chomba.
Utakavyokuja ndivyo utakavyonikuta.
Sasa umekuja kwa busara nami ntakujibu kwa busara.
1. UmeSema suala la kuchukuliana wanamuziki ni la kawaida, lakini kwa nini JUDITH kawahusisha Clouds?
Jibu ni kuwa Judith kawahusisha Clouds kwa kuwa tu Clouds wanaipaisha vilivyo Sky Light na pia mmiliki wa Sky Light yaani Sebastian Maganga ni mshkaji wa Ruge pia kama sikosei ni mfanyakazi pia wa Clouds...sawa? Mpaka hapo tayari, kuna conflict of interest kati ya Jide na Ruge. Kumbe anambana Jide ili kuipaisha bendi ya rafiki yake, lengo ni kumfuta Jide kwenye ramani ya muziki.
2. umezungumzia pia ishu ya Nyimbo za Jide kutopigwa redio Clouds.
Jibu ni kuwa Jide alipigiwa simu na Ruge ili wazungumzie tofauti zilizoanza kujitokeza kati yao...but Jide akamtukana jamaa. So hii ni adhabu kwake, na pia ameeleza kuwa kuna baadhi ya wasanii nyimbo zao hazipigwi kwenye vituo vya redio, akawataja miongoni mwao ni Diamond na Ray C...umenielewa? Ruge ataongea chochote ili aonekane mwema, hata maelezo ya Ruge yanaonesha kuwa hapendi maendeleo ya Jide.
3. kisha umehoji ishu ya wasanii wa THT haswa Lina na Barnaba kutoshiriki katika tamasha la Jide.
Jibu ni kuwa Jide alikuja huku anapiga salakasi ile hali kavaa taulo na kusema kuwa ati Lina na Barnaba wamebaniwa wasishiriki katika tamasha lake. Lakini Lina na Barnaba walijitokeza na kukanusha kisha wakasema wameshindwa kuafikiana ktk malipo. Lina na Barnaba wameongelea suala la ruhusa kutoka kwa waajiri wao, issue ya malipo inawekwa ili kufuta hoja ya ruhusa. Unafikiri Ruge angeweza kuwaruhusu kushiriki hiyo event ya Jide?
Jide anatafuta huruma za watu kama wewe ili aonekane bado wamo.
Ajipange upya, au laa anyoe nywele arudi kuimba kwaya Sabato.