Rukwa kinara wa kutapeliwa kwa njia ya simu

Rukwa kinara wa kutapeliwa kwa njia ya simu

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, (TCRA), imetoa takwimu za maeneo vinara ya utapeli kwa njia ya simu ikionesha kuwa mkoa wa Rukwa ni kinara kwa wananchi wake kutapeliwa

Katika kipindi cha robo ya mwisho ya mwaka uliopita 2022, kuanzia mwezi Oktoba 2022 hadi mwisho mwa mwezi Disemba matukio ya utapeli 12,613 yalirekodiwa huku takribani nusu ya matukio hayo yakiwa yametoka katika mkoa wa Rukwa.

Ripoti toka TCRA inaonesha kuwa asilimia 46 ya matukio hayo yametokea mkoani Rukwa ikifuatiwa na Morogoro (25%) kisha Dar es Salaam (13%)

Swali la kujiuliza hapa ni, je? wananchi wa Rukwa WANATAPELIWA KIRAHISI SANA, SIO WAJANJA au kuna siri gani nyuma ya hali hii?

simcard-pic.jpeg

 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, (TCRA), imetoa takwimu za maeneo vinara ya utapeli kwa njia ya simu ikionesha kuwa mkoa wa Rukwa ni kinara kwa wananchi wake kutapeliwa

Katika kipindi cha robo ya mwisho ya mwaka uliopita 2022, kuanzia mwezi Oktoba 2022 hadi mwisho mwa mwezi Disemba matukio ya utapeli 12,613 yalirekodiwa huku takribani nusu ya matukio hayo yakiwa yametoka katika mkoa wa Rukwa.
TCRA ya hovyo kabisa, takwimu zinatusaidia nini, majuzi wameleta habari kuwa facebook ni mtandao pendwa leo wanasema Rukwa wanatapeliwa nilitegemea wangetuambia mifumo yao imesaidia kuwashughulikia wahalifu wangapi, na itadhibiti wahalifu wangapi badala ya hadithi
 
Katika kipindi cha robo ya mwisho ya mwaka uliopita 2022, kuanzia mwezi Oktoba 2022 hadi mwisho mwa mwezi Disemba matukio ya utapeli 12,613 yalirekodiwa huku takribani nusu ya matukio hayo yakiwa yametoka katika mkoa wa Rukwa.

Ripoti toka TCRA inaonesha kuwa asilimia 46 ya matukio hayo yametokea mkoani Rukwa ikifuatiwa na Morogoro (25%) kisha Dar es Salaam (13%)
Kwahiyo investment yote ya lile jengo kazi yake kutuletea takwimu hizi!!
 
😁😁 watu wa huko wataanza kutokwa na povu kiufupi rukwa wanyasa tu acha walizwe
 
mmmh huku si ndio Sumbawanga tunakoaminishwa Ni wazee wa kazi?

Sisi kama Taifa ndio kitovu huko na ndio tunawategemea linapokuja swala la kupuliza sasa inakuwaje tena!

I am very disappointed
 
Ngoja tusubir uhakiki wa laini za simu uishe......😋😋😋
 
Itakuwa kuna wasukuma wengi sana huko.
 
Wapumbavu sana hao tcra,wanalea matapeli Kwa kushirikiana na Polisi,hao watu wanajulikana na hakuna anaewagusa
 
Back
Top Bottom