Rungu la TCRA lawashukia Wasafi Tv, Clouds FM, Carry Mastory, Radio one na RFA kwa kurusha maudhui yaliyo kinyume na Sheria

Hatuwezi kupata shida kukuza vijana walioshindikana kwa kuiga yanayorushwa kwenye media, wanatupa kazi kubwa kuwafunza na kuwaelimisha watoto wetu, safi tcra endeleeni kubana mpaka kieleweke
 
Awamu hii Media House mtaanza kufugia kuku ofisi zenu maana mnavyochakazwa ni Mungu ndio anajua.
 
Hapo kwa Clouds na Wasafi ni katika kujaribu kupumbaza watu kuhusu ishu ya kuifungia RFA, ni uhuni tuu na kujikomba Ila mwisho wao umefika..
#October
 
Naona hapo wasafi media online tv imefungiwa, Zuchu,sallam,mondi,babutale mnaendeleaje huko?
Zuchu aliwaimbia nyimbo na kutamka maneno 'wapinzani watetereke Sana'
 
daah ntaimiss sana jahazi ya efrahim kibonde ..!!a.k.a kbs daah ngojaaa niindelee kisikiliza ndinga mpya town na kina dj macky .
 
Mimi nilichokuwa siwafiki ni muda wa vipindi kama hivi iwe kuanzia saa 4 za usiku mpaka saa 11 alfajiri. Lakini neno hata likiwa tusi linawakati wake wa kutamkwa na ndio likaweza kuexist hilo neno.

Neno kama kutiana (sexual intercourse), mkundi (anus) yanasomeshwa mchana kweupe kwa watoto wetu wa Form1 aged just 15-16 na yamo kwenye vitabu vya Biology vinavopatikana libraries na madukani for anyone of any age to read. We have to be realistic venginevyo tunakoelekea smart phones zitabigwa marufuku nakuapia.
 
Nasikiliza hapa Gadina yupo lakini nasikia maudhui kidogo yanatofautiana na Jahazi ya kitambo.​
Sijasikia hata tangazo la Jahazi.​
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…