RUNGU: TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha matangazo kwa Miezi Sita (6) kuanzia leo kwa kurusha Maudhui ya utupu

Wakiumia ndiyo watakuwa makini kurusha maudhui yanayokubalika sawa na miongozo ya TCRA na utamaduni wa kitanzania. Huwezi kuacha kuadhibu kisa kuna watu wataumia, maana hata wafungwa wapo waliokuwa wanategemewa na familia zao ila kwa kuwa walitenda makosa hakuna namna
 
Gigy money kaharibu biashara ya watu huko[emoji3]

Mbona wasafi adhabu mara kwa mara kunani huko!

Anyway M5tena.
 
Huyo Dada hata hakukaa uchi
Bali kavaa jumpsuit ya gold nae tangu ya ngozi ni brown ndio mkawa mistaken yupo uchi sema tu inaonesha ndani hakuvaa chupi wala bra.

Hajakaa uchi na ndio hizi fashion zilivyo kwa mbali unaweza dhania yupo uchi.
 
Unaifungia wasafi miezi 6

1. Unakosa mapato kutokana na matangazo yanayotakiwa kurushwa ndani ya miezi 6 ya adhabu

2. Unakosa mapato kutokana na waajiriwa wa Wasafi kupoteza kipato( marupurupu n.k)

3. Unapunguza Wigo wa Ajira

4. Unawatisha na kuwakatisha tamaa wawekezaji waliotaka kuwekeza na waliowekeza kwenye media


Gharama yote hii unaingia kisa nguo za Giggy Money!!

Waafrika tujipime akili zetu
 
Wataenda popote, kwahiyo wasionywe kisa watakuwa hawana ajira? Hakna hiyo.
Sheria ni msumeno, hukata huku na huku. Safi kwa TCRA kufanya kazi yao kwa weledi
[emoji1666][emoji1666]
 
Hii ni sheria ya kijinga sana, eti Mtu atumie silaha kufanyia uhalifu mtu huyo ahukumiwe adhabu pamoja na silaha yake aliyoitumia!!!??.

Kituo cha TV kina kosa lipi hadi kifungiwe??
Hata mm sijaelewa hapa. Kwnn lkn
 
Kumbuka hawakujua Kama n kosa[emoji849]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…