Rupia: Hazina ya Mjerumani

Inasemekana avalon kituo Cha mwendokasi wamekula mzigo pipa mbili za red mercury thus walijifanya kufadhili mradi wa barabara ya mwendokasi kupitia kampuni ya ujerumani ya strabags lengo lilikuwa ni zuga jinsi gani watachukua site ya avalon.
Hizi kampuni zao za ujenzi zinajua site zote so ujifanya wanafadhili miradi ya barabara kumbe ni jinsi ya kulamba mizigo.
Wachina nao wakajenga reli ya tazara kwa kufuatisha ramani za site za wajerumani walizofichia Mali wakakomba Mali wakatuachia reli baada ya kuipata ramani ya Mali USA, then USA nao walipoona mchina kala Mali wakaja na mradi wa bomba la mafuta la tazama nao wakapitia humo humo mwambao wa reli ya tazara wakalamba Mali.
Aliyesema nchi hii ni tajiri shida yake anakula pekee yake hauweki huo utajiri kwa wananchi wafaidike nao
 
 
Rungwe mission iliasisiwa na kina nani.Nani Aliyeleta Moravian Mbeya
Nilisema kuhusu madai kuna hazina sokoni Mbeya mjini. Hapakuwa mji wa Mbeya wakati wa Wajerumani. Rungwe iko Tukuyu, iliyokuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni.
 
Nilisema kuhusu madai kuna hazina sokoni Mbeya mjini. Hapakuwa mji wa Mbeya wakati wa Wajerumani. Rungwe iko Tukuyu, iliyokuwa makao makuu ya serikali ya kikoloni.
Hazina nyingi hazikuifadhiwa maeneo walikokuwa wanaishi mzee hawakuwa wajinga kiasi hicho mawehifadhi sehemu mbali mbali
 
Kama kuna mtu mpaka leo ana fikra hizi anasikitisha
 
Graduate unawaza mafreemason
 
Kuna elimu kubwa sana kulizidi hako kaelimu kako unakokaita "GRADUATE" ambayo wewe huijui
Wapi nimekutajia elimu yangu?

Hata ungekuwa profesa bado inaonekana unawaza kishamba/kijinga

Msomi unafikiria eti mafreemason, sijui pesa zilichinjiwa damu[emoji28][emoji28][emoji28]
 
Wapi nimekutajia elimu yangu?

Hata ungekuwa profesa bado inaonekana unawaza kishamba/kijinga

Msomi unafikiria eti mafreemason, sijui pesa zilichinjiwa damu[emoji28][emoji28][emoji28]
Mambo hayo yapo na yanafanya kazi na sio lazima wewe uamini hilo
 

Nikimuona mtu anaamini haya mambo huwa namuona kama anakasoro fulani kwenye ubongo wake
Yaani ukianza kuambiwa sababu za hao wajerumani kuamua kufucha hizo mali unabaki kujiuliza inakuaje mtu mzima na akili zako timamu unaamini huo UTOPOLO?

Baba mkwe wangu tena maomi wa haja alistaafu akapewa mafao yake kama milioni 800
Ghafla akaanza kuambatana na hawa matapeli eti kuna mali za wajerumani.... akaanza kutumia hela kuyachimba ikiwemo kuagiza hadi mtaalamu wa kimizimu kutoka Congo, matambiko nk
Mwisho wa siku hakuona hata dini moja, huwezi amini anapanda daladala kauza nyumba magari mashamba nk

Binafsi tulipo pata tu taarifa anaanza nilienda kumsihi hadi nikampigia magoti asijiusishe huo ni utapeli
Mwanae akalia machozi siku tatu lakini mzee akatujibu tulieni nyie ntapiga hela mitawapatia na umasikini wenu sasa basi
Sasa hivi tukikutana hataki kuongea chochote
 
Wakuu hivi ni kweli hizi pesa za kijerumani zipo? Je kuna mtu yeyote anaushuhuda kuwa katajirika kupitia hizi hazina za kijerumani ?
 
Wakuu hivi ni kweli hizi pesa za kijerumani zipo? Je kuna mtu yeyote anaushuhuda kuwa katajirika kupitia hizi hazina za kijerumani ?
Jamani hii imani kweli ipo? Hakuna ukweli wowote. Wajerumani wangepata utajiri wapi??? Koloni ya Afrika ya Mashariki ilikuwa mradi uliohitaji pesa kutoka Ujerumani kwa kulipa mishahara ya watumishi na askari na kwa ajili ya ujenzi wa reli na kadhalika, haikuwa mradi uliozalisha utajiri.

Mfano wa pekee ninaojua ni sanduku la visenti vya Heller lililozamishwa kwenye ziwa la Masoko-Tukuyu. Lakini visenti hivyo havina thamani.

Lakini ni dhahiri watu wanapenda kutapeliwa na kuamini mambo ya freemasons, hazina zilizofichwa na kadhalika. (Pia wako wachache wanaopenda kujikimu kwa kuwatapeli wengine)
 
Asante kwa majibu
 
Mkuu naomba nikuulize, nimeona unapenda sana kutaja freemason kwenye comments zako, wewe kwa uelewa wako unaelewa nini kuhusu freemason?
 
Mkuu naomba nikuulize, nimeona unapenda sana kutaja freemason kwenye comments zako, wewe kwa uelewa wako unaelewa nini kuhusu freemason?
Sidhani kwamba ninapenda kutaja Freemasons. Ninavyosikia ni kundi kama klabu inayofanana na makundi mengine kama vile Lions Club, Rotary na kadhalika ambako watu wenye pesa (au wanaopenda kujitazama kama watu wenye umuhimu fulani) wanakutana. Tabia ya pekee ya Freemasons ni walianza miaka 300 iliyopita, tena kwa kuunda masimulizi eti wametokana na jumuiya za wajenzi wa karne zilizopita wakitunga desturi za ajabu kidogo na kujaribu kuficha sehemu za desturi hizo . Ambayo mimi naona ni tabia za kitoto kiasi....
Pia najua wako watu wanaosimulia hadithi za njama juu ya Freemasons ambazo ni kitoto zaidi kuliko hao wenyewe ...
 
Reactions: T11
Nimesema unapenda kuitaja freemason kwakuwa nimeona kwenye comments zako kadhaa ukihusisha freemason na hii issue ya Mali za mjerumani, kuwa wanaoamini freemason wako sawa na wanaoamini issue za rupia, anyway point yangu ni kwamba freemason sio kitu cha kusadikika maana wanajulikana na wapo, ila ukisema hizi mambo za Mali za mjerumani ni fix unaweza kueleweka maana ni ngumu kukutana na mtu aliepata hizo hela za mjerumani
 
Enzi za kutokuwa na sheria ya mitandao watu walikuwa wanafunguka sana

Kama kweli vile
 
Gramu 1 ya original red mercury ambayo imehifadhiwa vyema ni zaidi ya Bil 12. Hata kama imepungua nguvu kwa maana ya mionzi yake bado inauzika na utapata bei safi tu. Pm me kwa details
Itakuwa watu wamelizana sana humu
 
Bomu limewekwa mwaka 1900's huko linaweza kulipuka leo? Uzi ulijaa fix huu au sababu ya nyakati ulizoandikwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…