Rushwa ni halali Tanzania? Askari wa barabarani wanachukua rushwa bila kificho wala hofu

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Habari wanakamati?

Naomba kuuliza kaswali kadogo tu.

Hivi nchi hii ya Tanzania rushwa si kosa tena? Polisi kwenye vituo vyao wako busy kuchukua rushwa bila haya. Barabarani pia wanachukua rushwa kwa bodaboda, watu wa bajaji na daladala kweupe.

Ukitaka kuhakikisha haya panda daladala ujionee. Traffic Police anasimamisha gari na wala halitazami gari alilolisimamisha zaidi ya ku negotiate na dereva au konda.

Kuna center moja hapa Dar traffic wana ratiba maalum. Wanaanza kupiga pesa kwenye daladala, kisha private car, kisha bajaji, halafu bodaboda na kumaliza na magari ya mizigo.
 
Wale nini sasa, Acha nongwa mzee
 
Magufuli alihalalisha hiyo na kuiita hela ya kupiga brashi viatu.

Huku akijinadi kuwa kinara wa kupiga vita rushwa
 
alafu wanapeleka kwa waliowapanga golini, usipo peleka unarusdishwa kikosi cha fidifosi.
 
Malamba mawili pale gari lina simamishwa, konda anamkimbilia trafic baada ya kuambiwa wa dereva mpe buku 2 abiria tunasubiri arudi safari inaendelea.
 

Hii nchi ni ya aina yake. Ndiyo hawa hapa:


Wako ki rasmi zaidi.
 
Hiyo haiwezi kuguswa kwa mgao wake unapanda ngazi mpaka juu kabisa. Takukuru walijua wala hujishughulisha nalo
 
Magufuli alihalalisha hiyo na kuiita hela ya kupiga brashi viatu.

Huku akijinadi kuwa kinara wa kupiga vita rushwa
magufuli alikataa kuwa mnafiki kama wewe na mleta mada.
 
Trafiki ni aibu! na sugu!! Kama mnasingiziwa njoni mkanushe hapa kwa wazi! Taja jina lako na kituo chako na picha yako kisha kanusha tuhuma hizi!!
 
Swali?wamewakuta na makosa au la

Swali?mlitaka wawapeleke kituoni au ulikubali
Mmalizane pale

Ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…