RUSSIA ECONOMY: Ripoti mpya ya World Bank yaidhinisha Russia kuingia kundi la mataifa yenye kipato kikubwa duniani licha ya kuwa vitani na vikwazo

Ujerumani, Japan ni mataifa ya hovyo sana na kuna South Korea

Uchumi wa Japan nao unashuka huko

Hakuna faida ya kuziiishi sera za Marekani
 
Yeye anaona hiyo ni mpya kumbe wamestiki hapo kwa mda mrefu tu. Jambo zuri kwao ni kuilinda hiyo kutokushuka
 
Kuiba nako kunahitaji akili mtu wangu popoma utamuibia nani asishituke?
Haya nambie Japan anaiba wapi?
Kwahio Japan nae kampita yuesiei??,, na hao wengine walinufaika mapema na system zao za ukoloni na wakaja kuacha ukoloni mambo leo,,,,,......
 
Mtu anasupply gas kwako, anakupa mafuta, anatengeneza silaha na kuyauzia mataifa makubwa mengi duniani, yuko na madini mengi tena ya thamani. Its simple tu RU is a big nation, wewe unadhani anaanguka kirahisi tu
 
Mtu anasupply gas kwako, anakupa mafuta, anatengeneza silaha na kuyauzia mataifa makubwa mengi duniani, yuko na madini mengi tena ya thamani. Its simple tu RU is a big nation, wewe unadhani anaanguka kirahisi tu
Umesema vyema
 
Usimuamushe aliyelala, nafikiri pamoja Russia kuwa uchumi wake haikuwa mbaya lakini kwa matendo waliyomfanyia wamagharibi ameamka na kuwa aggressive zaidi katika kufanya biashara na mabara mengine bila kuitegemea ulaya pekee maana muda wowote ulaya inaweza kumuangusha. Hivyo tutegemee uwekezaji zaidi wa warusi katika afrika au Asia kwa miaka ijayo.
 
Urusi amewekewa vikwazo zaidi ya 16,000 vya aina mbalimbali ila wao wamelenga kupangua vile vikwazo vikubwa.

Hivi vikwazo Mrusi alikwishajiandaa navyo tangia 2014 alijipanga.

Moja ya vikwazo vikubwa ni kuzuia warusi wasiuze mafuta.

Lakini Mrusi akaja na meli ziitwazo "Shadow Vessels" yaani meli kivuli na meli hizi zajaza mafuta na zatumia bendera za mataifa mengine na zaenda hadi International waters na zikifika pale zafanya butter trade na nchi wanunuzi zapakia mafuta na kutia kwenye meli zao na kisha zasepa na biashara zaendelea huku Mrusi akitia fedha kibindoni.

Usione Xi Jinping aenda Moscow mara kwa mara au Modi wa India kesho aenda Moscow twaambiwa ni ziara, hizi si ziara kinofanyika ni kufanikisha biashara zao.

Au usione Putin atoka kidogo aenda kwenye nchi zenye uhitaji (demand) ya nishati, teknolojia na vingine ni biashara hizo warusi wazifanya hivyo hawawezi kuwa na uchumi wa chini.

Mrusi alokifanya amegawa uchumi wake upo uchumi wa kivita (economic war) na uchumi kivuli na uchumi wa kawaida ambao ndo rasmi lakini upo imara.

Uchumi wa kivita ni ule ambao viwanda vya Urusi vyaendelea kuzalisha silaha za aina zote zikiwemo zile za kukabiliana na silaha za NATO na Marekani kiteknolojia. Wakihitaji aina tofauti za silaha hiyo kazi wamepewa Iran na Korea Kaskazini ndo wamuuzia silaha.

Uchumi kivuli ndo huo wa kuuza mafuta kwa kutumia meli bandia na pia kununua malighafi kama machine za kufulia zinotumika kutengeneza ndege zisizo na rubani.

Uchumi wa kawaida ni ule wa kuhakikisha warusi wana uwezo wa kula, kuishi maisha ya kawaida kama hawako vitani na maduka yote yamejaa bidhaa hivyo ile PPP ipo kama kawaida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…