Ruto asema Majaji ni Wala Rushwa wakubwa na wanaendeshwa na Wanasiasa, asema Wananchi waamue atupa kule Hukumu ya mahakama!

Ruto asema Majaji ni Wala Rushwa wakubwa na wanaendeshwa na Wanasiasa, asema Wananchi waamue atupa kule Hukumu ya mahakama!

Safi kabisa....tabia ya kuchekeana ni very irritating..
We miss you JPM.
Pumzika kwa amani mwamba.
Apumzike ili iweje wakati yeye ndio alikuwa kinatra wa kuingilia mihimili mingine? Wanasiasa wangapi wa upinzani walifungwa jela kwa amri zake?Hopele kabisa.
 
Ila hiyo mahakama ilipompa ushindi wa urais haikuwa shida. Mnafiki huyo.
Huyu ananikumbusha chama fulani cha siasa. Mahakama ikiamua ni favor ya kesi zao haki imetendeka isipokuwa hivyo mahakama sio huru.Wakishinda uchaguzi husikii kelele za tume ya uchaguzi wakishindwa tume sio huru.
 
Dr Ruto amewaambia live Majaji kwamba wao ni Wala Rushwa wakubwa na wanaendeshwa na Wanasiasa

Rais Ruto ni kama amerudia kauli ya Mwanasiasa Maarufu nchini na Africa Mashariki Rostam Aziz kwamba Majaji huamua kwa Rushwa na kupigiwa Simu Moja tu

Ruto amemtaka Katibu mkuu wa Ujenzi kuendelea na Ujenzi wa barabara pamoja na Uwepo wa Zuio la mahakama, Ruto amesema Wananchi ndio mahakama ya Haki

Source: Citizen TV
Hiyo nayo ni siasa pia
 
Hivi Comment hii kweli imeandikwa na Lucas Mwashamba ninayemfahamu au simu yake leo amemuachia mtu mwingine??????????!!!!!!!!!!!!!???
Kwa hiyo imeandikwa na nani? Shida yako wewe unashindwaga kunielewa kutokana na kujenga mtizamo hasi juu yangu na hivyo kujipa ukipofu kwa chochote nitakacho kiandika humu unaona kibaya na hakifai na ni uchawa tu.
 
Safi kabisa....tabia ya kuchekeana ni very irritating..
We miss you JPM.
Pumzika kwa amani mwamba.
Jizi na muuaji katili, liendelee kuteseka kwa damu zisizo na hatia lilizomwaga
 
Sasa hapo anaonyesha mfano mbaya kwa Taifa lake.maana kushindwa kuheshimu na kuamini mahakama za nchini mwake anatoa mwanya kwa watu wengi zaidi na maafisa wengi zaidi wa serikali yake na matajiri wengi na wenye pesa zao kufanya maamuzi bila hofu wala uoga kwa kutambua kuwa hata hukumu ikitoka basi hawataiheshimu .

Lakini pia hakuna muwekezaji anayeweza kupenda kuwekeza mahali ambapo mihimili kama mahakama haiheshimiwi.kauli hiyo maana yake inawakimbiza wawekezaji na kuwakosesha imani kwa mifumo ya ndani ya utoaji haki kama vile mahakama. maana yake anataka yeye ndiye kuwa mahakama mwenyewe na muamuzi mwenyewe.jambo ambalo kwa wenye akili hawawezi kuliunga mkono maana anataka kuendesha nchi kibabe kama nyampara.

Pia kauli hiyo inaweza kuchochea Vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu na kujichukulia sheria mkononi kwa wananchi kwa kutambua kuwa maamuzi ya mahakama hayaheshimiwi na yanaweza kupuuzwa na kutupiliwa mbali na hivyo dawa ni kumalizana tu.

Kama anaona wananchi ndio watoa haki basi asimamishe mfumo wa mahakama ili kesi zote na mashitaka yote yawe yanapelekwa kwa wananchi wasio juwa hata vifungu vya sheria.lakini pia kauli hiyo ni shambulizi dhidi ya mahakama na mifumo yote ya utoaji haki.

Lakini pia kauli hiyo itawaumiza zaidi wanyonge na maskini kwa kukosa kimbilio la kupata haki zao,hasa pale kesi inapokuwa inawahusu wakubwa na wenye pesa zao au matajiri kwa kuwa watazichezea na kuzidharau hukumu na amri za mahakama na hivyo kuwafanya masikini kuishi kwa kukata Tamaa huku mioyo yao ikiwa inabubujikwa na machozi kwa kukosa mahali pa kukimbilia.jambo Ambalo Ni la hatari sana kwa usalama wa Taifa na utulivu maana watu wanaweza kuingia barabarani kwa kujitoa mhanga bila uoga kwa kusema bora kifo cha heshima cha kupigania haki zao kuliko kuishi kwa mateso ya kuonewa na kudhulumiwa haki zao.
Hakumu wa Mahakama ya Mwanzo
 
Asijidanganye, anaweza akawajibishwa kisheria na inaweza ikamgharimu yeye mwenyewe binafsi pamoja na Urais wake. Katiba ya Kenya ni nzuri, hairuhusu huo Udikteta wake anaotaka kuufanya.
Hivi Nyumba moja inakuwaje na ma baba wawili!? Baba mmoja akitoa amri hii kwa watoto, hapo hapo baba mwingine tena anakuja kutengeua amri ya baba wa kwanza, sasa hiyo nyumba mwisho wa siku lazima itakosa msimamo thabiti! Amiri Jeshi Mkuu apewe heshima zake kama Mkuu wa Nchi na siyo kuingiliwa kwenye maamuzi yake!!
 
Hivi Nyumba moja inakuwaje na ma baba wawili!? Baba mmoja akitoa amri hii kwa watoto, hapo hapo baba mwingine tena anakuja kutengeua amri ya baba wa kwanza, sasa hiyo nyumba mwisho wa siku lazima itakosa msimamo thabiti! Amiri Jeshi Mkuu apewe heshima zake kama Mkuu wa Nchi na siyo kuingiliwa kwenye maamuzi yake!!
Nchi ya Kenya kwa Katiba yake ile siyo "Banana Republic" kama ilivyo kwa nchi ya Tanzania. Kwa Kenya, Rais siyo 'Mungu' kama ilivyo kwa Tz.
Kama wewe kwenye nchi yako umezoea kuishi kiholela na hovyo hovyo bila utaratibu, usifikiri kwamba na watu wengine wote wanaishi hivyo ktk nchi zao, hapana. Katiba ya nchi, Sheria, Kanuni na taratibu ni lazima zufuatwe, Kenya haiendeshwi kwa Amri Haramu za Rais wa nchi kama ilivyo kwa Tz.
 
Back
Top Bottom