Ruvuma: Mamba aliyeua binadamu ageuzwa kitoweo

Ruvuma: Mamba aliyeua binadamu ageuzwa kitoweo

Joined
Sep 23, 2024
Posts
64
Reaction score
43
Kwa mujibu wa taarifa ya jeshi la polisi mnamo January 02 mwaka huu, wananchi wa Kijiji cha Ng’ombo wilayani Nyasa walimuua mamba na kufanya kitoweo.

Majira ya saa kumi na moja alfajiri kwenye fukwe za Ng’ombo-ziwa Nyasa, Kijiji cha Ng’ombo kata ya Chiwinda, mwanamke mmoja aliyetambulika kwa jina la Ester Mapunda (48) akiwa anaoga katika fukwe ya ziwa Nyasa alifariki dunia baada ya kukamatwa na mamba kisha kuzama nae majini.

Baada ya tukio hilo wavuvi wa fukwe hizo kwa kushirikiana na askari wa jeshi la polisi na maliasili walifanya msako mkali katika maeneo ya ziwa hilo na kufanikiwa kumuua mamba huyo na wananchi walimfanya kitoweo.
 
Walivyompata na kumuuwa hawakukuta mabaki ya marehemu tumboni kweli?

Au hawakujali muhimu ilikuwa ni kumpa displini mamba kwa kumla
 
Walivyompata na kumuuwa hawakukuta mabaki ya marehemu tumboni kweli?

Au hawakujali muhimu ilikuwa ni kumpa displini mamba kwa kumla
Mamna anaweza ku digest mpaka keratin ambayo wanyama wengine hawawezi. So probably wasingeweza kupata mabaki labda kama walimkamata muda/siku chache baada ya tukio.

NB: Keratin is a protein that makes up hair, nails, and the outer layer of skin. It is also found in feathers, horns, claws, and hooves.
 
Watu waache kuoga kwenye maeneo yenye mamba
 
Njaa. Nchi hii watu wana shida sana, ndiyo maana nasema kuwa kiongozi Bongo inatakiwa uwe na roho ya ukatili. Kuna watu wanamaliza miezi na miezi bila kula nyama. siyo kwamba na vegeterian bali wameikosa.
Imagine Tanzania ndio nchi ya tatu kwa ng'ombe wengi halafu bado kilo ya nyama ni elfu kumi na inazidi kupanda kwa baadhi ya maeneo.
 
Back
Top Bottom