Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Hizi picha hapa chini zinadaiwa ni za daraja la mto Muhuwesi wilayani Tunduru mkoani Ruvuma.
Inadaiwa kwamba inakaribia mwaka wa nne sasa tangu nguzo zake zicheze na halijafanyiwa marekebisho hivyo inalazimika gari zote zipite upande mmoja.
======
UPDATES
=======
Ufafanuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru ndugu Julius Mtatiro
=====
HABARI ZAIDI KUTOKA TANROADS;
Nguzo za daraja hazijaathirika wala hazikusogezwa na mafuriko kutoka sehemu moja kwenda nyingine (Daraja lingeanguka).
Kilichoathirika ni sehemu ya juu ya daraja (deck) ambapo nusu ya kwanza ya deck (m 54) ilisukumwa na mafuriko ya maji yaliyokuwa yamebeba magogo kwa takribani sentimeta 20. Deck hiyo ilitembea kupitia bearing zilizo juu ya nguzo za Daraja.
www.jamiiforums.com
Inadaiwa kwamba inakaribia mwaka wa nne sasa tangu nguzo zake zicheze na halijafanyiwa marekebisho hivyo inalazimika gari zote zipite upande mmoja.
======
UPDATES
=======
Ufafanuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Tunduru ndugu Julius Mtatiro
Julius Mtatiro said:Ni suala la uelewa tu wa kihandisi. Muhuwesi ni moja ya madaraja yale makubwa kabisa ambayo uhandisi wake ni wa juu na hata gharama za utengenezaji wake ni billions.
Mafuruko ya March 2022 kwenye mto Muhuwesi yalipelekea hili daraja kuhama kidogo kwenye njia yake.
TANROADS ambao ndiyo wasimamizi wa daraja husika walifika kutoka mkoani na Makao Makuu na kufanya tathmini yao - wakaelekeza daraja litumike upande mmoja mpaka pale watakapochukua hatua zaidi.
Kwa mujibu wa Tanroads, daraja ni salama kwa sasa na magari yanaweza kupita kama kawaida lakini wamechukua tahadhari ili kuruhusu magari yapite upande mmoja tu.
Kama kuna maswali au ufafanuzi zaidi ni muhimu mumtafute MD wa TANROAD na timu yao Makao Makuu kwani si rahisi mimi kufahamu kwa undani na kufafanua masuala ya kihandisi.
JSM,
Tunduru,
31 Machi 2023.
=====
HABARI ZAIDI KUTOKA TANROADS;
Nguzo za daraja hazijaathirika wala hazikusogezwa na mafuriko kutoka sehemu moja kwenda nyingine (Daraja lingeanguka).
Kilichoathirika ni sehemu ya juu ya daraja (deck) ambapo nusu ya kwanza ya deck (m 54) ilisukumwa na mafuriko ya maji yaliyokuwa yamebeba magogo kwa takribani sentimeta 20. Deck hiyo ilitembea kupitia bearing zilizo juu ya nguzo za Daraja.
TANROADS: Kilichoathirika ni Deck kusogea kwa sentimeta 20, sio nguzo za Daraja la Mto Muhuwesi Tunduru
Tunaomba kusahihisha kwamba: Nguzo za daraja hazijaathirika wala hazikusogezwa na mafuriko kutoka sehemu moja kwenda nyingine (Daraja lingeanguka). Kilichoathirika ni sehemu ya juu ya daraja (deck) ambapo nusu ya kwanza ya deck (m 54) ilisukumwa na mafuriko ya maji yaliyokuwa yamebeba magogo...