Ruvuma: Waathirika 4,023 waacha kutumia dawa za ARV sababu ya imani ya dini

Ruvuma: Waathirika 4,023 waacha kutumia dawa za ARV sababu ya imani ya dini

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Baadhi ya wakazi wa Mkoa wa Ruvuma ambao ni wathirika wa Virusi vya UKIMWI (VVU) wamebainika kutotumia ARV ambazo ni dawa za kufubaza makali ya VVU wanazopewa vituoni kutokana na imani ya dini.

Mratibu wa Kudhibiti UKIMWI Mkoani Ruvuma, Josephat Kalipesa amesema hatua hiyo imebainishwa licha ya takwimu za mwaka 2021-2022 kuonesha maambukizi mapya Mkoani Ruvuma ni zaidi ya watu 1,800 sawa na watu watano kuambukizwa kila siku.

Kalipesa ameeleza kuwa kwa jumla ripoti ya maambukizi ya mkoa huo inaonesha idadi ya watu 4,023 sawa na 7% wanadaiwa kuacha kutumia dawa za ARV kutokana na imani ya dini zao.

Amesema: "Kuna wanaotangaza kuwa wamepona ugonjwa wa UKIMWI kutokana na maombi."

Aidha, John Kahimba kutoka Baraza la Taifa la Watu Wanaoishi na VVU Tanzania (NACOPHA) anasema aliacha kutumia dawa lakini ndani ya miezi 9 hali yake kiafya ikawa mbaya akalazimika kuanza kutumia dawa za ARV.

Naye, Edmund Kapinga ambaye ni Mwenyekiti wa Waviu Songea anasema wengi walioacha kutumia dawa hizo muda mrefu madhara yalikuwa makubwa na mmoja wao alifariki hivi karibuni.


Source: Azam TV
 
Naomba takwimu za maambukizi
1.mbinga
2.Nyasa.
3.Tunduru
4.songea.
Mwenye nazo ani tag plz
 
Hatua hiyo imejulikana licha ya takwimu za mwaka 2021-2022 kuonesha maambukizi mapya Ruvuma ni zaidi ya watu 1,800 sawa na watu watano wanaoambukizwa kila siku, ambapo watu 4,023 sawa na 7% wanadaiwa kuacha kutumia dawa za ARV kutokana na imani ya dini zao.


_______________________

Alieelewa hapo Juu anieleweshe

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Nilipita Mbinga pale juzi Kati nikapiga manzi mmoja kavukavu ila nadhani Hana ngoma yule
 
Ukimwi unaua tumia ndomu na mmeze dawa!
 
Tunduru pale.hatari terminal pub na the Amazon.mmiombee
 
Nilipita Mbinga pale juzi Kati nikapiga manzi mmoja kavukavu ila nadhani Hana ngoma yule
Kavu kavu ina raha yake, hasa ukiwa umepigwa "tozo" la maana.

Au umesimangiwa sana kumpenda na kutukanwa kwa ajili ya huyo mtu, lakini leo umempata, yupo mikononi mwako!
 
Naomba takwimu za maambukizi
1.mbinga
2.Nyasa.
3.Tunduru
4.songea.
Mwenye nazo ani tag plz
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Lete kwanza za njombe plus makambako,

Nikupe za mbinga.
 
Back
Top Bottom