JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,780
- 6,607
Umoja wa wazee Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma, umewasilisha malalamiko yao kwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Laban Thomas wakiwatuhumu wahudumu wa Hospitali ya Wilaya hiyo kwa kuwanyima dawa, licha ya kutengewa dirisha lao katika hospitali hiyo.
Mkuu wa Mkoa Laban Thomas ametoa agizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Aziza Mangosongo kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki na pia watumishi wabadili lugha wanayotumia kwa wazee.
Naye, Katibu wa Hospitali hiyo, Shukuru Msimbe amedai kuwa wazee wengi wana magonjwa makubwa kuliko uwezo wa dawa uliopo hospitalini hapo.
Source: Azam TV
Mkuu wa Mkoa Laban Thomas ametoa agizo kwa Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Aziza Mangosongo kuhakikisha wazee wanapata huduma stahiki na pia watumishi wabadili lugha wanayotumia kwa wazee.
Naye, Katibu wa Hospitali hiyo, Shukuru Msimbe amedai kuwa wazee wengi wana magonjwa makubwa kuliko uwezo wa dawa uliopo hospitalini hapo.
Source: Azam TV