KERO Ruvuma: Waziri wa Ardhi tunakuomba uje Kata ya Liganga kutatua mgogoro wa ardhi, upimaji wa ardhi ufanywe upya, tunateseka

KERO Ruvuma: Waziri wa Ardhi tunakuomba uje Kata ya Liganga kutatua mgogoro wa ardhi, upimaji wa ardhi ufanywe upya, tunateseka

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Joined
Sep 23, 2024
Posts
64
Reaction score
43
WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.17_1a59bf71.jpg
Mimi Mkazi wa Songea Kijijini, Kata ya Liganga katika Jimbo la letu ambalo Mbunge wetu ni Jenista Muhagama, huku tuna changamoto ya ardhi.

Miaka 10 iliyopita tuliuziwa eneo na Kijiji ambapo kipindi hicho kilikuwa kinaitwa Kijiji cha Liganga, tulilitumia eneo hilo kwa ajili ya kufanya kilimo.

Baadaye Jimbo lilipona eneo hilo linaleta faida kwa aradhi kukubali kilimo, wakaongeza mipaka ambayo ilikuwepo ili waweze kulichukua na eneo letu hilo.

Suala hilo lilifika hadi Mahakamani, Hakimu aliyekuwepo awali aliwaambia waliokuwa wamechukua eneo letu na tupo nao kwenye kesi kuwa hawajatenda haki kwa kuwa wamezidisha eneo wanalosema ni la kwao.
WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.18_75faf7f8.jpg

WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.19_0541ed25.jpg
Kuna mwenzetu ambaye alikuwa kiongozi wetu pamoja na Mwenyekiti aliyeshiriki kutuuzia naye akatugeuka kwa kuwa walihadaiwa upande wa pili.

Wananchi ambao tunadai haki zetu za kuchukuliwa maeneo yetu tupo zaidi ya 500 na kuna ekari 1000.

Sisi ni raia ambao tunajichangacha, hatuna uwezo wa kushindana nao.

Wito wetu ni kuwa tunaomba Waziri wa Ardhi aje atusaidie kwa kuwa hizo bikoni zilizowekwa sasa hivi siyo halali, zimewekwa kwa lengo la kuchukua ardhi yetu sisi Wananchi wanyonge.

Hawa watu sisi tunashindwa kupambana nao kwa kuwa wana nguvu ya fedha kuliko sisi.

Sisi ni Watanzania na tuna haki ya kuishi maeneo yoyote yale, nyaraka ambazo zinaonesha tuliuziwa na Serikali ya Mtaa tunazo lakini hata baadhi ya wale waliotuuzia nao wametugeuka kwa kuwa wanashirikiana na hao washindani wetu.

Waziri wa Ardhi akija pamoja na maafisa wake wa Wizara wakapima na kubaini kuwa kweli eneo tunalolipigania lipo ndani ya bikoni ambazo zilikuwepo awali, sisi tutaondoka kwa amani lakini pia ikibainika wao ndio wameingilia eneo letu na kutotenda haki basi watuache tuishi kwa amani.

Pamoja na hivyo tunamuomba Mbunge wetu Jenista Mhagama naye awepo katika timu hiyo, Wananchi wake tunateseka.

Nimeambatanisha baadhi ya nyaraka zinazoonesha tulinunua kwa halali kwa kufuata hatua za Kiserikali:
WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.15_1ab4e093.jpg

WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.16_41c358a9.jpg

WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.16_12752831.jpg

WhatsApp Image 2025-01-10 at 14.10.17_ff5d1204.jpg
 
Yule aligalagala chini akasema kila kitu kipo sawa, ni nini tena shida?
 
Mimi Mkazi wa Songea Kijijini, Kata ya Liganga katika Jimbo la letu ambalo Mbunge wetu ni Jenista Muhagama, huku tuna changamoto ya ardhi.

Miaka 10 iliyopita tuliuziwa eneo na Kijiji ambapo kipindi hicho kilikuwa kinaitwa Kijiji cha Liganga, tulilitumia eneo hilo kwa ajili ya kufanya kilimo.

Baadaye Jimbo lilipona eneo hilo linaleta faida kwa aradhi kukubali kilimo, wakaongeza mipaka ambayo ilikuwepo ili waweze kulichukua na eneo letu hilo.

Suala hilo lilifika hadi Mahakamani, Hakimu aliyekuwepo awali aliwaambia waliokuwa wamechukua eneo letu na tupo nao kwenye kesi kuwa hawajatenda haki kwa kuwa wamezidisha eneo wanalosema ni la kwao.

Kuna mwenzetu ambaye alikuwa kiongozi wetu pamoja na Mwenyekiti aliyeshiriki kutuuzia naye akatugeuka kwa kuwa walihadaiwa upande wa pili.

Wananchi ambao tunadai haki zetu za kuchukuliwa maeneo yetu tupo zaidi ya 500 na kuna ekari 1000.

Sisi ni raia ambao tunajichangacha, hatuna uwezo wa kushindana nao.

Wito wetu ni kuwa tunaomba Waziri wa Ardhi aje atusaidie kwa kuwa hizo bikoni zilizowekwa sasa hivi siyo halali, zimewekwa kwa lengo la kuchukua ardhi yetu sisi Wananchi wanyonge.

Hawa watu sisi tunashindwa kupambana nao kwa kuwa wana nguvu ya fedha kuliko sisi.

Sisi ni Watanzania na tuna haki ya kuishi maeneo yoyote yale, nyaraka ambazo zinaonesha tuliuziwa na Serikali ya Mtaa tunazo lakini hata baadhi ya wale waliotuuzia nao wametugeuka kwa kuwa wanashirikiana na hao washindani wetu.

Waziri wa Ardhi akija pamoja na maafisa wake wa Wizara wakapima na kubaini kuwa kweli eneo tunalolipigania lipo ndani ya bikoni ambazo zilikuwepo awali, sisi tutaondoka kwa amani lakini pia ikibainika wao ndio wameingilia eneo letu na kutotenda haki basi watuache tuishi kwa amani.


Nimeambatanisha baadhi ya nyaraka zinazoonesha tulinunua kwa halali kwa kufuata hatua za Kiserikali.

Pamoja na hivyo tunamuomba Mbunge wetu Jenista Mhagama naye awepo katika timu hiyo, Wananchi wake tunateseka.
Kijiji ni Cha kwenu , waachieni ardhi itumike kwa faida ya wote


Pesa ya makaa ya mawe mle wenyewe ?
 
Back
Top Bottom