Rwanda kuanza kutumia robots ili kupunguza daktari na mgonjwa kukutana katika kuepuka Corona

Rwanda kuanza kutumia robots ili kupunguza daktari na mgonjwa kukutana katika kuepuka Corona

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Waziri wa Afya wa Rwanda Daniel Ngamije amesema wizara yake imepanga kusambaza roboti kwenye vituo vya kutibu virusi vya Corona na maeneo mengine ya umma.

Akiongea kupitia televisheni waziri Ngamije amesema Roboti tano zilizoagizwa kutoka nje ambazo zimepewa majina ya Kinyarwanda zitatumika kama kiunganishi kati ya dokta na mgonjwa, na hivyo kupunguza mawasiliano ya binadamu na hatari za kusambaa kwa virusi.

Waziri Ngamije amesema mbali na kutumika kwenye vituo vya matibabu, roboti hizo pia zitatumika kupima joto kwenye maeneo ya umma kama vile vituo vya mabasi na milango ya kuingilia maduka ya manunuzi, na kwamba baadhi ya roboti tayari zimeshafika Rwanda ambapo zitawekewa programu na kusambazwa kwanza.

Kwa mujibu wa wizara ya afya ya nchi hiyo hadi kufikia Ijumaa jioni, Rwanda imethibitisha wagonjwa wa virusi vya Corona 273, wakiwemo waliopona 136.
 
Ahsante kwa taarifa waambie sisi huku ni mwendo wa Nyungu tu na kurudishana bungeni hata hatuogopi sheria
 
Rwanda na majigambo, wazee wa kujigamba East Africa wakati uwezo ni 0.

Mpaka sasa Tanzania kutokana na maamuzi raisi magu aliyofanya ndio hata ma raisi wa ulaya wanabadili na kuelekea uelekeo ule ule wa Tz.Hii imenifanya nimheshimu huyu mzee kwa kweli.Sijaona East Africa, wengine bogus tu
.

Rwanda hamjafikia huo uwezo wa kutumia robots kupunguza maambukizi.
USA wana robots zinatengenezwa NASA na zinatumwa mpaka sayarini lakini Corona inawapiga 3 - 0.

Robots hazitosaidia chochote,bora hata sisi tuna Fanya research ya tiba asili.
 
Hao Rwanda wanatumiwa na mabeberu tu, sisi wazalendo tutapiga kikombe cha babu wa Madagaskar na pia kuna dawa yetu tumetengeneza pale NIMR kupambana na ka ugonjwa haka kadogo.
 
Back
Top Bottom