Rwanda kuanza kutumia robots ili kupunguza daktari na mgonjwa kukutana katika kuepuka Corona

Kumbe we boya kabisa! Hujui kitu.
 

Attachments

  • 1350_900_46160b50614d3a09e5bbb635-768x512.jpg
    40.1 KB · Views: 1
  • 20190301_111833-768x576.jpg
    35.4 KB · Views: 1
  • 1350_900_46160b50614d3a09e5bbb635-768x512.jpg
    40.1 KB · Views: 1
  • factory.jpg
    33.3 KB · Views: 1
  • images (2).jpeg
    8.5 KB · Views: 1
  • images (1).jpeg
    10 KB · Views: 1
  • images.jpeg
    9.9 KB · Views: 1
Rwanda ROBOTI Zitasaidia kufanya kazi za kuhudumia wagonjwa wa Covid19 zikisaidiana na wauguzi na madaktari

Rwanda imesema kuwa tayari inatumia roboti katika kuzuwia maambukizi ya virusi vya corona kwenye vituo vya ugonjwa huo. Hatuahii inakuja baada ya taifa hilo kulegeza masharti ya sheria ya kutotoka nyumbani. Zitasaidiakufanya kazi za kuhudumia wagonjwa wa Covid19 zikisaidiana na wauguzi na madaktari'', alisema Waziri wa Afya Dkt Daniel Ngamije.

'' Roboti inaweza kuchukua sampuli za mgonjwa katika badala ya muuguzi. Kuna kazi nyingi ambazo roboti zinaweza kufanya kuhudumia wagonjwa wa covid19, si kwamba wauguzi ama madaktari wameshindwa la hasha, ni kama kuwasaidia kupumua na pengine kuwapa nafasi kufanya mambo mengine ya kuwahudumia wagonjwa ipasavyo'' , anasema Dkt. Ngamije.

Roboti hizo mbazo zimepewa majina ya Kinyarwanda zinatarajiwa kusaidia katika huduma zinazotolewa na madaktari kwa wagonjwa na hivyo kupunguza hatari za usambazaji wa virusi baina ya wagonjwa wa Covid-19 na wahudumu wa afya, alisema Waziri wa afya awali katika mahojiano na Radio Rwanda.

Pamoja na kuwapelekea dawa wagonjwa, roboti pia zitatumika kupima viwango vya joto vya wagonjwa, katika maeneo mengine ya umma kama vile vituo vya mabasi pamoja na kwenye milango ya kuingia katika maduka ya jumla ya bidhaa alisema.
Tangu ulipotokea mlipuko wa COVID-19, Rwanda imekua ikitumia mfumo wa ndege ndogo zisio na rubani (drones) kuwasiliana na umma katika kuupa uelewa juu ya ugonjwa huo hatari.
 
Ngoja kwanza sisi tujipange kuishi na Corona kama mwenzetu tu. Mengine tuwe watazamaji.

Kwani mechi bila watazamaji inaweza kunoga?
 
Nilijua mapema kuwa COVID-19 ni mkakati wa kutambulisha maroboti uraini bila pingamizi.
 
Safi sana.

Wamefuata nyayo za China.

Kipindi kile COVID-19 inawasumbua waChina kabla haijasambaa Ulimwenguni kote, walikuwa wanaonesha kipindi maalum kuhusiana na gonjwa hili la mlipuko hali ilivyo China.

Jinsi Roboti zilivyokuwa zikifanya kazi Hospitalini, kuwapelekea wagonjwa chakula wodoni, madawa, n.k
 
Wanatumia drone kutangaza COVID-19,Kweki mnyalu ni mnyalu tu.
 
Rwanda wanastahili pongezi
Tanzania ndio ina stahili pongezi, Magu kwa kutofanya lockdown mwanzoni nchi nyingi ulaya zilikurupuka ila sasa hivi wanatuiga.
Tanzania tunastahili pongezi.
 
Tanzania ndio ina stahili pongezi, Magu kwa kutofanya lockdown mwanzoni nchi nyingi ulaya zilikurupuka ila sasa hivi wanatuiga.
Tanzania tunastahili pongezi.
Ngoja uzike mzazi au ndugu ndio tutaongea lugha moja
 
Usiwe unakurupuka chooni na kuja kuongea usioyajua.
 

Attachments

  • IMG_20200520_144448.jpg
    139 KB · Views: 1
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…