Rwanda na M23 sasa ni dhahiri

Rwanda na M23 sasa ni dhahiri

Raphael Thedomiri

JF-Expert Member
Joined
Sep 1, 2019
Posts
442
Reaction score
729
Wataalam huru wa Umoja wa Mataifa wamesema jeshi la Rwanda lilihusika kwenye ‘operesheni za kijeshi‘ dhidi ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika maeneo yanayokumbwa na machafuko mashariki mwa Congo.

Kulingana na ripoti ya wataalam hao ambayo shirika la habari la AFP limepata nakala yake, kuna ushahidi wa kutosha kwamba jeshi la Rwanda liliingilia kati moja kwa moja katika vita vya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo dhidi ya waasi wa kundi la M23, na kwamba jeshi hilo liliwaunga mkono waasi hao kwa kuwapa silaha, risasi na magwanda au sare za kivita.

Ripoti hiyo inajiri mnamo wakati Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imekuwa ikiishutumu Rwanda kwa kuliunga mkono kundi la M23.
Msemaji wa serikali mjini Kigali alikanusha madai kwamba Rwanda iliwaunga mkono waasi wa M23. Aidha alikataa kuzungumzia tuhuma nyinginezo dhidi ya Rwanda hadi pale ripoti hiyo ilipochapishwa rasmi.

Chanzo dw
Screenshot_20221223_094348_Samsung Internet.jpg
 
Wataalam huru wa Umoja wa Mataifa wamesema jeshi la Rwanda lilihusika kwenye ‘operesheni za kijeshi‘ dhidi ya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika maeneo yanayokumbwa na machafuko mashariki mwa Congo.

Kulingana na ripoti ya wataalam hao ambayo shirika la habari la AFP limepata nakala yake, kuna ushahidi wa kutosha kwamba jeshi la Rwanda liliingilia kati moja kwa moja katika vita vya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo dhidi ya waasi wa kundi la M23, na kwamba jeshi hilo liliwaunga mkono waasi hao kwa kuwapa silaha, risasi na magwanda au sare za kivita.

Ripoti hiyo inajiri mnamo wakati Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imekuwa ikiishutumu Rwanda kwa kuliunga mkono kundi la M23.
Msemaji wa serikali mjini Kigali alikanusha madai kwamba Rwanda iliwaunga mkono waasi wa M23. Aidha alikataa kuzungumzia tuhuma nyinginezo dhidi ya Rwanda hadi pale ripoti hiyo ilipochapishwa rasmi.

Chanzo dwView attachment 2455359
M23 ni kivuli cha RDF....hilo linafahamika kitambo.

Moronight walker mtu chake zitto junior
 
Kinachompa kiburi dhidi ya congo ni rafiki zake wa damu Uganda. Sasa sijajua kama kashawawaza hao wakubwa wa dunia 🤷‍♂️
Ndugu wa kubwa wa Dunia ndio wana mpa kiburi hata huyo mganda alishawahi mjibu kiburi, kajisahau sana.
 
Kagame anajiona Mungu mtu kwenye hili bara la Africa. Misifa yake ya kijinga itamcost siku moja.

Sent from my CPH1923 using JamiiForums mobile app
Akafunuwe kwenye vitabu vya historia amwangalie Mabutu, sadamu, Gadafi na wengineo walivyokuwa wanapakatwa na wakubwa wa Dunia kwa maslahi yao na sasa wako wapi? Ya huu ulimwengu kwakweli ni magumu sana na yakupita tu.
 
Unashangaa huyo mmoja, kagame ndie muhusika mkuu wa mauaji ya kimbali ya RAIA wa rwanda nchini rwanda na congo, zaidi ya RAIA wa rwanda 2 million walikufa.
Halafu sijui huyu jamaa aliponyokaje kwenye kesi ya yale mauaji ya kimbari! Wakati ukiisoma historia ya hiyo vita unamuona Kagame kama naye alihusika pakubwa tuu.

Labda kwa sababu yeye ni mtutsi na ndio walikuwa wahanga zaidi 🤷‍♂️
 
Back
Top Bottom