S. K. Macharia na Mungiki kumuunga mkono Railonzo ni dalili njema kwao?

S. K. Macharia na Mungiki kumuunga mkono Railonzo ni dalili njema kwao?

Royals

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2011
Posts
1,466
Reaction score
378
Wajumbe wa JF, hamjambo?

Wajumbe A. B. Tichaz, Kabaridi na wengineo wa Kenya, Mambo?

Mada ya hapo juu yahusika. Ni nini maoni yako juu ya kuungwa mkono kwa muungano wa CORD na baadhi ya watu maarufu kutoka nyumbani kwa kina Uhuru ni dalili njema kwa muungano huo?
 
Wajumbe wa JF, hamjambo?

Wajumbe A. B. Tichaz, Kabaridi na wengineo wa Kenya, Mambo?

Mada ya hapo juu yahusika. Ni nini maoni yako juu ya kuungwa mkono kwa muungano wa CORD na baadhi ya watu maarufu kutoka nyumbani kwa kina Uhuru ni dalili njema kwa muungano huo?

This is very signifacant boost kwa Raila, is you ask me. But S.K.Macharia anaweza pia akawa amesukumwa na kesi ya ICC. He would not like like his media empire to be associated na watuhumiwa wa ICC ,wouldn't he? After all, media personnel yumo kwenye ICC 4!
 
Anajisogeza ili jamaa akichukua amfanyie mipango ya kuificha kes yake huyo nimuuaj tu kama alivyo mwema nk hapa tz
 
Wajumbe wa JF, hamjambo?

Wajumbe A. B. Tichaz, Kabaridi na wengineo wa Kenya, Mambo?

Mada ya hapo juu yahusika. Ni nini maoni yako juu ya kuungwa mkono kwa muungano wa CORD na baadhi ya watu maarufu kutoka nyumbani kwa kina Uhuru ni dalili njema kwa muungano huo?

Hawa ni wanabiashara mashuhuri na wanajua hali halisi ilivyo Kenya kwa sasa na hii ishu ya ICC. They are simply
aligning themselves with the right side of history and going above tribal arithmetic and such like stuff.

If Kenya were to face sanctions huyu jamaa stands to lose a lot in terms of his business empire. He experienced
it when Moi was president na anajua japo Uhuru atapewa urais basi mambo hayatakua poa.
 
  • Thanks
Reactions: FJM
This is very signifacant boost kwa Raila, is you ask me. But S.K.Macharia anaweza pia akawa amesukumwa na kesi ya ICC. He would not like like his media empire to be associated na watuhumiwa wa ICC ,wouldn't he? After all, media personnel yumo kwenye ICC 4!

FJM S. K. hana cha kuogopa. Sheria inaoendesha vyombo vya habari haifanani na ile inayoendesha siasa. Hakuna sheria inayomfunga S. K. kumuunga mkono Raila au Uhuru ili kuepuka mtego wa ICC na kama kuna hali kama hii basi inatofautiana na kile sheria ya nchi au katiba mpya inaelezea.
 
Last edited by a moderator:
Wajumbe wa JF, hamjambo?

Wajumbe A. B. Tichaz, Kabaridi na wengineo wa Kenya, Mambo?

Mada ya hapo juu yahusika. Ni nini maoni yako juu ya kuungwa mkono kwa muungano wa CORD na baadhi ya watu maarufu kutoka nyumbani kwa kina Uhuru ni dalili njema kwa muungano huo?

Muungano huu wa CORD na kusajilishwa kwa walio na historia ya uhalifu kama Maina njenga inaonyesha mchanganyiko wa siasa na uhalifu imeshamiri katika siasa za kenya. Hali siasa ilivyo kenya ni mchanganyiko wa unafiki na hila mbali mbali za wanasiasa husika kutafuta ushindi kwa njia zezote. La kusikitisha ni yanatendeka wazi vikirekodiwa hewani kwenye vyombo vya habari. Nilivyomweleza na kumkosoa mdau mwenzangu moja kwamba S K kisheria hawajibiki kujilainisha au kujitambulisha na mwanasiasia yeyote kukwepa mtego wa ICC. Anaongozwa na ethics na professionalism za media. Hivyo, S K ana sababu zake binafsi kujilainisha na Raila ambayo kisheria na kikatiba inakubalika.

Nikukumbushe Royals, S K kuungana na Raila haibadilishi nia ya wakenya kuchagua kiongozi wanayemtaka. Wanasiasa wameonekana kueneza jitihada za kampeini zao kwenye vyombo vya habari kwa manufaa yao lakini bado kuna ile shughuli halisi ya upigaji kura ambayo imebaki mwamuzi wa kweli wa rais ajaye.

Sioni jinsi kuingia kwa Maina njenga kwa chama cha CORD kutamfariji. Huyu ni muhalifu ambaye ana rekodi chafu mno na tuhuma nyingi za mauaji chini ya kundi mungiki ambayo inaendesha shughuli zake kwa njia za kigaidi. Na kwa hivyo nahitimisha kwa kusema huu ni uhalifu. uwepo wake unaihujumu integrity ya chama cha CORD pamoja na kuwa huyu ni mshukiwa anayehusika na utekelezaji wa mauaji ya kimbari na mshaidi MKUU wa vurugu za uchguzi mnamo 2008.
 
FJM S. K. hana cha kuogopa. Sheria inaoendesha vyombo vya habari haifanani na ile inayoendesha siasa. Hakuna sheria inayomfunga S. K. kumuunga mkono Raila au Uhuru ili kuepuka mtego wa ICC na kama kuna hali kama hii basi inatofautiana na kile sheria ya nchi au katiba mpya inaelezea.
Kabaridi,

I agree with you, hakuna sheria yoyote inayomfunga S.K Macharia. But if there is one basi ni hii, "show me your friend and I will tell you who you are". Na ndio sababu nikasema huyu bwana mkubwa hakuta kukaa karibu na harufu ya ICC.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu wangu, Kabaridi, FJM, na Ab-Titchaz,

Ingawa jukwaa hili ni la mambo yaihusuyo Kenya pekee, bahati nzuri lina wasomaji na wachangiaji wengi kutoka nje ya Kenya.
Siasa za Kenya zinafurahisha sana kwa kuwa ni siasa za kibabe na ni kutumia hesabu za hali ya juu mno. Kwa ninyi ambao ni wenye nchi ni vizuri kuchangia kwa kina huku mkijua kuwa kuna washabiki wa Kenya wasio wa Kenya.

Tuje kwenye mchango wa Kabaridi.

Maina Njenga ni Mungiki aliyeokoka. Wakati ule alikuwa ni mtu mzuri sana kwa kundi ambalo silo aliloliunga mkono sana. Alipaswa kujutia makosa yake wakati ule baada ya kujitokeza hadharani. Kwenye siasa za Kenya zilivyo kila mtu muhimu katika jamii ni lazima ana wafuasi wengi nyuma yake ambao watafuatana naye kokote aendako. Ndio masna nikasema ni vizuri kupima jee hakumegui kura za wakikuyu na kuzihamishia kwa Raila?

Kwa mtazamo wangu ni kuwa Muungano wa CORD unazidi kuimarika zaidi katika sura ya Kitaifa zaidi kuliko muungano mwingine wowote jambo ambalo ni jema kwenye siasa.
 
Last edited by a moderator:
Wakuu wangu, Kabaridi, FJM, na Ab-Titchaz,

Kwa mtazamo wangu ni kuwa Muungano wa CORD unazidi kuimarika zaidi katika sura ya Kitaifa zaidi kuliko muungano mwingine wowote jambo ambalo ni jema kwenye siasa.

Kabaridi anaweza kupinga hili, but in my view CORD inaimarika and I will not be surprised kusikia vigogo - kwa magunia- wanarudi CORD mwezi ujao.
 
Kabaridi anaweza kupinga hili, but in my view CORD inaimarika and I will not be surprised kusikia vigogo - kwa magunia- wanarudi CORD mwezi ujao.

Mkuu FJM kwanini unaamini Kabaridi atapinga? au ameshatangaza ni upande gani anaunga mkono?
Kiukweli siasa za kenya ni za kipekee sana, wakati huu wanasiasa wanafanya biashara za hatari sana, ni kujipanga tu kwa kutazama wapi utaweza kuvuna inapofika march 4.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu FJM kwanini unaamini Kabaridi atapinga? au ameshatangaza ni upande gani anaunga mkono?
Kiukweli siasa za kenya ni za kipekee sana, wakati huu wanasiasa wanafanya biashara za hatari sana, ni kujipanga tu kwa kutazama wapi utaweza kuvuna inapofika march 4.

Yuko pande ile ingine, kiongozi!
 
FJM, kusema cord inazidi kuimarika ina maana you are admiting it is a weak coalition inayotegemea wingi wa wanachama kuuza kampeini zake.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: FJM
Wakuu wangu, Kabaridi, FJM, na Ab-Titchaz,

Ingawa jukwaa hili ni la mambo yaihusuyo Kenya pekee, bahati nzuri lina wasomaji na wachangiaji wengi kutoka nje ya Kenya.
Siasa za Kenya zinafurahisha sana kwa kuwa ni siasa za kibabe na ni kutumia hesabu za hali ya juu mno. Kwa ninyi ambao ni wenye nchi ni vizuri kuchangia kwa kina huku mkijua kuwa kuna washabiki wa Kenya wasio wa Kenya.

Tuje kwenye mchango wa Kabaridi.

Maina Njenga ni Mungiki aliyeokoka. Wakati ule alikuwa ni mtu mzuri sana kwa kundi ambalo silo aliloliunga mkono sana. Alipaswa kujutia makosa yake wakati ule

Cord na Raila ni sura ya kitaifa kwa kuwa mkikuyu yeyote asiyeungana na Raila hana sura ya kitaifa, is this what you are trying to tell us?!

Wtz wansaidia kueneza chili dhidi ya wakikuyu wakitaja njonjo. musisahau muda unayoyoma na vizazi vipya viaja
 
Last edited by a moderator:
Kabaridi anaweza kupinga hili, but in my view CORD inaimarika and I will not be surprised kusikia vigogo - kwa magunia- wanarudi CORD mwezi ujao.

Mkuu FJM,
"Vigogo kwa magunia wanarudi CORD mwezi ujao". Hii ndiyo semi kali zaidi ya mwezi huu. Hongera kwa kiswahili na utabiri.
Kwa sasa naona kama nguvu ya makundi iko kama ifuatavyo. Kundi la Raila liko na nguvu zaidi, likifuatiwa na lile la Mudavadi na kisha ni lile la Uhuruto katika tatu bora. Jana yuko mwania uraisi kaachia ngazi na kujiunga na CORD. Huenda ni kweli usemayo kuwa "vigogo wanakuja kwa magunia "
 
Cord na Raila ni sura ya kitaifa kwa kuwa mkikuyu yeyote asiyeungana na Raila hana sura ya kitaifa, is this what you are trying to tell us?!

Wtz wansaidia kueneza chili dhidi ya wakikuyu wakitaja njonjo. musisahau muda unayoyoma na vizazi vipya viaja

Mkuu Kabaridi,

Wakati Ruto na Uhuru wakifungua muungano wao siku ile Ruto alitangaza hovi katika kipaza sauti chake " hii ni kuwafahamisha wale wengine kuwa tangu sasa mkikuyu na mkalenjini atapiga kura pamoja"

Kutaja kabila kwenye hadhara ya wengi ni kuimarisha ukabila. Lakini pia muungano ule sasa na wenyewe sa wa kikabila zaidi kwa kuwa wako akina Gidion Moi ambao hawako nao na wamehikita zaidi kwenye kuimarisha kile chama cha baba na mama.

Sura ya kitaifa iko hivi, Uhuruto ni muungano wa vyama viwili tu na Railonzo ni muungano wa vyama kumi na vitano, hii si wazi kuwa mwenye macho haambiwi tazama?
 
Wakuu wangu, Kabaridi, FJM, na Ab-Titchaz,


Tuje kwenye mchango wa Kabaridi.

Maina Njenga ni Mungiki aliyeokoka. Wakati ule alikuwa ni mtu mzuri sana kwa kundi ambalo silo aliloliunga mkono sana. Alipaswa kujutia makosa yake wakati ule baada ya kujitokeza hadharani.

nakubaliana CORD inazidi kuimarika kwa kupata defectors. lakini kuokoka kwa maina njenga kulitokana na juhudi za kukaza buti dhidi ya kundi haramu mungiki ya waziri marehemu michuki. ni hali ya pwagu kapata pwaguzi
 
Mkuu Kabaridi,



Kutaja kabila kwenye hadhara ya wengi ni kuimarisha ukabila. Lakini pia muungano ule sasa na wenyewe sa wa kikabila zaidi kwa kuwa wako akina Gidion Moi ambao hawako nao na wamehikita zaidi kwenye kuimarisha kile chama cha baba na mama.
?

ipi hatari zaidi kati ya kutaja kabila hadharani na kueneza siasa za chuki dhidi ya kabila au makabila kwa mfumo wa 42 against 1?

usisahau mkuu kuwa makabila yote kenya (42) ni wakaazi wa kenya na asili yao ni kenya japokuwa tuna kabila ambazo jamii zao zina asili kutoka TZ na Kenya kama wamasaai. Royals IMO it is out of question to black mark some tribes.
Royals said:
Sura ya kitaifa iko hivi, Uhuruto ni muungano wa vyama viwili tu na Railonzo ni muungano wa vyama kumi na vitano, hii si wazi kuwa mwenye macho haambiwi tazama?

huenda ukawa wasema kweli kuwa CORD ni mkusanyiko wa vyama vingi, mfano ikiwa imebeba chama kama cha Cyrus Jirongo akiwa kielelezo kipya cha "haki na usawa"
 
Kabaridi, walipwa na TNA?lol.. Mtazamo wa wakenya kwa muungano wa TNA unashawishiwa na vitu vitatu;

kwanza ni sera za ugavi wa mamlaka kati ya TNA na URP ambayo ni ile ya nusu mkate, asilimia 50 kila upande jambo ambalo limewafanya hawa wenzetu wawili kuwa vigogo wakuu. Hebu tujikumbushe mtazamo wa wakenya kwa viongozi wao, weka kabila langu serikalini na pia mimi nipo serikalini. Sivyo? Wao walihubiri sana TNA/URP wakasahau uongozi jumilifu ingawa baadaye waliongeza kina Balala, Ongeri na the likes but mtazamo haujabadilika sana kwa mkenya .

Pili, Kenya imekuwa na viongozi watatu; mkikuyu na mkalenjin. Kwa kadri flani, wakenya wameshachoka. Mbona tusijaribu kigogo mwingine, laiti tu asiwe wa Mlima Kenya? Waelewa? Si eti taswira na sera za CORD ni kuhusu arubaini na moja dhidi ya moja. LA!!! Sisi kama wakenya ndio tumechoka, twataka mabadiliko endelevu kaka. uongozi wa nchi hauezi chezea eneo moja au mbili kila uchao. By chance it happens that the incumbent president is from central province and of which to me is alil counterproductive for one Uhuru Muigai.

La mwisho ni kwa waathiriwa wa uchaguzi, donda lipo bado, na kama halipo, nafsi yakataa. Wosia wangu ni huu; ni vema hawa wawili wakajinadhifishe kwa kina kule wanakohitajika kabla ya kukwea madarakani. Na kama hawawezi, natumai wakenya watakubali kuishi na mshikomshiko wa kiuchumi kama vile Sudan na nchi zinginezo zilizotengwa.

Ni hayo tu kwa sasa na si ukabila, sina ukoo na Raila, Uhuru ama Ruto. Naitamania tu nchi ya Kenya yenye mabadiliko mema na uongozi mwafaka. Si purukushani za kimataifa kila wakati kujaribu kutakasa ovu lililotendeka. CORD yaimarika, asilimia 51 ya wakenya wanadhania hivyo kulingana na kura za maoni.
 
nakubaliana CORD inazidi kuimarika kwa kupata defectors. lakini kuokoka kwa maina njenga kulitokana na juhudi za kukaza buti dhidi ya kundi haramu mungiki ya waziri marehemu michuki. ni hali ya pwagu kapata pwaguzi

"Kundi haramu la Mungiki la maremu waziri Michuki".

Kweli hapa ni Pwagu na Pwaguzi. Uzuri kidogo wa wa Kenya ni kuwa hawakubali kirahisi kuchezeshwa wimbo wasioupenda wakacheza. Huishi kwa kuangalia mwekekeo wa upepo unavovuma. Kwenye kelele nyingi ndiko kwenye sherehe.
 
"Kundi haramu la Mungiki la maremu waziri Michuki".

Kweli hapa ni Pwagu na Pwaguzi. Uzuri kidogo wa wa Kenya ni kuwa hawakubali kirahisi kuchezeshwa wimbo wasioupenda wakacheza. Huishi kwa kuangalia mwekekeo wa upepo unavovuma. Kwenye kelele nyingi ndiko kwenye sherehe.

nilimaanisha maina njenga ni pwagu kapata pwaguzi marehemu michuki ingawa ni maheremu lakini he dealt firmly with mungiki menace.
 
Back
Top Bottom