Saa zingine nampenda Magufuli

Sasa kwanini unasingizia katiba kutompa mamlaka rais kuweza kuwafuta watu kazi wanapotuhumiwa kula rushwa au kushindwa kusimamia kazi zao?, kwa taarifa yako, katiba ya Kenya inamruhusu rais kuwafuta kazi kuanzia CS, wakurugenzi na wateule wengi tu kama akipenda, kama ambavyo alivyofanya marekebisho madogo ya mawaziri hivi juzi.

Hii lugha ya kwamba hakuna serikali iliyopambana na rushwa hapo Kenya kushinda Jubilee, hayo ni maneno ya viongozi wa Jubilee kuwahadaa wananchi, wanekua wakiyasema mara kwa mara, lakini utafiti uliofanyika hivi karibuni, Wakenya wengi hawakubaliani, wengi wanasema Uhuru Kenyatta hana nia ya dhati Wala uwezo wa kupambana na rushwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shilingi inaimarika lakini Wakenya wanaendelea kufa kwa njaa, hii inakupa picha gani?," Kenya's economy is inversely proportion with better life"

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona ameenda hapo ujue ana intel zote.

Hakuna mkandarasi anayeweza kuchelewesha mradi kimaksudi, tatizo huwa pumba za urasimu serikalini halafu walivyo wavivu na mafisadi, mwisho wa siku mkulu kama ni mpenda kiki za wanahabari atakuibukia na kukuzomea zomea.
 
Hakuna mkandarasi anayeweza kuchelewesha mradi kimaksudi, tatizo huwa pumba za urasimu serikalini halafu walivyo wavivu na mafisadi, mwisho wa siku mkulu kama ni mpenda kiki za wanahabari atakuibukia na kukuzomea zomea.
Boss, wazembe nchi yetu wapo wengi Sana. Bila shuruti hawaendi.
 
Ile level ya indicipline tunayo Afrika, inataka watu kama Magufuli. Wacha wengine waonewe lakini inasaidia kuogopa public fund.

Afrika ni aibu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…