Sababu 10 kwanini Msuva Atachagua Yanga SC na Sio Simba SC

Sababu 10 kwanini Msuva Atachagua Yanga SC na Sio Simba SC

Wakati umeandika ulikuwa umetoka kulala au ulivuta Kwanza Ile kitu ya chuga hivi msuva huyu aliyechengana Na kombe la CAF au mwingne ukiona mchezaji timu za uarabuni hawamshobokei jua huyo ni wa kawaida Sana kitu kingne hivi yanga ambayo inaishia hatua ya awali kabisa ndo mtu aende ili aoneka email nje Uko serious kweli hii inayopigwa hat trick Na sopu au nyingine
Nakubaliana na wewe nimeliona hilo kwa Chama na Luis konde boy, waweza kuwa sahihi.

Niongeze volume?,🔥🔥
 
Kuelekea dirisha la ipo vita ya chini chini ya kuhusu Msuva kutamaniwa na Simba SC ili hali anahitajika Nyumbani “Jangwani”.

Ifahamike Simba SC walianza harakati zao mapema wakijua kumshawishi jamaa inahitaji jitihada ya ziada kwa kuwa hana vina saba nao.

Baada ya sakata lake la kesi baina ya muajiri wake Wydad Casablanca kuamuliwa, endapo kama hato pata timu nje ya Tanzania basi zifuatazo ni sababu 10 kwanini atachagua Yanga SC na kuwapotezea Simba SC.

1. Ushawishi wa Hersi.
Sote tunafahamu kuwa huyu jamaa ni mtanzania mwenye ushawishi nambari wani katika michezo hivi sasa. Ukiona mchezaji anafanya mazungumzo na hersi basi itakupasa ufanye zaidi ya kile ulichopanga ili umpiku.
View attachment 2287483


2. Nyumbani.
Factor nyingine ni kutaka kujihisi kuwapo nyumbani. Msuva hawezi chagua Simba kwa sababu ya kujihisi Mkimbizi katika mazingira atakayo hitaji utulivu.

3. Bingwa mtetezi.
Yanga SC ni mabingwa watetezi. Nani hataki kuwa sehemu ya wachezaji bora 11 katika Ligi.? Nani ataki kucheza katika kikosi bora cha msimu uliopita.? Ni mjinga tu atachagua kucheza katika mazingira yatakayo mlazimu afanye cha ziada ili kupata ushindi.

4. Project Mpya ya Yanga SC
Yanga SC iko katika project mpya ambayo inalenga kuifanya klabu kuwa ya kwanza kushiriki fainali na kutwaa kombe la CAF. Aina ya wachezaji waliopo wana akisi malengo ya project ya klabu. Bila shaka Msuva atapendelea zaidi kuwa sehemu ya project hiyo.

5. Exposure na Kujitangaza.
Msuva ana malengo ya kucheza nje ya mipaka kwa mara nyingine tena. Yanga SC inatoa platform pekee ya kumtangaza mchezaji kimataifa kutokana na muendelezo mzuri wa matokea na ubora wa kikosi.

6. Support ya dhati.
Saimon anatambua wazi kuwa mashabiki wa Simba wanamfahamu kuwa ana mapenzi ya dhati na klabu ya Yanga. Hivyo ni vigumu kupata support ya mashabiki ndani na nje ya uwanja.

7. Mazingira mazuri ya kufanya kazi.
Yanga SC inaongoza kuwa na mazingira mazuri ya mchezaji. Hakuna mchezaji anaweza kuchagua Bunju badala ya AVIC TOWN. Kambi na nyumba za wachezaji ni bora zaidi hapa afrika mashariki na kati.

8. Old Friends.
Kuwapo kwa old friends kikosini ni magnet kubwa sana kumvutia Msuva. Msuva hana mahusiano ya urafiki na mchezaji yeyote kutoka Simba SC.
View attachment 2287479


9. Maslahi.
Kimaslahi Yanga wanauwezo mkubwa sana wa kumlipa mchezaji kile anacho hitaji. Historia inaonyesha wakili msomi alishindwa kuongozewa mkataba wenye maslahi mapana na klabu yake. Sidhani kama Msuva yuko tayari kwa hilo.

10. Kikosi chenye njaa ya Mafanikio.
Sitaki kueleza mafanikio nadhani wengi wetu tunafahamu kuwa kuna mafanikio hewa na mafanikio kuntu. Kikosi cha Yanga kimejaa wachezaji vijana wenye kiu zaidi ya mafanikio. Na kiu yao inaonekana na kudhibitika uwanjani. Kwa Msuva hii ni destination mzuri zaidi.
View attachment 2287485

Simba kwa Sasa haina matumaini. Hakuna mchazaji wa maana ataenda Simba.
 
Sababu moja kubwa Msuva hakuwa kwenye mpango wa Club kubwa Simba Sports Club ni kuwa kiwango chake kimeshuka sana
club kubwa hii hii ya akina Kyombo?
FB_IMG_1644304521133.jpg


Sent from my Infinix X683 using JamiiForums mobile app
 
Simba kwa Sasa haina matumaini. Hakuna mchazaji wa maana ataenda Simba.
Kweli hakuna mchazaji atakaye kuja Simba bali Simba inasajili wachezaji. Mazao ya chuo cha kuzalisha wajinga hapo Yanga tunayaona hapa jukwaani Wahadhiri wenu. wanajituma sana.
 
Hiyo no 5 ni chai mkuu, labda ni yanga nyingine ambayo sisi hatuijui maana yanga yenyewe ilipigwa na kuondoshwa kwa aibu na mito united ya Nigeria, Sasa sijui atajitangazaje kimataifa kwa timu ambayo haifiki popote
Mito utd sio timu ya kubeza ndio bingwa wa nigeria yule
 
Utopolo hawaishiwi vituko[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]....
Nasikia wamemsajili waziri wa elimu wa zamani.....joyce

Sent from my PBBM00 using JamiiForums mobile app

Tena atakutana na makamu wake ZAWADI mauya pale wizarani.
 
Yanga bwana hyo project namba 4 ulivyoelezea kama unaelezea man city vile kumbe ni team iliyopigwa hatrick na SOPU na vibeki vyenu vifupi vile vikiongozwa na captain Maguire kutoka tanga

Mpira unachezwa kwa malengo.

Coast Union walikuja kutafuta HAT TRICK.

Yanga SC walikuja kutafuta KOMBE la ASFC.

Umeiona tofauti ya timu kubwa na timu za kawaida zisizo na uwezo wa kushinda taji?

[emoji23][emoji23]
 
Absolutely true, otherwise is magician people ndo watakuja kukupinga
 
Wakati umeandika ulikuwa umetoka kulala au ulivuta Kwanza Ile kitu ya chuga hivi msuva huyu aliyechengana Na kombe la CAF au mwingne ukiona mchezaji timu za uarabuni hawamshobokei jua huyo ni wa kawaida Sana kitu kingne hivi yanga ambayo inaishia hatua ya awali kabisa ndo mtu aende ili aoneka email nje Uko serious kweli hii inayopigwa hat trick Na sopu au nyingine
Kwahiyo timu za uarabuni ndo kipimo cha ubora wa mchezaji??

Yaani wewe huwezi kutumia akili yako uone kama mchezaji ni mzuri au lah hadi timu za uarabuni zimtake??
 
Back
Top Bottom