Sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010

MMM,

Kutaka Kikwete asigombee si ni KINYUME cha "UTARATIBU" wetu CCM? Au?

Mkuu,

Sidhani kama kuna mtu ambaye amemilikishwa uongozi wa maisha nchini kwetu,hivyo basi kila mtu anayo haki kabisa kikatiba kugombea nafasi yeyote ile kwenye uchaguzi ili mradi tu awe ametimiza minimum requirements.Huwezi ukanishawishi kuwa hata kama mtu amechemsha kipindi chake cha uongozi,apewe tu 'eti' kwa sababu 'UTARATIBU' ni kuwa lazima vipindi viwili(2) amalize.Tukifuata misingi hii tutaendelea kujenga taifa lisilo na misingi imara.Tukubali kuwa demokrasia ya kweli ni kukubali pia kupingwa.Usipokubali haya basi hautokuwa tofauti sana na dikteta.Kuna nini cha kuogopa mpaka tusikubali wagombea wengine?Kama kweli mtu yupo makini na rekodi yake ni nzuri(kwa kulinganisha mafanikio aliyoyapata kwenye kipindi chake cha kwanza na ahadi alizozitoa)then atadhibitisha kwenye kinyang'anyiro na siyo kukubali tu matokeo kuwa aendelee.

Kuendesha vyama kidikteta sio pia demokrasia.Kwani demokrasia inaanzia ndani na kuonekana nje.Kama ndani ya chama ndio kama haya,unategemea kweli nje mtu ataonekana anahubiri demokrasia?Hapa itakuwa ni kujidanganya na kudanganya wananchi.Kila mtu ana mtizamo wake na he/she is entitled to it.Kila mtu basi yupo responsible kutetea mtizamo wake kwa kutoa maelezo anayoona yana-support huo mtizamo.

Tusijenge tena msingi wa matope tena tukitegemea kuwa kesho utakuwa wa saruji!

Nawasilisha.
 
Sisi tumejiwekea utaratibu ndani ya cham na si katiba,Rais ambaye ni mwenyekiti wa Cham ndiye atakuwa mgombea pekee ili amalizie yale yalibaki na yatakayokuwepo kwenye 2010-15 CCM manifesto

Wenye Chama mnatuletea mtu safi - another 'Mr. Clean'?

Kutaka Kikwete asigombee si ni KINYUME cha "UTARATIBU" wetu CCM? Au?






Ni kweli kumwachia rais aliye madarakani kipindi kingine cha miaka 5 ndio utaratibu uliotumiwa na CCM kwa Mzee Rukhsa na Mkapa. Lakini hii sio sheria wala katiba ya CCM. Ila zipo sababu zilizowafanya wakapewa hiyo ridhia.
  1. Mzee Mwinyi aliweza kuiunganisha nchi kwa amani baada ya Mwalimu kuondoka madarakani. Pia aliweza kuifungua nchi kwenye soko huria ingawa iliingiza na tusiyoyapenda, rushwa ya wazi kwa viongozi.
  2. Mkapa alianza vema kwa kujenga insititution za uongozi na kuweka misingi ya maendeleo. Pia kipindi chake cha kwanza kabla ya Mwalimu kufariki, rushwa kwa viongozi ilikuwa nadra. Ingawa miaka 5 iliyofuatia bado alifanya kazi nzuri, lakini kulikuwa na mapungufu mengi.
  3. JK zaidi ya kutalii ulimwengu wote , fanikio lake pekee ninaloliona lingekua kumleta Maximo. Lakini nalo pia ni wazi kachemsha. Chini ya uongozi wake wa miaka 4 na ushee;
    • Umasikini umeongezeka,
    • Elimu imezidi kuwa duni,
    • Umeme aliokuta una matatizo umezidi kuwa mahututi,
    • Viongozi wake wamekuwa na utendaji mmbovu lakini wote wameweza kujilimbikizia utajiri,
    • Ameshindwa kushurutisha watendaji wake kuwashughulikia mafisadi
    • Mwelekeo wa maendeleo ya nchi haueleweki n.k, n.k.
Kwa hiyo JK hana sababu yoyote inayomfanya aombe kuruhusiwa kuendelea kuongoza nchi. Akijiuzulu hivi sasa ingekuwa nafuu kubwa kwa nchi.

Nakubalina 100% na MMJJ kuwa, kumpigia debe JK sio uzalendo.
 
Ukweli wenyewe JK has not done that bad in his first term. Yeah najua wengi tayari mnaguna. Ni raisi wa kwanza wa Tanzania ambae ame jaribu kuleta demokrasia yenye ukweli kwenye kipindi chake.

Tuna demokrasia ambayo ni changa na inachukua mkondo wake kwa namna moja au nyingine magazetini, mtandaoni na hata uraiani. Ingawa ni demokrasia ambayo bado ina tinted glass lakini imesaidia kuleta maendeleo fulani, kuwahamsha watu fulani na kufanya baadhi ya watanzania waweke hata sikio moja kwenye Siasa za nyumbani ni mwamko huo. Ambao unatokana na demokrasia leo hii mabomu mengi wanayo yamwaga wana JF humu ndani tunayachangia kwa matusi na kuwa-simulia hata wasiokuja humu, na wao kuchukizwa na matendo ya viongozi ni mwanzo huo.

Hivyo hii ni hatua muhimu kwetu na ni ya kumpongeza JK. Vile vile amejaribu kuwafanya viongozi wa mali za Umma wa ngazi za kati kufikiria mara mbili michezo ya fauli. Mfano ni jinsi alivyodili na baadhi ya laana ambazo zilianza na Mwinyi na kudekezwa na Mkapa, Ujambazi wa kutupwa na majambazi yalioukuwa yanaona kama kupora ni legitimate career au majambazi ya Benki ambayo assets za Benki walikua wakiziona kama mali zao. Mfano wa karibu na Liyumba na bwana Zombe hawa ni products wa awamu zilizopita.

Ndio kuna mapungufu mengi lakini JK unaweza sema ametuanzishia safari yenyewe, bado kuna mapungufu ambayo yamejijenga kwa zaidi ya miaka ishirini kwa sasa, ambayo ni muhimu tuyamalize kama hayo ya makundi Mzee MKJJ anayoyasema.

Kwani si Makundi tu bali ndio balaa lenyewe letu, lilipo hapo. Kila kundi lina nia ya kutumaliza kama hawa wa sasa wanavyotumaliza, kwa namna ya kusajili mikataba mibovu, kujilimbikizia assets za taifa na sasa mpaka kurithishana madaraka as if tunaishi kwenye Kingdom fulani hivi.

Hivyo alitukua jambo la busara kumnada kiongozi asie jinada. Ni lazima mwenye nia kuongoza nchi aje na ajitambulishe akaguliwe mapema sifa zake kabla atujaanza kumpigia debe. Vinginevyo tutajikuta tunaleta kiongozi ambae anaturudishia akina Zombe wengine. Wakati ni hatua ambayo tunataka kuifuta ktk historia yetu.

Ni kweli JK ametuangusha na ahadi zake nyingi, lakini tunasikia kutoka kwa takuruku kuna kesi kazaa uko jamaa wanazikwamisha. Mi naona JK has done phase one kuleta kitu muhimu scrutany, considering the context of our political history before he got into office ni mafanikio kutupa kiji sauti fulani ingawa ni kichanga. Phase ya pili iwe kujipunguzia madaraka au majukumu na kugawa sheria kihalali ili kuwe amna mwenye uwezo wa kulindwa na hilo ndio kongamano tunalolisiburi.
 

Usiwe na uhakika sana. Mimi nina wasichana wenzangu kama watano hivi ambao tulimpigia kura Kikwete kwa ajili ya kuipenda sura yake! He is handsome kusema ule ukweli!!
 
Nipe sababu moja tu kwamba kumpigia debe JK siyo uzalendo bali kuipigia debe CCM ni uzalendo....Sababu moja tu, ili niweze kupambanua vigezo mnavyotumia magreat thinker kuhusiana na upi ni uamuzi sahihi kati ya kuipigia debe CCM vs JK,hapo ndio uonevu unapojitokeza....Shida hapa ni kwamba,mnaupima ufanisi wa JK kwa kutumia vigezo vya mafanikio ya kitaifa kama maendeleo ya wananchi nk, na wakati huo huo mnatumia vigezo vya kichama wakati wa uamuzi wa either apigiwe debe ama la.
Tatizo mmesahahu kwamba ufanisi kwa maendeleo ya Taifa si kigezo cha kuchaguliwa kwa tiketi ya CCM,Hilo halipo na tuache unafiki,hakuna kiongozi utakayesema ni mzalendo wa kweli amewahi kupitishwa na ccm....Kigezo cha kuchaguliwa kwa tiketi ya CCM si uzalendo msi mix issues hapa.
 
Usiwe na uhakika sana. Mimi nina wasichana wenzangu kama watano hivi ambao tulimpigia kura Kikwete kwa ajili ya kuipenda sura yake! He is handsome kusema ule ukweli!!

Kwa hiyo una maana kwamba wewe si mwana CCM lakini uliamuwa kumpigia kura mwana ccm kwasababu ya sura?
 
Usiwe na uhakika sana. Mimi nina wasichana wenzangu kama watano hivi ambao tulimpigia kura Kikwete kwa ajili ya kuipenda sura yake! He is handsome kusema ule ukweli!!

Kwa hiyo nyie mliochagua sura yake inaelekea mlipata kweli ingawa hujasema kama katika miaka minne ya uongozi wake mlifanikiwa kupata mgao wenu, ila siye tuliotaka kiongozi tuliliwa ile mbaya.
 

Kupinga ngwe ya pili kwa JK si uhaini -kweli kabisa lakini toa ufafanuzi kwanza hakuna mwenye ubavu wa kupinga hilo kwakuwa kila mtanzania ana haki ya kugombea nafasi hiyo wakati tume itakapotangaza kwamba iko vacant kupitia chama cha siasa kilichosajiliwa...JK anayo haki hiyo kama mwanachama mwingine wa CCM, briefly hakuna mwenye haki ya kikatiba kumpinga JK asigombee ila wanachama wa CCM wataamua kumpitisha JK au wataamua kumpitisha mwingine kwa utaratibu wao....

Kumpigia debe si Uzalendo ...duh! hapo ndiko ulikochemsha uzalendo ni nini? unapimaje uzalendo? unafikiri kwamba wewe unayepigia debe asichaguliwe ni mzalendo zaidi kuliko yule ambaye anampigia debe achaguliwe? unataka kufikiri wewe na kundi lako mna haki zaidi kuliko wengine wanaompigia debe?

wewe toa sababu zako za kutompigia debe 51 na waache wengine watoe sababu zao za kumpigia debe JK..wote nyinyi ni wazalendo na mwamuzi ni "wapiga kura" kupitia uchaguzi huu ndio ustaarabu wa nchi yetu..labda kama unataka ustaarabu wa madagascar! ala

Lakini kujibatiza kwamba wewe na kundi lako linalopinga kumpigia debe JK ni wazalendo zaidi kuliko wale wanaompigia debe JK ni udikteta na ujinga ambao hautapita hivi hivi bila kupingwa..
 
kIKWETE ajiulize mwenyewe kama bado ana nguvu zinazostahili kuhimili vishindo vya miaka mingine mitano.Kwa vyovyote vile, kuna mengi ambayo hayaturidhishi walio wengi na naona kama vile hayaoni kama ni tatizo kwa uongozi wake.Ingekuwa mimi ningeenda kufanya retreat na kutafakari kama bado ni sawa kuendelea kugombea uongozi wa nchi
 
Nitaomba sana ufanyike mdahalo na wana ccm wenzake wataoomba kugombea...wasimuone kama mfalme maana akirudi kugombea anatakiwa awe mnyenyekevu na kufuata sheria...(Utaratibu) sasa wapambanishwe na waombaji wengine tuone nguvu ya hoja na demokrasia ichukue mkondo wake...ila tu isiwe ni mazoea na kuja kulipizana visasi na kujenga chuki!!iwe demokrasia ya kweli....hayo maturity yake anayosofiwa nayo aiweze ku practise!!
 
Hivi ni nani haswa tunayetaka achukue nafasi ya Kikwete? Nakubali kabisa Kikwete ana upungufu wake mkubwa tu. Lakini siko tayari kuona nchi inarudi enzi zile za kina Mkapa! Au hata za Mwinyi!

Kama kuna kitu kinachonivutia mimi ni jinsi Tanzania inavyokuwa kidemokrasia. Kwa mara ya kwanza sasa tutaona upinzani ukichukua dola Zanzibar. Hii ni kwa sababu haitawezekana tena masanduku ya kura kupelekwa kwa wakuu wa wilaya kuhesabiwa na watu kuuwawa wanapojaribu kuzuia hilo na kutetea haki yao ya kidemokrasia.

Na kwa mara ya kwanza sasa kama kina Zitto watatulia na kujenga upinzani imara tutaona wabunge zaidi ya 100 wa upinzani bungeni. Na ni kwa mara ya kwanza pia katika historia ya Tz tumeona na tutazidi kuona jinsi wabunge wa ccm na spika wao wanavyowaumbua mawaziri na viongozi wa chama chao.

Hivi mnataka nini zaidi ya hapo jamani? Au mnataka JamiiForum ifungiwe kwa kusema Rais wa TZ anauza sura na kucheka cheka hovyo ndio tuamini kwamba JK sio dhaifu? Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni jamani!

Give me a break!
 
Kikwete kuendelea kutawala (siyo kuongoza) kwa miaka mingine mitano ni kukaribisha maafa kwa taifa letu. Kipindi cha kwanza ambacho anahitaji kuungwa mkono kupata kipindi kingine ameharibu kiasi hiki na kuicha nchi mikononi mwa mafisadi huku yeye akipasua anga kutalii ughaibuni je kipindi kingine ambacho hahitaji tena kura zetu si ataiteketeza kabisa nchi? Hebu tuache ushabiki wa kijinga katika jambo nyeti kama hili . Huyu mtu hafai kupewa nafasi nyingine hao wanaoshabikia ni wachumia tumbo tu. Tanzania ni yetu sote
 

Nani atakayempitisha huyo 'mtu mwingine'? Vikao vyote vya mchakato wa kupata mgombea wa urais vinaongozwa na mwenyekiti ambaye ni JK. Sijawahi kuona wala kusikia mtu akiongoza kikao cha kujifuta kwenye mchakato. Na hata kama ataongoza mwingine vikao hivyo, kuna usemi wetu wa kiswahili kuwa 'meno ya mbwa hayaumani', tumeyaona Zimbabwe na Uganda, na hata Tanzania katika lile suala la 'kumwacha mzee wetu Mkapa apumzike' bila bughudha.
 
Wenye Chama mnatuletea mtu safi - another 'Mr. Clean'?

Mimi nadhani mtu safi tuu haitoshi! Tunataka awe pia ni competent in leadership. Awe imara na mwenye kufanya maamuzi muhimu na yenye tija kwa taifa na si chama ama wachache.
 
Nilisema mwanzoni kuwa mtu anaweza kuwa safi kwa sababu hajawahi kuwa karibu na uchafu; na mtu mwingine anaweza kuwa safi kwa sababu aliuondoa uchafu..
 
Je uchaguzi utafanyika ilhali kuna kesi ya msingi mahakamani?? (waliyoifungua NCCR-Mageuzi kudai tume huru ya uchaguzi)
Jamaa atatumia mwanya huo kupeta bila kura zenu
 


Kwa hiyo udhaifu wake unaweza kugeuka kuwa faida kwa Taifa!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…