Sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010

Siyo kwamba wapiganaji hawako tayari ila wanaogopa kukolimbiwa ndo maana hawagombei!
 

Namba 36, 39, 43 na 48; ni kati ya hayo ambayo mimi nimezingatia kupima kufaa mtu kuwa kiongozi wa nchi yenye lengo la kujikwamua kutoka kwenye umasikini. Maana haiingii akilini mtu anayejiita kiongozi aachie watu wafuje mali kupitia TANGOLD, MEREMETA na dada zake ili tu kunufaisha wachache halafu akanyamaza na kusema nitagombea tena. Unagombea kwa ajili ipi, je ni kuwatumikia watanzania ama ni kwa sababu hujaridhika na ulichochuma awamu inayoisha. Je, ni kukosa uzalendo ama kutokuwa na uwezo wa kuongoza ndiyo tatizo? Lolote kati ya hayo mawili linatosha kunifanya niseme hafai kuwaongoza watu wanaoimba muda wote kuondoa umasikini kichani mwao.

Tunahitaji mtu mwenye machungu na kuona watanzania wanavyoteseka na ana moyo wa dhati kutumia uwezo wake wa kuongoza kubadilisha maisha yao. Watu wanaingia madarakani kulinda masilahi ya chama zaidi na kusahau walivyoviimba wakati wakitafuta kupigiwa kura. Yako wapi leo? Matokeo yake sasa mabaya yanayomeza rasilimali za nchi yananyamaziwa ili chama kisiaibike, kuna uzalendo hapo? Nani alisema endapo kiongozi atakemea mabaya CCM itakosa umaarufu? Vinginevyo, na wewe ni muhusika, huwezi kunyamazia udhaifu kama huu ambao tumekuwa tukiuona tangu miaka saba hivi iliyopita ndani ya nchi yetu! Tena maovu yanayofanywa na wanasiana yanazidi kuongezeka siku hadi siku na wakubwa wananyamaza tu na kupigiana kampeni wenyewe atagombea peke yake. Wakati huo wengine wakiagizwa kunyamaza kujipigia kampeni.

Tunapelekwa wapi jamani? Unapofika wakati wa kuongelea masuala yanayohusu maisha yetu nawaomba watanzania waache kutania. Tunatakiwa tuwe wanasayansi kuifanya nchi yetu kutoka hapa ilipozama (kwenye umasikini). Watu anashindwa kushughulikia masuala nyeti, wanakimbilia kukata rufaa za hukumu ya mgombea binafsi! Woga wa nini? Kama serikali iko makini kiutendaji kupitia wanasiasa wake, wanaogopa nini kuwepo mgombea binafsi? Sasa tunaendelea kupoteza rasilimali zetu (fedha) kuwalipa kamati za kuandaa rufaa kama hizi zisizo na masilahi kwa umma.

Tunashindwa kusimamia matatizo ya kuhakikisha fedha za TANGOLD, MEREMETA na mengine maovu zinarudisha kwa uwazi kwa kuwashughulikia wote waliohusika kuchelewesha fedha hizo kutumika kwenye miradi ya maendeleo (hospitali, shule na miundombinu mingine mingi ya kuturahisishia kupigana vita ya umasikini). Wako wapi hao wanaosema wangependa waone mtu mmoja akisimama kugombea URAIS? Lengo lao ni nini? Wana masilahi gani? Je, wana uzalendo ndani ya mioyo yao? Hata hivyo sishangai maana mmoja wao alishasema siku moja, yuko kufa akimtetea mtu mmoja. Siyo kuwatetea masikini watanzania watoke kwenye dimbwi la umasikini.
 
Jamani kuongoza nchi sio sawa na kampuni ambayo sheria na operating guidelines zipo wazi. Kuongoza nchi ni sehemu ya SIASA.

Hata akipewa yeyote miongozi mwenu humu bado mapungufu yaktakuwepo tu.
 
Kikwete anagombea na anashinda, tuongelea 2015 tafadhali
 
Jamani kuongoza nchi sio sawa na kampuni ambayo sheria na operating guidelines zipo wazi. Kuongoza nchi ni sehemu ya SIASA.

Hata akipewa yeyote miongozi mwenu humu bado mapungufu yaktakuwepo tu.

ni jambo moja kuwa na mapungufu; ni jingine kutokuwa na uwezo!
 
ni jambo moja kuwa na mapungufu; ni jingine kutokuwa na uwezo!

Pia ni jambo lingine kuwa na uwezo na kutumia uwezo kuleta uharibifu

Kutokuwa na uwezo ni subjective term, wewe unaweza kusema JK hana uwezo mwingine akasema ana uwezo

Kama quantity (number of voters) ina determine ubora wa mtu JK amewashinda wengi na atawashinda wengi....siku zijazo

Mapungufu ya JK yanavumilika sana kuliko mapungufu ya Mkapa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…