Sababu kuu 5 zisizo za kisiasa za CRDB kupata hasara katika robo ya tatu 2016 ya Tshs.2 bilion.

Sababu kuu 5 zisizo za kisiasa za CRDB kupata hasara katika robo ya tatu 2016 ya Tshs.2 bilion.

article

Senior Member
Joined
Sep 10, 2016
Posts
186
Reaction score
344
1477907372905.jpg


Amani iwe nanyi!.

Nimepata nafasi ya kufanya uchambuzi wa wa taarifa za fedha (Statement of comprehensive income and statement of cash flows) za CRDB za robo ya tatu 2016 na kugundua sababu zifuatazo zilizosababisha Benki kupata hasara ya takribani Tsh.2 bilioni:
1477907487600.png

1.Kuongezeka kwa matumizi yasiyo ya riba kama vile mishahara na ada kwa 38.72% (kutoka Tshs.77,605 millioni.mpaka Tshs.107,651 milioni).

2.Kupungua kwa mapato yasiyo ya riba kama vile mapato yanayotokana na kubadilisha fedha za kigeni,ada kwa wateja na kamisheni kwa 12% (kutoka Tshs.44,036milioni mpaka Tshs.38,556 milioni.)

3.Kuongezeka kwa malipo/madai ya Riba yanayotokana na CRDB kukopa kutoka taasisi nyingine za fedha kwa 52.55%(kutoka Tshs.23,213 milioni mpaka Tshs.38,556 milioni).

4.Kuongezeka kwa hasara ambazo zitasababishwa na wateja waliochukua mikopo na "advance" kushindwa kurejesha fedha kwa 195%( kutoka hasara ya Tshs.13,093 milioni mpaka kufikia hasara ya Tshs. 38,687 milioni.)

5.Huduma mbaya za opereshini za kibenki za kila siku (operating activities) zilizopelekea hasara ya fedha taslimu Tshs15,173 milioni ukilinganisha na fedha taslimu Tshs 33,778 milioni zilizopatikana katika kipindi cha ulinganifu.

1477907459877.png

Napenda kuchukua nafasi hii kuuomba uongozi wa CRDB kutoa taarifa kwa wadau kuhusiana na hatua ambazo uongozi unatategemea kuchukua kurekebisha hasara hii pia Naupongeza uongozi wa benki kwa kwa kufanya vizuri kwenye uwekezaji(investing activities) kwa kupata fedha taslimu Tshs 235,694 milioni ukilinganisha na hasara ya fedha taslimu Tshs 64,240 milioni katika kipindi cha ulinganifu.

Nawakilisha,

Article.
 
Ahsante kwa analysis.Hata hivyo kuna Kitu ambacho nimekuwa nikifuatilia kwa muda kama Mmoja wa wanahisa crdb.Hisa za crdb zimekuwa zikiporomoka thamani yake Kuanzia November 2015 hadi sasa.Kwa Nini?
 
4.Kuongezeka kwa hasara ambazo zitasababishwa na wateja waliochukua mikopo na "advance" kushindwa kurejesha fedha kwa 195%( kutoka hasara ya Tshs.13,093 milioni mpaka kufikia hasara ya Tshs. 38,687 milioni.)

hiyo # 4 hujaeleweka, hiyo hasara itasababishwa au IMESABABISHWA NA WAFANYAKAZI KUJIKOPESHA na sasa mnashindwa kuirejesha

ukiingilia ngoma usiyoijua hutaweza icheza, wenzenu TWIGA maafisa wa BOT ndio wapo kauta na kwenye vitabu, ile biashara ya kizamani ya 10% @ mkopo wa Magufuli ndio mwisho

hebu tusubiri Desemba 2016
 
Katika lugha ya kitaalamu tunasema ni impairment of financila asset which implies a loss which could be incurred when the carrying amount of a financial asset exceed its recoverable amount.hayo nimakisio ya hasara ambayo yanateki into consideration asset quality of a borrowers especially those assets pledged as collateral for the loan...
 
Safi saana
Ila namaana wataalam wetu ndio uelewa wao mdogo mpaka kufikia hapo?
Maana sababu zote 5 sio za kufuatana,ni kwamba walianza kuona kasoro moja baada ya nyingine.Kwanini wasichukue hatua wakati hali haijafika hapo.

Na aslimia kubwa ya ambao hawajalipa madeni ni wakubwa,na kulindana ndio kumefika hapo.Kwa muono wangu ni kwamba haya mambo ya 10% haya ndio mwisho wake unafikia hapo.
Kama CRDB inafikia hivyo hivi hizi Banks nyingine hali inakuwaje,maana kwamie CRDB wana lead hapa nchini kwa kuwa na huduma bora za Ki bank na wateja wengi
 
Mifano nimetoa 1.juu hapa kwenye uzi soma vizuri.
 
Dawa ni wana hisa kuandamana hadi ubalozi wa Denmark kushinikiza board members kutoka danida wajiuzuru pamoja na ceo nae atupiwe virago, sidhani kama anazo mbinu mbadala za kuinusuru.
 
Niliwahi kutoa angalizo miaka saba iliyopita kuwa hii bank inaelekea kufa kwasababu inaendekeza biashara za ujanjaujanja na kukopeshana wachagga kwenye biashara zisizokuwa na tija.
 
Kuchaguliwa Askofu mkuu wa kanisa fulani hapa nchini toka kabila pendwa ambalo linanufaika sana na mikopo toka benki (ujenzi wa majengo ya vitega uchumi vya kanisa) wakati mwingine unatia shaka + kushindwa kwa mgombea urais wao 2015+CEO toka kabila pendwa pia+siasa baada ya uchaguzi ikiwemo kuhamisha pesa toka benki za kibiashara umechangia pakubwa anguko hili.
NB : mnisamehe, elimu yangu std.7 so sina mtiririko mzuri wa insha.
 
Mods wanatakiwa kuwa makini na haya mambo ya watu wasiokuwa na taaluma kutumia forums kama hizi na kutoa uchanganuzi wa mambo sensitive kwa wananchi bila kutueleza wao ni nani kitaaluma au kisheria.

Haya ni mambo ya taaluma hivyo lazima uoneshe waziwazi kitaaluma wewe ni nani na unatambuliwa na mamlaka zipi za taaluma au kisheria kusudi siku ukitupotosha na uchanganuzi wako tujue tunakupata wapi ili haki yetu isipotee.

Haya mambo ya kujitia ujuaji wa kuchanganua taarifa za fedha kwa wananchi bila ya kuwa na hayo mamlaka ya kisheria au kitaaluma yatakuja kuwatokea puani. Yaani kabisa unatumia na business logo ya benki kana kwamba ni taarifa rasmi toka benki yenyewe husika! Mwanzoni nilivyoona hiyo nembo ya CRDB nilifikiri ni wenye benki wametoa press release kumbe laaah!
 
Sababu ni nyingi lakini mi niliona kwa matawi ya kaskazini waajiriwa wake walikuwa wa upande mmoja hata kwa majina ungejua tu. Hili la wanasiasa kukopa mabilioni na kushindwa kulipa si la kuuliza.

Ushauri: Anza kufukuzia walala hoi kama wakulima stadi, mama/baba lishe, wafugaji n.k. Mkiendelea na kukumbatia matajiri mtaisoma namba hata kama imeandikwa kwa italics.
 
Perfect! Wengine vichwa vyao vimejaa siasa tu mwanzo mwisho.!
Sio ndio wale walipewa mic wamuulize mheshimiwa raisi wakabaki wanatumbua mijicho maaana wanatumia umbea kama vyanzo vya taarifa na habari zao.
 
Mkuu matumizi yasiyo na riba yakoje? Toa angalau mifano article
Ni mfano pale banki wanatoa pesa inakwenda kununua kitu ama kuazimwa mahala na inaporejeshwa inakuwa haijawekewa riba ili kule mahala ilikwenda na kutumika ifidiwe na riba kutokana na muda ilipokuwa huko nje.......sasa pesa mfano milioni miamoja zikitolewa halafu zikarejeshwa baada ya mwaka bila riba hiyo ni hasara kwa benki maana waliitoa katika mzunguko wake....
 
Kuchaguliwa Askofu mkuu wa kanisa fulani hapa nchini toka kabila pendwa ambalo linanufaika sana na mikopo toka benki (ujenzi wa majengo ya vitega uchumi vya kanisa) wakati mwingine unatia shaka + kushindwa kwa mgombea urais wao 2015+CEO toka kabila pendwa pia+siasa baada ya uchaguzi ikiwemo kuhamisha pesa toka benki za kibiashara umechangia pakubwa a nguo hili.
NB : mnisamehe, elimu yangu std.7 so sina mtiririko mzuri wa insha.

Na kufilisika kwa Twiga bank na kwenyewe kumesababishwa na wachaga? CEO wa Twiga Bank nae alikuwa mchaga? Acheni wivu wa kike leteni hoja
 
Sababu ni nyingi lakini mi niliona kwa matawi ya kaskazini waajiriwa wake walikuwa wa upande mmoja hata kwa majina ungejua tu. Hili la wanasiasa kukopa mabilioni na kushindwa kulipa si la kuuliza.

Ushauri: Anza kufukuzia walala hoi kama wakulima stadi, mama/baba lishe, wafugaji n.k. Mkiendelea na kukumbatia matajiri mtaisoma namba hata kama imeandikwa kwa italics.

Tatizo wengi mmejaa ukabila na udini usiokuwa na maana.Asilimia 99.9 ya wakazi wa Kilimanjaro ni wachaga na Wapare na wameenda shule ya kutosha.Ww ulitarajia nani aajiriwe? Asilimia iliyobaki yaani 0.1 ni wasambaa na warangi ambao ni maarufu kwa shughuli za nguvu nenda kariakoo utawakuta na bank hakuna kazi ya kutumia nguvu
 
Chief Kinyori sijasema popote mchaga acha kuniwekea maneno. Ingawa benk hii imekuwa kama imeanzishwa na Martin Luther. Kumbe ni ya wanahisa wengine hata hawana dini. Mtoeni huyo mzee asie na ubunifu mlete damu changa.ati mnadai hajamuandaa mrithi. Seriously!!
** mnafyatua matawi kila kona mfano kutoka mbezi beach mpaka Makumbusho mmefungua seven branches.....mbezi beach, kijitonyama, mlimani city, sinza,Ubungo, mabibo hostel. Na wengi wa mameneja/wafanyakazi ni kutoka kabila/dini fulani tu. MSITUTANIE! Mnajua mnachokifanya.
TWIGA BANCORP inataka uzi mpya kwa hapa tumalize hili kwanza.
 
Back
Top Bottom